Saturday, 30 November 2024
NAIBU WAZIRI SAGINI- MSIKATISHWE TAMAA KATIKA KUPAMBANIA HAKI ZA BINADAMU
Friday, 29 November 2024
BUTONDO ASHIRIKI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA
CHAUMMA YAPATA KITI KIMOJA SERIKALI ZA MITAA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa amesema Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kimepata kiti kimoja katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa upande wa wenyeviti wa mitaa katika uchaguzi uliofanyika jana Novemba 27, 2024.
Mchengerwa amesema hayo leo Novemba 28, 2024 wakati akitoa matokeo ya jumla ya uchaguzi huo akikitaja Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuongoza kwa kupata jumla ya viti 4,213 sawa na asilimia 98.83 huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikishika nafasi ya pili kwa kupata viti 36 sawa na asilimia 0.84.
Mapema akizungumzia kwa upande wa wenyeviti wa vijiji, Mchengerwa amesema huko pia CCM imeongoza asilimia 99.01 ( viti 12,150) huku Chadema ikipata asilimia 0.79 (viti 97).
Thursday, 28 November 2024
MKURANGA WAHAMASISHWA MALIPO YA HUDUMA ZA MAJI
WAZIRI KOMBO AWASILI MAKAO MAKUU YA EAC ARUSHA KUSHIRIKI MKUTANO WA 46 WA MAWAZIRI
MBOWE, LISSU WATUACHIE CHAMA CHETU
Wednesday, 27 November 2024
DC MUHEZA ATOA WITO KWA WANANCHI KUTIMIZA HAKI YAO YA MSINGI KUCHAGUA VIONGOZI
MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Zainab Abdallah Issa amewataka wananchi wilayani humo kutimiza haki yao ya msingi kuchagua viongozi wanaowataka kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaofanyika leo hapa nchini.
DC Zainab aliyasema hayo leo mara baada ya kushiriki zoezi la kupiga kura katika Ofisi ya Mtendaji Kata Mbaramo wilayani humo huku akisisitiza kwamba ulinzi na usalama umeimarishwa kwenye maeneo yote ya kupigia kura.

Alisema zoezi la kupiga kura ni haki ya kila mwananchi ambaye alijiandikisha hivyo uwepo wa ulinzi na usalama kwenye vituo vya kupigia kura unawapa nafasi wananchi kutimiza haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka.

Alisema kwamba ni muhimu wananchi kujitokeza mapema kupiga kura kutokana na kuwa zoezi hilo ni la muda mfupi wanapofika kwenye vituo wana hakiki majina na kuingia kwenye mchakato wa kupiga kura

“Nitoe wito kwa wana Muheza na Watanzania kujitokeza kwa wingi tutimize haki yetu ya msingi kuwachagua viongozi ambao tunawakata kwa maslahi ya maendeleo ya maeneo yetu kwa miaka mitano ijayo”Alisema

“Niwaombe leo ni siku ya mapumziko huna sababu ya kusubiri mpaka saa 10 jioni twendeni tukapige kura hali ya usalama kila mahali imeimarishwa na mungu atatujalia mpaka tutakapofunga tutafunga kwa usalama”Alisema DC Zainab.
Hata hivyo aliwapongeza wananchi wa wilaya hiyo waliojitokeza kwa wingi kwenye zoezi la uandikishaji huku akieleza kwamba katika zoezi hilo la upigaji kura wataendelee kuhamasishana.
“Pale ulipojiandikisha ndio utakapopiga kura imani yangu wana Muheza 187,000 kama walivyojiandikisha tutapiga kura na tutahakikisha zoezi linakamilika salama.
Awali akizungumza mara baada ya kupiga kura kwenye kituo hicho cha kupigia kura Mkazi wa Mbaramo wilayani Muheza Martha Joseph alisema wanamshukuru mungu wameanza kupiga kura saa mbili asubuhi na mpaka sasa zoezi linaendelea vizuri na hivyo wanaamini litamalizika salama.
RAIS SAMIA AMLILIA DKT. NGUGULILE
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameeleza kupokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni na Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, kilichotokea usiku wa kuamkia leo Novemba 27, 2024.
Rais Samia ametoa salamu za pole kwa familia, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson, Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wananchi wa Kigamboni, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote kufuatia Msiba huu Mzito.
Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amen
Tuesday, 26 November 2024
WAHAMIAJI HARAMU WAVAMIA SHINYANGA, JESHI LA POLISI LAKAMATA SABA, LATAKA USALAMA WAKATI WA UCHAGUZI
Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limeendelea kufanya doria na operesheni kubwa za kukabiliana na uhalifu na wahamiaji haramu, ambapo katika operesheni za hivi karibuni, wahamiaji haramu saba kutoka nchini Burundi wamekamatwa, hatua inayosemekana kuwa ni moja ya mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya uhamiaji haramu.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Jumanne Novemba 26,2024 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga SACP Janeth Magomi amesema mnamo Novemba 13, 2024, wahamiaji watatu walikamatwa huko Kijiji cha Mseki, Kata ya Bulungwa, Wilaya ya Ushetu, wakiwa wameingia nchini kinyume cha sheria.
Aidha, Novemba 17, 2024, wahamiaji wanne walikamatwa katika Kijiji cha Nyamilangano, Wilaya ya Ushetu, ambapo walikamatwa kwa kosa la kuingia nchini bila kibali cha mamlaka ya uhamiaji.
"Wahamiaji wote saba ni raia wa Burundi na wamepelekwa katika ofisi za uhamiaji kwa hatua zaidi",amesema.
Polisi Yakamata Wahalifu na Vifaa vya Wizi Kishapu
Huku operesheni za kudhibiti wahamiaji haramu zikiendelea, Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga pia limefanikiwa kukamata wahalifu katika Wilaya ya Kishapu, wakituhumiwa kwa wizi wa mbegu za pamba na bidhaa zingine za Serikali.
Kamanda Magomi ameeleza kuwa Mnamo Novemba 15, 2024, huko Kijiji cha Mwamishoni, Kata ya Bubiki, Polisi walikamata gari moja aina ya Fuso lilikokuwa limebeba mbegu za pamba 210, ambapo mifuko 107 ya pamba iliibiwa kutoka katika chama cha AMCOSS Mwamishoni. Aidha, mnamo Novemba 23, 2024, mtuhumiwa mmoja alikamatwa huko Kijiji cha Maganzo kwa kuuza mbegu za pamba za ruzuku kwa mtu ambaye bado anatafutwa na Polisi.
Mafanikio Makubwa Katika Kudhibiti Uhalifu na Ulinzi Barabarani
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, SACP Janeth Magomi, amesema kuwa kuanzia Oktoba 24, 2024 hadi Novemba 25, 2024, Jeshi la Polisi limefanikiwa kukamata jumla ya wahalifu 51 pamoja na vielelezo mbalimbali, vikiwemo Bhangi kilo 10, Pikipiki 09, Pombe ya moshi lita 15, Godoro 04, Container 02 za bati, Mashine 03 za Bonanza, Gari aina ya FUSO ikiwa na Nondo 130, Binding wire 11, Mifuko ya Saruji 100 vitu vinavyo dhaniwa kuwa vya wizi pamoja, Gari 01 aina ya Toyota Noah iliyotumika kubeba vitu vya wizi, Simu 02, Redio 07, Kabati 01, Fridge 01, na Kitanda 01 cha mbao.
Pia, Jeshi la Polisi limefanikiwa kukamata makosa 7,920 ya uendeshaji wa magari na vyombo vya usafiri, ambapo wahusika waliwajibishwa kwa kulipa faini za papo kwa papo.
Katika upande wa kesi za uhalifu, amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kuona hatua kubwa katika mfumo wa haki, ambapo washtakiwa kadhaa wamehukumiwa vifungo vizito.
Kesi mbalimbali zimepata mafanikio, ikiwemo Mshtakiwa mmoja katika kesi ya kulawiti amepewa kifungo cha maisha jela, Washtakiwa watatu katika kesi za kubaka wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kila mmoja na Washtakiwa wawili katika kesi za ukatili dhidi ya watoto na kusafirisha madawa ya kulevya wamehukumiwa kifungo cha miaka 5 kila mmoja.
Uhamasishaji wa Jamii na Usalama wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Kamanda Magomi amesisitiza umuhimu wa usalama katika uchaguzi mdogo wa Serikali za Mitaa, akitoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uchaguzi na kwamba Polisi wamejipanga kuhakikisha usalama wa raia kutoka majumbani hadi kwenye vituo vya kupiga kura na kurudi majumbani kwao.
NLD YAHIMITISHA KAMPENI KWA KISHINDO HANDENI YAWAOMBA WANANCHI KUWAPA RIDHAA WAGOMBEA WAO ILI WAWAPE MAENDELEO
BOSI ANATAKA NIMPE PENZI NDIO ANIPANDISHE CHEO

Jina langu ni Jesca kutokea Mwanza, Tanzania, naweza kusema itanichukua miaka mingi sana kuja kusahau kitendo cha Bosi wangu niliyekuwa namuheshimu sana alipoaniambia ili kupanda cheo kazini basi ni lazima nilale na angalau mara kadhaa.
Nilikataa mara moja kwani uwezo wa kazi ninao mzuri na isitoshe nimesoma vizuri na vyeti vya kitaaluma ninavyo. Nikajisema kimoyo moyo kama vipi nitaacha hii kazi akiendelea kunisumbua kuhusu jambo hilo.
Baada ya kumkatalia Bosi, haukuisha mwezi rafiki yangu wa kike ambaye alinikuta kazini nikiwa na miaka mitatu aliweza kupandishwa cheo pamoja na mshahara huku mimi nikisalia mtupu.
Nilijua fika ni hasira za Bosi dhidi yangu na asingeza kunifukuza kutokana mkataba wangu ulikuwa na kipengele iwapo nitafukuzwa wanilipe fidia kwa muda wote uliosalia.
Jambo hilo liliniacha na msongo sana wa mawazo, niliamua kumpigia rafiki yangu simu aliyepo jijini Kagera na kumuuliza kama naweza kuhamia huko kikazi maana maisha ya Mwanza yamenishinda.
Aliniuliza tatizo ni nini hasa?, nikamwambia mkasa wangu wote na Bosi wangu akanioneka sana huruma.
Akaniambia yeye alishapandishwa cheo zaidi ya mwaka mmoja uliyopita, nilimuuliza kama alilala na Bosi ndipo akapata fursa hiyo ambayo nimekuwa nikiipigania kwa miaka mingi.
Alinijibu hapana, bali ni mtu aliyemsaidia, nikamuuliza ni nani huyo?, ndipo alipomtaja Dr Bokko.
Basi akanitumia namba zake ambazo ni +255618536050, nilimpigia Dr Bokko na kuongea naye kwa undani zaidi kuhusu changamoto yangu, naye hakusita kunipa uhakika wa suluhisho.
Aliniambia ningoje ndani ya saa 48 nitakuwa nimepata majibu ya jambo hilo ila kabla hata ya saa 24 nilipigiwa simu na HR wa ofisi kwetu na kuniambia kuna barua ipo kwake kutoka kwa Bosi niende kuichukua.
Nilipofika na kukabidhiwa ile barua nilifungua na kukuta ni taarifa ya kuwa nimepandishwa cheo, ndani yake kulikuwa na mkataba mpya wa kazi ambao nilitakiwa kuusaini ili nianze kulipwa mshahara wa juu zaidi.
Nilisaini mara moja mkataba ule na kuurudisha kwa HR na kurudi nyumbani kupumzika kwani wiki inayofuata ningeanza majukumu mengine tofauti na yale ya awali.
Sasa ni takribani miezi 10 napokea mshahara mzuri katika cheo changu kipya na wala sijalala na Bosi kama alivyokuwa anataka yeye. Mpigie Dr Bokko kwa namba +255618536050.



















































