Sunday, 21 December 2025

TBS KANDA YA KATI YATOA ELIMU YA VIWANGO KWA WAFANYABIASHARA ITIGI

Itigi, Singida

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya Kati , leo Desemba 19, 2025 limetoa elimu kwa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha wafanyabiashara wanafanya shughuli zao kwa kuzingatia sheria, kanuni na Matakwa ya viwango vilivyowekwa na Serikali kupitia Shirika.

Elimu hiyo imetolewa kufuatia mkataba wa mashirikiano uliopo kati ya TBS na Halmashauri zote nchini, unaolenga kusimamia jukumu la udhibiti ubora wa bidhaa za Chakula na Vipodozi, ufuatiliaji wa usajili wa bidhaa hizo pamoja na majengo ya yanayotumiwa kuuza biashara hizo za vyakula na vipodozi.

Jukumu hili lilikuwa likitekelezwa na taasi iliyokuwa inaitwa TFDA.

Hata hivyo, mabadiliko hayo yalikuwa hayajaeleweka vizuri kwa baadhi ya wafanyabiashara, hali iliyopelekea TBS Kanda ya Kati kuamua kutoa ufafanuzi wa kina kwa wadau husika.

Akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo, Meneja wa TBS Kanda ya Kati, Bw. Hamisi Sudi Mwanasala, amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha wafanyabiashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi pamoja na Kata ya Mitundu kuelewa wajibu wao katika kusajili majengo ya biashara na kuhakikisha wanauza bidhaa za chakula na vipodozi zinazokidhi matakwa ya viwango vya ubora na zilizosajiliwa.

Bw. Mwanasala amesisitiza kuwa lengo kuu la TBS ni kuona kwamba inalinda afya na usalama wa jamii kwa kuuziwa bidhaa zenye ubora

Sambamba na hilo kuona kwamba wafanyabiashara waendeshe shughuli zao kwa kufuata sheria na kanuni zilizopo ili kuepuka migogoro na mamlaka za udhibiti.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Mitundu, Bi. Utukufu Gwimile, ameipongeza TBS kwa hatua ya kuamua kufika moja kwa moja kwa wafanyabiashara katika ngazi hadi ya kata na kutoa elimu hiyo, akisema kuwa kwa kufanya hivyo kumeondoa sintofahamu iliyokuwepo kwa wafanyabiashara walio wengi wa Kata ya Mitundu kuhusu utekelezaji wa kanuni za viwango ya mwaka 2021 inayosimamia kazi za TBS zinazofanywa na halmashauri.

Naye Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Kata ya Mitundu, Bw. Moshi Hassan, amepongeza juhudi za TBS akisema kuwa wafanyabiashara wamefurahishwa sana na elimu waliyoipokea.

Ameongeza kuwa kuanzia sasa wafanyabiashara wako tayari kuzingatia sheria zote za viwango na kutii taratibu zilizopo bila kushurutishwa.

TBS Kanda ya Kati inayohudumia mikoa ya Dodoma, Singida na Iringa imeendelea kusisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya wafanyabiashara, halmashauri na taasisi za udhibiti ili kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa na kuuzwa nchini zinakuwa zenye ubora na salama ili kuona kwamba afya na usalama wa walaji unatiliwa maanani.
Share:

Saturday, 20 December 2025

JAFO ARIDHISHWA NA UJENZI WA MABWENI NA MADARASA SHULE YA SEKONDARI DK. SELEMANI JAFO





MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akikagua ujenzi wa mabweni mawili na madarasa katika Shule ya Sekondari Dkt.Selemani Jafo,wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Kisarawe.

Na.Alex Sonna-Kisarawe

MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ameridhishwa na hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa mabweni mawili na madarasa katika Shule ya Sekondari Dkt.Selemani Jafo, na kuhimiza Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kuhakikisha mradi huo unakamilika mapema ili ifikapo Januari 2026 shule hiyo iweze kupokea wanafunzi wa bweni.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Kisarawe, Dkt. Jafo amesema ziara hiyo ni sehemu ya kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), hususan katika sekta ya elimu.

“Tumeendelea na ziara yetu ya kuhakikisha tunasukuma utekelezaji wa ilani wilayani Kisarawe, na eneo kubwa tulilolipa kipaumbele ni uimarishaji wa sekta ya elimu. Hapa Shule ya Sekondari Selemani Jafo kuna kazi kubwa inaendelea, ikiwemo ujenzi wa mabweni mawili na madarasa ili kuboresha mazingira ya utoaji wa elimu,” amesema.

Dkt. Jafo amepongeza usimamizi wa mradi huo, akieleza kuwa ujenzi umefikia zaidi ya asilimia 90, huku akielekeza Halmashauri kukamilisha haraka hatua zilizobaki ikiwemo uwekaji wa vigae.

“Ninapongeza sana usimamizi unaoendelea. Ujenzi umefikia zaidi ya asilimia 90, hivyo nimeelekeza Halmashauri ikamilishe kazi zilizobaki ili ifikapo Januari 2026 wanafunzi wakute miundombinu imekamilika,” ameongeza.

Aidha, amemshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuridhia kutoa fedha za ujenzi wa mabweni mawili na madarasa katika shule hiyo, hatua aliyosema inaonesha dhamira ya Serikali katika kuboresha elimu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe, Khalfan Sika, amesema miradi hiyo ni kielelezo cha utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa vitend“Nimshukuru sana Rais Samia kwa mapenzi makubwa kwa wana Kisarawe, lakini pia nimpongeze Mbunge wetu kwa kazi kubwa anayoifanya. Nina imani ifikapo Januari watoto wetu watasoma katika mazingira bora zaidi. Tunamuombea Rais na Mbunge wetu waendelee kutuhudumia wana Kisarawe,” amesema Sika.



MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akikagua ujenzi wa mabweni mawili na madarasa katika Shule ya Sekondari Dkt.Selemani Jafo,wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Kisarawe.



MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua ujenzi wa mabweni mawili na madarasa katika Shule ya Sekondari Dkt.Selemani Jafo,wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Kisarawe.



MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua ujenzi wa mabweni mawili na madarasa katika Shule ya Sekondari Dkt.Selemani Jafo,wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Kisarawe.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI DESEMBA 20,2025

Magazeti
 


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger