Tuesday, 27 December 2016
Monday, 26 December 2016
MPYA:HAYA HAPA MAJINA 505 YA WANAFUNZI WA MWENGE UNIVERSITY-MOSHI AMBAO HAWATA GRADUATE KISA SERIKALI KUTOKULETA ADA YAO YA CHUO
'Yesu nipe nyonyo‘: Wimbo Ambao Kenya Inataka Uondolewe Mtandaoni Kwa Kudhalilisha Dini
Gazeti
la Kenya liitwalo taifa leo limeripoti kwamba bodi ya filamu kwenye
nchi hiyo imehuzunishwa na Msanii wa muziki wa Injili SBJ kuimba wimbo
wa Injili ambao unadhalilisha Imani.
Wimbo wenyewe unaitwa ‘Yesu nipe nyonyo‘
ambapo mkuu wa bodi hiyo Ezekiel Mutua alisema baadhi ya Waimbaji wa
Kenya wamekosa maadili na kipaji cha kubuni au kutunga nyimbo nzuri
zisizochafua hali ya hewa.
Alisema wimbo huo unaendelea kukaguliwa kwa sababu Wakenya wamekasirishwa: "Nashangaa
sana mtu mzima anakaa chini na kuimba wimbo kama huu, Wasanii wetu
wamejua kuwa kama hawaongei uchafu ama kutoa video za utata
hawatasikilizwa wala kutazamwa na wanafanya hivyo ili wapate umaarufu”
Tayari
bodi hiyo ilikua kwenye mipango ya kuwaandikia Youtube ambao ndio
wanamiliki wa mtandao huo ili waiondoe hiyo video kwasababu bodi hiyo
inayo mamlaka na katiba haitakubali Wasanii kutunga nyimbo za
kudhalilisha imani.
Mpaka sasa wimbo huo bado upo kwenye mtandao na umeshatazamwa mara 93,812 mpaka sasa.
Rais Magufuli Atoboa Siri ya Kula Christmass Mkoani Singida
Rais
wa Jamhuri ya Muungano Tanzania,Dk.John Pombe Magufuli,amefichua siri
ya kusali Krismasi kwenye kanisa la Parokia ya Moyo wa Yesu, mjini
Singida mwaka huu.
Ametaja
siri hiyo kuwa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita, aliwahi
kusali kwenye kanisa hilo na wakati akitoka, alikutana na sista mmoja
(hamkumbuki jina) ambaye alimzawadia rozali, na kumwahidi kuwa itamsadia
kushinda uchaguzi huo.
Rais
Magufuli ametoa siri hiyo jana wakati akizungumza kwenye sherehe ya
Krismasi iliyofanyika kwenye kanisa la Porokia ya Moyo wa Yesu, na
kuhudhuriwa pia na mke wa Rais, Mama Janeth Magufuli.
Akifafanua,
alisema kuwa rozali hiyo amezunguka nayo kwenye kampeni yake, na mwisho
wa siku, alifanikiwa kupata kura za kutosha na hivyo kuwa mshindi.
“Hiyo
ndio sababu kubwa au siri ya mimi kufika mjini Singida, na kuungana na
wakazi wa mkoa wa Singida na Watanzania kwa ujumla, kusherehekea
kuzaliwa kwa Yesu kristo,” alisema na kusababisha mamia ya waumini kushangilia kwa nguvu.
Rais
Magufuli alitumia fursa hiyo kuwataka Watanzania wote kutumia sikukuu
hii ya Krismasi kuimarisha upendo, kuvumiliana na wala wasibaguane ,na
kwa njia hiyo,Tanzania itaendelea kupaa kimaendeleo.
Katika
hatua nyingine, alisema kuwa Watanzania na hususani wakulima,
wahakikishe wanazitumia vizuri mvua zinazonyesha kwa sasa nchini kwa
kuchapa kazi ya kilimo kwa nguvu zote na kulima mazao yanayostahimili
ukame.
“Ndugu
zangu waumini na Watanzania kwa ujumla, acheni kulialia kuwa fedha
zimepotea … fedha hazijapotea isipokuwa ninyi wenyewe hamfanyi kazi.
Vitabu vyote vya madhehebu ya dini vinasisitiza wajibu wa kuchapa kazi …
na vinasema asiyefanya kazi na asile,” alisisitiza.
Akiijengea
nguvu hoja yake ya hapa ni kazi tu, alisema kuwa Yesu kristo amezaliwa
na fundi mchapa kazi kweli kweli seremala, na hivyo tunaposherehekea
Krismasi Watanzania wote wenye uwezo wa kufanya kazi, wafanye kazi huku
wakijua hakuna cha bure.
Aidha,
Rais Magufuli, aliwataka wakazi wa mkoa wa Singida, kuongeza uzalishaji
wa zao la alizeti, ili kukiwezesha kiwanda kikubwa cha kukamua mafuta
ya alizeti cha Mount Meru kupata mbegu za kikudhi mahitaji ya kiwanda.
Awali
askofu wa kanisa katoliki jimbo la Singida, Edward Mapunda, alitumia
fursa hiyo kuwakumbusha wakazi wa mkoa wa Singida, kutunza mazingira,
ili yaweze kuwatunza na wao.
Alisema
hivi sasa hali ni mbaya kutokana na binadamu kuongeza kasi ya kuharibu
mazingira, kitendo kinachochangia madhara mengi ikiwemo uhaba wa mvua.
“Mimi
nashangaa sana, watu wanaendelea kuzaa huku wakiendelea kuharibu
mazingira na kutishia nchi kuwa jangwa. Tuna zaa watoto waje wateseke
kutokana na uharibifu wa mazingira. Kama tunaendelea kuharibu mazingira,
ni vema tuache kuzaa”, alisema Mapunda.
HII HAPA RATIBA YA KOMBE LA MAPINDUZI INAANZA RASMI DISEMBA 30 2016
Pazia la Mashindano ya Kombe la Mapinduzi linatarajiwa kuanza kutimua
vumbi lake Disemba 30, 2016 katika uwanja wa Amaan saa 2:15 Usiku
ambapo kutakuwa na mchezo wa Derby ya Jangombe kati ya Taifa ya Jangombe
na Jangombe Boys ambapo mashindano ya msimu huu yameshirikisha vilabu
9, vitano vikitokea Zanzibar, vitatu Tanzania bara na kimoja kutaka
Uganda ambao ndio mabingwa watetezi timu ya URA.
KUNDI A: Simba, URA, KVZ, Taifa ya Jangombe na Jangombe Boys.
KUNDI B: Yanga, Azam, Zimamoto na Jamhuri.
RATIBA KAMILI YA MAPINDUZI CUP
30/12/2016 Taifa ya Jang’ombe vs Jang’ombe boys saa 2:30 usiku.
1/1/2017 KVZ VS URA Saa 10:00 alasiri, Simba vs Taifa ya Jang’ombe saa 2:30 usiku.
2/1/2017 Azam vs Zimamoto saa 10:00 alasiri, Yanga vs Jamhuri saa 2:30 usiku.
3/1/2017 Jang’ombe boys vs URA saa 10:00 alasiri, KVZ vs Simba saa 2:30 usiku.
4/1/2017 Zimamoto vs Yanga saa 10:00 alasiri, Jamhuri vs Azam saa 2:30 usiku.
5/1/2017 KVZ vs Jang’ombe boys saa 10:00 alasiri, Simba vs URA saa 2:30 usiku.
6/1/2017 Taifa ya Jang’ombe vs KVZ saa 2:30 usiku.
7/1/2017 Jamhuri vs Zimamoto saa 10:00 alasiri, Yanga vs Azam saa 2:30 usiku.
8/1/2017 Simba vs Jang’ombe boys saa 10:00 alasiri ,Taifa ya jang’ombe vs URA 2:30 usiku.
10/1/2017 Saa 10: 00 nusu fainali ya kwanza , Saa 2:30 nusu fainali ya pili.
13/1/2017 Fainali saa 2: 30 usiku.
MICHEZO:HAJI MANARA AMUOMBEA MSAMAHA JERRY MURO KWA RAIS TFF
Mkuu
wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba Haji Sunday
Manara amejitokeza kwa mara ya kwanza kumuombea msamaha mtani wake Jerry
Muro ili kuifufua upya hamasa na kuongeza ushindani katika ulimwengu wa
soka la Bongo.
Manara
katika ujumbe aliouweka kwenye mtandao wake wa Instagram akiuelekeza
kwa Rais wa TFF Jamal Malinzi, amesema katika kuadhimisha sikukuu ya
Krismasi anaona ni wakati muafaka sasa kwa Rais Malinzi kutumia mamlaka
yake kumfungulia Jerry kwa kuwa amekwishatumikia takriban nusu ya
kifungo chake na kwamba soka la Bongo linamuhitaji sana kwa sasa.
"Nimekaa
nimetafakari sana,nimeamua kumuombea msamaha mtani wangu Jerry Muro
ambaye TFF mlimfungia mwaka mmoja kujihusisha na mpira wa miguu,
ninafanya hivi nikijua kabisa Jerry alikosea na tayari ameshatumikia
karibia nusu ya kifungo chake, ninajua kwa kufanya hivyo atakuwa
keshajifunza lugha za kutumia na pia itakuwa fundisho kwetu sisi
wasemaji na viongozi wa vilabu kwa ujumla. "Ameandika Manara
Manara pia hakusita kukumbushia jinsi ambavyo Jerry Muro amewahi kumtolea hata yeye mwenye lugha za kuudhi "
Nnafahamu
pia Jerry aliwahi kunitolea lugha zisizostahili mimi bnafsi, lakini
yale yashapita na binafasi amenihakikishia kutorudia tena, na nnaamini
viongozi na washabiki wa Simba watanielewa dhamira yangu hii njema,
ambayo inathibitisha uungwana tulio nao wanasimba".
manara
amemaliza kwa kusema kuwa soka la Tanzania linammis sana Jerry Muro na
kuomuomba Rais Malinzi kutumia mamlaka yake kumfungulia kwa kuwa Jerry
bado alikuwa hajawa na uzoefu wa kutosha katika siasa za mpira.
Kwa
upande wake Jerry Muro amefurahi na kushukuru kuona mtani wake Haji
Manara anamkumbuka na kutumia fursa hiyo kuomba msamaha kwa shirikisho
la soka Tanzania ili aendeleze hamasa ya soka aliyokuwa ameiweka nchini
yeye na Haji Manara.
MAOMBI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU,SERIKALI KUFANYA UPYA UHAKIKI WA FOMU ZA MAOMBI

Serikali imesema inaanza uhakiki upya, kwa kupitia fomu zote za maombi
zilizowasilishwa na wanafunzi kwenye bodi ya mikopo, baada ya kubaini
kuwa idadi kubwa ya wanafunzi walioomba mikopo ya elimu kupitia bodi ya
mikopo nchini wamejaza taarifa za uongo.
Profesa Simon Msanjila ambaye ni Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu,
Sayansi na Teknolojia amesema haya wakati wa mahafali ya nne ya Chuo
Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mbeya , akisema serikali imeanza
uhakiki mara moja kwa kupitia fomu zote zilizowasilisha kwenye bodi ya
mikopo , na atakaye bainika kuwa amejaza taarifa zisizo sahihi
atafikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Katika mahafali haya wanafunzi zaidi ya 800 wanehitimu kozi mbalimbali
zikiwemo za uhandisi, usanifu wa majengo, umeme na tehama.
Awali Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia Mbeya Profesa Mark
Mwandyosa ameandaa mhadhara ulioshirikisha wanazuoni na wasomi
mbalimbali ,na kumtaka Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Joseph
Msambichaka kufundisha watanzania sayansi na teknolojia, na sio
teknolojia pekee, ili kuandaa wanasayansi ukilinganisha na wahitimu
wengi wanaohitimu chuoni hapo ambao wanajikita zaidi kwenye teknolojia.
Saturday, 24 December 2016
Hatuhusiki na ajira za walimu - Wizara ya Elimu
Wizara ya Elimu, Sayansi,
Teknolojia na Ufundi imesema haihusiki na utoaji wa ajira za walimu
nchini, isipokuwa inachokifanya ni uhakiki wa taarifa za walimu wenye
sifa za kuajiriwa serikalini.
Mhandisi Stella Manyanya
Akizungumza na EATV , Naibu Waziri wa Elimu, Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa kwa sasa wizara hiyo inapitia taarifa (CV) za walimu waliohitimu ngazi ya Stashada na Stashahada, na baada ya hapo itazituma taarifa hizo katika Wizara ya Utumishi ambao ndiyo wanaohusika na kuajiri.
Akizungumzia sababu za kuwatenga wahitimu wa ngazi ya cheti, Manyanya amesema uhitaji mkubwa uliopo kwa sasa ni kwa walimu wa sekondari hususani wa masomo ya Phisics, Hisabati, Chemistry na Biolojia, hivyo inawahitaji kwa haraka zaidi walimu hao huku akisema wahitimu wengine ambao siyo wa masomo hayo na ambao siyo kwa ajili ya kufundisha sekondari, wasubiri utaratibu wa wizara inayohusika na utumishi.
"Siyo kwamba hatuhitaji walimu wa shule za msingi, lakini uhitaji mkubwa tulionao kwa sasa ni walimu wa sekondari, sisi hatuajiri, sisi tunafanya uhakiki, na sasa tunapitia CV za wahitimu waliotuma taarifa zao, tukishajiridhisha na wale ambao taarifa zao ni sahihi na wana sifa tunazohitaji, tunazipeleka Utumishi, hao ndiyo wataajiri, halafu majina yatapelekwa TAMISEMI kwa ajili ya kupangiwa maeneo ya kazi" Amesema Manyanya
Kuhusu idadi ya walimu wanaohitajika haraka, Manyanya amesema, wanahitajika walimu wengi kuliko idadi waliyoitoa mwanzo, na kuwataka wote waliotuma taarifa zao wawe na subira kwa kuwa mchako wa uhakiki bado unaendelea na majina yatatangazwa muda mfupi ujao ambao hautazidi kipindi cha miezi mitatu.
Kingunge Asema Bila tume huru Wapinzani Wasahau Kuingia Ikulu,Lowassa Akubali Yaliyopita Si Ndwele
Mwanasiasa
mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru amesema bila ya kuwa na tume
huru ya uchaguzi na Katiba Mpya, vyama vya upinzani visahau kushinda
urais katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Kauli
ya Kingunge imekuja siku moja baada Rais John Magufuli kumteua Jaji
Themistocles Kaijage kuwa mwenyekiti mpya wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
(NEC) baada ya Jaji Damian Lubuva kufikia muda wake wa kustaafu.
Kwa
muda mrefu, NEC imekuwa ikilalamikiwa na vyama vya upinzani kwa
kutokuwa huru kwa sababu ya uongozi wake wote huteuliwa na Rais ambaye
pia ni mwenyekiti wa CCM, huku sheria zikikataza matokeo ya nafasi ya
urais kupingwa mahakamani.
Mbali
na mwenyekiti kuteuliwa na Rais, wasimamizi wa uchaguzi wa majimbo ni
wakurugenzi wa wilaya ambao pia huteuliwa na Rais kwa kuwa NEC haina
wafanyakazi wake kote nchini.
Akizungumza
katika mkutano wa kuwafariji vijana waliokamatwa na Jeshi la Polisi na
kushtakiwa kwa makosa yaliyohusu Uchaguzi Mkuu uliopita, uliofanyika
jijini Dar es Salaam jana, Kingunge aliwatia moyo vijana hao, akisema
hakuna ushindi unaopatikana bila kupambana.
Kingunge,
aliyetumia muda mrefu kueleza historia ya maisha yake katika siasa na
jinsi alivyopambana katika harakati za kudai uhuru, alisema hali ya sasa
ni mbaya kuliko wakati wa wakoloni wa Kiingereza ambao walikujwa
wakali, kwa sababu CCM haifuati Katiba wala sheria.
“Yako
mambo ambayo itabidi tujitahidi yaamuliwe sasa kabla ya 2020. Mambo
hayo makubwa kwanza ni tume huru (ya uchaguzi). Suala hilo lazima
lizungumzwe sasa, hatuwezi kwenda 2020 na tume ya sasa na Katiba ya
mwaka 1977. Tukienda hivyo sahau habari ya upinzani kushinda uchaguzi,” alisema.
Kingunge
ambaye aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini ikiwamo ya waziri
anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na
mkuu wa mkoa alisema, “(Pia) Sheria inayohusu matokeo ya uchaguzi wa
Rais kuhojiwa. Hivi sasa sheria inasema matokeo ya uchaguzi wa Rais
hayahojiwi mahakamani. Lazima hilo suala lipate jibu sasa. Kwa hiyo
Katiba na sheria iseme, matokeo ya uchaguzi wa Rais yanaweza kuhojiwa
mahakamani. Tusipokuwa na hilo, tutakuwa na matatizo makubwa sana.”
Alisema
pamoja na kwamba Chadema inapendwa na wananchi wengi na Edward Lowasa
aliyegombea urais kwa tiketi chama hicho, anapendwa, bado ni vigumu
kushinda kwa sababu mfumo uliopo sasa.
“Tufanye
yoyote, lakini tuhakikishe, ama tunapata Katiba Mpya au vipengele hivi
vya sheria vinafanyiwa marekebisho. Kwa maoni yangu, kundi hili lililo
madarakani bila shinikizo kubwa kutoka kwa wananchi, halitataka
mabadiliko,” alisema.
Alisema
enzi zao walifanikiwa kupata uhuru kwa sababu walijitolea kwa nguvu na
wengine, na yeye akiwamo, waliacha kazi za mishahara mikubwa na kujiunga
na Tanu kupigania uhuru.
“Tulifanikiwa
kupata uhuru kwa sababu walijitoa mhanga. Wengi tu waliacha kazi, mtu
anamaliza chuo kikuu anasema sitaki kazi anaingia Tanu kusaidia. Kwa
hiyo tukawa na jeshi kubwa la vijana waliohakikisha nchi inapata uhuru,”
alisema.
“Ninyi
mnapambana katika mazingira magumu na wazee wenzenu walipambana katika
mazingira hayo. Haikuwa rahisi. Wapo wengi walitusaliti, wengine
hawakufanya lolote. Baba yangu tuligombana, nilipoacha kazi kwenda
kuitumikia Tanu. Miezi sita hatukuzungumza.”
Akizungumza
mkutano huo, Lowassa, ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema,
aliwatia moyo vijana walioshtakiwa wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka
2015, akisema bado jeshi kubwa la vijana linahitajika.
Penzi la Bibi wa Miaka 60 Laua Kijana wa Miaka 23
KIJANA
mwenye umri wa 23 na mpenzi wake, bibi mwenye umri wa miaka 60 , wakazi
wa kijiji cha Tentula, Kata ya Ikozi wilayani Sumbawanga, wanashikiliwa
na polisi wakihutumiwa kumshambulia na kumuua kikatili jirani yao
aitwae Desder Justino (23) kwa kile kinachoelezwa kuwa ni wivu wa
mapenzi.
Inaelezwa kuwa, Justino pia alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na bibi huyo.
Kamanda
wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, George Kyando alithibitisha tukio hilo na
kueleza kuwa mauaji hayo yalitokea Desemba 21 mwaka huu saa nne asubuhi
katika nyumba ya mwanamke huyo iliyopo kijijini Tentula.
Taarifa
kutoka kijijini humo zinadai kuwa, mwanamke huyo licha ya umri wake
kuwa mkubwa, alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na vijana hao wawili wa
rika moja.
Kamanda Kyando hakuwa tayari kutaja majina ya wapenzi hao ambao ni watuhumiwa wa mauaji kwa sababu za uchunguzi.
Lakini
alisema mwanaume ana umri wa miaka 23 huku mpenzi wake ana umri wa
miaka 60. Akielezea zaidi, Kamanda Kyando alisema siku ya tukio Justino
alikwenda nyumbani kwa mwanamke huyo ambaye anadaiwa kuwa na uhusiano
naye wa kimapenzi na kumkuta kijana mwingine (mtuhumiwa), na hapo ndipo
ugomvi ukaibuka baina ya vijana hao.Alisema Justino alijeruwa kichwani.
“Wawili
hao yaani wapenzi hao (mwanamke na mwanaume) walimshambulia Justino
(Desder) kwa kumpiga kichwani na kitu chenye ncha kali na kumjeruhi
vibaya na alikufa akiwa anatibiwa hospitalini,” alisema Kamanda
Kyando na kuongeza kuwa, watuhumiwa hao wanashikiliwa na watafikishwa
mahakamani uchunguzi wa awali utakapokamilika.
Makamu wa Rais ataka wazazi na walezi kuacha kuwaoza watoto wakiwa wadogo
MAKAMU
wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewataka wazazi na walezi wa visiwani
Zanzibar, kuacha tabia ya kuwaoza wasichana wakiwa na umri mdogo, bali
wawasomeshe kwa ajili ya manufaa yao ya jamii kwa ujumla.
Samia alisema hayo kwa nyakati tofauti, wakati akizindua madarasa ya kisasa iliyojengwa kwenye eneo la Kilimani na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa na ujenzi wa msikiti mkubwa kuliko yote nchini Tanzania unaojengwa katika eneo la Ijitimai Kidoti mkoani Kaskazini Unguja.
Ujenzi huo unafanywa kwa michango ya wananchi. Alisema hayo katika siku yake ya kwanza ya ziara ya Kikazi Unguja.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais, Zanzibar, ilieleza kuwa makamu huyo wa Rais yupo katika ziara visiwani Zanzibar.
Kwa
mujibu wa taarifa hiyo, Samia alisema kama wazazi na walezi watasomesha
watoto wa kike, elimu watakayopata itasaidia kwa kiasi kikubwa
wasichana hao, kufanya maamuzi sahihi na yenye tija katika jamii.
Alisisitiza
kuwa elimu ni haki ya msingi kwa mtoto wa kike, hivyo ni muhimu kwa
jamii ya Zanzibar ihakikishe watoto wa kike wote wanapata elimu, kwani
watakuwa na uwezo wa kuchagua na kuandaa mustakbali wa maisha yao ya
baadaye, ikilinganishwa na hali ilivyo sasa kwenye baadhi ya maeneo.
Kuhusu
elimu ya dini, aliwahimiza wazazi na walezi, kuwalea watoto katika
maadili mema kwa kuzingatia maandiko matakatifu ya Mtume Mohammad
(S.A.W).
Jaji Magimbi kusikiliza rufaa ya Godbless Lema Desemba 28
JAJI
Salma Magimbi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ndiye atakayesikiliza
rufaa ya kutaka dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema,
Desemba 28 mwaka huu katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana, Wakili wa Lema, Sheck Mfinanga alisema
rufaa hiyo namba 126 ya mwaka 2016, imepangiwa kusikilizwa na Jaji huyo.
Alisema kimsingi wanalalamikia uamuzi wa Mahakama kutomwachia huru,
licha ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kumpatia dhamana.
Awali,
uamuzi uliotolewa Novemba 11 mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi
Arusha na Hakimu Desderi Kamugisha, ambapo Lema anakabiliwa na kesi
namba 440 na 441 za uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli, uliweka wazi
dhamana.
Hakimu
Kamugisha alikubali kutoa dhamana kwa madai kuwa sheria haizuii kumpa
dhamana mtu kwa kesi ya uchochezi, ila kabla ya kutoa masharti ya
dhamana licha ya kutamka dhamana ipo wazi, mawakili wa serikali
walipinga kumpatia dhamana Lema, kwa madai wameonesha nia ya kukata
rufaa.
Kutokana na mawakili hao kusema hivyo, Hakimu aliamua kesi hiyo ibaki kama ilivyo na mtuhumiwa asubiri maamuzi ya Mahakama Kuu.
Lema
alilazimika kwenda mahabusu hadi sasa katika Gereza Kuu la Kisongo.
Baada ya hatua hiyo, mawakili wa Lema wakiongozwa na Sheck Mfinanga,
walianza kutafuta suluhisho la mteja wao kupata dhamana na walianza na
kuandika maombi na kuitaka Mahakama Kuu kufanya marejeo kwa kuitisha
faili la kesi hiyo kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.
Lakini,
ombi lilitupwa na Kaimu Jaji Mfawidhi, Sekela Moshi, Novemba 11 mwaka
huu kwa madai kuwa walikosea, badala ya kufanya marejeo walitakiwa
kukata rufaa. Mawakili hao walilazimika kukata rufaa siku hiyo hiyo na
Desemba 2 mwaka huu, ilitupwa na Jaji Fatuma Masengi kwa madai kuwa
ilikuwa nje ya muda.
Baada
ya hatua hiyo, mawakili hao walipeleka ombi Mahakama Kuu, kuomba
kuongezewa muda wa kupeleka notisi ya kukata rufaa yao juu ya dhamana na
hatimaye Desemba 20, Jaji Dk Modesta Opiyo, alikubali na kumwongezea
muda Lema wa siku 10.
Siku
hiyo ya kuongezewa muda, mawakili wa Lema walifanikiwa kukata rufaa
hiyo. Lema anashikiliwa kwa zaidi ya mwezi katika mahabusu ya Gereza Kuu
Kisongo.
Alikamatwa
Novemba 2 mwaka huu nje ya viwanja vya Bunge mjini Dodoma na
alifikishwa mahakamani Novemba nane mwaka huu, akikabiliwa na mashitaka
ya uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli.
Polisi Yanasa 200 Kwa Ujambazi Dar
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikilia watuhumiwa 200 wanaohusishwa na makosa mbalimbali.
Wanne
kati ya hao, wanatuhumiwa kukutwa na gari lililoibwa hivi karibuni
katika eneo la ofisi za Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA)
zilizopo Manispaa ya Ilala.
Mkuu
wa Operesheni Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya, alitaja
watu hao wanne wanaotuhumiwa kukutwa na gari hilo kuwa ni Leonard Said,
Omary Said, Shomaly Kilobo na Adam Unemba.
Alisema
katika uchunguzi wa awali, watuhumiwa wote wamekiri kuhusika katika
wizi wa gari hilo, aina ya Toyota Spacio lenye namba za usajili T 398
CAE, boksi la chuma la kutunzia fedha na televisheni ya ukubwa wa inchi
32.
Alisema
Desemba 5, mwaka huu alipokea taarifa kutoka kwa Mhasibu Mkuu wa TIRA,
Egnance Edward (53) kuwa wamekuta ofisi za mamlaka hiyo, zimevunjwa na
kuibwa baadhi ya vifaa ikiwemo gari hilo.














