Sunday 29 August 2021

WIKI YA MWANANCHI YAKAMILIKA ZANACO YA ZAMBIA IKIICHAPA YANGA SC 2-1 MBELE YA MAELFU YA MASHABIKI


Ikiwa leo ndo kilele cha wiki ya mwananchi kwa mashabiki wa klabu ya Yanga ambapo sherehe hiyo imefanyika Jijini Dar es Salaam wamecheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Zanaco Fc ya nchini Zambia ambapo wamefungwa mabao 2-1 licha ya kipindi cha kwanza kuongoza.

Mchezo wa leo ulikuwa na ushindani mkubwa baada ya utambulisho wa wachezaji mbele ya mashabiki wengi waliojitokeza Uwanja wa Mkapa Jijini Dar es salaam.

Alianza Heritier Makambo kupachika bao dakika ya 30 lilikuja kusawazishwa kipindi cha pili Hakim Mniba na lile la pili lilifungwa na Kelvin Kapumbu dk 77.

Kelvin Kaindu, Kocha Mkuu wa Zanaco amesema kuwa mchezo ulikuwa na ushindani mkubwa kutoka kwa wapinzani wao.

Kilele cha Wiki ya Mwananchi kulikuwa na matukio mengi ikiwa ni pamoja na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali kama Nandy, Mopao, Juma Nature na Temba ambao walitoa burudani za kutosha.

Sherehe hiyo ilihudhuliwa na baadhi ya viongozi wakubwa Serikalini akiwmo Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla ambaye alipata fursa kuzungumza na mashabiki katika hafla hiyo.

Mashabiki waliojitokeza walikuwa wengi na licha ya timu yao kupoteza bado waliwashangilia wachezaji wao.
Share:

RAIS SAMIA APONGEZA JITIHADA ZA BENKI YA CRDB KUCHANGIA MAENDELEO KATIKA JAMII


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan (katikati) akikata utepe kuzindua Afisi ya Maendeleo kata ya Kizimkazi Dimbani na nyumba mbili za madaktari zilizonjengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB na kugharimu shilingi milioni 300. Wengine pichani ni, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Zanzibar, Haroun Ali Suleiman (watatu kulia), Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Rashid Hadid Rashid (wakwanza kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dkt. Ally Hussein Laay (wapili kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wapili kulia) na Mwenyekiti wa CRDB Bank Foundation, Martin Warioba (wa kwanza kulia).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan (watatu kulia) akikata utepe kuzindua Afisi ya Maendeleo kata ya Kizimkazi Dimbani na nyumba mbili za madaktari zilizonjengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB na kugharimu shilingi milioni 300. Wengine pichani ni, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Zanzibar, Haroun Ali Suleiman (wapili kulia), Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Rashid Hadid Rashid (wakwanza kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dkt. Ally Hussein Laay (watatu kushoto), Mwenyekiti wa CRDB Bank Foundation, Martin Warioba (watatu kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wanne kushoto).
Zanzibar, 28 Agosti 2021 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amepongeza jitihada zinazofanywa na Benki ya CRDB katika kuchangia maendeleo katika jamii. Rais Samia ametoa pongezi hizo wakati wa kilele cha Tamasha la Kizimkazi alipokuwa akikabidhiwa miradi ya nyumba za madaktari na ofisi za shehia Kizimkazi Dimbani zilizojengwa kwa udhamini wa Benki hiyo.

Akipokea miradi hiyo iliyo gharimu kiasi cha shilingi milioni 300, Rais Samia alisema Serikali inajivunia ushirikiano wa kimaendeleo baina yake na Benki ya CRDB. Aliongezea kuwa Benki hiyo imekuwa mfano mzuri wa ushirikiano wa sekta binafsi na sekta ya umma (PPP) katika kufikia malengo yaliyowekwa katika Dira ya Maendeleo ya 2025.
“Suala la kuijenga nchi yetu ni wajibu wa kila mmoja wetu na si la Serikali peke yake, niwapongeze Benki ya CRDB kwa kujitoa kwenu kutatua changamoto zilizopo katika jamii. Leo hii mmetutoa kimasomaso kwa kutusaidia kuimarisha sekta ya afya na kuhakikisha wananchi wa Kizimkazi Dimbani wanapata huduma bora za kijamii, ama hakika hii ni Benki ya kizalendo,” alisema Rais Samia.

Aidha, Rais Samia alisifu mafanikio ya Tamasha la Kizimkazi kwa mwaka huu 2021 ambalo lililenga katika kuhamasisha jamii kudumisha utamaduni na kuongeza ujumuishaji wa kiuchumi kwa wananchi kwa kuonyesha fursa mbalimbali zitokanazo na tamaduni za Kitanzania. Tamasha hilo lilihusisha mafunzo kwa wajasiriamali zaidi ya 500 juu ya ubunifu wa bidhaa za asili, elimu ya fedha na uendeshaji biashara, pamoja na michezo mbalimbali ya asili.
Pia alieleza kwamba wakati umewadia kwa Watanzania kuacha utamaduni wa kigeni na kujivunia utamaduni wetu. Alitoa rai kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuwa na mikakati mbalimbali itakayosaidia kutoa elimu juu ya umuhimu wa kuenzi na kulinda utamaduni wa Kitanzania. Rais Samia alisema jamii pia ina wajibu wa kushiriki kikamilifu katika matamasha ya utamaduni ili kusaidia ukuzaji na uendelezaji wa mfumo wa utamaduni na sanaa katika jamii ya Kitanzania.

“Benki ya CRDB imetuonyesha kwa mfano kuwa tukiwekeza katika utamaduni wetu tutafungua fursa nyingi za kiuchumi kwa kutengeneza soko kwa bidhaa zetu za asili na Sanaa yetu. Kupitia Tamasha hili la Kizimkazi niiombe Wizara iweke mikakati ya kuanzisha matamasha ya utamaduni katika kila kanda hii itasaidia kukuza tamaduni za maeneo mbalimbali na kuchochea utalii,” alisisitiza Rais Samia.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulamjaid Nsekela alisema utekelezaji wa miradi hiyo na uandaaji wa Tamasha hilo la Kizimkazi ambalo zamani lilikuwa likijulikana kama “Kizimkazi Day,” ni muendelezo wa utekelezaji wa Sera ya Benki hiyo ya uwekezaji katika jamii ambayo inaelekeza asilimia 1 ya faida ya Benki kila mwaka kwa ajili ya kusaidia jamii kupitia program bunifu za uwezeshaji.

Nsekela alisema Benki hiyo imedhamiria kwa dhati kusaidiana na Serikali kujenga uchumi jumuishi na kuwa utamaduni ni moja ya eneo ambalo Taifa likiwekeza vizuri linaweza kusaidia kuongeza uchumi wa mtu mmoja mmoja na Pato la Taifa kwa ujumla. “Pamoja na vijielezi vingi vya neno utamaduni, sisi Kama Benki ya kizalendo tunaamini kuwa; utamaduni ni ujasiriamali, utamaduni ni utalii, utamaduni ni ajira, utamaduni ni uchumi.”

Aidha Nsekela alibainisha kuwa Benki hiyo imedhamiria kuweka mchango wake katika pande zote za Muungano na hivyo kuchochea maendeleo ya Taifa. Akielezea mchango wa Benki hiyo katika kukuza uchumi wa visiwa vya Zanzibar, Nsekela alisema katika nusu mwaka 2021 pekee Benki ya CRDB imetoa zaidi ya shilingi bilioni 150 kuwezesha sekta mbalimbali za maendeleo ili kuwezesha ajenda ya Serikali ya kujenga Uchumi wa Buluu.

Alimwambia Mheshimiwa Rais, Benki hiyo pia inajivunia zaidi kuleta mapinduzi makubwa katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Mwaka 2014 Benki ya CRDB iliunganisha mfumo wake wa kielekroniki wa ukusanyaji mapato na mfumo wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar, ambapo ndani ya mwaka mmoja tu makusanyo yaliongezeka kwa zaidi 600%,” aliongezea.
Nsekela alimuahidi Mheshimiwa Rais kuwa Benki ya CRDB kupitia kauli mbiu yake ya “Tupo Tayari” itaendelea kushirikiana na Serikali na wadau wengine wa maendelo nchini ili kufikia malengo yaliyowekwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025.

Pamoja na mafunzo ya ujasiriamali yaliyoendeshwa na Benki ya CRDB, Tamasha la Kizimkazi pia lilijumuisha usafi wa mazingira, mashindano ya michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu na pete, kufua na kukuna nazi, nage, karata , bao, kuvuta kamba, resi za baskeli, resi za ngalawa, shomooo , na mashindano ya kuhifadhi Qurani.

Wananchi pia walipata fursa ya kupata chanjo ya UVIKO 19 ambayo itatolewa katika viwaja vya Kizimkazi Dimbani Mji Mpya, zoezi ambalo liliongozwa na Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mh. Ahmed Nassor Mazrui.

Kilele cha Tamasha la Kizimkazi kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, wakiwa kwenye sherehe hizo.
Share:

TAASISI YA IBRAHIM HAJJ, JUMUIYA KSIJ WACHANGIA DAMU DAR ES SALAAM


:Mtaalam wa Maabara kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama Kanda ya Mashariki, Gisbert Ruseneka, akimtoa damu, mmoja wa waumini wa Juimuiya ya Khoja Shia Ithnasheri Jamaat (KSIJ), wakati wa kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha kiongozi wa dhehebu hilo Imamu Hussein, kwenye msikiti wa KSIJ jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa waumini wa Juimuiya ya Khoja Shia Ithnasheri Jamaat (KSIJ) akishiriki katika zoezi la uchangiaji damu wakati wa kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha kiongozi wa dhehebu hilo Imamu Hussein, kwenye msikiti wa KSIJ jijini Dar es Salaam.
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Omary Kumbilamoto akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi la uchangiaji damu lilioandaliwa na Jumuiya Khoja Shia kwa kushirikiana na Taasisi ya Ibrahim Hajj.

 ***
WANACHAMA wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithna-Asheri Jamaat (KSIJ) kwa kushirikiana na Taasisi ya Ibrahim Hajj, wamejitolea kuchangia damu kwa Mpango wa Taifa wa Damu Salama, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Imamu Hussein.


Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Omary Kumbilamoto, alihudhuria hafla hiyo ya uchangiaji damu, iliyofanyika Msikiti wa KSIJ katikati ya jiji, ambako aliwapongeza Wana Jumuiya hao kwa kudumisha utamaduni chanya wa kusaidia wenye uhitaji ikiwemo uchangiaji damu huo.


Meya Kumbilamoto alibainisha kuwa, KSIJ na Ibrahim Hajj, wameionesha jamii ya Watanzania namna wanavyopaswa kujitoa kwa ustawi wa maisha wenye uhitaji, na kwamba damu iliyochangwa na Wana Jumuiya hao, inaenda kuokoa maisha Wengi miongoni mwa wahanga wa ajali, wamama wajawazito na wagonjwa wa kansa ya damu.


Kumbilamoto aliwapongeza KSIJ na Ibrahim Hajj na kuzitaka taasisi zingine na jamii kuiga utamaduni chanya unaofanywa na wanachama hao, ambao unalenga sio tu kuakisi yalivyokuwa maisha ya kiongozi wao Imamu Hussein, bali kuunga mkono jitihada za Serikali katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watu wake.


"Nitoe wito kwa jamii, kuiga mfano wa KSIJ na Ibrahim Hajj, ambao wamekuwa wakijitolea damu kila mwaka. Awali walikuwa wakitoa mara moja kwa mwaka kila wanapokuwa na maadhimisho haya, lakini Sasa wamekuwa wakichangia damu kila wanapoombwa kufanya hivi.


"KSIJ na Ibrahim Hajj, wameenda mbali zaidi kwa Sasa kwa kujitosa katika utatuzi wa changamoto mbalimbali, hasa zinazoikabili sekta ya Elimu na Afya nchini, walikotoa vifaa tiba, vifaa vya elimu na hata ujenzi na maboresho ya miundombinu kwenye Sekta hizo muhimu kwa maendeleo ya jamii," alisisitiza Meya Kumbilamoto.


Akizungumza kwa niaba ya KSIJ, Ain Sharrif, ambaye ni Mwanachama Mwandamizi Jumuiya hiyo, alisema utamuduni huo wa kuchangia damu wamekuwa wakiufanya kila (Mwezi Muharram) wanapoadhimisha kifo cha kiongozi wao Sayyidina Hussein (Imamu Hussein), aliyekufa kwa kujitoa mhanga yapata miaka 1400 iliyopita.


"Tumekuwa tukifanya hivi tangu mwaka 2008, lengo likiwa ni kuyaishi maisha ya Imamu Hussein, ambaye alisimama imara katika kujitolea kwa ustawi wa maisha ya aliowaongoza na jamii iliyomzunguka. Nasi tunafanya haya na mengineyo ili kufuata nyayo zake na kutii wosia zake.


"Leo tunavyo vituo vitatu vinavyochangia damu jijini Dar es Salaam, ambapo pia kupitia Hospitali ya Ibrahim Hajj tumekuwa tukisaidia mamia ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kwa kuwapatia misaada mbalimbali kulingana na mahitaji yao, sambamba na huduma za matibabu," alisema Sharrif.


Naye Mtaalamu wa Maabara ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Samuel Mluma, aliishukuru KSIJ na Taasisi ya Ibrahim Hajj kwa kuthamini na kuijali jamii ya wenye uhitaji na kujitolea kuchangia damu, ambayo mahitaji yake ni makubwa.


"Kila mwaka KSIJ na Ibrahim Hajj wamekuwa wakichangia zaidi ya Unit 400 za damu kupitia maombolezo yao haya ama tunapowahitaji.


"Mahitaji nchini ni makubwa, takribani chupa 250,000 kwa mwaka, kwahiyo tunapowapata watu na Taasisi za mfano wa Kama KSIJ na Ibrahim Hajj, tunakuwa na uhakika wa makusanyo ya kutosha kukidhi mahitaji," alisema Mluma
Share:

ULEGA AAGIZA WATENDAJI KUSIMAMIA MAELEKEZO YA VIONGOZI


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), akitoa maelekezo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko kutoka wizarani Bw. Stephen Michael pamoja na uongozi wa machinjio ya jiji la Dodoma kufanya ukarabati sehemu ya kupakia nyama machinjioni hapo mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza kufuatilia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa ya ukarabati wa machinjio hayo. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi).



Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), akitoa maelekezo kwa Kaimu Meneja Mkuu wa machinjio ya Jiji la Dodoma Bw. Fabian Maselele (kushoto), wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika machinjio hayo kufuatilia maagizo aliyoyatoa juu ya ukarabati wa machinjio hayo yaliyoanza Tarehe 15 Mwezi Julai mwaka huu ambapo hadi sasa zimetumika Shilingi Milioni 40. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi).
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) akikagua baadhi ya vifaa vipya vilivyowekwa katika machinjio ya Jiji la Dodoma, mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza kufuatilia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa ya ukarabati wa machinjio hayo. Kushoto kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko kutoka wizarani Bw. Stephen Michael. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi).

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), akitoa maelekezo kwa uongozi wa machinjio ya Jiji la Dodoma, kukarabati beseni la kuhifadhia damu mara baada ya ng’ombe kuchinjwa wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika machinjio hayo kufuatilia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa ya ukarabati wa machinjio hayo. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi).
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), akitoa maelekezo kwa uongozi wa machinjio ya Jiji la Dodoma, kukarabati sakafu ya jengo la machinjio hayo wakati alipofanya ziara ya kushtukiza machinjioni hapo kufuatilia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa ya ukarabati wa jengo hilo pamoja na vifaa vya machinjio. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi).



Na. Edward Kondela

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) amesema atahakikisha kila maelekezo anayoyatoa anayafuatilia kwa karibu ili kujiridhisha na utekelezaji wake na kufikiwa kwa malengo ya serikali.

Naibu Waziri Ulega amebainisha hayo (29.08.2021) wakati alipofanya ziara ya kushtukiza kujionea maendeleo ya ukarabati wa machinjio ya Jiji la Dodoma yaliyoanza Tarehe 15 Mwezi Julai mwaka huu.

Mhe. Ulega amesema ameridhishwa na ukarabati unaondelea kufanywa ambapo hadi sasa zimetumika Shilingi Milioni 40 kwa kutumia mapato ya ndani ya machinjio hayo.

“Kila maelekezo tunayoyatoa, tunayatoa kwa wakati maalum na kinachofuata ni ufuatiliaji wa karibu, tunatoa maelekezo na kufuatilia utekelezaji wake, tunawapongeza watendaji wetu wizarani maana kila maelekezo tunayoyatoa wanayasimamia na mnafanya kazi nzuri maelekezo tunayoyatoa mnayafanyia kazi.” Amesema Mhe. Ulega

Mhe. Ulega amesema alitoa maelekezo ya kuona machinjio ya jiji la Dodoma, yanabadilika na kuwa bora na kwamba ameridhika na ukarabati unaoendelea hadi sasa ambapo awali uongozi wa machinjio ulihitaji Shilingi Bilioni Tatu, lakini aliwaelekeza kuanza kufanya ukarabati kwa kutumia mapato ya ndani.

Amefafanua kuwa yeye kama kiongozi anatoa maelekezo na kuhakikisha yanasimamiwa usiku na mchana na kuyafuatilia hadi mwisho wake na kutaka maboresho hayo yawe yamekamilika kufikia Tarehe 15 Mwezi Septemba mwaka huu.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Stephen Michael amesema hadi sasa ukarabati wa machinjio ya Jiji la Dodoma yamefikia zaidi ya asilimia 90 ambapo maeneo 13 kati ya 15 yatakuwa yamekamilika mwisho wa mwezi huu na maeneo mawili yaliyobakia yatakamilika ifikapo Tarehe 15 Mwezi Septemba

Bw. Michael amesema ni muhimu kwa wao kama watendaji wanaposimamia maelekezo ya viongozi ni kwamba wanajua athari zinazoweza kujitokeza kutokana na ulaji wa nyama isiyo na usalama na kwamba watasimamia ukarabati huo kwa weledi mkubwa.

Share:

PAKUA APP YA MALUNDE 1 BLOG TUKUTUMIE HABARI ZINAZOENDELEA BURE MOJA KWA MOJA KWENYE SIMU YAKO

Share:

TAMBUA DALILI ZA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME NA TIBA YAKE


Upungufu wa nguvu za kiume ni hali ya kushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu ,shughuli ya tendo la ndoa huhusisha akili, homoni, neva, misuli, hisia na mirija ya damu. Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kutokuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalohitaji tiba.

CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Tatizo la nguvu za kiume lina vyanzo vingi ambavyo mara nyingi wengi huvipuuza, hivyo vyanzo huathiri taratibu na vingine huathiri haraka, tunashauri watu kuwa makini sana ili kujiimarisha vizuri. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata tatizo la nguvu za kiume nayo ni pamoja na;


1. Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P) au ugonjwa wa moyo

2. Kuvuta sigala na unywaji wa pombe

3. Uzito kupita kiasi na unene uliozidi

4. Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi

5. Kisukari

6. Kuwa na mawazo na wasiwasi

7. Matumizi ya madawa mbalimbali

8. Umri hasa wazee

9. Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili

10. Kuwa na tatizo la kibofu

11. Tabia za kujichua kwa muda mrefu

12. Kutopata usingizi kamili

13. Matumizi makubwa ya dawa zenye kemikali za kutibia magonjwa kama kansa, vidonda vya tumbo, moyo, kisukari, B.P, na magonjwa mengine


DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Dalili za kuonesha kuwa una tatizo la upungufu wa nguvu za kiume karibia zote zinahusiana na hali itakayo onekana katika tendo la ndoa au mda wa kujamiiana, hizo dalili zake ni kama;


1. Kuwahi kufika kileleni

2. Kukosa hamu ya mapenzi

3. Kushindwa kurudia tendo la ndoa

4. Uume kusimama kwa ulegevu au kushindwa kusimamisha

5. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu; Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo

7. Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa)

8. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji


TIBA SAHIHI YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME

FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50
⇨ Inarutubisha maumbile ya uume na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


Pia tunatibu Magonjwa mengine kama


Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonda vya tumbo, Kisukari, Magonjwa sugu ya zinaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kung’oa


Ndugu mteja Epuka midawa inayouzwa mitaani ambayo sio sahihi kwa matumizi ya binadamu JALI AFYA YAKO OKOA NDOA NA MAISHA YAKO


Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27 utatumiwa sehemu yoyote ulipo
Share:

WATUMISHI WA UMMA WILAYANI NACHINGWEA WAPATIWA ELIMU KUHUSU MADHARA YA MATUMIZI YA BIDHAA HAFIFU

Afisa usalama wa chakula (TBS) Bw.Barnabas Jacob akitoa elimu kuhusu madhara ya vipodozi vyenye viambata sumu kwa watumishi wa TANESCO,TRA, TTCL, NIDA na Benki ya Biashara ya Posta (TCB). Elimu hiI itawawezesha watumishi hao kuwa mabalozi wazuri ndani ya jamii na familia zao kwa ujumla kupinga matumizi ya bidhaa hizo. Afisa usalama wa chakula (TBS) Bw.Barnabas Jacob akitoa elimu kuhusu madhara ya vipodozi vyenye viambata sumu kwa watumishi wa TANESCO,TRA, TTCL, NIDA na Benki ya Biashara ya Posta (TCB). Elimu hiI itawawezesha watumishi hao kuwa mabalozi wazuri ndani ya jamii na familia zao kwa ujumla kupinga matumizi ya bidhaa hizo. Watumishi wa TANESCO,TRA, TTCL, NIDA na Benki ya Biashara ya Posta (TCB) wakipata kuhusu madhara ya vipodozi vyenye viambata sumu kutoka kwa Afisa usalama wa chakula (TBS) Bw.Barnabas Jacob (hayupo pichani).




Na Mwandishi Wetu, Nachingwea

WATUMISHI wa umma katika taasisi mbalimbali wilayani Nachingwea mkoani Lindi, wamepatiwa elimu kuhusu madhara ya matumizi ya bidhaa hafifu hususani vipodozi ambavyo vimekatazwa kutumika nchini kutokana na kuwa na viambata sumu.

Mafunzo hayo kwa watumishi wa umma wilayani Nachingwea yametolewa kwa siku mbili na maofisa wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa lengo la kuwawezesha kuwa mabalozi ndani ya jamii kwa kupinga matumizi ya bidhaa hafifu, hususani vipodozi.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mafunzo hayo, Afisa Usalama wa Chakula wa TBS, Barnabas Jacob alisema mbali na kuelimishwa madhara ya bidhaa hafifu za vipodozi na vyakula, lakini pia wameelimishwa kuhusiana na majukumu ya shirika hilo.

Kwa mujibu wa Jacob miongoni mwa watumishi waliopatiwa elimu hiyo ni wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Benki ya ya Posta (TPB), Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) na wale wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Jacob alifafanua kwamba elimu hiyo itawawezesha watumishi hao kuwa mabalozi wazuri ndani ya jamii na familia zao kwa ujumla.

"Kwa hiyo elimu hii imelenga taasisi za umma ikiwa ni mwendelezo wa shirika kutoa elimu kwa umma kuhusiana na madhara ya vipodozi na vyakula vilivyopigwa marufuku," alisema Jacob na kuongeza;

"Tumeona tukitoa elimu hii kwa watumishi wa umma ana kwa ana inaweza kuwasaidia moja kwa moja hadi kwenye familia zao,majirani ,jamii kuhusu madhara ya vipodozi vyenye viambata vya sumu."

Alisema shirika haliwezi kushinda vita hiyo bila wananchi kupewa na elimu, ndiyo maana wameona wafike kwenye taasisi za umma ili kutoa elimu kwa watumishi kuhusu madhara ya kutumia bidhaa hafifu zilizokatazwa nchini zikiwemo za vipodozi na vyakula.

Kupitia mafunzo hayo watumishi hao wameelimishwa madhara ambayo mtu anapata iwapo anatumia vipodozi vyenye viambata sumu kwa muda mrefu.

Alitaja madhara makubwa ambayo anaweza kupata ni kuwashwa kwenye ngozi, kuvimba,ngozi kuharibika kuchanikachanika,madhara katika mfumo wa uzazi kwa mwanamke na hata kupelekea kupata kansa ya ngozi.

"Lakini viambata sumu vilivyomo kwenye vipodozi vilivyopigwa marufuku vinaweza kuingia ndani ya mwili na kuathiri viungo vya ndani, mfano maini, figo na wakati mwingine baadhi ya kemikali zinaweza zikaenda hadi kwenye mfumo wa uzazi kwa hiyo hayo madhara yanaenda hadi kwa watoto" alisema Jacob.

Alipoulizwa ni kwa jinsi gani watumishi hao walivyopokea mafunzo hayo, Jacob alisema wamefurahi sana na wameahidi kueneza elimu hiyo kwa familia zao, majirani na jamii kwa ujumla .

Wakati huo huo maofisa hao wa TBS wamefanya ukaguzi madukani kwa ajili ya kuondoa kwenye soko bidhaa zilizoisha muda wake na pamoja na zile zilizopigwa marufuku nchini.

"Tuna utaratibu wa kupita kwenye masoko kuangalia bidhaa na tukikuta zimeisha muda wake tunaziondoa na vipodozi vyenye viambata sumu tunavikamata na kuviondoa sokoni," alisema Jacob

Aidha, maofisi hao walitembelea wajasiriamali pamoja na wenye viwanda na kuzungumza nao katika maeneo yao ya biashara kwa lengo la kuwahamasisha wajitokeza TBS kupata alama ya ubora.

Alitoa wito kwa wajasiriamali na wenye viwanda wilayani Nachingwea kujitokeza TBS kwa ajili ya kupata alama ya ubora ambapo huduma hiyo hutolewa bure bila gharama zozote Kwa wajasiriamali wadogo na wa kati kwa kupitia Shirika la kuhudumia viwanda vidogo vidogo SIDO.
Share:

Isakamaliwa Secondary School

About Isakamaliwa Secondary School Isakamaliwa Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S1991 – Known as Shule ya Sekondari Isakamaliwa Secondary School Isakamaliwa Secondary School is located at Tabora. Isakamaliwa Secondary School is boys and girls school and it is doing well in Kiswahili, […]

This post Isakamaliwa Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Usongelani Secondary School

About Usongelani Secondary School Usongelani Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S1990 – Known as Shule ya Sekondari Usongelani Secondary School Usongelani Secondary School is located at Tabora. Usongelani Secondary School is boys and girls school and it is doing well in Kiswahili, […]

This post Usongelani Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Lupunga Secondary School

About Lupunga Secondary School Lupunga Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S1989 – Known as Shule ya Sekondari Lupunga Secondary School Lupunga Secondary School is located at Ruvuma. Lupunga Secondary School is boys and girls school and it is doing well in Kiswahili, […]

This post Lupunga Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI AGOSTI 29,2021


Share:

ALIYETAKA KUJILIPUA KWENYE MAZISHI YA KIGOGO WA POLISI AKAMATWA


Mshambuliaji anayeshukiwa kuwa wa kujitoa muhanga amekamatwa nchini Uganda kwa kupanga kujilipua katika mazishi ya kamanda wa jeshi anayefahamika kama ‘they lion of Mogadishu’’.

Meja Jenerali Paul Lockech alipewa jina hilo la bandia tangu wakati alipokuwa Mkuu wa kikosi cha Muugano wa Afrika kilichopo nchini Somalia (Amisom) kuanzia mwaka 2000. Alisifika kwa kuwaondosha wanamgambo wa al-Shabab katika mji mkuu Mogadishu.

Amisom kilisema kuwa itamkumbuka kama “ mnara wa ishara ya heshima katika mapigano dhidi ya wanamgambo wenye silaha” , na kwamba atakumbukwa kama urithi ambao hauwezi kusahaulika.

Meja Jenerali Lokech mwenye umri wa miaka 55, ambaye alikuwa anafanya kazi akiwa Inspekta Jenerali wa polisi alifariki kutokana na ugonjwa wa kuganda kwa damu nyumbani kwake siku ya Jumamosi.

Rais Yoweri Museveni amekuwa akitarajiwa kuhudhuria mazishi yake katika wilaya ya kaskani Mwa nchi hiyo ya Pader. Mshukiwa alikamatwa Alhamisi mchana katika operesheni ya pamoja baina ya maafisa mbalimbali wa usalama.

Msemaji wa jeshi Flavia Byekwaso amesema kuwa alipatikana na zana za kutengeneza mabomu, ikiwa ni pamoja na mabegi ya mabomu, fulana za mabomu ya kujitoa muhanga, na kifaa cha kukata waya wa kulipua mabomu. Washukiwa wenzake pia wametambuliwa na operesheni bado inaendelea ili kuwapata, alisema.
Share:

Saturday 28 August 2021

Mwega Secondary School

About Mwega Secondary School Mwega Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S1970 – Known as Shule ya Sekondari Mwega Secondary School Mwega Secondary School is located at Morogoro. Mwega Secondary School is boys and girls school and it is doing well in Kiswahili, […]

This post Mwega Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Dunda Secondary School

About Dunda Secondary School Dunda Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S1969 – Known as Shule ya Sekondari Dunda Secondary School Dunda Secondary School is located at Pwani. Dunda Secondary School is boys and girls school and it is doing well in Literature […]

This post Dunda Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Msata Secondary School

About Msata Secondary School Msata Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S1968 – Known as Shule ya Sekondari Msata Secondary School Msata Secondary School is located at Pwani. Msata Secondary School is boys and girls school and it is doing well in Kiswahili, […]

This post Msata Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Changalikwa Secondary School

About Changalikwa Secondary School Changalikwa Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S1967 – Known as Shule ya Sekondari Changalikwa Secondary School Changalikwa Secondary School is located at Pwani. Changalikwa Secondary School is boys and girls school and it is doing well in Kiswahili, […]

This post Changalikwa Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Miburani Day Secondary School

About Miburani Day Secondary School Miburani Day Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S1966 – Known as Shule ya Sekondari Miburani Day Secondary School Miburani Day Secondary School is located at Dar es salaam. Miburani Day Secondary School is boys and girls school […]

This post Miburani Day Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 02

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger