Tuesday, 7 May 2019

Picha : WANAFUNZI WA SHULE YA LITTLE TREASURES WATEMBELEA SHIRIKA LA SAVE THE CHILDREN


Wanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi Little Treasures iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga wametembelea kwenye ofisi za Shirika la Save The Children Mjini Shinyanga, kwa ajili ya kupewa elimu namna ya kupinga matukio ya ukatili dhidi ya watoto.


Ziara hiyo imefanyika leo Mei 7,2019 kwa kutembelea ofisi hiyo pamoja na ofisi ya Afisa Ustawi wa Jamii mkoa wa Shinyanga, ili kupewa elimu nanma ya kupinga matukio ya ukatili dhidi ya watoto ili wapate kutimiza ndoto zao.

Akizungumzia ziara hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, Alex Enock, amesema wamefarijika sana kutembelewa na wanafunzi hao wa Little Treasures, ili kuendeleza mapambano ya kupinga matukio ya ukatili dhidi ya watoto mkoani humo.

Amesema watoto wakielewa vizuri masuala ya ukatili itakuwa ni jambo jema, ambapo pale watakapokuwa wakifanyiwa matukio hayo watajua wapi pa kwenda kutoa taarifa ili hatua ziweze kuchukuliwa haraka, na kuweza kuzuia ukatili huo usiendelee kutendeka na hatimaye mtoto kupata haki yake.

“Shirika la Save The Children sasa hivi tunaadhimisha miaka 100 tangu kuanzishwa kwake, ambapo tumekuja na kampeni ya kupinga vita dhidi ya watoto, 'Stop War Against Children', ambayo imelenga kumkomboa mtoto pale vita vinapotokea, ikiwa wengi wamekuwa wakipata madhara kwenye vita hivyo,”amesema Enock.

“Hivyo ziara ya wanafunzi hawa ni faraja kwetu katika kuwapatia elimu hii ya kupinga vita dhidi ya watoto, pamoja na kupaza sauti pale wanapoona mwenzao ama wao wenyewe wanafanyiwa matukio ya ukatili, ili tuweze kupata taarifa mapema na kuweza kuyashughulikia kwa mujibu wa sheria na kuweza kupatikana kwa haki ya mtoto,”ameongeza Enock.

Naye Ofisa Ustawi wa Jamii mkoa wa Shinyanga Tedson Ngwale, amewataka wanafunzi hao wakawe mabalozi wazuri kwa wenzao, namna walivyopata elimu hiyo ya kupinga masuala ya ukatili dhidi ya watoto, yakiwamo ya ubakaji, ulawiti, kupigwa, kuolewa ndoa za utotoni pamoja na kuzuiwa kwenda shule.

Nao baadhi ya wanafunzi hao akiwemo Monica Shadraka, wamesema wamefarijika kupata elimu hiyo yakupinga masuala ya ukatili dhidi ya watoto, ambayo itawasaidia kuweza kutimiza malengo yao ya kielimu.

TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI


Kaimu mkurugenzi wa Shirika la Save The Children mkoani Shinyinga Alex Enock akiwaelezea wanafunzi kutoka shule ya Msingi Little Treasures namna shirika hilo lilivyoanzishwa hadi kujiingiza kwenye masuala ya kusaidia watoto.

Wanafunzi wa Little Treasures akisilikiza kwa makini elimu ya kupinga ukatili dhidi ya watoto kutoka kwa Kaimu kurugenzi wa Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga Alex Enock.

Kaimu mkurugenzi wa Shirika la Save The Children mkoani Shinyinga Alex Enock akiendelea kutoa elimu kwa wanafunzi.

Wanafunzi wakiendelea kusikiliza elimu ya kupinga ukatili kwa watoto.

Afisa Ustawi wa Jamii mkoa wa Shinyanga Tedson Ngwale akitoa elimu kwa wanafunzi hao na kuwataka wakawe mabalozi wazuri kwa wenzao katika kuhakikisha wanapaza sauti kwa kutoa taarifa juu ya matukio ya ukatili ili yapate kushughulikiwa kabla ya kuleta madhara na kuzima ndoto zao.

Wanafunzi wakisikiliza elimu ya kupinga ukatili .

Wanafunzi wakisikiliza kwa makini elimu ya kupinga ukatili dhidi ya watoto.

Wanafunzi wakinyoosha mikono juu kutoa ishara ya kupinga vita dhidi ya watoto "Stunt" ambayo ni kauli mbiu ya shirika la Save The Children katika kuadhimisha miaka 100.

Ishara ya kupinga vita dhidi ya watoto Stunt ikiendelea kuonyeshwa.

Ishara ya Stunt ikiendelea kuonyeshwa ili kupinga vita dhidi ya watoto.

Ishara ya Stunt ikiendelea kuonyeshwa na wanafunzi hao wa shule ya Little Treasures.

Awali wanafunzi wa shule ya Little Treasure wakiingia kwenye ofisi za Shirika la Save The Children Shinyanga Mjini.

Wanafunzi wa shule ya msingi binafsi Little Treasure wakipiga picha ya pamoja na wafanyakazi wa Shirika la Save The Children nje ya ofisi za Shirika hilo na kuonyesha ishara ya kupinga vita dhidi ya watoto (Stunt).

Na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog

Share:

IT Officer - Database & Systems Development Job at Exim Bank Tanzania

Jobs at:
Exim Bank Tanzania

Deadline of this Job:
22nd May 2019 
Duty Station:
Within Tanzania , Dar es Salaam , East Africa

Summary
Date Posted: 6th May 2019 , Base Salary: Not Disclosed

JOB DETAILS:
JOB TITLE: IT Officer - Database & Systems Development
REPORTING TO: Manager, Database and Systems Development
REGION: Dar es Salaam
• Job Category : IT
• Job Code : IT
• Job Name : Officer— Database &Systems Development
PURPOSE OF JOB
To analyze departmental and individual requirements for database solutions; participate in developing, implementing and maintaining applications; documenting system components; and serving as a technical advisor to staff and other bank personnel. .

PRINCIPAL RESPONSIBILITIES
• Provide technical expertise and recommendations in assessing new IT software projects and initiatives to support and enhance our existing Microsoft based systems.
• Make recommendations on custom applications which may include a number of data capture systems for banking operations and other databases.
• Identify opportunities that can improve efficiency of business processes.
• Investigate and resolve application functionality related issues and provide first level support and troubleshooting of banking systems
• Coordinate application development for multiple projects.
• Assist in troubleshooting software application issues.
• Assist in managing an outsource relationship for 3rd party application development and programming consultants.
• Troubleshoot technical issues and identify modifications needed in existing applications to meet changing user requirements.
• Analyze data contained in the corporate database and identify data integrity issues with existing and proposed systems and implement solutions.
• Provides assistance and advice to business users in the effective use of applications and information technology. Provide minor programming for some in-house IT projects.
• Write technical procedures and documentation for the applications including operations, user guide, etc. Produce technical documentation for new and existing applications.
• Verify database and data integrity.
• Participate in weekly meetings with the IT team to discuss progress and issues to be resolved, and report progress on a weekly basis to the Head of IT.
• Participate on IT project committees and be involved in the design phase of any new IT software development projects.
• Assist in the creation of the system design and functional specifications for all new development projects.
• Serve as a liaison and facilitator between all business units to assist in addressing and resolving IT software issues.
• Installing and applying of patches on Unix and Infrastructure virtualization environments.
• Installing and ensuring there is current hardware firmware version and support license.
INDEPENDENT DECISIONS
• Responsibilities include: working under limited supervision following standardized practices and/or methods; leading, guiding, and/or coordinating others; and operating within a defined budget.
• Utilization of resources from other work units is often required to perform the job’s functions.
• There is a continual opportunity to impact the organization’s services.

SKILLS
• Advanced Diploma/Degree in IT, IS, Computer Science/Engineering, Mathematics or related field
• Knowledge of structured query language (SQL), Unix and database management systems (DBMS).Source: Ajiraleo Tanzania
• At least 3 years relevant experience in the banking industry. Knowledge of programming languages such as PHP, Java, VB.net etc

QUALITIES
• Excellent problem-solving and organizational skills
• The ability to work to a high degree of accuracy
• Good analytical skills
• A good understanding of database architecture, software and database management systems
• A good understanding of banking products, procedures and systems
• The ability to work quickly, under pressure and to deadlines
• Good communication, presentation and negotiating skills
• A good understanding of the banking policies and regulatory requirements
• A willingness to keep up to date with developments in technology
• Good team-working skills

Job Education Requirements: Diploma/Degree in IT

Job Experience Requirements: Not Specified

Job application procedure


Share:

Picha : RAIS MSTAAFU JAKAYA KIKWETE ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA BUNGE LA AFRIKA


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele akimpokea Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete alipotembelea Makao Makuu ya Bunge la Afrika “Pan- African Parliament” yaliyopo Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini leo Mei 7,2019.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele akimkaribisha ofisini Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete. 
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete akizungumza na Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Roger Nkodo Dang (katikati) na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele. 
Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Roger Nkodo Dang akizungumza jambo wakati wa majadiliano hayo.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa majadiliano yake na Viongozi wa Bunge la Afrika.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele akizungumza wakati wa majadiliano kuhusu hali ya uchaguzi Afrika Kusini.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete ambaye anaongoza Timu ya Waangalizi wa Umoja wa Afrika kwenye Uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini mwaka 2019 akiongoza kikao cha kujadili maandalizi ya uchaguzi huo nchini Afrika Kusini.
Kikao cha kujadili maandalizi ya uchaguzi mkuu  nchini Afrika Kusini kati ya Viongozi wa Bunge la Afrika na  timu ya waangalizi ya Umoja wa Afrika inayoongozwa na Dkt. Jakaya Kikwete kikiendelea.
Waheshimiwa Mabalozi kutoka Kenya,Nigeria wa kiongozwa na Balozi Naimi Aziz wa kwanza kulia anayeiwakilisha Tanzania nchini Ethiopia na Umoja wa Afrika ambao wameambatana na Mheshimiwa Kikwete.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele (wa tatu kulia) akizungumza wakati wa kikao cha kujadili maandalizi ya uchaguzi mkuu mwaka 2019 nchini Afrika Kusini.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete  akitembelea ukumbi wa Bunge la Afrika.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele akipiga picha ya kumbukumbu ofisini kwake na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete katika Makao Makuu ya Bunge la Afrika, Jijini Johannesburg, Afrika Kusini. 

****
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete ametembelea Makao Makuu ya Bunge la Afrika “Pan- African Parliament” yaliyopo Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini.

Dkt. Kikwete ambaye ni Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Umoja wa Afrika wa Uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini mwaka 2019 amepokelewa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele leo Jumanne Mei 7,2019.

Amelipongeza Bunge la Afrika kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kusimamia Demokrasia, Utawala na Masuala ya Ulinzi na Usalama barani Afrika.

“Mimi nilikuwa miongoni mwa Mawaziri wa Mambo ya Nje ambao tulikutana kule Sirte Libya kuandaa kanuni za kuanzishwa kwa Bunge la Afrika,hivyo ninayo furaha kubwa kuona hatua kubwa ya maendeleo ya bunge,Nawapongeza sana Rais na Makamu wa Rais kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuendeleza bunge hili na Waafrika wote tunawatagemea”,amesema Dkt. Kikwete

“Leo na timu yangu ya uangalizi ambao tupo hapa Afrika Kusini kwa ajili ya uangalizi wa Uchaguzi mkuu wa mwaka huu,na ninashukuru miongoni mwa timu yangu wabunge wa bunge la Afrika ni miongoni mwa wajumbe wangu,nawapongeza sana Bunge la Afrika kwa kushirikiana na Umoja wa Afrika kusimamia demokrasia”,ameongeza Dkt. Kikwete.

Kwa upande,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele amemshukuru na kumpongeza, Mheshimiwa Kikwete kwa mchango wake mkubwa kwa bara la Afrika kwenye nyanja za afya,elimu na demokrasia.

"Sisi viongozi vijana tuna mengi ya kujifunza kutokana na uzoefu wako mkubwa kwenye masuala ya uongozi na siasa za kimataifa, binafsi nakushukuru sana kwa malezi yako  ambapo kwa uwezo wa mwenyezi Mungu nimeweza kufika hapa nilipo kiuongozi",amesema Mhe. Masele.

Aidha amemuahidi Mheshimiwa Kikwete kuwa Bunge la Afrika litatoa ushirikiano wote unaohitajika ili kuweza kutimiza majukumu yake katika uangalizi wa uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini mwaka 2019.

Na Kadama Malunde - Johannesburg,Afrika Kusini
Share:

Mbunge Haonga aachiwa kwa dhamana

Mbunge wa Mbozi mkoani Songwe, Pascal Haonga ambaye alikamatwa jana na Jeshi la Polisi mkoani humo ameachiwa kwa dhamana.

Wakili wa mbunge huyo, Gaston Gatubindi amesema kuwa Haonga ameachiwa kwa dhamana na anatakiwa kuripoti kwa mpelelezi wa Mkoa wa Dodoma siku ya Alhamisi.

Amesema kabla ya kupewa dhamana polisi walikwenda nyumbani kwa mbunge huyo kufanya upekuzi kwa mujibu wa taratibu.

Aidha baada ya kupewa dhamana, Haonga alikwenda moja kwa moja bungeni kuendelea na kikao cha bajeti ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto..


Share:

MC Pilipili Kizimbani kwa Makosa ya Mtandao....Aachiwa Huru kwa Dhamana

Mshereheshaji, Emanuel Mathias (34) maarufu kama MC Pili Pili na mwenzake wameachiwa kwa dhamana katika kesi ya kuchapisha maudhui katika mtandao bila kuwa na leseni ya  Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ( TCRA)

Mbali na Mathias, mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Heriel Clemence( 25) ambapo wamesomewa mashitaka yao na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustina Mmbando.

Wakili wa Serikali, Constantine Kakula alidai wakati akisoma hati ya mashtaka leo Mei 7, 2019, kuwa wawili hao walitenda kosa hilo kati ya Novemba 17, 2013 na Mei 2, 2019 wakiwa katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Kakula, ambaye alisaidiana na Batilda Mushi, alidai mbele ya hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama hiyo, Augustina Mmbando kuwa katika kipindi hicho, MC Pilipili na Clement walichapisha maudhui kwa kutumia televisheni ya mtandaoni  (online TV) inayojulikana kwa jina Mc Pilipili, bila kuwa na kibali cha TCRA.


Washtakiwa baada ya kusomewa shtaka lao, walikana kutenda kosa hilo na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika ambapo wakili wa utetezi Jebrah Kambole aliwaombea dhamana washitakiwa hao.

MC Pilipili na Clemence wameachiwa huru kwa masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja mwenye barua kutoka kwa Mtendaji wa Kata na barua ambayo imepitishwa kwa Mkurugenzi wa Manispaa, anakotokea mdhamini huyo.Kesi imeahirishwa hadi Mei 7, 2019.


Share:

MASELE AIKINGIA KIFUA SERIKALI YA TANZANIA KWENYE BUNGE LA AFRIKA


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akisisitiza jambo wakati akiongoza kikao cha Bunge la Afrika leo Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini.Picha na Kadama Malunde- Malunde1 blog

***
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele ameipongeza serikali ya Tanzania kwa kuchukua hatua za haraka kusaidia nchi za Kusini mwa Afrika (Msumbiji,Malawi na Zimbabwe) zilizoathirika na Kimbunga cha Idai. 

Mheshimiwa Masele ambaye pia ni Mbunge wa Shinyanga Mjini ametoa pongezi hizo leo Mei 7,2019  akiongoza kikao cha Bunge la Afrika kinachofanyika Jijini Johannesburg,nchini Afrika Kusini wakati wabunge wakijadili kuhusu Ripoti ya kazi ya Umoja wa Afrika (AU). 

Mhe. Masele alilazimika kutoa ufafanuzi baada ya hoja kuibuka hoja bungeni kuwa nchi za Umoja wa Afrika zimekuwa hazichukui hatua za haraka panapotokea majanga mbalimbali. 

“Nitumie fursa hii kuipongeza sana serikali inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli kwa kuchukua hatua za haraka kusaidia chakula na madawa kwa nchi zilizokumbwa na Kimbunga Idai”,alisema Mhe. Masele. 

“Serikali ya Tanzania ilikuwa mstari mbele kutoa msaada wa chakula,dawa na vifaa vya kujiihifadhi kwa nchi ambazo zimekumbwa na maafa ya mafuriko kufuatia tufani kali iliyolikumba eneo hilo la kusini mwa Afrika”,aliongeza Mhe. Masele.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akiongoza kikao cha Bunge la Afrika leo Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akiongoza kikao cha Bunge la Afrika leo Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini. Katikati ni Rais wa Bunge la Afrika, Mhe. Roger Nkodo Dang akitoa taarifa ya kazi ya Bunge la Afrika.
Wabunge wakiwa ukumbini.
Kikao cha bunge kikiendelea.
Share:

Serikari Kuwasilisha Taarifa Ya Utekelezaji Wa Malengo Ya Maendeleo Endelevu Umoja Wa Mataifa

Na Josephine Majura na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma
Katika kutekeleza ajenda za Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s), Serikali imejipanga kuwasilisha Taarifa ya Mapitio ya Hiari (VNR) katika Jukwaa la Siasa la Umoja wa Mataifa (HLPF) mwezi Julai mwaka huu mjini Newyork nchini Marekani.

Hayo yameelezwa na  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango (Sera), Bw. Adolf  Ndunguru wakati akifungua kikao cha kujadili Taarifa ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s).

Bw. Ndunguru alisema kuwa uwasilishwaji wa taarifa hiyo utakuwa ni wa kwanza miongoni mwa mfululizo wa taarifa za mapitio mengine ambayo yanatokana na mapitio hayo yanayoonesha namna nchi inavyotekeleza Malengo hayo.

Alisema kikao hicho ambacho kinahusisha wadau wa ndani na nje ya nchi, ni muhimu kwa maendeleo ya nchi na wananchi kwa ujumla kwa kuwa kitajadili taarifa mbalimbali za utekelezaji wa Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) kwa kuangalia maeneo muhimu kama elimu, afya na uchumi.

Bw. Ndunguru alisema kikao hicho kinatoa fursa kwa wadau hao kujadili rasimu ya awali ya taarifa ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) na kutoa nafasi kwa wadau hao kuchangia  maoni yao kuhusu namna ya kuboresha taarifa hiyo kabla ya kuiwasilisha Umoja wa Mataifa.

“Tukiwa kama wananchama wa Umoja wa Mataifa, tumekubali kuingia mkataba wa kuutekeleza  Maendeleo Endelevu katika ajenda ya 2030 , kwa lengo la kuboresha maisha ya watanzania, kwa kuhakikisha tunapeleka elimu bora, afya bora  na kuboresha miundombinu”, alisema Bw. Ndunguru.

Bw. Ndunguru alibanisha kuwa mpaka sasa Tanzania inatekeleza kwa kasi ajenda hiyo ya 2030 ya Maendeleo Endelevu  kwa kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kutoa kipaumbele katika masuala ya elimu, afya na kukuza uchumi wa nchi.

Naye mdau wa mkutano huo ambaye ni  mwakilishi wa Umoja wa Asasi za Kiraia nchini, Prisca Kowa alilisema kwa sasa nchi inaonekana imejipanga kisawasawa kutekeleza Maendeleo Endelevu kwa kuwa imeweza kuyahusisha maendeleo hayo katika mipango mikubwa ya maendeleo ya nchi.

 Ametoa wito kwa Serikali, Wizara, Taasisi na wadau wa maendeleo  kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuhakikisha taarifa sahihi za utekelezaji wa Maendeleo Endelevu zinapatikana kwa usahihi na kwa wakati.


Share:

TFF Kupiga Marufuku Matamasha Ya Muziki Kwenye Viwanja Vya Soka...Karia Amwaga Pesa Za Ukarabati.

Na Bakari Chijumba, Mtwara.
Shirikisho la soka Tanzania(TFF),limetenga jumla ya Dollar za kimarekani Million moja,kwa ajili ya kurekebisha viwanja kumi vya soka nchini,ikiwemo uwanja wa Nangwanda Sijaona uliopo mjini Mtwara.

Akizungumza na wanahabari Mkoani Mtwara,06 Mei 2019,Rais wa TFF Wallace Karia,amesema kati ya viwanja hivyo kumi, kila uwanja umetengewa Dollar laki moja.

"Kwenye mkutano mkuu uliofanyika Arusha,tulipeleka maombi kwa wajumbe,Kutenga Dollar Million moja ili kurekebisha viwanja kumi,ikiwemo hiki cha Nangwanda(Mtwara)..Tunaboresha Pitch(Dimba),vyumba vya Waamuzi na vyumba vya  kubadilishia wachezaji,pia eneo la wanahabari" amesema Karia.

Aidha Karia amesema katika kuhakikisha ubora wa viwanja hivyo kumi unaendelea kuimarishwa, wameanza mazungumzo na wamiliki wa viwanja hivyo(CCM),ili TFF ibebe jukumu la kusimamia mazingira ya ndani ya viwanja pindi ukarabati utakapokamilika.

"Tupo kwenye mazungumzo na wamiliki wa viwanja hivi kumi,vyote vinamilikiwa na CCM,ili tutakapovirekebisha eneo la katikati ya uwanja libaki kwa ajili ya mpira tu na siyo shughuli za muziki au  maonesho mengine, labda iwe shughuli za kitaifa..Hatutoruhusu kabisa shughuli tofauti na mpira na tutaomba CCM wabaki na maduka yanayozunguka uwanja,usimamizi wa Dimba watuachie sisi tutajua tunagawana vipi upande wa mapato" amesema Karia na kuongeza kwamba;

"Nasisitiza tukishavirekebisha viwanja hivyo,hatutoruhusu kutumiwa tofauti na shughuli za kisoka, bahati nzuri katibu wa Ccm tumekutana nae na wiki ijayo tunakwenda kukaa  nae ..kuhusu hela zipo, katika  hela ya FIFA Doola Milion 5 tumetenga  Dola million moja kwa kila kiwanja Dola laki moja"

Katika hatua nyingine Karia ametoa wito kwa viongozi kutoka kwenye maeneo ambayo viwanja hivyo vinakarabatiwa,kuweka jitihada za dhati ili kufanikisha hatua nyingine zitakazosalia.

"Rai yangu kwa vjongozi wa serikali, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wanachi wa mikoa tutakayotengenza viwanja, fedha ni kidogo ni  kidoog tunataka kurekebisha pia na sehemu ya wageni maalumu kupumzika (High Table), wadau watapatie Materials(Vitendea kazi) na sisi tutagharamia ufundi...Nyasi hazitokuwa za bandia ni za kawaida,tutatengeneza  miundombinu ya visima vya kumwagilia nyasi hizo...Ligi ikiisha tu tutaanzaa marekebisho hayo" amesema Karia.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Mtwara(MTWAREFA),Athmani Kambi ameishukuru TFF kwa uamuzi huo na kusema watashirikiana nao katika kuhakikisha uwanja wa Nangwanda unakuwa bora na wa kisasa.

"Naishukuru TFF ya sasa,nimekaa na TFF miaka kumi na kitu ila sijawahi kuona TFF ambayo inaweza kutoa Dola laki moja kukarabati viwanja..Pia tuwashukuru kwakuwa kwenye viwanja kumi na Nangwanda tumepewa fursa" amesema Athmani Kambi na kuongeza kuwa;

"TFF imetoa Dollar Laki moja,itatengeneza pitch,vyumba vya kubadilishia na eneo la wanahabari(Nangwanda)..Tutaongea na Mkuu wa Mkoa tupate wadau wengine watusaidie kujenga Majukwaa,Ndanda Sc ikifanya vzuri kama sasa hivi watu wanajaa ila majukwaa hayatoshi, tutapambana kukamilisha uwanja .


Share:

BIA YA SERENGETI LITE YATUNUKIWA TUZO YA SUPERBRAND

Mei 7,2019, Dar es Salaam: Bia ya Serengeti Premium Lite imepata tuzo ya Superbrands kwa mwaka 2019/2020 kama ishara ya kutambua ubora wake wa hali ya juu, kuaminika kwake na wateja na uhalisia kwa watumiaji wake.

Ikiwa imepigiwa kura na watu wapatao 1000 nchini kote na kuthibitishwa na baraza la huru la wataalamu wa sekta ya uzalishaji, Serengeti Lite inaingia katika duru za kihistoria kwa tuzo hii ya kifahari ikiwa moja ya ubunifu wa hivi karibuni kabisa uliofanywa na Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL). Bia mama ya Serengeti Premium Lager nayo ni pia ni mshindi wa tuzo ya Superbrands.

"Kushinda tuzo ya Superbrand ni muhimu zaidi kuliko wakati wowote hasa ukichukulia hali ya uchumi na ushindani katika sekta ya bia kwa ukanda huu unaongezeka kwa kasi kubwa. Hakika, kushinda tuzo hii ni ishara tosha ya juhudi za Serengeti Lite kuendelea kuwa bidhaa muhimu, ya tofauti na ya kuvutia machoni mwa watumiaji, "amesema AnithaRwehumbiza, Meneja Masoko wa SBL katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na kampuni leo hii.

Serengeti Lite inayotambulika zaidi kama ‘The only Lite with a Bite’ ikiwa na maana kwamba ya kuwa na ladha murua ilizinduliwa rasmi Mei, 2017 ambapo katika kipindi cha chini ya miaka miwili kwenye soko, Serengeti Lite imejiimarisha na kuwa lite bia inayoongoza hapa nchini.

Aidha, Kinywaji hicho kimekuwa mdhamini mkuu wa ligi kuu ya soka la wanawake Tanzania maarufu kama ‘Tanzania Serengeti Lite Women’s Premier League’ maarufu kama “The League with a Bite” ambayo imeleta mapinduzi makubwa kwenye soka la wanawake hapa nchini.

Kushiriki katika Superbrands ni kwa mwaliko tu, na mwaliko huo hutolewa kwa bidhaa bora zaidi katika soko.

Kila mwaka maelfu ya bidhaa kutoka sekta tofauti zinaamuliwa dhidi ya ya vigezo vitatu vya muhimu vya Superbrand: ubora, kuaminika na utofauti. Kufikia hali ya kutunukiwa hadhi ya Superbrands ina maana hadhi ya bidhaa husika inaongezeka na huwahakikishia watumiaji na wauzaji kuwa wananunua bidhaa iliyobora kabisa.

“Kipaumbele kikubwa kikiwa kwa wateja wetu kwa kila tunachokifanya, kutunikiwa tuzo ya Superbrand ni mafanikio ya kujivunia sana kwa SBL. Ikiwa ipo kwenye baa, klabu za usiku au maduka makubwa, tunataka kuwahakikishia wateja wetu kuhusu lengo letu la kuendelea kuwapa Lite bora zaidi wakati wote,” ameongeza Rwehumbiza. 
Share:

PolePole: Mzee Mengi alikuwa daraja kati ya CCM, sekta binafsi na serikali

Katibu Mwenezi wa CCM, Polepole amesema chama chake kinajivunia Mengi kuwa mwanachama wake kwa maelezo kuwa, alikuwa mshauri mkubwa wa masuala ya uchumi na biashara.

Polepole amesema mfanyabiashara huyo alikuwa bilionea mjamaa, alihangaika kuhakikisha kila binadamu anakuwa sawa na mwingine bila kujali hali wala nafasi yake na vilevile ndani ya CCM alikuwa kiungo kati ya chama na Serikali na wadau wa sekta binafsi.

“Alikuwa daraja kati ya sekta binafsi, CCM na Serikali yake, kila panapokuwa na mkwamo kabla mambo hayajaharibika Mzee Mengi alisimama kama kiungo kati ya chama, Serikali na wadau wa sekta binafsi ambao chama chetu kinaamini sana kwamba uchumi wetu unategemea ukuaji na uimara wa sekta hiyo,” amesema.

==>>Msikilize Hapo Chini


Share:

Lukuvi Awasimamisha kazi wenyeviti wawili wa mabaraza ya ardhi na nyumba

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewasimamisha kazi wenyeviti wawili wa mabaraza ya ardhi na nyumba wa wilaya za Karagwe na Kibaha kutokana na malalamiko aliyopokea.

Licha ya kuwasimamisha wenyeviti hao wawili, waziri  amewateua wenyeviti wa mabaraza 20 nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Mei 7, 2019 mkoani Dodoma, Lukuvi amesema huo ni mkakati wa kuimarisha mabaraza 97 yaliyopo nchini.

Amesema katika kusimamia nidhamu ya uendeshaji na usimamizi wa mabaraza hayo, amekuwa akipokea tuhuma nyingi za rushwa, utendaji mbaya na malalamiko ya wananchi kwa wenyeviti wa Karagwe na Kibaha.


Share:

Kafulila Asitisha Mkataba Na Tba Ujenzi Wa Nyumba Za Viongozi

Katibu Tawala  Mkoa wa Songwe  David Kafulila amesitisha Mkataba wa ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa Mkoa na ya Katibu Tawala Mkoa uliokuwa kati ya yake na Shirika la Ujenzi la Taifa (TBA), kutokana na kutoridhishwa na kasi ya ujenzi huo.

Kafulila akiambatana na wakuu wa Sehemu wa Sekretarieti ya Mkoa wa Songwe amefikia uamuzi huo jana mara baada ya kutembelea eneo la ujenzi wa nyumba hizo na kukuta hatua ya ujenzi iliyofikiwa hairidhishi.

Kafulila amesema kasi ya ujenzi wa nyumba hizo inatia mashaka kutokana na kuwa kazi iliyokwisha fanyika kwa muda wa siku sitini ni ndogo ukilinganisha kazi na muda uliobakia kufikia tarehe ya makubaliano ya kukamilika ujenzi.

“Kazi iliyobaki kiuhalisia haiwezekani TBA wakaikamilisha kwa muda uliobakia, kwani tuliwakabidhi eneo la ujenzi tarehe 2-2-2019 na tulikubaliana ikifika tarehe 30-06-2019 nyumba hizo mbili ziwe zimekamilika lakini kwa kipindi cha miezi miwili hakuna kitu wamefanya na kuna dalili zote za kutokamilisha kwa muda”, ameeleza Kafulila.

 Ameongeza kuwa TBA wamekuwa na tabia ya kutekeleza miradi ya ujenzi kwa kasi ndogo mkoani Songwe na hivyo kusababisha fedha kurudishwa hazina kuu kutokana na kutozitumia kwa muda unaotakiwa yaani ndani ya mwaka wa fedha wa serikali ambapo fedha hizo zinakuwa zimetolewa.

“TBA mmekuwa na kawaida ya kutekeleza miradi yetu kwa kasi ndogo na hivyo kusababisha fedha kurudishwa hazina, mfano ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wamesababisha takribani Bilioni 3.8 zirudishwe na sasa tunahangaika kuziomba tena, uzembe huu tunaona unelekea kujirudia tena na sisi kama Mkoa hatuko tayari kila mara tunapewa fedha za ujenzi halafu zinarudishwa kwa uzembe wa TBA”, ameongeza Kafulila.

Amesema kuwa Mkoa hauna matatizo na Wizara ya Ujenzi wala shirika hilo la TBA ila lazima hatua za kusitisha mkataba huo zichuliwe ili kunusuru fedha hizo kurudishwa hazina kuu kutokana na kuchelewa kuzitumia ndani yam waka wa fedha wa serikali pia ili nyumba hizo zikamilike kwa muda na kuwezesha makazi ya viongozi.

“Naomba ifahamike mimi na mkoa kwa ujumla hatuna matatizo na Wizara ya Ujenzi pamoja na TBA lakini tukilifumbia macho hili hata sisi tutapimwa utimamu wa akili zetu, nimetembelea eneo la ujenzi zaidi ya mara nne lakini hakuna maendeleo yoyote, kiuhalisia kwa kasi hii TBA Mtatuangusha, sisi tunapenda kufanya kazi kwa kuendana na kasi ya Rais wetu”, amesisitiza Kafulila.

Amesema gharama ya Ujenzi wa Nyumba ya Mkuu wa Mkoa ni shilingi milioni 499.9 na tayari TBA walipewa malipo ya awali ya shilingi milioni 74.9 huku nyumba ya Katibu Tawala Mkoa ikiwa na gharama ya shilingi milioni 499.7 na malipo ya awali yaliyotolewa ni shilingi milioni 74.9

Imeelezwa kuwa TBA hawajawahi kuwasilisha taarifa ya kazi iliyokwisha fanyika lakini pia hawajaomba fedha zozote tangu walipwe malipo ya awali huku muda uliobaki ukionyesha kuwa hataweza kukamilisha kazi iliyobaki.


Share:

WIZARA YA ELIMU: SCHOLARSHIP TENABLE IN EIGHT COUNTRIES IN EASTERN AND SOUTHERN AFRICA 2019-2020

WIZARA YA ELIMU: SCHOLARSHIP TENABLE IN EIGHT COUNTRIES IN EASTERN AND SOUTHERN AFRICA 2019-2020

Call for Application

The General Public is hereby informed that, The Inter-University Council for East Africa (IUCEA) in partnership with the World Bank invites female applicants to apply for the IUCEA-World Bank Masters Fellowships for 2019. Eligible candidates must obtain an admission from an Africa Center of Excellence (ACE) that isKenya, Ethiopia, Rwanda, Malawi, Zambia, Mozambique and Uganda

to study full-time in any of the priority disciplines of the ACE II Project: (i) STEM (Science, Technology, Engineering and Mathematics) or Industry (ii) Agriculture (iii) Health (iv) Education and (v) Applied Statistics.For further information about the scholarship, the fellowship award, eligibility criteria, pleasevisit the following links: https://iucea.org/index.php?option=com_content&view=article&layout=edit&id=543

Application Process and Procedures

Interested candidates are advised to fill in the application form found at ace2.iucea.org or www.iucea.org, attach all requested documents, and send by e-mail to exsec@iucea.org with a copy to ace2rfu@iucea.org.

Applications must be received not later than 5.00 PM East African Time on June 30, 2019.

Issued by:

Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
University of Dodoma,
College of Business and Law,
Block 10,
P .O. Box 10,
40479 Dodoma.

The post WIZARA YA ELIMU: SCHOLARSHIP TENABLE IN EIGHT COUNTRIES IN EASTERN AND SOUTHERN AFRICA 2019-2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WIZARA YA ELIMU: SCHOLARSHIP TENABLE IN THE GOVERNMENT OF PAKISTAN 2019-2020

WIZARA YA ELIMU: SCHOLARSHIP TENABLE IN THE GOVERNMENT OF PAKISTAN 2019-2020

Call for Application

The General Public is hereby informed that, the Government of Pakistan has offered scholarships opportunity to Tanzanian to study Master’s degree programme in the Public Universities. Eligible candidates may apply in field of Social Sciences, Gender Studies, Arts & Humanities, Management and Business Education, Agriculture and Veterinary Sciences, and Natural Sciences/Physical Sciences.

For further information, Procedure for application, Fields of study, Financial breakdownEligibility criteriaRequired documentsUniversities and Admission procedure please visit the following link:http://www.hec.gov.pk/english/scholarshipsgrants/ARL-FS/CWLDC/Pages/default.aspx

The application should be completed no later than May 15th, 2019.

Issued by:

Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
University of Dodoma,
College of Business and Law,
Block 10,
P .O. Box 10,
40479 Dodoma.

The post WIZARA YA ELIMU: SCHOLARSHIP TENABLE IN THE GOVERNMENT OF PAKISTAN 2019-2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Kutana na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

Kutana  na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff  Mwenye UWEZO wakufanya dua mbali mbali  Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?

Wasilina na Adam shariff Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO   Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? . Adam shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN  . Anatafsiri Ndoto. , KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na Biashara.


Mawasiliano: (+255 )715971688 au (+255  )756914036



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger