
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amesema atafanya uteuzi wa naibu waziri mwingine wa Madini baada ya aliyemteua, Francis Ndulane Kumba ambaye ni Mbunge wa Kilwa Kaskazini kushindwa kuapa leo Jumatano Desemba 9, 2020 Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Kumba alikuwa mmoja wa waliotakiwa kuapa lakini alikuwa akishindwa kutamka maneno na kutakiwa kukaa pembeni ili wenzake waendelee kuapa.
"Kila mmoja nimemuangalia mpaka wewe uliyeshindwa kuapa.
Tutamteua mtu mwingine anayeweza kuapa vizuri",amesema Rais Magufuli.
0 comments:
Post a Comment