Friday, 18 October 2019

BASI LA FREYS COACH LAUNGUA MOTO


Na Josephine Charles - Malunde 1 blog
Basi la Freys Coach lenye namba za usajili T119BDY Gari la Freys  Coachla linalofanya safari zake kutoka Shinyanga kwenda  Tanga limeungua moto katika  eneo la Mhizi Usanda Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga barabara ya Tabora - Shinyanga.


Tukio hilo limetokea leo Ijumaa Oktoba 18,2019 majira ya saa 12 na nusu baada ya kutoka Shinyanga Mjini kuelekea Tanga.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio wanasema basi hilo limeungua matairi mawili ya nyuma upande wa kulia na kwamba hakuna madhara yaliyojitokeza kwa abiria walishuka na kuanza zoezi la kuzima moto huo kwa maji na mchanga na muda mfupi Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lilifika eneo la tukio na kufanikisha kuzima moto huo.

"Tumezima kwa maji na mchanga,zimamoto nao wamefika,gari limezima,hakuna uharibifu wala majeruhi,gari halijateketea,abiria tumefanya juhudi za kuzima,tunasubiri magari mengine kutoka Mwanza ili tuendelee na safari",wamesema abiria wakizungumza na Malunde 1 blog .

Muonekano wa basi la Freys Coach baada ya kuungua leo. Picha zote na Josephine Charles - Malunde 1 blog
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 18,2019



Share:

Thursday, 17 October 2019

DHAMIRA YA SERIKALI NI KUHAKIKISHA MTAMBO WA KUZALISHA UMEME HALE UNAREJEA KWENYE HALI YAKE YA KAWAIDA-WAZIRI DKT KALEMANI

Share:

WAZIRI MKUU AAGIZA WAKURUGENZI WAWILI WA HALMASHAURI WAFIKE OFISINI KWAKE KESHO

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtama na Mkurugenzi wa Umwagiliaji wa Kanda ya Kusini, wafike ofisini kwake Dar es Salaam kesho asubuhi na taarifa kuhusu skimu wa umwagiliaji wa Narunyu.

Ametoa agizo hilo leo mchana (Alhamisi, Oktoba 17, 2019) wakati alipoenda kukagua skimu hiyo ambayo imekuwa ikilalamikiwa tangu 2017. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtama ni Bw. Warioba Gunze na Mkurugenzi wa Umwagiliaji wa Kanda ya Kusini, ni Mhandisi Mndeme.

Amechukua uamuzi huo baada ya kufika eneo la mradi na kupokea malalamiko ya wanajumuiya ya umwagiliaji kutoka kwa Mwenyekiti wao, Bw. Bakari Awadhi juu ya kusuasua kwa mradi huo lakini alipotaka apate maelezo ya wataalamu hakuna hata mmoja ambaye alikuwepo.

"Nilitaraji niwakute hapa Mkurugenzi wa Halmashauri, Afisa Umwagiliaji wa Wilaya na Mkurugenzi wa Umwagiliaji wa Kanda. Nimeagiza wanikute uwanja wa ndege Lindi au Dar es Salaam na kesho asubuhi waje ofisini kwangu wanipe taarifa kamili ya mradi huu. Nataka nijue fedha zilizobakia zaidi ya sh. milioni 240 ziko wapi."

"Walipaswa niwakute hapa wananisubiri kwa sababu nilitoa taarifa tangu jana kwamba nitapita hapa. Nimepata taarifa kwamba wamesafiri kutoka Mtwara na leo asubuhi walikuwepo Lindi mjini. Waje ofisini kesho, wakishindwa, nitachukua maamuzi mengine," amesema.

Akielezea umuhimu wa mradi huo wakati akizungumza na baadhi ya wanaushirika waliokuwepo, Waziri Mkuu amesema ni wa muhimu kwa sababu unatiririsha maji wakati wote. "Huu ni mradi wa kuringia. Mradi huu unatiririsha maji wakati huu wa kiangazi, tena mengi tu."

Amesema kutokana na umuhimu wa mradi huo, hivi sasa wangekuwa wanazalisha mazao ya kila aina. "Hapa ni mahali pa kuzalisha mazao mengi, leo unalima mahindi, ukivuna unapanda matikiti, ukitoa unapanda nyanya. Sasa nitapasimamia mwenyewe," amesisitiza.

Amewataka wanaushirika wanaounda jumuiya ya umwagiliaji wahakikishe kila mmoja anatambua eneo lake na mara kazi ikianza wawe tayari kuanza kilimo. "Huu mradi una manufaa kwa watu wa Ruo, Mahumbika hadi Mnazi Mmoja. Lazima tuung'ang'anie kwa sababu kuna idadi kubwa ya wakulima wanaoutegemea. Huu mradi lazima tuuvalie njuga."

Waziri Mkuu alipofika uwanja wa ndege wa Lindi, maafisa hao walikuwa hawajafika kwa sababu simu zao hazikupatikana, na akaagiza waje Dar es Salaam kesho asubuhi.

Mapema, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Bw. Shaibu Ndemanga alimweleza Waziri Mkuu kwamba katika mafaili aliyoyapitia ofisini kwake alibaini kwamba mradi huo ulitengewa sh. milioni 788 ambapo mkandarasi wa kwanza Chest Investments Company alilipwa sh. milioni 121 lakini akashindwa kazi.

"Mkandarasi wa pili ambaye ni D & L naye alilipwa zaidi ya shilingi milioni 400 naye pia akashindwa kazi ya kuondoka tope. Kwenye ripoti, inaonesha zilibakia sh. milioni 249," alisema.

Naye Mwenyekiti wa wanajumuiya ya umwagiliaji ya Narunyu, Bw. Bakari Awadhi alisema skimu hiyo yenye ukubwa hekta 1,200 imekuwa ikijaa maji na kufunika mitaro na hatimaye kujaa mchanga.

Alimwomba Waziri Mkuu awasaidie kuifufua skimu hiyo kwa sababu inawanufaisha wakazi wa mikoa ya Lindi na Mtwara.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
Share:

Picha : MKUU WA MKOA WA SHINYANGA AZINDUA CHANJO YA SURUA, RUBELLA NA POLIO



Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, amezindua Kampeni ya kitaifa ya Chanjo ya Surua, Rubella na Polio, mkoa wa Shinyanga ambayo itatolewa kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano ili kuwapatia kinga dhidi ya magonjwa hayo.


Uzinduzi wa chanjo hiyo umefanyika leo Oktoba 17, 2019 katika kata ya Lyabukande halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, na kuhudhuriwa na wananchi wa kata hiyo pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali wakiwemo wataalamu wa afya ngazi ya mkoa na wilaya.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo Telack amesema, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. John Magufuli, inathamini afya za wananchi wake hasa katika kuzuia magonjwa yanayozuilika kwa chanjo na ndiyo maana chanjo hiyo inatolewa bure.

“Nawaombeni wazazi wote mkoani Shinyanga mjitokeze kwa wingi kupeleka watoto wenu wenye kuanzia umri wa miezi tisa hadi 49 yaani miaka Minne na miezi 11 kupatiwa chanjo hii ya Surua, Rubella na polio ili kuwapatia kingi dhidi ya magonjwa haya”,amesema Telack.

“Ugonjwa wa Surua una madhara makubwa kwa watoto ambapo unaweza kumsababishia madhara ya upofu, kuhara, na utapiamlo, Rubela unaweza kumsabishia mtoto ulemavu, magonjwa ya moyo na mtoto wa jicho, Polio unaweza kumsabishia mtoto kupooza mwili wote, hivyo nawataka wazazi msipuuzie zoezi hili,”ameongeza.

Pia amewaonya wananchi ambao watapotosha zoezi hilo la utoaji chanjo kwani baadhi yao wamekuwa na tabia ya kufanya upotoshaji, na kubainisha kuwa atakayebainika atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Naye Mganga Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Dkt. Rashid Mfaume, ametaja takwimu za watoto ambao watapewa chanjo hiyo kwa mkoa mzima kuwa ugonjwa wa Surua na Rubella watafikiwa watoto 286,124 na Polio watoto 151,547.

Amesema zoezi hilo limeanza leo Oktoba 17 na litakoma tarehe 21 mwaka huu, ambapo huduma hiyo itatolewa kwenye maeneo yote ya huduma za afya mkoa wa Shinyanga.

Nao baadhi ya wazazi ambao walifika kwenye uzinduzi huo wa chanjo, pamoja na watoto wao kuanza kupatiwa chanjo hiyo akiwamo Monica Shija, wameipongeza Serikali kwa kujali afya za watoto wao na kuwapatia kinga.

TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI


Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akizungumza wakati akizindua chanjo ya Surua, Rubella na Polio leo Alhamis Oktoba 17,2019 katika kata ya Lyabukande halmashauri ya wilaya ya Shinyanga. Chanjo hiyo itatolewa kwa watoto waliochini ya umri wa miaka mitano. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack, akionya wananchi kuacha kupotosha juu ya utolewaji wa Chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akitoa wito kwa wazazi kujitokeza kwa wingi kupeleka watoto wao waliochini ya umri wa miaka mitano kupatiwa Chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga Dkt. Rashid Mfaume akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni ya chanjo ya Surua, Rubella na Polio namna itakavyo saidia kukinga watoto dhidi ya magonjwa hayo.

Mwananchi Monica Shija akiishukuru serikali kwa kutoa chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack, akizindua chanjo ya Surua, Rubella na Polio kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.

Dkt. Geofrey Anthony akitoa chanjo ya Surua, Rubela na Polio kwa mtoto.

Muuguzi wa Zahanati ya Lyabukande Godfrey Mbelela (kulia), akitoa maelezo kwa Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe.Zainabu Telack namna watakavyotoa huduma ya chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Wananchi wakiwa na watoto wao kwenye uzinduzi wa chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Wananchi wakiwa na watoto wao kwenye uzinduzi wa chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Wananchi wakiwa na watoto wao kwenye uzinduzi wa Chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Wananchi wakiwa na watoto wao kwenye uzinduzi wa Chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Wananchi wakiwa na watoto wao kwenye uzinduzi wa Chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Wananchi wakiwa na watoto wao kwenye uzinduzi wa Chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Wananchi wakiwa na watoto wao kwenye uzinduzi wa Chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Kikundi cha sanaa cha Shinyanga kikitoa Burudani kwenye uzinduzi wa Chanjo ya Surua, Rubella na Polio.

Awali Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akiwasili kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Chanjo ya Surua, Rubella na Polio, kwenye Kata ya Lyabukande halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akipiga picha ya pamoja na baadhi ya wazazi waliopeleka watoto wao kupatiwa Chanjo ya Surua, Rubella na Polio, wa kwanza kulia ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, na wakwanza mkono wa kushoto ni mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Mhe. Hoja Mahiba.

Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog


Share:

BODI YA MIKOPO HESLB YATANGAZA ORODHA YA KWANZA WANAFUNZI 30,675 WALIOPATA MIKOPO 2019/2019


Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (Heslb) imetangaza orodha ya kwanza ya majina ya wanafunzi 30,675 wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo kwa ajili ya mwaka wa masomo wa 2019/2020 yenye thamani ya Sh113.5 bilioni.

Kati ya idadi hiyo, wanaume ni 19,632 sawa na asilimia 64 ya waliopata mikopo awamu ya kwanza.

Mkurugenzi Mtendaji wa Heslb, Abdul-Razak Badru amesema orodha iliyotolewa leo ni ya kwanza lakini mchakato wa kuwapangia wanafunzi mikopo utaendelea kulingana na uhitaji na uchambuzi wa taarifa za wanafunzi wanaodahiliwa vyuoni.

Katika mwaka wa fedha wa 2019/2020, Serikali imetenga Sh450 bilioni kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu, ikiwa imeongezeka kutoka Sh427 bilioni zilizotengwa mwaka uliopita.

Badru amesema Sh125 bilioni tayari zimetolewa na Serikali ili kugharimia mkopo kwa awamu ya kwanza, ambapo Sh116 bilioni zimetengwa kwa ajili ya wanafunzi wa mwaka kwanza ambao wataanza masomo hivi karibuni.

Hata hivyo, amesema awamu ya pili ya waliopata mikopo itatangazwa wiki ijayo kabla ya Oktoba 25, baada ya kukamilisha uchambuzi wa maombi ya mikopo kwa wanafunzi waliochelewa kukamilisha taratibu za udahili vyuoni na maombi ya mkopo mtandaoni.

Wanafunzi waliopata mikopo wanatakiwa kuingia katika akaunti zao walizotumia kuomba mikopo hiyo.
Share:

RAIS MAGUFULI AMTUMBUA MKUU TAKUKURU

Rais Magufuli amemtumbua Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Mtwara, Stephen Mafipa kutokana na kukosekana kwake katika mkutano wa hadhara alioufanya katika Kijiji cha Chukuku kilichopo Masasi mkoani humo.

Akiwa Chukuku, wananchi walimueleza Rais kuhusu madai yao dhidi ya fedha wanazowadai vingozi wa chama cha msingi Amcos baada ya viongozi hao kutoweka na fedha hizo.

Baada ya kupata malalamiko hayo, Rais Magufuli alimuita Kamanda wa Polisi wa mkoa ambaye alieleza kuwa wanaendelea kuwatafuta watuhumiwa.

Jibu hilo lilionekana kutomfurahisha Rais Magufuli ndipo alipotoa siku tano kwa kamanda huyo kuhakikisha viongozi hao wanakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sharia.

“RPC nakupa ndani ya siku tano waliokula fedha za wananchi wa hapa wakamatwe na wapelekwe mahakamani, mshirikiane na Takukuru, kamanda wa Takukuru mkoa yuko wapi,” aliuliza Rais Magufuli bila kupata majibu

Kufuatia ukimya huo aliomba simu yake kutoka kwa wasaidizi wake ambapo alipewa na kumpigia Brigedia Jenerali Mbungo na kumuelekeza kumuondoa kamanda huyo wa mkoa na kumtaka ampeleke mtu mwingine kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.

“Brigedia Jenerali, nipo hapa Masasai, nimemuita Kamanda wako wa TAKUKURU hapa hayupo, nimemfuta kazi hapahapa. Sasa nakuagiza leo hii uteue Kamanda mwingine, aje hapa asaidizane na RPC kuwakamata hao wezi na kuwafikisha kwenye mikono ya sheria.

“Hatuwezi tukavumilia huu ujinga na siwezi kukubali wananchi wangu wakanyanyasika. nataka utekeleze mara moja,” alisema Magufuli wakati akitoa maelekezo hayo kwa Brigedia Jen. Mbungo kupitia njia ya simu ya mkononi.
Share:

MTANGAZAJI MAARUFU MAULID KITENGE 'CHUMVI' AIPIGA CHINI EFM...ATUA WASAFI FM


MTANGAZAJI maarufu wa Habari za Michezo Tanzania, Maulid Kitenge ‘chumvi’ ameweka wazi kuwa ameachana na Kituo cha Redio cha EFM na kujiunga Wasafi FM inayomilikiwa na mwanamuziki, Diamond Platinumz.

Maulid Kitenge alikuwa mtangazaji wa EFM tangu mwaka 2015 akiwa kama Mkuu wa Idara ya Vipindi vya Michezo, huku akitangaza vipindi vya michezo vya Sports Headquarters na E-Sport, pamoja na kusoma magazeti kwenye Kipindi cha Joto la Asubuhi ndani ya EFM iliyoko Kawe Beach Jijini Dar es Salaam. Katika kile kilichoelezwa kuwa ni sapraizi kwa mashabiki,jana EFM walimtambulisha msanii, Elizabeth Michael ‘Lulu’ asubuhi kama mbadala wa Kitenge na kuibua gumzo.

Spoti Xtra lilikuwa la kwanza kufichua ishu ya Diamond kumalizana na Kitenge wiki kadhaa zilizopita walipokutana nchini Marekani kwenye dili zao. Kitenge ameliambia Spoti Xtra jana kwamba ni kweli ameachana na EFM juzi Jumanne na amejiunga rasmi na Wasafi FM ambapo atakuwa akikiongoza Kipindi cha Michezo cha Sports Arena.
Kitenge ambaye amewahi kung’ara na Radio One, aliongeza kuwa, kipindi hicho kitaanza Jumatatu ijayo na kitakuwa kikiruka hewani kuanzia saa mbili hadi saa tano asubuhi.

“Ni kweli nimeachana na EFM na nimehamia Wasafi FM ambapo kuanzia Jumatatu ya wiki ijayo nitakuwa nafanya Kipindi cha Sports Arena ambacho kitakuwa hewani kuanzia saa mbili hadi saa tano asubuhi, lakini pia nitakuwa nasoma magazeti kwenye kipindi cha asubuhi saa moja na nusu.

“Katika kipindi hicho nitakuwa na Yusuph Mkule na Mwanaidi Suleiman ambao nilikuwa nikifanya nao kazi EFM, pia nitakuwa na watangazaji wengine kama Edo Kumwembe na Ahmed Abdallah.

“Baada ya wiki moja nitakuwa natangaza kipindi kingine cha michezo kitakachoanza saa moja usiku,” alisema Kitenge ambaye pia ni mchambuzi wa Gazeti la Championi Ijumaa.

CHANZO ; GLOBAL PUBLISHERS
Share:

KATIBU WA CHADEMA AONYA VITISHO NA LUGHA ZA MATUSI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA


Mhe. Conchesta Rwamlaza

Na Lydia Lugakila - Malunde 1 blog
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Kagera Mhe. Conchesta Rwamlaza ambaye pia ni Mbunge viti maalumu amewataka viongozi wa vyama vya siasa mkoani Kagera kuepuka na masuala ya vitisho na lugha zisizofaa katika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika Novemba 24,2019.

Akizungumza na waandishi wa habari Oktoba 16, 2019 amesema kazi ya viongozi ni kuongoza njia hivyo wanapaswa kuwa mfano kwa wananchi wao kwa kuongoza vyema jukumu kwa kujiepusha na masuala yasiyofaa katika jamii ikiwemo vitisho na lugha zisizofaa zinazoweza kubeza harakati na maendeleo ya chama kusonga mbele.

Amesema katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 24 ni kipindi ambacho kinawataka viongozi kutoa matokeo chanya katika maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla. 

"Katika kipindi cha nyuma wapo baadhi ya viongozi walitoa lugha za vitisho. Mimi kama kiongozi wa chama nayakemea madudu yote,viongozi wafuate misingi ya vyama vyao ili kuruhusu suala la maendeleo kuwa juu’’,alisema Rwamlaza.

Aidha amewataka wananchi kuteua kwa haki viongozi watakaokidhi matarajio ya wananchi katika kuwaletea maendeleo. 

Hata hivyo mbunge huyo amepongeza zoezi la uandikishaji kwenye daftari kwa ajili ya  uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kuyajali makundi maalumu kwani kwa asilimia kubwa makundi hayo yamehudumiwa ipasavyo.
Share:

Laboratory Technician Jobs at University of Dar es Salaam,

The University of Dar es Salaam Invites applications from suitably qualified Tanzanians to be considered for Immediate employment to fill the following vacant posts: Job Title: Laboratory Technician (1 post) Institute of Marine Sciences, Zanzibar Qualifications and Experience: Applicant should possess Full Technician Certificate (FTC) or Diploma in Fisheries Science and Technology or Aquaculture or Aquaculture Technology. Main… Read More »

The post Laboratory Technician Jobs at University of Dar es Salaam, appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Artisan IV Jobs at University of Dar es Salaam

The University of Dar es Salaam Invites applications from suitably qualified Tanzanians to be considered for Immediate employment to fill the following vacant posts: Job Title: Artisan IV (1 post) College of Engineering and Technology Department of Chemical and Mining Engineering Qualifications and Experience Applicant should possess Certificate of Secondary Education Examination (Form IV) plus Trade Test Grade… Read More »

The post Artisan IV Jobs at University of Dar es Salaam appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Director of Tanzania Health Information and Management Program Support Job

Director of Tanzania Health Information and Management Program Support Location: Dar es Salaam Social Solutions International, Inc. (Social Solutions) is a Hispanic and woman-owned business emphasizing quality research and evaluation, training and technical assistance, and institutional support services. We are a mission-driven organization that believes that superior science can improve the world. Social Solutions is dedicated to the… Read More »

The post Director of Tanzania Health Information and Management Program Support Job appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Procurement Officer Jobs at Rijk Zwaan,

Procurement Officer   Rijk Zwaan is active worldwide as a vegetable breeding company that focuses on the development of high-quality vegetable varieties for professional growers. Mutual respect, a strong sense of responsibility and a high degree of employee involvement are the important starting points for our company. Rijk Zwaan is active in Tanzania in seed production and breeding support… Read More »

The post Procurement Officer Jobs at Rijk Zwaan, appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger