Tuesday, 7 May 2019

PICHA: Zijue Alama za barabarani pamoja na matumizi yake


Credit: Jamii Forums


Share:

Ufugaji wa nguruwe : Gharama na Faida Zake

 Utangulizi
Nguruwe ni mnyama amabaye hutumika kama chakula / mboga na pia ni zao la biashara kwa mfugaji, mjasirimali na mfanyabiashara.
 
NGURUWE HUTEGEMEA SANA MAMBO YAFATAYO
1 . Banda imara na rafiki kwake
2. Usafi ni muhimu sana katika banda la Nguruwe
3 Mchaganyo bora wa chakula
4. Tiba bora na kinga
5. Maji na Lishe ( access ya vyakula Muhimu kwake )
 
CHANGAMOTO
KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE KUNACHAGAMOTO ZAKE LAKINI ZAWEZA KUTATULIWA KWA KUFATA MAMBO KADHAA.
Katika ufugaji wa nguruwe kunachagamoto ya vifo vya nguruwe wachanga ambao hupunguza faida ya biashara ya nguruwe kwa kupunguza idadi ya nguruwe wazima wa kuuzwa lakini utunzaji mzuri wa nguruwe wachanga huepusha vifo vinavyotokana na shida kama:
 
Matatizo ya kupumua
Ni kifo kinachosababishwa na mama anapomlalia nguruwe mchanga.chagamoto hii inaweza kutatuliwa kwa kuwatenga au kuwa na mabanda makubwa ya kulelea watoto.
 
Baridi
Nguruwe wachanga huathiriwa na baridi haswa katika majuma mawili au matatu ya mwanzo. Hii ni kwa kuwa wana kiwango kidogo cha utando wa mafuta wa kuwakinga.
 
Unashuriwa kuwaweka katika hali ya joto, wape matandiko na utumie vipasha joto kama vile kuwasha globu za joto kama utakuwa umewaweka kwenye mabanda ya kuta au nyumba yenye sakafu baridi.
 
Namna bora utunzaji wa nguruwe wachanga
Nguruwe moja wa kike ana uwezo wa kuzaa watoto 12. Namna ifuatayo itasaidia kupunguza idadi ya vifo vya nguruwe wachanga:
1.Pale nguruwe awapo na kidonda nyunyizia dawa ya ayodini 5% kwenye kovu ili kuzuia kuambukizwa kwa magonjwa.
2.Wawekee matandiko (nyasi kavu au maganda ya miti) mahali pa mapumziko ili wapate joto au utumie globu za joto.
3Wadunge sindano ya madini ya chuma (iron) siku ya tatu baada ya kuzaliwa ili kuzuia upungufu wa damu.
3. Yalainishe meno ya vichaga kabla ya masaa 24 ili kuzuia uharibifu wa matiti wakati wanaponyonya.
4. Watie vibandiko au utoboe masikio ili uwatambue na uhifadhi rekodi zao kama kuna umuhimu kama vile wafanyavyo wafugaji wa ng’ombe.
5. Wapime uzani wanapozaliwa na uhifadhi rekodi hiyo itakusaidia kujua ukuaji wao na maendeleo yao
6. Wahasi wale wa kiume juma la tatu, wale ambao hawafai katika kuendeleza kizazi kwa kutumia mtindo wazi (open method) kama unaona inafaa.
7. Wapatie dawa ya kuzuia minyoo pia zipo dawa za asili kama unga wa mkaa na majivu pia zipo za kitaalamu, wasiliana na wataalamu wa mifugo
8.Waachishe kunyonya katika juma la nane au wafikapo kilo 14 hadi 20 hii itasaidia kujitegemea na kukua kwa haraka.
 
Nguruwe Walioachishwa Kunyonya
1.Walioachishwa kunyonya wawekwe makundi ya 10 hadi 12 kulingana na uzito au ukubwa wao kwenye eneo ambalo watajitosheleza.
2.Watenganishe wakubwa kwa wadogo ili kuzuia kupigana.
3.Wakati wa kuwaachisha kunyonya mwondoe mama yao kutoka kwa watoto ili kupunguza usumbufu.
4Watoto wa nguruwe wa mama tofauti wasiwekwe pamoja maana hii husababisha mapigano kati yao na
5.Unapowachanganya watoto wa mama tofauti wapake mafuta ya gari yaliyotumika kwenye ngozi yao au mafuta ya kula ili kuiondoa harufu ya kutambulika ili wasipigane
 
FAIDA YA UFUGAJI WA NGURUWE
Faida kuu ya nguruwe ni zao la chakula lakini pia ni zao la kukuongezea kipato ukiwa kama mjasirimali / mfanyabiashara.
Lengo langu nikueleza namna unavyoweza kufuga na kutupa faida, Steps zifatazo ni muhimu kuzigatia.
 
JIPE MTAJI WA MILLION 4 / 3.5 KWA NGURUWE 50
UANDAAJI WA BADA WEKA MAKADILIO YA LAKI TANO (800,000/=) .
Hapo nazugumzia banda lenye heru U yenye mstatili ikiwa na kitako kirefu
Eneo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 50 litafaa zaidi ili kuhakikisha usalama wa nguruwe wako na ukuaji bora.
1. Tafuta mabati used kwa bei ya 5000 mfano mabati 20 ya futi 10 /10 = 100,000/=
2. Tafuta mabazi ya futi 10 kwa 2000 kila moja utapata mabazi pic 100 = 200,000/=
3. Tafuta miti ya nguzo na kechi ya 1000 na 2000 miti ya 1000*70 na 2000*3 = 120,000/=
4. Tafuta chagalawe / moramu trip 10*3000 =30000/=
5. Cement mifuko kwa ajiri ya sakafu na mashimo ya kulishia 5 *18000 = 90,000/=
6. Misumari ya aina 4, nch 6 kg5,nch 3 kg5 nch 5 kg10 na nch4 kg10, Bawaba na komeo =100,000/=
7. Malipo ya fundi 75000 fundi uashi na 75000 fundi seremala =150,000
JUMLA HAPO INAKUWA 790,000/= MAKADILIO INAKUWA 800,000/=
 
UNUNUZI WA NGURUWE WA KUANZIA .
Nguruwe wadogo wadogo ni vinzuri zaidi kuanza nao kwa sababu watakuzalia watoto wengi na kwa muda mrefu . Chukua mfano MILLION 2.5 . Nguruwe wadogo wa dogo wanauzwa 50000 au 40000 inategemeana na mahala na maelewano . Milioni 2.5 inakupa vitoto 50 au 55 . Hivyo unawexa kuwa na vitoto jike 50 na vidume 5. baadaye ukaongeza madume matano ya kuazima au kukondi kwa ajiri ya kupandishia
 
MAANDALIZI YA CHAKULA
Mchaganyiko wa chakula cha nguruwe na gharama zake tunaweza ukadilia kujitosheleza kwa laki tatu kwa mwenzi mmoja kwa nguruwe hao 50, kwa 300,000/= , ambapo itajumuisha tiba / kinga, lishe, vyakula vya nguruwe vinaweza kuwa pumba ya mpunga ile laini,pumba ya mahindi, mashundu, mabaki ya magada ya vianzi amba mabaki ya chakula yaliyosalama
 
MALIPO YA MSIMAMIZI NA ENEO LA KUWEKEZA
Katika kipengele hiki makadilio ya juu ama ya chini kwa msimamizi wa kazi yako waweza mlipa 100,000/= ama chini yake pia kwa mwenye eneo huwa nimaelewano tu aunaweza pata kwa fair au kukakodi kwa laki tatu, 300,000/= kwa mika miwili.
 
HIVYO JUMLA YOTE YA GHARAMA ZA UAZISHAJI UWEKEZAJI WA NGURUWE 50 ZITAKUGHARIMU MILLION 4 AMA MILLION 3.5 KWA MAANA KUWA HAPO JUU NIMETUMIA MAKADILIO YA JUU NA UKIINGIA KWENYE UHALISIA KAMA MJASIRIMALI LAZIMA IPUNGUE NA KUFIKIA 3.5

KIPATO AU FAIDA YA UFUGAJI NGURUWE
Nguruwe wanafaida ya haraka na nimradi wa uhakika kabisa, ukipitiia mchanganuo hapo juu wa nguruwe 50 utatupa faida kama ifatavyo
 
Nguruwe huzaa Mara mbili kwa mwaka na huzaa watoto zaidi ya watanoyaani huzaa watoto 12 ama nane .
Basi chukua nguruwe 50 * vitoto 5 yaani ufanye kuwa nguruwe wako 50 wakupatie vitoto vitano vya uhakika
Nguruwe 50*5 = 250 ukijumlisha na wale 50 wa mtaji umakuwa nao 300 . Chukua zao la nguruwe la 250 na uza kwa 200000 kwa kila nguruwe yaan bei ya kawaida kabisa. Utapata Million 50.

Hivyo zao la kwanza ndani ya robo tatu ya mwaka inakutegenezea million 50 pia na mienzi sita ijayo inakupa tena 50 na zaidi ili kukamilisha uzao wa pili hii inkupa uhakika wa kutegeneza million 100 za uakakika ndani ya mwaka mmoja na nusu ama miaka miwili ukijipa timeframe work lakini kumbuka hapo tumefanya kwa hesabu ya uzao wa chini kabisa ambapo tumeangalia na hasara ya vifo kama vifo visipotokea na uzao ukawa mkubwa utakuwa na uhakika wa kutegeneza million 150 kwa miaka miwili.

Kwenye hesabu ya kuwale unaweza kuwaza sana kuwa itaongezeka na kukughalimu sana jibu ni hapana mpka kufikia kuuza hawatokugharimu zaidi ya million 7 je million 7 kwenye million 150 ni kitu kisicho nafaida ?
 
NB . jambo lolote linahitaji umakini naa dhamira ya dhati pia kushirikisha wataalamu na wenye uzoefu ili kufikia leng Ewe ndugu kila kitu kinawezekana UTAYARI WAKO / UTHUBUTU WAKO, UAMINIFU .NA MAAMZI YAKO.
 


Share:

PICHA: Rais Magufuli na Viongozi Wengine wakiwa katika ukumbi wa Karimjee, kumuaga Dr. Mengi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, wakiwa katika ukumbi wa Karimjee, kumuaga Dr. Mengi.
Familia ya Dr. Mengi ikiusindikiza mwili wa Dr Mengi kwa ajili ya kuagwa katika ukumbi wa Karimjee



Share:

LIVE | Shughuli ya Kuagwa kwa Marehemu Dkt. Reginald Mengi - Ukumbi wa Karimjee DSM

Viongozi mbalimbali, ndugu na Marafiki wanashiriki katika tukio la kuagwa kwa aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP , Dkt Reginald Abraham Mengi. Shughuli hio inafanyika leo hii katika Ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es salaam. Tazama hapo chini


Share:

Hii ndio ratiba ya kumuaga Dkt. Reginald Mengi Karimjee

Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa makampuni ya IPP Media, Reginald Mengi, unaagwa leo Mei 07, katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Hapo chini ni ratiba ya tukio zima



Share:

Branch Manager – Tabora Job at Exim Bank Tanzania

JOB DETAILS:
JOB TITLE: Branch Manager
REPORTING TO: Cluster Head
RESPONSIBLE FOR: All Branch Staff
REGION: As per Branch location
• Job Category : Management
• Job Code : 2019
• Job Name : Branch Manager – Tabora
Deadline of this Job: 22nd May 2019
 
1. PURPOSE OF JOB
To meet branch Retail and SME Financial Targets through a World class Sales and Service Management system and within established product programs through the branch.
To work closely with Central Operations Unit to operate and maintain a smooth running and operationally efficient branch, that conform to the financial institutions and BOT regulations, rules and guidelines issued from time to time. This will include servicing corporate customers. .

RESPONSIBILITIES
• Accountable for all aspects of running a successful branch, delivering great business performance and leading and motivating a team that provides the best customer experience in your area.
• Primary responsibility will be to drive business (CASA and Fee Growth) product sales and Customer Service with oversight on branch operations, compliance and control.
• Understand your customer base and identify opportunities to build and grow profitable Relationships.
• Deliver against business and sales performance.
• Acquire new customers and retain and grow your relationships with existing customers.
• Responsible for the operational efficiency of the branch and productivity of its staff.
• Responsible for the operation and maintenance of the integrated systems, and retention of accurate and up to date records of all transactions including inter-bank transactions.
• Prepare periodic and statutory reports for management.Source: Ajiraleo Tanzania
• Have a good understanding of branch control procedures with specific focus on financial security.
• Take ownership for resolving complex problems, working with colleagues in other offices / Branches to provide a seamless experience for your customers.
• Provide a superior level of customer relations and promote the service culture through coaching, Guidance and staff motivation.
• Participate in community affairs to increase the bank’s visibility and enhance new and existing Business opportunities.
• Perform other duties in the absence of the MCSOP / Ops Manager as directed by the Cluster Head.
FINANCIAL RESPONSIBILITIES
• Manage your resources effectively and within budget.
INDEPENDENT DECISIONS
• Set challenging performance and business objectives.
• Work to your peoples’ strengths and instill in them the passion and commitment to deliver an exceptional service.
• Monitor your teams’ effectiveness by developing individual performance objectives and make recommendations for improvements, while also being accountable for achieving sales and customer satisfaction objectives.
• Address and manage under performance as soon as it is identified following company guidelines.
INTERACTION WITH OTHERS
Internal: Regular contact with the CEO, CFO, Head of Retail, Head of Liability, Cluster Heads and other Managers
External: Regular interaction with customers, clients and progress meetings with management

SKILLS
• At least 5 years experience in the banking Industry
QUALITIES
• Good leadership, people management and banking skills
• Knowledge of relevant legislation, sales and business principles,
• Outstanding communication skills
• Strong commercial know-how and first class decision making abilities.
• Be a good relationship builder and a strategic thinker rather than just operational.
• Resilient under pressure.

OTHER
• Carry out work in accordance with the banks procedures
• Perform the assigned tasks with due diligence
• Eliminate waste of whatever form, suggest the use of new practices and contribute to the continuous improvement of the bank..

Job Education Requirements: Degree in Business Administration

Job Experience Requirements: 5 years experience

Job application procedure


Share:

Naibu Waziri Mhe.kanyasu Apiga Marufuku Ukamataji Mchanga Pori La Akiba La Rungwa

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amepiga marufuku ukamataji wa  vifurushi vya mchanga unaodaiwa kuwa na madini ya dhahabu unaochimbwa na wachimbaji wadogo wadogo ndani ya Pori la Akiba la Rungwa wilayani Manyoni, mkoani Singida kinyume cha sheria na kuuagiza Uongozi wa Pori hilo kuhakikisha unaimarisha   ulinzi  katika maeneo yote yanayodaiwa kuwa na madini ndani ya pori hilo ili kuzuia Wachimbaji  kuingia na kuendesha shughuli ya uchimbaji wa mchanga kinyume cha sheria.

Marufuku hiyo imekuja kufuatia taarifa za kuwepo kwa baadhi ya Maafisa Wanyamapori  ambao wamekuwa wakiwaruhusu Wachimbaji hao kuingia ndani ya Pori hilo nyakati za usiku  kwa ajili ya  kuchimba mchanga unaodaiwa kuwa una madini kwa makubaliano yaliyo nje ya utaratibu.

Akizungumza  na Watumishi wa geti la Doroto katika Pori hilo wilayani Manyoni mkoani Singida, Mhe.Kanyasu amesema kuwa tuhuma hizo za rushwa zitaisha tu pale watakapoimarisha ulinzi katika eneo hilo na sio kukamata vifurushi vya mchanga kwenye geti hilo.

 Ameuagiza Uongozi huo kuhakikisha  unakamata vifurushi wanavyohisi ndani yake kuna madini  na lazima Afisa Madini awepo ili kuhakikisha anataja thamani ya madini  pamoja na taratibu zinazotakiwa kufuatwa  ili kukidhi matakwa ya sheria ya utaifishaji wa mali iliyokamatwa.

 Baadhi ya Wachimbaji wadogo walionyang'anywa mchanga wao wamedai kwamba Maafisa hao wamekuwa wakikagua magari kwenye geti la kutokea la Doroto na pale wanapokamata vifurushi hivyo bila kujua mchanga huo una madini kiasi gani wamekuwa wakimruhusu mtuhumiwa aende zake bila kumueleza taratibu zozote zile jambo ambalo ni kinyume na sheria.

Amesema kitendo hicho ni unyang'anyi na uonevu wa hali ya juu na ni kinyume cha sheria kwa sababu sheria ya utaifishaji wa mali iliyokamatwa inampa nafasi mtuhumiwa kujua thamani ya mali aliyokamatwa nayo  na ndipo taratibu za kesi kwenda mahakamani hufuata.

Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu amewaonya Maafisa Wanyamapori katika pori hilo kuacha tabia ya kuwaonesha wachimbaji hao mahali wanapohisi  kuwa kuna madini kwa kuwa kitendo hicho ni kinyume cha sheria.

Amesema ni ngumu kwa Mwananchi yeyote kujua sehemu ambako kuna madini ndani ya Pori bila kudokezwa na wenyeji ambao ni Wahifadhi wa Pori hilo

Amesisitiza kuwa endapo uchimbaji huo wa madini ndani ya Hifadhi utaendelea kufanyika itakuwa ni ushahidi tosha kuwa Meneja wa Pori hilo kashindwa kazi.

Aidha, Mhe.Kanyasu amewataka kuimarisha ulinzi katika maeneo yote ya Pori hilo ili kukomesha ujangili wanyamapori pamoja na ukataji miti ndani ya Pori hilo.

Kwa upande wake, Meneja wa Pori la Akiba la Rungwa, Patrick Kutondolana amekiri kuwa wamekuwa wakikamata mchanga huo kwa mashirikiano kati ya Kamati ya Ulinzi wa Wilaya hiyo ili kukomesha tabia hiyo ya uchimbaji mchanga ndani ya Hifadhi.

Amesisitiza kuwa si kweli kuwa wamekuwa na ushirikiano na Wachimbaji hao kwa makubaliano ya kupata rushwa ni kwamba hiyo imekuwa njama ya kutaka kuwachafua kwa lengo la kuwakatisha nia.



Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya May 7




Share:

Mbunge Chadema akamatwa na polisi Dodoma

Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga (Chadema), amekamatwa na Jeshi la Polisi jijini Dodoma leo Jumatatu Mei 6, wakati akitoka kuhudhuria vikao vya Bunge vinavyoendelea.
 
Akizungumzia tukio hilo, Katibu wa wabunge wa Chadema, David Silinde amesema hawajapata taarifa rasmi kwanini mbunge huyo amekamatwa.

“Huu ni mwendelezo wa matukio ya viongozi wetu kukamatwa, licha kwamba walitakiwa kuujulisha uongozi wa bunge,” amesema Silinde.

Alipoulizwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amesema hana taarifa za kukamatwa kwa mbunge huyo.

"Niko Gairo sijapata taarifa zozote za  kukamatwa kwa mbunge huyo," amesema Muroto.


Share:

Monday, 6 May 2019

Picha : MAELFU WAJITOKEZA KUUPOKEA MWILI WA MAREHEMU DR. MENGI DAR

Jeneza lenye Mwili wa marehemu Dk. Reginald Mengi ukiingizwa kwenye gari maalumu baada ya kuwasili nchini nchini ukitoa Dubai, tayari kwa safari ya kuelekea Hospitali ya Jeshi Lugalo, jijini Dar es salaam kwa kuhifadhiwa.

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MAELFU ya wananchi wa Jiji la Dar es Salaam leo Mei 6,2019 wamejitokeza kwa wingi kuupokea na kuulaki mwili wa aliyekuwa mfanyabishara maarufu nchini Tanzania na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Dk. Reginald Mengi ambaye amefariki dunia Mei 2 mwaka huu akiwa Dubai.

Mwili wa marehemu Dk.Mengi umewasili nchini saa nane mchana ambapo viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wastaafu na wananchi wa kada mbalimbali walijitokeza Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kuupokea.

Pia Mke wa Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete alikuwa miongoni mwa waliofika uwanjani hapo kuupokea mwili huo wa Dk.Mengi. Baada ya kuwasili na kupokelewa na kufanyika maombo kabla ya kuanza safari ya kuelekea Hospitali ya Lugalo.
Mjane wa Marehemu Dkt. Mengi, Bi. Jacquenine akiwana wa waombolezaji wengine pamoja na Mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete waliofika kwenye uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere kumlaki.

Maelfu ya wananchi waliamua kuweka kambi katika barabara ambazo mwili wa Mengi umepitishwa ambapo wapo baadhi ya wananchi walionekana wakigusa jeneza ambalo limebeba mwili kama ishara ya kuonesha upendo.

Wakati mwili unapitishwa katika barabara ya Nyerere, Buguruni, Ilala,Kigogo, Magomeni, Kinondoni na Morroco wakati ukielekea Mwenge na kisha Lugalo idadi ya watu ilizidi kuongezeka kuusubiri mwili wa Dk.Mengi.

Simanzi na majonzi yalikuwa yametawala katika nyuso za wananchi walioamua kwenda kuulaki mwili wa Dk.Mengi huku wengi wao wakionekana kukimbilia gari iliyobeba mwili huo kwa lengo la kulishika. Mengi enzi za uhai alijipambanua kuwa karibu na jamii ya Watanzania ambapo alitumia sehemu ya fedha zake kutoa misaada.
Kutokana na idadi ya watu waliokuwa wamejipanga barabarani, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda aliyekuwa kwenye msafara huo alionekana akihakikisha msafara huo unakwenda katika mazingira yaliyotulivu huku akisaidiwa na Jeshi la Polisi kupita Kikosi cha Usalama barabarani.

Katika msafara huo waendesha bodaboda nao hawakuwa nyuma kwani nao walikuwa sehemu ya wananchi ambao walihakikisha wanakuwepo katika mapokezi ya mwili huo.

Wananchi mbalimbali ambao walikuwa barabarani na kupata fursa ya kumzungumzia Dk.Mengi wamesema kuwa na mambo mengi ya kujifunza kutoka katika maisha ya Mengi ambaye enzi za uhai wake alikuwa na upendo kwa kila mtu na kubwa zaidi alihakikisha utajiri wake unawanufaisha na wengine kwani hakuwa mchoyo.
Sehemu ya waombolezaji wakiwa wamejitokeza kwa wiki maeneo mbalimbali jijini Dar es salaam kuulaki mwili wa marehemu Dk. Reginald Mengi uliowasili nchini mchana wa leo. 
Mjane wa Marehemu Dkt. Mengi, Jacqueline Mengi akilia kwa uchungu.
Share:

RC MOROGORO AWAASA MADAKTARI KUFANYA TAHMINI YA MAGONJWA NA AJALI ZITOKANAZO NA KAZI KWA KUZINGATIA MAADILI


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Kebwe Steven Kebwe, akitoa hotuba ya ufunguzi wa mafunzo ya siku tano kwa madaktarina watoa huduma za afya kuhusu namna ya kufanya tathmini ya magonjwa na ajali zitokanazo na kazi mjini Morogoro leo Mei 6, 2019. Mafunzo hayo ambayo yamewaleta pamoja madaktari kutoka hospitali na umma na binafsi kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Lindi na Mtwara yameandaliwa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF).
Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba, akitoa neon la utangulizi.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Steven Kebwe (wapili kulia), akipeana mikono na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Masha Mshomba, mara baada ya kufungua mafunzo ya siku tano kwa madaktari n a watoa huduma za afya kuhusu namna ya kufanya tathmini ya magonjwa na ajali zitokanazo na kazi. Mafunzo hayo yaliypowaleta pamoja Zaidi ya madaktari 100 kutoka mikoa mitano imeanza leo Mei 6, 2019 mjini Morogoro. Wakwanza kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Ttahmjni wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. Abdulsalaam Omary.
Mkurugenzi wa Uendeshaji WCF, Bw. Anselim Peter, akitoa mada kuhusu kazi za Mfuko
Mkuu wa Kitengo cha Sheria, WCF, Bw.Abraham Siyovelwa, akitoa mada kuhusu masuala ya kisheria katika kutekeleza majukumu ya Mfuko.
Mkurugenzi Mkuu, Bw. Mshomba (wapili kushoto), akibadilishana mawazo na wataalamu (wawezeshaji), Daktari bingwa mbobezi wa mifupa na viungo nchini, Dkt. Robert Mhina(watatu kushoto), Dkt. Hussein Mwanga na Bw. Yahya Kishashu.
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, MOROGORO
MKUU wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Steven Kebwe, amewaasa madaktari kufanya tathmini ya magonjwa na ajali zitokanazo na kazi kwa kuzingatia miongozo iliyopo.

Dkt. Kebwe ametoa wito huo leo Mei 6, 2019 wakati akifungua mafunzo ya siku tano kwa madaktari na watoa huduma za afya kuhusu namna ya kufanya tathmini ya magonjwa na ajali zitokanazo na kazi mjini Morogoro.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na zaidi ya madaktari 100 kutoka mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam na Morogoro wanashiriki mafunzo hayo.

“Mnapofanya tathmini vizuri mnausaidia Mfuko kulipa fidia stahiki, mfanye tathmini kwa haki, msije mkaingia kwenye mtego msikubali kurubuniwa na huu ndio wito wangu kwenu.” Alisema.

Dkt. Kebwe aliupongeza Mfuko kwa hatua iliyofikia hususan katika eneo la kutoa elimu kwa wadau kama madaktari ambao ndio huuwezesha Mfuko kutekeleza wajibu wake wa ulipaji Fidia kwa usahihi.

“Kwa sasa tayari mmetoa mafunzo kwa madaktari 764 kote nchini na leo hii idadi nyingine inaongezeka hili ni jambo ambalo mnastahili pongezi kwa kufikia hatua hii katika muda mfupi wa uhai wa Mfuko.” Alisema Dkt. Kebwe.

Alisema Mfuko huu ni muhimu katika nchi yetu katika kipindi hiki ambacho taifa linajenga uchumi wa viwanda.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba alisema licha ya kutoa mafunzo hayo, lakini pia Mfuko hutumia fursa hiyo kuwaelimisha kuhusu shughuli za Mfuko.

Alisema mafunzo hayo yatatolewa na wataalamu kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kwa kushirikiana na watalamu kutoka Taasisi ya Mifupa MOI na MUHAS.

Aidha Bw. Mshomba alimpongeza Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuona umuhimu wa kipekee katika kujenga uchumi wa viwanda kwa kuweka kipaumbele kwa nchi yetu kama namna ya kutufikisha kwenye uchumi wa kati ifikapo 2020-2025 kwani ni ukweli ulio wazi kwamba hakuna nchi iliyoendelea Duniani bila ya kuwa na uchumi wa viwanda na nilazima wote kama watanzania tusimame pamoja kumsaidia Mhe. Rais.

“Sisi kama Mfuko tutamsaidia Mhe. Rais katika azama yake kwa kuahkikisha kwamba, tunafanya kazi kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha na kuwakinga wafanyakazi kwa kutoa elimu ili kuhakikisha kwamba tunalinda nguvu kazi ya taifa kwa kuzuia ajali makazini au kuzipunguza na hata zinapotokea basi malipo ya Fidia yanafanyika kwa haraka”. Alisema.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger