Wednesday, 29 January 2020

Sales Executive at Park Hyatt

Sales Executive   Come and join us in our journey as we care for people so they can be their best! We believe that being your best is about being your true self – engaged, fulfilled and ready to take on the world. Sitting majestically on the beachfront in the heart of Stone Town, a designated UNESCO heritage site,… Read More »

The post Sales Executive at Park Hyatt appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Yasemavyo Magazeti Ya Kenya Leo Jumatano January 29

1. People Daily
Jumatatu, Januari 27, Rais Uhuru alifanya mkutano na naibu wake William Ruto katika Ikulu, jijini Nairobi na kumuelezea mikutano tofauti ya BBI inayopangwa na wandani wa Ruto.

Huku akimsomea Ruto hatia ya ghasia, Kiongozi wa Taifa alisema hakuridhishwa na mipango ya wapinzani wake kutaka kusambaratisha juhudi zake kuwaunganisha Wakenya kupitia BBI ambayo ni matunda ya handisheki ya mwezi Machi 9, 2018.

2. Taifa Leo
Gavana wa Kiambu, Ferdinand Waititu mnamo Jumanne, Januari 29, aliwaduwaza Maseneta baada ya kuonekana kumkana Susan Wangari Ndung'u kuwa mkewe. Waititu na mke wake Wangari walituhumiwa na ufisadi na walitolewa madarakani na bunge la kaunti lake

3. The Star
Mwanamume mmoja kutoka kaunti ya Busia amewaomba polisi kumsaidia kumtafuta mwanawe ambaye anaripotiwa kuuzwa KSh 18,000 na mke wake. Benard Ojiambo Oduori anaamini kuwa mke wake alimuuzia dada yake mtoto huyo ambaye ni tasa jijini Nairobi mnamo Desemba mwaka jana wakati malaika huyo alikuwa na wiki mbili.
 
4. The Standard
Wanasiasa kutoka Chama cha ODM kinachoongozwa na Raila Odinga, wamedai kuwa wabunge wa mrengo wa Tangatanga wamebuni njama ya kumwondoa Rais Uhuru Kenyatta madarakani. Kikosi hicho cha Raila kilisema Ruto aliwaagiza wandani wake kuanza kukusanya saini ili kuwasilisha mswada huo bungeni.

5. Daily Nation
Hatma ya Gavana wa Kiambu, Ferdinand Waititu itaamuliwa hii leo na maseneta ambao wataunga mkono ama kupinga uamuzi wa madiwani.

-TukoKenya


Share:

Mo Dewji akutana na Rais wa FIFA na kufanya naye mazungumzo

Wakati Simba ikitarajiwa kushuka dimba la Taifa leo saa moja usiku kuikaribisha Namungo FC kwenye mechi ya Ligi Kuu Bara, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya klabu hiyo, Mohamed 'Mo' Dewji, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (Fifa), Gianni Infantino

Katika mazungumzo yao, wawili hao waligusia mipango ya Fifa kuendeleza soka barani Afrika, Dewji akieleza matumaini yake juu ya maendeleo ya mpira wa miguu barani katika uongozi wa Infantino.

"Kwa kweli, nimefurahishwa sana kwa dira na shauku ya kuendeleza mpira wa ushindani na shauku Afrika. Nia ya Fifa ni kuboresha maendeleo ya mpira.

"Najua chini ya uongozi wa Gianni, mpira wa miguu kwenye bara letu, utapiga hatua zaidi," Dewji alieleza baada ya mazungumzo yake na bosi huyo wa Fifa.

Aidha, Dewji alimkabidhi Infantino jezi ya Simba ikiwa imeandikwa jina la rais huyo ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kupiga vita rushwa michezoni na ufujaji wa fedha uliokuwa ukifanywa ndani na nje ya shirikisho hilo kwa wanachama wake.

Dewji, mmoja wa mabilionea vijana barani Afrika, ameifanya Simba kuwa miongoni mwa klabu zinazoendeshwa kwa kisasa Afrika na sasa inatajwa kama timu inayotarajiwa kuwa tishio ndani ya miaka michache ijayo barani Afrika.


Share:

Waziri Kairuki Atikisa Wilaya 6 Za Mkoa Wa Pwani, Awahakikishia Wawekezaji Mazingira Mazuri Ya Uwekezaji.

NA. MWANDISHI WETU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Uwekezaji nchini Mhe. Angellah Kairuki amewahakikishia wafanyabiashara na Wawekezaji kuwa Serikali itaendelea kuwawekea mazingira mazuri ya Uwekezaji nchini.

Pia, Amesema Serikali imejipanga kuboresha mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara na wawekezaji ili kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kwa kuwekeza katika sekta mbalimbali zenye tija katika kuliingizia pato taifa.

Ameyasema hayo hivi karibu alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku 6 katika Wilaya 6 za mkoa wa Pwani ikiwemo; Bagamoyo, Kibaha, Kisarawe, Mkuranga, Mafia na Rufiji pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze.

Akieleza lengo la ziara hiyo Mhe.Kairuki amesema mkoa wa Pwani ni miongoni mwa mikoa yenye uwekezaji mkubwa katika sekta mbalimbali; Uvuvi, kilimo na ufugaji na amefanya  ziara hiyo ili kujionea mazingira  pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Akitoa majumuisho ya ziara hiyo Mhe. Kairuki amezitaja changamoto zilizojitokeza katika maeneo mengi aliyotembelea kuwa ni ukosefu wa maji ya kutosha, ubovu wa barabara, ucheleweshwaji wa vibali vya kazi, kukosa umeme wa uhakika na utitiri wa tozo.

Mbali ya changamoto hizo, Mhe. Kairuki ametaja vikwazo vingine kuwa ni kutotengwa kwa maeneo ya uwekezaji, Taasisi wezeshi kutokuwa karibu na wawekezaji, ukosefu wa mitaji ya uhakika na utoaji wa adhabu zisizo za lazima.

Ameongeza kuwa uelewa mdogo wa wawekezaji katika kujiunga na Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC) ni moja ya  changamoto na kuwataka  wawekezaji kwa hiari yao waone umuhimu wa kujiandikisha katika kituo hicho ili kutumia fursa zinazopatikana.

“Wawekezaji tunawakaribisha TIC ili mjue fursa ziliopo nchini zaidi na kuona namna mnavyoweza kunufaika na kituo hiki,”alisisitiza Waziri Kairuki.

Ameongoza kuwa, ipo haja ya kila Halmashauri kuendelea kutenga maeneo ya uwekezaji ili kutoa fursa zaidi kwa watu kuwekeza na kuhakikisha miundombinu muhimu inakuwepo.

“Natoa rai kwa kila Halmashauri kuhakikisha kila kijiji kinatenga walau heka 20 za maeneo ya uwekezaji na kuwasilisha taarifa zao TIC” alisema Waziri.

Aidha, Waziri Kairuki amewataka wawekezaji kuzingatia sheria na taratibu za uwekezaji nchini ili waweze kunufaika na mitaji yao waliyowekeza.

“Endeleeni kuwekeza pasipo kuvunja sheria na kanuni zilizopo ikiwa ni kulipa kodi au kulipa vibali mbalimbali mfanye hivyo tena kwa wakati ili isitokee mmewekeza kwa mitaji mikubwa halafu ikawa kwa hasara,”alisisitiza Waziri Kairuki

Aliwahakikishia wawekezaji kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano, inatambua mchango wao na imedhamiria kuhakikisha inaboresha miundombinu muhimu ikiwemo uwepo wa nishati ya umeme ya uhakika, barabara bora, upatikanaji wa maji safi, kuboresha mifumo ya mawasilino na upatikanaji wa huduma bora za mamlaka zinazosimamia masuala yanayohusu uwekezaji nchini.


Share:

LIVE: Mkutano Wa Kumi Na Nane - Kikao Cha Pili: Tarehe 29 Januari, 2020 - Asubuhi

RATIBA:

I. DUA
II. HATI ZA KUWASILISHA MEZANI
   - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMUYA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI
 
III. MASWALI
  - OFISI YA RAIS (TAMISEMI)
  - WIZARA YA MAJI
  - WIZARA YA NISHATI
  - WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI
  - WIZARA YA KILIMO
  - WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  - WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
  - WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA
  - WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII
  - WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
 
IV. HOJA ZA KAMATI
  - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI
  - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI ZA MITAA


Share:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Yatoa Tahadhari ya Mvua Kubwa

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari kwa wananchi wanaoishi katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, Kaskazini na Kanda ya Kati kukumbwa na mvua kubwa kwa siku tano mfululizo. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na mamlaka hiyo, mvua hizo zinatarajia kunyesha katika mikoa ya Mwanza, Simiyu, Shinyanga, Mara, Kagera, Geita na Tabora kwa Kanda ya Ziwa.

Mikoa ya Kanda ya Kati itakayokumbwa na mvua hizo ni Singida na Dodoma huku mikoa ya Kanda ya Kaskazini ikiwa Kilimanjaro, Arusha na Manyara.

Sambamba na mikoa hiyo, taarifa hiyo ilisema mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ambayo ni Rukwa, Iringa, Mbeya na Njombe pia itakumbwa na mvua hiyo.

Aidha, taarifa hiyo ilieleza kuwa mvua hizo zinatarajia kusababisha uharibifu wa miundombinu na mali kwa baadhi ya maeneo pamoja na makazi kuzungukwa na maji.

"Athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua hizo ni baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, ucheleweshwaji wa usafiri na kusimama kwa muda kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi na kijamii," ilisema taarifa hiyo.

Kutokana na hatari hiyo, TMA imewatahadharisha wananchi wanaoishi katika mikoa hiyo, kuchukua tahadhari mapema pamoja na kujiandaa.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano January 29






















Share:

Tuesday, 28 January 2020

Mganga Wa Kienyeji Ahukumiwa Kifungo Cha Maisha Jela Kwa Kumbaka Mtoto wa Miaka 8

Mahakama ya Wilaya Kigoma Mkoa wa Kigoma imemhukumu mganga wa kienyeji, Venas Edward (48), mkazi wa Ujiji Manispaa ya Kigoma/Ujiji kutumikia kifungo cha maisha jela kwa kosa la kumnajisi mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minane

Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Katoki Mwakitalu, baada ya upande wa mashtaka kuthibitisha kosa hilo pasipokuacha shaka yoyote.

Hakimu Mwakitalu alisema katika kesi hiyo upande wa mashtaka ulikuwa ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Raymond Kimbe, na ulipeleka mashahidi wanne na kielelezo kimoja ambacho ni PF3.

Alisema mama wa mtoto huyo alimpeleka mtoto wake nyumbani kwa mshtakiwa kwa ajili ya kutibiwa, na baada ya kumfikisha, mganga alimtuma mama huyo aende dukani kununua wembe.

Alisema baada ya mama kwenda dukani, mshtakiwa alimfanyia mtoto huyo kitendo hucho cha kikatili.

Alieleza kuwa baadaye mama wa mtoto huyo alifika kutoka dukani na kumchukua mtoto wake na kurudi nyumbani kwake.

Alieleza zaidi kuwa baada ya muda mama alisikia mtoto wake analalamika kusikia maumivu sehemu zake za siri, ndipo mama alipomkagua na kugundua kuwa mtoto wake alikuwa amenajisiwa.

Aliendelea kueleza kuwa mama wa mtoto huyo alimbana mtoto wake kwa kumuuliza ni nani aliyekufanyia kitendo hicho ndipo alimjibu kuwa ni mshtakiwa.

Mshtakiwa huyo baada ya kuhukumiwa kwenda jela maisha, aliangua kilio hadharani na kusababisha ndugu zake nao kuanza kuangua vilio mahakamani mbele ya umati uliofika mahakamani kwa ajili ya kusikiliza hukumu hiyo.

Awali akisoma hati ya mashtaka Wakili Kimbe alidai kuwa Aprili 23, mwaka 2019 majira ya asubuhi eneo la Kasoko Ujiji, mshtakiwa alinajisi mtoto huyo na kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri.


Share:

Administrative Assistant Job at World Vision Tanzania

Administrative Assistant Job at World vision Tanzania 15685-12N01018 AfricaTanzania Kigoma Administrative Services Fixed term, Full-time Deadline : 08-Feb-20 International Role – No – Only National applicants will be considered. Other Competencies/Attributes: Must be a committed Christian, able to stand above denominational diversities. Perform other People & Culture duties as required. Qualifications: Education/Knowledge/Technical Skills and Experience The following may… Read More »

The post Administrative Assistant Job at World Vision Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

klabu ya yanga yaitisha mkutano wa dharura kwa wanachama wake




Share:

Kilichoendelea Mahakamani Katika Kesi ya Mume Anayetuhumiwa Kumuua Mkewe kwa Kumchoma Moto

Upande wa utetezi katika kesi inayomkabili Mfanyabishara Hamisi Luongo anayetuhumiwa kumuua Mkewe na kumchoma kwa gunia la mkaa, umeutaka upande wa mashtaka kukamilisha uchapishaji wa jarada la kesi hiyo ya mauaji ili shauri liendelee.

Hayo yamebainishwa na upande wa utetezi, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Salum Ally baada ya Wakili wa Serikali, Janeth Magoho kuieleza Mahakama ya Kisutu kuwa jarada halisi la shauri hilo lipo Polisi kwenye hatua ya kuchapwa.

“Shauri lilikuja kwa ajili ya kutajwa lakini jarada halisi lipo polisi kwenye hatua ya uchapishaji hivyo naiomba Mahakama hii iahirishe kesi hii”- Magoho.

Baada ya maelezo hayo Hakimu Ally ameahirisha kesi hiyo hadi February,2020 litakapokuja kwa ajili ya kutajwa.


Share:

Business Development Officer Job at World vision Tanzania

Business Development Officer Job at World vision Tanzania 15686-12N01018 AfricaTanzania Dar es Salaam Administrative Services Fixed term, Full-time Deadline 08-Feb-20 International Role – No – Only National applicants will be considered. Purpose of the position: Under the direction of the Business Development Manager, the Business development Officer will support the efforts of World Vision Tanzania to develop and… Read More »

The post Business Development Officer Job at World vision Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH)

DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) TANZANIA COMMISSION FOR SCIENCE AND TECHNOLOGY (COSTECH) Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) began operations in 1986 and since then, it has been the principal advisory organ of the government on all matters relating to science, technology and innovation (STI). It is… Read More »

The post DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Citizen Voice & Action Officer Job at World vision Tanzania

Citizen Voice & Action Officer Job at World vision Tanzania   15687-11N29007 AfricaTanzania Tanga Support Services Application Deadline 03-Feb-20 International Role – No – Only National applicants will be considered. Purpose of the position: To enhance World Vision Tanzania’s role in empowering communities to effectively demand for improved services on issues related to climate change and natural resources… Read More »

The post Citizen Voice & Action Officer Job at World vision Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH)

DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) POST DETAILS POST DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – 1 POST POST CATEGORY(S) IT AND TELECOMS EMPLOYER Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) APPLICATION TIMELINE: 2020-01-27 2020-02-09 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES (i)To promote knowledge sharing through the organization’s and strengthen links… Read More »

The post DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

TCRA kuja na msako kwa waliowasajilia wenzao laini za Simu

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na watoa huduma, imetangaza kufanya uhakiki wa laini zote za simu zilizosajiliwa ili kuondoa wale waliosajili kwa kutumia kitambulisho cha mtu mwingine.

Pia uhakiki huo utawahusu wale waliosajili laini zao kwa kutumia kitambulisho tofauti ambao wote watachukuliwa hatua za kisheria.

Kwa mujibu wa tangazo la mamlaka hiyo, TCRA imeamua kufikia uamuzi huo ili kujiridhisha waliosajili laini zao za simu kwa kutumia kitambulisho sahihi.

Katika tangazo hilo, TCRA ilisema kuwa kwa kushirikiana na watoa huduma itafanya uhakiki huo.

"Kusajili laini ya simu kwa kutumia kitambulisho cha mtu mwingine ni kosa sanjari na kupewa laini iliyojasiliwa na mtu mwingine.”
 
Tangazo hilo limesema kuwa onyo na tahadhari zitaendelea kutolewa kwa makundi yote yanayohusika na usajili wa laini hizo.

“Kwa waliositishiwa huduma za laini zao za simu kuanzia Januari 20, wanaweza kuendelea na utaratibu wa usajili kwa lengo la ama kurudisha laini hizo zilizofungwa kama zitakuwa bado zipo au kupata mpya, mchakato huu ni endelevu,” sehemu ya tangazo hilo ilisema.

Pia tangazo hilo linasema watumiaji au waombaji wapya wa laini za simu wataendelea kusajiliwa muda wowote kwa kutumia kitambulisho cha Taifa na kuhakikiwa kwa alama za vidole.


Share:

LIVE: Rais Magufuli Akipokea Hati Za Utambulisho Wa Mabalozi – Ikulu DSM

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anapokea hati za utambulisho wa Ubalozi kutoka katika Mabalozi wateule tisa (9) walioteuliwa na kuziwakilisha Nchi zao hapa Nchini. Wanaowasilisha ni pamoja na -:

1. Mhe. Maria Amelia Mario De Paiva – Balozi mteule wa Ureno nchini mwenye makazi yake Nchini Msumbiji

2. Mhe. Douglas Foo Peow Yong – Balozi mteule wa Singapore nchini mwenye makazi yake Nchini Singapore

3. Mhe. Alex G. Chua – Balozi mteule wa Ufilipino nchini mwenye makazi yake Nchini Kenya

4. Mhe. Angela Veronica Comfort – Balozi mteule wa Jamaica nchini mwenye makazi yake Nchini Afrika Kusini

5. Mhe. Dkt. Christian Fellner – Balozi mteule wa Austria nchini mwenye makazi yake Nchini Kenya

6. Mhe. Fransisca Ashiete Odunton – Balozi mteule wa Ghana nchini mwenye makazi yake Nchini Kenya

7. Mhe. Jesus Agustin Manzanila Puppo – Balozi mteule wa Venezuela nchini mwenye makazi yake Nchini Kenya

8. Mhe. Yacin elmi Bouh – Balozi mteule wa Djibouti nchini mwenye makazi yake Nchini Kenya

9. Mhe. Oded Joseph – Balozi mteule wa Israel nchini mwenye makazi yake Nchini Kenya

Hafla inayofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam Januari 28, 2020


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger