Tuesday, 13 January 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 13,2026

Magazeti
 






Share:

Monday, 12 January 2026

Tanzania: IPTL's Patience Pays Off in $168m Dispute with Standard Chartered Bank

 

By Staff Writer

Independent Power Tanzania Limited (IPTL) has won an appeal filed by Standard Chartered Bank Hong Kong in the Court of Appeal of Tanzania   which is Civil Appeal No. 386 of 2022. IPTL challenged in the High Court of Tanzania - commercial division in Commercial Application No. 67 and 75 of  2017.

The registration of foreign judgment of High Court of Justices of England, Queens Bench Court, commercial court which ordered IPTL to pay Standard Chartered Bank Hong Kong an amount tuned to $168 million and the High Court rejected the registration of the said foreign judgment hence Standard Chartered Bank Hong Kong appealed to Court of Appeal.

The ruling was handed down by Judge M.C. Levira, Judge L.E Mgonja, and Judge G. J Mdemu, justice of the Court of Appeal of Tanzania on January 9, 2026, stricking out the appeal filed by Standard Charted Bank Hong Kong and upholding the objections raised by IPTL in regards to the competency of the appeal.

According to a court order signed by W. A Hamza, Deputy registrar court of appea of Tanzania l, the appeal was deemed incompetent due to procedural irregularities and the fact that the underlying claim had already been settled under a government sovereignty guarantee. The Court of Appeal of Tanzania, Dar es Salaam, handling Civil Appeal No. 386 of 2022, which was filed by Standard Chartered Bank (Hong Kong) Limited and Standard Chartered Bank Malaysia Berhad as the 1st and 2nd appellants.

The appeal was brought against Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Pan Africa Power Solutions (T) Limited, and VIP Engineering and Marketing Limited as the 1st, 2nd, and 3rd respondents respectively in the case.

On 14th February 2025, the 1st & 2nd respondents filed a Notice of Preliminary Objection in the Court of Appeal. In the notice, the respondents argue that the appellants' appeal should be dismissed on three procedural grounds.

The first objection is that the appeal is incompetent because the respondents were not served with the Memorandum of Appeal, violating Rule 97(1) of the Court of Appeal Rules. The second objection asserts that the appeal was wrongly filed, breaching Rule 90(1) of the Court of Appeal Rules, since the request for a copy of the ruling was submitted out of time. The third objection contends that the appeal is unmaintainable because the underlying claim was already settled under a government sovereignty guarantee.

The respondents also note that the High Court of Tanzania had issued a decree in Civil Case No. 90 of 2018, rendering the court _functus officio_ in this matter. The respondents are requesting the Court of Appeal to strike out the appeal with costs. They argue that the appellants no longer have valid legal standing to pursue the matter further.

The notice was dated 14th February 2025 and filed on 17th February 2025 at the Dar es Salaam Sub-Registry, Commercial Division.

The case is now pending a preliminary hearing where the court will decide on the validity of the respondents' objections. The preliminary hearing will determine whether the appeal can proceed or be dismissed based on the objections raised.

The legal teams of both parties are preparing submissions regarding the preliminary objections for the upcoming hearing.

The Court of Appeal's decision is seen as a significant victory for IPTL and its co-respondents. Harbinder Singh Sethi, IPTL Executive Chairman, welcomed the court's ruling, saying it was a just decision.

Mr. Seth thanked the court, saying, “We thank the Court of Appeal for making the right decision to uphold justice and dismiss the incompetent appeal.”

The case has been closely watched by legal experts and industry stakeholders. The outcome is likely to have implications for similar cases in Tanzania's commercial courts.

The Court of Appeal's ruling brings an end to a long-running dispute between IPTL and Standard Chartered Bank. The decision is a testament to the strength of Tanzania's judicial system in resolving complex commercial disputes.

The IPTL team is pleased with the outcome and looks forward to putting the matter to rest. The company's management is reviewing the court's decision and will provide further updates in due course.

The ruling is expected to have a positive impact on IPTL's financial position and operations. IPTL remains committed to resolving all outstanding issues and moving forward with its business plans. The company appreciates the support of its stakeholders and partners throughout this process.

Share:

BILIONI 6.7 KUBORESHA AFYA YA MAMA NA MTOTO KAHAMA

 







UJENZI WA JENGO LA GHOROFA TATU WAFUNGUA ENZI MPYA YA HUDUMA ZA AFYA MANISPAA YA KAHAMA


Na Neema Nkumbi, Kahama


Manispaa ya Kahama inaendelea kuandika historia mpya katika sekta ya afya baada ya kuanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa ujenzi wa jengo la kisasa la mama na mtoto lenye thamani ya shilingi bilioni 6.7, hatua inayolenga kuboresha huduma za afya ya uzazi, kupunguza vifo vya mama na mtoto, pamoja na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Manispaa ya Kahama.


Mradi huo ni miongoni mwa miradi ya kimkakati inayotekelezwa na halmashauri hiyo kupitia mapato ya ndani ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita zinazoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuimarisha huduma za afya nchini.


Akizungumza kuhusu mradi huo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama, Masudi Kibetu, amesema mazingira mazuri ya kiutendaji yaliyoanzishwa na serikali yameiwezesha halmashauri hiyo kuongeza ukusanyaji wa mapato na kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo katika sekta mbalimbali.


Amesema mafanikio hayo yamechochea utekelezaji wa miradi ya elimu, afya, miundombinu ya barabara na sekta nyingine za kijamii, huku sekta ya afya ikipewa kipaumbele kikubwa kutokana na umuhimu wake kwa ustawi wa jamii.


"Tunamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha mazingira mazuri ya utendaji, Kupitia ongezeko la mapato ya ndani na usaidizi wa Serikali Kuu, tumeweza kuanza ujenzi wa jengo la mama na mtoto lenye gharama ya shilingi bilioni 6.7 hadi kukamilika kwake," amesema Kibetu.


Ameeleza kuwa ujenzi wa jengo hilo unaendelea vizuri chini ya mkandarasi SUMA JKT, huku halmashauri ikiendelea kusimamia utekelezaji wake kwa karibu ili kuhakikisha linakamilika kwa wakati na kwa viwango vilivyopangwa.


Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Manispaa ya Kahama, Dkt. Baraka Msumi, amesema jengo hilo la ghorofa tatu litakapokamilika litakuwa kituo kamili cha huduma za mama na mtoto, kikitoa huduma zote muhimu chini ya paa moja.


Amesema huduma zitakazotolewa ni pamoja na huduma kwa mama mjamzito, wajawazito wanaosubiria kujifungua, wodi za kujifungulia, wodi za akina mama waliokwisha kujifungua kwa uangalizi, pamoja na wodi maalum kwa akina mama wanaopata changamoto baada ya kujifungua.


"Kutakuwa pia na wodi ya uangalizi maalum (ICU), chumba cha upasuaji, wodi za watoto, wodi za watoto wanaohitaji uangalizi maalum, ICU ya watoto, ofisi za madaktari, ukumbi mdogo wa mikutano pamoja na vyumba vya wauguzi kwa ajili ya kupumzika," amesema Dkt. Msumi.


Ameongeza kuwa jengo hilo litakuwa na uwezo wa kulaza zaidi ya wagonjwa 70 kwa siku kwani Kwa mujibu wa takwimu za hospitali hiyo, zaidi ya wajawazito 700 hujifungua kila mwezi, hali inayosababisha msongamano mkubwa wa wagonjwa, jambo litakalopungua kwa kiasi kikubwa baada ya kukamilika kwa jengo hilo.


Dkt. Msumi ametoa wito kwa akina mama wajawazito kutumia vituo vya kutolea huduma za afya vilivyopo karibu na makazi yao, akitaja Kituo cha Afya Kagongwa na Kituo cha Afya Nyasubi ambavyo vina uwezo wa kutoa huduma za upasuaji, X-ray na ultrasound, huku rufaa ikitolewa pale inapohitajika kwenda Hospitali ya Manispaa.


Akizungumza kuhusu maendeleo ya ujenzi, Mhandisi kutoka kampuni ya SUMA JKT, Elihakimu Royal, amesema mradi unaendelea vizuri na hakuna changamoto yoyote inayokwamisha utekelezaji wake.


Amesema mkandarasi huyo amejiandaa kukamilisha kazi kwa wakati uliopangwa, akitoa shukrani kwa Serikali na uongozi wa Manispaa ya Kahama kwa imani waliyoionesha kwa kampuni hiyo.


Ujenzi wa jengo la mama na mtoto Manispaa ya Kahama unaakisi utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika sekta ya afya, inayolenga kujenga jamii yenye afya bora, inayopata huduma za afya zilizo jumuishi, za kisasa na kwa gharama nafuu.


Mradi huo pia unaendana na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs), hususan lengo namba 3 la kuhakikisha afya njema na ustawi kwa watu wa rika zote, kwa kupunguza vifo vya akina mama na watoto wachanga.


Wananchi wa Manispaa ya Kahama wameelezwa kunufaika moja kwa moja na mradi huo mara utakapokamilika, huku wito ukitolewa kwa jamii kushirikiana na serikali katika kutunza miundombinu ya afya ili idumu na kuendelea kutoa huduma bora kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Share:

Saturday, 10 January 2026

PROF. MKENDA AIPONGEZA LALJI FOUNDATION KUUNGA MKONO SEKTA YA ELIMU NCHINI


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda ameipongeza taasisi ya LALJI FOUNDATION kwa kuendeleza juhudi za kusaidia watoto wa familia zenye uhitaji kwa kugawa sare na vifaa vya shule, akisema hatua hiyo inaunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita katika kuhakikisha elimu jumuishi na bora kwa wote.

Mkenda ametoa pongezi hizo wakati wa hafla ya kugawa sare na vifaa vya shule kwa watoto 400 kutoka vituo saba vya makao ya watoto jijini Dar es Salaam vilivyotolewa na taasisi ya LALJI FOUNDATION ikiwa ni sehemu ya taasisi hiyo kuunga mkono juhudi za Serikali kuinua elimu kwa watoto kutoka familia zenye uhitaji.

Akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Mkenda amesema hatua hiyo ya kusaidia watoto walio katika mazingira magumu inaonyesha mshikamano wa taasisi binafsi na Serikali katika kuhakikisha elimu inapatikana kwa usawa na bila ubaguzi.

“Watoto hawa sasa watajiunga na wenzao mashuleni wakiwa na furaha na hali ya kujiamini Watakuwa na sare, mabegi, viatu na vifaa vya kujifunzia sawa na wenzao. Hii ni hatua muhimu katika kuondoa unyonge na kuleta matumaini mapya kwa watoto hawa,” alisema Prof. Mkenda.

Kwa upande wake, Kamishna wa Elimu Tanzania Lyabwene Mutahabwa alisema msaada huo utapunguza changamoto zinazowakabili watoto katika kuanza mwaka wa masomo.

“Watoto hawa sasa watahudhuria shuleni kwa wakati, bila kubeba mzigo wa kutafuta sare au vifaa. Hii itaongeza mahudhurio na hatimaye kuongeza ufaulu,” alisema Mutahabwa.

Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Abubakar Zubeir, aliwahimiza Watanzania kutenda matendo ya huruma kwa jamii, hasa kusaidia familia zenye uhitaji.

“Kutoa kwa ajili ya wenye uhitaji ni ibada inayompendeza Mwenyezi Mungu. Wito wangu kwa jamii ni kujitoa kusaidia kadiri ya uwezo wetu, kwani thawabu ni kubwa mbele za Mungu,” alisema Mufti Zubeir.

Kwa upande wake mlezi wa taasisi ya LALJI FOUNDATION Mohsin LALJI ( Sheni) alieleza kuwa taasisi hiyo itaendelea kusaidia jamii katika sekta ya elimu, afya na ustawi wa jamii, ikiwa ni sehemu ya kurudisha kwa jamii.
Share:

MAKAMU WA PILI WA RAIS KUZINDUA MASHINDANO MAKUBWA YA QUR’AAN DUNIANI


::::::::



MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mashindano makubwa zaidi ya Qur’aan Tukufu duniani yanayoandaliwa na Taasisi ya Alhikma Foundation.

Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika mwaka 2026 kwa mara ya 26 tangu kuanzishwa kwake, yakihusisha washiriki kutoka mataifa mbalimbali duniani.




Akizungumza Leo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Alhikma Foundation, Sheikh Nurdeen Kishki, alisema maandalizi ya mashindano hayo yamekamilika kwa asilimia 90.

Alisema taasisi hiyo inaendelea na utekelezaji wa mipango kwa kuzingatia ratiba, huku akisisitiza kuwa hakuna ucheleweshaji wowote.

Mashindano hayo yatazinduliwa rasmi Februari 1, 2026, na mgeni maalumu atakuwa Sheikh Abdul Rashid Ali Sufi kutoka Qatar, huku taarifa kamili za mashindano zikitangazwa baada ya uzinduzi.







Share:

Friday, 9 January 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 9,2026



Magazeti










Share:

Thursday, 8 January 2026

SERIKALI IMEFANIKISHA AJIRA 1400 NJE YA NCHI: SANGU

 

Serikali imefanikiwa kuzalisha ajira zaidi ya 1,400 za vijana na wanawake kwenda kufanya kazi nje ya nchi katika kipindi cha mwezi Novemba 2025 hadi sasa ikiwa ni matokeo ya mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na nchi za nje ili kusaidia kupunguza tatizo la ajira.

Akizungumza kwenye hafla ya kuwaaga vijana 109 waliopata fursa ya kazi katika nchi za ughaubini leo (08 Januari 2026) jijini Dar es Salaam, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu alisema mafanikio hayo ni utekelezaji wa maono ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kukuza ajira.

"Tangu Novemba mwaka 2025 hadi Januari mwaka huu Serikali imefanikisha vijana 1,432 kwenda kufanya kazi nje ya nchi ikiwa ni matokeo ya jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan kukuza mahusiano ya kidiplomasia na mataifa ya nje", alisema Waziri Sangu.

Sangu alitaja mafanikio mengine ya Serikali kuwa ni pamoja na upatikanaji wa fursa za ajira 8,000 nje ya nchi ifikapo mwisho wa mwaka huu ambapo tayari nafasi za ajira 500 za madereva pikipiki zimetangazwa kwa nchi ya Falme za Kiarabu (UAE) na mchakato wa usaili utakamilika mwezi Februari mwaka huu.

Alitaja fursa nyingine ya ajira 50,000 nchini Japan za kukuza ujuzi kwa vijana kwenye sekta ya ujenzi   ambapo majadiliano  yanaendelea na yatakapokamilika vijana kote nchini watatangaziwa kuomba.

Waziri Sangu aliwahakikishaia vijana hao 109 walioagwa leo kuwa Serikali imeratibu suala la mikataba yao, usalama wao na mazingira ya kazi wanapokwenda kupitia Mabalozi wanaowakilisha nchi hivyo amewataka waende wakafanye kazi kwa weledi, nidhamu na kudumisha mila za Kitanzania.

Akizungumza awali Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Zuhura Yunus alisema kwenda kufanya kazi nje ya nchi ni fursa nzuri ya ambapo tukio la leo kuwaaga vijana 109 ni uthibitisho wa lengo la Serikali kuzalisha ajira kwa makundi ya vijana na wanawake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Mawakala wa Ajira Tanzania Bara (TRAA) Abdallah Khalid Mohamed alisema ushirikiano kati yao na Serikali umefanikisha kupatikana kwa fursa za ajira nje ya nchi na ndani kwa watanzania wengi.

Mohamed aliongeza kuwa TRAA ilianzishwa mwaka 2000 imekuwa mdau mkubwa wa Ofisi ya Waziri Mkuu katika jitihada za kutafuta fursa za ajira kwa watanzania pamoja na kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo kwa watu.

Vijana hao 1,432 hadi sasa wamenufaika kwenda katika nchi za Ujerumani, Canada, Falme za Kiarabu (UAE), Qatar, Saudia Arabia, Kuwait, na Oman ambapo wanafanya kazi katika fani za ufundi umeme, ujenzi, uuguzi,ufundi magari, udereva wa magari na pikipiki na kazi za majumbani.

Share:

KILA MTU NILIYEMWAMINI ALIISHIA KUNISALITI, HADI NIKAGUNDUA KWA NINI

Jina langu ni Daniel, na ninatoka mji wa Eldoret nchini Kenya. Kwa muda mrefu, usaliti ukawa utaratibu mchungu maishani mwangu. Kila mtu niliyemwamini hatimaye alinigeuka. Marafiki niliowasaidia walinisema vibaya nyuma yangu. Washirika wa biashara walitoweka na pesa. Hata watu niliowatendea kama familia walisaliti imani yangu. Mwanzoni, nilifikiri ilikuwa bahati mbaya tu au uamuzi mbaya kwangu.

Kilichoniuma zaidi ni kwamba mimi ni mwaminifu na mkarimu kiasili. Sikuwahi kumdanganya mtu yeyote au kuwatakia wengine mabaya. Niliwaunga mkono watu walipokuwa wakipambana, lakini wao waliniacha au kunisaliti mara tu walipofanikiwa. Baada ya matukio kadhaa yenye uchungu, niliacha kuwaamini watu kabisa. Niliishi kwa hofu, nikitarajia usaliti unaofuata kila wakati.

Nikiwa naishi Eldoret, mtindo huu uliathiri kila eneo la maisha yangu. Sikuweza kujenga ushirikiano thabiti au mipango ya muda mrefu. Hata watu wema walipoingia maishani mwangu, jambo fulani lingebadilika ghafla. Kutoelewana kungetokea, uongo ungesemwa, na mahusiano yangevunjika. Nilianza kujilaumu, nikijiuliza kama nilikuwa nimelaaniwa au kama kuna kitu kunihusu kilivutia usaliti.

Mabadiliko yalikuja nilipoamua kuacha kurekebisha tatizo ambalo lilikuwa la kawaida. Nilijua usaliti mara moja au mbili ulikuwa wa kawaida, lakini si kila wakati. Utafutaji huo wa majibu ulinipeleka kwa Madaktari wa Magongo. Nilielezea hali yangu kwa uaminifu, ikiwa ni pamoja na jinsi mtindo huu ulivyokuwa ukinifuata kwa miaka mingi licha ya nia yangu nzuri.

Baada ya kusikiliza kwa makini, Madaktari wa Magongo walifichua kwamba nilikuwa nikiteseka kutokana na mtindo wa usaliti wa kiroho, unaosababishwa na wivu uliofichwa na ushawishi mbaya unaowekwa katika maisha yangu. Walielezea kwamba nguvu kama hizo zinaweza kuwafanya watu wakugeukie bila sababu dhahiri, hata wakati hujafanya kosa lolote. Ukweli huu ulinishtua, lakini hatimaye ulikuwa na maana.

Walinipa uchawi wenye nguvu ili kuondoa nguvu za usaliti na kusafisha njia yangu, ingawa sikuwatembelea kimwili. Nilifuata maagizo yao haswa na nikaendelea kuwa mvumilivu. Ndani ya wiki chache, niligundua tofauti. Mazungumzo yakawa wazi zaidi, kutoelewana kukapungua, na watu walinitendea kwa heshima ya kweli tena.

Uthibitisho mkubwa zaidi ulikuja wakati mtu wa zamani wa biashara aliporudi kwa hiari kuomba msamaha na kutatua suala lililosababisha hasara hapo awali. Ushirikiano mpya uliundwa vizuri bila dhihaka. Kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi, nilihisi salama kuamini tena. Mahusiano yaliacha kuporomoka, na amani yangu ikarudi.

Leo, maisha yangu huko Eldoret, Kenya, ni tofauti kabisa. Sasa ninaelewa kwamba usaliti wa mara kwa mara hausababishwi kila wakati na dosari za tabia au chaguo mbaya. Wakati mwingine, kuna suala la kina zaidi linalohitaji uingiliaji kati unaofaa. Mara tu liliposhughulikiwa, kila kitu kilibadilika kiasili.

Ninashiriki ushuhuda wangu ili yeyote anayepitia usaliti unaorudiwa ajue kwamba hayuko peke yake. Madaktari wa Magongo husaidia katika usaliti, bahati mbaya, mahusiano yaliyofungwa, kushindwa kwa biashara, na mashambulizi ya kiroho. Wanaweza kufanya kazi kwa ufanisi hata kama hupo kimwili.

Ikiwa usaliti umekuwa mtindo katika maisha yako, usiupuuze. Unaweza kuwasiliana na Magongo Doctors kupitia info@magongodoctors.com au piga simu +255740700621. Kwangu mimi, kugundua chanzo halisi ilikuwa mwanzo wa amani, utulivu, na mahusiano ya kuaminika tena.

Share:

HAPPY BIRTHDAY MALUNDE!






Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger