Friday 14 May 2021

MAZISHI YA MKURUGENZI WA PRINCESS RECORDS 'CHIEF CHRISS' KUFANYIKA KESHO LALAGO MASWA

Chief Chriss enzi za uhai wake
***
Mazishi ya Mwili wa Mkurugenzi wa Studio ya Princess Records, Christopher Joseph Mayenga maarufu Chief Chriss aliyefariki dunia Mei 12,2021 yanatarajiwa kufanyika kesho Jumamosi Mei 15,2021 mchana katika makaburi ya Mwandete Lalago wilayani Maswa mkoani Simiyu.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 14,2021




















Share:

Thursday 13 May 2021

Taarifa Ya Chama Cha Mapinduzi Kuhusu Mwenendo Wa Kampeni Za CCM Majimbo Ya Buhigwe Na Muhambwe Kuelekea Uchaguzi Wa Marudio


Chama Cha Mapinduzi kilifanya uzinduzi wa kampeni za ubunge katika Jimbo la Muhambwe tarehe 4 Mei 2021 na Jimbo la Buhigwe tarehe 5 Mei 2021 ukiongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Ndugu Kassim Majaliwa.

Chaguzi hizi ni kutokana na kufariki kwa Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Ndg. Atashasta Nditye na Mbunge wa Buhigwe, Ndugu Philip Mpango aliyeteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ifuatayo ni tathimini fupi ya Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa marudio katika majimbo hayo ya Muhambwe na Buhigwe.

Lengo kubwa la kampeni za CCM ni kutekeleza majukumu yafuatayo;

i.    Kutangaza Sera na Ilani ya CCM, kuwaeleza wananchi jinsi tulivyojipanga kuwaletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

ii.    Kuwanadi kwa wananchi (wapigakura) wagombea wetu Dkt Frolence George Samizi wa Jimbo la Muhambwe na Mwalimu Eliadory Felix Kavejuru wa jimbo la Buhigwe.

Majimbo ya Buhigwe na Muhambwe ni ya CCM. Tulipoteza Mbunge wa CCM kwa kifo kule Muhambwe, hivyo wananchi wanachokitaka ni kuifariji CCM. Kwa Jimbo la Buhigwe wananchi wenyewe wanataka kumpa ahsante Mhe Rais Samia kwa kumteua Makamu wa Rais aliyekuwa mbunge wao Dkt Philip Mpango.

CCM imedhihirisha kivitendo uwezo wake mkubwa wa kuwatumikia wananchi katika awamu zote za uongozi. Kazi kubwa ya kisera na utekelezaji wa miradi, kuondoa kero imefanyika  chini ya CCM kwenye majimbo ya Muhambwe na Buhigwe hivyo ushindi wa CCM ni jambo lisilo na shaka  wala wasiwasi.

Mfumo wa Kampeni kwa Wagombea wetu ulijielekeza katika kufanya zaidi mikutano midogo, kukutana na kuzungumza na makundi ya kijamii katika maeneo yao/makazi/vijiji vyao.

Dkt Florence George Samizi amefika katika Kata zote 19 na amefanya mikutano midogo ya Kampeni na kukutana na makundi maalum ya Vijana, Wanawake, Wazee, Wafanyabiashara na makundi mengine ya kijamii. Wakati wote wa kampeni wananchi wamejitokeza kwa wingi kuhudhuria katika mikutano yetu ya Kampeni jimboni humo na kuonyesha matarajio yao kwa mgombea wa CCM Dkt Samizi.

Ndg  Eliadory Felix Kavejuru amefanya kampeni katika Kata zote 20, na kukutana na wananchi katika Vijiji 44 sawa na asilimia 100 ya vijiji vyote na anaendelea kumalizia kampeni katika vitongoji vinane (8) vilivyobaki kati ya 192.

Mikutano mikubwa imefanywa kimkakati katika viwanja vya Shule ya Msingi Buhigwe, Munanila, na Muyama maeneo hayo yana wakazi wengi  waliojiandikisha katika kupiga  kura. Mikutano midogo 62 aliyoifanya Mgombea wa CCM Ndugu Kavejuru pamoja na mazungumzo mahsusi na makundi ya kijamii yamemkutanisha na kumpa uhakika zaidi wa kupata ushindi .

Chama kimezishirikisha Jumuiya  zake zote katika kampeni za majimbo ya Muhambwe na Buhigwe pamoja na kuwatumia makada wake mbali mbali ambao wote tulia na lengo moja la kupata ushindi.

Viongozo na Makada hao wamekuwa wakihutubia mikutano  ya hadhara kwa kutumia sera za chama Sera nzuri za CCM ambazo zimekuwa zikitekelezeka na kuleta manufaa kwa wananchi

Kampeni za CCM katika Majimbo yote mawili zitafungwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Nd. Philip Isdor Mpango tarehe 14 na 15 Mei 2021 katika uwanja wa Taifa kwa jimbo la Muhambwe na uwanja wa shule ya Mayama kwa jimbo la Buhigwe.

Tathmini ya awali imeonesha katika majimbo hayo CCM itashinda si chini ya 80% na ikumbukwe ushindi huu hautakuwa mgeni kwetu kwani CCM ni kinara na baba wa mageuzi ya demokrasia ya nchini, Afrika Mashariki na Kati.

Nilisema Siku ya uzinduzi na ninaendelea kusisitiza CCM itashinda Buhingwe na Muhambwe  kwa haki, amani na utulivu mkubwa pamoja na yote lakini ya sababu kubwa za ushindi ni imani kubwa walionayo wananchi kwa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na Chama Cha Mapinduzi.

Chini ya Uenyekiti wa CCM wa ndugu Samia Suluhu Hassan tutaendelea kuvilea vyama vya siasa chini ili viendelee kufanya siasa safi na yenye tija kwa Taifa baada ya kufanya siasa za danadana. Sote tunajenga nyumba moja hakuna sababu kugombeana fito.

Ikumbukwe kuwa tokea siasa za nchi hii kuanzia TANU hatimae CCM Chama chetu hakijawahi kufanya makosa katika mambo ya msingi yanayohusu maslahi ya Taifa tunakumbusha kuwa uchaguzi wa Buhingwe na Muhambwe umebeba maslahi mapana ya Taifa kwa maana unakwenda kuzalisha wabunge wanakwenda kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan katika kuleta maendeleo endelevu ya kiuchumi, kijamii na kisiasa hivyo hatuwezi kufanya makosa.

Tumejipanga kuhakikisha Wanachama wetu waliojiandikisha wanajitokeza kwa wingi katika vituo vya kupigia kura na kuwachagua Wabunge wanaotokana na Chama chao pendwa.

Aidha tunatoa wito kwa vyama vingine na wananchi kwa ujumla kuendelea kudumisha  amani, usalama na utulivu ambao umekuwepo  wakati wote wa kampeni zetu.

Imetolewa na;

SHAKA HAMDU SHAKA
KATIBU WA H/KUU - ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI
13 MEI 2021


Share:

Waziri Mchengerwa Azitaka Taasisi Za Kifedha Kutoa Mikopo Kupitia Hatimiliki Zinazotolewa Na MKURABITA

 


Na. James K. Mwanamyoto-Zanzibar
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amezitaka taasisi za kifedha nchini kutoa mikopo kwa wananchi wenye hatimiliki za kimila zinazotolewa na Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) ili kuwawezesha wananchi hao kuendesha shughuli zao na kuinua kipato.

Akikabidhi hatimiliki hizo kwa baadhi ya wananchi wa Shehia ya Welezo, Zanzibar, Mhe. Mchengerwa amesema, hatimiliki hizo zinalenga kutoa fursa kwa wananchi kupata mikopo itayowawezesha kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo na biashara ili kuboresha maisha yao.

“Taasisi za kifedha zitambue hatimiliki hizi na kupunguza masharti ili kuwawezesha wafanyabiashara wadogo kukopa na kuongeza mtaji.” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Akiwa katika kituo Jumuishi cha Urasimishaji na Uendelezaji Biashara kilichoko katika Baraza la Biashara, eneo la Darajani Wilaya ya Mjini, Mhe. Mchengerwa amezitaka pia taasisi za kifedha kutoa mikopo kwa wajasiriamali waliorasimisha biashara zao na kuongeza kuwa, mikopo hiyo itawaongezea mitaji ya kuendesha shughuli zao za ujasiriamali.

Kutokana na uwepo wa kituo hicho, Mhe. Mchengerwa amehimiza zoezi la urasimishaji biashara lisichukue muda mrefu ili kutoa hamasa kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kurasimisha biashara zao.

Akieleza mchango wa ofisi yake katika zoezi la urasimishaji biashara, Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum amesema kituo hicho kimejengwa ili kuondoa changamoto za urasimishaji walizokuwa wakikutana nazo wafanyabiashara wadogo.

Dkt. Salum ameongeza kuwa kutokana na faida za uwepo wa kituo hiki, Serikali imedhamiria kujenga kituo kama hiki Pemba ili wananchi wa eneo hilo nao waweze kunufaika.

Naye Mratibu wa Mkurabita, Dkt. Seraphia Mgembe amesema utekelezaji wa MKURABITA Zanzibar umewanufaisha wananchi wa Zanzibar kwa kuwapatia mafunzo ya utunzaji wa kumbukumbu za biashara ambapo hivi sasa wanazo takwimu sahihi za maendeleo ya biashara zao.

Mhe. Mchengerwa amehitimisha ziara yake ya kikazi Zanzibar ya kukagua miradi inayotekelezwa na taasisi zilizo chini ya ofisi yake ikiwa ni pamoja na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa Sekretarieti ya Ajira ofisi ya Zanzibar.


Share:

Wizara ya Maliasili na Utalii Yafungua Milango Mipya Ya Uwekezaji Katika Maeneo Ya Uhifadhi Nchini


Wizara ya Maliasili na Utalii imefungua milango mipya katika Sekta ya Utalii nchini kwa kutia saini ya  Uwekezaji wa kimkakati katika  maeneo ya Uhifadhi nchini kwa Wawekezaji wenye mitaji mikubwa wa kutoka ndani na nje ya nchi.

Ameyasema hayo leo Jijini Dodoma, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro   wakati akitia saini  kanuni za Uwekezaji wa kimkakati katika maeneo ya Uhifadhi nchini.

Waziri wa Maliasili na Utalii amesema utiaji saini huo ni miongoni mwa  njia  zitakazochangia kuongeza idadi ya Watalii kufika milion 5  na mapato yapatayo bilion 6 ifikapo mwaka 2025 kupitia Sekta ya Utalii nchini.

Kwa mujibu wa Kanuni hizo Wawekezaji wataweza kuwekeza katika maeneo ya Mapori ya Akiba, Mapori Tengefu pamoja na Maeneo ya Wazi ya Wanyamapori kwa miaka isiyopungua 25.

Akizungumza kabla ya utiaji saini huo, Waziri Dkt.Ndumbaro amesema kanuni hizo zimelenga Wawekezaji wenye mitaji mikubwa ambao hata watalii watakaokuja katika maeneo hayo ni Watalii wenye fedha nyingi ikiwemo watu maarufu duniani.

Amesisitiza kuwa kanuni hizo zitawezesha Wawekezaji hao kujenga mahoteli katika maeneo ya Uhifadhi pamoja na kuweka miundombinu ya Utalii itakayosaidia kuwavutia Watalii wengi kutembelea katika maeneo hayo.

Awali amesema kanuni hizo ni mpya na uwekezaji huo katika maeneo hayo utakuwa wa aina yake kwa vile umelenga Wawekezaji wenye mitaji mikubwa watakaowavutia Watalii matajiri hali itakayopelekea pato la taifa kuongezeka maradufu kupitia sekta ya utalii nchini.

Awali Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania ( TAWA) Meja Jenerali ( Mstaafu)  Hamis Semfuko amesema utiaji saini wa kanuni  ni moja ya hatua muhimu ya kupanua fursa zitokanazo na sekta ya utalii nchini.

” Tuliamua kuja na wazo hili ili Wawekezaji wenye mitaji mikubwa waweze kuwekeza katika maeneo ya Uhifadhi ambapo awali uwekezaji wa namna hii ulikuwa hauwezekani” alisisitiza Mwenyekiti huyo Meja Jenerali ( Mst) Semfuko

Kwa upande wake , Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt.Allan Kijazi amesema atahakikisha Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, ( TFS ) nao wanasaini kanuni za namna hiyo nao waweze kuwavutia Wawekezaji kuwekeza katika maeneo yao kwa vile wa maeneo yenye sifa kawa yalivyo ya TAWA


Share:

Zaidi Ya Bilioni 7 Zatumika Kufikisha Umeme Kisiwa Kilichopo Ziwa Tanganyika


Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kupitia Nakuroi Investment Co. Ltd inayotekeleza Mradi wa awamu ya tatu mzunguko wa kwanza wanaendelea na zoezi la kulaza nyaya chini ya maji katika ziwa Tanganyika ili kufikisha umeme katika kisiwa cha Mandakerenge, kilichopo kata ya Kipili Wilayani Nkasi, Mkoani Rukwa.

Zoezi hilo litakalogharimu zaidi ya shilingi bilioni 7 ni la kipekee kufanyika katika ziwa Tanganyika, na mikoa ya kanda ya ziwa, hali iliyopelekea Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mwanza na timu kutoka makao makuu ya Shirika la umeme nchini (TANESCO) kufika katika eneo hilo na kujifunza utandazaji wa nyaya hizo ili kuja kuutumia ujuzi huo kufikisha umeme kisiwani Ukerewe, Mkoani Mwanza.

Akiongea wakati wa kushiriki kulaza nyaya hizo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amesema kuwa tukio hilo linaonesha ni kwa namna gani serikali inavyowatahamini wananchi wake na kuzingatia haki zao za kupata huduma za kijamii saw ana watu wanaoishi katika mengine ya nchi.

Aidha amewapongeza wazamiaji wazawa wanaofanya kazi hiyo, TANESCO Mkoa Pamoja na Mkandarasi wa Mradi huo pamoja na kuwaomba wananchi wa kisiwa na Kijiji cha Mandakerenge kuutumia umeme huo vizuri ikiwa ni pamoja na kuanzisha viwanda vya kuchakata samaki pamoja na mashine za kusaga na kukoboa

“Serikali ya Tanzania inathamini wananchi popote pale walipo na umeme huu utakwenda kila mahali ndani ya vijiji vyetu vya mkoa wa Rukwa, baada ya kufikisha umeme katika kisiwa cha Mandakerenge itakuwa ni takriban vijiji 181 vitakuwa vimefikiwa na umeme na nimeambiwa huyu mkandarasi Nakuroi amebakiza kama vijiji viwili vitatu ili vitimie vijiji 184 ambavyo vitakuwa vinapata umeme na vijiji vinavyobaki kama 155, hivi vijiji vitapata umeme ndani ya kipindi cha mwaka mmoja na nusu,” Alisema.

Amesema kuwa katika ya vijiji hivyo 155 vilivyobaki, vijiji 125 vimeingizwa katika mradi wa awamu ya tatu mzunguko wa pili na vijiji 30 vimeingia kwa maombi maalum na hivyo kufanya jumla ya vijiji vya mzunguko wa kwanza na wapili kuwa 339 ambavyo ni idadi ya vijiji vilivyopo mkoani Rukwa.

Kwa upande wake Meneja wa TANESCO Mkoa wa Rukwa Mhandisi Yusuf Ismail alieleza kuwa zoezi hilo lilitakiwa kukamilika ndani ya wiki nne lakini kutokana ushiriki mzuri wa wanakijiji katika mradi, hali nzuri ya hewa ziwani Pamoja na kasi ya kazi hiyo huenda zoezi hilo likamalizika chini ya muda uliopangwa.

“Serikali imewashirikisha wananchi ili kwanza wajue thamani ya mradi ambayo imewekezwa hapa lakini pia iwe ni kutoa elimu kwa wavuvi wengine au kwa wananchi wengine ambao wako ng’ambo ambao wanaweza kukutana na kitu kama hiki wajue thamani yake, mheshimiwa mkuu wa mkoa naomba nikushuruku kwa kuja kutupa moyo katika kazi hii naamini wazamiaji na wafanyakazi wote wa TANESCO tumfurahia ujio wako,” Alimalizia.

Kwa upande wake mwakilishi wa mkandarasi wa mradi huo wa REA Mkoani Rukwa Mhandisi Pascal Ndunguli alisema kuwa kwa upande wao walikabdihiwa kukamilisha mradi huo katika vijiji 137 na kati yahi vyo vijiji 135 tayari vimewashwa umeme na hivyo kubakiwa na vijiji 2 kimojawapo kikiwa ni hicho cha kisiwa cha Mandakerenge ambacho wanatazamia kukimaliza kabla ya mwezi wa sita mwaka huu.

“Mpaka sasa tupo hatua ya kulaza nyaya na baada ya hapo, wazamiaji watakuwa hawana kazi watafuata watu wa kitengo cha umeme na hivyo wahandisi watakuja kwaajili ya kukamilisha zoezi na baada ya hapo tutawaalika TANESCO kuja kufanya majaribio na kuthibitisha kuwa umeme unapita na kisha tutafikisha umeme katika Kijiji hicho na umeme utaanza kufanya kazi,” Alisema.

Katika ziara hiyo alikuwepo mwakilishi wa wavuvi na wanakijiji cha Kijiji cha Mandakerenge Seif Seba ambaye naye alitoa shukurani kwa serikali ya Tanzania, “Tunatoa shukurani za dhati kwa serikali yetu kwa kutujali kwa suala la kutuletea umeme hapo kisiwani na tunaiahidi serikali kuwa tutaulinda huu way ana hakuttotokea athari ya namna yoyote,” Alimalizia.

Kisiwa cha Mandakerenge kipo umbali wa km 1.2 kutoka bara ambapo shughuli kubwa za wanakijiji wa kisiwa hicho ni uvuvi na TANESCO wametandaza waya wenye urefu wa km 1.7 kutoka bara kwenda kisiwani ili wanakijiji hao nao wafaidike na mradi huo.


Share:

Taarifa Ya Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya


KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA WA MATUKIO YA UVUNJAJI NA WIZI.


Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa wawili 1. KELVIN TOBIAS [32] fundi kuchomelea, mkazi wa Iyela na 2. JOSHUA AMBAKISYE [18] mkazi wa Mwanjelwa jijini Mbeya kwa tuhuma za kujihusisha na matukio mbalimbali ya uvunjaji na wizi katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Mbeya.

Watuhumiwa wamekamatwa katika misako inayoendelea katika maeneo mbalimbali ndani ya Jiji la Mbeya na wamekiri kujihusisha na matukio ya uvunjaji na wizi. Katika upekuzi uliofanywa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya katika maeneo ambayo watuhumiwa wamekiri kuuza mali za wizi, mali zifuatazo zimepatikana:-
  1.     Kompyuta 2 [Desk top] aina ya HP,
  2.     Laptop 2 aina ya HP na Dell.
  3.     CPU 2 aina ya Dell,
  4.     TV flat screen aina ya Hicence inchi 55,
  5.     TV flat screen aina ya LG inchi 32,
  6.     TV flat screen aina ya Singsung inchi 32,
  7.     TV flat screen aina ya Samsung inchi 32,
  8.     Mitungi miwili mikubwa ya gesi Oryx,
  9.     Mitungi mitatu midogo ya gesi Oryx,
  10.     Redio Sub-woofer 6 aina tofauti,
  11.     Jiko moja la Gesi aina ya Afrox,
  12.     Blanketi 13,
  13.     Saa 2 za ukutani na
  14.     Redio 2 mali ya wizi.

Upelelezi unaendelea ili kubaini mtandao mzima wa matukio ya uvunjaji na wizi wa mali mbalimbali. Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa wananchi walioibiwa mali zao kufika kituo kikuu cha Polisi Mbeya Mjini kwa ajili ya  utambuzi wa mali zao.

KUKAMATWA KWA MTUHUMIWA WA TUKIO LA MAUAJI.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa GODLOVE PIMBI [50] Mkazi wa Lusonjo – Kisyosyo kwa tuhuma za mauaji ya mke wake aitwaye ELIZABETH MWAIKE [22] Mkazi wa Lusonjo – Kisyosyo.

Tukio hili limetokea mnamo tarehe 11.05.2021 nyumbani kwa mtuhumiwa huko Kijiji cha Kisyosyo kilichopo Kata ya Matema, Tarafa ya Ntebela, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya.   

Chanzo cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi. Mwili wa marehemu ulikutwa umbali wa mita 500 kutoka nyumbani kwake ukiwa na jeraha la kupigwa na kitu kizito kichwani. Upelelezi wa tukio hili unaendelea na mara baada ya kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ULRICH MATEI anatoa rai kwa jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi dhidi ya migogoro ya kimapenzi na badala yake watafute suluhisho kwa kukaa meza moja ya mazungumzo ili kutatua migogoro hiyo.

ASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA MAUAJI.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia CHIKU ABOUBAKARI [41] Mkazi wa DDC – Mbalizi kwa tuhuma za mauaji ya ROSE MWANDANJE [45] Mfanyabiashara na Mkazi wa DDC – Mbalizi.

Tukio hilo limetokea tarehe 11.05.2021 majira ya saa 20:00 usiku huko Mtaa wa DDC – Mbalizi uliopo Kata ya Utengule – Usongwe, Tarafa ya Usongwe, Wilaya ya Mbeya Vijijini, Mkoa wa Mbeya ambapo marehemu ROSE MWANDANJE [45] Mkazi wa DDC – Mbalizi aliuawa kwa kukatwa panga sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo nyuma ya shingo na viganja vya mikono yote kutoka na mtu / watu wasiofahamika akiwa sebuleni katika nyumba anapoishi.

Chanzo cha tukio hilo kinachunguzwa. Jeshi la Polisi mkoani hapa linaendelea na msako mkali dhidi ya watuhumiwa wengine waliohusika katika tukio hilo la kinyama. Aidha Jeshi la Polisi linaendelea kutoa rai kwa wananchi na watendaji wa mitaa kutoa ushirikiano kwa kuwafichua wahalifu ili wakamatwe na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

MTU MMOJA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKIWA NA KIFUSI.

Mtu mmoja aitwaye MWASHALA NYUNDURU [32] Mkazi wa Kabwe Jijini Mbeya alifariki dunia baada ya kuangukiwa na kifusi cha mchanga akiwa anafanya shughuli za uchimbaji mchanga katika eneo la Shewa.

Tukio hili limetokea tarehe 11.05.2021 majira ya saa 17:33 jioni huko maeneo ya Mtaa wa Shewa, Kata ya Mwakibete, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya wakati marehemu akiendelea na shughuli za uchimbaji mchanga akiwa na wenzake. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ULRICH MATEI anatoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari wakiwa katika shughuli za uchimbaji ili kuepuka madhara yanayoweza kuepukika hasa katika kipindi hiki ambacho mvua za mwishoni zinaendelea kunyesha.



Share:

SUPER – NHESHA: Dawa Bora Ya Kutibu Tatizo La Kisukari


SUPER – NHESHA
Ni dawa ya kutibu tatizo la sukari au jina la kitaalamu (Diabetes Mellitus) ni kundi la magonjwa yanayohusiana na ufanyaji kazi wa mwili ambapo Mtu anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya Glucose katika mwili kutokana na mwili wake kukosa uwezo wa kutengeneza Insulin ya kutosha au seli za mwili wake kutumia insulin iliyopo au pengine mwili kuwa na matatizo yote kwa pamoja na kupelekea mgonjwa wa sukari kupata haja ndogo mara kwa mara (Polyuria) uhisi kiu kila wakati (Polydipsia) Na (Polyphagia).


AINA YA KISUKARI
Kuna aina chache tofauti za ugonjwa wa kisukari (1) ni ugonjwa wa Auto hii aina mgonjwa wa Auto hushambulia mfumo wa kinga na kuharibu seli katika kongosho ambako insulin huzalishwa asilimia 10% ya watu wenye ungonjwa wa kisukari wanayo aina hii (Auto).


AINA YA PILI
Hii hutokea wakati mwili wako unakuwa sugu kwa insulin na sukari hujenga katika damu yako hii husababishwa na kuwa na sukari nyingi kwenye damu yako kuliko kawaida.


CHANZO CHA UGONJWA SUKARI
Viko vyanzo vingi mbalimbali vya sukari
1.     Shinikizo la damu (B.P)
2.     Viwango vya juu vya triglyceride (mafuta)
3.     Lishe yenye mafuta mengi na wanga
4.     Utumiaji mkubwa wa pombe kupita kiasi
5.     Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi
6.     Mtindo wa maisha usiofaa kiafya
7.     Uzito na unene uliozidi
8.     Kutofanya mazoezi
9.     Umri
10.     Kurith


UNAJUAJE KUWA UNADALILI ZA KISUKARI
1.     Kusikia njaa mara kwa mara
2.     Kusikia kiu mara kwa mara
3.     Kupungua uzito
4.     Maono machafu
5.     Uchovu mara kwa mara
6.     Ukipata kidonda hakiponi
7.     Kushuka kwa kinga mwili


DALILI ZA KISUKARI KWA MWANAUME
Mbali na dalili za jumla za ugonjwa wa sukari wanaume wenye tatizo hilo wanakuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kushindwa kufanya tendo la ndoa uume hushindwa kusimama misuri hulegea na kusinyaa, maumivu ya mgongo, kiuno, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kupata choo  kama cha mbuzi


DALILI ZA WANAWAKE
Wanawake wenye ugonjwa wa sukari wanaweza pia kuwa na dalili kama vile maambukizi kwa njia ya mkojo (U.T.I) maambukizi  ya gonzi kukakamaa


TIBA YA MAGONJWA YA SUKARI
Ugonjwa wa sukari unatibika bila kujali ni mda gani umepata hilo tatizo wengi wamekata tama na kuwa wabishi amini tatizo hili linatibika vizuri sana wengi wemepona.


Tumia dawa ya SUPER-NHESHAambayo ni dawa ya miti shamba yaani (asilia) ambayo humfanya mtu kupona na kuimalika kabisa.


Tutakuelekeza pia mfumo wa mtindo wa maisha utakao takiwa kutumia ili kutoluhusu tatizo hilo kurudi tena.


BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO/KANISANI NJIA PANDA YA KWENDA SINZA  SIMU: 0652 102 152/0788 330 105/ 0755 684 297 NYOTE MNAKARIBISHWA PIA TUNATUMA MIKOANI WHATAPPS NO 0652 102 152 



Share:

Watatu washikiliwa kwa tuhuma za mauaji Moshi


 Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro linawashikilia watuhumiwa watatu kwa madai ya kuhusika na tukio la mauaji ya kijana wa bodaboda, Rogers Kesy, mkazi wa Mnazi- Kiboroloni, Manispaa ya Moshi.


Akisimulia tukio hilo mbele ya waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Amon Kakwale amesema mmoja wa watuhumiwa, Sifael Sarun alimkodisha marehemu ampeleke nyumbani kwake lakini baada ya kufikishwa nyumbani alimuua kijana huyo kwa kumpiga na nyundo kichwani na kisha kumnyonga na waya shingoni.

Kamanda Kakwale amesema mara baada ya mtuhumiwa huyo kutekeleza mauaji hayo waliuweka mwili wa kijana huyo kwenye mfuko wa sandarusi na kuutupa pembeni mwa barabara kuu ya Moshi - Himo.

Amesema Sifael Sarun alishirikiana na wenzake wawili Emanuel Sarun na Elia Laizer ambao wote wako chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi na kuwa uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.

Aidha, amesema Jeshi la Polisi limefanikiwa kukamata pikipiki yenye namba MC 880 AYR ambayo ilitumika kubeba mwili wa marehemu na kwenda kuutupa barabarani.




Share:

Mwalimu atuhumiwa kufanya mapenz kitanda kimoja na wanafunzi wawili

Mkuu wa  Wilaya  ya Magu mkoani Mwanza, Salim Kali, ameagiza kuhamishwa  wilayani kwake mwalimu anayetuhumiwa  kufanya mapenzi na wanafunzi watatu wa kike wa shule ya msingi ya Ilungu  katika kitanda kimoja.

Mwalimu huyo aliyetajwa na Mkuu wa wilaya kwa jina la Martin  Mambosasa anadaiwa kufanya vitendo hivyo kwa nyakati tofauti kwa miaka saba.

Mkuu huyo wa wilaya, alisema mwalimu huyo aliwahi kukamatwa na vyombo vya  dola na kufikshwa mahakamani, lakini akahonga wazazi wa watoto hao wakaharibu ushahidi.

Alitoa agizo hilo juzi kwenye kongamano la kuweka mikakati ya kukabiliana na ongezeko la vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto, mimba katika umri  mdogo na utoro kwa wanafunzi.

Alisema  mikakati hiyo itasaidia  kuongeza ufaulu na kwamba  mwaka 2020, takwimu zinaonyesha matukio ya ukatili wa kijinsia yalikuwa 304.

Alimuagiza mratibu Elimu wa  kata na ofisa elimu wa wilaya kumhamishia mwalimu huyo  sehemu nyingine Ili asionekane wilayani kwake.

"Huyu mwalimu amekuwa akidhalilisha watoto wadogo kwa kipindi kirefu na naagiza ahamishwe sitaki kumsikia wala kumuona hapa wilayani kwangu," alisema

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa  Wilaya ya  Magu,  Amandus Mboya alisema  mambo yanayochangia ongezeko la vitendo vya ukatili wa kijinsia ni pamoja na wazazi kushindwa kuwapatia huduma muhimu.

Alitaja huduma zingine wanazokosa kuwa ni pamoja na kukosa taulo za kike, mafuta ya kupaka pamoja  na kukosa fedha za kunyoa nywele 

 

Credit:Nipashe




Share:

Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) Kusogeza Huduma Kwenye Kanda

 


Na Asteria Muhozya, Ruvuma
Imeelezwa kuwa, Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) inatarajia kuongeza wigo wa huduma kwa kuanzisha Vituo vya Huduma za Maabara na Ushauri Elekezi katika Kanda zenye uzalishaji wa Madini kwa wingi.

Hayo yamebainishwa Mei 12, 2021 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila wakati akifungua mafunzo kwa wachimbaji wadogo wa madini ya mwongozo wa namna bora ya uchukuaji wa sampuli za uchunguzi na uchenjuaji madini  Mkoani Ruvuma.

Prof. Msanjila ameongeza kuwa, hivi karibuni GST itaanza kutoa huduma hizo katika Mkoa wa Geita na baadaye Chunya, na hivyo kuwataka wachimbaji wadogo nchini kuitumia vyema taasisi hiyo kutokana na manufaa watakayoyapata kutoka kwa wataalam wenye ujuzi na waliobobea katika fani mbalimbali katika Sekta ya Madini.

‘’Ni muda muafaka sasa kushirikiana na GST kwa karibu zaidi kwa kuanza kuchukua sampuli zitakazozingatia mafunzo haya na kuziwasilisha maabara ya GST kwa huduma bora na majibu ya uhakika ikizingatiwa kwamba, maabara ya GST inatambuliwa kimataifa kwa kuwa na ITHIBATI ya ubora katika uchunguzi wa dhahabu,’’ amesisistiza Prof. Msanjila.

Ameongeza kwamba, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu inatambua umuhimu wa wachimbaji wadogo, hivyo, kutokana na wajibu wa GST katika kuhakikisha sekta inafanya vizuri imepelekea kufanyika kwa mafunzo hayo ambayo yanalenga kuwasaidia wachimbaji wadogo kuondokana na uchimbaji wa kubahatisha kwa kufanya uchimbaji endelevu na wenye tija ili kuwasaidia wachimbaji kuongeza uzalishaji na hatimaye kuongeza mchango wao kwenye pato la taifa ambao  hivi sasa bado ni mdogo .

Aidha, Prof. Msanjila ameipongeza GST kwa jitihada inazozifanya katika kuwasaidia wachimbaji wadogo nchini ikiwemo kuwa karibu nao kwa kuwapatia elimu mbalimbali zinazohusiana na masuala ya madini kupitia machapisho, vitabu, huduma za maabara, ushauri elekezi na mafunzo mbalimbali yakiwemo hayo ambayo  yanatolewa katika maeneo mbalimbali nchini.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu Prof. Msanjila ameipongeza Ofisi ya Madini Mkoa wa Ruvuma kwa kuvuka lengo la makusanyo katika Mwaka wa Fedha 2020/2021 ambapo hadi kufikia mwezi Aprili, 2021 imekusanya shilingi bilioni 8.9 sawa na asilimia 141 na hivyo kuvuka lengo la kukusanya shilingi  bilioni 7.5 iliyopangiwa kukusanya.

‘’ Nipende kuwaambia mnafanya kazi nzuri sana. Kama wizara, tunajua Ruvuma mnafanya vizuri ndiyo sababu hata migogoro hakuna. Nawaomba pamoja na kuendelea na majukumu yenu lakini mzidi kujiendeleza kielimu,’’ amesisitiza Prof. Msanjila.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Steven Ndaki ameipongeza wizara

na GST kwa kuwezesha mafunzo hayo kufanyika mkoani humo na kueleza kwamba, yatawawezesha wachimbaji kufanya shughuli zao kwa uhakika. Aidha, ameipongeza wizara kwa kuanzisha masoko ya madini mkoani humo hivyo kurahisisha biashara ya madini.

Naye, Mwenyekiti  wa Chama Cha Wachimbaji Wadogo Mkoa wa Ruvuma , Issack Ngaladela ameishukuru GST kuwezesha mafunzo hayo na kusema kuwa, awali wachimbaji walikuwa wanachimba kwa hisia na kwa miaka mingi imewapelekea kupoteza muda mwingi na mitaji. ‘’ Mafunzo haya yatatubadilisha, sasa tutachimba kisayansi,’’ amesema.

Mbali na wachimbaji, katika siku ya kwanza mafunzo hayo pia  yamewashirikisha  Wakuu wa Wilaya za Mkoa huo, Makatibu Tawala na viongozi wa wachimbaji wa mkoa husika.

Vilevile, katika ziara hiyo pia, Prof, Msanjila ametembelea Mgodi wa wachimbaji wadogo wa Makaa ya Mawe wa GodMwanga uliopo katika kijiji cha Malinyi wilaya ya Nyasa kwa lengo la kusikiliza changamoto na kushauri namna bora ya kufanya shughuli zao.


Share:

VIDEO : Wini Ft. Darassa – I Do

 VIDEO : Wini Ft. Darassa – I Do



Share:

Ntobo Mik 1....Ni Dawa Ya Asili ya Vidonda Vya Tumbo Iliyofanyiwa Utafiti Kwa Miaka Mingi


 NTOBO MIK 1
Ni Dawa ya vidonda vya tumbo iliyofanyiwa utafiti kwa miaka mingi  mwanga wa matumaini kwa wanao teseka na Vidonda vya Tumbo.

Huwezi kuzungumzia magonjwa yanayotesa Jamii ya watu wengi Duniani bila kuzungumzia Vidonda vya Tumbo.

Ugonjwa huu husababishwa na aina ya bakteria anayeitwa kwa jina la HP (Helicobacter Palory) mtu hujikuta anateseka na maumivu makali ya Tumbo bila kujuwa kuwa ni vidonda vya tumbo

DALILI ZAKE:
1.     Tumbo kuwaka moto
2.     Tumbo kujaa gesi au haja kubwa kuwa ngumu
3.     Kutokupata choo vizuri
4.     Kiungulia cha mara kwa mara
5.     Kichwa kuuma
6.     Maumivu makali ya tumbo lajuu wengi huuita chembe ya moyo
7.     Kukosa hamu ya kula
8.     Kizunguzungu
9.     Kichefu chefu

Ugonjwa huu ukishamili sana mgonjwa hujikuta anatapika damu au kujisaidia choo chenye mchanganyiko na damu.

Nini suluhisho;
BABU MADUHU MTAALAMU MWENYE UWEZO MKUBWA WA KUTIBU VIDONDA VYA TUMBO
BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL KITUO CHA KANISANI
PIGA SIMU NO. 0755 684 297/ +255 652 102 152 (WHATSAPP)

 




Share:

RC SHIGELLA AKABIDHI ZAWADI ZA EID EL FITR KWA MAKUNDI MATATU MAALUMU MKOANI TANGA

MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati aliyevaa suti akimkabidhi Msaada wa Chakula kwa ajili ya sikuu ya Eid El Fitr Afisa Mfawidhi wa Makazi ya Wazee Wasiojiwezea Msufini Muheza Anna Mgelwa kushoto ambapo msaada huo ulitolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Judica Omari
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati aliyevaa suti akiendelea kukabidhi Msaada wa Chakula kwa ajili ya sikuu ya Eid El Fitr ambapo msaada huo ulitolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Judica Omari
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati aliyevaa suti akiendelea kukabidhi Msaada wa Chakula kwa ajili ya sikuu ya Eid El Fitr ambapo msaada huo ulitolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Judica Omari
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Judica Omari
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi msaada huo wa pili kutoka kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Judica Omari




MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella ametoa msaada wa chakula na vifaa mbalimbali kwa makundi ya watu wenye mahitaji maalumu mkoani humo vyenye thamani ya Sh .Milioni 3.6 kwa ajili ya sikukuu ya Eid El Fitri.

Msaada huo umekabidhiwa kwenye makundi hayo maalumu ya watu wenye mahitaji maalumu kupitia kituo cha Wazee cha Mwanzange,Misufini na kituo cha Kulea Watoto wenye mahitaji maalumu kilichopo eneo la Pongwe Jijini Tanga katika halfa iliyofanyika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Msaada uliotolewa ni pamoja na Mbuzi wa tano,mchele,mafuta ya kula,sabuni,mashuka,mavazi na vyengine kwa ajili ya huduma za afya ikiwemo Taulo za kike na pampasi.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo,RC Shigella alisema kwamba wameamua kutoa msaada huo ili kuwawezesha makundi hayo maalumu waweze kusheherekea sikuuu ya Eid El Fitri  vema kwa kuwawezesha mahitaji hayo muhimu

Alisema wameona waweke utaratibu huo mzuri zaidi badala ya kuwaalika na kula nao pamoja wakaona waandae kutengeneza chakula kwa ajili ya sikukuu wakiwa kwenye maeneo hayo kwa kusheherekea.

“Nimpongeze Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Judica Omari na Menejimenti ya Ofisi kwa utaratibu  huu ambao unaenda kugusa furaha ya ndugu zetu waliopo kwenye mazingira magumu na mazingira ya uhitaji na msaada huu ni mahususi kwa ajili ya Sherehe kwani kipindi cha siku 30 waislamu kote dunia na mkoa wa Tanga wameshiriki kikamilifu kwenye kufunga  na kwenye funga ndio mahala pekee walikuwa wakiwasiliana na mwenyezi mungu kwa ajili ya toba na kuiombea nchi yetu”Alisema

 Mkuu huyo wa Mkoa alisema wanapohitimisha funga wanakuwa na sherehe watu wanasherekea na kuomba baraka wakaona watengeneza utaratibu wa kugusa nafsi na nyoyo za makundi hayo maalumu mkoani Tanga ili angaliu watakaposherehe wasihangaike wapata wapi chakula kwani angalau vitu hivyo vikiwepo wanaweza kusheherekea vizuri.

 “Nitumie nafasi hii kuwapongeza viongozi wa dini kwa namna walivyoshiriki kwenye kipindi cha mwenzi wa ramadhani watu wameendelea kushirikiana hivyo tuendelee kuiweka nchi yetu kwenye maombo ili Rais wetu Samia Suluhu aweze kuyatumiza malengo aliyokusudia kwenye kipindi chake cha awamu ya sita”Alisema RC Shigella.

Hata hivyo aliwatakia waislamu kote nchini na mkoani Tanga maadhimisho mema ya sikukuu ya Eid El Fitri huku akieleza kwamba wataimarisha ulinzi na usalama ili wananchi mahala watakaposhiriki washeherekee kwa usalama,amani na furaha.

Awali akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Judica Omari alisema mkuu wa mkoa ametoa mchango wake kwenye mwezi huu wa ramadhani kwani ameona kama mkoa wasiweze kuishia kimyakimya wao waweze kushiriki kutoa sadaka kwa dugu zao wazee wanaoishi kwenye vituo vya serikali na watoto wanaoisni kwenye mazingira magumu.

Hata hivyo aliwatakia heri ya sikuuu ya Eid El Fitri waislamu wote mkoani Tanga na kuwataka washeherekee kwa utulivu na amani

Naye kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Tanga Imani Clemence alisema vituo ambavyo vimeainishwa kupatiwa mahitaji hayo ni kituo cha Wazee Mwanzange,Kituo cha Wazee Misufini na Kituo cha watoto wenye mahitaji Maalumu cha Pongwe .

Imani alisema mafanikio walioyapata ni Serikali kutenga fedha kwa ajili ya kutatua changamoto nyingi zilizokuwa zinakabili makazi ya wazee mfano huduma ya afya ambapo kwa sasa imetenga fedha kwa ajili ya kununua dawa ambazo hazipatikani hospitalini.

“Lakini mafanikio mengine ni Serikali kutenga fedha kwa ajili ya matumizi madogo ya vituo kama dharura ndogo ndogo zinazojitokeza”Alisema

Share:

RPC MAGILIGIMBA AONYA WAVUNJIFU WA AMANI SIKUKUU YA EID EL-FITR SHINYANGA….ASHUKURU WADAU KWA USHIRIKIANO

Share:

Project Officer – SAUTI Youth Project at World Vision

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The SAUTI YOUTH Project Officer, will be responsible of  Formation and mobilizing CVA (Citizen Voice Action) Youth groups, To empowers the youth to have the capacity to engage with the communities and monitor relevant government services and policy influence to climate change trough CVA Preparation of Monthly and quarterly project report Monitoring of the groups, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

NIMEMLIPIA ADA YA CHUO KIKUUU MCHUMBA WANGU NA BAADA YA MASOMO ETI ANATAKA KUOLEWA NA MWANAUME MWINGINE

  Sisi wanaume tunatumia nguvu nyingi katika kutafuta pesa na mtu yoyote akichezea jasho lako haki inauma sana.

Nimi naitwa Mbaraka mkazi wa Gongo la Mboto najishughulisha na Biashara ndogo ndogo hapa mjini. Katika pitapita zangu nilikutana na msichana anaitwa Rehema.Nilimfahamu Rehema kupitia kwa dada yake Zainabu ambaye alikuwa rafiki yangu sana na mteja wangu wa uhakika.

Nilivutiwa sana muonekano na tabia aliyekuwa nayo Rehema hadi ikafika hatua ya kuwa wapenzi.Kipindi nafahamiana nae alikuwa amemaliza kidato cha sita hivyo alikuwa kwa dada yake Zainabu akiwa anasubiri matokeo ya mtihani kutoka.

Kulingana na jinsi tulivyopendana dada yake alikuwa anamruhusu anakuja kazini kwangu na kunisaidia kazi mara kwa mara. Miezi 3 kupita matokeo yalitoka na yeye alikuwa miongoni mwa wenye sifa za kujiunga masomo ya Chuo Kikuu. Kwa Upande wangu nilifurahi sana kuona mke wangu mtajariwa anaenda kujiunga na masomo ya Chuo Kikuu na muda si muda alijiunga na chuo cha Makumira Arusha kwa kozi ya Sheria.

Siku ilipowadia ya kuripot chuoni niliweza kwenda nae hadi chuo na kumpangishia sehemu ambayo atakuwa anaishi. Semister ya kwanza ilipoisha mchumba wangu alirudi Dar na kufikia kwangu maana dada yake na mama yake walikuwa wanafahamu mahusiano yetu na ada ya kujiunga chuo mimi ndiyo nilimlipia mchumba wangu maana mama yake alikuwa amekosa pesa ya kumlipia hata mkopo kutoka kwa serikari hakupewa.

Baada ya likizo alirudi chuo kwa ajili ya semister ya pili ila muda wa kufunga ulipowadia Rehema hakuja Dar au kwenda kwao Mtwara bali alibaki Arusha. Mimi nilifunga safari hadi Arusha nikakaa nae kwa siku mbili tu na kurejea Dar na katika mazungumzo nilimuuliza mbona hukuja Dar akaniambia kuwa semester ya pili ilikuwa ngumu kwake.

Tangu hapo Rehema kuna muda alikuwa anakuja Dar na muda mwingine haji kabisa . Hiyo tabia iliniumiza sana ikabidi nitafute usaidizi ndipo nilikutana na rafiki yangu Amimu na kuniambia kuwa Dr.Kiwanga anaweza nisaidia kwa sababu huyo Dr ndiye alimsaidia yeye na mke wake kupata mtoto baada ya kuhangaika kwa miaka 6 wakitafuta mtoto na bila mafanikio.

Alinipatia namba ya simu ya Dr. Kiwanga ambayo ni +254 769404965. Nilipanga safari kutoka Dar Hadi Kenya kwa Dr. Kiwanga niliweza fika kwenye ofisi ya Kiwangadoctors kisha kueleza shida iliyonileta, .Ndipo niliambiwa kuwa mchumba wangu Rehema kuna Mwalimu ambaye anataka kumuoa baada ya masomo.

Kulingana na maelezo ya Dr Kiwanga asilimi 100 nilikubali maana kuna kipindi mchumba wangu alikuwa anawasiliana na mwalimu moja mara kwa mara nilikuwa nauliza anasema kuwa ni mtu anawasaidia tu wala hakuna kitu kingine.Mwalimu yule mwaka wa kwanza hadi wa nne ila kwa kuwa sikufika chuo kikuu hivyo sikuweza fahamu zaidi.

 Nikiwa ofisini kwake Dr.Kiwanga akaniambia kuwa atanisaidia na relationship spells hadi nimpate Rehema kwa muda wa masaa 48.Baada ya kutoka ofisini kwake haukupita muda Rehema alijileta hadi kwangu na kuomba tufunge ndoa haraka maana kachoka na kusumbuliwa na wanaume,bila kupoteza muda nikijulisha baadhi ya ndugu na Jamaa kisha ndoa ikawepo na kwa sasa tuna watoto wawili na Rehema kanisaidia Biashara yangu kupanda kwa asilimia 75.

Natoa uwito kwa mwenye shida ya mapenzi,kumpata mpenzi wa ndoto zako,Nguvu za kiume,mwenye nuksi na mikosi wasiliana Dr. Kiwanga kwa Namba: +254 769404965 Website: www.kiwangadoctors.com Emails: kiwangadoctors@gmail.com

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger