Wednesday, 9 October 2019

IGELEKE FC BINGWA WA SAUTI YA SIMBA SUPER CUP 2019

Diwani Nguvu Chengula wa kata ya Mwangata na mkurugenzi wa shule za Sun Academy ambaye alikuwa  ndiye mdhamini wa mashindano hayo ya  Sauti ya Simba Super Cup 2019 akiongea baada ya kupatikana kwa mshindi wa kombe hilo
Diwani Nguvu Chengula wa kata ya Mwangata na mkurugenzi wa shule za Sun Academy ambaye alikuwa  ndiye mdhamini wa mashindano hayo ya  Sauti ya Simba Super Cup 2019 akionyesha jezi ambazo alizigawa kwa mshindi wa kwanza na wapili wa mashindano hayo 
Diwani Nguvu Chengula wa kata ya Mwangata na mkurugenzi wa shule za Sun Academy ambaye alikuwa  ndiye mdhamini wa mashindano hayo ya  Sauti ya Simba Super Cup 2019 akitoa mpira kwa mshindi wa tatu wa mashindano hayo 
***
NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

MASHINDANO ya Sauti ya Simba Super Cup 2019 kata ya Mkimbizi yamefikia tamati siku ya jana baada ya kuchezwa fainali kati ya Mkimbizi FC na Igeleke FC katika viwanja vya shule ya msingi Mkimbizi na Igeleke FC kuibuka mshindi.

Mashindano haya ya mpira wa miguu yaliyokua yanahusisha zaidi ya timu nane ambazo ni Mkimbizi fc, Masoko fc,Mtwivila fc,Romanithelc Rc,Rutherana kkkt,Igereke fc,Bima fc na Vetaran fc za kata ya Mkimbizi yalikuwa yanadhamini na mkurugenzi wa shule za Sun Academy ambaye pia ni diwani wa kata ya Mwangata Nguvu Edward Chengula kwa kuwa amekuwa mdau mkubwa kwenye sekta ya michezo manispaa ya Iringa

Na ikumbukwe kuwa hivi karibuni diwani Nguvu Chengula alidhamini mashindano makubwa yaliyofanyika kata ya Kihesa yaliyokwenda kwa jina la Bidii Cup mashindano hayo yalikuwa yana msisimko na mvuto wa hali ya juu sana na  vijana walionesha uwezo mkubwa wa kusakata kabumbu kiasi kwamba wadau na viongozi wanaohusika na michezo katika mkoa wa Iringa walikunwa na uwezo uliooneshwa na vijana.

Akizungumza wakati wa kuwakabidhi zawadi mshindi wa kombe hilo Chengula alisema kuwa mpira wa miguu kwa sasa umekuwa unatoa ajira na kuwaajiri watu wengi hivyo vijana wanatakiwa kuonyesha vipaji vyao.

“Saizi mnatakiwa kuonyesha vipaji vyenu kweli kweli kwa kuwa kwa sasa mpira wa miguu umekuwa ajira ambayo wachezaji wamekuwa wanalipwa mamilioni ya fedha tofauti na miaka ya nyuma ilivyokuwa” alisema Chengula

Chengula alisema kuwa amekabidhi jezi seti moja na mpira mmoja kwa mshindi wa kwanza,mshindi wa pili alijinyakulia jezi seti moja huku mshindi wa tatu alijinyakulia mpira mmoja.

Aidha Chengula aliwataka wananchi kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari za mpiga kura kwa kuwa kila mkazi wa wanahaki wa kujitokeza kujiandikisha na kupata haki ya kumchagua kiongozi wanaemtaka.

“Hii ni fursa pekee ya kuhakikisha unapata nafasi ya kumchagua kiongozi ambaye atasaidia kukuletea maendeleo kwenye mtaa au kijiji chako kwa kipindi cha miaka mitano hivyo wakazi wote nawaomba mjitokeze kwa wingi kujiandikisha” alisema Chengula

Lakini Chengula aliwakumbusha vijana kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kujiandikisha na kugombea nafasi mbalimbali za kiuongozi kwa kuwa nao wanahaki ya kuwa viongozi wa kuongoza mitaa ambayo wanaishi kwa maendeleo ya jamii.


Vilevile Chengula ndiye alikuwa mdhamini mkuu wa mashindano ya kusaka vipaji vya vijana wanaoweza kuimba na kucheza (dancers) mashindano hayo yalikwenda kwa jina la Mwangata House of Talent na yalikuwa na msisimko mkubwa kwa kuwa vijana waliimba na kujishindia zawadi mbalimbali zikiwemo fedha tasilimu laki sita,vijana wote walioonesha uwezo mkubwa katika mashindano hayo chama cha mapinduzi (CCM) Iringa waliahidi kuviendeleza vipaji hivyo

Katika maswala ya soka mkurugenzi wa shule za Sun Academy amekua mstari wa mbele kabisa kuhakikisha vijana wanapata burudani, wanajenga afya zao na wanapata nafasi ya kujitengenezea ajira kupitia vipaji vyao vya kusakata soka, mpaka sasa emesaidia pia mashindano ya mpira pale kata ya Mlandege na kuwasaidia vijana kwa kuwapa vitendea kazi ikiwemo mipira na jezi katika mashindano yale.

Vijana hawahitaji mambo mengi,vijana wanahitaji kupata kile wanachokipenda. Suala la michezo kwa vijana ni suala mtambuka na linalopendwa na kila kijana. Vijana wana vipaji na uwezo mkubwa sana hasa wanapopewa nafasi ya kuonesha vipaji vyao. Hivyo kama kiongozi anayejali ni lazima aliangalie kundi hili kwa umakini mkubwa.
Share:

Naibu Waziri wa Fedha Dkt. Kijaji Aipa Tra Siku 75 Kuandaa Orodha Kamili Ya Walipakodi, Majengo Na Mabango

Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, ameipa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA miezi miwili na nusu hadi ifikapo Disemba 31 mwaka 2019, kuandaa na kuwasilisha wizarani orodha ya  walipakodi, idadi ya majengo na mabango yote yaliyoko katika mkoa wa Dar es Salaam  ili kupata takwimu sahihi za idadi ya walipakodi.

Dkt. Kijaji ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya kikazi katika Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Mkoa wa Kikodi wa Temeke ili kukagua utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka hayo ili kubaini fursa na changamoto za masuala ya ukusanyaji kodi.

Amesema kuwa pamoja na Mamlaka hiyo kufanya vizuri katika makusanyo ya mapato Mwezi Septemba, 2019, ambapo kiasi cha shilingi trilioni 1.78 kimekusanywa, kiasi hicho bado ni kidogo ikilinganishwa na mwamko wa wananchi uliopo hivi sasa katika kulipa kodi.

Aidha Mhe. Kijaji amerejea kuitaka TRA kuwasilisha kwake takwimu ya ongezeko la walipa kodi lililotokana na zoezi la kugawa vitambulisho vya wajasiriamali nchini kwa kuwa lengo la Mhe. Rais Dkt. John Magufuli kugawa vitambulisho hivyo lilikuwa ni kuongeza wigo wa walipa kodi watakao kuwa wanafuzu kwa kuongeza mitaji yao, hivyo ni vyema kujua idadi yao kamili na mahali walipo.

Kwa upande wa kodi ya majengo, Dkt. Kijaji ameitaka Mamalaka ya Mapato Tanzania kuhakikisha inapata orodha ya nyumba zote nchini kwa kuorodhesha wamiliki wa nyumba hizo na mawasiliano yao na kisha kuandaa kanzidata itakayosaidia kurahisisha ukusanyaji wa kodi hiyo.

“Ili kuongeza mapato yanayotokana na kodi ya majengo ni lazima TRA wafanye kazi usiku na mchana kuhakikisha kanzidata hiyo inakamilika ambayo itatumika kuwakumbusha walipa kodi kupitia ujumbe mfupi wa simu ambapo itasaidia katika ukusanyaji wa kodi hiyo kama ilivyo kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inapowakumbusha wananchi kulipa kodi a ardhi kupitia simu zao

” Alisema Dkt. Kijaji

“Nataka pia mkague watumiaji wote wa mashine za utoaji risiti za kieletroniki (EFD) kwa wafanyabiashara wa Temeke ili kuhakikisha kila anayeuza anatoa risiti na anayenunua anadai risiti na kwa kufanya hivyo itasaidia  kuongeza makusanyo ili Taifa liendelee kujitegemea kimapato” alisisitiza Dkt. Kijaji

Awali akimkaribisha Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, Mkoa wa Kikodi wa Temeke, Bw. Paul Walalaze, alisema mkoa wake una idadi ya walipakodi 437,539 na kwamba katika mwaka 2018/19, mkoa wake ulipanga kukusanya shilingi bilioni 395 na kufanikiwa kukusanya sh. bilioni 328.5 sawa na asilimia 85 ya lengo.

“Tumekusanya pia kodi ya majengo sh. bilioni 1.4 kati ya malengo ya kukusanya bilioni 1.6, kodi ya mabango sh. bilioni 2.2 kati ya lengo la kukusanya sh. bilioni 2.3 sawa na mafanikio ya asilimia kati ya 87 na asilimia 95" aliongeza Bw. Walalaze.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Bw. Hamisi Lupenja, amemhakikishia Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Kijaji kwamba watatekeleza maelekezo yote yaliyotolewa ili kuboresha ukusanyaji wa mapato ya Serikali ikiwemo kutoa elimu kwa walipakodi.

Mwisho


Share:

Waziri Mkuu Asisitiza Mshikamano Kwa Watanzania ....Ashiriki Mbio Za Mwenge Kijijini Kwao

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania waendelee kushikamana na wazingatie ujumbe wa mbio za mwenge za mwaka huu unaohimiza umuhimu wa maji, uchaguzi wa Serikali za mitaa, vita dhidi ya rushwa, malaria, UKIMWI na dawa za kulevya.

Ametoa wito huo leo asubuhi (Jumatano, Oktoba 9, 2019) wakati akizungumza na viongozi wa Halmashauri za Lindi na Ruangwa na wananchi wa kijiji cha Nangumbu kwenye uwanja wa shule ya msingi Nangumbu ambako mwenge huo ulipokelewa saa 1:44 asubuhi ukitokea Nyangao wilayani Lindi.

Waziri Mkuu ambaye ni mbunge wa jimbo la Ruangwa, aliwasili wilayani Ruangwa jana jioni, ili kushiriki mbio za mwenge. Kesho (Alhamisi, Oktoba 10) mwenge huo utaelekea Nachingwea, ambapo Ijumaa (Oktoba 11) utaenda Liwale, Jumamosi (Oktoba 12) utaenda Kilwa na Jumapili (Oktoba 13) utakuwa Manispaa ya Lindi ambako utahitimisha mbio hizo na kuzimwa Oktoba 14, mwaka huu.

Waziri Mkuu amewataka wananchi wote wajiandikishe kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili Tanzania iweze kupata viongozi bora. “Tuitikie kaulimbiu ya mwaka huu kwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Hapa Ruangwa, hadi jana jioni watu 28,000 walikuwa tayari wamejiandikisha. Tukachague viongozi wachapakazi na waadilifu watakaoleta maendeleo kwa nchi yetu,” amesisitiza.

Mapema, akizungumza baada ya kupokea mwenge huo saa 2:21 asubuhi, Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Bw. Hashim Mgandilwa alisema utakimbizwa kwenye kata saba na vijiji 17 ambapo miradi mitatu mikubwa yenye thamani ya sh. bilioni 2.9 itazinduliwa.

Katika kijiji cha Nangumbu, mwenge ulizindua mradi wa mabweni na klabu ya kupiga vita rushwa kwenye shule ye sekondari ya Hawa Mchopa. Ukiwa njiani, mwenge huo ulipitishwa kijiji cha Nandagala ambako Waziri Mkuu alizaliwa. Pia aliupokea na kuukimbiza kidogo akiwa na wanakijiji wenzake, kisha mwenge huo ukaendelea kukimbizwa kuelekea kata ya Likunja ambako watazindua mradi wa maji wa Kitandi. Pia mwenge huo utazindua mradi wa barabara ya lami kwenye kata ya Nachingwea, iliyoko Ruangwa mjini.

Akizungumza kabla ya kuanza kwa mbio za mwenge wilayani Ruangwa, kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa, Bw. Mzee Ali Mkongea alimshukuru Waziri Mkuu kwa kujumuika na wananchi kushiriki ratiba ya mapokezi ya mwenge wilayani humo.

Alisema Serikali ya awamu ya tano, ndani ya miaka mitatu (2015-2018) imekamilisha kwa wakati miradi 124 ya maji ambapo aliitaja baadhi yake kuwa ni miradi mikubwa ya Chalinze, Bagamoyo, Arusha, Tabora na Musoma. Pia alisema Serikali imeendelea na uchimbaji wa visima virefu na vifupi vya maji kwa gharama ya sh. bilioni 14.

“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzana kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zimeingia mkataba na Serikali ya India wa dola za Marekani milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maji kwenye miji 28 ya Tanzania. Lakini kuna changamoto nyingi kwenye miradi hii ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za umma na wakandarasi kujenga baadhi ya miradi chini ya kiwango.”

“Pia kumekuwa na shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji. Wananchi tusaidiane kuvilinda vyanzo hivi kwa sababu kazi ya kuvitunza si ya Serikali peke yake bali inaanza na mimi na wewe,” alisema.

Aliwasihi wananchi hao wajitokeze kwa wingi kujiandikisha kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili waweze kuchagua viongozi wazalendo ambao wana calibre ya Rais, Dkt. John Pombe Magufuli.

Akitoa takwimu za ugonjwa wa malaria nchini, Bw. Mkongea alisema mkoa wa Kigoma unaongoza kwa maambukizi ya ugonjwa huo kwa asilimia 24, ukifuatiwa na Geita (asilimia 17), Mtwara (asilimia 15) na Lindi wenye asilimia 12. 

“Niwasihi wananchi tumieni vyandarua vinavyotolewa bure na Serikali hasa akinamama wajawazito na watoto walio na umri chini ya miaka mitano. Kuna maeneo tumekuta baadhi ya watu wakivitumia kuvulia samaki na kufungia bustani ili kuku wasiingie. Haya si matumizi yake hata kidogo,” alisisitiza.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo


Share:

MAADHIMISHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KITAIFA 2019 KUFANYIKA MKOANI SINGIDA

 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mjini hapa leo, kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani Kitaifa 2019 yanayo tarajiwa kuanza kufanyika mkoani Singida kuanzia kesho. 
 Waandishi wa habari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na Waandishi wa habari ukiendelea.





Na Dotto Mwaibale, Singida

MAADHIMISHO ya Siku ya Chakula Duniani Kitaifa yanatarajiwa kufanyika mkoani Singida ambapo Tanzania itaungana na nchi wanachama wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) katika kusherehekea siku hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana Mkuu wa
Mkoa wa Singida Dkt. Rehema 
Nchimbi alisema mgeni rasmi katika maadhimisho hayoanatarajiwa kuwa Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga na kuwa yatazinduliwa kesho katika Uwanja wa Bombadia.

"Ndugu Wananchi napenda kuwafahamisha kuwa mkoa wetu
wa Singida umepewa heshima na Taifa kuwa mwenyeji wa Siku ya ChakulaDuniani.Maadhimisho haya yatazinduliwa kesho Oktoba 10, 2019 natoa wito kwawananchi wa Singida na mikoa jirani kujitokeza kwa wingi kwenye Uwanja waBombadia ambako maadhimisho hayo yatafanyika kuanzia kesho na kufikia kilele
chake Oktoba 16, 2019.

Dkt. Nchimbi alisema kaulimbiu ya maadhimisho hayo  inasema “Lishe Bora kwa Ulimwengu Usio na Njaa” na kuwa kauli mbiu
hiyo inalenga kuhamasisha jamii na wadau wote wa sekta kilimo kuchangia katikakuhakikisha nchi na dunia inakuwa na chakula cha kutosha wakati wote.

Alisema Takwimu za Wizara ya Kilimo zinaonyesha hali ya
upatikanaji chakula mwaka 2019/2020 ni nzuri, kwani nchi, ina chakula cha kutosha. Kiwango cha utoshelevu wa chakula ni asilimia 119. Uzalishaji wa mazao ya chakula ulifikia tani 16,408,309 ukilinganisha na mahitaji ambayo ni
tani  13,842,536. 


Kati ya hizo Tani9,007,909 ni mazao ya nafaka na tani 7,400,400 ni mazao yasiyonafaka.Tunawapongeza watanzania kwa kutekeleza kauli mbiu hii kwa vitendo.

Share:

7 Job Opportunities at Geita Gold Mining Ltd (GGML), Service Crews

Service Crews  Geita Gold Mining Ltd (GGML) is committed to promoting skills and development of its employees through on job training and career opportunities both on site and within AngloGold Ashanti. This facilitates knowledge transfer between employees which in a long run enables the company to have a dedicated talent pool for a variety of positions in its… Read More »

The post 7 Job Opportunities at Geita Gold Mining Ltd (GGML), Service Crews appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

HALMASHAURI YA BUKOBA KUANZISHA KLABU ZA LISHE SHULENI


Afisa lishe wa Halmashauri ya wilaya ya Bukoba Desdery Karugaba 
Na Lydia Lugakila- Malunde 1 blog
Halmashauri ya wilaya ya Bukoba mkoani Kagera kwa kushirikiana na wadau wa lishe wameweka mkakati wa kuanzisha klabu za lishe katika shule za msingi na sekondari ili kutoa elimu hasa kwa kundi la vijana balehe kutokana na kundi hilo kuwa mahitaji makubwa ya ki lishe.

Hayo yamebainshwa Oktoba 8, 2019 na Afisa lishe wa halmashauri hiyo,Desdery Karugaba wakati wa kikao cha kamati ya lishe kwa kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Bukoba mkoani Kagera.

Afisa huyo amesema halmashauri hiyo imefanikiwa katika mpango wa lishe kwa makundi ya watoto wachanga,wajawazito isipokuwa kundi ambalo limesahaulika ni vijana barehe ambalo ni eneo muhimu kwa uzazi ujao hivyo wamepanga mikakati ya kuanzisha klabu za lishe katika shule za msingi na sekondari.

Amesema Vijana balehe (wenye umri wa miaka 9 hadi 20) ni kundi ambalo lina mahitaji makubwa ya ki lishe kwa sababu ukuaji wake huenda kwa kasi na kusababisha mahitaji ya ki lishe kuongezeka hivyo kundi hili lazima lipate elimu ya kutosha ya ki lishe ili kujua ni vyakula gani vinahitajika.


Share:

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*


Share:

Kasi Ya Usilizaji Mashauri Imemaliza Mrundikano Wa Kesi Mahakamani

Na Ismail Ngayonga-MAELEZO
KATIKA nchi inayoazimia kuwa na uchumi unaokuwa kwa kasi, ni lazima migogoro inayowasilishwa Mahakamani ikamilike kwa haraka ili kuwawezesha wananchi watumie muda wao mwingi katika uzalishaji mali.

Kumekuwa na dhana kuwa mashauri ya jinai na madai yanapochelewa kukamilika mahakamani, basi ni mahakama tu ndiyo inayochelewesha utoaji haki pasipo na kuelewa kuwa katika mnyororo wa utoaji haki kuna wadau muhimu wanaopaswa kutimiza wajibu wao kwa wakati.

Wadau hao ni pamoja na Wizara ya Katiba na Sheria, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Ofisi ya Taifa ya Mashtaka/DPP, Jeshi la Polisi, Mkemia Mkuu wa Serikali, Jeshi la Magereza, Mabaraza ya Ardhi na Nyumba, Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Tume ya Kurekebisha Sheria (LRC).

Wengine ni pamoja na Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kamishna wa Kazi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Serikali ni wadau muhimu na wezeshi kwa Mahakama na utoaji haki ambao wamekuwa wakishirikiana kwa karibu zaidi na wananchi kwa kuhakikisha kuwa wanafuata taratibu za kimahakama za uendeshaji mashauri, wanahudhuria Mahakamani kadri wanavyoitwa pamoja na kukata rufaa ndani ya muda uliowekwa kisheria.

Hatua zote hizi zitasaidia Mahakama kuwahudumia kwa wakati, na kwa ubora zaidi pamoja na kuwahimiza wananchi  kuwa na jukumu la kufahamu taratibu za sharia ikiwemo hatua za mwanzo zinazopaswa kufahamika na mwananchi katika kufungua shauri Mahakamani na kuhakikisha kuwa  anafahamu hatua zote kesi yake itapitia katika ngazi ya Mahakama zote hadi Mahakama ya Rufani.

Akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2019/2020 Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Augustine Mahiga anasema  kupunguza mlundikano wa mashauri mahakamani ni ni moja ya vipaumbele muhimu vya Serikali katika kuhakikisha kuwa wananchi wote wanapata haki sawa na kwa wakati.

Anaongeza kuwa katika kufanikisha azma hiyo, Mahakama ya Tanzania  mwaka 2018 ilianza ikiwa na jumla ya mashauri 65,223, na kusajili mashauri mapya 259,476 katika ngazi zote za Mahakama, ambapo mashauri 255,836 yalitolewa uamuzi ikiwa ni sawa na asilimia 99 ya mashauri yote yaliyofunguliwa katika kipindi hicho.

Dkt. Mahiga anaongeza kuwa mashauri yaliyobaki mahakamani ni 68,863 na kati ya hayo, mashauri yenye umri zaidi ya miaka miwili (mashauri ya mlundikano) ni 3,435 sawa na asilimia 5 tu ya mashauri yote yaliyobaki.

Kwa mujibu wa Waziri Mahiga anasema Kwa ngazi ya Mahakama ya Rufani, mwaka 2018 ulianza na mashauri 2,933 na kusajili mashauri mapya 1,499 ambapo mashauri 1,184 yalisikilizwa na kutolewa uamuzi, sawa na asilimia 79 ya mashauri yote yaliyosajiliwa katika kipindi hicho na mashauri yaliyobaki mahakamani ni 3,248.

’Bila shaka, ongezeko la idadi ya majaji wa Mahakama ya Rufani baada ya uteuzi wa hivi karibuni wa majaji 6 wa mahakama hiyo litasaidia kuharakisha usikilizaji wa mashauri ikilinganishwa na miaka iliyopita’ anasema Waziri Mahiga.

Waziri Mahiga anasema katika ngazi ya Mahakama Kuu, Masjala Kuu, Kanda na Divisheni, mashauri yaliyokuwepo ni 19,207 na mashauri mapya yaliyosajiliwa ni 18,284 na mashauri yaliyoamuliwa katika kipindi hicho ni 17,046, sawa na asilimia 93 ya mashauri yaliyosajiliwa wakati mashauri yenye umri wa miaka miwili na zaidi ni 1,860 sawa na asilimia 6 ya mashauri yaliyobaki, yakiwemo mashauri 100 yenye miaka 5 na zaidi.

Akifafanua zaidi Waziri Mahiga anasema kwa upande wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya, zilianza mwaka 2018 na mashauri 24,840 na kusajili mashauri mapya 51,161 ambapo jumla ya mashauri 47,089 yalimalizika, sawa na asilimia 92 na kubakiwa na mashauri 28,912, yakiwemo mashauri 837 yenye umri wa kati ya mwaka mmoja na miaka miwili.

‘Mahakama za mwanzo nchini ndizo zinazoongoza kwa kufungua na kusikiliza idadi kubwa ya mashauri kuliko mahakama za ngazi nyingine ambapo katika mwaka 2018 mahakama hizi zilianza na mashauri 15,055 na kusajili mashauri mapya 177,566’ anasema Waziri Mahiga.

Kwa mujibu wa Waziri Mahiga anasema Mashauri yaliyomalizika ni 176,542 sawa na asilimia 99, na kubakia mashauri 16,079 tu kwa nchi nzima na kati ya mashauri 16,079 yaliyobaki, mashauri ya mlundikano yaliyokuwa na zaidi ya miezi 6 Mahakamani kwa ukomo wa Mahakama hizi ni tisa ambayo yapo katika wilaya za Babati (1), Muleba (6) na Tarime (2).

Aidha Waziri Mahiga anasema katika kuimarisha utawala bora, maadili na uwajibikaji wa watumishi, Mahakama ya Tanzania ilifanya ukaguzi wa huduma za kimahakama katika kanda zote 14 za Mahakama Kuu na kuhusisha vituo 839 vya mahakama.

Anazitaja Mahakama hizo ni pmaoja na Mahakama za mwanzo, mahakama za wilaya na Mahakama Kuu kati ya vituo 980 vilivyopo nchini, sawa na asilimia 86 ikiwemo Vituo vya Mahakama za Mwanzo 717 841 sawa na asilimia 85, Mahakama za Wilaya 97 kati ya Mahakama 111, sawa na asilimia 89 na Mahakama za Hakimu Mkazi vituo 25 kati ya 28 sawa na asilimia 89.

‘Aidha, jumla ya malalamiko 1,046 ya wananchi yanayohusu kero za upatikanaji wa huduma mbalimbali za mahakama yalipokelewa ambapo malalamiko 951, sawa na asilimia 91 yalishughulikiwa’ anasema Waziri Mahiga.

Wadau wa Mahakama wakimaliza wakitimiza wajibu wao kwa wakati, wanaiwezesha mahakama kumaliza mashauri na mwanachi kupata haki yake kwa wakati sambamba na wananchi kusoma sheria ili angalau wawe na uelewa ili kutowaachia wanasheria peke yao jukumu la kufahamu taratibu za sheria.

MWISHO



Share:

TAKUKURU KUMPANDISHA KIZIMBANI HAKIMU KUOMBA RUSHWA AKISINGIZIA HAKIMU MWENZAKE KISHAPU


Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Hussein Mzee Mussa
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Shinyanga inatarajia kumfikisha Mahakamani Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Kishapu Benjamin Charles Mhangwa kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa kinyume cha kifungu cha 15 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na 11 ya Mwaka 2007.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Oktoba 9,2019 Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Hussein Mzee Mussa amesema hakimu huyo aliomba na kupokea kiasi cha shilingi 200,000 kati ya shilingi 300,000/= alizoomba kutoka kwa Juma Mbugi kuwa ametumwa na hakimu wa wilaya ya Kishapu Wilberforce Luwago ili kusaidia kupata ushindi katika kesi ya kubakwa kwa mwanawe.

Aidha kwa mujibu wa uchunguzi uliofanyika umebaini kuwa fedha hizo hazikuombwa na hakimu Mkazi Mfawidhi wa wilaya ya Kishapu Wilberforce Luwago hivyo mtuhumiwa huyo aliomba na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Share:

Halmashauri Zatakiwa Kupitia Upya Maeneo Yaliyotengwa Kwa Shughuli Za Jamii

Na Munir Shemweta, WANMM MWANZA
Halmashauri zote nchini zimetakiwa kupitia upya maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii kama vile makaburi, maeneo ya wazi, ujenzi wa taasisi za umma na masoko ili kujiridhisha kama bado yanafaa kwa matumizi yaliyokusudiwa au yamevamiwa ili kurasimisha.

Agizo hilo limetolewa jana na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula wakati akikagua utekelezaji wa kupitia maeneo yaliyovamiwa katika wilaya za Ilemela na Nyamagana linalotekelezwa na wataalamu wa Ardhi kutoka Wizarani, Ofisi ya kanda ya Ziwa na Maafisa ardhi wa wilaya hizo.

Dkt Mabula alikemea kitendo kinachofanywa na baadhi ya halmashauri nchini kutolipa fidia katika maeneo wanayoyatwaa kunakosababisha kuzalisha migogoro isiyo ya lazima na uvamizi mpya katika maeneo hayo.

‘’Halmashauri zote nchini naziagiza kupitia upya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za kijamii tujue maeneo hayo yamevamiwa kwa kiasi gani, tuwafanyie urasimishaji wananchi walipe kodi ya serikali na kama eneo bado halijavamiwa basi tulilinde ili lisiendelee kutumika kwa matumizi yaliyo,kusudiwa ‘’ alisema Mabula

Aidha, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliwataka wataalamu wa ardhi nchini kuacha kukaa ofisini na badala yake waende kwa wananchi ili kuepuka kuitia hasara serikali kwa kutoa taarifa zisizo na uhakika.

Alitoa hofu wananchi wa mitaa ya Nyagungulu, Mwambani na Bukengwa yaliyopo kata ya Ilemela mkoani Mwanza kuwa, serikali ya awamu ya tano itaendelea kutatua migogoro ya ardhi kwa kuzingatia haki , sheria na ubinadamu.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Stanslaus Mabula, mbali na kumpongeza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kazi kubwa anayoifanya pia alimshukuru Rais John Pombe Magufuli kwa kuunda timu ya Mawaziri kupitia maeneo yote yenye changamoto za ardhi huku akiiomba halmashauri ya jiji la Mwanza kuhakikisha ulipaji fidia kwa wananchi wenye migogoro ya ardhi unafanyika.

Naye Kmaishna Msaidizi wa Ardhi kanda ya Ziwa Makwasa Biswalo alieleza kuwa, zoezi la ukaguzi maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za kijamii lilianza septemba 30, 2019 na kumalizika Oktoba 4, 2019 kabla ya kuongezwa siku nne na Naibu Waziri Dkt Mabula ambapo aliomba ushirikiano kutoka kwa wananchi na viongozi ili kukamilisha zoezi hilo kwa haraka na ufanisi.


Share:

MBOWE KUONGOZA MAZISHI YA MSANII WA CHADEMA LEO


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe leo Jumatano, Oktoba 09, 2019 ataongoza makundi mbalimbali ya waombolezaji kuuaga wa aliyekuwa mtunzi wa na msanii nyimbo za Chama hicho, Fulgence Mapunda.

Mwili wa mwanamuziki huyo utaagwa katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Moyo wa Mtakatifu wa Yesu, Manzese, jijini Dar es Salaam, shughuli hiyo ya utoaji wa heshima za mwisho itaenda sambamba na salaam za rambirambi na pole kutoka kwa makundi mbalimbali.

Taarifa iliyotolewa na chama hicho imeeleza kuwa ibada ya kumuombea marehemu Fulgence Mapunda itakayofanyika kanisani hapo kuanzia saa 6 mchana, baada ya mwili kuchukuliwa kutoka Hospitali ya Mwananyamala ulikohifadhiwa, na baada ya hapo mwili huo utasafirishwa kwenda Ruvuma.

Mazishi yatafanyika siku ya Ijumaa, Oktoba 10, 2019, katika Kijiji cha Lituhi, Nyasa.

Marehemu Fulgence Mapunda alifariki Dunia majira ya saa 4 usiku siku ya Jumapili, Oktoba 6, mwaka huu, akiwa Hospitali ya St. Monica alipokuwa amelazwa kwa ajili ya matibabu.
Share:

Mbowe kuongoza mazishi ya aliyekuwa mtunzi na msanii wa nyimbo za CHADEMA

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe leo Jumatano, Oktoba 09, 2019 ataongoza makundi mbalimbali ya waombolezaji kuuaga wa aliyekuwa mtunzi  na msanii wa nyimbo za Chama hicho, Fulgence Mapunda.

Mwili wa mwanamuziki huyo utaagwa katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Moyo wa Mtakatifu wa Yesu, Manzese, jijini Dar es Salaam, shughuli hiyo ya utoaji wa heshima za mwisho itaenda sambamba na salaam za rambirambi na pole kutoka kwa makundi mbalimbali.

Taarifa iliyotolewa na chama hicho imeeleza kuwa ibada ya kumuombea marehemu Fulgence Mapunda itakayofanyika kanisani hapo kuanzia saa 6 mchana, baada ya mwili kuchukuliwa kutoka Hospitali ya Mwananyamala ulikohifadhiwa, na baada ya hapo mwili huo utasafirishwa kwenda Ruvuma.

Mazishi yatafanyika siku ya Ijumaa, Oktoba 10, 2019, katika Kijiji cha Lituhi, Nyasa.


Share:

LIVE: Ziara Ya Rais Dkt.john Pombe Magufuli Mkoani Rukwa Leo October 9

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli anafanya ziara ya siku tatu Mkoani Rukwa ambapo anafungua na kukagua miradi ya Maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi wa Maeneo mbalimbali ya Rukwa na Wilaya zake


Share:

Jeshi La Polisi Dodoma Lakanusha Kuhusika Na Taarifa Za Kumpiga Mwananchi

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Jeshi la Polisi mkoa wa Dodoma limekanusha kuhusika na  taarifa za kumpiga Raia mmoja ajulikanaye kwa jina la   Elisha Hezron Wanjara[39] na kudai kuwa taarifa hizo sio za kweli na zimerushwa na Baadhi ya Vyombo vya Habari bila kufanyiwa uchunguzi.
 
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dodoma,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Girres Muroto amesema Tarehe 7,oktoba ,2019 Mwandishi wa Habari kupitia GLOBAL TV ONLINE ,Bw.Mohamed Zengwa alirusha katika mitandao ya kijamii habari ya mtu mmoja aitwaye ELISHA HEZRON WANJARA[39]MJITA Fundi Ujenzi wa Barabara katika kampuni ya STECOL inayofanya kazi za ujenzi hapa Dodoma  ambapo taarifa hizo zilidai mtu huyo alipigwa na Jeshi la Polisi.
 
Kamanda Muroto amesema katika taarifa hiyo ilifafanua kuwa Bw.WANJARA alipigwa na askari polisi wa doria na kuporwa simu pamoja na fedha kiasi cha Tsh.Elfu 70 na kupakiwa kwenye gari la polisi na kuwekwa kwenye mahabusu ya Polisi  na baadaye kuachiliwa huru bila matibabu,bila kurejeshewa simu na pesa zake  na alikwenda kwa mkuu wa wilaya na kuongea naye juu ya jambo hilo na kurusha mtandaoni.
 
Hata hivyo,Kamanda Muroto amesema habari hiyo ni ya uongo na haina ukweli wowote  hivyo Bw.WANJARA alisema  uongo ,hakuibiwa simu ,hakuporwa fedha wala kupigwa na askari  kama alivyojieleza kwa mwandishi wa habari mbele ya mkuu wa wilaya wa  Dodoma mjini.
 
Aidha,Kamanda Muroto ameelezea Ukweli wa tukio kuwa ,siku ya Tarehe 6/10/2019  Bw.Elisha Hezron Wanjara na Mwenzake mmoja aliyejulikana kwa jina la utani NGINJANGINJA walikwenda nyumbani kwa Paulo Mkazi wa Mtaa wa IPAGALA akitafuta chumba cha kupanga na walimchukua mwenyeji wao wakaenda kunywa pombe za kienyeji nyumbani kwa mama Eliza.
 
Kamanda Muroto ameendelea kufafanua kuwa ,wakati wanaendelea kunywa pombe ,Bw.WANJARA alimpatia Simu Bw.PAULO CHIPAGALA awapige picha na aliwapiga picha mbalimbali wakati wanakunywa pombe na baada ya kulewa walianzisha ugomvi mkubwa  na kupigana kwa muda mrefu.
 
Hivyo,waliumizana na wote wakasambaratika eneo hilo  na haikujulikana kila mmoja alikokwenda  na simu aliendelea kubaki nayo PAULO CHIPAGA  aliyepewa na mwenye simu kabla ya kulewa na kupigana.
 
Kamanda Muroto amebainisha ,usiku wa saa 3:45 Elisha Wanjara aliokotwa na wapiti njia na kumpeleka kituo cha polisi  Central Dodoma akiwa amelewa pombe ,hajitambui na ana majeraha ya kupigwa  na aliandikiwa PF3 ili aende kutibiwa  na waliompeleka ni watu walewale waliomleta kituoni.
 
Baada ya kurudisha PF3 aliyopewa kituo  cha Polisi ,kulipopambazuka alikwenda kwa mkuu wa wilaya ya Dodoma ,akatoa taarifa na maelezo ya uongo kuhusu jeshi la polisi akisingizia askari kumpiga ,kupora simu na fedha.
 
Kamanda Muroto amevieleza vyombo vya habari kuwa,Jeshi la polisi limefanya uchunguzi kuhusu tukio hilo  na kubaini ukweli na mafanikio ambayo ni Bw.WANJARA hakukamatwa na askari polisi kwenye msako,simu haikuporwa,bali alimpatia PAULO CHIPAGA na ilipatikana kutoka kwa CHIPAGA,Majeraha aliyopigwa ni kutokana ugomvi wake na mwenzake.
 
Mambo mengine yaliyobainishwa na Jeshi la polisi kuwa ni hakuporwa Tsh.70,000,na siku ya tukio aliomba Tsh.5000 kutoka kwa JOHN NTALE Msimamizi wake wa kazi,amewasingizia askari polisi na kutoa maelezo ya uongo kwa mkuu wa Wilaya  na kuudanganya umma wa Tanzania na kulichafulia jeshi la Polisi kwa tukio la kuunda na Maneno ya uongo.
 
Kwa upande wake Bw.WANJARA amehojiwa na amekiri kuwa alitoa taarifa za uongo na alikuwa amelewa pombe.
 
Kutokana na tukio hilo,mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi la polisi na amefunguliwa mashtaka kwa kutoa taarifa za uongo  na atafikishwa mahakamani hivyo kamanda Muroto ametoa onyo kwa wanaotumia vibaya ofisi za serikali kutoa taarifa za uongo  na kuwataka wanahabari kuzifanyia uchunguzi na subira habari kabla ya kuzirusha ili kuondoa mkanganyiko katika jamii.






Share:

TAKUKURU SHINYANGA YAWAONYA WAGOMBEA KUENDEKEZA RUSHWA KWENYE UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA


Kaimu Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Shinyanga Hussein Mzee Mussa akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu mikakati mbalimbali ya TAKUKURU kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 24 mwaka huu. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Shinyanga imetoa onyo kwa wagombea wote katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24,2019 kutojihusisha na vitendo vya rushwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Oktoba 9,2019, Kaimu Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Shinyanga Hussein Mzee Mussa amesema ni vyema wagombea wote katika uchaguzi kuwa makini na mienendo yao na kuhakikisha kwa namna yoyote hawajihusishi na vitendo vya rushwa.

"Wagombea wote wawe makini na vitendo vyovyote kinyume na sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na.11 ya mwaka 2007 pamoja na sheria ya gharama za uchaguzi kama zilivyoanishwa na sheria ya gharama za uchaguzi Na. 6 ya mwaka 2010",amesema Mussa.

Amebainisha kuwa mikakati ya TAKUKURU kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ni kutoa elimu ya rushwa kwa njia ya mikutano ya hadhara,semina mbalimbali na kupitia vyombo vya habari.

"Tunatoa elimu ya rushwa kwa wananchi wote wakiwemo wapiga kura na watakaogombea nafasi za uongozi. Elimu hii inahusu athari za rushwa kwenye uchaguzi,makosa ya rushwa katika uchaguzi kisiasa,sheria ya gharama za uchaguzi kama zilivyoainishwa na sheria ya gharama za uchaguzi Na. 6 ya mwaka 2010 na makosa yaliyo kwenye sheria ya Kuzuia na kupambana na rushwa Na. 11 ya mwaka 2007",ameeleza Mussa.

"Nitoe wito kwa wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa TAKUKURU ili kuhakikisha kuwa tunaondoa kero ya rushwa hasa katika kipindi hiki tunachoelekea kuanza michakato ya uteuzi wa wagombea wa uongozi wa serikali za mitaa",ameongeza Mussa.
Share:

Majengo Matatu Yakabidhiwa Kwa Wizara Ya Madini

Na Tito Mselem, Simiyu
Naibu Waziri wa Wadini Stanslaus Nyongo akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Atashasta Nditiye amekabidhiwa jengo la kituo cha umahiri Mkoani Simiyu.

Mpaka sasa majengo matatu ya Wizara ya Madini yamekabidhiwa baada ya kukamilika kwa asilimia 100 ambayo yamegharimu zaidi ya shilingi bilioni 4.4 ambapo Wizara kupitia mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP) ilitenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vitua vya umahiri  saba nchi nzima kikiwemo kituo cha Simiyu kilicho gharimu shilingi Bilioni 1.308

Imeelezwa kuwa kampuni ya SUMA JKT iliingia mkataba na Wizara ya Madini ili kukamilisha Ujenzi wa Vituo vyote saba nchi nzima ambapo Kituo cha Simiyu Ujenzi wake ulianza tarehe 5 septemba, 2018 na kukamilika Septemba, 2019.

Akizungumza kwenye makabidhiano hayo Naibu Waziri wa Madini Nyongo alisema Lengo la vituo hivi pamoja na mambo mengine ni kutoa mafunzo ya kitaalam  yahusuyo Madini, mafunzo haya yatahusu Utafiti wa Madini, ikiwa ni pamoja na kuonesha  mikanda ya Madini ilipo na muelekeo wake,  Uchimbaji wa Madini wenye tija na salama, Uchenjuaji wenye kuleta uvunaji mkubwa wa madini na hivyo kuwapatia faida kubwa wachimbaji, pia katika majengo haya kutakuwa na mafunzo ya kuomba leseni kwa njia ya mtandao na kutakuwa na usagaji wa mawe  na kupima sampuli za madini mbalimbali.

“Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) ulifanya utafiti wa kijiolojia na kubaini maeneo saba muhimu ambayo vituo vya umahiri vitajengwa pakiwemo Simiyu,” Nyongo alisema.

Baada ya Naibu Waziri kukabidhiwa jengo hilo nae alilikabidhi kwa Tume ya Madini na kuwataka Ofisi ya Madini Simiyu kulitumia vizuri jengo hilo ili lilete manufaa yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na kuwapatia wachimbaji wadogo mafunzo ya namna bora ya kuendesha shughuli zao ili wafanye shughuli zao kwa ufanisi na hatimae kuongeza makusanyo ya Serikali.
 
Wakati huo huo, Naibu Waziri ametoa wito kwa wachimbaji wa madini na wananchi kwa ujumla wakitumie kituo hicho cha Simiyu ili kujifunza na kupata taarifa kuhusiana na shughuli za utafiti na uchimbaji madini kwa kuwa kituo hiki kimejengwa kwa ajili ya wananchi na kwa kodi za wananchi.

Kwa upande upande wake mkuu wa Mkoa wa Simiyu Antony Mtaka aliipongeza Wizara ya Madini kwa ujenzi wa kituo hicho muhimu kitakacho wasaidia wachimbaji wengi wa madini katika Mkoa wa Simiyu.

Aidha wake kaimu meneja wa mradi wa usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP) Veronica Francis alisema kuwa   mradi huo umegawanywa katika sehemu kuu tatu ambazo ni kuongeza unufaikaji kutokana na sekta ya Madini kwa Nchi, kukuza uwazi na uwajibikaji katika Sekta ya Madini na Mafunzo na Usimamizi wa Mradi.   

“Mradi ulijikita katika kutekeleza kazi mbalimbali zikiwemo  ujenzi wa vituo saba vya umahiri, ujenzi wa vituo vya mfano, ukarabati wa ofisi za madini, ununuzi wa vifaa vya ofisi za madini, ununuzi wa samani za ofisi, utafiti wa kijiolojia katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya uchimbaji mdogo, na kuongeza ushirikiano na serikali za mitaa zinazofanya shuguli za madini,” Veronica alisema.

“Tumeamua kujenga kituo cha umahiri Simiyu kwa kuwa utafiti wa kijiolojia umebaini kuwepo na mashapo ya kutosha katika maeneo ya Nyaranja Meatu na kuwepo na madini ujenzi, pia Mkoa kuna taarifa za awali za kijiolojia zikionesha utafiti mkubwa wa Madini ya Nickel kule Dutwa na Ngasamo,” Veronica aliongeza.

Vilevile, Wizara kupitia Mradi imejenga jengo la taaluma katika Chuo cha Madini (MRI) kwa ajili ya matumizi ya ofisi, madarasa, kumbi za mikutano na ofisi za ushirika wa wachimbaji madini wanawake Tanzania kwa ajili ya kuendeshea shuguli zao.

Kazi za ujenzi kwa baadhi ya majengo zimekamilika na mengine yapo katika hatua za ukamilishaji na Mkandarasi anatarajia kukabidhi Majengo hayo hivi karibuni kwa jumla ya gharama ya Sh.7.897 kwa majengo yote saba.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger