Saturday, 4 January 2020

NIDA Waagizwa Kufanya Kazi Masaa 16 ili Kutimiza Agizo la Rais Magufuli

Na Mwandishi Wetu
Katika kwenda sambamba na siku 20 zilizongezwa na Rais Dkt.John Magufuli wakati akisajili laini yake ya simu kwa alama za vidole Desemba 27,2019 mjini Chato mkoani Geita,Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA) wametakiwa kuongeza idadi ya watumishi katika kituo cha kuchakata taarifa za waombaji nchi nzima kilichopo Kibaha mkoani Pwani ili  kuhakikisha kila mwananchi anayekidhi vigezo kupata  Kitambulisho cha Taifa ili aweze kusajili  laini yake ya  simu.

Akizungumza baada ya kutembelea kituo hicho Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dkt. Anold Kihaule kuongeza idadi ya watumishi katika kituo hicho na kuongeza pia masaa ya kufanya kazi kutoka nane mpaka kumi na sita ili kuhakikisha wananchi wanapata namba na vitambulisho baada ya nyongeza ya siku 20 ziliyotolewa na Rais Magufuli.

“Nimetembea katika vituo mbalimbali vya NIDA nchi nzima,changamoto kubwa wanayotoa wananchi ni kwenda kila siku kufuatilia kitambulisho au namba katika kituo husika lakini wamekua wakipata majibu kwamba bado kipo kwenye mchakato,wakati mwingine ameomba miaka mitatu iliyopita sasa anapoteza muda na gharama kufuatilia kitambulisho lakini nimetembelea hapa leo nimegundua uchache wa watumishi,mkurugenzi ongeza watumishi hapa..” alisema Masauni

“……naomba pia ongeza muda wa kufanya kazi,kutoka masaa nane mpaka kumi na sita,Rais ashasema muda hautaongezwa wa usajili laini za simu,sasa wananchi wanafurika na kupata taabu vituoni huko,sisi ndio wawakilishi wao lazima tuwasemee na mkuu wa nchi ashatoa maelekezo sasa ni utekelezaji tu” aliongeza Masauni

Akizungumza katika ziara hiyo Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dkt. Anold Kihaule alisema watayatekeleza maagizo hayo ya serikali huku akiwaasa wananchi ambao tayari wana namba za utambulisho waende kusajili laini zao ili kwenda sambamba na muda ulioongezwa na Rais Dkt. Magufuli.

 “Jumla ya watu milioni 7.6 tayari wana namba za utambulisho nchi nzima na kila siku tunaendelea kutoa namba hizo sehemu mbalimbali nchini na mnaweza kuona kwa Dar es Salaam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja tunatoa namba pale nani zoezi la siku zote za wiki,hatuna sikukuu wala siku za mwisho za wiki” alisema Dkt.Kihaule

Kila mmiliki wa simu ya mkononi anatakiwa kusajili laini yake kwa alama za vidole kwani kutofanya hivyo itamaanisha kutoweza kupiga wala kupokea simu,vile vile muhusika hatoweza kutuma wala kupokea ujumbe mfupi wa maneno.


Share:

Waziri Mkuu Atoa Maagizo Kwa Wizara Ya Kilimo Sakata la Malipo Ya Korosho

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo ihakikishe asilimia tatu ya wakulima wa zao la korosho waliosalia wanahakikiwa na kulipwa.

Hadi sasa zaidi ya asilimia 96 ya wakulima wa korosho waliouza korosho zao katika msimu wa 2018/2019 wameshahakikiwa na kulipwa.

Ameyasema hayo jana (Ijumaa, Januari 3, 2020) wakati alipokutana na baadhi ya wakulima wa korosho kutoka wilaya za Ruangwa, Masasi na Tandahimba.

Baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wakulima hao, Waziri Mkuu amewataka waendelee kuwa na subira na kwamba haki yao itapatikana.

 “Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli ipo makini, hivyo hakuna Mtanzania yeyote atakayepoteza haki yake.”

Kadhalika, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wanachama wa vyama vya ushirika pale watakapoona ushirika wao hauendi vizuri wasisite kutoa taarifa Serikalini.

Amewaagiza wakuu wa mikoa na wilaya wawachukulie hatua viongozi wote wa vyama vya ushirika watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Kwa upande wao, wakulima wameishukuru Serikali kwa kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi na kwamba wanaimani ya kulipwa madai yao.

Mmoja wa wakulima hao Bi. Mariamu Mganda amesema anamshukuru Waziri Mkuu kwa kukubali kuwasikiliza kwani wamepata tumaini la kulipwa fedha zao.
 
Mkulima Mwingine Bw. Abdulkareem Said amesema ameridhishwa na utendaji kazi wa Serikali hususan baada ya Waziri Mkuu kukubali kusikiliza kero zao.

(mwisho)
IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

Wimbo Mpya wa Harmonize – Hainistui

Wimbo Mpya wa  Harmonize – Hainistui


Share:

Video Mpya Ommy Dimpoz x Nandy – Kata

Video Mpya Ommy Dimpoz x Nandy – Kata


Share:

Video Mpya ya Roma Ft. One Six – Mkombozi

Video Mpya ya Roma Ft. One Six – Mkombozi


Share:

Programme Associate (Nutrition/Agriculture) G6at WFP

Programme Associate (Nutrition/Agriculture) G6 Job Opportunity at WFP Programme Associate (Nutrition/Agriculture) G6 Requisition # 111521 – Posted 01/01/2020 WFP Tanzania, – Dodoma PROGRAMME & POLICY WFP seeks candidates of the highest integrity and professionalism who share our humanitarian principles. Selection of staff is made on a competitive basis, and we are committed to promoting diversity and gender balance.… Read More »

The post Programme Associate (Nutrition/Agriculture) G6at WFP appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Jobs at Mkombozi Commercial Bank

Jobs Opportunities at Mkombozi Commercial Bank Mkombozi Commercial Bank PLC was established in 2009 and operates as a fully-fledged commercial Bank. The Bank offers wide spectrum of banking services and wishes to expand its business operations across the country. The Bank is inviting suitable applicants to fill the following positions below: Job Title: Chief Internal Auditor Functional Reporting… Read More »

The post Jobs at Mkombozi Commercial Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Monitoring Assistant (Agriculture/Nutrition) at WFP

Monitoring Assistant (Agriculture/Nutrition) Jobs Opportunities at WFP, Monitoring Assistant (Nutrition/Agriculture) G5 Equivalent – Service Contract Appointment (111642) Requisition # 111642 – Posted 02/01/2020 – Short Term-SC WFP – Africa, Central & Eastern – Tanzania, United Republic of – Dodoma – Working Job Language (1) – PROGRAMME & POLICY  Job Description Print Preview Apply Save Job Email Job… Read More »

The post Monitoring Assistant (Agriculture/Nutrition) at WFP appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Jobs at Magare Company Limited

Magare Company Limited is one of the Tanzanian Electrical and Mechanical Engineering Company whose vision is to be the leading engineering company in providing Mining and Industrial Electro-mechanical Solutions in Africa. Magare Company Limited invites applications from qualified candidates in the following positions; ELECTRICAL TEAM Chief Electrical Engineer (1) Qualifications:  Holder of Bachelor’s degree in Electrical and… Read More »

The post Jobs at Magare Company Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi January 4

















Share:

Friday, 3 January 2020

Picha : MBUNGE MASELE AFANYA ZIARA KATA ZA LUBAGA,KAMBARAGE NA MJINI...AAHIDI KUIPIGA TAFU ZAHANATI YA BUSHUSHU


Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele (CCM) ametembelea na kukagua ujenzi wa zahanati ya Bushushu iliyopo katika kata ya Lubaga katika Manispaa ya Shinyanga na kuahidi kupeleka moramu na kutafuta fedha ili kukamilisha ujenzi huo ambao umefikia hatua ya renta. 

Mhe. Masele amefika katika zahanati ya Bushushu leo Ijumaa Januari 3,2020 ikiwa ni mwendelezo wa ziara  katika Jimbo lake kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzungumza na wajumbe wa kamati za siasa CCM ngazi ya matawi na kata. 

“Nimeridhishwa na kasi ya ujenzi wa zahanati ya Bushushu yenye vyumba 15 ambayo mimi mwenyewe niliuanzisha kwa kwa kuchangia mifuko 100 ya saruji.Niwapongeze sana wananchi na wadau mbalimbali kwa ushirikiano wenu kushiriki ujenzi wa zahanati hii. 

“Nimerudi tena kwa mara pili kuwaunga mkono wananchi ili tukamilishe ujenzi huu na wananchi waanze kupata huduma za afya. Nitaleta moramu kujaza jengo hili pamoja na kutafuta fedha lakini pia nitazungumza na Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga ili amalizie ujenzi kwa kupaua jengo hili kwani sisi wananchi tumeshajenga boma. Kwa utaratibu uliopo wananchi wakijenga boma,serikali inatakiwa kumalizia ujenzi”,alieleza Masele. 

Mbunge huyo alisema serikali inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya barabara,maji na umeme huku akibainisha kuwa huwezi kuzungumzia maendeleo ya mji wowote bila kugusa miradi hiyo ambayo inahitaji mikakati mizuri kuitekeleza badala ya bla bla. 

“Huwezi kutenganisha maendeleo ya Shinyanga Mjini na Mbunge wa Jimbo. Tunayo ‘Master Plan’ tuliyoitengeneza tangu mwaka 2011,Huu ni mkakati wa kuboresha mji wa Shinyanga uwe wa Kisasa. Utekelezaji wa awamu ya kwanza naweza kusema umeisha mwaka 2019 ambapo tumefanikiwa kujenga barabara za lami kilomita 13 za  kupitia Benki ya dunia. Na katika awamu ya pili tunatarajia kujenga kilomita 18 za barabara za lami zingine mpya.

Hizi kilomita 13 za barabara tulizojenga hadi sasa tu zimeufanya mji wa Shinyanga upendeze kiasi hiki ambapo kuna barabara za lami na taa zake. Je tukiongeza barabara zingine kilomita 18 muonekano wa mji utakuwaje?,ndiyo maana nikisema tunataka Shinyanga iwe mji wa Kisasa kuna baadhi ya watu hawanielewi kwa sababu hawajui mipango iliyopo”,alifafanua Masele. 

Masele alisema mpango uliopo ni kuhakikisha kata zote za Jimbo la Shinyanga Mjini zinaunganishwa kwa barabara za lami na kuwaomba wananchi kutumia fursa ya mji wa Shinyanga kufanya shughuli za kujiinua kiuchumi. 

Mbali na kutembelea kata ya Lubaga, Mhe. Masele ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika (PAP) akiwa ameambatana na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wilaya ya Shinyanga mjini amekutana na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Mjini na Kambarage.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele (mwenye suti nyeupe) akitembelea na kukagua ujenzi wa zahanati ya Bushushu iliyopo katika kata ya Lubaga katika Manispaa ya Shinyanga leo Januari 3,2020 wakati akiendelea na ziara yake Jimboni. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele (mwenye suti nyeupe) akizungumza kwenye zahanati ya Bushushu na kuahidi kupeleka moramu kwenye zahanati hiyo.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele (mwenye suti nyeupe) akipokea maelezo kuhusu ujenzi wa zahanati ya Bushushu ambayo ilianza kujengwa kwa nguvu za wananchi na mbunge kuchangia mifuko ya saruji na sasa ujenzi umefikia hatua ya renta.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akikagua jengo la zahanati ya Bushushu.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akiondoka katika zahanati ya Bushushu.
Muonekano wa jengo la zahanati ya Bushushu.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Lubaga wakati wa ziara yake leo Januari 3,2020.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Lubaga wakati wa ziara yake leo Januari 3,2020.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Lubaga wakati wa ziara yake leo Januari 3,2020.
Katibu Msaidizi wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Rashid Mnunduma akizungumza wakati wa kikao cha Mbunge Stephen Masele na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Lubaga.

Mwenyekiti wa CCM kata ya Lubaga Anord Makombe akizungumza wakati wa kikao cha Mbunge Stephen Masele na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Lubaga.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Kambarage wakati wa ziara yake leo Januari 3,2020.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Kambarage wakati wa ziara yake leo Januari 3,2020.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Kambarage wakati wa ziara yake leo Januari 3,2020.
Mwenyekiti wa CCM kata ya Kambarage Rehema Namanilo akizungumza wakati wa kikao cha Mbunge Stephen Masele na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Kambarage.
Diwani wa kata ya Kambarage Hassan Mwendapole akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kata ya Kambarage.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Amri Migeyo wakati Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Kambarage wakati wa ziara yake leo Januari 3,2020.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Mjini wakati wa ziara yake leo Januari 3,2020.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa kamati ya siasa Chama Cha Mapinduzi CCM wa ngazi ya matawi na kata ya Mjini wakati wa ziara yake leo Januari 3,2020.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

100 Job Opportunities at University Of Dar es Salaam (UDSM)....Mwisho Tarehe 7 Mwezi Huu

Overview:
The University of Dar es Salaam is the oldest and biggest public university in Tanzania. It is situated on the western side of the city of Dar es Salaam, occupying 1,625 acres on the observation hill, 13 kilometers from the city centre. It was established on 1st July 1970, through parliament act no. 12 of 1970 and all the enabling legal instruments of the constituent colleges.

The University of Dar es Salaam invites applications from suitably qualified Tanzanians to be considered for immediate employment to fill the vacant posts as described in attached PDF file:

Click link below to download PDF File attached for full jobs details and mode of application:



Share:

Download App Yetu Kwenye Simu Yako Ili Uweze Kupata Habari Zetu Kwa Haraka Zaidi

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.



Share:

BABA AUA MTOTO WA MIAKA MITATU KWA KUMCHARANGA MAPANGA BUKOBA

Picha haihusiani na habari hapa chini

Na Ashura Jumapili - Malunde 1 blog Bukoba
Mwanaume aliyejulikana kwa jina la Leonard Kishenya anatuhumiwa kumuua kikatili mtoto wake wa kambo mwenye umri wa miaka mitatu kwa kumcharanga mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake kisha kutenganisha mkono wa kushoto.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 03,2020 ofisini kwake  Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera (ACP )Revocatus Malimi alisema tukio hilo lilitokea Januari mosi mwaka huu ,usiku wa kuamkia mwaka mpya saa 6:40 usiku katika kijiji cha Katorerwa Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera ambapo mtoto Careen Crispine mwenye umri wa miaka (03) aliuawa.

Alisema marehemu alikuwa anaishi na mama yake mzazi aitwaye Domina Andrew (30 )aliyekuwa ameolewa na Leonard Kishenya (36 ) ambaye anatuhumiwa kwa mauaji ya mtoto huyo.

Alisema kabla ya tukio hilo la mauaji wanandoa hao walitoka kwenda kwenye mkesha wa mwaka mpya wa 2020 walikuwa wanakunywa pombe na walirudi nyumbani majira yasaa 6:40 usiku na walipofika kulitokea ugomvi kati ya wanandoa hao ambao chanzo chake hakijafahamika.

Kamanda Malimi alieleza kuwa kutokana na ugomvi huo kuwa mkali, mke aliamua kukimbia na kwenda kulala kwa jirani na kumuacha mtoto wake ndani akiwa amelala.

Alisema Januari Mosi mwaka huu majira ya saa moja asubuhi mke alirudi nyumbani na kushuhudia mtoto wake akiwa ameuawa kwa kukatwakatwa na kitu chenye makali sehemu mbalimbali za mwili wake kama vile kichwani na kuutenganisha mkono wa kushoto na mwili.

"Mwili wa mtoto huyo ulikutwa umelala kifudifudi nje ya nyumba yao wakati alikuwa, amelala ndani. Mume ambaye ni mtuhumiwa wa tukio hilo hakuwepo na alikuwa ametorokea kusikofahamika",alieleza.

Alisema jeshi la polisi kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kumkamata na wanaendelea kumhoji chanzo cha kufanya mauaji ya kikatili kwa mtoto asiyekuwa na hatia naatafikishwa mahakamani.
Share:

WASHINDI PROMOSHENI YA KISHINDO CHA FUNGA MWAKA YA TIGO WAKABIDHIWA ZAWADI ZAO


Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Tigo Pesa, Angelica Pesha akizungumza na waandishi wa habari . katika hafla ya kuwakabidhi washindi wa promosheni ya Kishindo cha Funga Mwaka na Tigo.
“Tunapenda kuwashukuru sana wateja wetu wote ambao walishiriki kwenye promosheni hii lakini kwa leo tumeweza kuwapata washindi watatu ambao wanahitimisha promosheni hii ambayo ilifanyika nchi nzima na tulikuwa na washidi zaidi ya 331 ambao wameshinda milioni 500,” Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Tigo Pesa, Angelica Pesha akifafanua jambo kwa waandishi wa habari leo
“Mimi nimfanya biashara wa vifaa vya umeme hapa Dar es Salaam na mtaji wangu ni wa kawaida tu lakini kupitia ushindi huu naamini kabisa malengo yangu ya kumiliki biashara kubwa zaidi yatatimia.Nawashukuru sana Tigo kwa kuanzisha promosheni hii kwani ushindi huu utabadilisha maisha yangu kwa kiasi kikubwa,”Mshindi wa kwanza Salum Biwi mkazi wa Manzese baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya Sh20 milioni leo Januari 3, 2019.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Tigo Pesa, Angelica Pesha akimkabidhi mfano Hundi Hamidu Mtabiage kutoka mkoani Lindi aliyeshinda Sh15 milioni alisema “Naishukuru sana Tigo Pesa kwasababu mimi ni mfanyabiashara mdogo wa vifaa vya pikipiki na kwa kushinda pesa hizi zitaniwezesha kukuza mtaji wangu kutoka kuuza vifaa hadi kuuza pikipiki kwani hii ni ndoto yangu ya muda mrefu.
Anna Mkongwa kutoka Dodoma ndiye mshindi wa tatu wa promosheni ya #KishindoChaFungaMwaka aliweka pesa kwenye Tigo pesa ili ashinde pesa.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Tigo Pesa, Angelica Pesha akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa Promosheni ya kishindo cha Funga Mwaka na Tigo , Mara baada ya kukabidhiwa hundi zao mapema leo.

Dar es Salaam. Huenda changamoto za Januari zikawa historia kwa baadhi ya washindi ambao wamejipatia fedha kupitia promosheni ya Kishindo cha Funga mwaka kutoka Kampuni ya Tigo (Tigo Pesa) jambo linalowaweka katika nafasi nzuri ya kukabiliana na mambo mbalimbali yanayojitokeza hasa katika kipindi hiki cha mwanzo wa mwaka.


“Nilipigiwa simu Jumatano iliyopita nikataarifiwa kwamba ni mshindi wa shillingi milioni 20m, kwa kweli sikuamini mpaka nilipoona jina langu katika mitandao ndio nikaamini. Nimshukuru Mungu kwani nilikuwa nina shiriki katika promosheni hii,kwa matarajio ya kwamba na mimi nitaibuka mshindi wa million hata moja,ili niweze kuongeza mtaji,kwa bahati nzuri nimeibuka mshindi wa kwanza wa shilling million 20” ndivyo alivosema Salum Biwi mkazi wa Manzese baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya Sh20 milioni leo Januari 3, 2019.


Biwi ambaye ni mshidi wa kwanza wa Kampeni hiyo alisema ushindi huo ni mkubwa kwake na kwamba amejipanga kutumia fedha hizo kuongeza mtaji kwenye biashara yake ya sasa.


“Mimi nimfanya biashara wa vifaa vya umeme hapa Dar es Salaam na mtaji wangu ni wa kawaida tu lakini kupitia ushindi huu naamini kabisa malengo yangu ya kumiliki biashara kubwa zaidi yatatimia.Nawashukuru sana Tigo kwa kuanzisha promosheni hii kwani ushindi huu utabadilisha maisha yangu kwa kiasi kikubwa,” alisema Biwi.


Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo kwa washindi, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Tigo Pesa, Angelica Pesha alisema promosheni hiyo ilifanyika mwezi Desemba kwa lengo la kuwashukuru wateja kwa kutumia huduma ya Tigo Pesa kwa kipindi chote cha mwaka 2019.


“Tunapenda kuwashukuru sana wateja wetu wote ambao walishiriki kwenye promosheni hii lakini kwa leo tumeweza kuwapata washindi watatu ambao wanahitimisha promosheni hii ambayo ilifanyika nchi nzima na tulikuwa na washidi zaidi ya 331 ambao wameshinda milioni 500,” alisema Pesha.


Kwa upande wake Hamidu Mtabiage kutoka mkoani Lindi aliyeshinda Sh15 milioni alisema “Naishukuru sana Tigo Pesa kwasababu mimi ni mfanyabiashara mdogo wa vifaa vya pikipiki na kwa kushinda pesa hizi zitaniwezesha kukuza mtaji wangu kutoka kuuza vifaa hadi kuuza pikipiki kwani hii ni ndoto yangu ya muda mrefu.”


Naye, Anna Mkongwa aliyeshinda Sh10 milioni, alisema pamoja na kuwa yeye ni mtumishi wa Umma, fedha alizozipata zitamsaidia kutimiza malengo mbalimbali hasa mwanzo huu wa mwaka.


“Kiukweli pesa hizi ni nyingi na sikutegemea kama ningeshinda hivyo kwa sasa nitakachokifanya ni kuweka malengo vizuri na pesa hii itanisaidia kuyatimiza,” alisema Mkongwa mkazi wa Dodoma.




Mbali na washindi hao, Kampeni hiyo ilikuwa ikitoa zawadi kwa washindi 8 wa Sh1 milioni kila siku na washindi 8 wa Sh5 Milioni kila wiki na tayari wamekwisha pokea zawadi zao.
Share:

Nini Chanzo Cha Mgogoro Huu Kati Ya Iran Na Marekani?...Tazama Hii Video Inayosimulia Kila Kitu

Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa anasisistiza kuwa mataifa ya Ulaya yanastahili kuchukua hatua madhubuti kuilipa fidia Tehran kutokana na hasara ya kiuchumi iliyosababishwa na vikwazo vya marekani dhidi yake - la sivyo itaendelea na mpango wake wa uundaji silaha za nyuklia. 

Nayo Marekani inataka kubuni muungano wa kimataifa wa kijeshi kulinda mipaka ya majini katika eneo la Iran na Yemen.

Lakini mzozo ulioshuhudiwa hivi karibuni kati ya mataifa hayo mawaili sio jambo geni- 

Nchi hizi zimekuwa na uhasama wa miongo kadhaa.

Tazama hii Video!


Credit:BBC


Share:

Viwanja Vinauzwa Bunju Mpakani c/o Mapinga

Viwanja Vinauzwa Bunju Mpakani c/o Mapinga

Viwanja vya makazi na biashara vinauzwa mpakani mwa Bunju na Mapinga opposite na Kimele Hotel (Resort).

Vipo viwanja kuanzia milion 5 (20/20), milion 7 (20/30), milion 10 (20/40),  sqm 1600 kwa milion 23, sqm 2400 kwa milion 30.

Viwanja viko umbali wa km 2 tu kutoka main road  (Dar to Bagamoyo Road).
Huduma zote zipo: maji, umeme, barabara, shule, makanisa na miskiti.

Ukipata ujumbe huu mjulishe ndugu/jamaa/rafiki, na biashara hii haina dalali/udalali.

Mpigie mhusika: 0758603077 au whatsap 0757489709


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger