Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Friday 6 December 2019

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa December 6



















Share:

Thursday 5 December 2019

HR Officer (Tanzania) at Smollan Tanzania

Smollan is recruiting for an HR Officer, to provide a full generalist HR functions to the relevant business unit(s), including recruitment, performance management, training and development, IR and general HR administration and reporting Key Responsibilities and Deliverables: Effective recruitment, selection and on-boarding Identify recruitment need and what the business is looking for and create and load advertisement on… Read More »

The post HR Officer (Tanzania) at Smollan Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Android APP developer at KOPAGAS – Dar Tanzania

You will report to the Head of Engineering and collaborate cross-functionally with Kopa teams.   Responsibilities: Build, own, and maintain android applications. Develop unit-testing code for robustness, including edge cases, usability, and general reliability Review design documents, perform code reviews and contribute to implementation decisions. Support and collaborate with cross-functional teams (Product, Operations and Services) to ship excellent… Read More »

The post Android APP developer at KOPAGAS – Dar Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Small and Medium Business Adviser – Remote at VSO

Role Overview The ideal Candidate will be providing technical support to microfinance institution (s) to improve their capacity to strengthen loan scheme systems targeting smallholder farmers in Zanzibar Island, Tanzania. Liaise with Small Business advisors to advise CBOs / Parents to set up appropriate income generation activities. Skills, Knowledge And Experience Skills, qualifications and experience Minimum of 8… Read More »

The post Small and Medium Business Adviser – Remote at VSO appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Partner Help Desk Coordinator at Airtel Tanzania PLC

Airtel Tanzania PLC is looking for a suitable Tanzanian candidate  for the Partner Help Desk  Coordinator Position. The incumbent will assist in enhancing partner satisfaction and ensure timely release of payments to the partners. Key deliverables; Handle all partner queries and resolve them accordingly Educate partners on process flow and update them on invoice status Invoice Management Timely payment follow… Read More »

The post Partner Help Desk Coordinator at Airtel Tanzania PLC appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Software Developer at NMB Bank Plc December 2019

Job Purpose To build, test and implement in-house well designed new business applications or modify/upgrade existing business software applications to meet key business goals. Main Responsibilities Integrate technical and application components to meet business requirements Code and test program modules that meet design specifications Maintain, tune and repair applications in order to keep them performing according to technical… Read More »

The post Software Developer at NMB Bank Plc December 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Picha : AGAPE, POLISI WAADHIMISHA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA




Shirika lisilo la kiserikali Agape Aids Cotrol Program la mkoani Shinyanga, limefanya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia  kwa kupinga vitendo vya ubakaji, ulawiti, mimba na ndoa za utotoni, pamoja na kutoa lugha chafu za matusi kwa wafanyabiashara wanawake sokoni.


Maadhimisho hayo ambayo kilele chake ni Desemba 10 mwaka huu, yamefanyika kwenye viwanja vya Zimamoto Shinyanga mjini leo Desemba 5,2019  ambapo mgeni rasmi alikuwa Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Sophia Jongo.

Akizungumza kwenye maadhimisho hayo ,Kamanda Jongo, ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Shinyanga kuacha tabia ya kuwafanyia vitendo vya ukatili watoto wadogo, ikiwemo ubakaji, ulawiti, vipigo, kuwapa mimba pamoja na kuwaozesha ndoa za utotoni.

Amesema mkoa wa Shinyanga unashika nafasi ya tano kitaifa dhidi ya matukio ya ubakaji, ikiwamo wanafunzi kupewa ujauzito pamoja na kuozeshwa ndoa za utotoni, jambo ambalo linauchafua mkoa, na hivyo kuwataka wananchi waachane na matukio hayo ili watoto wapate kusoma kwa bidii na kuweza kutimiza ndoto zao.

“Nayapongeza sana mashirika haya ambayo siyo ya kiserikali likiwamo la Eguality For Growth (EFG) pamoja na Shirika la Agape, kwa kazi nzuri sana ambayo wanayoifanya mkoani hapa kwa kupambana kutokomeza matukio ya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto,”amesema Jongo.

“Pia naomba waendelee na mapambano haya ya kutokomeza ukatili huu wa kijinsia, kwa kutoa elimu kwa wananchi pamoja na wanafunzi dhidi ya madhara haya ya kufanya ukatili, ambapo mkoa wetu unaongoza kwa matukio ya ubakaji watoto na tunashika nafasi ya tano kitaifa,”ameongeza.

Naye mkurugenzi wa Shirika la Agape John Myola, amesema Shirika hilo limekuwa likijihusisha na miradi mbalimbali ya kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto, ikiwemo miradi ya kupinga mimba na ndoa za utotoni, pamoja na ukatili dhidi ya wanawake sokoni.

Pia amelipogeza Jeshi la Polisi kwa kushirikiana vyema na Shirika hilo la Agape dhidi ya mapambano ya matukio ya ukatili, ambapo wao wanapokuwa wakitoa taarifa za matukio hayo, polisi hufika mara moja kwenye eneo la tukio na kumkamata mtuhumiwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Equality For Growth kutoka Jijini Dar es salaam Jane Majigita, ametoa wito kwa wananchi pamoja na watoto, wawe wanatoa taarifa za matukio ya ukatili wa kijinsia, ili yafanyiwe kazi na wahusika kuchukuliwa hatua kali za kisheria, hali ambayo itapunguza matukio hayo.

Aidha kauli mbiu ya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia mwaka huu inasema "Kizazi Chenye Usawa, Simama Dhidi ya Ubakaji".

TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga Sophia Jongo akizungumza leo Desemba 5,2019 kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia,ambapo kilele chake kitafanyika Desemba 10 mwaka huu. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog

Mkurugenzi wa Shirika la Agape mkoani Shinyanga John Myola akizungumza kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Mkurugenzi wa Shirika la Equality For Growth (EFG) kutoka Jijini dar es salaam Jane Majigita, akizungumza kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Mkuu wa kituo cha Polisi wilaya ya Shinyanga Grace Salia akizungumza kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia

Afisa Maendeleo ya Jamii manispaa ya Shinyanga Anjel Mwaipopo akizungumza kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Wanafunzi pamoja na Askari Polisi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwenye viwanja vya Zimamoto Shinyanga Mjini.

Wanafunzi pamoja na askari polisi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwenye viwanja vya Zimamoto Shinyanga Mjini.

Wanafunzi pamoja na askari Polisi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwenye viwanja vya Zimamoto Shinyanga Mjini.

Wazazi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Watumishi wa Serikali na Askari Polisi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Wanafunzi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Wanafunzi wakiwa kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Jeshi la Zimamoto na uokoaji wakitoa elimu ya majanga ya moto namna ya kutumia kifaa cha kuzimia moto kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Wanafunzi kutoka Shule ya Msingi Mwenge wakitoa burudani.

Kikundi cha Ngoma kutoka Mwawaza kikitoa burudani.

Burudani ikiendelea kutolewa kwenye maadhimisho hayo ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwa kucheza na nyoka.

Kiongozi wa kikundi cha ngoma, Mahona Mtoba, akitoa burudani Meza kuu.

Awali wanafunzi wakiandamana kutoka Bwalo la Polisi hadi kwenye viwanja vya Zimamoto kwa ajili ya kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Maandamano yakiendelea.

Wanafunzi wakionyesha mabango yenye ujumbe mbalimbali.

Mgeni Rasmi akipokea maandamano pamoja na meza kuu.

Kaimu kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga Sophia Jongo, akitoa zawadi ya vifaa vya shule kwa ajili ya wanafunzi wenye uhitaji katika shule ya Sekondari Uhuru, akimkabidhi mwalimu wao.

Kaimu kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga Sophia Jongo, akitoa zawadi ya vifaa vya shule kwa ajili ya wanafunzi wenye uhitaji katika shule ya Msingi Mwenge, akimkabidhi mwalimu wao.

Mgeni rasmi kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Sophia Jongo akipiga picha ya pamoja na wafanyakazi kutoka Shirika la Agape, pamoja na mkurugenzi wa Shirika la EFG, Jane Majigita (wa kwanza mkono wa kushoto aliyekaa kwenye kiti).

Mgeni rasmi kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Sophia Jongo akipiga picha ya pamoja na kikundi cha ngoma.

Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog.

Share:

BINTI AFARIKI AKIMUOKOA MWANAUME KWENYE MTO ULIOJAA MAJI

Waokoaji nchini Kenya wameuopoa mwili wa kijana mmoja aliyekufa maji alipokuwa akijaribu kumuokoa mwananume ambaye alikuwa akiomba usaidizi alipokuwa akivuka mto uliokuwa umefurika.

Anna Nduku mwenye umri wa miaka 19 alianguka katika mto Kandisi karibu na eneo la Ongata Rongai , viungani vya mji mkuu wa Nairobi siku ya Jumanne.

Ni miongoni mwa zaidi ya watu 130 ambao wamefariki kutokana na mafuriko yanayosababishwa na mvua kubwa ambayo imekuwa ikinyesha tangu siku ya Jumanne.

Bi Nduku alikuwa akijibu kilio cha mwanaume aliyekuwa akining'inia katika eneo moja la daraja ambalo liikuwa likijengwa.

Mwanaume huyo aliokolewa lakini yeye akaanguka katika mto huo alipojaribu kumuokoa.

Mamake Nduku, Elizabeth Mutuku, alikuwa karibu wakati ajali hiyo ilipotokea.

''Nilimuona akijaribu kujitoa katika maji nikajaribu kumuokoa. Nilimwita Anna Anna! Nilitaka kumrushia kijiti ili kujaribu kumvuta lakini mto huo ulikuwa umejaa maji hivyo basi alikuwa akirushwa kutoka eneo moja hadi jingine kabla ya kusombwa na maji hayo''.

Mto huo ulikuwa umefurika kutokana na mvua kubwa inayonyesha ambayo ilianza siku ya Jumatatu.

Ni baadhi ya mvua zilizoripotiwa katika eneo la Afrika mashariki katika wiki za hivi karibuni.

Wakazi wanasema kwamba hii ni miongoni mwa ajali za hivi karibuni ambazo zimefanya watu kadhaa kusombwa na maji katika kipindi cha miaka miwili iliopita.

Daraja la zamani liliondolewa mwaka 2017 na daraja jipya bado halijakamilishwa. Hatua hiyo imewafanya wakaazi kupitia maji kwa kutumia mawe wanayokanyaga ili kuvuka mto huo.

Dada yake Nduku , Maryam Zenneth, amelaumu serikali za mitaa kwa kushindwa kumaliza daraja hilo ambalo ni kiunganishi muhimu kati ya kijiji chake na mji wa soko wa Ongata Rongai.

''Watu wengi wanafariki na wao wanatazama watu wakiendelea kupoteza maisha'' , aliiambia BBC huku akiwa amejawa na hasira.

''Wanakuja na kuomboleza nawe lakini hawachukui hatua yoyote, leo ni dada yangu kesho atakuwa nani''?

''Daraja hilo ndio barabara kuu miongoni mwa watoto wanaokwenda shule. Kwa nini waliliondoa daraja lililokuwepo ili kuanza kujenga jipya na hawalimalizi kulijenga''?Watu hupanda katika daraja hilo ambalo halijakamilisha ili kujaribu kuvuka mto huo

Serikali ya mitaa katika eneo hilo bado haijatoa tamko lolote . Akikumbuka kuhusu maisha ya mwanawe, mamake amesalia akiwa amevunjika moyo. 'Nina huzuni, pengine angekuwa kiongozi wa siku zijazo ama hata mwalimu. Kupoteza maisha kama hayo kutokana na daraja ni uchungu mwingi."

Mvua zaidi inatarajiwa kunyesha katika taifa hilo katika siku zijazo , na serikali inawashauri watu wanaoishi katika maeneo ambayo yametabiriwa kuathiriwa vibaya kuhamia katika maeneo salama.

Maeneo mengine katika eneo hilo , watu sita wamefariki mashariki mwa Uganda kufuatia maporomoko ya ardhi baada ya mvua kunyesha kwa siku mbili mfululizo na kufikia sasa takriban watu 50 hawajulikani waliko.
Share:

MSHINDI WA PROMOSHENI YA TIGO CHEMSHA BONGO 2019 AKABIDHIWA GARI LAKE


Mkazi wa Zanzibar, Shaban Khamis Ali(49) akifurahia mara baada ya kukabidhiwa gari yake aina Renault Kwid yenye thamani ya 23m/- baada ya kuibuka mshindi wa promosheni ya Tigo Chemsha Bongo 2019.  
BAHATI IMEMUANGUKIA Mzee Shaban Khamis kutoka Zanzibar kushinda Gari aina ya Renault Kwid. Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Joseph Mutalemwa, amempongeza Mzee Shaban kwa kutumia fursa ya #TigoFiesta2019 Chemsha Bongo vizuri 
Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Joseph Mutalemwa,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kumkabidhi zawadi Mshindi wa promosheni ya Tigo Chemsha Bongo 2019 
“Kuna vitu vikitokea kwenye maisha yako inakuwa ngumu kuficha hisia zako. Nashukuru TIGO kwa kuleta mchezo huu wa #TigoChemshaBongo nilicheza nikiamini nitashinda pesa lakini nimeambulia zawadi kubwa kabisa ya gari” ,Mzee Shaban Khamis
Dar es Salaam Desemba 5 2019.Mkazi wa Zanzibar, Shaban Khamis Ali(49) amekabidhiwa rasmi gari yake aina ya Renault Kwid yenye thamani ya 23m/- baada ya kuibuka mshindi wa promosheni ya Tigo Chemsha Bongo 2019.
Promosheni hiyo iliyodumu kwa siku 90 kuanzia tarehe 4 Agosti hadi 14 Novemba 2019 na wateja wa Tigo walipata nafasi ya kujishindia zawadi za pesa taslim kila siku na droo ya mwisho mshindi alikuwa anajinyakulia zawadi ya gari. Promosheni hii ilishuhudia washindi 90 kila siku waliojishindia Tshs 100,000 na washindi wengine 90 waliojishinda Tshs 50,000. Pia tuliwapa washindi 12 kili wiki kwa mda wa wiki 12, Tshs 1,000,000.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Shabaan alisema “Wakati napigiwa simu,nilikuwa nyumbani najipanga kutoka kuenda katika mihangaiko yangu ya kibiashara, basi nilipopata ile taarifa kwamba nimeibuka mshindi nilifurahi sana kwani sikutegemea kabisa kuwa ningeibuka mshindi katika promosheni hii, habari hizi naziona kama ndoto kwangu, nashukuru Tigo kwa kunifungia mwaka vizuri na kutimiza ndoto yangu ya kumiliki gari, kwani itanisaidia katika mizunguko yangu ya kibiashara “alisema kwa furaha.

Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Joseph Mutalemwa, alimpongeza mshindi huyo na kutumia fursa hiyo kuwashukuru wateja wote wa kampuni ambao walishiriki na baadhi yao kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo zawadi za fedha taslimu ambayo yalitolewa na kampuni hiyo.

“Tunayo furaha kubwa katika kipindi hiki tunachoelekea katika msimu wa sikukuu kumkabidhi mshindi wetu wa gari ya aina Renault Kwid,yenye thamani ya 23m/-, gari hili ni jipya kabisa,. Tunawashukuru wateja wetu nchi nzima walioshiriki kwenye promosheni hii ya miezi mitatu ambayo imemalizika mwishoni mwa mwezi wa Novemba 2019”,alisema Mutalemwa.

Aliongeza kuwa, promosheni hii ambayo ilianza jijini Mwanza katika msimu wa Tigo Fiesta 2019-Saizi Yako imepata mafanikio makubwa kutokana na wateja wengi kujitokeza kushiriki na baadhi yao kufanikiwa kujishindia zawadi(fedha taslim) mbalimbali na hivyo Tigo kufanikisha lengo lake ambalo lilikuwa ni kuwashukuru wateja kwa kuiunga mkono kampuni kupitia kununua bidhaa zake mbalimbali.

Mutalemwa aliwashukuru wateja wote wa Tigo kwa kuendelea kuunga mkono kampuni na kuahidi kuwa promosheni mbalimbali za kunufaisha wateja wa kampuni hiyo zinatendelea kubuniwa katika siku za usoni.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger