Monday, 13 May 2019

Waziri Mkuu Apokea Watalii 330 Kutoka China ..... Ni Kundi La Kwanza Kati Ya Watalii 10,000 Wanaotarajiwa Kuja Tanzania

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewapokea watalii 330 wakiwemo wafanyabiashara na wawekezaji kutoka jimbo la Zhejiang, China ambao waliwasili jana usiku kwenye uwanja wa ndege wa KIA.

Watalii hao ni kundi la kwanza miongoni mwa watalii 10,000 ambao wanatarajiwa kutembelea Tanzania mwaka huu, chini ya mpango unaosimamiwa baina ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Bodi ya Utalii Tanzania na kampuni ya TouchRoad International Holding Group ya China.

Akizungumza na watalii hao kwenye chakula cha jioni kilichoandaliwa kwenye hoteli ya Mount Meru jana usiku (Jumapili, Mei 12, 2019), Waziri Mkuu alimshukuru Mwenyekiti wa Touchroad Group, Bw. Liehui He kwa kuwaunganisha Watanzania na Wachina kupitia mpango wake wa kukuza utalii.

“Mbali na kutuunganisha Watanzania na Wachina, tunakushukuru pia kwa kuamua kuitangaza Tanzania kuwa nchi yenye fursa nyingi za kitalii duniani,” alisema.

Waziri Mkuu alitaja vivutio vingine vilivyopo ambavyo watalii hao wanaweza kuvifurahia kuwa ni mbuga za Ngorongoro, Serengeti, Manyara, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Katavi na akawataka waende visiwa vya Zanzibar kuona fukwe zenye mchanga mweupe na kupata marashi ya karafuu.

Waziri Mkuu aliwapongeza watendaji wa Bodi ya Utalii na makampuni ya utalii kwa maandalizi na mapokezi mazuri kwa watalii hao. Pia alimpongeza Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kushirikiana na TouchRoad na kuifanya Tanzania ipokee watalii wengi.

Akielezea ujio wa kundi la kwanza la watalii, Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini, Bi. Devotha Mdachi alisema watalii hao wametokea Djibouti ambako walikaa kwa siku moja, hapa Tanzania watakaa kwa siku nne na kisha wataelekea Bulawayo, Zimbabwe ambako watakaa kwa siku mbili na kurejea China.

Mapema, akizungumza katika mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Prof. Palamagamba Kabudi alisema ujio wa watalii hao ni sehemu ya mpango mkubwa wa nchi wa kuongeza watalii kutoka China unaofahamika kama Tour Africa - The New Horizon.

Aliwataka Watanzania wachangamkie fursa ya ujio wa wageni ili waweze kunufaika kiuchumi. “Naomba niwasihi Watanzania, hii ni fursa hatuna budi kuichangamkia ili wao wafurahie utalii nchini lakini nasi tunufaike na uwepo wao.”

Naye Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangallah alisema Serikali imeamua kuwekeza zaidi kwenye utalii kwa kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini ili iweze kuongeza idadi ya watalii na hatimaye kukuza uchumi.

Alisema wameamua kubadilisha maeneo ya vipaumbele vya utalii na kujitangaza kwenye nchi nyingine ili tuweze kufikia lengo letu la kuongeza idadi ya watalii.

“Tuliamua kuwekeza katika nchi tano za kipaumbele cha kwanza ambazo ni Marekani, Ujerumani, Uingereza, Ufaransa na Italia. Sasa hivi uelekeo wetu ni China, Israel, Oman na nchi zote za Ghuba, Australia na Urusi,” alisema.

Jimbo la Zhejiang liko Kusini Mashariki mwa China na majimbo yenye nguvu ndogo kisiasa lakini ni mojawapo ya majimbo yenye wakazi wengi na matajiri. Pia jimbo hilo ni maarufu kwa shughuli za kilimo na linaongoza kwa uzalishaji wa chai na mazao yatokanayo na uvuvi.

Viongozi wengine waliokuwepo ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Kangi Lugola, Waziri wa Nchi (OWM-Uwekezaji), Bibi Angela Kairuki, Naibu Waziri (OWM-KAV), Bw. Anthony Mavunde, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Dkt. Damas Ndumbaro, Balozi wa Djibouti nchini China na Balozi wa Tanzania nchini China.

(mwisho)
IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Serikali Yafanikiwa Kupeleka Huduma Za Kibenki Vijijini

Na. Peter Haule na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma
Serikali imesema kuwa Vituo vyote vya huduma ndani ya Ofisi za Shirika la Posta vimeunganishwa kwenye mtandao na mfumo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano- TEHAMA wa Benki ya TPB  kwa wateja wa vijijini na pembezoni mwa miji, ili kuwawezesha wananchi kupata huduma kwa wakati kama ilivyo kwa wateja wengine wanaohudumiwa na matawi makubwa na madogo

Hayo yameelezwa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) alipokuwa akijibu swali la Msingi la Mbunge wa wa Tumbatu Mhe. Juma Othman Hija, aliyetaka kujua iwapo Benki ya TPB imefikia malengo ya kupeleka huduma vijijini na maeneo yasiyofikika kwa urahisi.

Dkt. Kijaji alisema kuwa lengo la Benki ya TPB ni kuongeza wigo  wa biashara ya benki kwa kutumia teknolojia ya kisasa katika maeneo ya vijijini, hivyo Benki hiyo imefanikiwa kuboresha huduma katika ofisi 200 za Shirika la Posta Tanzania kwa kutumia teknolojia ya TEHAMA inayomuwezesha mwananchi kupata huduma za kibenki kupitia simu za kiganjani, mawakala wa kampuni za simu pamoja na mashine za kutolea fedha (ATM) .

“Benki ya TPB  imeongeza idadi ya matawi makubwa kutoka 30 kwa mwaka 2017 hadi 36 kwa mwaka 2018 na matawi madogo yaliongezeka  kutoka 37 mwaka 2017 hadi kufikia 40 kwa mwaka 2018, yakiwa yanawawezesha wateja kupata huduma bila kutembelea matawi walipofungulia akaunti zao”, alieleza Dkt. Kijaji.

Alisema kuwa Idadi hiyo ya matawi inahusisha matawi yaliyokuwa ya Benki ya Twiga na Benki ya Wanawake Tanzania, aidha jumla ya akaunti 227,052 zilifunguliwa na wananchi wa vijijini na pembezoni mwa miji kwa kutumia mfumo wa kibenki kwa njia ya simu za kiganjani unaojulikana kama TPB Popote.


Share:

Serikali Inafanya Mazungumzo Na Cyprus Ili Kuwalipa Wateja Wa Benki Ya FBME

Na. Peter Haule na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Serikali ya Tanzania inafanya mazungumzo na Serikali ya Cyprus ili kuweza kutatua changamoto za malipo kwa wateja walioweka amana zao katika Benki ya FBME ambayo ilifutiwa leseni ya kufanya shughuli za kibenki hapa nchini na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Hayo yameelezwa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) alipokuwa akijibu swali la Msingi la Mbunge wa Viti maalaum  Mhe. Asha Abdullah Juma, alieuliza kuhusu hatua zilizochukuliwa na Serikali kuwasaidia wananchi walioweka amana zao katika Benki ya FBME.

Dkt. Kijaji alisema kuwa zoezi la kukusanya mali na fedha zilizokuwa za Benki ya FBME katika taasisi mbalimbali za fedha hasa zilizopo nje ya nchi, limekumbwa na changamoto za kisheria kati ya Tanzania na Cyprus ambako benki ya FBME ilikuwa ikiendesha sehemu kubwa ya biashara zake hivyo kusababisha ucheleweshaji wa ukusanyaji na ugawaji wa fedha na ufilisi.

“Hakuna tarehe rasmi ya kuanza kulipa fedha kwa sasa kutokana na uwepo wa kesi zinazokwamisha zoezi la ukusanyaji mali na madeni ya Benki ya FBME”, alieleza Dkt. Kijaji.

Alisema kuwa, Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006 inaeleza kuwa amana au akiba za wateja katika Benki au Taasisi zina kinga ya Bima ya Amana ya kiasi kisichozidi Sh. milioni 1.5,  na iwapo mteja ana salio la amana la kiasi kisichozidi Sh. 1.5 atapata fidia ya asilimia 100.

Aidha wateja walio na zaidi ya Sh. milioni 1.5 wanalipwa Sh. milioni 1.5 kama fidia ya bima ya amana na kiasi kinachobakia kinalipwa kwa mujibu wa Sheria na taratibu za Ufilisi.

Hata hivyo malipo kwa mujibu wa Sheria na taratibu za ufilisi yanategemea makusanyo ya fedha kutoka kwenye mauzo ya mali pamoja na fedha zilizowekwa na benki katika taasisi mbalimbali za fedha za ndani na nje ya nchi.

Mwisho.


Share:

Mkurugenzi wa Uchaguzi Dkt. Kihamia aridhishwa na utendaji kazi wa watumishi wa NEC

Hussein Makame
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Dkt. Athumani Kihamia ameeleza kuridhishwa na utendaji kazi wa watumishi wa tume hiyo kutokana na kufanya kazi kwa bidii, ushirikiano, weledi na uzalendo.
 
Dkt. Kihamia ameeleza hayo wakati alipokutana na wafanyakazi wa NEC kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kujadili mambo mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa majukumu ya Tume.
 
Alisema katika kipindi alichokaa Tume amegundua kuwa sasa utendaji kazi wa mazeoa umepungua na watumishi wengi wamekuwa wakitekeleza majukumu yao kwa wakati, kwa uaminifu, kutunza siri na kuepuka matumizi ya fedha yasiyo ya lazima.
 
Mkurugenzi huyo wa NEC alifafanua kuwa katika kikao chake cha kwanza na watumishi wa Tume cha Agosti 7 mwaka 2018, alijadili changamoto zinazowakabili watumishi hao ambazo zilikuwa kikwazo cha utekelezaji wa majukumu yao kwa njia moja au nyingine.
 
“Tuligundua kuwa changamoto nyingi zilitokana na tabia binafsi za baadhi ya watumishi, na baadhi yao kufanya kazi kwa kuigiza yaani kwa mazoea kwa kisingizio cha mchakato”, alisema Dkt. Kihamia na kufafanua kuwa:
 
“Lakini sasa hivi jambo la kufurahisha asilimia kubwa ya watumishi wanafanya kazi sio kwa mazoea, lakini pia ufanisi wa kazi zao umeongezeka kwa kiwango kikubwa”.
 
Alibainisha kuwa kwa sasa Tume imeimarika vya kutosha kwa kuwa wakati alipofika wastani wa utendaji kazi ulikuwa asilimia 52, ikimaanisha kuwa zaidi ya asilimia 48 ya watumishi walikuwa hawawajibiki ipasavyo, lakini sasa uwajibikaji umefikia wastani wa asilimia 65 baada ya kuwekeana malengo.
 
“Kwa hiyo tulipo sasa tupo juu ila ni lazima tuendelee kuwa kitu kimoja, ingawa katika kuimarika huko wapo wenzetu wachache sana wenye matatizo madogo madogo, hivyo wanatakiwa warekebishwe” alisisitiza Dkt. Kihamia
 
Alifafanua kuwa kuimarika kwa utendaji kazi ni jambo kubwa kwa maendeleo ya nchi kwa kuwa kutowajibika ipasavyo kwa watumishi wa umma katika nchi nyingi za Afrika kumesababisha udumavu wa maendeleo ya nchi hizo.
 
Hivyo aliwataka watumishi wa NEC kuendeleza tabia ya uwajibikaji kwa mustakbali wa maendeleo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Tanzania kwa ujumla kwa kuacha kufanya kazi kwa mazoea ili kuwa chachu ya maendeleo ya nchi.
 
Ili kuboresha zaidi utendaji kazi wa Tume, Dkt. Kihamia aliziagiza kila idara ziainishe vipaumbele (priorities) vitakavyotekelezwa na idara husika kwa kipindi chote kuanzia Julai 1 mwaka huu.
 
Alisema baada ya kupata vipaumbele hivyo kutoka kila idara vitaunganishwa kupata vipaumbele vya Tume na aliwataka watumishi kutambua kuwa majukumu ya kila idara ni majukumu ya Tume hivyo ni muhimu kuwa kitu kimoja katika kuyatekeleza.
 
“‘Checklist’ ni jambo kubwa sana kwa sababu kuna mtu ukienda kwenye idara yake ukimuuliza amefanya mambo gani, anaweza akawa amefanya mambo mazuri tu lakini hayakumbuki mpaka ayafikirie ndio akwambie” alisema Dkt. Kihamia na kufafanua kuwa:
 
Alisema checklist ni mpango kazi ambao hata watafiti wanaofanya tafiti za kisasa wamegundua kwamba kampuni nyingi za kibiashara zinazofilisika ni zile ambazo hazina checklist za kisasa.
 
“Kwa hiyo checklist ni moja ya agenda ambayo nimekuja kuizungumzia leo kwa sababu tunafanya kazi kwa mipangokazi na unapokuwa na checklist unajua hili nimelifanya hili sijafanya” alisema Dkt. Kihamia.
 
Alisema mtumishi asipokuwa na checklist ya kazi zake hawezi kuwa na muendelezo (consistency) mzuri wa majukumu ambayo mtumishi anataka kuyatekeleza na ukamilifu wa kazi zake hautakuwepo.
 
Alisema wataalamu wanasema kwamba checklist ndio njia pekee kwa sasa inayoaminika katika kutekeleza majukumu kwa ufasaha.
 
“Mtafiti mmoja aliwahi kusema checklist ni aina ya mpangilio wa majukumu ambao unapunguza kushindwa (failure)katika kazi, ina maana usipokuwa na checklist uwezekano wa kushindwa ni mkubwa” aliongeza Dkt. Kihamia.
 
Kwa upande mwingine Dkt. Kihamia alimtaka kila mtumishi wa Tume atambue majukumu ya msingi ya NEC na ikiwemo kufahamu Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ni nini na kufahamu taratibu zote za uchaguzi.
 
“Watu wajifunze kuwepo kwa nafasi wazi ni nini maana watu wanalalamika kwamba Serikali inatumia fedha nyingi kufanya chaguzi ndogo za mara kwa mara lakini wanasahau kwamba suala hilo lipo kwenye katiba na ni utarabu.” alisema Dkt. Kihamia.
 
Dkt. Kihamia tangu alipoteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi amejiwekea utaratibu wa kukutana na watumishi wa tume hiyo huku hiki kikiwa ni kikao chake cha tatu.
 
Katika kikao cha kwanza cha tarehe 7 Agosti mwaka 2018, Dkt. Kihamia aliainisha vipaumbele vyake 30 vya kuzingatia katika utekelezaji wa majukumu ya Tume na kuvifanyia tathmini kwenye kikao cha pili kilichofanyika mwezi Desemba mwaka 2018.
 
Baadhi ya vipaumbele alivyosisitiza ni kuweka mpango kazi wa kila idara, kitengo na mtumishi na utekelezaji wake kwa kile mwezi, kuandaa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya kila idara, kutambua madeni ya kila idara na kitengo na kuonesha kama yamehakikiwa au la, sababu ya madeni hayo na kuwepo rejesta na mpango kazi wa malipo.
 
Katika vikao hivyo wakuu wa Idara wamepewana nafasi ya kufafanua mambo mbalimbali katika idara zao na watumishi kuwepo nafasi ya kueleza mambo mbalimbali kuhusu utekelezaji wa majukumu yao.


Share:

Kifo cha Kijana Anayedaiwa Kujirusha Ghorofani Jijini Mwanza Chaibua Utata

Wakazi wa jiji la Mwanza wamekumbwa na sintofahamu baada ya kijana mmoja asiyefahamika kusadikiwa kujirusha kwenye jengo la ghorofa ya tatu katika  hoteli ya Gold Crest iliyopo jijini humo.

Taarifa za awali za kifo cha kijana huyo zinaeleza kuwa baada ya kudondoka kutoka ghorofani, alipoteza maisha papo hapo.

Wakizungumza mapema asubuhi, wakazi wa mji wa Mwanza wameonyesha kusikitishwa na kifo cha kijana huyo anayesadikiwa kuwa na umri kati ya miaka 25 hadi 30 ambae chanzo cha kifo chake hakijafahamika.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro amelizungumzia tukio la kifo cha kijana huyo akisema kuwa taarifa za awali walizozipata kuhusu tukio hilo hazikuwa za kweli kwa kuwa eneo ambalo inadhaniwa amejirusha na eneo ambalo umekutwa mwili wake ni tofauti.

"Haiingii akilini kuwa umbali ule ambao inadhaniwa mtu amejirusha na eneo la barabara ambalo amekutwa, haiwezekani pia mtu amejirusha akafika chini akawa mgongo wake mzima, kichwa kizima na hakuna hata tone la damu, kwahiyo kwa taarifa za awali, mimi nakanusha kuwa mtu huyu hajajirusha".


Share:

Waziri wa Kilimo Hasunga Apigilia Msumari Marufuku Ajira Kwa Watoto Kwenye Sekta Ya Tumbaku

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Tabora
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesisitiza marufuku yake aliyoitoa hivi karibuni kuhusu ajira kwa watoto ambao wapo chini ya miaka 18.

Mhe Hasunga amepiga marufuku hiyo leo tarehe 13 Mei 2019 wakati akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa wa sekta ya Tumbaku katika hafla ya ufunguzi wa msimu wa masoko ya Tumbaku mwaka 2019 iliyofanyika katika maghala ya kampuni ya Alliance One Wilaya ya Urambo mkoani Tabora.

Alisema kuwa suala la ajira kwa watoto ni miongoni mwa mambo yanazuiliwa kwenye Sheria za kimataifa kupitia Shirika la Kazi Duniani (International Labour Organization) na Sheria za Ajira hapa nchini hivyo mdau yeyote atakayebainika kukiukwa maelekezo hayo atashtakiwa.

“Nawasihi wadau wote tuendelee kupiga vita ajira kwa watoto katika tasnia ya tumbaku kwa kuwa ni eneo ambalo limeendelea kulalamikiwa na wadau” Alikaririwa Mhe Hasunga

Kadhalika, Mhe Hasunga alisema kuwa katika kuhakikisha zao la tumbaku linaendelea kutoa mchango mkubwa katika pato la mkulima na Taifa, Wizara imejiwekea malengo ya haraka yanayopaswa kutekelezwa ambayo ni pamoja na kukamilisha usajili wa wakulima wote wa tumbaku ifikapo tarehe 30 Juni 2019, kuwapatia vitambulisho na kuwaingiza kwenye kanzidata ili kupata takwimu za uhakika za maeneo wanayolima na kuiwezesha serikali kusimamia upatikanaji wa pembejeo kulingana na mahitaji yao.

Malengo mengine ni Tumbaku yote inayovunwa na wakulima sasa inauzwa ifikapo mwisho wa masoko tarehe 31 Julai, 2019 huku akiiagiza Bodi ya Tumbaku kushirikiana na wakulima wote kusimamia kwa makini masoko ili tuweze kuanza mapema maandalizi ya zao la msimu wa 2019/2020.

Aidha, mipango mingine ni kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo kwa wakati kwa kuweka utaratibu wa kumwezesha mkulima kujitegemea kwa pembejeo ili aache kuwa tegemezi wa mikopo ya mabenki yenye riba kubwa.

Mhe Hasunga ameiagiza Bodi na Tume ya Maendeleo Ushirika kuhakikisha wanavishirikisha wakulima kupitia vyama vyao kuweka akiba ya fedha kununua pembejeo kwa kukatwa kiasi watakachokubaliana wakati wa mauzo ya tumbaku.

Pamoja na malengo hayo ya haraka, Wizara ya Kilimo inasimamia utekelezaji wa malengo ya muda mrefu yakiwemo Upatikanaji wa wanunuzi wapya wa tumbaku kwa sasa na kwa miaka ijayo kabla ya Juni, 2020, Kuongeza ubora wa zao la tumbaku kutoka asilimia 87 ya sasa hadi asilimia 92 ifikapo Juni 2022 na Kuongeza mbegu mpya na bora za tumbaku ili tuweze kupata masoko katika nchi nyingine kama vile China.

Alisema ili kufikia malengo hayo wadau wote wa tasnia ya tumbaku wanapaswa kushirikiana ili kufikia malengo hayo na wakulima kunufaika na jasho lao.

“Viongozi ngazi ya Mkoa na Wilaya wakiwemo Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Waheshimiwa Wabunge, Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi wa Halmashauri wanaowajibu na mchango mkubwa kuendeleza zao hili kwa kusimamia Sheria zinazosimamia zao hili, kusimamia huduma za ugani na kutenga fedha kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri” Alisisitiza Mhe Hasunga

Tumbaku ni miongoni mwa mazao makuu ya kimkakati ya yaliyopewa kipaumbele na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mhe Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mazao mengine ni pamoja na Tumbaku,  Kahawa, Pamba, Korosho, Chai, michikichi na alizeti. 

Mhe Hasunga alisema kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa malengo ya uzalishaji yanafikiwa kwa kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa pembejeo kwa wakati, kuboresha huduma za ugani na kutafuta masoko mapya ya tumbaku.

Serikali inatumia mfumo wa uagizaji wa mbolea kwa pamoja ili kuhakikisha mbolea inafika kwa wakati, kwa bei nafuu na kudhibiti upandishaji holea wa bei. “Nichukue nafasi hii kuigiza Bodi ya Tumbaku na viongozi wa vyama vya ushirika kuhakikisha kuwa wakamilisha kwa wakati kuweka malengo ya uzalishaji na mahitaji ya mbolea ili uagizaji wa mbolea ufanyike mapema” Alisema Mhe Hasunga

Takwimu zinaonesha kwamba kwa kipindi cha zaidi ya miaka 10 hadi kufikia mwaka 2016 tumbaku imekuwa na mchango mkubwa wa kuliingizia Taifa fedha za kigeni.  Kwa mfano katika mwaka 2017, tumbaku iliingiza fedha za kigeni kiasi cha Dola za Kimarekani Milioni 195.8 ikishika nafasi ya pili baada ya zao la korosho. Licha ya faida kwa taifa, pia, uzalishaji wa tumbaku unawanufaisha wakulima, wanunuzi, viwanda vya kusindika tumbaku, mabenki, wasambazaji wa pembejeo, Halmashauri za wilaya na wadau wengine katika mnyororo wa thamani.


Share:

Tume ya Madini yatoa leseni za madini 832 ndani ya miezi mitatu. .... Wawekezaji wazidi kumiminika

Na Greyson Mwase, Dodoma
Mkurugenzi wa Huduma za Leseni na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) wa Tume ya Madini, Mhandisi, Yahya Samamba amesema kuwa kati ya kipindi cha mwezi Januari, 2019 na Machi, 2019, Tume ya Madini imepitisha maombi ya leseni za madini 832 kati ya maombi 951 yaliyowasilishwa.

Mhandisi Samamba ameyasema hayo kwenye kikao cha Kamati ya Ufundi ya Tume ya Madini kilichofanyika mapema leo tarehe 13 Mei, 2019 jijini Dodoma chenye lengo la kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Tume ya Madini katika kipindi cha mwezi Januari, 2019 hadi Machi, 2019.

Kikao hicho kilishirikisha Makamishna wa Tume ya Madini, Profesa Abdulkarim Mruma na Dk. Athanas Macheyeki, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Tume, William Mtinya, Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini, Dk. Venance Mwase pamoja na mameneja na watendaji kutoka Tume ya Madini.

Alifafanua kuwa awali Idara yake ilipokea na kushughulikia  maombi mapya ya leseni za madini  951 ikiwa ni pamoja na maombi ya leseni za utafutaji wa madini 77, maombi ya leseni za uchimbaji mdogo wa madini 728 na maombi ya leseni za uchenjuaji wa madini 15.

Maombi mengine yaliyopokelewa ni pamoja na maombi ya leseni za biashara ya madini 131 ambapo yalihakikiwa  kama yamekidhi matakwa ya Sheria ya Madini na Kanuni zake.

Alisisitiza kuwa mara baada ya zoezi la uchambuzi kukamilika  maombi ya leseni za madini 832 yalipitishwa na kusisitiza kuwa bado Tume ya Madini inaendelea kupokea maombi ya leseni mbalimbali za madini na kuyafanyia kazi.

Akizungumzia mafanikio katika sekta ya madini kwa ujumla, Mhandisi Samamba alisema kuwa Serikali imeboresha Sheria ya Madini pamoja na kanuni zake inayomtambua mzawa kama mmiliki wa madini na kuwataka wananchi hususan wachimbaji wadogo kuchangamkia fursa mbalimbali.

Katika hatua nyingine Mhandisi Samamba aliwataka wachimbaji wadogo wa madini wasio rasmi kuunda vikundi na kuomba leseni za madini na kusisitiza kuwa Tume ya Madini kupitia Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa ipo tayari kuwasaidia.


Share:

Kampuni ya UDA-RT, yasitisha hudumuma ya mabasi ya mwendo kasi

Taarifa kwa umma
Kampuni ya UDA-RT inautaarifu umma kuwa huduma za mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, imesitisha huduma zake kati ya Kimara - Kivukoni, Kimara - Gerezani, Morroco - Kivukoni na Morroco - Gerezani kuanzia saa 10: 30 alfajiri leo Jumatatu Mei 13, 2019, kufuatia kujaa maji katika eneo la Jangwani. 

Huduma zinazotolewa sasa ni kati ya Kimara - Mbezi, Kimara - Magomeni Mapipa, Kimara - Morroco, Gerezani - Muhimbili, Kivukoni - Muhimbili na Gerezani - Kivukoni. 

Tunaendelea kufuatilia hali ya maji katika eneo husika, maji yakipungua huduma zitarejea katika hali ya kawaida. Tunaomba radhi kwa usumbufu unatokana na kusitishwa kwa safari hizo.

Deus Bugaywa
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano UDA-RT.


Share:

Wakurugenzi hawana mamlaka na fedha za mfuko wa jimbo

Wakurugenzi wa halmashauri nchini hawaruhusiwi kutumia fedha za mfuko wa jimbo bila idhini ya mwenyekiti wa mfuko huo ambaye ni mbunge.

Kauli hiyo imetolewa bungeni leo Jumatatu Mei 13, na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mwita Waitara wakati akijibu swali la Mbunge wa Konde, Khatibu Said Haji (CUF).

Katika swali lake, mbunge huyo alitaka kujua kuhusu umuhimu wa Serikali kuongeza viwango vya fedha ili kuleta ufanisi.

Aidha, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye ulemavu, Jenista Mhagama, amesema serikali itatoa waraka mpya kuhusiana na fedha hizo kuwakumbusha wakurugenzi kwamba hawana mamlaka na fedha hizo.


Share:

VIDEO: Moni Centrozone - MTITI

VIDEO: Moni Centrozone - MTITI


Share:

Wezi waiba vitu vya thamani na pesa taslimu kwenye jumba la kifahari la mzee Mengi

Huku bado familia inaomboleza kifo cha mfanyabiashara tajiri, Reginald Mengi aliyefariki mapema mwezi huu, wapo ambao wamefaidika kiharamu na msiba huo; wameiba vito, vifaa vya thamani na fedha taslimu katika nyumba mbili tofauti.

Vitu hivyo, ambavyo ni mikufu ya dhahabu, kompyuta mpakato pamoja na fedha taslimu ambazo kiwango chake hakijaelezwa, ni mali ya familia na waombolezaji na zilikuwa katika jumba la kifahari la mjane wake, Jacqueline Mengi na katika ya familia ambako mwenyekiti huyo wa kampuni za IPP alizikwa Alhamisi iliyopita.

Mengi, ambaye pia anajihusisha na uchimbaji madini na kumiliki vyombo vya habari, alifariki Mei 2 akiwa Dubai, Falme za Kiarabu alizika kijijini kwao Nkuu, Machame mkoani Kilimanjaro.

Msemaji wa familia hiyo, Benson Mengi alisema kwa sasa hawawezi kuzungumzia jambo hilo kwa kuwa bado uchunguzi unaendelea.

“Bado uchunguzi wa polisi unaendelea,” alisema Benson ambaye ni mtoto wa mdogo wake na Reginald Mengi anayeitwa Benjamin Mengi.

Kamanda wa polisi mkoa Kilimanjaro, Hamis Issah alisema tayari wanawashikilia watu wawili wakiwatuhumu kuhusika na wizi huo.

Kamanda Issah alisema tukio hilo limefanywa na watu wanaodaiwa kuwa wa ndani na familia hiyo na taarifa zinaonyesha walitokea jijini Dar es Salaam.

“Ni kweli nyumbani kwa Mengi kumeibiwa,” alisema kamanda huyo.

“Suala hilo ni la ndani na tukianza kulishughulikia kikamilifu litahusisha watu ambao ni wa ndani. Sasa sijui tutakuwa kwenye msiba au tutakuwa tunakamatana, maana tumeongeza huzuni juu ya huzuni.

“Kumetokea watu mchanganyiko. Familia ile watu wengi walikuwa haifahamiani, matokeo yake kila mtu anasema mimi na kila mtu anaingia mahali ambako hahusiki na matokeo yake ni wizi.”

Alisema tayari polisi inamshikilia mwanamume na mwanamke mmoja ambao wanaonekana ni wageni wa familia hiyo.

“Ila bado tunaendelea na uchunguzi, ili kubaini undani zaidi wa tukio hili na kuwapata wahusika,” alisema.

Alisema baadhi ya watu ambao hawakutaka majina yao yatajwe, walidai baadhi ya waliohusika walikuwa wamevalia vitambulisho vilivyoandikwa IPP.

Credit: Mwananchi


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya May 13




Share:

Sunday, 12 May 2019

Askofu Nkwande Akemea Uchawi, Ushoga Na Utoaji Mimba.....Asema Ni Ushamba Wa Elimu, Ni Uuaji, Ni Dhambi

ASKOFU MKUU wa Jimbo Kuu la Mwanza, Mhasahamu Renatus Nkwande anasikitika kila anaposikia watu wanaongelea mambo ya uchawi na kusema kwamba huo ni usahamba wa elimu.

“Mtu akivimba tumbo unasema amelogwa na tena unamtaja na fulani ndiye mchawi. Huo ni ushamba wa elimu na tena huko ni kukosa imani na kushindwa kumuamini Mwenyezi Mungu,” amesema.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumapili, Mei 12, 2019) wakati akitoa shukrani kwenye ibada ya kumsimika kuwa Askofu Mkuu wa jimbo hilo iliyofanyika kwenye viwanja wa Kawekamo jijini Mwanza.

“Watu wetu wana hofu mbalimbali ambazo zimewakamata tangu utoto wao. Tuwasaidie waumini hawa ili wamwamini Mungu kwamba anaokoa na anaweza kuwaponya madhila waliyonayo. Tuwasaidie watu wetu wajikomboe kielimu, wajiendeleze kwenye masomo ya fizikia, kemia na kadhalika,” amesema.

Amesema anashangaa tabia ya Waafrika ya kupenda kuiga mambo ya ajabu kwa vile tu yameletwa na wazungu. “Sisi Waafrika ni watu wa ajabu tunaiga vitu visivyo na msingi. Wameleta ushoga, tunaiga! Wameleta utoaji mimba, tunaiga. Leo hii kuna taasisi zinasambaza hata vifaa vya kutolea mimba, nasi tumekaa tunaangalia tu.”

“Wazee wetu walipoona wamechoka ukoloni, walipigana ili kupata uhuru. Leo na sisi tupiganie uhuru kwa kukataa masuala ya ushoga na utoaji mimba. Huo ni uuaji, hiyo ni dhambi. Miongoni mwetu leo wapatikane watu wa kusimamia hayo ili ukoloni huu usiendelee kutawala akili za watu wetu,” amesema.

Amewaomba Watanzania wamuombe Mungu awabariki, alibariki Taifa la Tanzania ili yanayofanyika yawasaidie kwenda mbinguni.

Pia ametumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwaletea wananchi maendeleo na hatimaye kuwatoa kwenye umaskini. “Tunaamini yote anayofanya ni kwa manufaa ya Watanzania wote,” amesema.

Akizungumza kwa niaba ya Rais Magufuli na mamia ya waumini na viongozi waliohudhuria ibada hiyo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema anatambua kuwa kuwaongoza watu kiroho na kimwili ni jambo lenye uzito mkubwa. Na kwamba uteuzi wake unadhihirisha kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya katika kumtumikia Bwana.

“Sisi viongozi na waumini kwa kutambua kazi nzuri uliyoifanya hadi kufikia kupata wadhifa huo tuna imani utaweza. Nakuomba upokee mzigo huo kwa matumaini na bila kusita kwani waumini wa kanisa hili wako pamoja nawe na viongozi wenzako wote tunategemea watatoa ushirikiano kwako. Tunachosema ni kwamba, jipe moyo kwa kuzingatia yaliyoandikwa katika Wafilipi 4:13 kwamba “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”. Jitwishe mzigo huo kwa imani na utaubeba bila kuchoka, sisi sote tuko pamoja nawe,” amesema.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kusisitiza suala la kutunza amani ya nchi na akawaataka viongozi wa dini na waumini kote nchini kuendeleza upendom hurma na kuwa na roho ya msamaha. “Tuhurumiane sasabu sisi si wakamilifu, kwa hiyo tuongeze msamaha miongoni mwetu,” amesisitiza.

“Nawaombeni wote, tuendelee kutumia nyumba zetu za ibada kuliombea Taifa hili ili tuendelee kuishi kwa amani, upendo na mshikamano. Tuepuke migogoro ya mara kwa mara katika nyumba zetu za ibada. Tuendelee kujenga waumini wetu wakue kiroho na kujenga dhana ya umoja na upendo katika Taifa letu. Watu wa Mungu ni watu wa upendo, watu wa Mungu ni watu wa amani, watu wa Mungu ni watu wa kiroho.”

Mapema, akitoa salamu za Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Rais wa TEC, Askofu Mkuu Gervas Nyaisonga aliwataka waumini wa kanda ya ziwa wawe na mshikamano na wampe ushirikiano Askofu Mkuu Nkwande.

“Kuweni na upendo kama Bwana Yesu alivyofundisha na pia ombeeni utumishi mwema kwa viongozi wote wa Serikali na watumishi wote wenye jukumu la kuongoza watu.”

Askofu Nyaisonga aliishukuru Serikali kwa kulipa nafasi Kanisa Katoliki ya kushirikiana na Serikali kutoa huduma za jamii kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini hususani katika sekta ya elimu na afya.

“TEC inapenda kuhimiza mshikamano baina ya Serikali na kanisa ili kuwe na ufanisi wa huduma tunazotoa za kumlinda mama na mtoto na kijana. Ufanisi huu utapatikana kwa kuimarisha miundombinu hasa katika ngazi za chini,” alisema.

Waziri Mkuu ameondoka jijini Mwanza mchana huu kuelekea Arusha kupokea kundi la watalii zaidi ya 200 kutoka China ambao wanatarajiwa kuwasili leo jioni.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Picha : ASKOFU MAKALA AFUNGUA RASMI SHULE YA KKKT MAKEDONIA ENGLISH MEDIUM SHINYANGA

Kanisa la kiinjili la Kilutheli Tanzania Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria chini ya Usharika wa Makedonia uliopo Jimbo la Shinyanga,limezindua rasmi shule ya 'KKKT Makedonia English Medium' iliyopo Lubaga Mjini Shinyanga ambapo mgeni rasmi wa uzinduzi huo alikuwa ni Askofu Dkt. Emmanuel Joseph Makala.

Uzinduzi huo umefanyika leo Jumapili Mei 12,2019 katika ibada takatifu iliyoongozwa na Askofu wa kwanza wa Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Dkt. Emmanuel Joseph Makala.

Katika mahubiri yake Askofu Makala, amesema "Uendeshaji na utoaji wa huduma za kijamii kama elimu kwa jamii ni sehemu moja muhimu kwa kanisa la Mungu na ndiyo mambo muhimu tuliyoitiwa kuyafanya katika umoja wetu".

Katika risala yake, mwenyekiti wa kamati ya kikosi kazi Bwana Shuma amesema mchakato wa kuanzisha shule hiyo ulianzishwa mwaka 2015 chini ya mchungaji Helman Gacha aliyeleta wazo la kuanzisha kituo Day Care Center na wazo hilo lilipokelewa na kuanza kutekelezwa mara moja. 

Amesema baadaye usharika uliamua kununua kiwanja kwa ajili ya kuendeleza shule hiyo na kiwanja hicho kilipatikana maeneo ya Lubaga manispaa ya Shinyanga. Chini ya mchungaji Harlod Mkalo pamoja na mchungaji mwenza Mathias Masele waliamua kuongeza nguvu kazi ndani ya kamati ya kikosi kazi ili kuhakikisha mambo hayakwami.

Mwenyekiti wa kamati hiyo amesema wakati shule hiyo inaanzishwa rasmi ilianza ikiwa na wanafunzi wawili na walimu wawili na baada ya miezi mitatu idadi ya wanafunzi ilifikia 27.
Askofu Dkt. Emmanuel Joseph Makala akisoma maandiko wakati wa uzinduzi wa shule hiyo.
Askofu Dr Emmanuel Joseph Makala,wakuu wa majimbo pamoja na wachungaji wakiendelea na ibada ya uzinduzi wa shule ya Makedonia English Medium.
Askofu Dkt. Emmanuel Joseph Makala akijiandaa na ufunguzi.
Baada ya uzinduzi na uwekaji wakfu wa shule ya Makedonia English medium.
Askofu Dr Emmanuel Joseph Makala akiendelea na ufunguaji wa majengo ya shule hiyo.
Muonekano wa gari la shule ya Makedonia English Medium.
Muonekano wa gari ya shule ya Makedonia English Medium kwa ajili ya wanafunzi.
Baadhi ya walimu na wanafunzi wa shule ya Makedonia English Medium
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Makedonia English Medium
Mwonekano wa majengo ya shule ya Makedonia English Medium
Mwonekano wa majengo ya shule ya Makedonia English Medium

Picha zote na Isaac  Masengwa Masengwa Blog 
Share:

Askofu Kakobe aibukia kanisani kwa Gwajima....Amtetea sakata La Video ya Ngono

Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zachary Kakobe, ameibuka katika Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima na kukanusha kuwa video za ngono zinazosambaa mitandaoni zikimuonyesha Askofu huyo kuwa si za kweli.

Akizungumza katika ibada iliyofanyika katika kanisa hilo leo Jumapili Mei 12, Kakobe amesema vitabu vya dini haviamini ushahidi wa picha isipokuwa mashahidi watakaozungumza juu ya ukweli wa tukio husika.

“Yuko wapi huyo mshitaki mpaka sasa, mbona hayupo amefutika na kama hayupo huo tunauita unafiki, mshitaki wa Gwajima yuko wapi ? Polisi ndio wanamtafuta sasa hivi, sasa kama una ushahidi wa halali kwanini unajificha.

“Hatukubali Mashitaka juu ya Askofu Gwajima isipokuwa kwa vinywa vya mashahidi wawili watatu watakaosimama na kuthibitisha juu ya video ile,” amesema Askofu Kakobe.

Aidha, Kakobe amesema neno alilolitoa Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima katika sherehe za kanisa lake kutimiza miaka 30 alijua litakuwa na majibu.

Kakobe amesema wengi walichukia kwa nini Makonda alialikwa katika sherehe hizo na wengine walichukia zaidi baada ya Gwajima kukumbatiana na mkuu huyo wa mkoa huku wakibaki kutega masikio leo wakisubiri kuanzisha awamu ya pili ya mafarakano jambo ambalo halipo.

“Kwa neno alilolitoa Gwajima lilikuwa limejaa upako nilijua tu kuna kitu lazima kitokee na kama isingekuwa hivyo basi shetani angekuwa amekufa,” amesema Kakobe.

Amesema shetani hapendi kuona watu wakiwa wamoja na ndiyo maana hujaribu kuwatawanya ili iwe rahisi kuwatawala.

“Mshikamano huu wa wachungaji na manabii shetani wa kuubomoa bado hajazaliwa kwa sababu shetani anajua mkiwa wamoja katika kristo, baraka za Mungu ndiyo zinapowajia,” amesema Kakobe. 


Share:

Mapigano makali Yaibuka Tena Libya Kati Ya vikosi vya Haftar na vya serikali ya umoja wa kitaifa

Vyombo vya habari vya Libya vimetangaza kujiri mapigano makali jana usiku kati ya vikosi vya kundi linalojiita jeshi la kitafa la Libya linaloongozwa na Jenerali Khalifa Haftar na vile vya serikali ya umoja wa kitaifa ya nchi hiyo kusini mwa mji mkuu Tripoli.

Vyombo hivyo vimetangaza kuwa hadi jana usiku mapigano makali kati ya pande mbili hizo yalikuwa yakiendelea katika eneo la barabara inayoelekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Tripoli na katika eneo la al Aziziyah yapata umbali wa kilomita 45 kusini mwa mji mkuu.

Mapigano katika mji mkuu wa Libya Tripoli yanaendelea  katika hali ambayo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa juzi Ijumaa lilitaka kutekelezwa usitishaji mapigano nchini humo na pande zinazozozana kurejea kwenye meza ya mazungumzo.

Kundi linalojiiita jeshi la kitaifa la Libya chini ya kamanda Khalifa Haftar ambalo kwa miaka kadhaa limekuwa likidhibiti maeneo ya mashariki mwa Libya kutokana na uungaji mkono wa Saudi Araba, Misri, Imarati na baadhi ya nchi za magharibi katika miezi ya karibuni lilisonga mbele kuelekea upande wa kaskazini mwa nchi.

 Jenerali Haftar tarehe nne Aprili mwaka huu aliwaamuru wapiganaji wake kuanzisha mashambulizi ya pande zote dhidi ya mji mkuu Tripoli kwa kuungwa mkono na nchi hizo tajwa.  
 
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), zaidi ya watu 440 wameshauawa na zaidi ya 2000 wengine wamejeruhiwa tangu yalipoanza mashambulizi hayo, mbali na watu 55 elfu wengine kukimbia makazi yao kutokana na vita hivyo.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger