Tuesday, 24 March 2026
KAMATI YA BUNGE YARIDHIA BAJETI OFISI WAZIRI MKUU KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO
Monday, 23 March 2026
WAGANGA WA TIBA ASILI WAJIWEKA SAWA KUNOLEWA NA MKEMIA MKUU
Waganga wa tiba asili na tiba mbadala wanatarajia kukutana na Mkemia Mkuu wa Serikali ili kupatiwa elimu thabiti itakayowawezesha kuendelea kutoa huduma sahihi kwa jamii.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Waganga wa Tiba Asili na Tiba Mbadala nchini (TAMESOT), Bw. Lukas Joseph Mlipu, alipokuwa katika Kata ya Butengorumasa mkoani Geita akiwahamasisha waganga kuhusu umuhimu wa kushiriki mafunzo yatakayotolewa na Mkemia Mkuu wa Serikali.
Amesema mafunzo hayo yanayowalenga waganga wote yana umuhimu mkubwa kutokana na changamoto mbalimbali zinazoikabili taaluma ya tiba asili. Ameeleza kuwa juhudi za serikali, ikiwemo utoaji wa elimu kwa wataalamu hao, zitasaidia kuboresha huduma za tiba asili na kuhakikisha zinaendeshwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu.
Aidha, Bw. Mlipu amefafanua kuwa Mkemia Mkuu wa Serikali atatoa mafunzo hayo tarehe 23 Machi, 2026, mkoani Geita. Hivyo, ametoa wito kwa waganga wote kuhakikisha hawakosi fursa hiyo muhimu kwa mustakabali wa taaluma yao.
Sunday, 22 March 2026
NIMEZINDUA MADARASA YATAKAYO ONDOA MSONGAMANO WA WANAFUNZI - PROF. SHEMDOE










Saturday, 21 March 2026
KIJANA SERIKALI HAIHITAJI KELELE INAHITAJI USHIRIKA WAKO
Katika ulimwengu wa sasa unaoendeshwa na matokeo, dhana ya kijana kukaa pembeni na kupiga kelele kuishtumu serikali inazidi kupitwa na wakati, badala yake nafasi iliyo wazi na yenye tija ni ile ya kuwa mshirika (partner) wa maendeleo.
Mfano bora na hai wa namna ushirika huu unavyoweza kuleta mageuzi makubwa ni kupitia kazi zilizotukuka za Doris Mollel na taasisi yake ya Doris Mollel Foundation.
Kiukweli Doris hajaishia tu kulalamika kuhusu changamoto za watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (njiti) au afya ya uzazi nchini, bali amekuwa mshirika mkuu wa serikali katika kuboresha huduma za afya, kiasi cha kuandika historia inayotambulika kimataifa.
Hivi karibuni, katika Makao Makuu ya Shirika la Afya Duniani (WHO) mjini Geneva, Uswisi, Doris Mollel amepokea tuzo ya utambuzi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus.
Tuzo hiyo ni kielelezo cha uongozi wake thabiti na ahadi yake isiyoyumba katika kuendeleza afya ya mama na mtoto nchini Tanzania, jambo ambalo limethibitisha kuwa masuluhisho yanayoongozwa na wazalendo wa ndani yana nguvu kubwa ya kubadili mfumo wa afya.
Utambuzi huu wa kimataifa kwa Doris Mollel si tu sifa kwake, bali ni ujumbe kwa kila kijana wa Kitanzania kuwa inawezekana kufanya makubwa ukiwa hapa nchini kwako.
Badala ya kupoteza muda mwingi kwenye mijadala isiyo na tija mitandaoni , Doris amewekeza nguvu zake katika "locally-led solutions"—masuluhisho yanayotokana na jamii yenyewe—ambayo ndiyo mwelekeo wa sasa wa maendeleo duniani.
Serikali inapopata washirika kama Doris, mzigo wa huduma za kijamii unapungua na ufanisi unaongezeka, jambo ambalo linajenga taifa imara na lenye heshima kimataifa. Huu ni wakati wa vijana kuacha kulalamika kuwa hakuna fursa, na badala yake kuanza kutengeneza fursa kwa kuwa sehemu ya suluhisho la changamoto zinazotuzunguka, iwe katika elimu, afya, kilimo au teknolojia.
Mafanikio ya Doris Mollel kule Geneva ni kielelezo kuwa ulimwengu unatazama, na unathamini wale wanaojitofautisha kwa vitendo kuliko maneno. Ni mwito kwa kila kijana kujitathmini: Je, wewe ni mpiga kelele au ni mshirika wa maendeleo?

































