Friday, 9 January 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 9,2026



Magazeti










Share:

Thursday, 8 January 2026

SERIKALI IMEFANIKISHA AJIRA 1400 NJE YA NCHI: SANGU

 

Serikali imefanikiwa kuzalisha ajira zaidi ya 1,400 za vijana na wanawake kwenda kufanya kazi nje ya nchi katika kipindi cha mwezi Novemba 2025 hadi sasa ikiwa ni matokeo ya mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na nchi za nje ili kusaidia kupunguza tatizo la ajira.

Akizungumza kwenye hafla ya kuwaaga vijana 109 waliopata fursa ya kazi katika nchi za ughaubini leo (08 Januari 2026) jijini Dar es Salaam, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu alisema mafanikio hayo ni utekelezaji wa maono ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kukuza ajira.

"Tangu Novemba mwaka 2025 hadi Januari mwaka huu Serikali imefanikisha vijana 1,432 kwenda kufanya kazi nje ya nchi ikiwa ni matokeo ya jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan kukuza mahusiano ya kidiplomasia na mataifa ya nje", alisema Waziri Sangu.

Sangu alitaja mafanikio mengine ya Serikali kuwa ni pamoja na upatikanaji wa fursa za ajira 8,000 nje ya nchi ifikapo mwisho wa mwaka huu ambapo tayari nafasi za ajira 500 za madereva pikipiki zimetangazwa kwa nchi ya Falme za Kiarabu (UAE) na mchakato wa usaili utakamilika mwezi Februari mwaka huu.

Alitaja fursa nyingine ya ajira 50,000 nchini Japan za kukuza ujuzi kwa vijana kwenye sekta ya ujenzi   ambapo majadiliano  yanaendelea na yatakapokamilika vijana kote nchini watatangaziwa kuomba.

Waziri Sangu aliwahakikishaia vijana hao 109 walioagwa leo kuwa Serikali imeratibu suala la mikataba yao, usalama wao na mazingira ya kazi wanapokwenda kupitia Mabalozi wanaowakilisha nchi hivyo amewataka waende wakafanye kazi kwa weledi, nidhamu na kudumisha mila za Kitanzania.

Akizungumza awali Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Zuhura Yunus alisema kwenda kufanya kazi nje ya nchi ni fursa nzuri ya ambapo tukio la leo kuwaaga vijana 109 ni uthibitisho wa lengo la Serikali kuzalisha ajira kwa makundi ya vijana na wanawake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Mawakala wa Ajira Tanzania Bara (TRAA) Abdallah Khalid Mohamed alisema ushirikiano kati yao na Serikali umefanikisha kupatikana kwa fursa za ajira nje ya nchi na ndani kwa watanzania wengi.

Mohamed aliongeza kuwa TRAA ilianzishwa mwaka 2000 imekuwa mdau mkubwa wa Ofisi ya Waziri Mkuu katika jitihada za kutafuta fursa za ajira kwa watanzania pamoja na kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo kwa watu.

Vijana hao 1,432 hadi sasa wamenufaika kwenda katika nchi za Ujerumani, Canada, Falme za Kiarabu (UAE), Qatar, Saudia Arabia, Kuwait, na Oman ambapo wanafanya kazi katika fani za ufundi umeme, ujenzi, uuguzi,ufundi magari, udereva wa magari na pikipiki na kazi za majumbani.

Share:

KILA MTU NILIYEMWAMINI ALIISHIA KUNISALITI, HADI NIKAGUNDUA KWA NINI

Jina langu ni Daniel, na ninatoka mji wa Eldoret nchini Kenya. Kwa muda mrefu, usaliti ukawa utaratibu mchungu maishani mwangu. Kila mtu niliyemwamini hatimaye alinigeuka. Marafiki niliowasaidia walinisema vibaya nyuma yangu. Washirika wa biashara walitoweka na pesa. Hata watu niliowatendea kama familia walisaliti imani yangu. Mwanzoni, nilifikiri ilikuwa bahati mbaya tu au uamuzi mbaya kwangu.

Kilichoniuma zaidi ni kwamba mimi ni mwaminifu na mkarimu kiasili. Sikuwahi kumdanganya mtu yeyote au kuwatakia wengine mabaya. Niliwaunga mkono watu walipokuwa wakipambana, lakini wao waliniacha au kunisaliti mara tu walipofanikiwa. Baada ya matukio kadhaa yenye uchungu, niliacha kuwaamini watu kabisa. Niliishi kwa hofu, nikitarajia usaliti unaofuata kila wakati.

Nikiwa naishi Eldoret, mtindo huu uliathiri kila eneo la maisha yangu. Sikuweza kujenga ushirikiano thabiti au mipango ya muda mrefu. Hata watu wema walipoingia maishani mwangu, jambo fulani lingebadilika ghafla. Kutoelewana kungetokea, uongo ungesemwa, na mahusiano yangevunjika. Nilianza kujilaumu, nikijiuliza kama nilikuwa nimelaaniwa au kama kuna kitu kunihusu kilivutia usaliti.

Mabadiliko yalikuja nilipoamua kuacha kurekebisha tatizo ambalo lilikuwa la kawaida. Nilijua usaliti mara moja au mbili ulikuwa wa kawaida, lakini si kila wakati. Utafutaji huo wa majibu ulinipeleka kwa Madaktari wa Magongo. Nilielezea hali yangu kwa uaminifu, ikiwa ni pamoja na jinsi mtindo huu ulivyokuwa ukinifuata kwa miaka mingi licha ya nia yangu nzuri.

Baada ya kusikiliza kwa makini, Madaktari wa Magongo walifichua kwamba nilikuwa nikiteseka kutokana na mtindo wa usaliti wa kiroho, unaosababishwa na wivu uliofichwa na ushawishi mbaya unaowekwa katika maisha yangu. Walielezea kwamba nguvu kama hizo zinaweza kuwafanya watu wakugeukie bila sababu dhahiri, hata wakati hujafanya kosa lolote. Ukweli huu ulinishtua, lakini hatimaye ulikuwa na maana.

Walinipa uchawi wenye nguvu ili kuondoa nguvu za usaliti na kusafisha njia yangu, ingawa sikuwatembelea kimwili. Nilifuata maagizo yao haswa na nikaendelea kuwa mvumilivu. Ndani ya wiki chache, niligundua tofauti. Mazungumzo yakawa wazi zaidi, kutoelewana kukapungua, na watu walinitendea kwa heshima ya kweli tena.

Uthibitisho mkubwa zaidi ulikuja wakati mtu wa zamani wa biashara aliporudi kwa hiari kuomba msamaha na kutatua suala lililosababisha hasara hapo awali. Ushirikiano mpya uliundwa vizuri bila dhihaka. Kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi, nilihisi salama kuamini tena. Mahusiano yaliacha kuporomoka, na amani yangu ikarudi.

Leo, maisha yangu huko Eldoret, Kenya, ni tofauti kabisa. Sasa ninaelewa kwamba usaliti wa mara kwa mara hausababishwi kila wakati na dosari za tabia au chaguo mbaya. Wakati mwingine, kuna suala la kina zaidi linalohitaji uingiliaji kati unaofaa. Mara tu liliposhughulikiwa, kila kitu kilibadilika kiasili.

Ninashiriki ushuhuda wangu ili yeyote anayepitia usaliti unaorudiwa ajue kwamba hayuko peke yake. Madaktari wa Magongo husaidia katika usaliti, bahati mbaya, mahusiano yaliyofungwa, kushindwa kwa biashara, na mashambulizi ya kiroho. Wanaweza kufanya kazi kwa ufanisi hata kama hupo kimwili.

Ikiwa usaliti umekuwa mtindo katika maisha yako, usiupuuze. Unaweza kuwasiliana na Magongo Doctors kupitia info@magongodoctors.com au piga simu +255740700621. Kwangu mimi, kugundua chanzo halisi ilikuwa mwanzo wa amani, utulivu, na mahusiano ya kuaminika tena.

Share:

HAPPY BIRTHDAY MALUNDE!






Share:

VETA MOSHI YATAJWA MFANO WA MAFANIKIO YA ELIMU YA UFUNDI STADI



Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.

Na.Mwandishi Wetu-MOSHI

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, ameielekeza VETA Moshi kuimarisha ushirikiano na makampuni na viwanda ili kuongeza fursa za ajira kwa wahitimu na kukuza matumizi ya teknolojia mpya, sambamba na uelekeo wa taifa uliobainishwa katika Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, sera za kisekta na miongozo mbalimbali ya kitaifa.

Mhe. Ameir ametoa maelekezo hayo Januari 07, 2026, alipotembelea chuo hicho, amesisitiza kuwa ushirikiano huo unaboresha mafunzo na kulingana na mahitaji ya soko la ajira.

Aidha, amesema kuwa utekelezaji wa mafunzo ya sekta ya madini kupitia programu jumuishi ya ufundi wa teknolojia ya uchimbaji madini kwa kushirikiana na Chemba ya Madini Tanzania utawezesha utoaji wa mafunzo yanayoakisi mahitaji halisi ya sekta hiyo muhimu kwa taifa.

"Serikali itaendelea kuwekeza katika kuongeza fursa na kuinua ubora wa mafunzo ya ufundi stadi kwa kununua vifaa vya kisasa, kuimarisha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia, pamoja na ujenzi wa vyuo vipya vya VETA 64 nchini."amesema Mhe. Ameir

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Antony Kasore, amesema kuwa Chuo cha VETA Moshi kimeendelea kuwa mfano wa mafanikio ya elimu ya ufundi stadi kwa kuimarisha ushirikiano na viwanda na migodi, hatua inayowezesha mafunzo yanayotolewa kuendana na mahitaji ya soko.

CPA Kasore amesema ushirikiano huo umewezesha vijana kupata ajira kwa haraka kutokana na ujuzi wa vitendo wanaopata wakati wa mafunzo, na kwamba baadhi ya wahitimu kutoka VETA Moshi wamefanikiwa kupata ajira nje ya nchi, jambo lililosaidia kuboresha uchumi wa familia zao na kuchangia pato la taifa.

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali, zinazotekelezwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na wadau katika kuimarisha Elimu Amali, Mbunge wa Moshi Mjini, Mhe. Ibrahim Shayo, ameahidi kufadhili masomo ya vijana 10 kila mwaka katika Chuo cha VETA Moshi.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akizungumza mara baada ya kutembelea Chuo cha VETA Moshi.


Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Antony Kasore,akielezea mafanikio yaliyopatikana katika Chuo cha VETA Moshi mara baada ya Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, kutembelea Chuo cha VETA Moshi.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 8, 2026











Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger