Friday 6 December 2019
Thursday 5 December 2019
HR Officer (Tanzania) at Smollan Tanzania
Smollan is recruiting for an HR Officer, to provide a full generalist HR functions to the relevant business unit(s), including recruitment, performance management, training and development, IR and general HR administration and reporting Key Responsibilities and Deliverables: Effective recruitment, selection and on-boarding Identify recruitment need and what the business is looking for and create and load advertisement on… Read More »
The post HR Officer (Tanzania) at Smollan Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.
Android APP developer at KOPAGAS – Dar Tanzania
You will report to the Head of Engineering and collaborate cross-functionally with Kopa teams. Responsibilities: Build, own, and maintain android applications. Develop unit-testing code for robustness, including edge cases, usability, and general reliability Review design documents, perform code reviews and contribute to implementation decisions. Support and collaborate with cross-functional teams (Product, Operations and Services) to ship excellent… Read More »
The post Android APP developer at KOPAGAS – Dar Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.
Small and Medium Business Adviser – Remote at VSO
Role Overview The ideal Candidate will be providing technical support to microfinance institution (s) to improve their capacity to strengthen loan scheme systems targeting smallholder farmers in Zanzibar Island, Tanzania. Liaise with Small Business advisors to advise CBOs / Parents to set up appropriate income generation activities. Skills, Knowledge And Experience Skills, qualifications and experience Minimum of 8… Read More »
The post Small and Medium Business Adviser – Remote at VSO appeared first on Udahiliportal.com.
Partner Help Desk Coordinator at Airtel Tanzania PLC
Airtel Tanzania PLC is looking for a suitable Tanzanian candidate for the Partner Help Desk Coordinator Position. The incumbent will assist in enhancing partner satisfaction and ensure timely release of payments to the partners. Key deliverables; Handle all partner queries and resolve them accordingly Educate partners on process flow and update them on invoice status Invoice Management Timely payment follow… Read More »
The post Partner Help Desk Coordinator at Airtel Tanzania PLC appeared first on Udahiliportal.com.
Software Developer at NMB Bank Plc December 2019
Job Purpose To build, test and implement in-house well designed new business applications or modify/upgrade existing business software applications to meet key business goals. Main Responsibilities Integrate technical and application components to meet business requirements Code and test program modules that meet design specifications Maintain, tune and repair applications in order to keep them performing according to technical… Read More »
The post Software Developer at NMB Bank Plc December 2019 appeared first on Udahiliportal.com.
Picha : AGAPE, POLISI WAADHIMISHA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA
Shirika lisilo la kiserikali Agape Aids Cotrol Program la mkoani Shinyanga, limefanya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwa kupinga vitendo vya ubakaji, ulawiti, mimba na ndoa za utotoni, pamoja na kutoa lugha chafu za matusi kwa wafanyabiashara wanawake sokoni.
Akizungumza kwenye maadhimisho hayo ,Kamanda Jongo, ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Shinyanga kuacha tabia ya kuwafanyia vitendo vya ukatili watoto wadogo, ikiwemo ubakaji, ulawiti, vipigo, kuwapa mimba pamoja na kuwaozesha ndoa za utotoni.
Amesema mkoa wa Shinyanga unashika nafasi ya tano kitaifa dhidi ya matukio ya ubakaji, ikiwamo wanafunzi kupewa ujauzito pamoja na kuozeshwa ndoa za utotoni, jambo ambalo linauchafua mkoa, na hivyo kuwataka wananchi waachane na matukio hayo ili watoto wapate kusoma kwa bidii na kuweza kutimiza ndoto zao.
“Nayapongeza sana mashirika haya ambayo siyo ya kiserikali likiwamo la Eguality For Growth (EFG) pamoja na Shirika la Agape, kwa kazi nzuri sana ambayo wanayoifanya mkoani hapa kwa kupambana kutokomeza matukio ya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto,”amesema Jongo.
“Pia naomba waendelee na mapambano haya ya kutokomeza ukatili huu wa kijinsia, kwa kutoa elimu kwa wananchi pamoja na wanafunzi dhidi ya madhara haya ya kufanya ukatili, ambapo mkoa wetu unaongoza kwa matukio ya ubakaji watoto na tunashika nafasi ya tano kitaifa,”ameongeza.
Naye mkurugenzi wa Shirika la Agape John Myola, amesema Shirika hilo limekuwa likijihusisha na miradi mbalimbali ya kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto, ikiwemo miradi ya kupinga mimba na ndoa za utotoni, pamoja na ukatili dhidi ya wanawake sokoni.
Pia amelipogeza Jeshi la Polisi kwa kushirikiana vyema na Shirika hilo la Agape dhidi ya mapambano ya matukio ya ukatili, ambapo wao wanapokuwa wakitoa taarifa za matukio hayo, polisi hufika mara moja kwenye eneo la tukio na kumkamata mtuhumiwa.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Equality For Growth kutoka Jijini Dar es salaam Jane Majigita, ametoa wito kwa wananchi pamoja na watoto, wawe wanatoa taarifa za matukio ya ukatili wa kijinsia, ili yafanyiwe kazi na wahusika kuchukuliwa hatua kali za kisheria, hali ambayo itapunguza matukio hayo.
Aidha kauli mbiu ya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia mwaka huu inasema "Kizazi Chenye Usawa, Simama Dhidi ya Ubakaji".
TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI
Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga Sophia Jongo akizungumza leo Desemba 5,2019 kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia,ambapo kilele chake kitafanyika Desemba 10 mwaka huu. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Shirika la Agape mkoani Shinyanga John Myola akizungumza kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Mkurugenzi wa Shirika la Equality For Growth (EFG) kutoka Jijini dar es salaam Jane Majigita, akizungumza kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Mkuu wa kituo cha Polisi wilaya ya Shinyanga Grace Salia akizungumza kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia
Afisa Maendeleo ya Jamii manispaa ya Shinyanga Anjel Mwaipopo akizungumza kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Wanafunzi pamoja na Askari Polisi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwenye viwanja vya Zimamoto Shinyanga Mjini.
Wanafunzi pamoja na askari polisi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwenye viwanja vya Zimamoto Shinyanga Mjini.
Wanafunzi pamoja na askari Polisi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwenye viwanja vya Zimamoto Shinyanga Mjini.
Wazazi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Watumishi wa Serikali na Askari Polisi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Wanafunzi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Wanafunzi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Jeshi la Zimamoto na uokoaji wakitoa elimu ya majanga ya moto namna ya kutumia kifaa cha kuzimia moto kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Wanafunzi kutoka Shule ya Msingi Mwenge wakitoa burudani.
Kikundi cha Ngoma kutoka Mwawaza kikitoa burudani.
Burudani ikiendelea kutolewa kwenye maadhimisho hayo ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwa kucheza na nyoka.
Kiongozi wa kikundi cha ngoma, Mahona Mtoba, akitoa burudani Meza kuu.
Awali wanafunzi wakiandamana kutoka Bwalo la Polisi hadi kwenye viwanja vya Zimamoto kwa ajili ya kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Maandamano yakiendelea.
Wanafunzi wakionyesha mabango yenye ujumbe mbalimbali.
Mgeni Rasmi akipokea maandamano pamoja na meza kuu.
Kaimu kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga Sophia Jongo, akitoa zawadi ya vifaa vya shule kwa ajili ya wanafunzi wenye uhitaji katika shule ya Sekondari Uhuru, akimkabidhi mwalimu wao.
Kaimu kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga Sophia Jongo, akitoa zawadi ya vifaa vya shule kwa ajili ya wanafunzi wenye uhitaji katika shule ya Msingi Mwenge, akimkabidhi mwalimu wao.
Mgeni rasmi kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Sophia Jongo akipiga picha ya pamoja na wafanyakazi kutoka Shirika la Agape, pamoja na mkurugenzi wa Shirika la EFG, Jane Majigita (wa kwanza mkono wa kushoto aliyekaa kwenye kiti).
Mgeni rasmi kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Sophia Jongo akipiga picha ya pamoja na kikundi cha ngoma.
Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog.