Wednesday, 17 February 2016

WAKURUGENZI WANNE WA HALMASHAURI MKOANI KAGERA,MTWARA,GEITA NA TUNDUMA WASIMAMISHWA KAZI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

WAZIRI nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mtaa,George Simbachawane amewasimamisha kazi wakurugenzi wa nne  kwa  tuhuma  za  kuwahonga wakaguzi wa fedha  kutoka katika ofisi ya Mkaguzi mkuu wa  Hesabu za  serikali (CAG) ili wapewe hati  safi huku Halmashauri hizi zikiwa na ufisadi .
Wakurugenzi  waliosimamishwa  kazi  ni   Elizabeth Chitundu wa Halmashauri za Misenyi mkaoni Kagera, Ally Kisengi wa Halmashauri ya Nanyumbu mkaoni Mtwara  na  Abdalla Mfaume wa Halmashauri ya Mbogwe mkoani Geita.
 
Pia,Waziri Simbachawene   amemsimamisha kazi  mkurugenzi Halmashauri ya  Tunduma Mkoani  Mbeya Bi Halima Ajali  ili kupisha uchunguzi kutokana matumizi mabaya ya madaraka ikiwa ni pamoja na kuwatumia watoto wake katika shuguli za halmashauri na kuwalipa posho na kusababisha upotevu wa mapato.
 
Aidha, Waziri Simbachawane pia ameziagiza mamlaka husika kuwasimisha kazi watendaji wa ofisi ya mkaguzi wa Hesabu za Serikali nchini,CAG  waliohusika kupokea rushwa kutoka kwa wakurugenzi hao ili watoe  hati safi kwenye Halmashauri hizo huku zikiwa na ubadilifu wa fedha za Umma.
 
Akizungumza na waandishi wa habari leo mchana Jijini Dar es Salaam,Waziri Simbachawene amesema Wakurugenzi hao wamegundulika  baada ya uchunguzi wa kina uliofanywa na wizara yake
 
Akibainisha makosa ya kila mkurugenzi,Waziri Simbachawene amesema Mkurugenzi wa Halmashauri ya Misenyi, Bi Chitundu  alimwagiza  mweka hazina wake Majaliwa Bikwato atoe rushwa ya Milioni tatu kwa maafisa wa  ofisi ya CAG kwa lengo la kuficha kasoro walizoziabini katika ukaguzi huo  huku akijua ni kosa kisheria. Watumishi wa  wa ofisi ya CAG  waliopokea pesa hizo ni Stevin Buawa,John Elias pamoja na Kilembi Mkole
 
Katika Halmashauri ya Nanyumbu, Simbachawene amesema  kuwa  tarehe 26 Juni 2015, mkurugenzi wake bwana Kasengi pamoja na mweka hazina Pasco Malowo na mwasibu Emmanuel Mugesa walimkabidhi fedha Milioni 3 na laki tano  afisa wa ofisi ya  CAG  kwa lengo la kutoa hati safi
 
Waziri Simbachawene amesema mwezi Novemba mwaka jana , Mkurugenzi wa Halmashauri  ya  Mbogwe mkoani Geita Abdalla Mfaume na mweka hazina wake waliwapatia milioni 16  maafisa wakaguzi wa ofisi ya CAG  ili wafiche ufisadi walioubaini
 
Amesema katika Halmashauri hiyo pia kumegundulika kuwepo na ufisadi mkubwa ikiwemo malipo ya mishahara hewa pamoja na malipo ya milioni 200 yaliotolewa pasipo kuwa na Stakabadhi
Share:

SADC ESSAY WRITING COMPETITION 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

|\ |
The Southern African Development  Community (SADC) Secretariat has organized SADC Students Essay Writing Competition for theyear 2016. The Essay writing competition is intended to broaden knowledge of the school going population on SADC activities.

The topic for the year 2016 is “Transformation of Natural Endowment  and Improved Human Capital will accelerate  industrialisation  in  SADC Economies”.

The competition is open to students in Form 1 to 6 who are required to write essays between 1000 – 2000 words. The students are required to begin researching on the topic prior writing and submitting to their Heads of Schools by 5thApril, 2016. 

The Heads of School will then be expected to constitute a marking panel which will choose  best essay of the school. The panel should go through the essays (Please do not mark the essays) and choose the three best essays to be submitted to Permanent Secretary Ministry of Education, Science, Technology   and Vocation by  15thApril, 2016.

Following are the guidelines for essay writing  competition
  • The essay should not be longer than 2000 words and not shorter than 1000 words.
  • Where students have access to computers, they are advised to type their essays and submit both the soft and hard copies.
  • Students who will type their essays will have to sign and initial the hard copies to make sure that they have not been altered.
  • The essay should be written in English language.
  • The front page or cover page will display the name, sex, class, school address and stamp, Headmistress/Headmaster’s email address, signature and phone number, region, country.
  • The title of the essay should be written on the cover page (students should not paraphrase the title)
  • The handwritten essays will be written on one side of the A4 paper with double margin of two centimeters.
Thank you for your cooperation.


PERMANENT SECRETARY
Share:

New Audio|Download| KINGDOM-"ZANZI"

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

DOWNLOAD BY CLICKING 

AU
BONYEZA HAPO CHINI KUSIKILIZA

Share:

DOWNLOAD DIOFEICER FT KINGDOM-waniweza(wakubwa)

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 AU
BONYEZA HAPO CHINI KUSIKILIZA
Share:

DOWNLOAD KINGDOM FT JACKO MUSIC-nikikupata

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 AU
BONYEZA HAPO CHINI KUSIKILIZA 
Share:

NEW AUDIO:DOWNLOAD|KINGDOM FT YOUNG PLATNUMZ-WANIWEZA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

AU

BONYEZA HAPO CHINI KUSIKILIZA
Share:

New AUDIO | Admo - Waubani | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

DOWNLOAD via HULKSHARE
http://old.hulkshare.com/dl/4nw4uyafl7eo/Admo_-_Waubani...mp3?d=1
Share:

SUA:WANAFUNZI WALALAMIKA KWA KUTOKUPEWA PESA YAO YA SPECIAL FACULT ALLOWANCE

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 
Wanafunzi wa chuo kikuu cha sua wakati wakiwa wanaelekea kumaliza muhula wao wa kwanza wa masomo tangu walipofungua mwezi wa kumi na moja mara baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana,kumetokea uhaba wa fedha baada ya kucheleweshewa pesa yao ya special faculty allowance ambayo inatakiwa alipwe mwanafunzi wakati tu akiwa amewasili chuoni.

tukizungumza moja kwa moja na mwanafunzi wa kozi ya aquaculture na toursim management (majina tumeyahifadhi) kwa wakati tofauti wamesema kwamba kiukweli hali ya kimaisha ni ngumu sana kwani hadi sasa hawajui watakula nini kwani wamekuwa wakishindia mkate na maji kwa ukosefu wa pesa.

Maswayetu blog team tulitinga ofisi za bodi ya mikopo ,kuulizia swala hilo na kuambiwa kwamba maelezo yote yapo chuoni kwani pesa zote zilishatolewa.

tutaendelea kufatilia swala hili na kukuletea majibu yaliyosahihi mara tutakapofika chuo husika na kupata maelezo kutoka kwa viongozi husika.
Share:

Sikiliza Barua Aliyoiandika Mtanzania Jackline Cliff Kutoka Gerezani China...

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Jackline Cliff ni Mtanzania ambaye alikamatwa kwenye uwanja wa ndege na kufungwa gerezani huko Macao China kwa kosa la kujaribu kuingiza dawa za kulevya miaka miwili iliyopita, sasa leo kamuandikia mwandishi wa habari na Mtangazaji Millard Ayo barua ili aisome kwa Watanzania, bonyeza play kwenye hii video hapa chini….
Share:

PHD and Postdoc Scholarships at UDSM

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

PHD and Postdoc Scholarships at UDSM

Click Here to download the details of  PHD scholarship  at UDSM
Click Here to download the details of Postdoc Scholarship
Share:

TANGAZO LA KAZI- SEKRETARIETI YA AJIRA

Share:

TANGAZO KUTOKA SEKRETARIETI YA AJIRA-Accountant II WAFUATAO WANAHITAJIKA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


TANGAZO LA KAZI DEC 29, 2015 Waombaji kazi wafuatao wa kada ya Uhasibu (Accountant II) ambao walifanya usaili wa Mchujo tarehe 12 Februari, 2016 wanaombwa kufika kwenye usaili wa Mahojiano Oral Interview utakaofanyika tarehe 22 Februari, 2016, saa moja kamili asubuhi katika Ofisi za Sekretarieti ya Ajira.
Share:

Mimba ya Wema Sepetu 'Yatoweka Ghafla'........., Idris aandika ya moyoni kuhusu kupoteza mapacha wake

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mpenzi wa Wema Sepetu, Idris Sultan usiku wa kuamkia Jumatano hii amepost picha ya watoto mapacha huku akiandika ujumbe unao onyesha mimba ya mpenzi wake (Wema Sepetu)  imearibika.

Kupitia instagram idris ameandika
To my unborn twins,
    So quickly you came into our lives,
    So quickly torn away.
    Never got the chance to meet you,
   There’s so much I want to say. 
 
All these thoughts running  through my head,
    It’s enough to drive me insane.
    Though you lived only 13 short weeks,
    You were loved so very much.
    I wish that I could hold you,
    I long to feel your touch.
I pray that in another life, We get the chance to meet. God brings and takes as he plans and we cannot complain but only pray that all that was for a better reason and a better plan in store for us. 
We have learnt lessons painfully but wont stop trying again and again and do swear by the time your brothers and sisters are made to come to this world we will be more than ready for them.
    
Sincerely Your Dad. 
-----------
 
==>Hivi ndivyo unavyosomeka ujumbe wa Idris kwa lugha ya Kiswahili

Kwa mapacha wangu ambao walikuwa bado hawajazaliwa

“Ni haraka sana mmeingia katika mfumo wa maisha yetu, lakini ni haraka pia mmetuacha, sikuwahi kupata nafasi ya kukutana na nyinyi, nina vingi nataka niseme ninavyofikiria ndani ya kichwa changu vinatosha kunifanya mwendawazimu, ukizingatia mmeishi kwa wiki sita pekee, tuliwapenda sana na natamani ningepata nafasi ya kuwashika, mungu ametoa na mungu ametwa kama ambavyo amepanga na hatuwezi kulalamika huenda ametuandalia mengine mazuri zaidi”
Share:

Waziri Mahiga Amtetea Rais Magufuli Kwa Kutohudhuria Sherehe Ya Mwaka Ya Mabalozi

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Dk Augustine Mahiga amemtetea Rais John Magufuli kwa kutohudhuria hafla ya mwaka ya mabalozi akisema alikuwa Singida kwenye maadhimisho ya miaka 39 ya CCM.

Balozi Mahiga alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla hiyo iliyofanyika Ikulu ya kukaribisha mwaka mpya wa mabalozi ambayo kwa kawaida mwenyeji huwa ni Rais.

Dk Mahiga alitoa ufafanuzi huo kwa waandishi wa habari jana baada ya kuulizwa sababu za Rais kushindwa kuhudhuria hafla hiyo, lakini maelezo hayo yalichanganya zaidi, kwa kuwa hafla hiyo ya mabalozi ilifanyika Februari 8 wakati kilele cha sherehe za CCM kilikuwa Februari 6.

Kuhusu tofauti hiyo ya siku, Dk Mahiga alisema baada ya sherehe ya Singida, Rais alipitia kwenye ziara ambayo hata hivyo hakuifafanua.

Wakati huohuo, Waziri Mahiga alisema licha ya Dk Magufuli kuwakilishwa kwenye mikutano katika nchi mbalimbali, nchi hizo zinafahamu anachokifanya na bado nchi inaheshimika.

Akitoa mfano, katika mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika ulioandaliwa na China ambao ulifanyika Afrika Kusini, alisema licha ya Tanzania kuwakilishwa na makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, ilikuwa miongoni mwa nchi nne kati ya 54 za Afrika zilizopewa kipaumbele na kuwekeza katika sekta ya viwanda. Nchi nyingine zilizopewa kipaumbele ni Kenya, Ethiopia na Afrika Kusini.

“Utaona namna tunavyokubalika kimataifa kati ya nchi 54 za Afrika tunakuwa miongoni wa nchi nne zitakazopewa kipaumbele,” alisema.

Alisema wizara yake itaendelea kubana matumizi kwa kuziwezesha balozi za nje ili ziwe na uwakilishi imara.

Akitoa mfano, Dk Mahiga alisema juzi alirejea kutoka Angola ambako alimwakilisha Rais Magufuli kwenye mkutano wa Maziwa Makuu, akiongozana na watu watatu tofauti na zamani ambako angekuwa na msururu wa watu.

Alisema hata Makamu wa Rais alipokwenda Ethiopia kwenye mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) alisafiri na watu 14 wakati zamani angesafiri na zaidi ya watu 30.
Share:

Mfanyakazi Wa Kihindi Afukuzwa Kazi Nchini Kwa Kuwaita Watanzania Nyani

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Raia wa India, Dennis Smith ameachishwa kazi katika Hoteli ya Ramada kwa madai ya kuwatukana wafanyakazi wa ngazi za chini akiwaita nyani.

Smith, ambaye ni meneja wa chakula na vinywaji wa hoteli hiyo, aliwatukana na kuwadhalilisha wafanyakazi hao siku ya Sikukuu ya Wapendanao akiwatuhumu kushindwa kuandaa meza vizuri.

Kutokana na udhalilishaji huo, wafanyakazi wa hoteli hiyo jana waligoma wakishinikiza meneja huyo asimamishwe kazi au wao waache kazi.

Wakizungumza jana, baadhi ya wafanyakazi ambao waliomba majina yao yahifadhiwe walisema tabia ya meneja huyo imekuwa sugu na tukio la juzi lilikuwa halivumiliki. Walisema raia huyo wa India amekuwa mwenye majivuno na kutoa lugha chafu dhidi yao.

“Tumechoshwa, anatuitaje sisi nyani, hii tabia ni ya muda mrefu na sasa hatuwezi kuivumilia,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao.

Mwakilishi wa wafanyakazi hao, Mathew Misalaba alisema bosi huyo amekuwa akiwarushia maneno ya kuwadhalilisha kila wanapofanya makosa hata kidogo.

Alisema licha ya uongozi wa hoteli kuahidi kumsimamisha kazi Smith, wamelipeleka suala hilo polisi ili hatua stahiki zichukuliwe.

Meneja Rasilimaliwatu wa hoteli hiyo, Sebastian Nchimbi alisema tayari Smith ameachishwa kazi kutokana na tukio hilo.

“Tulizungumza na wafanyakazi wakatuambia kuwa hawataki Smith awepo kazini na sisi tukafanya uamuzi ili kuwalinda wafanyakazi wetu,” alisema.

Alisema waliamua kumwachisha kazi Smith baada ya kupata malalamiko mengi kutoka kwa wafanyakazi hao.

“Si tukio la mara ya kwanza na ndiyo maana tulipoona yamezidi tuliamua kuchukua hatua,” alisema.

Hata hivyo, Nchimbi alimsifu Smith akisema ni mtendaji mzuri na alikuwa na tija kwa hoteli hiyo ya kitalii lakini hakuwa na kauli nzuri kwa wafanyakazi Waafrika.

“Kiutendaji ni mzuri mno… yaani kwetu sisi tunapoteza mtu hasa, tatizo ni mdomo tu,”
alisema.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger