Wednesday, 26 March 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO MACHI 26,2025


Magazeti
 




Share:

COSTECH WAKABIDHI RASMI ENEO LA MRADI KWA MKANDARASI KWA AJILI YA UJENZI WA JENGO JIPYA LA STI JIJINI DODOMA

TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imekabidhi rasmi eneo la mradi kwa mkandarasi TIL Construction Limited kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo jipya la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (STI)  jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kukabidhi eneo hilo la mradi Machi 25,2025 jijini Dodoma  Mratibu Msaidizi wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) kutoka COSTECH, Dkt. Aloyce Andrew, amesema hatua hiyo inalenga kurahisisha utoaji wa huduma kwa wadau wa taasisi hiyo.

"COSTECH ina jengo Dar es Salaam lakini tumeamua kujenga Dodoma kwa ajili ya kuwahudumia wadau wetu kwa ukaribu zaidi...,Jengo hili litakuwa na sehemu ya kuhudumia wabunifu, kuatamia kampuni changa, na kuratibu masuala ya utafiti," amesema Dkt. Andrew.

Amesema ujenzi wa jengo hilo, ambalo litajengwa eneo la Azina jijini humo  lenye mita za mraba 4,800, unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 12 kufuatia kusainiwa kwa mkataba Machi 24, 2025.

Kwa upande wake, Mshauri Elekezi wa mradi huo kutoka Kampuni ya MEKON, Benedict Martin, amesema wamekuwa wakihusika katika usanifu wa jengo hilo tangu mwaka jana (2024) baada ya kushinda zabuni kutoka COSTECH.

"Tulishirikiana na COSTECH kuhakikisha jengo hili linakidhi mahitaji yao yote. Pia tuna uhakika kwamba mkandarasi tuliyempata ana uwezo wa kutekeleza mradi huu kwa ubora unaotakiwa," alisema Martin.


Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa TIL Construction Limited, Ding Fubing, ameahidi kwamba kazi itafanyika kwa ufanisi na kumalizika kwa wakati.

"Tunaanza rasmi kesho kwa kulisafisha eneo lote, na baada ya wiki mbili hadi tatu, tutaingia kwenye ujenzi wenyewe. Tunaahidi kufanya kazi nzuri na kukamilisha mradi kwa muda uliopangwa au hata kabla," alisema Fubing.


Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi wa COSTECH, Imanuel Mgonja, amesema taasisi hiyo ina imani na mshauri elekezi pamoja na mkandarasi, akiwashukuru kwa kujitolea kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ubora unaohitajika..

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO MACHI 26,2025


Magazeti
 




Share:

SIMBACHAWENE AWATAKA WATENDAJI WA SERIKALI KUWAHESHIMU WAKAGUZI WA NDANI



Na Barnabas Kisengi ,MWANZA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene amewataka Watendaji Wakuu pamoja na Bodi ya Wakurugenzi kuacha kuwachukulia Wakaguzi wa Ndani kama maadui badala yake wawape ushirikiano ili Taasisi zao zisipate hati chafu.

Amesema kumekuwa na kasumba iliyojengeka kwa Watendaji wengi wa Serikali ya kuwaona Wakaguzi hao wa Ndani kama sio Watumishi na wapo pale kwa ajili ya kuharibu mipango yao ilhali wao ni watu muhimu na jicho la Taasisi.

Mhe.Simbachawene ametoa kauli hiyo leo Machi 24, 2025 jijini Mwanza wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan kufungua Mkutano wa tatu wa Wakaguzi wa Ndani wa Sekta ya Umma.

Amesema Mtendaji yeyote wa Serikali anayewatumia vizuri Wakaguzi wa Ndani hawezi kuingia kwenye matatizo ya ubadhirifu wa fedha za umma huku akisisitiza kuwa Wakaguzi hao wapo kwa ajili ya kumsaidia yeye na Taasisi anayoiongoza.

"Acheni kuwaona Wakaguzi wa Ndani kama wageni na watu wasiotakiwa kwenye maeneo yenu ya kazi badala yake watumieni ili kuhakikisha fedha za umma zinatumika kwa ajili ya miradi ya maendeleo iliyokusudiwa.

Amesema Wakaguzi wa ndani wanatekeleza jukumu nyeti la kuhakikisha fedha za umma zinatumika kwa busara, uwazi na kwa madhumuni sahihi. " Bila kazi yenu, serikali haiwezi kufanya kazi kwa ufanisi" amesisitiza Simbachawene .

Katika hatua nyingine, Mhe.Simbachawene amewataka Wakaguzi hao kuhakikisha wanapata mafunzo ya mara kwa mara ili waweze kuendana na mabadiliko ya matumizi ya kidijitali katika ukaguzi wa fedha hususani katika matumizi ya akili mnemba (AI).

Ameongeza kuwa '' Dunia inabadilika, teknolojia imeleta mageuzi ya jinsi tunavyofanya kazi, na kwa hiyo ukaguzi wa ndani na vyombo vya usimamizi wa taasisi navyo vinapaswa kubadilika.

Amesema matumizi ya mifumo hiyo imechangia mageuzi makubwa kwenye taasisi za serikali yenye hatua kubwa zaidi dhidi ya wanaobainika na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Ameongeza kuwa kesi vikubwa zimechunguzwa na viongozi waliothibitika kuhusika, wameachishwa kazi, wameshtakiwa na fedha zilizochotwa wamezirejesha, akisema huo ni ujumbe wa wazi kwamba utumishi wa umma ni kuwatumikia watu na sio wa kujinufaisha.

Amesema Serikali imedhamiria kuwa na mfumo wa kuhakikisha rasilimali zinasimamiwa ipasavyo.

Kwa upande wake, Rais wa Taasisi ya Wakaguzi wa Ndani, Zelia Njeze amesema mahudhurio ya Wakaguzi wa Ndani ni mazuri lakini kwenye ngazi ya Halmashauri yamekuwa hafifu hali inayochangia wataalamu hao kukosa mafunzo na hivyo kuendelea kufanya makosa yale yale kwenye kaguzi zao.

Amesema mkutano huo utafanyika kwa muda wa siku tano ambapo zaidi ya washiriki 800 watajifunza mbinu mbalimbali za ukaguzi ikiwemo matumizi ya akili mnemba kwenye ukaguzi na hii inatokana na mabadiliko makubwa yanayotokea duniani kote katika ukaguzi wa fedha za umma.


Share:

Tuesday, 25 March 2025

Video Mpya : LUTEMA Ft. MAGODI THE DON - MAJUNGU

 

Share:

MBUNGE ELIBARIKI KINGU AKABIDHI PIKIPIKI, BATI, TILES NA FEDHA KWA UVCCM SINGIDA

Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu, ameonesha uongozi wa kipekee kwa kutoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa UVCCM Mkoa wa Singida. 

Katika hafla iliyofanyika Machi 24, 2025, katika Ukumbi wa RC Mission, Mkoani Singida, Kingu alikabidhi pikipiki 6 kwa makatibu wa UVCCM katika Wilaya zote sita za Mkoa wa Singida. 

Aidha, ametoa bati 120 yenye thamani ya milioni 3.1 kwa UWT Mkoa wa Singida na tiles za milioni 7 kwa Ofisi ya CCM Wilaya ya Ikungi. Kingu pia ametoa shilingi milioni 3 kwa Jumuiya za Wilaya ya Ikungi.

Katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohamed Kawaida, ambaye alikuwa mgeni rasmi, amekabidhi gari la jumuiya hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa. Pikipiki sita zilizotolewa na Mbunge Kingu zilikabidhiwa kwa UVCCM Wilaya ya Singida Magharibi.

Mbunge Kingu amekumbusha ahadi aliyotoa kwa vijana wa Mkoa wa Singida kwamba atawasaidia kwa vifaa vya kazi ili kuhakikisha wanapata fursa za maendeleo. 

Amesisitiza kuwa, kwa kushikamana na vijana wake, ataendelea kuwaunga mkono kwa uwezo wake wote na kurejesha heshima kwa chama chake.

Kingu ameongeza kuwa aliagiza pikipiki hizo kutoka Uingereza na kusema alitumia fedha taslimu kiasi cha milioni 16.2 kwa ununuzi wa pikipiki 6, ambazo zimesajiliwa kwa jina la UVCCM na tayari zimelipiwa kodi zote.

Hafla hiyo imekamilika kwa risiti ya ununuzi wa pikipiki hizo, ambayo Kingu alikabidhi kwa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohamed Kawaida, kama uthibitisho wa malipo yaliyofanywa.

  

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger