Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Friday 16 August 2019

Tanzania Universities and colleges Prospectus 2019/2020

Download Undergraduate and Postgraduate Prospectus For all Universities In Tanzania – Undergraduate Prospectus 2019 / 2020 University Prospectus introduces you to life at University , describing the campus and detailing the services, admission requirements and facilities that the university provides for students. Details of all undergraduate programmes are provided. Download University Prospectus to Find a list of all… Read More »

The post Tanzania Universities and colleges Prospectus 2019/2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Nyumba ya Biashara Inauzwa: Tabata Relini (DSM)

Nyumba ya Biashara Inauzwa: Tabata Relini (DSM)


Nyumba ina vyumba 6, iko main road (Tabata Reli)
Nyumba ina kiwanja cha sqm 400 kinafaa kwa kujenga jengo la Biashara (commercial building)

Bei ya nyumba hii ni tsh 105 milion na maongezi yapo.
Call 0758603077


Share:

VIKAO VYA KAMATI ZA BUNGE KUANZA AGOSTI 19.....MKUTANO WA BUNGE SEPT 3,2019



Share:

Wadaiwa Sugu Kodi Ya Ardhi Sikonge Kubanwa

Na Munir Shemweta, WANMM SIKONGE
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameiagiza idara ya ardhi katika halmashauri ya Sikonge mkoani Tabora kuhakikisha inawafikisha kwenye Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya wadaiwa wote sugu wa kodi ya pango la ardhi katika wilaya hiyo wanaodaiwa kiasi cha takriban milioni 150.

Dkt Mabula alitoa agizo hilo tarehe 15 Agosti 2019 katika halmashauri ya Wilaya ya Sikonge wakati wa ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi sambamba na kukagua masiajala ya ardhi na mifumo ya ukusanyaji kodi kwa njia ya kielektroniki mkoani Tabora.

Dkt Mabula alishangazwa na idara ya ardhi katika halmashauri hiyo kushindwa kuwafikisha wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi kwenye Baraza la Ardhi na Nyumba wakati sheria inaelekeza baada ya siku kumi na nne mdaiwa asipotii wito afikishwe kwenye Baraza.

Alisema, katika halmashauri ya Sikonge kuna baadhi ya wamiliki wa ardhi ambao kwa mara ya mwisho walilipa kodi ya ardhi mwaka 2000 lakini idara ya ardhi imeshindwa kuwadai ama kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria jambo alilolieleza kuwa halikubaliki.

Kaimu Afisa Ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Sikonge Martin Ukongo alieleza kuwa ofisi yake tayari ilishasambaza ilani 105 kwa wadaiwa sugu wa kodi ya ardhi kuanzia januari hadi machi 2019 lakini baadhi yake pamoja na kushindwa kulipa hawajafikishwa kwenye Baraza la Ardhi jambo lililomfanya Naibu Waziri kuagiza hatua za kuwafikisha kwenye Baraza zifanyike.

Dkt Mabula pia ameigiza halmashauri ya wilaya ya Sikonge kupitia idara ya ardhi kuhakikisha inapima mashamba yote yaliyopo katika halmashauri hiyo na kueleza kuwa kutopimwa kwa mashamba hayo kunatoa fursa kwa wamiliki wake kutolipa kodi ya ardhi.

‘’Sikonge mna mashamba hayajapimwa wakati ni ya wafanyabiashara wakubwa hapa wanakwepa kulipa kodi why hamjawapimia na kuwapatia hati ili walipe kodi?’’ Alihoji Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Mabula

Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Denis Masami alisema kuwa Wizara yake kwa sasa imeimarisha mfumo wa ukusanyaji kodi ya pango la ardhi kwa kurahisisha ukadiriaji na kufanya malipo kupitia kupitia simu ya mkonini jambo linalowarahisishia wamiliki kuepukana na usumbufu wa kufika ofisi za ardhi kwa ajili ya malipo.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Peres Magiri alimueleza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa katika kipindi cha mwaka 2018/2019 wilaya hiyo ilifanikiwa kukusanya kodi ya pango la ardhi shilingi milioni 29,127,334.50 sawa na asilimia 87.55 wakati lengo ilikuwa kukusanya milioni 33.2. Hata hivyo Magiri alisema wilaya yake imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kama vile kutoa matangazo na kuelimisha jamii kupitia mikutano umuhimu wa kulipa kodi kwa wakati.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Sikonge Joseph Kakunda alimpongeza Naibu Waziri Dkt Mabula kwa uamuzi wake wa kufanya ziara katika wilaya hiyo na kueleza kuwa huyo ni Waziri wa Ardhi wa kwanza kuitembelea wilaya hiyo toka ianzishwe.

Hata hivyo, Kakunda alimueleza Dkt Mabula kuwa wilaya ya Sikonge ni wilaya iliyoko nyuma   katika suala la Mapango wa Matumizi Bora ya Ardhi na kuomba Wizara ya Ardhi kuipa kipaumbele katika upimaji ili kuepusha migogoro ya ardhi hasa ile ya wakulima na wafugaji.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521


Share:

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Kuanza Kwa Vikao Vya Kamati Za Bunge

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kuanza vikao vya kamati za kudumu siku ya Jumatatu tarehe 19 Agosti hadi tarehe 02 Septemba 2019, Jijini Dodoma, kabla ya kuanza kwa mkutano wa kumi na sita wa Bunge uliopangwa kuanza tarehe 3 Septemba 2019.

Taarifa iliyotolewa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa cha Bunge leo Ijumaa 16 septemba 2019 imesema pamoja na mambo mengine kamati tisa za sekta na kamati ya bajeti zitachambua taarifa za taasisi na wizara za Serikali kuhusu utekelezaji wa shughuli mbalimbali.

Mbali na kupokea taarifa mbalimbali za wizara/taasisi, kamati hizo zitachambua taarifa ya CAG.

Shughuli nyingine zitakazofanywa na kamati hizo ni pamoja na uchambuzi wa sheria ndogo, pamoja na uchambuzi wa taarifa za uwekezaji wa mitaji ya umma.


Share:

POLISI WAZUIA MKUTANO WA ZITTO KABWE....KATIBU WA ITIKADI NA UENEZI WA ACT- WAZALENDO ACHUKULIWA KWA MAHOJIANO


Katibu wa  Itikadi na Uenezi wa ACT- Wazalendo, Ado Shaibu  amechukuliwa  na Jeshi la Polisi kwa Mahojiano  alipokuwa katika Makao Makuu ya chama hicho, Kijitonyama jijini Dar es salaam  akiandaa mkutano wa kiongozi mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe kwa ajili ya kuzungumza na waandishi habari.

Jeshi la Polisi Kanda Maalim ya Dar es Salaam lilifika katika makao makuu ya chama hicho  na kuzuia  mkutano  huo ambao ulitarajiwa kufanyika leo Ijumaa Agosti 16,2019 saa 5 asubuhi.

Polisi waliwasili Makao Makuu ya chama hicho  na kumhitaji kiongozi yoyote wa chama baada ya kumkosa Zitto Kabwe.

"Ndugu waandishi huu mkutano usubiri kwanza, kwa hiyo ninawaomba mtawanyike mara moja," alisema askari mmoja.

Wakati waandishi wakitawanyika aliwasili Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu ambaye walimchukua  na kuondoka  naye kwa ajili ya mahojiano.


Share:

#Kimataifa: Israel yawazuia wabunge wa kiislamu wa Marekani kuingia nchini humo

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Israel imetangaza kuwa waziri mkuu Bw. Benjamin Netanyahu amewazuia wabunge wanawake wawili wa kwanza wa kiislamu kuchaguliwa kuwa wabunge wa Marekani, Rashida Tlaib na Ilhan Omar, kuingia nchini mwake kwa madai kuwa wanapambana na Israel.

Uamuzi huo umekuja saa chache baada ya Rais Donald Trump kuandika katika ukurasa wake wa Twitter kuwa Omar na Tlaib wanaichukia Israel na Wayahudi. 

Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani Bibi Nancy Pelosi amekosoa vikali hatua hiyo na kusema imeonyesha dalili ya udhaifu na kupunguza uadilifu wa Israel.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Marekani, viongozi hao wawili walikuwa na ziara ya kikazi Jumapili hii, ambayo pia ingelijumuisha wao kufika eneo tata la Temple Mount mjini Jerusalem, linalotambuliwa na Waislamu kama Haram al-Sharif.

Pia walikuwa na mpango wa kukutana na wanaharakati wa amani wa Israel na Palestina na kusafiri hadi ukingo wa Magharibi wa Jerusalem katika miji ya Bethlehem, Ramallah na Hebron.



Share:

PICHA: Rais wa Shelisheli Danny Faure Awasili Nchini kwa ajili ya kushiriki mkutano wa 39 wa SADC

Rais wa Shelisheli Danny Faure, amefika nchini na kupokelewa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa, kwa ajili ya kushiriki mkutano wa 39 wa SADC utakaofanyika kesho.

Rais Faure ni Rais wa pili kuja nchini baada ya kutanguliwa na Rais wa Afrika Kusini


Share:

Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) Yatakiwa Kuwezesha Kampuni Nyingi Kuorodheshwa Soko La Hisa

 Na Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Serikali imeitaka Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) kuhakikisha Kampuni nyingi zinaorodheshwa katika Soko la hisa ili kuweka uwazi zaidi katika utendaji wa kampuni hizo na hivyo kuwezesha Serikali kukusanya kodi stahiki na kuchangia katika ongezeko la mapato ya Serikali.

Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, alipofanya ziara katika Mamlaka hiyo ikiwa ni sehemu ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 katika Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Dkt. Kazungu, alisema kuwa CMSA iendelee kusimamia masoko ya Mitaji ya Dhamana kwa kuorodhesha Kampuni nyingi zaidi katika soko hilo la hisa kwa kuzingatia masharti ya kuorodheshwa kampuni ili kuongeza uwazi, utawala bora na ufanisi wa kampuni hizo kwa kuweka mazingira mazuri ya uendeshaji na uwazi wa hesabu zao, hatua itakayochangia kukuza uwekezaji na mapato ya Serikali hususani katika eneo la kodi.

“Muendelee na kasi ya kutoa elimu kwa wananchi wengi ili waweze kujiunga na Masoko ya Hisa hususani kwa wananchi walio katika Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi”, alieleza Dkt. Kazungu.

Alisema kuwa iwapo wananchi wengi watajiunga katika Masoko la Hisa kutawafanya kuongeza mapato yao lakini pia kushiriki katika umiliki wa uchumi wa nchi yao.

Dkt. Kazungu alisema kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa uchumi wa viwanda, uchumi unaotarajiwa kujengwa katika kipindi kifupi wakati wa kuelekea katika uchumi wa kati hivyo ni vema wawekezaji wakahimizwa kupata mitaji ya kuendeleza na kupanua uwekezaji kupitia masoko ya mitaji na kutoa fursa nyingi za uwekezaji kwa wananchi.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Bw. Nicodemus Mkama, amesema Mamlaka yake imeweka mkakati wa kutoa elimu kwa umma na wawekezaji mbalimbali jinsi ya kutumia masoko ya mitaji kupata fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo.

“CMSA inaendelea kutoa elimu kwa umma na kwa makundi mbali mbali ya wanataaluma, wanafunzi wa elimu ya juu, watunga sera ikijumuisha Kamati za Bunge. Elimu hii inalenga kuelimisha umuhimu na fursa ya masoko ya mitaji katika kukuza uchumi na ushirikishwaji wa wananchi katika Sekta ya Fedha hususani masoko ya mitaji” alifafanua Bw. Mkama.

Alisema kutokana na jitihada hizo, kwa sasa uhitaji katika uwekezaji katika Soko ni mkubwa, hii inawafanya kuongeza bidhaa zinazokidhi matakwa ya wawekezaji ndani na nje ya nchi.

“Hii imejidhihirisha hivi karibuni kwa kuongezeka kwa kampuni nyingi katika sekta ya fedha kuorodhesha hatifungani ikiwa ni njia sahihi ya taasisi hizo kupata fedha za mahitaji mbalimbali ya utoaji mikopo na kutekeleza miradi ya maendeleo.

Alisema elimu hiyo pia imeleta matokeo chanya na mwitikio wa matoleo ya hatifungani za Kampuni ya Kuendeleza Sekta ya Nyumba – TMRC, Benki ya Biashara ya DCB na Benki ya Biashara ya NMB na unaonyesha wazi kuwa kuna ongezeko kubwa la uelewa wa wananchi kushiriki katika uwekezaji kwenye masoko ya mitaji.

Toleo la hatifungani ya NMB Bank limeweka historia kubwa katika maendeleo ya masoko ya mitaji hapa nchini kwa kupata kiwango cha shilingi bilioni 83.3, ikiwa ni mafanikio ya asilimia 333 ikilinganishwa na shilingi bilioni 25 zilizotarajiwa kukusanywa.

Bw. Mkama alisema kuwa mauzo hayo yamekuwa na idadi na thamani kubwa kuliko mauzo yote ya hatifungani yaliyowahi kufanyika hapa nchini, ambapo jumla ya wawekezaji 2,264 wameweza kushiriki. Kati ya wawekezaji hao, asilimia 99.5 ni wawekezaji wadogo wadogo, na wawekezaji Kampuni ni asilimia 0.5.

“Tumeshatoa maelekezo kwa watendaji na washiriki (wanaotoa dhamana) katika Masoko ya Mitaji kuhakikisha wanakuja na bidhaa zinazokidhi mahitaji ya wawekezaji ili kuvutia wawekezaji wengi zaidi watakao sababisha ongezeko la mapato yao na upatikanaji wa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo jambo litakalochangia kushiriki kikamilifu katika uchumi wa nchi”, alieleza Bw. Mkama.

Alisema kuwa katika utoaji wa elimu, CMSA inatumia mbinu mbalimbali za kibunifu ikiwa ni pamoja na kuweka mashindano kwenye Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania Bara na Visiwani kwa kuwezesha wanafunzi kujifunza elimu ya masoko ya mitaji kwa njia ya kujibu maswali na kuandika insha

Alibainisha kuwa, wanafunzi wanaofanikiwa kushinda nafasi ya kwanza hadi ya tatu wanapewa tuzo mbalimbali zikiwemo fedha taslimu kuanzia shilingi milioni moja hadi milioni 1.8 kama kivutio cha ushiriki huku wanafunzi walioshika nafasi 20 za juu wanazawadiwa shilingi laki 2 kila mmoja na kwamba washindi wa nafasi ya kwanza hadi ya tatu wa mwaka huu (2019) watapelekwa nchini Namibia kwa ziara ya mafunzo.


Share:

Mabalozi 42 watembelea mradi wa SGR.....Dr Wilibrod Slaa Ammwagia Sifa Rais Magufuli

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa amewataka mabalozi wa Tanzania kushirikiana na shirika hilo ili kuweza kuleta maendeleo ya mradi inayoendelea hapa nchini na pia kulitangaza taifa kwa ujumla.

Akizungumza na Mabalozi hao waliotembelea mradi mkubwa wa ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge(SGR) unaendelea, Kadogosa amesema kuwa mpaka sasa ujenzi umefika asilimia 60.4 hivyo amewashukuru mabalozi waliokuja kuangalia mradi wa kimkakati kwani kutawawezesha kulitangaza taifa kwa mazuri yanayoendelea.

“Kama tunaweza kutekeleza miradi hii kwa pesa yetu, watu wa nje wanatuheshimu kwahiyo uwekezaji mkubwa kama huu unawagusa wawekezaji wa nje kwahiyo sisi tunawashukuru mabalozi kuja kuangalia miradi hii hivyo watakaporudi huko watawaelezea watu wa huko miradi hii walioyoiona kwa ukubwa wake,”amesema Kadogosa.

Aidha, Kadogosa amesema kuwa gharama za kutengeneza fensi katika ujenzi wa reli hiyo kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro ni dola bilioni 1.2 kujumlisha na kodi na kutoka Morogoro kwenda Maktupola Singida ni dola bilioni 1.9 pamoja na kodi hivyo jumla ya gharama zitakazotumika ni takribani bilioni 3.1.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Swedeni, Wilibrod Slaa amewataka watanzania waweze kujivunia kumpata Rais mwenye kufanya maamuzi kwani wameona miradi mingi ikifanyika hapa nchini kwani hata nchi zilizoendelea wamekuwa wakifanya uwekezaji na ulipaji kodi ambazo zinasaidia kuibua miradi mbalimbali.


Share:

LIVE Kutoka Morogoro: Ziara Ya Rais Wa Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa....Tazama Hapa

Live Kutoka Morogoro: Ziara Ya Rais Wa Afrika Kusini  Mhe. Cyril Ramaphosa....Tazama Hapa


Share:

MWANAMUZIKI MBALAMWEZI WA KUNDI LA THE MAFIK AFARIKI DUNIA


Mwanamuziki Mbalamwezi ambaye ni mmoja wa Wasanii  wanaounda kundi la The Mafik amefariki dunia kutokana na majeraha ambayo yanahusishwa na kupigwa.

Baadhi ya ndugu wamesema taarifa za awali ni kwamba Mwili wake ulikutwa maeneo ya Africana Dar es salaam ukiwa hauna nguo ikiwa ni saa kadhaa zimepita toka msanii huyo atokomee bila kujulikana alipo. 

Msanii huyo ameshiriki katika kazi za kundi ambazo zimefanya vizuri kama Passenger, Sheba,Carola, Vuruga, na Dodo, pia ameshirikishwa katika nyimbo za Ruby na Ben Pol.




Share:

Ajali ya Basi na Lori Yaua Watu Wanne Morogoro

Watu 4 wamefariki dunia na wengine 26,  wamejeruhiwa kufuatia ajali iliyohusha basi la abiria na Lori  kugongana uso kwa uso katika eneo la nanenane Manispaa ya Morogoro.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo imehusisha basi la abiria lenye namba za usajili T212 DNU na Lori.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa,Chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa basi ambaye alitaka kulipita gari lililokuwa mbele yake bila kuchukua taadhari.

"Ni kweli usiku wa kuamkia leo Ijumaa August 16, saa saba na nusu usiku imetokea ajali eneo la Nanenane, Morogoro, basi mali ya kampuni ya Safari Njema ambayo ilikuwa inatokea DSM kwenda Dodoma imegongana kwa ubavu na lori mali ya Tumbaku Alliance, watu 4 wamefariki.

"Ingawa watu 4 wamefariki ila abiria wengine waliokuwa kwenye basi walikimbizwa Hospitali ya Mkoa Morogoro sababu ya mshtuko na wengi wametibiwa na kuruhusiwa, wamebakia abiria 3 wanaendelea na matibabu, dereva wa lori ni miongoni mwa waliofariki.

"Chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa basi ambaye aliovertake pasipo kuchukua tahadhari na kukutana na gari nyingine mbele kisha ajali ikatokea, dereva wa basi ametoweka na tunamtafuta, kama hatopatikana tutamkamata mmiliki wa basi ili atuoneshe dereva alipo". Amesema Mutafungwa



Share:

Waziri Jafo Aingilia Kati sakata la watumishi wa Hospitali kulipishwa mashine ya Ultrasound iliyoibiwa

Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jafo ameingilia kata sakata la watumishi wa Hospitali ya Mji wa Bariadi  na kuamruru wasichangishwe fedha kufidia mashine ya Ultrasound iliyoibwa hospitalini hapo.

Jafo ametoa kauli hiyo jana Alhamisi Agosti 15, kauli ambayo inamuunga mkono Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini ya kutaka watumishi hao wasilipishwe fedha kama walioamriwa na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga  Jumatano Agosti 14.

Pamoja na mambo mengine, Jafo amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka kuunda tume ya uchunguzi ili kuwabaini waliohusika na wizi wa mashine hiyo.

“Kulikuwa na maelekezo kuwa wale watumishi 137 walipie ile mashine kwa kukatwa kwenye mshahara yao, nielekeze kwamba watumishi wetu hawa wanafanya kazi katika mazingira magumu sana, na tukumbuke hata tulipopata janga pale Morogoro watumishi wetu wa idara ya afya muda mwingi ndiyo walikuwa kimbilio kuwasaidia wananchi.

“Kitendo kama hiki ni kuwakatisha tamaa na kuwaweka katika ya sintofahamu lakini kumbe inawezekana kuna watu walihusika. Lengo hapa ni kuwatafuta waliohusika, wabainishwe ni kina nani wachukuliwe hatua lakini pia wahakikishe mashine hii inarudi.

“Kwa hiyo nitoe maelekezo kuwa watumishi hawa wasichangishwe fedha ya aina yoyote kwa sababu siyo jukumu lao, ni jukumu la ulinzi kwa hiyo Mkuu wa Mkoa namuelekeza kwanza aunde tume ya uchunguzi kuwabaini wahusika na watumishi hao waachwe wafanye kazi kwa sababu tunawategemea sana haipaswi kuwabebesha mzigo usiowahusu,” amesema Jafo.

Mashine hiyo inadaiwa kuibiwa pamoja na kifaa chake cha kudurufu picha (printer) ambapo ilikua maalumu kwa matumizi ya wodi mpya ya akina Mama wajawazito na iliibiwa ikiwa katika wodi hiyo.


Share:

TPA YAKABIDHI MASHINE MBILI KWA AJILI YA KUHIFADHI WATOTO NJITI KWENYE HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO ZENYE THAMANI YA MILIONI 25

 Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Mhandisi Witonde Philipo kulia akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kushoto  mashine mbili za incubator kwa ajili ya kusaidia kuhifadhi watoto njiti zenye thamani ya Sh milioni 25 katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga anayeshuhudia katikati ni Meneja wa Bandari ya Tanga Ajuaye Msese
 Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Mhandisi Witonde Philipo kulia akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kushoto  mashine mbili za incubator kwa ajili ya kusaidia kuhifadhi watoto njiti zenye thamani ya Sh milioni 25 katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga anayeshuhudia katikati ni Meneja wa Bandari ya Tanga Ajuaye Msese
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza mara baada ya kupokea msaada wa  mashine mbili za incubator kwa ajili ya kusaidia kuhifadhi watoto njiti zenye thamani ya Sh milioni 25 katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga vilivyotolewa na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kushoto ni Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Mhandisi Witonde Philipo akifuatiwa na  Meneja wa Bandari ya Tanga Ajuaye Msese kulia ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Abdiely Makange
 Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Mhandisi Witonde Philipo akizungumza wakati wa halfa hiyo kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kushoto ni Meneja wa Bandari ya Tanga Ajuaye Msese 
 Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Abdiely Makange akizungumza wakati wa hafla hiyo
 Meneja wa Bandari ya Tanga Ajuaye Msese akizungumza wakati wa halfa hiyo
 PRO wa Bandari ya Tanga Moni Jarufu akizungumza jambo wakati wa halfa hiyo ya makabidhiano
 Sehemu ya msaada wa vifaa vilivyokabidhiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa ajili ya kuhifadhi watoto njiti zenye thamani ya Sh milioni 25 katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Ta
 kuhifadhi watoto njiti zenye thamani ya Sh milioni 25 katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Ta
 Sehemu ya watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo wakiwa kwenye halfa hiyo
  Sehemu ya watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo wakiwa kwenye halfa hiyo
  Sehemu ya watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo wakiwa kwenye halfa hiyo
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati akisisitiza jambo kwa Meneja wa Bandari ya Tanga  Ajuaye Msese wakati alipowasili kwenye hospitali ya mkoa wa Tanga Bombo kwa ajili ya kupokea msaada mashine mbili za incubator kwaajili ya kusaidia kuhifadhi watoto njiti zenye thamani ya Sh milioni 25 katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga. uliotolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kushoto ni Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mhandisi Witonde Philipo



MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imetoa msaada wa mashine mbili za incubator kwaajili ya kusaidia kuhifadhi watoto njiti zenye thamani ya Sh milioni 25 katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga.

Akikabidhi msaada huo Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mhandisi Witonde Philipo amesema kuwa mamlaka hiyo ilikuwa imetenga bajeti ya Sh milioni 50 kwa ajili ya kusaidia jamii katika sekta ya elimu na afya.

Akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo Mhandisi Witonde alisema kwamba wao wanashukuru kupewa nafasi ya kujumuika kwenye mkoa wa Tanga kusaidia kuboresha maisha ya wakazi wa mkoa huo.

Alisema kwamba walipata maombi ya kuwepo kwa changamoto hizo na wao wakaona wafanye jambo hilo hivyo wanaimani uongozi wa mkoa huu ungeweza kupata watu wengine lakini wakawaona wao.

Mhandisi Witonde alisema kwamba mamlaka hiyo imekuwa na utaratibu kila mwaka kutenga bajeti kwa ajili ya kusaidia jamii kwenye ameneo ya afya, elimu na maeneo mengine ya kijamii.

Alisema katika mwaka wa fedha walipanga kutumia kiasi cha milioni 50 kutoa huduma hizo huku akieleza kwamba vifaa hivyo vitasaidia kuokoa maisha ya watoto.

“Kabla ya zoezi hili siku chache tulikwisha kukabidhi mabati 378 shule ya sekondari Tanga School yenye thamani ya milioni 15 na yamekarabati nyumba tano lakini pia tutaendelea kuona namna ya kuwasaidia kwa kadiri mungu atakavyowajalia”Alisema 

Awali akizungumza wakati wa hafla hiyo ya makabidhiano Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella aliwashukuru TPA kwa kutenga fedha hizo milioni 50 kwenye mwaka wa fedha na kuwezesha kwenye katika mkoa wetu kuleta vifaa hvyo ambavyo vitakuwa ni chachu kuwasaidia kuboresha sekta ya afya.

Alisema kwani kutenga fedha ni jambo moja na kufanikisha ni jambo la pili hivyo niwapongeze TPA kwa kutekeleza wale walioyapanga na kuhaidi

“Nimshukuru MKurugenzi Mkuu wa TPA kwani Tanga imekuwa ni nyumbani kwenu kuja mara kwa mara na kuweza kuwasaidia tunatambua jitihada kubwa mnazofanya katika kuhakikisha mnasaidia jamii na watanzania kwa ujumla”Alisema

Alisema wanatambua jitihada kubwa mnazofanya TPA kuhakikisha mnasaidia jamii na watanzania kwa ujumla ukiacha suala la kusimamia mapato na kujenga mazingira mazuri ya kuwa lango kuu la kibiashara kati ya nchi yetu na jirahi bandari imekuwa ni msaada kuwasaidia shughuli mbalimbali za kijamii na maelezo yako ulioyayatoa yanadhihiridha

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa mkoa huo, Abdiel Makange, amesema mashine hizo zitaweza kusaidia kuokoa maisha ya watoto njiti ambao wanazaliwa katika hospitali hiyo.

“Hospitali ilikuwa ina mashine mbili tayari, hivyo uwepo wa nyingine za ziada kutawezesha kupunguza changamoto ya vifo kwa watoto hao” amesema.

Mwisho.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa 16 August

























Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger