Tuesday 20 April 2021

RAIS SAMIA AKUTANA NA SPIKA NDUGAI IKULU DODOMA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa katika mazungumzo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai leo tarehe 20 Aprili, 2021 Ikulu Jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiagana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai mara baada ya mazungumzo yao leo tarehe 20 Aprili, 2021, Ikulu Jijini Dodoma.
Share:

MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AKUTANA NA KATIBU MKUU KIONGOZI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, akisalimiana kwa Ishara maalum na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Hessein Katanga walipokutana na kufanya mazungumzo Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Chamwino Jijini Dodoma leo April 20,2021.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Share:

WAZIRI UMMY AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI HALMASHAURI YA SENGEREMA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Ummy Mwalimu amemsimamisha Kazi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Magesa Boniphace kuanzia leo 20 Aprili, 2021 ili kupisha uchunguzi dhidi yake.

Amechukua hatua hiyo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi na viongozi mbalimbali akiwemo Mbunge wa Jimbo hilo, Hamis Tabasamu kuhusu tuhuma za ubadhirifu wa fedha za miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo.

Tuhuma hizo zinasema Mkurugenzi kwa kushirikiana na Wakuu wa Idara, wamekuwa wakifanya ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za Umma zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Share:

NAIBU WAZIRI KATAMBI: SERIKALI KUENDELEA KUWAPATIA VIJANA WA KITANZANIA MAFUNZO YA STADI ZA KAZI

Na: Mwandishi Wetu – Dodoma

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Patrobas Katambi amesema Serikali imeendelea kutambua umuhimu wa kuwapatia vijana ujuzi wa stadi za kazi na maarifa kama hatua mojawapo ya kuwawezesha vijana kumudu ushindani katika soko la ajira la ndani na nje.

Aliyasema hayo hii leo Aprili 20, 2021 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majiliwa (Mb) ambalo liliulizwa na Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Latifa Khamis Juakali, ambaye alitaka kujua ni lini vijana wa Tanzania watapewa stadi mbalimbali za kuwaongezea ujuzi wa maarifa kupitia mfuko wa uwekezaji wa wananchi kiuchumi.

Akijibu swali hilo Mheshimwa Katambi, alieleza kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu imeendelea kutekeleza Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi inayolenga kuwezesha nguvu kazi ya Taifa kupata ujuzi na stadi za kazi stahiki ili kumudu ushindani katika soko la ajira.

“Jumla ya vijana 5,538 wamepatiwa Mafunzo ya kukuza ujuzi kwa njia ya uanagenzi (Apprenticeship) katika fani za ufundi stadi katika nyanja mbalimbali kupitia Taasisi ya Don Bosco na Vyuo vilivyo chini ya VETA,” alieleza Katambi

Aliongeza kuwa, Serikali imeingia Mkataba na VETA wa kurasimisha ujuzi kwa vijana katika Mikoa yote nchini katika fani mbalimbali ikiwemo za Ufundi wa Magari, Useremala, Uashi, Upishi, Huduma za vyakula na vinywaji, Ufundi Umeme, Uchomeleaji vyuma, Ufundi bomba, Uchongaji Vipuri na Ushonaji wa Nguo.

“Katika mwaka wa fedha 2020/2021 kufikia Februari, 2021 jumla ya vijana 10,178 walikuwa wamerasimishwa na kati yao 28 ni Watu wenye Ulemavu,” alisema

Sambamba na hayo, alielezea Mafunzo ya Uzoefu Mahala pa Kazi ambayo yametoa fursa kwa Vijana wengi wanaohitimu elimu ya juu kuendelea kuwashikiza kwa Waajiri ili kupata uzoefu makazini.

“Kwa mwaka wa fedha 2020/21 hadi kufikia Februari 2021, jumla ya wahitimu 1,203 wa Vyuo vya Elimu ya Juu na Kati wamekamilisha mafunzo ya uzoefu kazini kupitia Viwanda, Taasisi na Kampuni mbalimbali za Sekta binafsi na Umma nchini na wahitimu 2,037 wanaendelea kupata ujuzi na uzoefu katika Taasisi binafsi na za umma na kati yao, wahitimu 92 ni Watu wenye Ulemavu,” alieleza Katambi

Aidha, Naibu Waziri Katambi alieleza vijana hao wanapomaliza mafunzo yao wamekuwa wakiwezeshwa kiuchumi kupitia mikopo yenye riba nafuu ikiwemo mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu kupitia halmashauri zilizopo nchini pamoja na Mfuko wa Maendeleo ambayo imekuwa chachu kwa vijana kuanzisha miradi mbalimbali.

Pia alibainisha kuwa serikali imekuwa ikitenga maeneo kwa ajili ya shughuli za vijana katika halmashauri zilizopo nchini ili kuwasaidia vijana kutumia fursa za kiuchumi zinazopatikana katika maeneo yanayowazunguka.

 

Share:

RAIS WA CHAD AUAWA KWA KUSHAMBULIWA NA WAASI


Jeshi la Chad limetangaza kuwa Rais wa nchi hiyo Idriss Deby amefariki baada ya kupata majeraha kwenye mapambano dhidi ya waasi.

Deby alienda mwishoni mwa wiki kuvitembelea vikosi vya nchi hiyo ambavyo vinapambana na waasi kaskazini mwa nchi hiyo. Waasi hao wamevuka mpaka wakitokea Libya.

Kifo chake kimetokea ikiwa ni saa chache tu tangu matokeo ya awali ya uchaguzi uliofanyika Aprili 11 kuonesha kuwa anaongoza kwa asilimia 80. Kwa ushindi huo, Deby angeiongoza nchi hiyo kwa awamu ya sita mfululizo.

Serikali na bunge vimevunjwa na sasa baraza la kijeshi ndilo litakaloiongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miezi 18 ijayo.



Share:

TBS YAFANYA UKAGUZI WA KUSHTUKIZA KANDA YA MAGHARIBI KWENYE MADUKA YA VYAKULA NA VIPODOZI

Wakaguzi wa TBS wakiendelea na ukaguzi na usajili wa majengo ya bidhaa za chakula na vipodozi Mkoani Pwani. TBS inawakumbusha wauzaji na waagizaji wa bidhaa hizo kuhakikisha wanasajili ili kuhakiki ubora na usalama wake ili kuepuka usumbufu usio wa lazima sambamba na kuzingatia taarifa muhimu kwenye bidhaa husika kama vile muda wa matumizi na orodha ya viambata.
Mkaguzi wa TBS, Bw. Elisha Meshack akimfanyia usajili mmiliki wa duka la chakula mara baada ya ukaguzi wa duka lake wilayani Kakonko. TBS inawakumbusha wenye majengo ya chakula na vipodozi kufanya usajili mara moja ili kuepuka usumbufu
 Mmiliki wa duka la chakula na vipodozi wilayani Kakonko akionesha vibali vyao vya majengo kwa wakaguzi wa TBS wakati wa ukaguzi wa kushtukiza sokoni na usajili wa majengo ya bidhaa za chakula na vipodozi. TBS inawakumbusha wenye majengo hayo kusajili ili kuepuka usumbufu
Mkaguzi wa TBS, Bw. Emmanuel Mushi akiendelea na ukaguzi wa kushtukiza wilayani Kakonko ili kuhakiki ubora na usalama wa bidhaa za chakula na vipodozi hususani muda wa mwisho wa matumizi.
Wakaguzi wa TBS wakiwa katika ukaguzi wa kawaida katika kiwanda cha kuzalisha maji ya kunywa wilayani Kibondo kijulikanacho kama " Malagarasi Mineral General Supply". TBS inawahimiza wazalishaji kuthibitisha ubora wa bidhaa zao ili kuepuka usumbufu.
Mkaguzi wa TBS, Bw. Elisha Meshack akiwa kwenye ukaguzi wa bidhaa za vilainishi Wilayani Uvinza ambapo sampuli zilichukuliwa kwa ajili ya kupimwa katika maabara ili kujiridhisha kama zimekidhi ubora wa kiwango husika.

**********************************

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa kushirikishana na mkoa na Halmashauri husika, limeendelea na mpango wa ukaguzi wa kushtukiza sokoni kwa wasambazaji na wauzaji wa bidhaa za vilainishi, vipuli vya magari, vifaa ya ujenzi, chakula na vipodozi uliofanyika Kanda ya Magharibi Mkoani Kigoma katika wilaya za Kakonko, Kibondo, Buhigwe, Kasulu, Uvinza na Kigoma.

Ukaguzi huo umelenga kuhakiki iwapo bidhaa zinazouzwa soko ni kama zimekidhi ubora wa kiwango husika kulingana na ukaguzi uliofanyika katika maeneo ya uzalishaji na wakati zikiingizwa kutoka nje ya nchi, ili kuhakikisha wanapunguza tatizo la uwepo wa bidhaa hafifu sokoni aidha zinazoingizwa kupitia njia zisizo rasmi au kuzalishwa kwa kutozingatia matakwa ya kiwango husika.

Ukaguzi huo ulienda sambamba na utoaji elimu kwa wauzaji na wanunuaji juu ya uhifadhi sahihi wa bidhaa na umuhimu wa kuzingatia na kusoma taarifa sahihi na muhimu katika vifungashio.

TBS imefanya ukaguzi huu sambamba na usajili wa majengo ya chakula na vipodozi ili kuhakikisha majengo husika yanazingatia ubora na usalama wa bidhaa za chakula na vipodozi vinavyohifadhiwa au vinavyouzwa ndani ya majengo hayo.

Kaimu Mkuu wa Kanda ya Magharibi (TBS),Bw. Rodney Alananga ametoa wito kwa waingizaji na wauzaji wa bidhaa zilizo katika viwango vya lazima kuzingatia sheria na taratibu za uingizaji na uuzaji bidhaa kwa kuuza na kuingiza bidhaa ambazo ni bora na salama ili kukuza biashara na kuepuka kupoteza masoko na kero ya kukutwa na bidhaa hafifu ambayo itawalazimu kuziteketeza kwa gharama zao.

Pia aliwashauri wasisite kuwasiliana na ofisi ya TBS mara kwa mara pale wanapohitaji msaada wa kitaalamu.

Kwa upande wake Afisa Usalama wa Chakula (TBS ), Bw. Elisha Meshack alisema ukaguzi huo ni iendelevu kwani ni moja ya majukumu ya Shirika na utahusisha bidhaa mbalimbali katika sekta zote kasoro dawa na unaendelea pia katika wilaya za Mpanda, Tanganyika, Mpimbwe, Sumbawanga, Kalambo na Nkasi kwa upande wa Kanda ya Magharibi.

"Huu ni mwendelezo tu wa shughuli zetu za kila siku, kwani Shirika linahakikisha ukaguzi kama huu unafanyika katika kila wilaya nchi nzima ili kuhakikisha tatizo la bidhaa hafifu linapungua kwa kiasi kikubwa kama sio kwisha kabisa " alisema.

Afisa udhibiti ubora (TBS), Bw. Emmanuel Mushi aliwasisitiza wafanyabiashara wa maduka ya chakula na vipodozi ambao wamefanyiwa ukaguzi na kupewa gharama za malipo na bado hawajalipia gharama za usajili kulipia mara moja ili wapate kibali cha kuuza bidhaa husika katika majengo hayo ili kuepuka usumbufu na wale ambao hawajasajili majengo yao kusajili mara moja.

Meneja wa kiwanda cha kuzalisha maji wilayani Kibondo kijulikanacho kama "Malagarasi Mineral General Supply",Bw. Samir Adam ameipongeza TBS kwa kusogeza huduma karibu na amekuwa akipata ushirikiano wa kutosha kutoka ofisi ya kanda ya magharibi- Kigoma.

" Hapo mwanzo tulipoanza tulikuwa na changamoto ya kupata cheti na kutembelewa kwa wakati ila kwa sasa nashukuru ofisi ya TBS kanda ya magharibi iko jirani na inanipa ushirikiano mkubwa sana" alisema.

Pamoja na ukaguzi huo TBS inatumia fursa hiyo ya kukutana na mfanyabiashara mmoja mmoja kuelezea majukumu ya Shirika ikiwa ni pamoja na yale yaliyokua yakifanywa na iliyokuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa ( TFDA).
Share:

Tanzia : MKURUGENZI WA SHUWASA FLAVIANA KIFIZI AFARIKI DUNIA




Flaviana Kifizi enzi za uhai wake
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA),Flaviana Kifizi amefariki dunia leo alfajiri Jumanne Aprili 20,2021wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam baada ya kuugua muda mrefu.

 R.I.P Flaviana Kifizi




Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRILI 20,2021















 


Share:

Monday 19 April 2021

WAZIRI MKUU AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI WA FEDHA WA WAKALA WA MABASI YA MWENDO KASI 'DART'


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Fedha wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), Suzana Steven Chaula baada ya kutoridhishwa na utendaji wake.

Akizungumzia kuhusu Mtendaji Mkuu wa wakala huo, Mhandisi Ronald Rwakatare, Waziri Mkuu amesema suala hilo atalikabidhi kwa Mamlaka ya uteuzi.

Waziri Mkuu amechukua hatua hiyo leo (Jumatatu, Aprili 19, 2021) wakati alipotembelea kituo cha Kikuu cha DART-Gerezani ambapo alionesha kutoridhishwa na utendaji wa viongozi hao.

“Tangu Mtendaji Mkuu ameingia DART ana miaka mitano hakuna hata basi moja alilonunua, na anasema hana fedha kwani abiria hawasafiri si kila siku wanapigania kule Kimara na wote wanalipa unasemaje hakuna fedha ya kununulia magari”.

Waziri Mkuu amesema kuwa tangu mradi huo ulipoanza mabasi yamekuwa yakipungua kutoka 140 hadi 85. “Watendaji wapo tu wamekaa ofisini wanapigwa na AC (viyoyozi) wananchi wanaumia. Hatuna sababu ya kumbakiza mtu kama hafanyi kazi”.

Amesema wakala huo ulianzishwa na Serikali kwa ajili ya kuondoa adha ya usafiri kwa wananchi lakini viongozi hao wameshindwa kusimamia vizuri na hivyo kusababisha mradi huo kutoendelea vizuri.

Waziri Mkuu amesema mapato mengi ya Serikali yamekuwa yakipotea kutokana na uendeshaji wa wakala huo. “Kwa nini ukatishaji wa tiketi haufanyiki kwa njia ya kielektroniki kwa asilimia 100? Tiketi zinauzwa kwa vifurushi.”

“Haiwezekani watu wanafanya ujanja ujanja tu wakuja na tiketi zao za mfukoni alafu wakimaliza anauza za POS (Mashine ya Kielektroniki ya Kukusanyia Mapato) na wasimamizi wapo tu Mkurugenzi wa Fedha yupo tu ameshindwa kusimamia hili na lipo mikononi mwake”.

“Kwa nini mnauza tiketi kwa vifurushi hamtumii mashine kukata tiketi. Mnaua wakala huu kwa sababu wauzaji wa tiketi wanakuja na tiketi zao na nyingine mnazileta nyinyi. Hamuwezi kusimamia mradi huu wa kimkakati”.

Pia, Waziri Mkuu ametembelea karakana ya UDA ya Kurasini, Dar es Salaam na ameshuhudia baadhi ya mabasi ya wakala huo yakiwa mabovu na alipouliza yanakabiliwa na changamoto gani Mhandisi Rwakatare alisema yanatatizo la mfumo wa gia (Gearbox).

Hata hivyo Mheshimiwa Majaliwa alibaini kuwa magari hayo yanachangamoto nyingine na siyo gearbox pekee kwa sababu baadhi yake yalikuwa yameondolewa baadhi ya vipuri, viti pamoja na matairi.

“…Unanidanganya gearbox ndiyo imeharibika wakati magari chakavu hivi yameharibika kabisa, kama gearbox ndio tatizo mbona kwenye magari mengine mmetoa hadi viti na matairi?

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amemuagiza Meneja wa Forodha Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Njaule Mdendu ahakikishe mzigo ya wateja katika bandari hiyo inatoka kwa wakati. Ametoa agizo hilo alipotembelea Kituo cha Forodha Bandari Kavu iliyopo Ubungo mkoani Dar es Salaam.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Share:

KOCHA JOSE MOURINHO AFUKUZWA KAZI



Kocha wa Tottenham Jose Mourinho amepigwa kalamu baada ya kuisimamia timu hiyo kwa miezi 17 pekee.

Raia huyo wa Ureno alichukua mahala pa Mauricio Pochettino kama mkufunzi wa Spurs mwezi Novemba 2019 na kuiongoza klabu hiyo kuwa katika nafasi ya sita katika ligi ya Premia msimu uliopita.

Kwa sasa Spurs wako katika nafasi ya saba, baada ya kuvuna pointi mbili kutoka mechi tatu zilizopita na waliondolewa katika Ligi ya Europa mwezi Machi. Spurs inatarajiwa kukabiliana na Manchester City katika fainali ya Kombe la Carabao siku ya Jumapili.

Msimu huu, Tottenham chini ya usimamizi wa Mourinho imeshapoteza michezo 1. Rekodi ya kupoteza michezo mingi hivyo ni ya mara ya kwanza kwa Mourinho katika kazi yake ya ukufunzi.

Hakuna klabu ya ligi ya Premia iliopoteza pointi nyingi kutoka kwa klabu zinazofanya vizuri msimu huu zaidi ya Spurs ambao wamepoteza pointi 20.


Siku ya Jumapili , Tottenham walikuwa miongoni mwa timu sita za ligi ya Premia kutangaza kwamba walikuwa wanajiunga na ligi mpya ya Ulaya ya Superleague.


Mechi ya mwisho ya Mourinho akiisimamia timu hiyo ilikuwa sare ya 2-2 dhidi ya Everton siku ya Ijumaa.

Chanzo - BBC Swahili
Share:

TIC YARIDHISHWA NA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA SARUJI CHA TANGA CEMENT JIJINI TANGA

MENEJA wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Daudi Riganda wa pili kulia akisisitiza jambo kwa  Mkazi Mtendaji wa Kiwanda cha Tanga Cement, Mhandisi Benedict Lema leo wakati walipotembelea na kujionea shughuli za uzalishaji zinazofanywa na Kiwanda cha Saruji cha Tanga Cement kilichopo Jijini Tanga kulia ni Nestory Kissima na kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha fedha kwenye kiwanda hicho Issac Lupokela

 

Mkuu wa Kitengo cha fedha wa Kiwanda cha  cha Tanga Cement,Isaac Lupokela akisisitiza jambo wakati wa ziara hiyo katikati ni Mhandisi Benedict Lema akifuatiwa na
MENEJA wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Daudi Riganda na Nestory Kissima
Mkazi Mtendaji wa Kiwanda cha Tanga Cement, Mhandisi Benedict Lema akizungumza jambo wakati wa ziara hiyo

Mkazi Mtendaji wa Kiwanda cha Tanga Cement, Mhandisi Benedict Lema akisisitiza jambo wakati wa ziara hiyo
Mkazi Mtendaji wa Kiwanda cha Tanga Cement, Mhandisi Benedict Lema akisisitiza jambo wakati wa ziara hiyo wa pili kutoka kulia ni Meneja wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Daudi Riganda
Mkazi Mtendaji wa Kiwanda cha Tanga Cement, Mhandisi Benedict Lema akisisitiza jambo wakati wa ziara hiyo kulia ni Meneja wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Daudi Riganda



TANGA

MENEJA wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Daudi Riganda leo ametembelea na kujionea shughuli za uzalishaji zinazofanywa na Kiwanda cha Saruji cha Tanga Cement kilichopo Jijini Tanga huku akieleza kuridhishwa na maendeleo makubwa yaliyofikiwa na kampuni hiyo kwa kuchangia kiasi kibwa katika maendeleo ya nchi.

Meneja huyo wa TIC,Daudi Riganda amefanya ziara leo Jumatatu Aprili 19,2021 akiwa ameambatana na Nestory Kissima.

Akizungumza mara baada ya kutembelea maeneo mbalimbali kwenye kiwanda hicho, Bw. Riganda alisema mwekezaji wa Kampuni ya Tanga Cement ni miongoni mwa wawekezaji mahiri waliosajiliwa kupitia Kituo cha Uwekezaji Tanzania na kupewa hadhi ya wawekezaji mahiri.

Bw. Riganda alisema wamefika kiwandani hapo kuangalia uwekezaji uliofanyika na kuangalia mkataba “Performance Contract” uliosainiwa baina ya Serikali na Wawekezaji hawa ni namna gani ulivyotekelezwa na kila upande. 

 

Katika ziara hii, TIC wamejionea uwekezaji wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 147.65 uliofanywa na kampuni hii, huku ajira zipatazo 330 za moja kwa moja na 677 zisizo za moja kwa moja zikitengenezwa kupitia uwekezaji huu. Kampuni ya Tanga Cement ni miongoni mwa makampuni yanayoongoza katika kulipa kodi katika Kanda ya Kaskazini. 

Aidha Alisema imeonekana kwamba kuna matokeo makubwa yaliyopatikana upande wa teknolojia ambazo zimeingizwa nchini kupitia mradi huo huku akieleza kufurahishwa zaidi na namna kampuni hiyo ilivyofanikiwa kuajiri idadi ndogo ya wafanyakazi wa kigeni huku idadi kubwa ikiwa ni wafanyakazi wa Kitanzania, wengi wao wakiwa ni vijana wa kitanzania.

“Wapo wafanyakazi wa kigeni hawazidi watano na idadi kubwa walioajiriwa kwenye mradi huu wakiwa  ni vijana wa Kitanzania kwa hakika hili limetufurahisha sana “Alisema

Meneja huyo alisema suala lingine ambalo limewafurahisha ni jinsi suala la mazingira na usalama kazini yalivyozingatiwa tokea unapoingia getini mpaka unapotoka kiwandani.

Hata hivyo, imebainika kuwa Serikali imeshindwa kutekeleza wajibu wake kupitia mkataba walioingia na wawekezaji hawa hasa katika kipengere cha msamaha wa kodi ya zuio “withholding tax” kwenye mkopo wa kigeni ulioingizwa na kampuni hii kutoka nchini Afrika ya Kusini kwa vile serikali ilipaswa kutoa notisi kwenye Gazeti la Serikali kuruhusu msamaha huo kitu ambacho hadi hii leo hakijafanyika.

Kutokana na dosari hii maafisa wa TRA waliwaandikia kuwataka kulipa kodi yote kama inavyopaswa na pale walipotoa maelezo walijikuta wakifungiwa akaunti zao za benki, kitu kilichowafanya kuanza kulipia kodi hiyo.

Bw. Riganda aliahidi kufuatilia suala hilo ili kuhakikisha mamlaka za serikali zenye dhamana ya kuhakikisha mikataba inayoingiwa baina ya Serikali na wawekezaji inasimamiwa kama ilivyosainiwa.

Meneja huyo alisema wao kama Kituo cha Uwekezaji watawasilisha malalamiko hayo kwa mamlaka za serikali kupitia Mkurugenzi wao wa kituo cha Uwekezaji ambaye atazungumza na Waziri wa Uwekezaji ndani ya ofisi ya Waziri Mkuu kuangalia namna gani mikataba hiyo baina ya wawekezaji mahiri na serikali inaheshimika ili kuepusha changamoto ambazo zinaweza kuwapata wawekezaji nchini.

Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo Mkazi Mtendaji wa Kiwanda cha Tanga Cement, Mhandisi Benedict Lema alisema huo ni mradi mpya wa laini ya kuzalisha Clinka uliogharamu kiasi cha Dola za Kimarekani Milioni 147 na walisaini mkataba huo na TIC.

“ Lakini mpaka sasa haijatangazwa na Gazeti la Serikali na hivyo  kuifanya Serikali kuonekana haijatimiza wajibu wake kulingana na mkataba ulioingiwa na pande hizo mbili, kitu kilichosababisha usumbufu kwa wawekezaji hasa kwenye masuala ya kodi ambazo TRA inawadai”, alisema.

Kampuni ya Tanga Cement ilikuwa na mpango wa kufungua kiwanda kingine cha saruji mkoani Arusha jirani na eneo la uwanja wa ndege wa KIA, mradi ambao ulikadiriwa kuwa na thamani ya Dola za Kimarekani Milioni 50,hata hivyo wawekezaji hao wamesitisha mpango huo ambao ungetengeneza ajira na mapato zaidi kwa serikali, hadi hapo suala hili la kimkataba “performance contract” litakapopata suluhisho na kodi hiyo kusamehewa kama ilivyobainishwa kwenye mkataba.

Share:

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA VIONGOZI MBALIMBALI JIONI HII


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali leo Aprili 19,2021.
Share:

MPINA AMVAA CAG HASARA ATCL

 

Mbunge wa Kisesa Mhe. Luhaga Mpina

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina ametilia shaka ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa namna ilivyoripoti hasara ya sh. bilioni 60 kwenye Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na kusababisha mkanganyiko mkubwa kwa wananchi.

Mpina amesema kwa mujibu wa Taarifa ya CAG inaonesha kuwa Kampuni ya ATCL ilipata hasara ya sh. bilioni 60 mwaka (2019/20), sh. bilioni 23 (2018/19) na kwamba sababu ya hasara hiyo iliyotajwa na CAG ni matumizi yanayohusisha usafirishaji wa abiria na mizigo kuongezeka kwa asilimia 45 kutoka sh. bilioni 133.6 mwaka 2018/2019 hadi kufikia sh. bilioni 193.6 mwaka 2019/2020.

Pia ripoti hiyo ilieleza mapato yaliongezeka kwa asilimia 41 kutoka sh. bilioni 116 hadi sh. bilioni 157.6 lakini cha kushangaza sababu za kuongezeka kwa matumizi hayo hazikuwekwa kwenye ripoti ya CAG licha ya kuwa zinafahamika wazi na kusababisha mkanganyiko mkubwa kwa wananchi.

Mpina amesema sababu hizo ni pamoja na kutokea mlipuko wa Covid-19 katika kipindi cha mwaka 2019/2020 na kuathiri usafiri wa anga ambapo hapa nchini ndege zilikuwa zinafanya kazi kwa asilimia 20 tu.

Kampuni ya Air Tanzania iko kwenye mageuzi makubwa ambapo katika mwaka 2019/2020 ndege mpya 2 aina ya Boeing na Bomberdear zilinunuliwa na ndege zingine zilinunuliwa mwishoni mwa mwaka wa fedha 2018/2019 na hivyo kupelekea gharama za uendeshaji na utunzaji kuongezeka.

Pia ndege zinazotumiwa na Shirika la  Air Tanzania zimekodiwa kwa Wakala wa Ndege za Serikali na hivyo Kampuni inalazimika kulipa gharama ya ukodishaji kwa wakala huyo.

Kutokana na kuongezeka kwa ndege Shirika limelazimika kuajiri marubani na watumishi wengine ili kukidhi mahitaji ya utoaji huduma .

Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 Shirika liliongeza kituo kipya cha nchini cha Mpanda na kufungua kituo nje ya nchi cha Mumbai India, Pia shirika liliongeza miruko katika  vituo vya Dodoma, Mwanza na Kilimanjaro.

Pia Kampuni ya ATCL ina deni la miaka ya nyuma la sh. bilioni 217 ambapo inalazimika kulipa riba kila mwaka  na mwaka huu wa 2019/20 shirika limelipa riba ya deni sh. bilioni 12.5 ikilinganishwa na malipo ya riba ya sh. bilioni 8 ya mwaka 2018/2019.
Kampuni ya ATCL imeanza mageuzi ya uwekezaji miaka miwili tu iliyopita na hivyo sio rahisi kupata faida leo.

Pia amewatoa wasiwasi wananchi kuwa Kampuni yetu ya ATCL inazidi kuimarika na kuwataka wanaobeza kwa namna moja au nyingine waache na badala yake wapende vitu na mafanikio ya nchi yao.

Mpina amebainisha ushahidi wa kampuni yetu kuimarika na mafanikio yaliyopatikana kwani kabla ya hatua hizi kuchukuliwa na Serikali ya awamu ya tano  shirika lilikuwa halina uwezo wa kulipa watumishi wake mishahara hivyo Serikali ililazimika kulipa mishahara yote kwa 100% lakini tunapozungumza leo Shirika letu linajitegemea kulipa mishahara ya watumishi wake kwa 87%.

Katika kipindi cha ukaguzi shirika lilikuwa na ukwasi wa bilioni 17.5 huu ni ushahidi kuwa kampuni yetu inaendelea vizuri
Kampuni imeajiri marubani waliofikia 80 na wote ni wazawa wakiwemo marubani wanawake ambao wote tunawaona wakirusha ndege zetu kwa umahiri mkubwa.

Pia kwa kufanya ulinganifu na makampuni mengine ya kigeni  mfano Kenya Airways (KQ) ambapo Kampuni ya KQ toka mwaka 1977 inaendelea kupata hasara kila mwaka lakini Serikali yake inaendelea kuwapa fedha za kuendesha shirika hilo kwa kutambua kuwa faida za usafiri wa anga ni mtambuka.

Kuongezaka kwa idadi ya watalii nchini ni ushahidi mwingine wa mafanikio ya shirika letu ambapo watalii wameongezeka kutoka milioni 1.1 (2015) hadi milioni 1.5 (2019) na mapato yatokanayo na utalii yameongezeka kutoka Dola za Marekani bilioni 1.9 (2015) hadi Dola za Marekani bilioni 2.6 (2019).

Huduma za biashara na uwekezaji nchini zimekuwa na ufanisi mkubwa najua watanzania hawajasahau abiria, bidhaa na mizigo yote kutoka nchini kwetu ilitegemea ndege za nje mfano. Mbogamboga, Maua, Samaki, Mabondo, Nyama kwenda masoko ya nje najua hatujasahau na hatutasahau.

Faida nyingine ni kuwahisha wagonjwa kupata matibabu ndani na nje ya nchi kwa gharama ndogo baada ya kununua ndege zetu mfano zamani mgonjwa alitakiwa kupelekwa India lazima apitie kwanza Dubai kuunganisha ndege za India kwa gharama kubwa na kutumia muda mrefu lakini baada ya kununua ndege zetu na kuanzisha ruti ya India gharama ya usafiri imepungua kwa asilimia 40 na muda umepungua kwa kiwango kikubwa na hivyo kuwahi kwenye huduma.

Kuhusu usimamizi na uendeshaji wa Shirika la ndege Tanzania ni Mpina ameshauri watanzania wenzetu wanaobeza Kampuni yetu ya ATCL waache mara moja.

Pia Serikali ilipe deni la nyuma la ATCL la sh bilioni 217, Serikali iendelee kuwekeza kwa kuongeza idadi ya ndege za abiria na mizigo, kupanua na kujenga viwanja vipya vya ndege, kuongeza safari, marubani na kukarabati miundombinu muhimu mingine muhimu hii ni pamoja na  ujenzi wa uwanja mpya wa ndege Mkoa wa Simiyu.
Share:

WAKAMATWA WAKIIBA SIMU MECHI KATI YA SIMBA SC NA MWADUI FC IKIENDELEA...RPC ATAKA WALIOIBIWA WAKAZICHUKUE

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linawashilikilia wanaume watatu kwa tuhuma za wizi wa simu za mkononi wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara kati ya Mwadui Fc na Simba Sc ikiendelea katika uwanja wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema wamewakamata watuhumiwa hao jana Jumapili Aprili 18, 2021 majira ya saa kumi jioni huko katika uwanja wa CCM Kambarage Manispaa ya Shinyanga.

Kamanda Magiligimba amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Amos Shija (38) na Gerald Abdallah (18) wakazi wa Majengo pamoja na Rashid Hamis (25), mkazi wa Tabora ambao watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Akielezea kuhusu tukio hilo, Kamanda Magiligimba amesema askari wakiwa katika majukumu ya kuhakikisha ulinzi na usalama unaimarishwa wakati wa Mechi ya Ligi Kuu kati ya Mwadui Fc na Simba Sc ikiendelea waliwakamata watuhumiwa hao wakiwa wameiba simu tano.

“Tuliwakamata watuhumiwa wakiwa na simu tano ambazo ni Iphone 5 aina ya s7+ rangi nyeusi, Infinix hot 08, Sony xperia, Itel ndogo na Tecno rangi ya silver”, amesema Kamanda Magiligimba.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga anaomba wananchi walioibiwa simu zao siku ya tarehe 18/4/2021 ndani ya uwanja wa CCM Kambarage kufika kituo kikubwa cha polisi Shinyanga ili kubaini simu zao.

Katika mechi hiyo, bao pekee la Nahodha John Raphael Bocco liliipa Simba SC ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Mwadui FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Bocco alifunga bao hilo dakika ya 66 kwa kichwa akimalizia mpira uliounganishwa kwa kichwa pia na beki Mkenya, Joash Onyango kufuatia kona ya winga Mghana, Bernard Morrison kutoka upande wa kulia.

Ushindi huo unawafanya Wekundu hao wa Msimbazi wafikishe pointi 52 baada ya kucheza mechi 22 na kurejea nafasi ya pili, sasa wakizidiwa pointi mbili na Yanga SC ambao hata hivyo wamecheza mechi tatu zaidi.
Share:

WANAUME WAWILI WAANGUKA NA KUZIMIA BAADA YA KUIBA NGURUWE WA BIBI

Kumetokea tukio la aina aina yake huko Shinyalu, Kaunti ya Kakamega nchini Kenya baada ya wanaume wawili wanaodaiwa kuiba nguruwe wa ajuza mmoja kuanguka na kupoteza fahamu. 

Afisa Mkuu msaidizi wa polisi eneo la Shisembe Mike Shivanda amethibitisha kisa hicho kulingana na ripoti ya OB iliyowasilishwa katika Kituo cha Polisi cha Shinyalu kwamba nguruwe hao waliibiwa Aprili 17,2021 majira ya saa nne asubuhi.

"Iliripotiwa na Mike Shivanda, chifu msaidizi, eneo dogo la Shisembe, kwamba wanaume wawili walianguka na kupoteza fahamu ndani ya kijiji cha Munyolo katika eneo la Murhanda takriban kilomita sita kaskazini mwa kituo hicho. 

"Maafisa walitembelea eneo la tukio na kupata wanaume wawili, ambao ni; Nicholas Abung'ana, mwanaume wa Luhya mwenye umri wa miaka 50, na Alexander Savala, wa kiume wa Luhya mwenye umri wa miaka 50 wakiwa wamelala katika nyumba zao, hawawezi kuongea au kuamka," ripoti ilisema.

Mwanamke mzee ambaye nguruwe wake waliibwa alitambuliwa kwa jina Doris Achitsa, 65, ambaye anadaiwa kuwa mwajiri wa Abung'ana.

 Achitsa ni binamuye Savala, ambaye ni mmoja wa washukiwa ambaye alipatikana amepoteza fahamu. 

Kulingana na ripoti ya polisi kwenye kitabu cha matukio (OB), mwanamke huyo ambaye alionekana mwenye masikitiko makubwa alitafuta huduma za mganga mmoja Kaunti ya Bungoma ambaye alimtembelea nyumbani kwake majira ya saa 12 jioni na kufanya ibada zake kabla ya kuondoka ambapo ilipotimia saa 1 usiku, wanaume hao wawili walianguka na kupoteza fahamu.

 Mfuasi huyo alikuwa ameacha maagizo kwamba mtu yeyote atakayeathiriwa asichukuliwe hospitalini bali aachwe katika hali yoyote aliyokuwa nayo hadi asubuhi atakaporudi. 

Ndugu zao walisisitiza kwamba maagizo ya mfuasi wa ibada yazingatiwe. 

Ripoti ya maendeleo ya kesi ya PUI ifuatwe," iliongeza.

SOMA ZAIDI <<HAPA>>




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger