Thursday, 7 April 2016

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 7.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Magazeti ya leo alhamisi april 7 2016
20160407_042520

20160407_042543
magazeti ya leo alhamis tarehe 7/4/2016
20160407_042559
20160407_042609
20160407_042836
20160407_042859
20160407_042624
20160407_042640
20160407_042650
20160407_042707
20160407_042723
20160407_042735
20160407_042747
20160407_042758
20160407_042913
20160407_042924
20160407_042937
20160407_042948
20160407_043004
20160407_043015
20160407_043043
20160407_043054
20160407_043141
20160407_043152
20160407_043209
20160407_043219
20160407_043235
20160407_043244
20160407_043255
20160407_043303
20160407_043323
20160407_043332
20160407_043343
20160407_043352
20160407_043405
20160407_043415
20160407_043449
20160407_043506
20160407_043606
20160407_043618
Share:

Wednesday, 6 April 2016

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ateketea kwa Moto Akiwa Ndani ya Gari Lake

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mhadhiri  wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Idara ya Sayansi na Uhandisi wa Kompyuta (CoICT), Dk Richard Mgaya amefariki baada ya kuteketea ndani ya gari lake jijini Dar es Salaam juzi.

Gari la Dk Mgaya liliteketea baada ya kugongana na lori katika eneo la Mbezi Africana, Wilaya ya Kinondoni usiku wa kuamkia juzi na kuwaka moto uliosababisha kifo chake.

Juzi picha mbalimbali zilisambaa zikionesha gari aina ya Toyota Prado lililopata ajali eneo hilo la Africana baada ya kugongana na lori, baadaye ilibainika kuwa aliyekuwa katika gari hilo ni Dk Mgaya.

Akizungumza  kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Christopher Fuime alisema gari la Dk Mgaya liliteketea na hata kushindwa kujulikana dereva wa gari hilo.

Alisema baadaye ndugu wa marehemu ndio walithibitisha kuwa gari hilo lililoteketea na dereva aliyekuwemo ni Dk Mgaya ambaye hata hivyo naye aliteketea ndani ya gari hilo.

“Lile gari liliungua na hakuna kitu kilichopatikana, hata wakati polisi wanafika eneo la tukio walikuta tayari dereva amekuwa majivu kutokana na kuteketea kwa moto… labda baada ya kupima vinasaba ndio itathibitika kama ilikuwa ni yeye,” alisema Kamanda Fuime.

Alisema hata gari hilo hawakuweza kulitambua mara moja na baada ya kufuatilia Mamlaka ya Mapato (TRA) ilibainika kuwa mmiliki wake ni Dk Mgaya.

Alisema “ndugu wa marehemu ndio wamesema kuwa ni ndugu yao.” 
Dk Mgaya alijiunga na idara hiyo miaka kadhaa iliyopita akitokea masomoni nchini Marekani na alikuwa ni mtaalamu wa artificial intelligence.
Share:

MECHI ZA LEO JUMATANO UEFA TAREHE 6.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
UEFA LEO TAREHR 6.4.2016
Share:

MATOKEO MECHI ZA UEFA JANA TAREHE 5.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Ezekiah Wenje Afunga ushahidi akiwa Shahidi pekee ......Ni baada ya Mahakama Kuu kukataa ombi la kutumia fomu alizotaka kuzitumia

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Upande wa madai katika kesi ya kupinga matokeo ya ubunge wa Nyamagana jana ulifunga ushahidi baada ya Mahakama Kuu kukataa ombi la kutumia fomu namba 21B kwa ajili ya mashahidi wengine.

Baada ya kufunga ushahidi katika kesi hiyo namba 5/2015, mbunge wa zamani wa jimbo hilo (Chadema), Ezekiah Wenje dhidi ya Stanslaus Mabula (CCM), upande wa utetezi leo unatarajiwa kuwasilisha hoja iwapo nao unafunga ushahidi au utaita mashahidi mahakamani.

Hatua hiyo imekuja jana baada ya Jaji Kakusilo Sambo kukubaliana na pingamizi lililowekwa na upande wa wajibu maombi wakipinga mleta maombi kutumia fomu hizo katika ushahidi wake. 
Katika pingamizi la mawakili wa utetezi, Vicent Tangoh anayemuwakilisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Constantine Mutalemwa anayemuwakilisha Mabula, walidai mdai hakutoa fomu hizo kwa utetezi ili kuzihakiki kwa muda mwafaka kama alivyoagizwa na Mahakama, hivyo hazistahili kutumika mahakamani.

Upande wa utetezi ulidai licha ya kutowasilisha fomu hizo kwa muda mwafaka, pia mlalamikaji aliziwasilisha kwa kutumia vifungu tofauti bila kuieleza Mahakama sababu za msingi za kutaka aruhusiwe kuzitumia kama kielelezo.

“Fomu hizi ndizo kiini cha maombi haya na mdai alipewa siku 10 kuzikabidhi kwa upande wa utetezi ili kuzihakiki na kuandaa hoja za majibu, hakufanya hivyo na kushindwa kutoa sababu za msingi za kutofanya hivyo,” alidai wakili Tangoh.

Baada ya Mahakama kukubaliana na pingamizi hilo, wakili wa Wenje, Deya Outa aliomba kufunga ushahidi kwani hawataweza kuita shahidi mwingine kutokana na ushahidi wao wote kutegemea fomu zilizokataliwa.

Jaji Sambo alikubaliana na ombi hilo baada ya upande wa utetezi kutokuwa na pingamizi na kuahirisha kesi hiyo hadi leo mawakili hao wa utetezi watakapowasilisha hoja zao, iwapo wanafunga ushahidi au kuita mashahidi kupinga ushahidi wa Wenje ambaye ni shahidi pekee wa upande wa mlalamikaji
Share:

MWENYEKITI WA CHADEMA MKOANI IRINGA AFARIKI KWA AJALI YA GARI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mwenyekiti Wa Chadema Mkoa Wa Iringa Afariki Kwa Ajali


Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Iringa Vijijini  Ndg.Sinkala Mwenda amepata ajali jana  jioni  eneo la Tanangozi na kukimbizwa Hospitalini kwa ajili ya matibabu lakini bahati mbaya akafariki dunia muda mfupi wakati madaktari wakijitahidi kuokoa uhai wake. Pumzika kwa amani Kamanda Sinkara.!

 

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRIL TAREHE 6.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRIL 06, 2016





Share:

Tuesday, 5 April 2016

MECHI ZA LEO JUMANNE UEFA TAREHE 5.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
UEFA TAR 5.4.3016
Share:

Watu wawili wafariki kwa kuangukiwa na Kifusi Geita

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Watu wawili wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa vibaya huku mama mmoja Felista Mganga (65) akivunjika miguu yote baada ya kuangukiwa na kifusi wakati wakichimba mawe yanayodaiwa kuwa na dhahabu.

Tukio hilo limetokea juzi katika kijiji cha Busaka tarafa ya Nyamilembe Wilayani Chato Mkoani Geita wakati watu hao walipokuwa ndani ya mashimo hayo.

Wakizungumza na Channel Ten katika eneo hilo likiwa limefungwa kwa ajili ya usalama huku walinzi wakiwa wanalinda, baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wanaeleza jinsi hali ilivyokuwa.

Pamoja na ajali hiyo,wachimbaji hao wamepaza sauti zao na kuiomba Serikal kuwapatia maeneo salama zaidi ya kuchimba dhahabu kama ilivyoahidi wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka jana.

Kaimu Afisa Madini Mkoa wa Geita Fabiani Mshai amesema wachimbaji hao walivamia eneo hilo baada ya kuvumbuliwa na mchoma mkaa kuhu jeshi la Polisi Mkoa wa Geita likithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Mwezi uliopita kijijini Mgusu Wilayani Geita watu wanane walifukiwa na kifusi huku watano wakipoteza maisha. 
Share:

VIDEO: Wezi wa Laptop kwenye magari wanalostisha sana… tazama walichowafanyia kina Master J kwa Sugu

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Rais Magufuli aombwa kuwa makini na uteuzi wa wakuu wa wilaya

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Watanzania wamemwomba Rais Magufuli kufanya mabadiliko katika Halmashauri za wilaya,manispaa na majiji nchini yakiwemo ya watendaji wake kwa madai kwamba zimejaa ufisadi wa kutisha pengine kuzidi ule wa bandarini.

Dereva taksi mjini Singida,Saad Mhando Mangala,amesema wakati huu Rais Dk.Magufuli akiwa kwenye maandalizi ya kuteua wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmshauri kwa nafasi za ukurugenzi auangalie kwa jicho la kipekee.

Akifafanua,alisema kwenye halmashauri hakuhitaji mtu awe na elimu kubwa ndipo aweze kuwa kiongozi, anatakiwa atambue jinsi rasimali za umma zikiwemo fedha zinavyotumika kinyume na makusudio yake.

“Watendaji katika halmashauri kuanzia mhudumu hadi mkurugenzi wapo vizuri ……wanamiliki mali mbalimbali zilizo nje ya uwezo wa mishahara yao, wakusanya mapato wana vitabu vya stakabadhi mbali mbali,kimoja cha halmashauri na kingine cha kwao na wakubwa wao waliowakabidhi stakabadhi hizo,” alisema.

Akifafanua zaidi, Mangala alisema kwa vile serikali ya awamu ya tano inahitaji watumishi waadilifu,waaminifu na wachapa kazi na upo umuhimu mkubwa safu ya watendaji kuanzia ukurugenzi ikafumuliwa au kufanyiwa mabadiliko makubwa.

“Kwenye halmashauri ambazo ndizo zipo karibu zaidi na wananchi wanatakiwa watendaji kuanzia nafasi ya ukurugenzi na kushuka chini, wawe ni watu watakaoendana na kasi ya utendaji ya Rais Magufuli usio na mzaha na wazembe na wabadhirifu wa mali za umma,” alisema dereva taksi huyo.

Aidha, Mangala alitumia fursa hiyo kumpongeza rais Magufuli kwa uteuzi wake makini wa kuteua wakuu wa mikoa na amemwomba aendeleze utamaduni wake huo wa kuchagua watu wenye elimu stahiki na wawajibikaji katika nafasi ya ukuu wa wilaya.

“Binafsi nisingependa urafiki, ushikaji au sura ya mtu apewe nafasi katia uteuzi wa wakuu wa wilaya. Achanguliwe mkuu wa wilaya mwenye elimu safi na ambaye atamudu kwenda na kasi ya rais wetu Magufuli,” alisema.

Kwa upande wake mkazi wa mjini hapa, Avi Mohammed, alisema wakuu wa wilaya waliopo ambao wameacha kuwatumikia wananchi wakisubiri uteuzi upite wao watumbuliwe na waonyeshwe mlango wa kutokea.

Avi alisema wakuu wa wilaya waliopo madarakani hivi sasa, wanalipwa mishahara kwa kazi ya kuwatumikia wananchi, hivyo kama wameacha kutekeleza majukumu yao ipasavyo watakuwa wanakwenda kinyume na mikataba yao ya kazi.

“Natarajia kuona uteuzi unazingatia watu wenye uwezo wa kukemea na kuwawajibisha watendaji wa chini yao wanao waonea wananchi. Pia wenye kutambua kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu kwa wakati. Wasiteuliwe watu wenye harufu ya rushwa na wavivu,” alisema.

Na Nathaniel Limu, Singida



Mkazi wa mji wa Singida, Avi Mohammed, amemshauri Rais Magufuli, asiwateue wakuu wa wilaya ambao kwa sasa hawatekelezi majukumu yao wakisubiri uteuzi.(Picha na Nathaniel Limu)



Dereva taksi mjini Singida, Saad Mhando Mangala, amshauri Rais Dk.Magufuli. 
Share:

Mbunge wa Moshi Mjini akutwa na mazito, namba yake yatumika kutapeli

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY



Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini Jafary Michael (Chadema) anatoa tahadhari kwa umma ya kuwa kuna baadhi ya watu wenye nia mbaya wanatumia namba yake ya simu ya mkononi ya mtandao wa Vodacom kufanya utapeli.
Watu hao wamekuwa wakituma ujumbe mfupi (SMS) kwa watu mbalimbali kwa lengo la kutapeli wakiomba kutumiwa fedha.

Wakati akishughulikia suala hilo katika vyombo vya dola ametoa ombi kwa yeyote atakayepata ujumbe huo kuupuza na kutoa taarifa kwa yeyote atakaye fikwa na kadhia hiyo.
Ukipata ujumbe huu mfahamishe na mwenzako.
Imetolewa na :
Japhary Michael
Mbunge wa Moshi mjini
Share:

Kuungua kwa Shule ya Iyunga Wanafunzi kidato cha sita waathirika

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Wanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya Sekondari ya Ufundi Iyunga Mkoani Mbeya wamesema kuungua moto kwa shule hiyo, kumewaathiri kimasomo baada ya shule kufungwa, ambapo baadhi yao walilazimika kupanga vyumba na kuishi maisha ya geto ili waendelee kujisomea.

Wakizungumza na Channel Ten wanafunzi hao, ambao wanataraji kuanza mtihani wao wa mwisho mwanzoni wa mwezi Mei, wanasema walishindwa kurudi nyumbani kwao kutokana na umbali na gharama za nauli kuwa kubwa, lakini pia wakawashukuru wadau waliojitokeza kuchangia shule hiyo na kwamba kwa sasa imekuwa kwenye hali nzuri tofauti na awali kabla ya kuungua moto.

Aidha, Afisa elimu Sekondari Lidya Halbert anasema uongozi wa shule umejipanga ambapo wanafunzi wa kidato cha sita baada ya masomo ya kawaida, watasoma masomo ya jioni ili kuziba pengo la siku ambazo hawakuwepo shuleni.

Hata hivyo wadau mbalimbali wameendelea kujitokeza kuisaidia shule hiyo, ambapo Benki ya Axcess tawi la Mbeya imetoa msaada wa mifuko 56 ya sement.

Shule hiyo ambayo iliungua moto mara mbili katika kipindi cha juma moja pia ina uhitaji wa vitanda 250, hivyo kuomba wadau mbalimbali kujitokeza kuisaidia shule hiyo. 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger