Tuesday, 28 January 2020

Ndege ya Kijeshi ya Marekani Yaanguka Afghanistan....Taliban Yadai Kuipiga Kombora, Marekani Yakanusha

Jeshi la Marekani limekiri  kuanguka kwa Ndege yake moja  ya kijeshi  katika eneo la Deh Yak, jimbo la Ghazni huko Afghanistan lakini limekanusha vikali madai kwamba ndege hiyo imedunguliwa na Wapiganaji wa Taliban.

"Wakati tukiendelea na uchunguzi wa ajali hii, hadi sasa hakuna viashiria vyovyote vinavyoonesha kwamba ndege  yetu iliangushwa kwa Kombora " Amesema msemaji wa Jeshi la Marekani Col. Sonny Leggett

Awali, Waziri wa Ulinzi wa Marekani alikataa kutoa maelezo kuhusiana na ndege ya nchi hiyo iliyoanguka nchini Afghanistan.

Mark Esper aliwaambia waandishi wa habari kwamba, anazo habari kuhusu tukio hilo lakini kwa sasa hawezi kutoa maelezo zaidi. 


Duru za kuamininika zinasema kuwa, ndege hiyo ilikuwa aina ya  Bombardier E-11A na kwamba ilikuwa ikiunganisha mawasiliano baina ya ndege zisizo na rubani za Marekani katika kanda hii.

Kijiji ambacho ndege hii imeanguka, kusini magharibi mwa mji mkuu Kabul, ni eneo lenye idadi kubwa ya kundi la Taliban. 


Msemaji wa kundi la Taliban, Zabihullah Mujahid amesema kuwa, ndege hiyo iliyotunguliwa ilikuwa na askari wa Marekani waliokuwa katika operesheni ya ujasusi kwenye anga ya mkoa wa Ghazni.

Mujahid ameongeza kuwa, ndege hiyo imetunguliwa na wapiganaji wa Afghanistan na kwamba ilikuwa na maafisa kadhaa wa ngazi za juu wa shirika la ujasusi la Marakeni, CIA.

Taarifa iliyotolewa na kundi la Taliban imesema watu waliokuwemo katika ndege hiyo ya jeshi la magaidi wa Marekani wakiwemo maafisa wa CIA wameaga dunia




Share:

Jobs at World vision Tanzania 2020

Citizen Voice & Action Officer Job at World vision Tanzania   15687-11N29007 AfricaTanzania Tanga Support Services Application Deadline 03-Feb-20 International Role – No – Only National applicants will be considered. Purpose of the position: To enhance World Vision Tanzania’s role in empowering communities to effectively demand for improved services on issues related to climate change and natural resources… Read More »

The post Jobs at World vision Tanzania 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

LIVE: Bunge La 11 Mkutano Wa 18 Kikao Cha Kwanza Jijini Dodoma

LIVE: Bunge La 11 Mkutano Wa 18 Kikao Cha Kwanza Jijini Dodoma


Share:

Macho Yote ya Watanzania leo ni Kwa Mbwana Samatta!!

Macho Yote ya Watanzania leo ni Kwa Mbwana Samatta  wakati atakaposhuka dimbani majira ya saa 4:45 usiku kuichezea timu yake mpya ya Aston Villa kwa mara ya kwanza, kwenye mechi ya Kombe la Ligi dhidi ya Leicester City katika Uwanja wa Villa Park.

Samatta alianza kujifua na wachezaji wenzake kwa mara ya kwanza Ijumaa iliyopita na Kocha wa Aston Villa, Dean Smith, alisema anaweza kuwa tayari kwa mchezo wa nusu fainali ya pili ya Kombe la Ligi (Carabao Cup) dhidi ya Leicester City leo.

Hata hivyo, mashabiki wa Aston Villa wametakiwa kuwa watulivu kwa Samatta kwa kuwa haitakuwa rahisi kwake kuzoea ‘ligi hiyo ngumu zaidi duniani’.

Samatta, 27, ambaye alikamilisha uhamisho wake kutoka KRC Genk ya Ubelgiji kwenda Villa wiki iliyopita kwa takriban pauni milioni 8.5 hadi anaondoka alishacheka na nyavu mara 10 kwenye mashindano yote huku msimu uliopita akiifungia timu hiyo ya jumla ya mabao 42.


Share:

Kocha wa Yanga achukizwa na mbwembwe za Morrison..... ''Kitendo alichofanya ni kuwakosea heshima wapinzani''

Kocha Mkuu wa Klabu ya Yanga, Luc Eymael amesema hapendi kuona mchezaji wake, kiungo Bernard Morrison akiwadhalilisha wapinzani wake kwa staili yake ya uchezaji.

Kauli hiyo ameitoa  Januari 26, 2020 baada ya kumalizika kwa mchezo wake na Timu ya Tanzania Prisons katika  Kombe la Shirikisho 'Azam Sports Federation Cup (ASFC)' ambapo Yanga iliibuka na ushindi wa 2-0,

Kocha Eymael amesema kuwa ameshaoongea na mchezaji huyo juu ya aina yake ya mchezo ambao unawadhalilisha wapinzani.

"Mimi sipendezwi kuona mtu anawadhalilisha wengine, ukifanya vile Ulaya utafanyiwa 'tackle' ya hatari sana. Ukiangalia Liverpool, Mo Salah anaweza kufanya hivi?, Sadio Mane anafanya hivi? hapana na mimi nimeshaongea na Morrison nimemwambia sipendi staili hii", amesema Eymael na kuongeza kuwa;

"Mashabiki wanapenda kuona mchezaji akifanya hivyo lakini kwangu mimi ni kutowaheshimu wapinzani na nimeshamwambia Bernard Morrison",

Katika michezo miwili ya Yanga, Morrison ametokea kupendwa na mashabiki wa klabu hiyo kutokana na aina ya uchezaji wake uliojaa mbwembwe za kupanda juu ya mpira huku mashabiki wa timu hiyo wakimpa sifa lukuki na kudai Morrison ni wakina Chama 500 (Chama ni mchezaji wa Simba).


Share:

Polepole Amvaa Zitto Kabwe...."CCM Itashinda Hata Wakizuia Mkopo Wao"

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Hamphrey Polepole  amemtolea uvivu Zitto Kabwe kwa kitendo cha kuzuia fedha za elimu huku akisema watashinda Uchaguzi Mkuu hata akizuia fedha hizo.

Zitto ambaye  ni kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo aliandika barua za kutaka Benki ya Dunia kusitisha mkopo wa elimu baada ya kudai serikali inakiuka taratibu kwa kuwazuia wanafunzi waliopata ujauzito wasiendelee na masomo.

Pia zitto alisema mkopo huo sio kweli ulilenga kuwanufaisha wanafunzi na kwamba ni kwa ajili ya kampeni za kisiasa 2020.

Polepole baada ya kuona taarifa hiyo alimjibu kuwa; Kumbe tatizo ni Uchaguzi 2020. Kabwe anaomba tunyimwe mkopo wa kuongeza umadhubuti wa elimu ya watoto wetu kwasababu anajua ni jukumu letu kujenga shule na sifa zitakuja CCM, inayokwama si CCM, ni watoto wa Kigoma Ujiji. Kushinda tutashinda tu! Najiuliza watoto wake wanasomawapi?


Share:

Waziri Mkuu wa Iraq alaani shambulizi la roketi katika ubalozi wa Marekani katikati ya Baghdad

Waziri Mkuu wa Iraq Adel Abdul Mahdi ametoa taarifa akilaani shambulizi la roketi katika ubalozi wa Marekani kwenye eneo la Green Zone katikati mwa Baghdad.

Shambulizi hilo limetokea tena dhidi ya ubalozi wa nchi za nje, wakati roketi za Katyusha zilipotua ndani ya eneo la ubalozi wa Marekani. 

Amekemea vikali muendelezo wa vitendo hivi vya kukiuka sheria ambavyo vinadhoofisha taifa na utawala. 

Abdul Mahdi ambaye pia ni kamanda mkuu wa jeshi la Iraq, amesema amevielekeza vikosi vya Iraq kupeleka askari na kuwatafuta washambuliaji, pamoja na kuanzisha uchunguzi juu ya tukio hilo, ili kuwakamata wote waliorusha roketi. 

Pia ameahidi kuwa serikali italinda balozi zote na kuchukua hatua za lazima kwa mujibu wa sheria.


Share:

Head of Watetezi Online TV at Watetezi Online TV

Opportunity title: Head of Watetezi Online TV Work Station: Dar Es Salaam Application deadline: 5th of February 2020 The Tanzania Human Rights Defenders Coalition (THRDC) is an umbrella organization of more than 180 Human Rights focused organization operating in both Tanzania Mainland and Zanzibar. The main focus of the Coalition is to put on the ground efforts towards… Read More »

The post Head of Watetezi Online TV at Watetezi Online TV appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Valuer II required at TANROADS

The regional Manager’s office TANROADS -Kigoma, on behalf of the Chief Executive TANROADS, intends to recruit suitably qualified and competent Tanzanians to fill the post of valuer for the period of three years with possibility of contract renewal. Successful applicants must be ready to work on assigned office work accordingly and to various upgraded road projects to bitumen… Read More »

The post Valuer II required at TANROADS appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WIZARA YA ELIMU TANZANIA: SHORT TRAINING COURSES SCHOLARSHIP TENABLE IN INDIA FOR THE ACADEMIC YEAR 2019/2020

WIZARA YA ELIMU TANZANIA: SHORT TRAINING COURSES SCHOLARSHIP TENABLE IN INDIA FOR THE ACADEMIC YEAR 2019/2020   Call for Application The General Public is hereby informed that the Government of India through the Indian Technical and Economic Cooperation (ITEC), has granted a full funded scholarship to eligible Tanzanian to pursue Short courses at Indian Public Institutions for the… Read More »

The post WIZARA YA ELIMU TANZANIA: SHORT TRAINING COURSES SCHOLARSHIP TENABLE IN INDIA FOR THE ACADEMIC YEAR 2019/2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Tamko la TFF Kuhusu Tuhuma za Ramadhani Kabwili wa Yanga kwa Simba




Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne January 28





















Share:

Volunteer role: Obstetrician/Gynaecologist at Voluntary Service Overseas ( VSO)

Type of role: Healthcare Location: Uganda, Tanzania, Ethiopia and Sierra Leone, Various Countries Application Closing Date: 30 Jun 2020 Interview date: As soon as possible Start date: As soon as possible   VSO is the world’s leading international development charity that works through volunteers to create a fair world for everyone. At VSO we pride ourselves on doing development… Read More »

The post Volunteer role: Obstetrician/Gynaecologist at Voluntary Service Overseas ( VSO) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Monday, 27 January 2020

Country Support Associate, Pediatric HIV and eMTCT Jobs at Clinton Health Access Initiative

Country Support Associate, Pediatric HIV and eMTCT Jobs at Clinton Health Access Initiative Deadline Date: Saturday, 22 February 2020 Organization: Clinton Health Access Initiative Country: United Republic of Tanzania City: Boston Overview The Clinton Health Access Initiative, Inc. (CHAI) is a global health organization committed to saving lives and reducing the burden of disease in low-and middle-income countries,… Read More »

The post Country Support Associate, Pediatric HIV and eMTCT Jobs at Clinton Health Access Initiative appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Program & Communications Intern at Seed Change Tanzania

Program & Communications Intern at Seed Change Tanzania Deadline Date: Friday, 21 February 2020 Organization: Seed Change Tanzania Country: United Republic of Tanzania City: Kigoma About the position: The majority of people in Western Tanzania have their livelihoods in agriculture but they suffer from poverty due to an underdeveloped agriculture system. You will use your skills in storytelling,… Read More »

The post Program & Communications Intern at Seed Change Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Rocktools Manager Job Vacancy at Sandvik Mining and Rock Technology

Rock tools Manager Job Vacancy at Sandvik Mining and Rock Technology   Sandvik Mining and Rock Technology is looking for a Rocktools Manager Currently, we have an opening for a Rocktools Manager located in Mwanza, Tanzania. The successful applicant will be responsible for managing the sales, distribution, implementation and profitability of the Rock Tools department. This role is crucial… Read More »

The post Rocktools Manager Job Vacancy at Sandvik Mining and Rock Technology appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Secondary Teacher Jobs at Dar es Salaam International Academy Dar es Salaam, Tanzania

Secondary Teacher Jobs at Dar es Salaam International Academy Dar es Salaam, Tanzania Dar es Salaam International Academy is a privately owned international school located in Dar es Salaam, Tanzania. Implementing the International Baccalaureate Primary, Middle Years & Diploma Programmes. We are currently recruiting teachers for our 2020/21 Academic Year. A DIA teacher has a pivotal role in… Read More »

The post Secondary Teacher Jobs at Dar es Salaam International Academy Dar es Salaam, Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger