Tuesday, 23 February 2016

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Akana Kutoa Amri ya Kufuta Matokeo ya Uchaguzi Zanzibar

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Taifa na Rais Mstaafu Dokta Jakaya Kikwete amewataka watanzania kupuuzia uvumi unaoenezwa kuwa yeye ndiye aliyetoa amri ya kufuta matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar.

Amesema Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ina mamlaka kamili na hakuna mtu ambaye anaweza kuiingilia
Share:

video:download jambo squad -digidigi

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

BASI LA NATA RAHA LAPATA AJALI BUNDA LEO ASUBUHI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Watu wanne wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa wajeruhiwa leo asubuhi baada ya basi la Nata Raha toka Serengeti kuacha njia na kugonga nguzo eneo la Kwa Sabato, Bunda. Mganga Mkuu Nicholas Machochota athibitisha kutokea kwa vifo hivyo, pia majeruhi wamepelekwa katika hospitali ya Bungando kwa matibabu zaidi.

ENDELEA KUTUFUATILIA KWA TAARIFA ZAIDI

CHANZO: ITV TANZANIA
Share:

Lipumba Amtaka Rais Magufuli Atangaze Mshahara Na Marupurupu Yake

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amemtaka Rais John Magufuli atangaze mshahara na marupurupu yake, kwa kuwa amejivisha joho la kuwa Rais wa wanyonge.

Profesa Lipumba amelieleza gazeti la Mwananchi kuwa Rais Magufuli amejipambanua kuwa kiongozi anayeguswa na matatizo ya wanyonge, hapendi makuu, anahimiza ukusanyaji wa mapato ya Serikali na matumizi mazuri ya fedha za umma, lakini watanzania hawajui mshahara wake ni kiasi gani

Profesa huyo aliyejikita katika masuala ya uchumi, alirejea mijadala mbalimbali iliyowahi kuibuliwa kuhusu mshahara wa Rais, ikiwamo ule uliyowahi kuibuliwa mwaka 2013 na Zitto Kabwe, wakati huo akiwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema kuwa Rais analipwa Sh32 milioni kwa mwezi.

Pia alirejea taarifa iliyochapishwa na Mwananchi, Julai 27, 2015, iliyoandikwa kutoka katika mtandao wa African Review kuwa Rais mstaafu Jakaya Kikwete ni wa nne miongoni mwa marais wa Afrika kwa kupata mshahara mkubwa wa dola za Marekani 192,000 kwa mwaka sawa na dola 16,000 kwa mwezi, ambayo ni sawa na Sh32 milioni kwa mwezi. Hadi jana jioni, dola moja ya Marekani ilikuwa sawa na Sh2,187.

“Taarifa ya Ikulu ilikanusha vikali habari zilizochapishwa na Mwananchi. Ikulu ilieleza kuwa habari hizo siyo za kweli. Hata hivyo, haikueleza mshahara wa Rais na marupurupu yake ni kiasi gani?

Pia, katika mjadala wa mshahara wa Rais, Naibu Spika wa Bunge lililopita ambaye ndiye Spika wa sasa, Job Ndugai alinukuliwa akieleza kuwa mshahara wa mtu ni siri yake.

Waziri wa Nchi Katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya utumishi wa Umma wa wakati huo, Celina Kombani (kwa sasa ni marehemu) alisema kuwa ni kosa kutangaza mshahara wa Rais.

“…Kwa hivi sasa Rais Magufuli atangaze mshahara na marupurupu yake na kama mapato yake ni Sh32 milioni kwa mwezi, basi ajitolee alau nusu ya mapato hayo kuchangia elimu na afya ya wanyonge. Hatua hii itaimarisha taswira inayojengeka barani Afrika kuwa yeye ni Rais wa wanyonge,” amesema  Lipumba.

Wakati akizungumza na wazee wa Dar es Salaam wiki iliyopita, Rais Magufuli aliwataka mawaziri, naibu mawaziri na makatibu wakuu wachangie Sh1 milioni katika mishahara yao kuchangia elimu.

Pia Rais alieleza kuwa yeye mwenyewe, makamu wake na waziri mkuu watachangia Sh6 milioni kila mmoja, ili zifike Sh100 milioni kusaidia changamoto za elimu bure Mkoa wa Dar es Salaam.

Kutokana na tangazo hilo, Profesa Lipumba alisema, “Ikiwa Sh6 milioni zitakatwa katika mshahara wake wa mwezi mmoja ni wazi mshahara wake na ule wa makamu wake na waziri mkuu ni zaidi ya Sh6 milioni kwa mwezi.

“Mishahara na marupurupu ya viongozi wa Tanzania hayako wazi. Watanzania hawajui kila mwezi Rais, Makamu wa Rais na viongozi wakuu wa Serikali wanalipwa kiasi gani? Malipo ya wabunge pia hayako wazi?” alihoji.

Profesa Lipumba ambaye amewahi kuwa msaidizi wa Rais katika masuala ya uchumi kati ya mwaka 1991 na 1993, alisema kwa kuwa Rais Magufuli amejivisha joho la kuwa Rais wa wanyonge, anawajibika kuwaeleza Watanzania mshahara na marupurupu yake.

“Ikiwa mshahara ni mkubwa sana achukue hatua za kuupunguza kama alivyofanya Mwalimu Nyerere mwaka 1965.”

Hata hivyo, alisema kifungu cha Katiba cha 43 (2) kinaeleza kuwa mshahara na malipo mengineyo yote ya Rais havitapunguzwa wakati Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba.

Profesa Lipumba alisema Rais Magufuli akitaka kupunguza mshahara wake itabidi kwanza abadilishe kifungu hicho cha Katiba.

“Anaweza kujitolea mchango wa kudumu utakaokatwa kutoka kwenye mshahara wake kusaidia sekta ya afya au elimu,”alisema.

Profesa Lipumba ambaye ni mshauri wa Benki ya Dunia (WB) na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika masuala ya uchumi, alisema ili kuimarisha utawala bora ni muhimu uongozi ulio madarakani utumie mamlaka waliopewa kwa manufaa ya Taifa.

“Mishahara na marupurupu ya viongozi yawe wazi na yaamuliwe na kupangwa na taasisi iliyo huru. Kuweka utaratibu ulio wazi wa kuamua mishahara na marupurupu ya viongozi wa umma wakiwamo Rais na makamu wake, mawaziri, wabunge, majaji, makatibu wakuu na viongozi wengine,”alisema.

Alisema ni muhimu katika ujenzi wa utawala bora, uwajibikaji na uwazi wa viongozi wa umma kwa wananchi wanao waongoza.

“ Inasemekana mshahara wa mbunge katika Bunge lililopita ulikuwa Sh3.4 milioni kila mwezi.Pia mbunge alilipwa Sh8.2 milioni, nyingine kama posho ya jimbo, gharama za ofisi, mafuta, malipo ya wasaidizi wake na dereva.

“Vile Vile, mbunge anapohudhuria kikao cha Bunge alilipwa posho ya Sh80,000 za kujikimu, Sh50,000 za mafuta ya gari na Sh200,00 za kuhudhuria kikao cha Bunge, jumla ni Sh330,000 kwa siku.

“Posho ya siku moja ya mbunge ni zaidi ya mara mbili ya kima cha chini cha mshahara wa Serikali kwa mwezi mzima ambacho ni Sh150,000. Mishahara inakatwa kodi, marupurupu hayakatwi kodi,”alisema.
Share:

TBS Yawataka Wazalisha Nondo Kuanza Kuweka Lebo ( TBS steel bar ID & labelling )

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 
Share:

Serikali Yapanga Bei Elekezi Kwa Hospitali Binafsi

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY



SERIKALI imesema itatoa bei elekezi katika sekta ya afya hivi karibuni baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kubariki bei hizo kuanza kutumika kwa lengo la kuwapunguzia mzigo wa gharama wananchi.

Bei elekezi kwa vituo vya afya zimeshasainiwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na baadhi ya vituo vya afya vimeshaanza kutumia bei hiyo.

Aidha, serikali imepanga kuweka utaratibu wa wagonjwa kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ikiwa ni hatua ya kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali hiyo.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dk Hamis Kigwangalla wakati akizungumza na waaandishi wa habari baada ya kuzindua Matokeo ya Utafiti wa Kutathimini utoaji wa huduma za afya nchini kwa mwaka 2014/2015.

“Bei elekezi ziko mbioni kutoka na baadhi ya vituo wameshaanza kuzitumia kwa sababu zimeshasainiwa na Waziri, sasa hivi tunasubiri Baraka za Waziri Mkuu akiziridhia tutazitangaza rasmi,” alisema Dk Kigwangalla.
Share:

Magufuli Atinga GHAFLA Kivukoni

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY



Rais John Magufuli ameendelea kufanya ziara za kushtukiza, baada ya kutembelea ofisi za Kivukoni Dar es Salaam kimyakimya juzi jioni kuangalia mwenendo wa utoaji huduma za vivuko.

Mashuhuda waliokuwepo eneo hilo Jumapili jioni wakati Rais anafanya ziara hiyo, walieleza mtindo alioingia nao Dk Magufuli ulikuwa ni wa kawaida na vigumu kwa mwananchi wa kawaida kung’amu uwapo wa Rais.

Mfanyabiashara wa eneo hilo, Sharif Mkamba alisema Rais Magufuli aliingia saa 11 jioni akiwa na msafara wa magari matatu ya kawaida yaliyokuwa na namba za kiraia.

“Hakukuwa na king’ora chochote kama tulivyozoea bali ulikuwa ni msafara wa kimya kimya. Aliingia moja kwa moja kwenye zile ofisi na alitumia kati ya dakika 10 hadi 15 kabla ya kutoka,” alisema Mkamba.

Said Likoko alisema kuwa baada ya kugundua kati ya magari matatu alikuwepo Rais, walisogea kufuatilia kwa kina kwa kuwa haijazoeleka na walitegemea huenda baadhi ya watumishi wangewajibishwa.

“Aliteremka na kumuuliza aliyemkusudia na taarifa tulizozipata jana zinadai hakumkuta huyo bosi, sijui ni meneja au ofisa sisi hatujui,” alisema Likoko ambaye hujishughulisha pia na biashara ndogondogo eneo la kivukoni.

Likoko alisema pamoja na kwamba aliingia kimya kimya, Rais Magufuli hakusita kuwasalimia wasafiri waliokuwa wakisubiri kivuko wakati alipofanya ziara hiyo.

Alieleza kuwa kama wananchi walifurahishwa na hatua hiyo ya Rais, kwa kuwa watendaji wengi hawafanyi kazi siku za wikiendi licha ya huduma zake kufanyika siku zote.

Tangu jana asubuhi kumekuwa na video inayosambaa ikimuonyesha Rais Magufuli akiwa Kivukoni akitembea kwa miguu ndani ya eneo hilo huku akishangiliwa na wasafiri waliokuwa wakingoja kivuko.

Hata hivyo, jitihada za kutafuta mamlaka husika kueleza kwa undani malengo ya ziara hiyo ziligonga mwamba baada ya Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue kutopokea simu.

Ofisa habari wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) Theresia Mwami, alitaka utafutwe uongozi wa juu kueleza yaliyojiri kwenye ziara hiyo kwa kuwa yeye yupo likizo.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMANNE FEBRUARY 23 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
                       





Share:

Monday, 22 February 2016

TCRA yatoa ruksa kwa video ya Zigo Remix yake AY kuchezwa usiku tu kwenye television!

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Weka mbali na watoto, video ya Zigo Remix ya AY aliomshirikisha Diamond Platnumz, ruksa kuchezwa usiku kwa mujibu wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania, TCRA.
 
Share:

TCRA Yaifungia Video mpya ya Wimbo ‘Zigo remix’ ya AY ft diamond

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Ambwene Yessaya ‘AY’ amethibitisha kupokea taarifa ya kufungiwa kwa video ya wimbo ‘ Zigo remix’ aliyomshirikisha Diamond Platnumz.

Akizungumza na 225 katika kipindi cha XXL cha Clouds FM, Jumatatu hii, AY amesema alipokea barua yenye amri hiyo kutoka kwa rafiki yake ambae anafanya kazi katika chombo kimoja cha habari.

“Sijaelewa maadili gani kwa sababu kama maadili niliyokosea mimi ni kushoot kwenye swimming pool, na kama kwenye swimmig pool watu nimevalisha jeans au maturubai hapo nitakuwa nimekosa maadili,” alisema AY.

“Mavazi ya kwenye swimming pool yako kila mahali, hata kwenye taarifa za habari (Michezo) wanaonyesha waogeleaji, kama hiyo pia ni kukiuka maadili ni sawa. Inashangaza mamlaka zetu wanafocus kwenye kufungia nyimbo zetu na kuacha video za nje. Sijawahi sikia muziki wa Kenya, Uganda au Marekani umefungiwa, kama wanaona nyimbo za Nicki Minaj zina maadili halafu Zigo ya AY haina maadili baasi unaacha tu iwe hivyo ,” aliongeza AY.
 
Pia AY alisema barua hiyo ilitoka kwa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) ikisema kwamba video hiyo inakiuka maadili.
Kwa mujibu wa Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungi, amethibitisha kuvitumia vituo vya luninga nchini taarifa ya namna ya kupembua kazi za wasanii zisizo na maadili.
Share:

Mpya:Bodi ya Wakurugenzi wa Magazeti ya Serikali,(TSN) Yamsimamisha Kazi Mhariri Mtendaji

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

BODI ya wakurugenzi wa magazeti ya Serikali,(TSN) imemsimashisha kazi Mhariri Mtendaji wa magazeti hayo Bw Gabrieli Nderumaki kupisha uchunguzi kutokana na utendaji usioridhisha ndani ya kampuni hiyo.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bw Prof Moses Warioba amesema hatua za kumsimamisha kazi Mhariri Mtendaji huyo umetokana na kuwepo kwa malalamiko mengi kutoka kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo ambapo nafasi yake itachukuliwa na Naibu Mhariri Bi Tumma Abdalah.

“Kumekuwa na mambo mengi yanayofanyika bila kufuata utaratibu ndani ya kampuni hii ikiwemo wafanyakazi kutoelewana na menejimenti katika kulipwa stahili zao, pamoja na wafanyakazi kupewa majukumu ambayo hawana uwezo wa kuyatekeleza”.Alisema Prof Warioba.

Aidha Prof Warioba ametengua uteuzi wa Bw Felix Mushi aliyekuwa Meneja mauzo na masoko katika kiwanda cha uzalishaji kwa kukosa sifa na utendaji mbovu uliopelekea kampuni kushuka katika uzalishaji.

Hatua hiyo ya kuwawajibisha watendaji hao imetokana na Ziara ya Mhe. Nape Nnauye Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo katika Kampuni hiyo ambapo pia hakuridhiswa na utendaji mbovu uliopelekea wafanyakazi 21 kuacha kazi.

“Nataka Bodi itafakari juu ya malalamiko yaliopo kwa wafanyakazi na wachukue hatua kabla mimi sijakutana na wafanyakazi hao wiki ijayo ili kujua mapungufu yako wapi.”Alisema Mhe Nape.
Hata hivyo Bodi hiyo ya wakurugenzi inaendelea kutafuta namna ya kuboresha utendaji ndani ya kampuni ili iendane na kasi iliyopo katika uzalisahaji wa magazeti kwa kiwango kikubwa.
Share:

VIDEO:DOWNLOAD YAMOTO BAND-MAMA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
https://youtu.be/F9-3gZpK0zQ
Share:

Majipu Yaendelea Kutumbuliwa......Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Asimamishwa Kazi

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

WAZIRI  wa nchi,ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi  wa Umma na Utawala bora,Angella Kairuki amemsimisha kazi mkuu wa chuo cha utumishi wa umma nchini Said Nassoro kutoka na uzembe ulioisababishia serikali  hasara  ya  bilioni 1.
 
Vilevile Waziri Kairuki amewasimamisha  kazi Mkuu wa chuo hicho tawi la Dar es salaam,Joseph  Mbwilo na Silvanus  Ngata ambaye naye ni Mkuu wa chuo hicho tawi la Tabora.
 
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam,Waziri Kairuki amesema amefikia hatua hiyo ya kuwasimamisha kazi watumishi hao baada ya kubaini utendaji usioridhisha katika vyuo hivyo.
 
Amesema Nassoro amemsimisha kazi baada ya kushindwa kuwasimamia watumishi wa chini yake katika  chuo hicho.
 
“Mwaka  2011 hadi  2013 bwana Silvanus Ngata aliongeza gharama za ujenzi wa jengo la chuo hicho tawi la  Mtwara tofauti na fedha iliyokuwa imepangwa.  

"Chakushangaza, huyu Nassoro ambaye ni mkuu wao,  baada ya kugundua kosa hilo alishindwa kumuwajibisha na badala yake aliamua kumhamishia tawi la chuo cha Tabora. Sasa mimi nawasimamisha kazi wote ."Amesema Kairuki
 
Pia waziri Kairuki amesema amemsimamisha Mbwiro kutokana na matumizi mabaya ya fedha za chuo.
 
“Huyu Mbwiro kwa mwaka 2013 alitumia vibaya fedha za ada za wanafunzi  kiasi cha bilioni 1 ,lakini licha ya ubadhilifu huo, Nassoro alimteua bwana Mbwiro kuwa Kaimu mkuu wa chuo kwa upande wa fedha." Alisema Waziri Kairuki.
 
Wakati Waziri Kairuki akitumbua majipu hayo,mmoja wa watendaji hao,Said Nassoro alikuwepo kwenye mkutano huo na wanahabari huku akiwa hajui kinatakachotokea
Share:

Rais Magufuli Kuwatema Wakuu wa Mikoa 20

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Wakati  Rais Dk. John Magufuli akitarajia kutangaza safu ya wakuu wa mikoa  na wilaya wapya, imebainika wapo zaidi ya 20 ambao watatemwa kutokana na sababu mbalimbali za utendaji.

Habari za kuaminika zinasema miongoni mwa  wakuu wa mikoa watakaoachwa wamo walioshindwa kutatua kero sugu zikiwamo za mapigano ya wakulima na migogoro ya ardhi ambayo kila kukicha imesababisha watu kadhaa kufariki dunia.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, pia wamo wakuu wa mikoa  ambao wanaweza kuachwa kutokana na kuwa na umri mkubwa na wanaonyesha wazi hawawezi kwendana na kasi ya utendaji kazi wa serikali ya awamu ya tano ambayo inatumia falsafa ya Hapa Kazi Tu.

Habari hizo zinasema wapo wakuu wa mikoa ambao wameshindwa kutatua migogoro ya ardhi katika maeneo yao kwa zaidi ya miaka 10 hadi 15 na kusababisha vurugu kuibuka kila wakati.Miongoni mwa mikoa iliyokithiri kwa migogoro hiyo ni Morogoro, Tanga na Manyara.

“Wapo wakuu wa mikoa  ambao hawatarudi kutokana na rekodi za matukio, wapo ambao kwenye maeneo yao   migogoro imedumu kwa zaidi ya miaka 10 na kuendelea, sasa viongozi wa aina hii unadhani watabaki kweli kwenye Serikali?

“Nakuhakikisha kule ambako kuna migogoro ya ardhi na mapigano ya kila siku wako hatarini kupoteza kibarua… unajua mheshimiwa kila siku anajiuliza hivi inakuwaje mkoa ambao una kamati za ulinzi na usalama za wilaya zinashindwa kuchukua hatua za kumaliza mapigano haya?

“Inawezekana zinafanya kazi kwa kutegeana au wengine wanakula kwa wafugaji na wakulima.

“Mpaka wiki iliyopita tumedokezwa kwamba ma-RC  20 hawatarudi katika nafasi zao kwa sababu wameshindwa kuonyesha kama wanaweza kuwajibika ipasavyo,” kilisema chanzo cha habari hii.

Chanzo  hicho kilisema pia kuwa wengine ambao wako hatarini kutemwa ni wale wenye umri mkubwa ambao kwa namna moja au nyingine wanapaswa kustaafu.

“Sikutajii ni mikoa gani kwa sababu hawa wanajulikana vizuri…pale kanda ya ziwa, nyanda za juu kusini na mikoa ya kaskazini ni maeneo  ambayo yataguswa mno.

“Unajua Dk. Magufuli na timu yake wanaangalia kwa kina mno  hata mikoa ya kanda ya magharibi nao hawako salama kwa sababu wapo wazee wetu ambao inaonekana wazi umefika wakati wa kupisha kizazi kingine ambacho kitasaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo,”kilisema chanzo chetu.

Kuhusu wakuu wa wilaya, chanzo hicho kilisema hakuna tofauti na wakuu wa mikoa kwa vile kila mmoja atapimwa kutokana na namna alivyoweza kusimamia majukumu ya Serikali tangu alipoteuliwa.

“Jambo moja kubwa ndugu yangu, hapa kila mmoja atapimwa kutokana na uwezo wake… nadhani unakumbua Rais mwenyewe alisema anawachunguza, tutarajie mabadiliko makubwa,” kilisema chanzo chetu.

Hivi karibu Rais Magufuli, alisema wakuu wa mikoa na wilaya wajiandae kuwajibika endapo maeneo wanayoongoza yatakuwa na ukosefu wa chakula na kusababisha wananchi kukumbwa na njaa wakati maeneo mengi ya nchi yamepata mvua ya kutosha.

Mikoa ambayo imekuwa ikikumbwa   na njaa mara kwa mara  ni pamoja na Mara, Iringa, Dodoma,Tanga na Shinyanga.
Share:

Shule ya Sekondari Ilboru sasa Kuchuja Wanafunzi

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Kufuatia kutofanya vizuri kitaifa katika mtihani wa kidato cha nne, shule ya sekondari ya watoto wenye vipaji maalumu, IIboru itaanza kuwachuja wanafunzi wasio na uwezo wanaopangiwa kusoma shuleni hapo.
 
Mkuu wa shule hiyo, Julius Shula amesema licha ya Ilboru kuwa ya kwanza kwa shule za Serikali nchini, lakini imebaini upungufu katika upatikanaji wanafunzi.
 
Amesema kuna wanafunzi kutoka shule za binafsi wanaopangiwa IIboru, wamebainika hawana uwezo, hivyo kutilia shaka alama walizopata katika mitihani yao ya kuhitimu darasa la saba.
 
“Tayari tumewapa mitihani waliongia kidato cha kwanza, huwezi amini kuna wanafunzi wanapata alama 0, lakini ukifuatilia matokeo ya kuja hapa wana wastani wa alama zaidi ya 200 sasa hili ni tatizo kubwa,” alisema. 
Share:

BREAKING NEWS:HAYA HAPA MATOKEO KIDATO CHA NNE 2015

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

BONYEZA HAPO CHINI KUANGALIA
>>>>  <<<<<Matokeo CSEE 2015>>>>>>


PIA TAZAMA MATOKEO YA>>>>>
<<<<<<Matokeo ya QT 2015>>>>

NOTE:UKITAKA KUANGALIZIWA JINA LAKO TAFADHALI TUMAHAPO CHINI KWENYE FACEBOOK COMENT,EXAM NO YAKO NA JINA LA SHULE
maswayetu blog team! 
Share:

Magazeti ya leo jumatatu february 22 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY



'
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger