Monday, 11 May 2020

Naibu Waziri wa Afya Dkt Faustine Ndugulile Akanusha Taarifa Kwamba Ni Mgonjwa

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Faustine Ndugulile, amekanusha taarifa za kwamba yeye ni mgonjwa na hali yake ni mbaya, zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

Dkt Ndugulile amezikanusha taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa Twitter leo Mei 11, 2020, na kusema kuwa taarifa hizo zipuuzwe kwamba yeye ni mzima wa afya.


Share:

MBUNGE WA KISHAPU SULEIMAN NCHAMBI KUENDELEA KUSOTA RUMANDE..KESI YAKE YA UHUJUMU UCHUMI YAPIGWA KALENDA HADI MEI 25

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mbunge wa Jimbo la Kishapu mkoani Shinyanga Suleiman Masoud Nchambi (CCM),  imetajwa tena leo Jumatatu Mei 11,2020 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Shinyanga na kuahirishwa hadi Mei 25, 2020 itakapotajwa tena kwa ajili ya maombi ya dhamana.


Katika mashtaka 12 ya uhujumu uchumi anayokabiliwa nayo Mbunge huyo ni pamoja na shtaka la kwanza, tatu ambayo ni kupatikana na silaha, shtaka la pili ni kupatikana na risasi, la nne ni kumiliki silaha aina ya Riffle kinyume na sheria kwa mujibu wa Sheria ya kumiliki silaha Na. 2 ya mwaka 2015, shtaka la tano, sita, saba, nane na tisa ni kumiliki risasi bila kibali, shtaka la 10 ni kumiliki silaha bila kibali na 11 ni kumiliki risasi isivyo halali.

Mbunge huyo alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Mei 8, 2020 mahakamani hapo katika shauri la uhujumu uchumi namba 10 la mwaka 2020 na kusomewa mashitaka 12 ya uhujumu uchumi mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Ushindi Swalo.       

Upande wa mshtakiwa ukiongozwa na Wakili Frank Mwalongo uliomba mteja wao apate dhamana lakini maombi yao yalishindikana baada ya upande wa Mashitaka ukiongozwa na Mkuu wa Mashtaka mkoa wa Shinyanga, Margareth Ndaweka kupinga na kueleza kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kutoa dhamana hiyo ambapo Hakimu Swalo alikubaliana na hoja hiyo na kuahirisha shauri hilo hadi Mei 25, mwaka huu ambapo litaletwa kwa ajili ya kutajwa tena na kushughulikia dhamana, ambapo mshtakiwa amerudishwa tena rumande.

Wakili wa mshtakiwa, Frank Mwalongo amewaeleza waandishi wa habari  kuwa mteja wake amekosa dhamana kwa kuwa hati ya mashtaka haijataja thamani (kiasi) anachodaiwa kuhujumu mshtakiwa, hivyo haina mamlaka ya kutoa dhamana na kuwataka waombe mahakama kuu ambayo ina mamlaka ya kutoa dhamana hiyo.

Share:

Katibu baraza la ardhi Kiteto kizimbani kwa rushwa

Na John Walter-Manyara
Ofisi ya TAKUKURU Kiteto, imemfikisha mahakamani katibu wa baraza la ardhi kata ya Sunya, Hamisi Hemedi Saidi kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa kinyume na kifungu cha 15 (1) (a) pamoja na kifngu cha 15 (2) vya sharia ya kuzuia na kupambana na rushwa ya mwaka 2007.

Akisomewa mashitaka mbele ya hakimu wa mahakama ya wilaya ya Kiteto, Joakim Mwakiyolo, mwendesha mashtaka wa TAKUKURU Wilayani humo, Wakili Yahaya Masakilija alisema, mtuhumiwa ni mkazi wa Kijiji cha Sunya na katibu wa Baraza la Ardhi katika kata hiyo, tarehe 4.5.2020 aliomba rushwa ya shilingi 200,000 kutoka kwa mwananchi ili ampe tahafifu ya kesi yake ambayo imesajiliwa kwake namba 13/2019.

Shitaka la pili tarehe 5.5 2020 mtuhumiwa huyo tena akiwa katika nafasi yake ya ukatibu wa baraza, aliomba na kupokea rushwa ya kiasi cha shilingi laki 120,000 kama kishawishi ili aweze kumsaidia kushinda kesi shauri la ardhi namba 13/2019 ambalo lipo katika baraza lake hilo.

Katika mashitaka hayo yote mawili mshitakiwa Hamisi Hemedi Saidi alikana shitaka na yupo nje kwa dhamana, kesi hiyo ya Jinai namba 55/2020 itaendelea kusikilizwa hoja za awali mahakama ya wilaya ya Kiteto tarehe 9.6.2020.


Share:

Dawa ya Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) yatoa mwanga wa matumaini kwa wagonjwa wa corona

Dawa  iliyofanyiwa kazi na Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), imetoa mwanga wa matumaini kwa wagonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na virusi vya corona.

Dawa hiyo iliyopewa jina la NIMRCAF (pichani), inatokana na mchanganyiko wa vyakula; na katika majaribio imeonesha ina uwezo mkubwa wa kudhibiti virusi vya corona.

Akielezea mchanganyiko huo, Mkurugenzi wa Kitengo cha Tiba Asili cha NIMR, Dk Justine Omolo alisema ni fomula ya tiba lishe, ambayo ina mchanganyiko wa pilipili kichaa, tangawizi, limao na kitunguu saumu, asali na maji. Alisema dawa hiyo inasaidia kumpa nafuu mgonjwa wa corona, kwa kutibu dalili zinazotokana na ugonjwa huo, na kwamba tayari imeshaonyesha matokeo chanya.

“Mchanganyiko wa tiba lishe hiyo sio dawa ya corona, lakini inasaidia kumpa nafuu mgonjwa wa corona kwa kuwa inatibu dalili zinazoambatana na ugonjwa huo,” Dk Omolo amesema na kuongezea kwamba mpaka sasa tiba lishe hiyo imeshaleta matokeo chanya kwa kuwa imesaidia wagonjwa wengi wa corona. Alisema kwa sasa mahitaji yamekuwa ni mengi, tofauti na awali.

“Mwanzo tulikuwa tukitengeneza chupa 1,000 na tumekuwa tukisambaza hospitali kwa wagonjwa kwa siku chupa 120 hadi 200, lakini sasa mahitaji yamekuwa makubwa na imeonyesha matokeo mazuri kwa wagonjwa,” alisema

Alisema kutokana na mafanikio hayo, serikali imewaongezea vifaa ambapo kuanzia wiki ijayo wataanza kuzalisha chupa 5,000 kwa siku.

Alisema chupa hiyo yenye ujazo wa nusu lita, inauzwa Sh 10,000 na ni dozi ya mtu mmoja ambayo inanyweka kwa siku tano, ambapo mgonjwa atalazimika kunywa mara tatu kutwa.

Dalili za ugonjwa huo wa corona ni joto mwilini na kikohozi kikavu; na baada ya wiki moja kikohozi hicho kinaweza kusababisha tatizo la kushindwa kupumua.

Utafiti uliofanywa na Shirika la Afya duniani (WHO) kwa wagonjwa 56,000, ulibaini kuwa asilimia 80 ya wale walioambukizwa, hupata dalili zisizo kali kama vile kukohoa, joto mwilini na mara nyingine homa ya mapafu, asilimia 14 hupatwa na dalili kali, kama vile tatizo la kupumua.

Asilimia sita hukumbwa na tatizo la mapafu kushindwa kufanya kazi na viungo vingine mwilini na hata kusababisha kifo.

Miongoni mwa dalili nyingi zilizoripotiwa na wagonjwa, asilimia 88 walidai kuwa na joto mwilini, asilimia 68 kikohozi kikavu na asilimia 38 waliripoti uchovu. Tatizo la kupumua liliwapata asilimia 19 ya wagonjwa, asilimia 13 waliripoti kuumwa na kichwa na asilimia nne waliripoti kuharisha.

Omolo alisema kwa mtu ambaye hana dalili, anapaswa kutumia dawa hiyo mara moja kwa siku na hiyo itamsaidia kujikinga na ugonjwa huo wa corona.

“Watu wanapaswa kujua kwamba virusi vya corona au Covid 19 ni mojawapo ya homa, hivyo basi vina dalili nyingi zinazofanana na homa ya kawaida’’, alisema

“Lazima uwe makini iwapo unahisi tatizo la kupumua. Ni muhimu kutafuta msaada wa matibabu haraka. Tiba lishe hii haina madhara, watu waitumie ili kujikinga na janga hili la corona, “ alisisitiza


Share:

Wakusanyaji Mapato Mkoani Tabora Ambao Hawajapeleka Fedha Benki Kuchukuliwa Hatua

NA TIGANYA VINCENT
SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imeagiza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa watumishi wote waliopewa mashine za kukusanyia mapao (POS) ambao hadi hivi wadaiwa mapato waliyokusanya kwa kutoyawasilisha Benki.

Kauli hiyo imetolewa jana na Katibu Mkoa wa Tabora Msalika Makungu wakati wa kikao cha robo ya tatu cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Urambo.

Alisema kitendo hicho ni kinyume cha kifungu cha 60 cha Sheria ya fedha za umma yam waka 2001.

Makungu alisema dosari za aina hiyo ndio zimekuwa zikisababisha upotevu wa fedha za umma na kuziagiza Halmashauri kuhakikisha zinasimamia kwa ajili ya kuziondoa.

Aidha Katibu Tawala huyo wa Mkoa amepiga marufuku kwa Wakurugenzi na Waweka Hazina kuruhusu utaratibu wa Wakusanyaji mapato kuchukua asilimia zao(commission) kutoka makusanyo ya fedha za mapato ya ndani kabla ya kupelekwa Benki.

Alisema vitendo hivyo vinasababisha matumizi ya pesa  ‘mbichi’ na kupelekea Halmashauri kupoteza mapato yake na kusababisha uzalishaji wa hoja za kiukaguzi.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala huyo wa Mkoa wa Tabora ameziagiza Menejimenti za Halmashauri zote za Mkoa huo kuhakikisha hazizalishi madeni yanayotokana na stahili za watumishi wanahama na wale wanaopandishwa madaraja.

Alisema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alishaagiza hakuna mtumishi atayehamishwa bila kulipwa stahili na kuongeza kuwa kwenda kinyume cha hapo ni kutenda kosa.

Makungu aliongeza kuwa kuchelewa kulipa stahiki za watumishi kunavunja morali ya kufanyakazi jambo ambalo linaweza kusababisha mgawanyiko miongoni mwa Watumishi.

Aidha Katibu Tawala huyo aliagiza Halmashauri zote kuanza kuandaa stahiki za posho za Madiwani ili Mabaraza yatakapovunja wasipate usumbufu wa kufuatilia.

MWISHO


Share:

RAS Tabora Anzeni Kulima Mazao Mengine Kukabiliana Na Matatizo Ya Kushuka Kwa Uzalishaji Wa Zao La Tumbaku

NA TIGANYA VINCENT
HALMASHAURI ambazo zinazotegemea sehemu ya mapato kutoka kwenye zao la tumbaku zimeakiwa kuandaa mkakati mpya ambao utawawezesha kulima mazao mengine ili kuwa na msingi wa vyanzo vipya vya mapato ya ndani.

Hatua hiyo inafuatia Kampuni zinazonunua tumbaku Mkoani Tabora kuendelea kushusha makisio ya uzalishaji kwa wakulima wa tumbaku.

Kauli hiyo imetolewa jana na Katibu Mkoa wa Tabora Msalika Makungu wakati wa kikao cha robo ya tatu cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Urambo.

Alisema Kampuni za Tumbaku zimekuja ya staili mpya ya kudai kuwa zitanunua tumbaku kilo chache lakini badala yake zimekuwa zikinunua tumbaku nyingi iliyolimwa nje ya mkataba kwa bei inamuumiza mkulima na kusababisha Halmashauri kupata mapato kidogo.

Aidha Makungu alisema ni vema Halmashauri zikaanzisha kilimo kikubwa cha maembe kwa kuwa Mfanyabiashara Bakharesa ameshaonyesha nia ya kununua embe zote zinazozalishwa Mkoani Tabora.

Alisema cha msingi kuwaelimisha wakulima kulima kitaalamu na kutoa huduma za ugani kwao ili waweze kuzalisha maembe bora.

Makungu aliongeza ni vema Halmashauri zikasisitiza kilimo cha korosho na Alizeti kwa ajili ya kuwawezesha wakulima kuwa na vyanzo vingi vya kujipatia kipato.

MWISHO


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu May 11



















Share:

Tumefanya Maboresho Kwenye App Yetu ya Mpekuzi Ili Kukuwezesha Kupata Habari zetu Haraka hasa Wakati huu wa janga la Corona

Tumefanya maboresho katika App yetu ya MPEKUZI ili kuendana na changamoto ya sasa ya janga la Corona inayoikumba dunia Nzima

Usikubali kupitwa na taarifa muhimu zinazoendelea hapa nchini na Duniani  kwa Ujumla . Tumejipanga vizuri sana kukupatia taarifa sahihi na kwa wakati.

👉1. Tumebadili muonekano na kuufanya kuwa mzuri zaidi
👉2. Kila habari tunayoweka kuanzia sasa utapata notification kwenye simu yako 
👉3. Habari zote kwa sasa zinafika kwa haraka kwenye simu yako kuliko ilivyokuwa hapo awali

KUMBUKA: App yetu ni BURE. Unachotakiwa kukifanya ni kuingia Playstore na kupakua MPEKUZI APP

Kama tayari unayo, basi Ingia Playstore kwa ajili ya kupata UPDATE hii ya Toleo Jipya

Tumekurahisishia, Unaweza pia ...<<KU BOFYA HAPA>> Kupata toleo hili Bure Kabisa


Share:

Sunday, 10 May 2020

Wagonjwa Wa Corona Nchini Kenya Wafika 672

Idadi ya wagonjwa wa corona nchini Kenya imeongezeka hadi 672 baada ya wagonjwa wapya 23 kukutwa na virusi hivyo katika kipindi cha saa 24, huku idadi ya waliopona virusi ikifika 239 baada ya wagonjwa wengine 32 kupona virusi hivyo.


Share:

Iran Yasema Iko Tayari Kubadilishana Wafungwa na Marekani

Msemaji wa serikali ya Iran Ali Rabiei amesema kuwa Marekani bado haijajibu ombi lao la kubadilishana wafungwa.

Kwa mujibu wa Idhaa ya Kishwahili DW, Rabiei amesisitiza kuwa Tehran iko tayari kubadilishana wafungwa na Marekani bila masharti yoyote.

Iwapo hilo litatokea, basi itakuwa ni mojawapo ya matukio machache ya ushirikiano kati ya Marekani na Iran, mataifa mawili ambayo yamekuwa kama mfano wa pamba na moto.

Uhusiano wa Marekani na Iran umezidi kuwa mbaya hasa baada ya Rais Donald Trump kuingia madarakani

Kumetolewa wito na nchi zote mbili kubadilishana wafungwa kutokana na janga la virusi vya Corona.

Katika eneo la Mashariki ya kati, Iran imeathirika pakubwa na janga hilo nayo Marekani ikiongoza kwa idadi ya vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Covid 19 kote duniani.


Share:

Korea Kusini Yaamuru kufungwa kwa maeneo yote ya kuuza vileo na kumbi za starehe baada ya kuzuka visa vipya vya Corona

Mamlaka za mji mkuu wa Korea Kusini, Seoul zimeamuru kufungwa kwa maeneo yote ya kuuza vileo na kumbi za starehe baada ya kuzuka visa vipya vya virusi vya corona vinavyoibua wasiwasi wa kutokea wimbi la pili la kusambaa virusi hivyo hatari. 

Meya wa mji huo Park Won-soon amesema amri hiyo itakayoendelea bila kikomo imefuatia maambukizi mapya ya virusi vya corona yaliyogundulika kwenye wilaya ya Itaewon, yenye shughuli nyingi nyakati za usiku. 

Zaidi ya visa 24 vinahusishwa na mwanaume mmoja aliyegundulika kuwa maambukizi ya COVID-19 baada ya kutembelea kumbi tano za starehe kwenye wilaya ya Itaewon wiki iliyopita. 

-DW


Share:

Mashambulizi makali ya waasi yaharibu Uwanja wa Ndege wa Tripoli Libya

Mashambulizi makali ya maroketi yaliyofanywa jana Jumamosi na waasi dhidi ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mitiga, jijini Tripoli, Libya yameua raia sita na kusababisha hasara kubwa kwenye uwanja huo.

Raia wengine kadhaa wamejeruhiwa katika shambulio hilo la waasi wanaoongozwa na Jenerali Khalifa Haftar ambao wanaungwa mkono na Saudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati), Misri na baadhi ya nchi za Magharibi.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya inayotambuliwa kimataifa amesema kuwa, takriban maroketi 80 yamevurumishwa kwenye uwanja huo wa ndege, na kuteketeza ndege mbili aina ya Airbus, kusababisha moto katika maghala ya mafuta na kuteketeza magari ya Zima Moto.

Kwa upande wake, Waziri wa Uchukuzi wa Libya amesema, moja na ndege zilizoshambuliwa ilikuwa inajiandaa kupaa kuelekea Uhispania kwa ajili ya kuwachukua raia wa Libya waliokwama katika nchi hiyo ya Ulaya kutokana na janga la corona.

Uwanja wa Ndege wa Mitiga ndio pekee unaofanya kazi katika mji mkuu wa Libya, Tripoli. Hata hivyo, safari za abiria wa kawaida zilisimama tangu mwezi Machi kutokana na kushambuliwa mara kwa mara uwanja huo hata kabla ya nchi hiyo kuchukua hatua za kufunga maeneo ya nchi hiyo kutokana na corona.

-Parstoday


Share:

HAPPY MOTHER'S DAY!!


Leo Mei 10 tunasheherekea siku ya akina Mama duniani. Malunde 1 blog inawatakia heri, baraka, maisha marefu, furaha na mambo yote mazuri akina Mama wote!

Mungu awabariki sana kwa upendo wenu hatuna cha kuwalipa zaidi ya kuwaombea kwa Mungu.

Happy Mother's Day!!


Kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla kwa kupakua/ kudownload App ya Malunde 1 blog tukuhabarishe masaa 24.

Tembea na dunia kiganjani mwako sasa.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. Hii ndiyo mpya kabisa,ina alama hii ↡↡
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog

Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

https://bit.ly/2Qb7qyF


Share:

International Istqaama Muslim Commuty Yatoamsaada Kwa Wafungwa Kahama

SALVATORY NTANDU
Jumuiya ya kiislamu ya  International  Istiqaama muslim Community  imetoa msaada ya vyakula mbalimbali kwa Wafungwa waliofunga katika Gereza la wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ili kuwasaidia katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Akikabidhi Msaada huo Mei 9 mwaka 2020 kwa mkuu wa Gereza hilo, Misana Shigumha Katibu wa Masijd Alwahab  kahama,  Shekhe Ahmed  Haroun  Alnoobiy amesema msaada huo umetolewa na watu kutoka taifa la Oman kwaajili ya wafungwa na kuwataka kuendelea kuwaombea ili mwenyezi mungu aendelee kuwapa kheri zaidi.

 “Tumeleta kilo 200 za mchele, kilo 200 maharage ndoo saba za mafuta ya kula, na sukari kilo 100,tunaomba mpokee,ndugu zenu wa oman wamewakumbuka kwa msaada huu naombeni muendeleze dua katika kipindi hiki cha toba,”alisema Alnobiy.

Aliongeza kuwa Jumuiya hiyo hapa nchini inahusika na kuisaidia jamii  hususani yatima, masikini na wagonjwa ndio maana ikaamua  kuwasaidia wafungwa hao ili nao waweze kumrudia Mwenyezi Mungu kwa  kufanya toba katika kipindi hiki maalumu cha mwezi Mtukufu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Masijd Alwahab Kahama, Shekhe Mohamed Issa amewaomba wafungwa kuutumia mfungo huu wa  Mwezi wa Ramadhani kwa  kumwombea Rais, Dk John Pombe Magufuli ili Mwenyezi Mungu aendelea kumpa hekima za kuliongoza taifa kwa amani.

“Dumisheni dua ili Mwenyezi Mungu aweze kutuondelea janga la Corona ambalo linaendelea kuutikisa ulimwengu,tunaimani Allah atatukinga na kutuepusha dhidi ya COVID 19,”alisema Issa.

Akipokea Msaada huo kwa niaba ya Kamishana Jenerali wa Jeshi la Mageraza nchini,Mkuu wa Gereza hilo,Misana Shigumha ameishukuru jumuiya hiyo kwa msaada huo na kusema kuwa utawafikia wafungwa hao kwa wakati.

Sambamba na hilo Misana amesema kuwa katika jitihada ka kukabiliana na ugonjwa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona katika gereza hilo wanaendelea kuzngatia maelekezo yote yaliyotolewa na serikali ikiwa ni pamoja na kuzingatia unawaji wa mikono na upimaji wa joto kwa wafungwa,mahabusu na watu wengine wanaotembelea eneo hilo.


Share:

Barabaraya Uyogo – Ulowa Katika Halmashauri Ya Ushetu Yapandishwa Hadhi

SALVATORY NTANDU
Serikaili imesema kuwa barabara ya kutoka Uyogo hadi Ulowa katika halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama mkoani  Shinyanga imepandishwa hadhi na kutoka kuwa chini ya wakala wa barabara za mjini na vijijini (TARURA) nakuwa chini ya wakala wa barabara Tanzania, (Tanroads). 

Barabara nyingine ni ile inatoka Masumbwe wilayani mbogwe mkoani geita kwenda Ulankulu mkoani Tabora ambayo nayo ilikuwa chini ya Tarura Sasa itakuwa ni ya Tanroads.

Hayo yalielezwa jana  na waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano, Elias Kwandikwa katika kijiji cha Mbika  kata ya Ushetu,  wakati akikabidhi gari la wagonjwa katika kituo cha afya mbika,lilotolewa na serikali.
 
Alisema kuwa tayari timu ya wataalam imekwisha fanya uhakiki ili kuruhusu taratibu za kuzipandisha barabara hizo na kwamba lengo ni kutambua mchango mkubwa unaotokana na barabara hizo inazotumika kupitisha mazao ikiwamo zao la tumbaku na Pamba.

Akizungumzia msaada wa gari la wagonjwa, Kwandikwa alisema  gari Hilo lenye  thamani  ya shilingi  Milioni 120 ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri mkuu aliyoitoa wakati wa ziara yake katika halmashauri ya Ushetu.

Aidha Kwandikwa alisema kuwa lipo gari lingine la wagonjwa  ambalo ni aina ya naoh ambalo litaletwa hivi karibuni kwaajilibya kusaidiabkubeba wagonjwa.

Akipokea msaada wa gari Hilo Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Ushetu Michael Matomora alisema gari Hilo litatumika katika kituo Cha afya Mbika kutokana na kituo hicho kuwa kinahudumia  wagonjwa wengi kutoka halmashuri hiyo na  kata jirani za mkoa wa Tabora, na kwamba gari Hilo pia litasaidia vituo vya afya jirani katika  halmashauri ya UShetu.

Naye Diwani wa kata ya Ushetu Pili Sonje aliipongeza serikali kwa msaada huo na kwamba Sasa itarahisisha kwa Kiasi kikubwa kuhudumia wagonjwa hasa kina mama wanaopatabrufaa ya kwenda katika hospitali ya halmashuri ya mji wa Kahama na wanaopewa rufaa ya kwenda Shinyanga au Bugando.

Mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha alitoa wito kwa watumishi na wananchi kwa ujumla kuwa na desturi ya kutunza rasilimali za umma ili ,ziweze kudumu na kunisaidia jamiii huku Aliwakumbusha wananchi kuendelea kuchukua tahadhali ya ugonjwa wa Covid 19 unaosabaishwa na virusi vya Corona.


Share:

FULL POWER , ZAT 50 NI SULUHISHO LA KUDUMU TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume


⇒Ngiri,

⇒Henia

⇒Kisukari

⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri

⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu

⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi

⇒Msongo wa mawazo 



⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.



FULL POWER



⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.



⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50



⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

DAWA YA NIMRCAF INAYOFANYIWA KAZI NA NIMR KUTIBU CORONA YALETA MATUMAINI TANZANIA

DAWA iliyofanyiwa kazi na Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), imetoa mwanga wa matumaini kwa wagonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na virusi vya corona.

Dawa hiyo iliyopewa jina la NIMRCAF (pichani), inatokana na mchanganyiko wa vyakula; na katika majaribio imeonesha ina uwezo mkubwa wa kudhibiti virusi vya corona. 

Akielezea mchanganyiko huo, Mkurugenzi wa Kitengo cha Tiba Asili cha NIMR, Dk Justine Omolo alisema ni fomula ya tiba lishe, ambayo ina mchanganyiko wa pilipili kichaa, tangawizi, limao na kitunguu saumu, asali na maji. Alisema dawa hiyo inasaidia kumpa nafuu mgonjwa wa corona, kwa kutibu dalili zinazotokana na ugonjwa huo, na kwamba tayari imeshaonyesha matokeo chanya. 

“Mchanganyiko wa tiba lishe hiyo sio dawa ya corona, lakini inasaidia kumpa nafuu mgonjwa wa corona kwa kuwa inatibu dalili zinazoambatana na ugonjwa huo,” Dk Omolo amesema na kuongezea kwamba  mpaka sasa tiba lishe hiyo imeshaleta matokeo chanya kwa kuwa imesaidia wagonjwa wengi wa corona. Alisema kwa sasa mahitaji yamekuwa ni mengi, tofauti na awali.

“Mwanzo tulikuwa tukitengeneza chupa 1,000 na tumekuwa tukisambaza hospitali kwa wagonjwa kwa siku chupa 120 hadi 200, lakini sasa mahitaji yamekuwa makubwa na imeonyesha matokeo mazuri kwa wagonjwa,” alisema.

Alisema kutokana na mafanikio hayo, serikali imewaongezea vifaa ambapo kuanzia wiki ijayo wataanza kuzalisha chupa 5,000 kwa siku.

Alisema chupa hiyo yenye ujazo wa nusu lita, inauzwa Sh 10,000 na ni dozi ya mtu mmoja ambayo inanyweka kwa siku tano, ambapo mgonjwa atalazimika kunywa mara tatu kutwa.
Dalili za ugonjwa huo wa corona ni joto mwilini na kikohozi kikavu; na baada ya wiki moja kikohozi hicho kinaweza kusababisha tatizo la kushindwa kupumua. 

Utafiti uliofanywa na Shirika la Afya duniani (WHO) kwa wagonjwa 56,000, ulibaini kuwa asilimia 80 ya wale walioambukizwa, hupata dalili zisizo kali kama vile kukohoa, joto mwilini na mara nyingine homa ya mapafu, asilimia 14 hupatwa na dalili kali, kama vile tatizo la kupumua.

Asilimia sita hukumbwa na tatizo la mapafu kushindwa kufanya kazi na viungo vingine mwilini na hata kusababisha kifo.

Miongoni mwa dalili nyingi zilizoripotiwa na wagonjwa, asilimia 88 walidai kuwa na joto mwilini, asilimia 68 kikohozi kikavu na asilimia 38 waliripoti uchovu. Tatizo la kupumua liliwapata asilimia 19 ya wagonjwa, asilimia 13 waliripoti kuumwa na kichwa na asilimia nne waliripoti kuharisha.

Omolo alisema kwa mtu ambaye hana dalili, anapaswa kutumia dawa hiyo mara moja kwa siku na hiyo itamsaidia kujikinga na ugonjwa huo wa corona, ambao takwimu za WHO zinaonesha hadi Mei 6, mwaka huu, ulikuwa mewakumba watu 3,588,773.

“Watu wanapaswa kujua kwamba virusi vya corona au Covid 19 ni mojawapo ya homa, hivyo basi vina dalili nyingi zinazofanana na homa ya kawaida’’, alisema
“Lazima uwe makini iwapo unahisi tatizo la kupumua.

Ni muhimu kutafuta msaada wa matibabu haraka. Tiba lishe hii haina madhara, watu waitumie ili kujikinga na janga hili la corona, “ alisisitiza Watalamu wanasema zipo njia nne za kudhibiti vimelea vya magonjwa hasa virusi ambavyo havina tiba.

Njia ya kwanza ni chanjo na ya pili ni kuzuia virusi visiweze kujishikiza kwenye seli zilizopo mwilini. Njia ya tatu ni kudhibiti visizaliane au kuongezeka mwilini na njia ya nne ni kuongeza protini mwilini ili kusaidia kupambana na virusi hivyo.

Kwa mujibu wa Dk Omolo, NIMRCAF ina vitamini C kwa wingi na vitamini K, na kitaalamu mchanganyiko unaopatikana katika tiba lishe hiyo unaitwa ‘Polyphenols’.

Mchanganyiko huo unazuia damu kuganda.

Alisema seli zinazopokea virusi vya corona, zipo kwenye mapafu na virusi vikiingia humo, husababisha damu kuganda na kuleta matatizo kwenye mfumo wa upumuaji. “Mgonjwa akitumia tiba lishe hii, ndani ya nusu saa lazima atasikia nafuu.

Wagonjwa wengi waliokuwa hoi walipoitumia, wamepata matokeo mazuri na wengine wamepona kabisa,”alisema Alisema walianza utafiti wa dawa hiyo muda mrefu, kabla dunia haijakumbwa na janga la corona.

Walifanya utafiti huo kwa kushirikiana na watalamu mbali mbali wa tiba asili. Walikuwa katika kutafiti tiba ya Ukimwi.

NIMR imekuja na dawa lishe hiyo, ikiwa ni siku chache baada ya WHO kutoa taarifa yake, ambayo ilieleza kuwa wanatambua na kuthamini mchango wa tiba asili kutoka Afrika.

 WHO ilieleza kwamba dawa hizo, pia zinapaswa kupewa nafasi sawa katika kufanyiwa majaribio, kama dawa kutoka maeneo mengine duniani.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger