Monday, 22 February 2016

Vita ya ubunge yahamia kortini

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

MASHAURI 13 ya uchaguzi wa wabunge yanatarajiwa kuanza kunguruma leo katika kanda mbalimbali za Mahakama Kuu ya Tanzania nchini.
Miongoni mwa mashauri yatakayonguruma ni yale yaliyofunguliwa na aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila, aliyekuwa mgombea ubunge Iringa Mjini Fredrick Mwakalebela, aliyekuwa Mbunge wa Kahama James Lembeli, aliyekuwa Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje na aliyekuwa Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu.
Kwa mujibu wa taarifa ya Msajili wa Mahakama Kuu, Ilvin Mugetta wiki iliyopita, mashauri hayo yataanza kusikilizwa kwa njia ya vikao vya Mahakama Kuu katika vituo mbalimbali vya Mahakama hiyo nchini.
Mugetta alizitaja kesi zitakazoanza kusikilizwa kuwa ni kesi ya kupinga matokeo ya ubunge wa Longido yaliyompa ushindi Onesmo ole Nangole (Chadema) iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk Stephen Kiruswa.
Itasikilizwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha. Aidha, alisema kesi nyingine ni ile ya kupinga matokeo ya uchaguzi iliyofunguliwa na Benedicto Mutungirehi (Chadema) dhidi ya mshindi wa ubunge katika Jimbo la Kyerwa, Innocent Bitakwate (CCM). Kesi hiyo itasikilizwa Bukoba.
Mkoani Iringa, pia kutakuwa na kesi iliyofunguliwa na Mwakalebela ya kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyompatia ushindi wa ubunge katika Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema).
Alitaja kesi nyingine kuwa ni ya kupinga matokeo ya ubunge inayomkabili Mbunge wa Njombe, Edward Mwalongo (CCM) iliyofunguliwa na Emmanuel Godfrey (Chadema).
Kesi nyingine ni ile ya kupinga matokeo ya ubunge katika Jimbo la Mafinga, iliyofunguliwa na William Mungai (Chadema) dhidi ya mbunge wa jimbo hilo, Cosato Chumi wa CCM.
Pia kesi iliyofunguliwa na Zella Abraham ya kupinga matokeo ya ubunge Mbeya Vijijini dhidi ya Oran Njeza nayo itasikilizwa na kesi nyingine ni iliyofunguliwa na Fanuel Mkisi dhidi ya ushindi wa ubunge katika Jimbo la Vwawa wa Japhet Hasunga. Kesi hizi zitasikilizwa Mbeya.
Aidha, kesi nyingine zitakazoanza kusikilizwa siku hiyo ni pamoja na kesi dhidi ya Mbunge wa Newala, George Mkuchika iliyofunguliwa na Juma Manguya anayepinga ushindi wa mbunge huyo na kesi iliyofunguliwa na Mangungu dhidi ya ushindi wa matokeo ya ubunge Kilwa yaliyompatia ushindi Vedastor Ngombale wa CUF.
Pia Msajili huyo alisema kesi nyingine ni ile iliyofunguliwa na Wenje ya kupinga matokeo yaliyompatia ushindi Stanslaus Mabula (CCM) itakayosikilizwa Mwanza wakati kesi iliyofunguliwa na Lembeli ya kupinga matokeo ya ubunge Kahama yaliyompatia ushindi Jumanne Kishimba itasikilizwa Shinyanga.
Kesi nyingine zilizopangwa kusikilizwa ni iliyofunguliwa na Kafulila kupinga matokeo ya ubunge Kigoma Kusini yaliyompatia ushindi Husna Mwilima wa CCM na kesi yao itasikilizwa Tabora wakati kesi iliyofunguliwa na Amina Mwidau kupinga matokeo ya ubunge Pangani yaliyompatia ushindi Jumaa Aweso wa CCM itasikilizwa Tanga.
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo mbali na washindi wa ubunge ni pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Msimamizi wa Uchaguzi katika Jimbo husika.
Hivi karibuni, Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman alisema tayari Mahakama hiyo imejipanga kumaliza kesi zote za uchaguzi hadi Juni mwaka huu, na imejipanga kusikiliza kesi 20 za wabunge.
Tangu uchaguzi huo umalizike Oktoba mwaka jana, jumla ya kesi 221 zilifunguliwa kati ya hizo 53 ni za ubunge na 173 madiwani na jumla ya Sh bilioni tatu zinahitajika kukamilisha usikilizaji wake.
Share:

Nape: Maslahi tasnia ya habari kulindwa

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amesema Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha maslahi ya wanahabari na tasnia ya habari nchini vinalindwa na kupewa uhuru wa kutosha lakini kwa kutanguliza maslahi ya taifa.
Pia amebainisha kuwa Muswada wa Sheria ya Kusimamia Vyombo vya Habari uko katika hatua za mwisho baada ya kushirikisha na kujumuisha mapendekezo ya wadau wa habari na kusisitiza kuwa endapo sheria hiyo itapitishwa itakuwa ni sheria bora itakayoijenga tasnia hiyo na itadumu kwa muda mrefu.
Amevitaka vyombo vya habari nchini kutumia fursa iliyopo kuibua matatizo yaliyopo kwenye jamii na hivyo Serikali kuvitumia kama sehemu ya kupatia taarifa na kuzifanyia kazi kwa maslahi ya Watanzania na Taifa kwa ujumla.
Nape aliyasema hayo juzi usiku katika kipindi cha Siku 100 za Rais John Magufuli madarakani katika sekta ya habari, utamaduni, sanaa na michezo kilichorushwa na televisheni ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).
Alisema tangu Rais John Magufuli aingie madarakani amekuwa akiishi yale anayoyazungumza na hivyo ndivyo Serikali yake itakavyokuwa kwani hata yeye tangu alipoteuliwa kuwa Waziri wa Habari aliahidi kuijenga na kuilinda tasnia hiyo jambo ambalo ameapa kulifanikisha.
“Nawahakikishia wanahabari kwamba wako salama chini ya Serikali ya Awamu ya Tano na uongozi wake,” alisisitiza.
Alisema alipoanza kazi ya uwaziri, alikutana na makundi mbalimbali ya wadau wa habari wakiwemo wanahabari na wahariri wa habari lengo likiwa ni kukusanya na kuangalia mambo ambayo hayako sawa katika tasnia hiyo na kupokea maoni yao yaingizwe kwenye Muswada wa Sheria ya Habari.
Alisema kupitia maoni aliyoyakusanya kutoka katika makundi hayo ya wadau wa habari, mapendekezo yao yamefanyiwa kazi kwa kutumika kwenye muswada wa sheria hiyo ya habari ambayo iko katika hatua za mwisho na inatarajiwa kuwasilishwa bungeni.
Alisema sheria hiyo ya habari kwa kuzingatia mapendekezo hayo, itakuwa ni sheria nzuri, bora na itakayoijenga tasnia ya habari, na ni sheria itakayochukua muda mrefu kufanyiwa marekebisho kutokana na ubora wake.
Akizungumzia uhuru wa vyombo vya habari, alisema uhuru huo ulianza kupanuliwa tangu Serikali zilizopita ikiwemo ya Awamu ya Nne na umekuwa ukitekelezwa kwa kuzingatia sheria zilizopo za habari na maslahi ya taifa.
Alisema ndani ya Serikali ya Awamu ya Nne, uhuru wa vyombo vya habari nchini ulipanuliwa kwa wigo mkubwa ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika.
“Najua kumekuwa na malalamiko mengi hasa ndani ya siku hizi 100 za Mheshimiwa Rais, pale nilipolifungia gazeti la Mawio. Nilichukua hatua ile baada ya kupitia kwa umakini mwenendo mzima wa gazeti lile na kwa kweli lilikuwa na makosa na ndio maana hata baada ya hatua kuchukuliwa, Mawio wenyewe hawapigi kelele wanaopiga kelele ni wengine,” alisisitiza.
Alisema gazeti lile mwenendo wake wa uandishi ulikuwa hauendani na maadili ya uandishi wa habari na kukiuka sheria ya vyombo vya habari kupitia taarifa zake mojawapo ikiwemo ya kumtangaza kinyume cha Sheria ya Uchaguzi mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad kuwa ndiye Rais mteule wa Zanzibar.
Aidha, alisema pia alifuatilia mwenendo wa namna gazeti hilo linavyojibu barua za kulionya na kuonekana kama linajibizana na Msajili wa Magazeti na hata lilipoandika habari ya kumtangaza Maalim Seif kuwa Rais wa Zanzibar, majibu yake ya kujieleza yalikuwa ni ya kejeli na kiburi.
“Walipoandikiwa barua ya kujieleza kuhusu habari hiyo yenye uchochezi, walijibu eti wanaishangaa Serikali kwa nini inahoji wao kumtangaza mshindi Zanzibar, na kusisitiza kuwa walipaswa kupongezwa. Huu ni uhaini kutangaza Rais bila kuwa na mamlaka. Huu ni uchochezi na ndio maana tulichukua hatua,” alisema Nape.
Alisema pamoja na kwamba sheria iliyotumika kulifungua gazeti hilo inalalamikiwa akiwemo yeye mwenyewe kutoridhika nayo, ni vyema vyombo vya habari vitakatambua kuwa sheria hiyo bado ipo hadi pale utakapopitishwa Muswada wa Sheria ya Habari.
Alivitaka vyombo vya habari kuitekeleza kwa vitendo changamoto aliyoitoa Rais Magufuli wakati akizungumza na wazee hivi karibuni, kwa kuandika habari za utafiti zinazoibua masuala nyeti yanayohitaji kufanyiwa kazi na Serikali kwa maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.
“Hata mheshimiwa Rais Magufuli alisema tutumie vyombo vya habari kupata taarifa muhimu za kufanyia kazi. Ili Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Dk Magufuli ifanikiwe, ni lazima itoe uhuru wa kutosha kwa vyombo vya habari kufanya kazi zake,” alisema Nape.
Katika hatua nyingine, Nape amesema Serikali imejipanga kuhakikisha Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) linakuwa chombo cha kuaminika na linafanya kazi zake kuendana na kasi ya utendaji wa Serikali hiyo.
Aidha, amesema imepanga kuanza kulipa madeni yote ambayo shirika hilo na Shirika la Magazeti ya Serikali, Tanzania Standard Newspapers (TSN) wachapishaji wa magazeti ya Daily News, SpotiLeo na HabariLeo, inaidai Serikali ili mashirika hayo yajiendeshe kwa ufanisi.
Nape alisema katika kufanikisha azma hiyo tayari akiwa Waziri mwenye dhamana ameunda Bodi mpya ya TBC na Rais Magufuli ameshamteua Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Balozi Herbert Mrango baada ya Bodi iliyopita kumaliza muda wake kwa mujibu wa sheria.
“Tunataka TBC kuwa chombo cha umma kinachoaminika nchini kuanzia kwenye vipindi na taarifa za habari na matukio. Kila Mtanzania anaona kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano. Ni kasi kubwa hata taasisi zilizo chini ya wizara zetu ikiwemo TBC, tunataka ziende na kasi hiyo,” alisisitiza Nape.
Pamoja na hayo, Waziri Nape alisema Serikali inatambua kuwa shirika hilo linakabiliwa na tatizo la uchakavu wa mitambo na kukabiliwa na madeni makubwa ambayo taasisi za Serikali zinadaiwa na kuahidi kulifanyia kazi.
“Tayari Rais Magufuli ameagiza madeni yote ambayo TBC inadai taasisi za Serikali yaanze kulipwa pamoja na madeni ambayo Shirika la Magazeti la Serikali (TSN) linazidai taasisi hizo. Mashirika haya yanaidai Serikali fedha nyingi inabidi yalipwe ili yafanye kazi zake kwa ufanisi,” alisisitiza.
Share:

Jecha: Tunamtambua Maalim Seif mgombea

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha

LICHA ya Chama cha Wananchi (CUF) na vyama vingine sita vya siasa kuandika barua ya kueleza kutoshiriki Uchaguzi Mkuu wa marudio uliopangwa kufanyika Machi 20, mwaka huu, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha amesema ofisi yake bado inawatambua wagombea wa vyama hivyo.
“Mgombea Urais wa CUF na wagombea wake wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani, na vyama vingine sita waliandika barua kwa ZEC wakisema hawatashiriki uchaguzi huo. Kwa bahati mbaya, wagombea wote na vyama vyao vya siasa vinavyodai kususia, wameshindwa kufuata taratibu.
“Inaelezwa wazi katika Kifungu cha 31 na 37A na Sura ya 46 na 50 ya Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar, kuhusu taratibu za uteuzi wa wagombea na jinsi gani wagombea wanaweza kujitoa katika uchaguzi. Hakuna hata mgombea mmoja aliyefuata sheria hiyo,” alisema Jecha katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana.
Jecha alisema kulingana na kanuni, ni jukumu la chama cha siasa kuandika kwa ZEC kuhusu kuondoa udhamini wake kwa mgombea. Alisema hata CUF ambayo mgombea wake ni Maalim Seif Shariff Hamad, imeshindwa kufuata kanuni hizo.
“Ni muhimu sana kuelewa na kufuata sheria za uchaguzi. Tumekuwa tukiwasiliana na vyama vyote 14 vya siasa, sambamba na kusambaza vifaa vya uchaguzi kwa wilaya zote kumi na moja kabla ya kuvitawanya baadaye kwenye vituo 1,580 vya kupigia kura,” alisema Jecha.
Alisema wagombea wote 14 wa urais, watu wanaowania Uwakilishi kutoka katika majimbo 54 na wagombea 111 katika ngazi ya Udiwani, bado wanaendelea kutambulika kama wagombea halali kwa uchaguzi wa mwezi ujao.
Jecha amekiri kupokea barua kutoka CUF na vyama vingine sita wakisema hawatashiriki uchaguzi huo, wakati vyama vingine vinane kikiwamo CCM, ACT, ADC CCK AFP, SAU, TLP na ADA-TADEA vimethibitisha kushiriki.
“Tunakamilisha taratibu ili kuwapatia wagombea wote wa urais ulinzi kwa saa 24 hadi wakati matokeo ya uchaguzi yatakapokuwa yametangazwa,” alisema Jecha na kuongeza kuwa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura litawekwa katika sehemu mbalimbali ili wapiga kura waone vituo vyao vya kupigia kura.
Alisema kuwa maandalizi kwa ajili ya marudio ya uchaguzi huo yanaendelea vizuri na tayari uteuzi na kuajiri maofisa wa uchaguzi na wafanyakazi wengine umefanyika na kufuatiwa na mafunzo kuhusu jinsi gani ya kusimamia vizuri uchaguzi.
Alisema mafunzo kwa ajili ya wasimamizi wa uchaguzi (ngazi ya majimbo) yanatarajiwa kuanza leo hadi Februari 28, wakati mafunzo kwa maofisa wa vituo vya kupigia kura yataanza Machi 11 hadi 13, mwaka huu.
Mafunzo kwa ajili ya mawakala wa vyama vya siasa na maofisa wa kusimamia usalama yatafanyika Machi 14 na 15, mwaka huu, kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo wa ZEC.
Mwenyekiti huyo wa ZEC alisema maandalizi ya awali ya kuchapisha karatasi za kura yamekamilika, na mchapaji ambaye hakutaka kumtaja anaendelea na kazi ya kuchapa karatasi hizo ambazo zinatarajiwa kuletwa Zanzibar mapema mwezi ujao.
“Tunawaomba wananchi wajiandae kwa uchaguzi wa marudio na wagombea wote kutoka vyama tofauti vya siasa kufuata kanuni na sheria za uchaguzi,” alisema Jecha.
Uchaguzi huo wa marudio wa Machi 20, mwaka huu utafanyika baada ya ule wa Oktoba 25, mwaka jana, kufutwa kutokana na kasoro mbalimbali zilizoufanya usiwe huru na wa haki. Juhudi za kuwapata wasemaji wa CUF jana hadi tunaenda mitamboni hazikufanikiwa.
Share:

Bandari wazidi kubanwa

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Edwin Ngonyani ameonya na kuahidi kuwachukulia hatua baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) Tanga watakaobainika kuendelea kuhamasisha wananchi waliolipwa fidia kupisha ujenzi wa Bandari ya Mwambani tangu mwaka 2011 wasihame katika eneo hilo.
Ametoa kauli hiyo wakati wa majumuisho ya ziara yake ya siku moja iliyolenga kukagua shughuli za bandari hiyo ambako alitembelea eneo la ujenzi wa bandari mpya ya Mwambani lenye ukubwa wa hekta 174.2 pamoja na mita za kupimia mafuta zilizoko maeneo ya Raskazone na Chumvini.
Naibu Waziri alisema pamoja na serikali kukamilisha malipo ya fidia ya zaidi ya Sh bilioni 2.5 kwa ajili ya TPA kulitwaa eneo hilo kutoka kwa wananchi waliokuwa wakilimiliki awali, amebaini kwamba wapo baadhi ya watumishi wa bandari wanaowashawishi wananchi kutokuondoka katika eneo hilo mpaka sasa ili wadai fidia zaidi.
“Dhamira yetu ya kujenga bandari iko pale pale, ila nasikia uchochezi uko ndani ya wafanyakazi wa hapa bandarini … watu wamelipwa fidia hawajaondoka na wanaowafanya hao wasiondoke wanaowapa matumaini naambiwa ni ninyi wafanyakazi wa bandarini,” alisema Naibu Waziri.
Aliongeza, “Hiyo tabia muiache mara moja ili mtoe fursa kwa serikali pamoja na TPA kutimiza azma yake ya kujenga bandari mpya Mwambani pamoja na reli yake ya kwenda Musoma,” aliongeza Ngonyani.
Alisema serikali itahakikisha ndani ya awamu hii ya tano ya uongozi ujenzi wa Bandari ya Mwambani utatekelezwa na kwamba kazi inayoendelea hivi sasa ni kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Reli ya Tanga hadi Musoma.
“Kwamba kitakachofuata sasa ni kutafuta fedha za kujenga reli kutoka Mwambani hadi Musoma… tukijenga hiyo reli tutakuwa tumefungua biashara ya Bandari ya Mwambani,” alieleza.
Akizungumzia matumizi ya mita za kupimia mafuta wakati wa ushushaji wa mafuta kupitia Bandari ya Tanga ambayo imefungiwa tangu mwaka 2011 mpaka sasa, alitaka TPA kukamilisha haraka marekebisho katika mita hizo zilizoko eneo la Raskazone ili zitumike katika shehena inayotarajiwa kushushwa mapema mwezi ujao.
“Mimi naamini wanaozuia flow meters kutotumika ni sisi…wanaonufaika na hilo ni wafanyabiashara wa mafuta wanaotumia nguvu zao kupitia sisi humu humu ndani,” alisema Naibu Waziri na kuongeza: “Maamuzi mbalimbali ya kipuuzi yamefanyika kama huo uamuzi wa kuzifungia hizo flow meters zisitumike tangu mwaka 2011. Ni uamuzi wa kipuuzi ukiuchunguza kwa makini utabaini sisi wote tunahusika kwa sababu ulipotolewa mwaka huo mpaka sasa hakuna mtumishi yeyote wa bandari aliyethubutu kuupigia kelele.”
Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Tanga, Mussa Mbaruku ameiomba TPA na Mamlaka ya Mapato (TRA) Mkoa wa Tanga kushughulikia tatizo la matumizi ya mita za mafuta ili zisaidie kuongeza mapato mkoani humo.
Share:

Rais Magufuli aombwa kulilinda Shirika la Posta

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Rais Dkt John Magufuli

RAIS John Magufuli ameombwa kulilinda Shirika la Posta kwa kuzilazimisha taasisi, wizara na Idara za Serikali kutumia huduma zinazotolewa na shirika hilo.
Mwenyekiti wa Chama cha Mtandao wa Simu Nchini (TEWUTA), Pius Makuke alisema jana kuwa njia hiyo ndiyo pekee itakayoliokoa shirika hilo lisife.
Alisema kwa sasa taasisi nyingi za Serikali zinatumia mashirika binafsi hata kusafirisha vifurushi na barua na kuomba hatua alizochukua Rais Magufuli za kuzuia sukari kutoka nje ili kulinda viwanda vya ndani, pia atumie mbinu hiyo kuzilazimisha taasisi za Serikali kutumia huduma za Posta ili lipate mtaji wa kutosha liweze kujiendesha kwa faida.
Alisema wanatoa ombi hilo kwa Rais kwani baada ya Shirika la Posta kuanzishwa mwaka 1994, Serikali iliahidi kulipatia mtaji, lakini hata hivyo mtaji huo hadi leo haukupatikana jambo linalofanya lishindwe kujiendesha.
Aliongeza kuwa Serikali ilipoamua kutenganisha Shirika la Posta na Kampuni ya Simu (TTCL) mwaka 1994 baada ya kuvunjwa kwa lililokuwa Shirika la Posta na Simu, Serikali kwa mujibu wa sheria iliyounda Shirika la Posta iliazimia kutoa mtaji ili lijiendeshe vyema kibiashara.
“Hata hivyo kwa masikitiko makubwa toka mwaka huo wa 1994 hadi leo Shirika la Posta halijawezeshwa kimtaji na Serikali ambayo ndio mwenye mali,” alisema Makuke.
Aliongeza kuwa kipimo kizuri cha utendaji kazi hivi sasa ni uwezo wa mtaji na akaongeza kuwa iwapo kuna mtaji ni rahisi kuwatathmini viongozi katika ufanisi wao.
“Ombi letu kwa Serikali yetu tunaomba Shirika la Posta kuwezeshwa mtaji wa kujiendesha katika mwaka huu wa fedha,” alisema mwenyekiti huyo.
Alisema uwezeshaji wa Shirika la Posta kimtaji unaweza usiwe na fedha taslimu ili shirika lifikie malengo tarajiwa, ni lazima Serikali itoe maamuzi mazito na mwongozo kwa taasisi zote za Serikali na Wakala za Serikali kutumia huduma zinazotolewa na shirika hilo kwa ajili ya usafirishaji wa barua, vifurushi na vipeto.
Alisema kwa sasa inasikitisha kuona baadhi ya taasisi za umma zimekuwa zikitumia kampuni binafsi katika kusafirisha vifurushi, barua na vipeto jambo ambalo alisema Tewuta inaamini kuwa halifanyiki kwa maslahi ya Taifa, bali ni kwa maslahi binafsi.
Share:

CHADEMA Waanza Kutimuana Jijini Mbeya

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Mbeya Mjini, John Mwambigija pamoja na wajumbe wa kamati ya utendaji ya wilaya hiyo wamevuliwa uongozi kwa kile kilichodaiwa kuwapo kwa msuguano miongoni mwao.
 
Uamuzi huo ulifikiwa usiku wa kuamkia jana kwenye kikao cha mashauriano kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Zanzibar), Issa Said Mohamed.
 
Mohamed alipoulizwa kuhusu uamuzi huo, aligoma kulizungumzia kwa undani akidai hayo mambo ya ndani ya chama.
 
Hata hivyo, alikiri kusimamia kikao hicho ambacho kilianza saa 2.00 usiku na kumalizika saa 11.00 alfajiri.
 
Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoliki uliopo Maghorofani jijini Mbeya.
 
Taarifa za ndani ya chama zilizopatikana jana asubuhi, zilidai kuwa awali, wajumbe walimuomba makamu mwenyekiti huyo kufika jijini hapa na kuitisha kikao hicho kujadili msuguano uliopo.
 
Mmoja wa wajumbe waliokuwapo kwenye kikao hicho ambaye hakutaka kuandikwa  jina , alisema kuliibuka malumbano makali huku wajumbe wakinyoosheana vidole kwa kutuhumiana.
 
Alisema wajumbe ndiyo wanaoharibu chama na kutengeneza makundi yasiyokuwa na tija.
 
“Ile kamati ya utendaji ya Wilaya iligawanyika kitambo sana, tangu wakati ule wa kuwapata wagombea kupitia viti maalumu, sasa baada ya kuona vile na mpasuko ukizidi kuwa mkubwa, ndiyo kundi moja likamuomba makamu mwenyekiti aje aitishe kikao cha mashauriano cha jimbo.
 
“Sasa kwenye kikao cha usiku ilionekana mpasuko ni mkubwa na hakuna anayeweza kuendesha chama,” alisema mjumbe huyo.
 
Alisema kutokana na malumbano yaliyojitokeza kwenye kujenga hoja baina ya makundi hayo mawili, Mohamed akaamuru kumsimamisha kila mjumbe huku akiwauliza kama wana sababu ya kuendelea kuwapo kwenye nyadhifa zao.
 
Alisema mwisho wa kikao wajumbe hao wakakubaliana kukaa pembeni na kutoa nafasi kufanyika kwa uchunguzi wa kina.
 
Baada ya kamati hiyo kuvuliwa nyadhifa zao, makamu mwenyekti huyo aliamuru ofisi ya chama hicho wilaya iongozwe na madiwani kwa muda wakisaidiwa na uongozi wa chama Mkoa wa Mbeya.
 
Akiendelea kuzungumzia uamuzi huo wa chama Mohamed alisema: 
 
“Kilikuwa kikao cha ndani ya chama ambacho ni siri yetu, hivyo siwezi kukwambia kilichojadiliwa wala hatua zilizochukuliwa. 
 
“Uamuzi wote wa ndani unaamriwa na kumalizwa ndani ya vikao vya kamati ya utendaji, kwa hiyo subiri hadi kamati kuu itakapoamua kuzungumza nje.” 
 
Hata hivyo, Mwambigija alikiri kuondolewa kwa kamati nzima huku akisema chanzo ni makundi yaliyojitokeza kwenye harakati za kumpa mgombea umeya wa Mbeya mjini ndani ya chama hicho.
 
“Nilichokiona, ni kwamba eti nilikuwa upande wa meya aliyepita (Mchungaji David Mwashilindi) hivyo kundi lile ambalo lilishindwa ndiyo limetengeneza zengwe,” alisema Mwambigija.
Share:

Sunday, 21 February 2016

WAGOMBEA SABA WA URAIS ZANZIBAR WAKABIDHIWA WALINZI ,TUME YASEMA WAPO KIHALALI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Jecha
Wagombea saba wa nafasi ya urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa marudio wa Machi 20 wamekabidhiwa walinzi binafsi kutoka Jeshi la Polisi, imeelezwa.

Mgombea wa nane, Rais Ali Mohamed Shein ataendelea na ulinzi wake kutokana na wadhifa alionao.

Wagombea urais waliokabidhiwa walinzi ni Khamis Iddi Lila wa (ACT-Wazalendo), Juma Ali Khatib (TADEA), Soud Said Soud (AFP), Hamad Rashid Mohamed(ADC), Issa Mohamed Zonga(SAU), Hafidh Hassan Suleiman (TLP) na Ali Khatib Ali (CCK).

Taarifa hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Salum Khasim Ali alipokuwa akitoa mwongozo wa Tume katika Kikao cha Viongozi wa Vyama na wagombea.

Alipoulizwa kuhusu mgombea wa chama chake kupewa ulinzi wakati walishatangaza kutokugombea kwenye uchaguzi huo, Mwenyekiti wa CCK, Constantine Akitanda, alisema hawatambui suala hilo.

“Kwa nini serikali itoe ulinzi wakati viongozi wa chama hatuna taarifa, ikuna kamati inashughulikia suala hilo na imeshakamilisha kazi ila sijapitia maelezo yao, nipo msibani,” alisema.

Wagombea ambao hawakuhudhuria katika Kikao hicho ni Mohamed Masoud Rashid wa CHAUMA, Seif Ali Iddi (NRA), Kassim Bakar Ali (Jahazi asilia), Abdalla Kombo Khamis (DP), Tabu Mussa Juma (D-Makini) na Maalim Seif Sharif Hamad (CUF) ambao wametangaza kujitoa katika uchaguzi huo.

Vyama sita hivyo vinapinga kufanyika uchaguzi wa marudio kwa madai kuwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka jana ulikuwa huru na wa haki.

Vyam hivyo vinanukuu ripoti za waangalizi wa uchaguzi wa ndani na je waliokuwepo visiwani hapa mwaka jana kushuhudia Uchaguzi Mkuu huo.

ZEC imesisitiza uchaguzi wa marudio utafanyka bila ya wagombea kufanya kampeni katika visiwa vya Ungunja na Pemba.

Licha ya vyama vingi kutangaza kujitoa katika uchaguzi huo, ZEC imesema karatasi za kupigia kura zitakuwa kama zilizotumika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.

Mgombea urais wa Jahazi Aslia, Ali alisema chama chake hakipo tayari kupokea matokeo yoyote kama tume imegoma kuondoa majina yao katika karatasi za kupigia kura.

Alisema hata kama ZEC watatangaza matokeo watakuwa wanafanya kazi ya kujifurahisha kwa sababu hawatoyatambua matokeo yake.

Alisema kuwa ni jambo la kusikitisha ZEC kuendelea kung'ang'ania wagombea walioamua kujiondoa katika uchaguzi wa marudio wakati kushiriki au kutoshiriki ni hiyari ya mgombea.

Naye Mkurugenzi wa Mawasiliano wa CUF, Hamad Masoud Hamad alisema ZEC lazima itambue uteuzi wa Septemba 6 mwaka jana wa wagombea, na kiapo walichokula mahakamani ilihusu Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 na si uchaguzi wa marudio wa Machi 20.

Hamad alisema wananchi na dunia inatambua kuwa CUF imejitoa katika uchaguzi wa marudio na hawatokuwa tayari kupokea matokeo yoyote ya uchaguzi huo.

Alisema ZEC inatakiwa kuheshimu maamuzi waliofanya wananchi Oktoba 25 mwaka jana na kukamilisha kufanya majumuhisho katika majibo 23 yaliyokuwa yamebakia kati ya 54 na kumtangaza mshindi wa urais katika uchaguzi huo.

Mgombea wa CUF, Hamad na wawakilisihi wa chama hicho walikuwa wakiongoza wakati ZEC ilipotangaza kufuta matokeo hayo ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka jana ambao pia ulitumika kuchagua Rais wa Jamhuri na Wabunge.

Alisema kuwa katiba ya Zanzibar hairuhusu kufanyika uchaguzi mara mbili ndani ya miaka mitano na hakuna kifungu cha katiba au sheria kinachompa uwezo mwenyekiti wa tume kufuta matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar.
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO BATCH YA 15 SUA 2015/16

Share:

Nay Wa Mitego anusurika kutekwa

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Msanii wa Nay wa Mitego ambaye kwa sasa yupo kwenye seke seke baada ya kuachia wimbo wake wa shika adabu yako ambao amewa diss watu wengi maarufu, siku kadhaa zilizopita alinusurika kutekwa na watu wasiojulikana.

Nay amekiambia kituo kimoja cha redio kuwa kuna siku alikuwa anatoka studio akaona gari limekuja kupaki nyuma ya gari lake,alipoanza kutoka gari hilo likaanza kumfuatilia kwa nyuma kila ndipo hapo alipoanza kutia mashaka.

Nay amesema kuwa alipata mashaka zaidi baada ya kuona kuwa gari hilo linazidi kumfuata hata baada ya kujaribu kubadilisha uelekeo aliokua kuwa akienda ndipo alipoamua kuwapigia marafiki zake ili waje kumsaidia.

Nay anasema baada ya kuzunguka sana ili kuwakwepa watu hao mwishowe alifanikiwa kufika manzese usiku sana kwa masela wake na kukuta amepishana nao kwa vile walikwenda kumfuata,akibidi awapige warudi haraka na ndipo hapo ilikuwa ponea yake.

Nay amesema anahisi vugu vugu la wimbo wake wa shika adabu yako linaweza likwa ndio chanzo na pia amesema anafanya mipango ya kujilinda zaidi.
Share:

Shilole Amkana Nedy Music, Asema Sio Mpenzi wake...Agoma Kumzungumzia Demu Mpya wa Nuh

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mwanadada anayetamba kwenye muziki wa bongo fleva na bongo muvi,Shilole amekana kutoka kimapenzi na msanii anayechipukia kwenye bongo fleva,Nedy Music.

Akihojiwa na redio moja Shilole amesema kuwa msanii huyo ni mshikaji wake tu hakuna kinachoendelea baina yao na kukanusha kuwa msanii huyo anaishi nyumbani kwake.

“Nedy music ni mshikaji wangu..anakaa kwake mimi nakaa kwangu.Mimi ni mwanamke mtafutaji kwa hiyo mambo ya mapenzi siyaweki saana,nafocus kwenye kazi” alifunguka Shilole.

Alipoulizwa kuwa inasemekana mpenzi wake wa zamani Nuh Mziwanda ameopoa demu mkali kuliko yeye,Shilole alikataa kata kata kuzungumzia hilo na kusema hana muda wa kumwongelea mtu.
Share:

MASWAYETU BLOG TEAM INAWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA UDSM NA MZUMBE UNIVERSITY

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Habari yenu;
Uongozi mzima wa Maswayetu Blog unapenda kuwatakiwa mtihani mwema wanafunzi wote mnaotarajia  kuanza mitihani yenu mapema hapo kesho.
Tunawaombea kwa mwenyezi Mungu awalinde na kuwaongoza mkapate kujibu mliyoulizwa na walimu wenu.
Mungu awabariki na awasaidie mpate kufaulu.
Share:

Download | Mash J - Nakopesha [Audio]

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Download | Mash J - Nakopesha [Audio]

https://my.notjustok.com/track/download/id/70483
- See more at: http://www.johventuretz.com/2016/02/mash-j-nakopesha.html#sthash.kVbiLtPh.dpuf

https://my.notjustok.com/track/download/id/70483
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger