Thursday, 30 January 2020

Senior Accountants at Air Tanzania Company Limited (ATCL) ( 4 posts)

Senior Accountants (4 Posts) Air Tanzania Company Limited (ATCL) is in the process of revamping its operations and has introduced new equipment to its fleet as part of implementation of its five years Corporate Strategic Plan (2017-2021). In line with this expansion, the company is also making some reforms in its structure, internal operations and staffing to accommodate business… Read More »

The post Senior Accountants at Air Tanzania Company Limited (ATCL) ( 4 posts) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Business Development Officer at World Vision

Business Development Officer Purpose of the position: Under the direction of the Business Development Manager, the Business development Officer will support the efforts of World Vision Tanzania to develop and diversify its sources of funding, including local resource mobilization. Program Development and Resource Acquisition Working with Business Development Manager, SMT and Technical Leads identify funding opportunities from Support… Read More »

The post Business Development Officer at World Vision appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MFANYABIASHARA KIZIMBANI KWA MASHITAKA 28 YA UHUJUMU UCHUMI


Mkurugenzi wa kampuni ya Jaluma General Supplies Limited,  Lucas Mallya  na wenzake wanane wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka 28 yakiwemo ya  kukwepa kodi na kuisababishia Serikali  hasara ya zaidi ya Sh31.57 bilioni.

Mbali na Mallya washtakiwa wengine ni Emmanuel Peter,  mkurugenzi wa Happy Imports Assosiates, Happy Mwamugunda; Prochesi Shayo; Prokolini  Shayo;  Godfrey Urio;  Nyasulu Nkyapi; Tunsubilege Mateni na Nelson Kahangwa

Akisoma mashtaka hayo jana Jumatano Januari 29, 2020 mbele ya Hakimu mfawidhi, Godfrey Isaya wakili wa Serikali, Faraja Ngukah alidai washtakiwa walitenda makosa hayo kati ya Januari Mosi, 2015 na Januari 7, 2020 maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.

Washitakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi.

Hata hivyo, upande wa mashtaka ulidai upelelezi wa kesi hiyo unaendelea hivyo, waliomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa na kukamilisha upelelezi.

Hakimu Isaya aliahirisha kesi hiyo hadi Fabruari 12, 2020 kwa ajili ya kutajwa na washtakiwa walipelekwa rumande kwa sababu mashtaka ya utakatishaji fedha hayana dhamana kisheria.


Share:

SHIRIKA LA AFYA ULIMWENGUNI, WHO LAITISHA KIKAO CHA DHARURA KUHUSU VIRUSI VYA CORONA

Shirika la afya ulimwenguni, WHO kwa mara nyingine linataraji kuitisha kikao cha kamati yake ya wataalamu baadae hii leo ili kujadiliana kuhusu iwapo wanaweza kutangaza mripuko wa virusi vya Corona kama dharura ya afya duniani.


Virusi hivyo tayari vimeshawaua watu zaidi ya 160 na zaidi ya watu 7, 711 wameambukizwa tangu kulipotambuliwa mgonjwa wa kwanza katika jiji la Wuhan nchini China, Disemba 31.

Mkurugenzi mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Gebreyesus, aliyerejea kutoka China amesema ilikuwa ni muhimu kuitisha mkutano mwingine, ambao ni wa tatu kwa wiki hii kwa kuwa virusi hivyo vimekwishasambaa hadi nje ya China, akisema ni hali inayozidi kutia wasiwasi.

 Nchi wanachama wa timu hiyo ya WHO iliamua wiki iliyopita kwamba janga hilo lilikuwa bado halijafikia kiwango cha kutangazwa dharura ya dunia. 

Hatua kama hiyo ilitangazwa na WHO wakati wa mripuko wa Ebola na mafua ya ndege.


Share:

Field Monitor at World Vision

Field Monitor Purpose of the position: To monitor the delivery, distribution, documentation and reporting associated with all commodities supported to refugees. Work hand in hand with relief committee members Observe mission and core values of World Vision and demonstrate a quality of spiritual life that is an example to others Major Responsibilities: Commodity management Ensure that all commodities… Read More »

The post Field Monitor at World Vision appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Community Help Desk at World Vision

Community Help Desk   Receiving, recording/documenting and responding to all complaints channeled via help desk Engage into daily pre-address speech Make a link between beneficiaries and Distribution staff. Record all complaints and feedback received related to World Vision programs, commitments or conduct, this can include Food, GBV, security, Peace building & Child protection related issues. Ensuring that, all complaints… Read More »

The post Community Help Desk at World Vision appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Administrative Assistant at World Vision

Administrative Assistant  Other Competencies/Attributes: Must be a committed Christian, able to stand above denominational diversities. Perform other People & Culture duties as required. Qualifications: Education/Knowledge/Technical Skills and Experience The following may be acquired through a combination of formal or self-education, prior experience or on-the-job training: Minimum Qualification required: Bachelor Degree in Human Resources, Public Administration or related field. Experience: 2 year… Read More »

The post Administrative Assistant at World Vision appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

BUNGE LA ULAYA LAPIGA KURA KURUHUSU UINGEREZA KUONDOKA EU


Wabunge wa bunge la Umoja wa Ulaya wamepitisha kwa wingi sheria inayoruhusu Uingereza kuondoka kwenye Umoja huo ama Brexit, wiki hii na kuondoa kizingiti kikubwa cha mwisho kabla Brexit yenyewe kufanyika. 

Bunge hilo limepiga kura ya kuyapitisha makubaliano ya Brexit kwa kura 621 dhidi ya 49 ambao walipinga. 

Kulitakiwa wingi mdogo wa kura kwenye bunge hilo lenye wabunge 75. 

Nchi wanachama hivi sasa wanatakiwa kutoa idhini ya mwisho kwenye makubaliano hayo kupitia utaratibu wa maandishi. 

Uingereza inataraji kuondoka Umoja wa Ulaya usiku wa kuamkia Ijumaa, baada ya miaka mitatu tangu Waingereza walipoanzisha mchakato wa kuondoka ama kusalia kwenye Umoja huo, katika kura ya maoni ya mwaka 2016.


Share:

Information,Communication & Technology Officer at World Vision

Information,Communication & Technology Officer   Purpose of the position: To ensure effective and efficient implementation of all network/ system applications and hardware maintenance for smooth running of ICT operations Communicate World Vision’s Christian ethos and demonstrate a quality of spiritual life that is an example to others. Maintain ICT infrastructure in line with partnership guidelines within the office Facilitate… Read More »

The post Information,Communication & Technology Officer at World Vision appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Nutrition Offic at World Vision

Nutrition Officer   Purpose of the position To facilitate effective implementation of Burundian Refugee Supplementary Program targeting children under five, Pregnant and Lactating Women (PWL) and vulnerable groups; the project aims to stabilize and improve the nutritional status of Nduta and Mtendeli refugee Camps Ensure that district health management team, DNuOs, health care providers and community volunteers trained on… Read More »

The post Nutrition Offic at World Vision appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Head, Priority Banking at Standard Chartered

Head, Priority Banking Job: Retail Banking Primary Location: Africa & Middle East-Tanzania-Dar es Salaam Schedule: Full-time Employee Status: Permanent Posting Date: 29/Jan/2020 Unposting Date: 13/Feb/2020 About Standard Chartered  We are a leading international bank focused on helping people and companies prosper across Asia, Africa and the Middle East. To us, good performance is about much more than turning a… Read More »

The post Head, Priority Banking at Standard Chartered appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MAALIM SEIF KUCHUKUA FOMU YA KUGOMBEA NAFASI YA UONGOZI KATIKA CHAMA CHA ACT- WAZALENDO

Kama inavyofahamika, Chama cha ACT Wazalendo tayari kimetangaza rasmi kuanza kwa Uchaguzi wa Viongozi wa Kitaifa ndani ya Chama baada ya kukamilika chaguzi katika ngazi za chini. 


Shughuli ya kuchukua na kurejesha fomu kwa nafasi mbali mbali za uongozi katika ngazi ya Taifa imetangazwa kufanyika kuanzia tarehe 27 Januari hadi 26 Februari, 2020.

Kwa taarifa hii, tunawajulisha kuwa leo siku ya Alkhamis, tarehe 30/01/2020 saa 5.00 asubuhi Maalim Seif Sharif Hamad anatarajia kuchukua fomu ya kugombea nafasi mojawapo kati ya nafasi za uongozi zilizotangazwa kugombewa katika Chama Cha ACT Wazalendo. Shughuli hiyo itafanyika Ofisi Ndogo ya Chama iliyopo Vuga, Zanzibar.

Kwa taarifa hii, ndugu waandishi wa habari mnaalikwa rasmi kushuhudia tukio hilo la uchukuaji wa fomu.

 Maalim Seif pia anatarajia kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu dira na mwelekeo wake juu ya nafasi ya uongozi anayokusudia kuiomba katika Chama.

Nyote mnakaribishwa.

Imetolewa na;
Ofisi ya Maalim Seif Sharif Hamad
30/01/2020


Share:

AFISA USALAMA WA TAIFA FEKI AKAMATWA AKITAPELI WATUMISHI HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA SHINYANGA

                                      Sheliku Sweya
                      Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Rufaa mkoa wa Shinyanga Dk. Rose Malisa amenusurika kutapeliwa na mwanaume aitwaye Sheliku Sweya (45)ambaye alijifanya kuwa ni ofisa usalama wa taifa akimtaka ampe rushwa ya ngono ili amsaidie kutatua changamoto zilizopo hospitalini huku Dk. Geofrey Mboye akitapeliwa Sh 300,000 ili asaidiwe kupata uhamisho wa kwenda mkoani Dodoma.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari juzi,Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga Debora Magiligimba alisema baada ya kupata taarifa hizo waliweka mtego na kufanikiwa kumkamata Januari 23,2020, ambapo katika uchunguzi wa awali wamebaini mtuhumiwa siyo ofisa usalama wa taifa bali amekuwa akitumia cheo hicho kujipatia kipato au rushwa ya ngono ili kufanikisha malengo yake.

Alisema madaktari wote ni watumishi katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga ambapo Dk .Malisa ambapo alielezwa kuwa iwapo atatoa rushwa ya ngono atapatiwa vifaa tiba na kuongezewa watumishi wa afya ikiwa ni pamoja na kumuahidi kumfutia deni kiasi cha Shilingi milioni 40  anazodaiwa na taasisi ya afya alikopatia masomo yake ya udaktari bingwa wa magonjwa ya akina mama.

"Kutokana na ushirikiano mkubwa uliofanyika na Dk.Malisa tuliweka mtego na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa kabla hajafanikiwa kupata rushwa ya ngono,anaendelea kuhojiwa na jeshi la polisi na atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika",alisema kamanda Magiligimba.

Katika maelezo yake polisi Dk. Rose Malisa alieleza kuwa alimtilia mashaka mtuhumiwa na kutoa taarifa polisi ambao walishirikiana ikiwa ni pamoja na kuweka mtego ambao ulisaidia kufanikiwa kumkamata mtu huyo aliyejifanya ofisa usalama wa taifa ili kufanikisha malengo yake.
Share:

Kagame: Sitashurutishwa kufungua mpaka na Uganda


Rais wa Rwanda Paul Kagame, alisema Jumatano kwamba serikali yake itafungua mpaka na Uganda wakati itajihisi kufanya hivyo akisisitiza kwamba hakuna mtu wala nchi yoyote itamshurutisha kufanya hivyo.

Akihutubia mabalozi katika mkutano wa kila mwaka na waakilishi wa nchi za nje pamoja na mashirika ya kimataifa katika ikulu ya raia mjini Kigali, Kagame alizungumzia swala la Uganda na Rwanda, akigusia kwamba maafisa wake wanajitayarisha kwa mkutano wa Angola kuzungumzia uhusiano kati ya nchi hizo mbili.

Hata hivyo, rais huyo alisisitiza kwamba hakuna litakalobadilika iwapo matakwa ya Rwanda hayatazingatiwa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu ya rais mjini Kigali, iliyowekwa kwenye ukurasa wa twitter wa serikali ya Rwanda, rais Kagame amesema mgogoro wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili, ni jirani wake Uganda akielezea kwamba tatizo lililopo ni kubwa kuliko kufungwa kwa mpaka kama inavyoripotiwa.

“Hata iwapo tunafungua mpaka wa Rwanda na Uganda, swala kuu ni kukamatwa na kuzuiliwa kwa raia wetu nchini Uganda”, amesema rais Kagame.

Mwezi Desemba mwaka uliopita 2019, Uganda iliachilia huru raia kadhaa wa Rwanda, waliokuwa wanazuiliwa kwa maadai ya kuifanyia Rwanda ujasusi.

“Swala hili sio la kufunga wala kufungua mpaka. Ni swala la raia wetu kukamatwa wakiwa Uganda. Tumefunga mpaka kwa sababu hatutaki raia wetu kuingia Uganda kwa sababu watakamatwa. Lakini raia wa Uganda wapo huru kuingia Rwanda”, aliendelea kusema rais Kagame.

Uganda imekuwa ikikanusha madai ya kuakamata raia wa Rwanda wanaotii sheria, ikisisitiza kwamba wanaokamatwa wanashukiwa kufanya uhalifu.

Kagame alitaja hatua ya Uganda ya kuachilia huru raia wa Rwanda kuwa nzuri lakini akawa mwepesi wa kuongezea kwamba haitoshi na kwamba ni idadi ndogo sana ya raia wa Rwanda waliachiliwa huru, akidai kwamba raia wawili wa Rwanda walikufa wakiwa kizuizini Uganda kutokana na mateso.

Kagame pia alisema kuongoza jumuiya ya Afrika mashariki ni kazi ngumu sana kuliko kuongoza umoja wa Afrika – AU.

“Na wakati haya yote yanaendelea, tunazungumza sana kuhusu ushirikiano katika jumuiya ya Afrika mashariki. Tutaendelea tu kuzungumza kuhusu ushirikiano huo bila mafanikio kama tunayofanya ni tofauti na tunayosema. Tunastahili kufanya yaliyo sawa”, aliendelea kusema Kagame.

Rwanda inaishutumu Uganda kwa kuunga mkono makundi ya wapiganaji yenye lengo la kupindua serikali ya Kagame, kuwakamata raia wa Rwanda, na kuhujumu uchumi wake.

Rwanda imeweka marufuku ya biashara na kufunga mpaka wake na Uganda tangu Februari mwaka uliopita 2019 na kuwaonya raia wake kutoingia Uganda.

Uganda nayo inaishutumu Rwanda kwa kuiwekea marufuku ya kibiashara, kufanya upelelezi dhidi ya serikali ya rais Yoweri Museveni kwa lengo la kutatiza usalama wake, kuwafuta kazi maafisa wa ngazi ya juu raia wa Uganda waliokuwa wakifanya kazi Rwanda na kueneza habari za chuki dhidi ya Uganda na maafisa wake serikalini.

Rwanda imekuwa na uhusiano mbaya na majirani wake Burundi na Uganda, huku Burundi ikiishutumu kwa kuyapatia silaha makundi yanayopinga utawala wa rais Piere Nkurunziza na kupanga njama za kuangusha utawala wake katika mapinduzi yaliyofeli ya mwaka 2015.

Uganda imekataa kuzungumzia mgogoro wake na Rwanda katika vyombo vya habari.


VOA





Share:

Eneo kubwa linauzwa: Mapinga(Bagamoyo) ......Bei ni Nzuri Kabisa

Eneo kubwa linauzwa: Mapinga(Bagamoyo)

 Eneo kubwa la ekari 5 linauzwa bei nafuu sana. Eneo linafaa kwa uwekezaji wa shule, hospitali, chuo, yard, kiwanda n.k
Eneo liko sehem nzuri, yenye view nzuri na barabara ya uhakika.


Umbali kutoka Bunju  ni 5km

Bei ya kila ekari moja ni tsh 20 mil fixed.

Call 0758603077


Share:

Waziri Ummy: Tanzania Haina Mgonjwa Wa Corona

Na. WAMJW-Dodoma
Mpaka sasa Tanzania haina Mgonjwa wala muhisiwa wa ugonjwa unaosababishwa na kirusi cha Coromna (Hona kali ya mafua) hata hivyo kutokana na mwingiliano mkubwa uliopo hasa kibiashara na kijamii kati ya Tanzania na nchi za bara la Asia ikiwemo nchi ya China nchi inakuwa katika hatari pia ya ugonjwa huo.

Haya yamesemwa jana na Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati akitoa tarifa kwa umma kuhusu mwenendo wa ugponjwa huo jijini hapa.

“Ugonjwa huu unasababiswa na kirusi jamii ya Corona na ni kipya “Novel (New) Corona virus 2019” (2019-nCOV) ambacho ni tofauti na virusi vingine vya jamii hiyo ambavyo viliwahi kusababisha milipuko ya ugonjwa uliojulikana kama ‘SARS-CoV’ mwaka 2003 na MERS-CoV Corona Virus mwaka 2013”.Amesema Waziri Ummy.

Aidha, waziri Ummy amesema ugonjwa huo huambukizwa kwa njia ya hewa kwa kuingiwa na majimaji yenye virusi kutoka mtu mmoja kwa njia ya kukohoa au kupiga chafya au kwa kugusa majimaji au makamasi kutoka kwa mgonjwa aliyethibitishwa kuwa na dalili za ugonjwa huo na dalili huanza kuonekana kati ya siku moja hadi kumi na nne tangu kupata maambukizo.

Hata hivyo ametaja dalili za ugonjwa huu ni pamoja na Homa, mafua, kuumwa kichwa, mwili kuchoka, kikohozi, kubanwa mbavu, maumivu ya misuli, vidonda vya koo, mapafu kuathirika, kupumua kwa shida na hata kifo.

“Ugonjwa huu hauna chanjo wala tiba ya moja kwa moja, hivyo kama yalivyo magonjwa mengine yanayosababishwa na virusi, matibabu hufanyika kwa kuzingatia dalili zilizopo na ufuatiliaji wa karibu” Amesisitiza Waziri Ummy.

Wakati huo huo waziri huyo amewashauri wananchi kuchukua hatua ili kujikinga na ugonjwa huo ikiwemo kuzingatia kanuni za afya na usafi ikiwa ni pamoja na kukaa mbali na mtu mwenye dalili za mafua mwenye historia ya kusafiri katika nchi zilizokumbwa na mlipuko na kufunika mdomo na pua wakati wa kukohoa kwa kitambaa safi au nguo uliyovaa sehemu za mikono

“Kutokana na mwenendo na kasi ya kusambaa kwa ugonjwa huo kipindi hiki cha mlipuko, Wizara inashauri kusubiri na kuepuka safari zisizo za lazima kwenda kwenye maeneo yaliyoathirika na inapolazimu kusafiri basi


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi January 30



















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger