Thursday, 26 March 2020

Matarajio ya Hali Mbaya ya Hewa kwa siku Tano

Mvua kubwa zinatarajiwa katika baadhi ya maeneo ya Ziwa Victoria, nyanda za juu kaskazini mashariki na maeneo ya kati ya nchi.



Share:

Mtuhumiwa Aliyemuua Binti Wa Kazi Kwa Kipigo Apandishwa Kizimbani Tena

Na Ahmed Mahmoud Arusha
Kesi ya mauaji namba 5 ya mwaka 2020 imekuja kutajwa tena kwa Mara ya pili Leo katika mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Arumeru.
Pichani ni mtuhumiwa wa kesi ya mauaji ya binti wa kazi akiingizwa kwa hakimu mkazi mfawidhi Analia Mushi kutajwa kwa kesi yake huku akijifunika uso gubigubi kama alivyokutwa na kamera ya matukio kwenye mahakama ya wilaya ya Arumeru leo jijini Arusha.Picha zote na Ahmed Mahmoud Arusha

Sehemu ya umati wa watu waliofuatilia kesi ya Mkami Shrima mshukiwa wa mauaji ya binti wa Kazi Marehemu Salome Zakaria
__________________

Hisia za wakazi wa Jiji la Arusha imewavuta kujazana mahakamani hapo kufuatilia kesi hiyo ambapo mtuhumiwa huyo Mkami Shirima alifikishwa mahakamani hapo kwa usiri mkubwa huku akiwa amejifunika gubigubi na mtandio wa dera.

Kesi hiyo ipo kwa hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Arumeru Analia Mushi ambapo imeelezwa kuwa mshtakiwa Mkami Shirima huko maeneo ya  Elkurei mnamo 3 Mwezi March alitenda kosa la kumpiga Mfanyakazi wake wa ndani  na kumsababishia kumuua Marehemu Salome Zakaria  akijua ni kosa kisheria.

Ilielezwa mahakamani hapo kwamba mnamo tarehe sita mwezi wa tatu huu huko maeneo ya mianzini mtuhimiwa Mkami Shirima alimpiga mfanyakazi wake Salome Zakaria ambaye ni marehemu kwa Sasa akijua ni kosa kisheria.

Hata hivyo kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 8 Mwezi wa nne mwaka huu itakapo kuja kutajwa tena na mtuhumiwa amerudishwa rumande gereza kuu la Kisongo.

Upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kesi hiyo itakuja kutajwa tena mbele ya hakimu mkazi mfawidhi Analia Mushi wa mahakama hiyo Mwezi ujao.




Share:

Job vacancies at Eyes Africa Limited

11 Job opportunities at Eyes Africa Limited Eyes on Africa is a Travel Company specializing in African Safaris and Travel to Africa. The company was created with the vision of sharing the wonders of the African continent with those who are eager to explore some of the world’s most magnificent areas…areas that combine pristine, natural beauty, incredible wildlife,… Read More »

The post Job vacancies at Eyes Africa Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Video Mpya : NYANDA MADIRISHA OBHADO - CORONA



Ni Kawaida ya Malunde 1 blog kukusogezea Nyimbo za wasanii wa Nyimbo za asili... Leo nakualika Kutazama Video ya Nyanda Madirisha Obhado  'Maliganya' kutoka Kahama Mkoani Shinyanga inaitwa Corona..

 Tazama video ya Nyanda Madirisha Obhado  'Maliganya' - Corona hapa chini
Share:

Job vacancies at Halotel Tanzania

Share:

MBOWE AJIWEKA KARANTINI BAADA YA MTOTO WAKE KUTHIBITIKA KUWA NA CORONA


Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amejiweka karantini siku chache baada ya kutangaza kuwa mwanaye Dudley amepata maambukizi ya Corona.

Mbowe amesema amejitenga na familia yake ambayo itakuwa karantini kwa wiki mbili, na hivi sasa yupo nyumbani Dodoma akisubiri majibu ya vipimo ili kufahamu kama naye ana Virusi hivyo.

Akiongea na Clouds Media Mbowe amesema tangu aonane na Dudley siku 12 zilizopita, amekutana na watu wengi hivyo ni jambo la kuomba Mungu asikutwe na Corona ili aliokutana nao pia wawe salama.

Aidha, Mbowe ameeleza kuwa mkakati wa pamoja unahitajika ili kukabiliana na mlipuko wa Corona ambao amesema ni suala ya kitaifa.


Share:

Chief of Party at DAI

Chief of Party   DAI is an international development company. For more than 45 years, we have worked on the frontlines of international development, tackling fundamental social and economic development problems caused by inefficient markets, ineffective governance, and instability. Currently, DAI is delivering results that matter in some 80 countries. Our development solutions turn ideas into impact by bringing… Read More »

The post Chief of Party at DAI appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

General Manager Technical at Jubilee Insurance

General Manager Technical   Jubilee Insurance Company of Tanzania is a top ranking insurance company operating in Tanzania. They wish to recruit the following personnel for their head office in Dar Es Salaam. GENERAL MANAGER TECHNICAL- RE ADVERTISED To be responsible for underwriting, claims and reinsurance for the company. To have in depth knowledge and practical experience in handling… Read More »

The post General Manager Technical at Jubilee Insurance appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Rais Magufuli Amteua Brigedia Jenerali Mbungo Kuwa Mkurugenzi Wa Takukuru

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amthibitisha Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) Brig. Jenerali John Mbungo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo baada ya kuokoa Shilingi Bilioni 8.8 za wakulima.

Rais Dkt. Maguguli Amechukua uamuzi huo baada ya kupokea ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) na ripoti ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mapema leo katika Ikulu ya Chamwino Jijini, Dodoma.


Share:

Rais Magufuli Asema Uchaguzi Mkuu wa Mwaka Huu Uko Palepale na Hauwezi Kuahirishwa

Rais Magufuli amesema uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu hautaahirishwa licha ya kuwepo kwa mlipuko wa virusi vya corona (Covid-19).

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Machi 26, 2020 wakati akipokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na ripoti ya Taasisi ya Kuzuna Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, Dodoma.

“Sisi tunaendelea kukutana, ndiyo maana hata Bunge linaendelea na vikao vyake, hata huko kwenye nchi zilizoathirika kabisa, mamilioni ya watu wamekufa kwa corona, bado mabunge yao na mabaraza ya madiwani yanakutana. Kazi lazima ziendelee.

“Na uchaguzi tutafanya, wapo wanaofikiri kwamba tutaahirisha, unafikiri nani anataka kukaa kwenye maofisi haya muda wote huo,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameeleza kushangazwa na mwandishi mmoja kuandika habari kwamba “Baraza la madiwani lafanya mkutano licha ya corona” na kuhoji kama mikutano ya aina hiyo imezuiwa.

Amesisitiza kwamba kazi lazima ziendelee kufanyika licha ya uwepo wa virusi hivyo na mikutano ya baraza la madiwani, Bunge na hata ile anayoifanya yeye itaendelea kufanyika kwa sababu ni sehemu ya kazi zao.


Share:

Rais Magufuli amtumbua balozi wa Tanzania Nchini Ethiopia

Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia kutokana na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Rais ameyasema hayo leo Ikulu ya Chamwino, Dodoma alipokuwa akizungumza baada ya kukabidhiwa ripoti za ukaguzi zilizoandaliwa na ofisi ya Madhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, pamoja na ripoti ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

“Mmetusaidia [TAKUKURU] kwa ripoti yenu kuhusu wizi wa mabilioni uliofanywa na ubalozi wetu wa Ethiopia, na balozi wa Ethiopia nimeshamrudisha, si balozi tena kule,” amesema Magufuli.

Amesema uamuzi huo uwe fundisho kwa watumishi wengine kwamba kiongozi akiharibu kwenye ofisi yake ajiandae kubeba msalaba.

Aidha, amewaomba viongozi wenzake kuitumia ripoti ya TAKUKURU ya mwaka unaoishia Juni 2019 kurekebisha yale yaliyotajwa, yakiwemo matumizi mabaya ya fedha za umma na manunuzi bila kuwa na mkataba.


Share:

Ripori Ya CAG Yabaini Ubadhirifu CUF, CCM

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, amebainisha ubadhirifu kwenye vyama vya siasa wakati akikabidhi ripoti za ukaguzi wa hesabu za Serikali na taasisi za umma kwa mwaka 2018/2019.

Akiwasilisha ripoti hiyo kwa Rais John Magufuli leo Alhamisi Machi 26, Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, CAG amesema katika ukaguzi ilibainika kuwa Chama cha Wananchi (CUF) kilipokea ruzuku ya Sh milioni 369.38 lakini Sh milioni 300 zilihamishwa kwenye akaunti ya chama na kuwekwa katika akaunti binafsi na Sh milioni 69 zilitolewa kama fedha taslimu.

Kichere amesema nyaraka za matumizi ya fedha hizo hazikuwasilishwa kwake kwa ajili ya ukaguzi.

“Nilibaini Sh milioni 47 zilitolewa kwenye akaunti ya chama bila idhini ya Katibu Mkuu wa chama kama ilivyoelekezwa katika kanuni za fedha za chama cha wananchi.

“Ninashauri mifumo ya udhibiti wa ndani ya chama cha CUF uboreshwe ili kuhakikisha matumizi yanazingatia kanuni zilizowekwa,” amesema CAG.

Aidha amesema alibaini Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ilimwondoa mpangaji bila kufuata taratibu na kusababisha mpangaji huyo kuonesha nia ya kufungua kesi ya madai na kutaka kulipwa fidia ya Sh milioni 800, hata hivyo jumuiya hiyo ililipa kiasi cha Sh milioni 60 kama fidia ya hasara baada ya mazungumzo ya kirafiki kufanyika na suala hilo kumalizika nje ya mahakama.


Share:

Communication Assistant at IITA

Communication Assistant   IITA-TZ2020-CRS-003-NRS-DSM Background: The International Institute of Tropical Agriculture (IITA) invites applications for the position of Communication Assistant. The International Institute of Tropical Agriculture (IITA) is a member of a world-wide network of International Agricultural Research Centers. IITA’s research focuses on smallholder cropping systems in sub-Saharan Africa. IITA has a regional hub in Dar es Salaam,Tanzania which… Read More »

The post Communication Assistant at IITA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Senior Governance Specialist – Public Sector at World Bank

Senior Governance Specialist – Public Sector Job #: req6758 Organization: World Bank Sector: Public Sector Development Grade: GG Term Duration: 2 years 0 months Recruitment Type: Local Recruitment Location: Dar Es Salaam,Tanzania Required Language(s): English, Swahili Preferred Language(s): Closing Date: 4/15/2020 (MM/DD/YYYY) at 11:59pm UTC Description We are on a mission to change the world; do you want to… Read More »

The post Senior Governance Specialist – Public Sector at World Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

RAIS MAGUFULI AMTEUA BRIGEDIA JENERALI MBUNGO KUWA MKURUGENZI WA TAKUKURU



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) Brig. Jenerali John Mbungo kuwa Mkurugenzi wa taasisi hiyo kwa kazi nzuri aliyoifanya ikiwemo ya kurejesha bilioni 8.8 walizodhulumiwa wananchi.

Rais amefanya uteuzi huo leo, Machi 26, 2020 katika hafla ya kupokea ripoti kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali CAG na ripoti ya TAKUKURU katika Ikulu ya Chamwino Jijini Dodoma.
Share:

Relationship Manager, Corporate Banking – Lake Zone – at NMB Bank

Relationship Manager, Corporate Banking – Lake Zone  Reporting Line: Functionally to Senior Manager, Corporate Banking and Administratively to Zonal Manager Location: Lake Zone Job Purpose To develop and maintain relationships with a portfolio of corporate clients within Lake Zone [Mwanza, Kagera , Mara & Geita Regions] , while developing, improving, promoting and selling NMB’s products and services to… Read More »

The post Relationship Manager, Corporate Banking – Lake Zone – at NMB Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

RAIS MAGUFULI : UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2020 HAUTAAHIRISHWA LICHA YA KUWEPO KWA CORONA

Na Peter Elias, Mwananchi 
 Rais John Magufuli amesema uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu hautaahirishwa licha ya kuwepo kwa mlipuko wa virusi vya corona.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Machi 26,2020 Ikulu ya Chamwino, Dodoma wakati akipokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na ripoti ya Takukuru.

Amesema baadhi ya watu wamekuwa wakifikiri kwamba kazi hazifanyiki na hakuna kukutana kwa sababu ya corona. Amesema hata nchi zilizoathirika zaidi na virusi hivyo, bado mabunge yao yanakutana kama kawaida.

"Sisi tunaendelea kukutana, ndiyo maana hata Bunge linaendelea na vikao vyake, hata huko kwenye nchi zilizoathirika kabisa, mamilioni ya watu wamekufa kwa corona, bado mabunge yao yanakutana. Kazi lazima ziendelee.

"Na uchaguzi tutafanya, wapo wanaofikiri kwamba tutaahirisha, nani anataka kukaa kwenye maofisi haya muda wote huo," amesema Rais Magufuli wakati akizungumza kwenye hafla ya kupokea ripoti hizo.

Rais Magufuli ameeleza kushangazwa na mwandishi mmoja kuandika habari kwamba "Baraza la madiwani lafanya mkutano licha ya corona" na kuhoji kama mikutano ya aina hiyo imezuiwa.

Amesisitiza kwamba kazi lazima ziendelee kufanyika licha ya uwepo wa virusi hivyo na mikutano ya baraza la madiwani, Bunge na hata ile anayoifanya yeye itaendelea kufanyika kwa sababu ni sehemu ya kazi zao.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger