Saturday, 15 April 2023

NIDHAMU, KUJITUMA SABABU WANAFUNZI WENGI KUFANYA VIZURI KWENYE MITIHANI.

Mgeni Rasmi katika mahafali ya 13 shule ya Sekondari Isimila iliyopo Mkoani Iringa Bw. Masozi Nyirenda (wa pili kutoka kulia) akiingia ukumbini na msafara wa wahitimu. Kulia ni Mkuu wa Shule Bw. Frank Mahenge na kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule Dkt. Nasra Habib.
Mgeni Rasmi Masozi Nyirenda (kulia) na Mkuu wa shule Frank Mahenge (kushoto) wakifurahia burudani kutoka kwa wahitimu (hawapo kwenye picha) katika sherehe za mahafali ya 13 ya kidato cha sita shule ya Sekondari Isimila iliyopo mkoani Iringa.
Mgeni Rasmi Masozi Nyirenda (katikati) akipokea nakala ya risala kutoka kwa wahitimu wakati wa mahafali ya 13 ya kidato cha sita shule ya Sekondari Isimila mkoani Iringa. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule Dkt. Nasra Habib na kushoto ni Mkuu wa Shule Frank Mahenge.
Wahitimu wakidato cha Sita wakisoma risala mbele ya Mgeni Rasmi (hayupo pichani) katika sherehe za mahafali ya 13 ya kidato cha sita shule ya sekondari Isimila mkoani Iringa.
Mkuu wa Shule Bw. Frank Mahenge akielezea historia ya shule wakati wa mahafali ya 13 ya kidato cha sita shule ya Sekondari Isimila Mkoani Iringa. Waliokaa ni Mgeni Rasmi Masozi Nyirenda na Mwenyekiti wa Bodi ya Shule Dkt. Nasra Habib.
Mgeni Rasmi Bw. Masozi Nyirenda akisisitiza jambo katika sherehe za mahafali ya 13 ya kidato cha sita shule ya Sekondari Isimila Mkoani Iringa. Waliokaa ni Mkuu wa shule Frank Mahenge na mdau wa shule Dkt. Ave Maria Semakafu.
Mgeni Rasmi Masozi Nyirenda akitoa vyeti kwa wahitimu wa kidato cha sita Shule ya Sekondari Isimila mkoani Iringa katika mahafali ya 13 shuleni hapo.

*************************

Na MWANDISHI WETU.

WANAFUNZI wengi wanaomaliza masomo yao ya Sekondari na kufanya vizuri sababu imetajwa kuwa ni bidii ya kujituma katika kufikia ndoto zao lakini pia nidhamu ya kujali muda na kusimamia malengo waliyojiwekea kwenye masomo yao.

Hayo yametajwa katika sherehe za mahafali ya 13 ya kidato cha sita Shule ya Sekondari Isimila mkoani Iringa wakati wa hafla iliyofanyika jana shuleni hapo ambapo mgeni rasmi alikuwa Meneja Miradi kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Bw. Masozi Nyirenda akimuwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo.

Awali akielezea historia ya shule hiyo Mkuu wa shule Bw. Frank Mahenge alisema, shule ina wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha sita na jumla ya wanafunzi 1,178 wasichana wakiwa ni 835 na wavulana 343 huku kidato cha tano na sita wakiwa ni wasichana pekee.

Amesema, shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri kwenye mitihani ya mwisho ya Taifa na kwamba kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo 2020 - 2022 shule imekuwa ikifaulisha kwa asilimia 100 daraja la kwanza hadi la tatu hivyo kuwafanya wanafunzi wengi kutamani kusoma katika shule hiyo.

"Shule yetu inafanya vizuri kwenye matokeo ya mwisho hivyo kuvutia wanafunzi kuomba nafasi za kujiunga na hii imepelekea tuwe na upungufu wa miundombinu ya kujifunzia na kufundishia kama vile mashine ya kurudufu, maktaba kwa ajili ya kujisomea, jengo la utawala, nyumba za walimu pamoja na bwalo, alisema Mahenge’’

Nao wahitimu wa kidato cha Sita katika risala yao walisema, wanajivunia kuwa sehemu ya familia ya shule ya sekondari Isimila kutokana na misingi, mikakati na malengo ya shule hiyo ambayo inawawezesha kufanya vizuri na kuifanya shule hiyo kuwa bora.

Mgeni Rasmi katika mahafali hayo Bw. Masozi Nyirenda Meneja Miradi kutoka TEA alisema, inafurahisha kuona kuwa shule ya Sekondari Isimila ni miongoni mwa shule zinazofanya vizuri ambapo matokeo ya miaka mitatu yameonesha hakuna aliyepata ufaulu wa daraja sifuri. Nidhamu na bidii ya masomo imesaidia wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani yao ya mwisho.

“Nimefurahishwa kuona namna uongozi wa shule hii unavyoendelea kuweka mikakati ya kuhakikisha wanafunzi wake wanaendelea kupata matokeo mazuri. Miongoni mwa mikakati hiyo ni pamoja na kuongeza vyumba vya madarasa vinne, Ofisi mbili lakini pia kushirikiana na Mkurugenzi wa Halmashauri kutengeneza madawati 130, amesema Nyirenda”

Nyirenda alisema, Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ilianzishwa kwa lengo la kuratibu uendeshaji wa Mfuko wa Elimu wa Taifa ambao unalenga kusaidia jitihada za Serikali za kuongeza upatikanaji wa Elimu bora na kwa usawa hapa nchini. Kupitia Mfuko huo wa Elimu wa Taifa, ufadhili wa miradi ya Elimu yenye thamani ya Bilioni 1.1 katika Mkoa wa Iringa umetolewa katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2015/2016 hadi 2022/2023

Aidha, aliushauri uongozi wa shule kuwasilisha maombi ya ufadhili kwenye Ofisi za Mamlaka kwa ajili ya upungufu wa miundombinu ili maombi hayo yaweze kufikiriwa kadri ya upatikanaji wa fedha, lakini pia kutumia michango ya wadau wa Elimu ndani ya Halmashauri kwani inaweza kusaidia kupunguza changamoto hizo.

Aliwapongeza wahitimu wote wa kidato cha sita kwa hatua waliyofikia na kuwakumbusha kuwa, mafanikio hayaji pasipo maandalizi hivyo anaamini wamejiandaa vya kutosha na wako tayari kwa mitihani yao ya mwisho ili waweze kuendelea na ngazi nyingine ya Elimu baada ya kuhitimu.
Share:

ROYAL TOUR YA RAIS SAMIA YAZAA MATUNDA YA TAWTO.


Na John Mapepele

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mohamed Mchengerwa na Katibu Mkuu Dkt. Hassan Abbasi wameungana na wadau wa sekta ya utalii jijini Arusha leo usiku huu April 14, 2023, kuzindua Chama cha Waongoza Utalii Wanawake (TAWTO) kinacholenga kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara kutangaza Utalii kama Mhe Rais alivyofanya katika filamu ya Royal Tour.

Hafla hiyo pia imehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu Ndug. Anderson Mutatembwa.

“ Sekta ya utalii mtarajie ushirikiano mkubwa kutoka kwangu na timu yangu kuliko wakati wowote katika kuhifadhi na kutangaza utalii,” alisema Mhe. Mchengerwa.

Ametoa rai kuwa madhumuni ya Chama hicho ni muhimu yaende sambamba na kuhamasishana kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu za kuendesha shughuli za utalii nchini hususan Sheria ya Utalii ya Mwaka 2008 na kanuni zake. Pamoja na kuzingatia muongozo wa maadili kutoka Shirika la Utalii Duniani (UNWTO).

Aidha amesisitiza kuwa wabunifu zaidi katika kuandaa vifurushi vya safari za watalii (Tour Packages) ambavyo zitafungamanisha vivutio na mazao mbalimbali ya utalii kama fukwe, michezo, mikutano na matukio, Utamaduni na Utalii wa vyakula ili kuvutia watalii wengi zaidi, kuongeza idadi ya siku za wageni kukaa nchini na hivyo kuongeza mchango wa utalii katika Pato la Taifa.

Pia, ametilia mkazo utoaji wa huduma bora katika sekta yetu ya utalii na ukarimu ambapo amesema hatua hiyo itasaidia nchi yetu kuongeza idadi ya watalii na watalii kurudi kutembelea Tanzania.

Hapa naomba nisisitize makundi yanayohudumia watalii kama Waongoza Watalii (Tour Guides) na wafanyakazi katika tasnia ya ukarimu na huduma za malazi. Hawa ndio wanaokaa na wageni muda mrefu zaidi na hivyo ndio hasa mabalozi wa utalii wetu. Ni vema kuweka utaratibu mzuri wa kujenga uwezo kwa makundi haya ili kuhakikisha wanatimiza wajibu wao ipasavyo na kwa weledi. hali kadhalika, kwa kuzangitia kuwa sekta ya utalii kwa kiasi kikubwa inaendeshwa na sekta binafsi Serikali iliona umhuhimu wa wadau wa utalii kuwa na shirikisho la vya waendeshaji utalii yaani TCT, kwa msingi huo nitoe wito kwa chama chenu kujiunga na kushirikiana kikamilifu na shirikisho hilo (TCT), kwa mukthaza mzima wa kundeleza na kukuza sekta ya utalii nchini" amesisitiza, Mhe. Mchengerwa

Awali Mhe. Mchengerwa ameeleza kwamba Sekta ya utalii ni moja ya Sekta zilizoathirika zaidi na janga la UVIKO-19. Hata hivyo, kutokana na juhudi za Serikali ya awamu ya sita na wadau wa Sekta binafsi hali ya sekta imeanza kurejea katika hali yake, ambapo pia amesema idadi ya Simba imepanda na kukadiliwa Tanzania kuwa na zaidi ya Simba 17000 kwa sasa.

"Mathalan, kwa mwaka 2022, idadi ya watalii wa nje imeongezeka hadi kufikia 1,454,920 na mapato yatokanayo na utalii kufikia Dola za Marekani Milioni 2,527,77. Idadi ya watalii wa ndani wanaotembelea maeneo ya hifadhi imefikia 2,363,260. Ni wazi kuwa bado tuna kazi kubwa ya kuendelea kushirikiana katika kukuza utalii wa ndani lakini pia kutengeneza vifurushi vya utalii vya gharama nafuu ili kuhamasisha utalii wa ndani. Lengo la Serikali ni kufikia watalii milioni 5 na mapato yatokanayo na utalii kufikia bilioni 6 ifikapo mwaka 2025." Amehitimisha Mhe. Mchengerwa


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRILI 15,2023



















Share:

ROYAL TOUR YA RAIS SAMIA YAZAA MATUNDA YA TAWTO.


Na John Mapepele

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mohamed Mchengerwa na Katibu Mkuu Dkt. Hassan Abbasi wameungana na wadau wa sekta ya utalii jijini Arusha leo usiku huu April 14, 2023, kuzindua Chama cha Waongoza Utalii Wanawake (TAWTO) kinacholenga kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara kutangaza Utalii kama Mhe Rais alivyofanya katika filamu ya Royal Tour.

Hafla hiyo pia imehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu Ndug. Anderson Mutatembwa.

“ Sekta ya utalii mtarajie ushirikiano mkubwa kutoka kwangu na timu yangu kuliko wakati wowote katika kuhifadhi na kutangaza utalii,” alisema Mhe. Mchengerwa.

Ametoa rai kuwa madhumuni ya Chama hicho ni muhimu yaende sambamba na kuhamasishana kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu za kuendesha shughuli za utalii nchini hususan Sheria ya Utalii ya Mwaka 2008 na kanuni zake. Pamoja na kuzingatia muongozo wa maadili kutoka Shirika la Utalii Duniani (UNWTO).

Aidha amesisitiza kuwa wabunifu zaidi katika kuandaa vifurushi vya safari za watalii (Tour Packages) ambavyo zitafungamanisha vivutio na mazao mbalimbali ya utalii kama fukwe, michezo, mikutano na matukio, Utamaduni na Utalii wa vyakula ili kuvutia watalii wengi zaidi, kuongeza idadi ya siku za wageni kukaa nchini na hivyo kuongeza mchango wa utalii katika Pato la Taifa.

Pia, ametilia mkazo utoaji wa huduma bora katika sekta yetu ya utalii na ukarimu ambapo amesema hatua hiyo itasaidia nchi yetu kuongeza idadi ya watalii na watalii kurudi kutembelea Tanzania.

Hapa naomba nisisitize makundi yanayohudumia watalii kama Waongoza Watalii (Tour Guides) na wafanyakazi katika tasnia ya ukarimu na huduma za malazi. Hawa ndio wanaokaa na wageni muda mrefu zaidi na hivyo ndio hasa mabalozi wa utalii wetu. Ni vema kuweka utaratibu mzuri wa kujenga uwezo kwa makundi haya ili kuhakikisha wanatimiza wajibu wao ipasavyo na kwa weledi. hali kadhalika, kwa kuzangitia kuwa sekta ya utalii kwa kiasi kikubwa inaendeshwa na sekta binafsi Serikali iliona umhuhimu wa wadau wa utalii kuwa na shirikisho la vya waendeshaji utalii yaani TCT, kwa msingi huo nitoe wito kwa chama chenu kujiunga na kushirikiana kikamilifu na shirikisho hilo (TCT), kwa mukthaza mzima wa kundeleza na kukuza sekta ya utalii nchini" amesisitiza, Mhe. Mchengerwa

Awali Mhe. Mchengerwa ameeleza kwamba Sekta ya utalii ni moja ya Sekta zilizoathirika zaidi na janga la UVIKO-19. Hata hivyo, kutokana na juhudi za Serikali ya awamu ya sita na wadau wa Sekta binafsi hali ya sekta imeanza kurejea katika hali yake, ambapo pia amesema idadi ya Simba imepanda na kukadiliwa Tanzania kuwa na zaidi ya Simba 17000 kwa sasa.

"Mathalan, kwa mwaka 2022, idadi ya watalii wa nje imeongezeka hadi kufikia 1,454,920 na mapato yatokanayo na utalii kufikia Dola za Marekani Milioni 2,527,77. Idadi ya watalii wa ndani wanaotembelea maeneo ya hifadhi imefikia 2,363,260. Ni wazi kuwa bado tuna kazi kubwa ya kuendelea kushirikiana katika kukuza utalii wa ndani lakini pia kutengeneza vifurushi vya utalii vya gharama nafuu ili kuhamasisha utalii wa ndani. Lengo la Serikali ni kufikia watalii milioni 5 na mapato yatokanayo na utalii kufikia bilioni 6 ifikapo mwaka 2025." Amehitimisha Mhe. Mchengerwa


Share:

Friday, 14 April 2023

WANANCHI WAMPONGEZA MBUNGE WA JIMBO LA KISHAPU BUTONDO KUTUMIA FEDHA VIZURI ZA MFUKO WA JIMBO KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

 

Wananchi wa Kishapu wamemshukuru Mbunge wa Jimbo la Kishapu Boniphace Butondo kwa mgawanyo mzuri wa Fedha za mfuko wa jimbo kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kuangalia hasa sehemu zenye uhitaji.

Shukurani hizo wamezitoa leo mbele ya Katibu wa Mbunge kwenye hafla fupi ya kukabidhi Saruji pamoja na Bati kwajiili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ndani ya Halmashauri ya Kishapu

Diwani wa Kata ya Kishapu Mhe, Joel Charles Ndettoson ameishukuru Ofisi ya Mbunge kwa kuendelea kuunga juhudi za wananchi wake kwa kuwapatia saruji mifuko 50 kwaajili ya ujenzi wa darasa katika shule ya Msingi Lubaga

“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kupitia Mfuko wa Jimbo ameweza kusaidia kata ya Kishapu, hii ni awamu ya tatu sasa kwa awamu hii ameweza kutusaidia mifuko 50 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya msingi Lubaga, Mwaka jana alitupatia Bati 62 na Mifuko 50 ya Saruji, Mwaka juzi alitupatia Bati 100 kwa hiyo mfuko wa jimbo unaendelea kupunguza changamoto kwa jamii pia nimshukuru sana Mheshimia Rais kwa kuendelea kutupatia fedha kupitia mfuko wa Jimbo 

Naye Diwani wa Kata ya Lagana Mhe, Luhende Sana amesema kuwa Mfuko wa Jimbo umekuwa msaada mkubwa sana kwa wananchi hasa wanapojitolea nguvu zao katika kunyanyua maboma na kuona juhudi zao zinaungwa mkono kupitia mfuko wa Jimbo kwenye hatua za ukamilishaji

Kwanza nimshukuru Mhe. Mbunge ndugu yangu Boniphace Butondo kwa kuona Lagana ni miongoni mwa kata ambazo zinasitahili kupata mgawanyo wa mfuko wa Jimbo hii inaleta hamasa kubwa sana kwa wananchi ambao wanajitolea nguvu zao pindi wanapoona hatua za ukamilishaji wa mabona unafanyika hii itasaidia sana kwa wananchi kuwa wazalendo katika kuchangia nguvu zao kwenye miradi ya maendeleo. Kwa kata ya Lagana tumepata mifuko 150 ya saruji pamoja na Bati 46

Aidha katibu wa Mbunge Ndugu, godfrey Nchimika ametoa wito kwa watendaji wote wanaohusika na Utekelezaji wa miradi kuwa wazalendo kwa nchi yao na hasa katika usimamizi wa miradi ili iweze kukamilika kwa wakati pamoja na utunzaji wa vifaa kwa uaminifu ili usitokee upotevu wa vifaa vya ujenzi.








Share:

WAMILIKI WA KUMBI ZA STAREHE WATAKIWA KUFUATA SHERIA KUDHIBITI KELELE NA MITETEMO

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla akizungumza katika Mkutano na Wadau wa Mazingira kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira leo Aprili 14,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Samuel Gwamaka akizungumza katika Mkutano na Wadau wa Mazingira kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira leo Aprili 14,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mwanahamisi Mnkunda akizungumza katika Mkutano na Wadau wa Mazingira kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira leo Aprili 14,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akiwa katika Mkutano na Wadau wa Mazingira kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira leo Aprili 14,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Wadau mbalimbaali wa Mazingira wakiwa kwenye mkutano kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira leo Aprili 14,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

(PICHA NA EMMANUEL MBATILO)


******************

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla ameongoza Mkutano na Wadau wa Mazingira kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki leo tarehe 14 April 2023, uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika Mkutano huo, Mhe.Makalla amesema kuna umuhimu mkubwa viongozi wa dini wakapatiwa elimu kusimamia katazo na zuio la mifuko ya plastiki pamoja na udhibiti wa makelele kwenye maeneo ya makazi ya watu ili kuondoa changamoto hizo ambazo zimekuwa zikitokea katika maeneo mbalimbali kwenye Jiji la Dar es Salaam.

Mhe. Makala amesisitiza juu ya changamoto ya viwango vya juu vya kelele katika kumbi za starehe na nyumba za ibada pamoja na kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki akiwaasa wanajamii kuepuka matumizi ya mifuko hiyo kwani ni chanzo cha uharibifu wa mazingira na kutoa muda wa wiki moja kwa NEMC na TBS kuweka ratiba ya kupita katika wilaya za jiji la Dar es salaam kufanya ukaguzi wa kutoa elimu ya matumizi sahihi ya mifuko ya plastiki.

Amesema "Dar es salaam bila mifuko ya plastiki na kelele zilizodhidi viwango inawezekana na ni wakati wa kila mmoja kuwajibika na kuhakikisha haki inatendeka bila kupepesa macho na kwa wazalishaji kusalimisha mifuko ya plastiki waliyoizalisha katika ofisi za NEMC bila kuchukuliwa hatua."

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Samuel Gwamaka amewataka wananchi kufuata Kanuni na Sheria za Uhifadhi wa Mazingira kwa kudhibiti viwango vya kelele na mitetemo katika maeneo mbalimbali hususani kumbi za starehe na makanisa pamoja na kupunguza matumizi ya mifuko ya plastiki iliyopigwa marufuku kwani ni chanzo cha uchafuzi wa mazingira.

Amesisitiza kuwa "wazalishaji, wasambazaji na wauzaji wa mifuko ya plastiki wahakikishe kuwa viwanda vyao vinasajiliwa na Baraza na kupata cheti cha Tathmini ya Athari kwa Mazingira kabla ya kuanza uzalishaji na kufuata matakwa ya Sheria na viwango sahihi vilivyowekwa."

Pia ametoa angalizo kwa wazalishaji na wasambazaji wa mifuko ya plastiki kunisalimisha kwani Baraza litatoa donge nono kwa yeyote atakaye toa taarifa juu ya uwepo wa kiwanda au wasambazaji wa mifuko na vifungashio visivyokidhi viwango.

Aidha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya amesema "wale wote wanaomiliki viwanda vya kuzalisha plastiki ambao wana leseni ya TBS endapo watahitaji kuhuisha leseni au kuchukua leseni mpya lazima wawe na Cheti cha Mazingira kutoka NEMC.

Nao wadau wa mazingira walitoa maoni yao juu ya udhibiti wa viwango vya kelele na mitetemo kwa kuomba kupatiwa vifaa vya kupimia sauti, kuboreshaji njia za utoaji elimu kwa wananchi ili kuwezesha kudhibiti kelele chafuzi pamoja na kupewa vibali maalum ili kuwezesha viongozi katika ngazi za mtaa kuchukua hatua stahiki kwa wanaokiuka Sheria.

Kwa upande wa katazo la mifuko ya plastiki wadau wameisihi Serikali kuhakikisha kuwa wananchi wanapata taarifa sahihi juu ya mifuko iliyopigwa marufuku na pia kuboresha njia bora za kuwadhibiti wale wote wanaozalisha mifuko ya plastiki kwa kuwachukulia hatua za Kisheria ili kuweza kutokomeza tatizo hili.
Share:

SEKTA YA MAKAA YA MAWE YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MIONGOZO YA USALAMA NA AFYA

Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini Bw. Wilbert Ngowi akitoa elimu ya masuala ya usalama na afya katika uchimbaji na uchukuzi wa makaa ya mawe kwa wafanyakazi na viongozi wa kampuni za BECCO na ARIA Commodities Mkoani Ruvuma.
Viongozi na Wafanyakazi wa Kampuni za ARIA Commodities na BECCO Limited wakifuatilia mada ya masuala ya usalama na afya mahali pa kazi kutoka kwa Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini Bw. Wilbert Ngowi (hayupo pichani)
Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini Bw. Wilbert Ngowi akijibu swali kutoka kwa mfanyakazi wa BECCO Limited aliyeuliza kuhusu namna sahihi ya kujikinga dhidi ya vumbi la makaa ya mawe katika maeneo ya ofisi na mgodi.
Mfanyakazi wa Kampuni ya uchimbaji wa Makaa ya mawe ya JITEGEMEE Limited akiuliza swali kwa Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini Bw. Wilbert Ngowi (hayupo pichani) kuhusu njia sahihi za kuzuia na kudhibiti vihatarishi katika maeneo yao ya migodi.

************************

Na Mwandishi wetu

Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) umetoa wito kwa wawekezaji na waajari wa sekta ya makaa ya mawe kuhakikisha wanazingatia ipasavyo sheria na miongozo ya usalama na afya ili kuwalinda wafanyakazi wao dhidi ya ajali na magonjwa yanayoweza kuwapata katika maeneo yao ya kazi.

Wito huo umetolewa kupitia kwa Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini, Bw.Wilbert Ngowi alipokuwa akihitimisha programu maalumu ya siku nne ya mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa Viongozi na Wafanyakazi wa sekta ya makaa ya mawe Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma.

“Sekta ya makaa ya mawe inakabiliwa na vihatarishi mbalimbali kama ilivyo kwa sekta zingine za madini mfano mfanyakazi anapovuta vumbi la makaa kwa muda mrefu anaweza kupata ugonjwa wa nimonia ya mapafu meusi (coal worker’s pneumoconiosis), ugonjwa huu hauna dalili za haraka wala tiba hivyo mfanyakazi akiathirika na huu ugonjwa utakuwa ndio ulemavu wake wa maisha na pengine unaweza kumsababishia kifo,”

“Hivyo basi kutokana na sekta hii kukabiliwa na vihatarishi vingi na vinavyoweza kuhatarisha Maisha ya wafanyakazi tumeona tuanze kuchukua tahadhari mapema kwa kuendesha programu maalumu ya mafunzo kwa lengo la kuwapa elimu wafanyakazi hawa ili waweze kuepukana na vihatarishi hivi vya ajali na magonjwa vinavyoweza kuwapata katika maeneo yao ya kazi ikiwa ni pamoja na kuepukana na vumbi la makaa ya makaa ya mawe”. Alisema Bw. Ngowi akiongeza kwa kutoa wito kwa wawekezaji.

“Nitoe wito kwa Waajiri na Wawekezaji wa Sekta ya Makaa ya Mawe wahakikishe kwamba wanazingatia taratibu zote za usalama na afya katika maeneo yao yote ya kazi kwa kuchukua tahadhari zote stahiki ikiwa ni pamoja na kuhakikisha vumbi linapungua katika maeneo yao pia wahakikishe vifaa vyote vinavyotumika katika shughuli mbalimbali vinamkinga mfanyakazi dhidi ya vihatarishi vya ajali na magonjwa.” aliongeza Bw. Ngowi.

Aidha kupitia progamu hiyo ya mafunzo, Mkurugenzi wa Oparesheni wa Kampuni ya uchimbaji wa Makaa ya mawe ya Jitegemee Holdings, Bw.Boscow Mabena ameeleza namna ambavyo kampuni hiyo imehamasika katika kuimarisha mifumo ya usalama na afya katika Kampuni yake.

“Tunawashukuru sana OSHA kwa kutupatia elimu hii ya usalama na afya katika sekta yetu ya makaa ya mawe, wamekuwa wakitutembelea na kutupa miongozo mbalimbali ya namna sahihi ya kuboresha mazingira ya kazi hivyo tumehamasika kwa kiasi kikubwa sana na tayari tumetenga bajeti ya mafunzo ya usalama na afya, tutapeleka wafanyakazi wakahudhurie mafunzo hayo yanayotolewa na OSHA” alisema Bw. Mabena.

Kwa upande wao washiriki wa mafunzo hayo kutoka kampuni mbalimbali wanaeleza namna ambavyo elimu hiyo itawaongezea tija katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

“Nime elimika kwa kiasi kikubwa sana na kama kiongozi itanisaidia kuwasimamia vyema wafanyakazi wenzangu katika eneo letu la kazi ikiwemo kuwalinda dhidi ya vumbi la makaa ya mawe linaloweza kusababisha ugonjwa wa nimonia ya mapafu meusi vivilevile tunaahidi kutekeleza mambo yote yaliyoagizwa na sheria ya usalama na afya ikiwemo kuhakikisha wafanyakazi wote wana tekeleza majukumu yao wakiwa wamevaa vifaa kinga.” Alisema Rajabu Miraji

Kwa upande wake Bi. Merce Gerald ambaye ni Mhandisi kutoka Kampuni ya Jitegemee ameeleza kuwa mafunzo haya yataleta mabadiliko ya kiusalama kwa kiasi kikubwa sana katika maeneo yao ya kazi.

“Elimu hii itatusaidia sana kujikinga na vihatarishi mbalimbali tunavyokabiliana navyo katika maeneo yetu ya kazi hivyo niombe OSHA waendelee kutoa mafunzo haya kwa migodi mingine ili waweze kuokoa Maisha ya wafanyakazi wengine wa sekta hii.”alisema Bi. Merce Gerald.

Programu hii maalumu ya mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi katika sekta ya uzalishaji wa makaa ya mawe imefanyika kuanzia tarehe 11 – 14/04/2023 na jumla ya wafanyakazi 400 kutoka kampuni za TANCOAL, RUVUMA COAL, JITEGEMEE HOLDINGS, ARIA COMMODITIES na BECCO LTD wamefikiwa na elimu hiyo.
Share:

DKT RWEZIMULA: TUJIPANGE MIKOPO KWA WANAFUNZI 'SERA YA ELIMU BILA ADA

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk.Franklin Rwezimula akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Abdul-Razaq Badru wakati Naibu Katibu Mkuu huyo alipotembelea HESLB jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Abdul-Razaq Badru (mwenye miwani) akizungumza wakati Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk.Franklin Rwezimula alipotembelea HESLB jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk.Franklin Rwezimula akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Abdul-Razaq Badru wakati Naibu Katibu Mkuu huyo alipotembelea HESLB jijini Dar es Salaam.


**********************





Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetakiwa kujiandaa kwa ongezeko kubwa la wanafunzi wahitaji wanaotokana na sera ya elimu ya msingi na sekondari bila ada ambao wanatarajia kujiunga na taasisi za elimu ya juu kuanzia mwaka 2026/2027.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Franklin Rwezimula amesema kuwa ni muhimu kwa HESLB kuwa na mipango inayoendana na mageuzi makubwa ya elimu yanayofanywa na Serikali ikiwemo kuwawezesha watoto kupata elimu ya msingi na sekondari bila malipo ya ada.

“Bajeti ya mikopo kwa mwaka huu wa 2022/2023 ni TZS 654 bilioni, na mwakani tutarajie itaongezeka zaidi … sasa ni vema mipango yenu (HESLB) iendane na ongezeko linalokuja kuanzia mwaka 2026/2027 ambapo matunda ya sera ya elimu bila ada yataanza kwenda elimu ya juu,” amesema Dkt. Rwezimula.

Dkt. Rwezimula ameyasema hayo alipokutana na Menejimenti ya HESLB katika ofisi za taasisi hiyo jijini Dar es salaam alipofika kujitambulisha na kubadilishana uzoefu baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 26 Februari mwaka huu.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amesema Menejimenti ya HESLB imejipanga na kuandaa mapendekezo ya kuhimili ongezeko la wanafunzi wahitaji wa mikopo katika miaka ijayo.

“Hivi karibuni, tumefanya utafiti kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Uchumi (HEET) kuhusu matokeo ya elimu bila ada katika ugharimiaji wa elimu ya juu miaka ijayo … taarifa ipo na tutawasilisha kwa ajili ya ushauri na maandalizi,” amesema Badru.

HESLB ilianzishwa mwaka 2005 ikiwa na majukumu makuu mawili – kutoa mikopo kwa wanafunzi wahitaji wa elimu ya juu na kukusanya fedha za mikopo zilizoiva zilizotolewa kwa wanafunzi tangu mwaka 1994/1995.
Share:

KAILIMA AMPONGEZA WAZIRI MHAGAMA KWA BAJETI KUPITA BUNGENI


Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa akiwa Bungeni pamoja nae ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (wapili kushoto), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Prof. Joyce Ndalichako (wapili kulia) na Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas Paschal Katambi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama akichangia hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka 2023/24 Bungeni Jijini Dodoma leo Aprili 13,2023. Kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Prof. Joyce Ndalichako
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Ramadhani Kailima akimpongeza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama pamoja na viongozi wengine wa Wizara baada ya kuhitimishwa kwa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka 2023/24 Bungeni Jijini Dodoma leo Aprili 13,2023.




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Prof. Joyce Ndalichako pamoja na manaibu Waziri na Makatibu wakuu wa Wizara zao wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Taasisi mbalimbali zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu baada ya kuhitimishwa kwa bajeji ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha wa 2023/24 Bungeni jijini Dodoma Aprili 13,2023.
***************


Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama amesema Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu imezingatia vipaumbele muhimu katika maeneo yote yanayoratibiwa na Ofisi hiyo ili kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na tija kwa Taifa.

Ametoa kauli hiyo mapema leo wakati akichangia Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya Mwaka wa fedha 2023/24 wakati wa Kikao cha Bunge la 12 Mkutano wa 11 Kikao cha sita Mjini Dodoma.

Waziri Mhagama amesema pamoja na mambo mengine, Bajeti ya Mwaka huu ya Ofisi ya Waziri Mkuu imezingatia masuala muhimu ikiwemo la Uratibu wa shughuli za Serikali kwa kueleza tayari ofisi hiyo umeunda Idara ya ufuatiliaji na Tathimini ya utendaji wa serikaliambapo itawezesha kuwa na taarifa sahihi za utekelezaji wa Shughuki za Serikali.

Akizungumzia kuhusu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Waziri Mhagama amesema, Mamlaka imefanya kazi ya kutosha katika maeneo yote manne ya kimkakati ya kupambana na dawa za kulevya, kupunguza uingizaji wa dawa za kulevya, kufanya ukaguzi katika maeneo yanayofanya biashara ya kemikali bashirifu na kufanya maboresho ya sheria na kuteketeza mashamba mengi ya bangi nchini.

Aliongeza kwa kusema kuwa, Mamlaka imefanya vizuri katika kutoa elimu ya uelewa kuhusu matumizi ya madawa ya kulevya.

“Tumefanya vizuri katika kupunguza athari za madhara ya dawa za kulevya kwa waathirika, na huduma ya za kutibu urahibu wa dawa za kulevya na bado tunaendelea kufanya mashirikiano ya nchi, kikanda na kimataifa ili kukabiliana na jambo hili mtambuka.”Alisisitiza

Kwa Upande wa suala la Sera ya lishe, Waziri amesema Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, itakuja na Mkakati wa kuwa na Sera ya lishe, UKIMWI na Janga la matumizi ya Dawa za kulevya.

Pamoja na hilo, Waziri alieleza kuwa ofisi yake inasimamia Dawati la Afya Moja linaloshughulikia uratibu wa magonjwa ya mlipuko yanayoambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu, ili kuweza kukabiliana nayo na kuangalia usalama wa wananchi.

Aidha alitumia nafasi hiyo kumpongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa kwa falsafa yake ya kuliwezesha Taifa kuwa na ustahimilivu na kuleta mabadiliko makubwa ya kiuongozi, kidemokrasia, kiuchumi na mahusiano ya kimataifa na kuwataka wabunge kuunga mkono falsafa hiyo.
Share:

CCM MKOA WA IRINGA WAIONGEZA NGUVU YA TSH MILIONI 2 MKWAWA QUEENS KWENDA KUIVAA SIMBA QUEENS



Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Daud Yassin akikabidhi kiasi Cha Tsh Milioni 2 Kwa uongozi wa Timu ya Mkwawa Queens inayocheza Ligi kuu ya Soka la wanawake Tanzania inayotarajia kusafiri jumapili kwenda Dar,Kucheza na Simba Queens kiasi Cha TshMilioni 3.4 zinahitajika ambazo zilikuwa zikihitajika Kwa ajili ya safari hiyo .

Akikabidhi msaada huo Leo Kwa uongozi wa timu hiyo ,Yassin alisema chama Cha Mapinduzi kinatambua mchango mkubwa wa Timu ya Mkwawa Queens na Timu nyingine Katika michezo na kuwa kutokana na changamoto ya timu hiyo .

Hivyo alisema Katika kuunga mkono jitihada za Timu hiyo na jitihada za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Katika kuendelea michezo nchini wao kama CCM mkoa wa Iringa wataendelea kuuunga mkono jitihada hizo ikiwa ni pamoja na kusaidia sekta ya michezo ndani ya mkoa wa Iringa.

Alisema jitihada za Mkwawa Queens wanaziona na kuwa ili Timu hiyo kutimiza vema majukumu yake ni vema wadau kuendelea kuunga mkono Timu zote ndani ya mkoa .

"Niwapongeze Sana Uongozi wa Mkwawa Queens Kwa kuendelea kuwakilisha mkoa Katika soka la wanawake na sisi kama chama tupo pamoja "

Aidha Yassin alimpongeza mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendego pamoja na Viongozi wengine wa mkoa huo Kwa kuendelea kusaidia Timu .

Afisa habari wa Mkwawa Queens Francis Godwin alipongeza mchango huo wa chama na kuwa huo ni mchango mkubwa Kwa Timu kupokea .

Alisema Kwa Sasa Timu hiyo inasafari ya kwenda Dar es salaam kucheza na Simba Queens siku ya Jumanne na kuwa timu itaondoka Iringa Jumapili safari ambayo itaigharimu Timu Tsh Milioni 3.4 baada ya hapo inajiandaa Kwa mchezo wake Dodoma na Mkoani Lindi ambako ili kufanikisha Mzunguko uliobaki zaidi ya Tsh Milioni 10 zinahitajika .

Hivyo aliwaomba wadau kuendelea kuisaidia Timu hiyo na kumpongeza jitihada za Mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendego na uongozi wa CCM mkoa chini ya Mwenyekiti Daud Yassin na wote ambao wameendelea kuichangia Timu hiyo .

Godwin pia alimpongeza mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati Kwa mchango wake wa Tsh 200,000 na wote wanaondelea kujitolea Kwa ajili ya Timu akiwemo katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazin Jackson Mnyawami kuchangia Timu namba hii 0715621222 jina la mpokeaji Maryam Swaleh
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger