Thursday, 13 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 14,2023





















Share:

MBUNGE MTATURU AIKUMBUSHA SERIKALI KULIPA WASTAAFU


MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu ,ameendeleza kilio chake cha kucheleweshwa kwa mafao ya wastaafu ambapo safari hii ameikabidhi serikali barua yam zee Simon Albert Makiya kwa ajili ya utekelezaji.

Mei 2022,katika swali lake la msingi Mtaturu aliihoji serikali lini itamaliza changamoto ya kucheleweshewa mafao kwa wastaafu ambapo serikali ilieleza jitihada zake ikiwemo kulipa deni la mfuko wa PSSSF ikiwa ni pamoja na kutoa hatifungani ya Shilingi Trilioni 2.17 ambazo zitaimarisha mtiririko wa mapato na kuwezesha kutoa mafao kwa wakati.

Aidha,Mei 2020,akichangia mjadala wa bajeti ya wizara ya fedha na mipango,Mtaturu aliiomba serikali kuwalipa mapema wastaafu mafao yao na kuwataja wazee wawili wa Ikungi Mohammed Ntandu na Gamilliel Massawe suala ambalo serikali iliahidi kulishughulikia.

Leo April 13,2023,ni mara ya tatu kutoa kilio hicho,“Eneo hili limekuwa likilalamikiwa sana na wabunge wamepata malalalmiko hayo,kuna mzee wangu mmoja ambaye barua yake ninayo ameniletea kama mbunge wake Simon Albert Makiya kutoka Siuyu,

“Barua hii nitaomba niikabidhi kwa waziri,mzee huyu amekuwa akilalamika anasubiri fedha zake za kustaafu na amekuwa akija hapa bungeni akifanya juhudi za kumuona waziri ili asikilize kilio chake,naomba watu wa aina hii watendewe haki ,”amesisitiza.
Share:

HUAWEI CALLS FOR A 'NON-STOP' DIGITAL FUTURE FOR AFRICA'S BANKING INDUSTRY

[Cape Town, ] Huawei today announced its ‘Non Stop Banking’ initiative. Unveiled at the Huawei Intelligent Finance Summit for Africa 2023, the initiative calls for hand-in-hand collaboration between the ICT and banking industries and facilitate a digital future of ‘non-stop’ services, ‘non-stop’ development, and ‘non-stop’ innovation.


In a keynote speech announcing the initiative, Leo Chen, president of Huawei Sub-Saharan Africa Region spoke about why going digital has become such a major imperative for the banking industry. Not only does it make it easier for banks to broaden their customer base, he said, it also saves operational costs, allows them to develop new products, and deepen the customer relationship, thus generating revenues for banks.



In Africa, he added, there’s an even greater imperative for banks to embrace digitization, as it allows for greater financial inclusion. While Chen lauded the innovative work done by many African banks in embracing digitization, he pointed out that all players in the industry need to go further if they’re to embrace the ‘non-stop’ approach that will characterise the future of banking.



Huawei has already served more than 2500 financial customers in over 60 countries and regions, including 50 of the world's top 100 banks. Numerous Huawei technologies, Chen said, are helpful on this front. Over the years, it has provided the foundation and backbone for the digitalization of the banking industry in Africa by supporting the construction of the continent’s ICT infrastructure and digital connectivity in rural areas. Its extensive focus on research and development (R&D), meanwhile, means that it’s well-poised to help the industry shape its future too.



From a technical perspective, he pointed to Huawei's strength in storage, fibre optic networks, IP networks and data communication, which enable ‘multi-domain collaboration’ solutions for banks. For example, its ‘storage and optical connection coordination (SOCC)’ solutions can reduce system switchover time from two minutes to two seconds after a network breakdown, ensuring zero transaction interruptions. The multilayer ransomware protection (MRP) technology, meanwhile, can provide 6-layer protections, from storage, to network, to applications and other layers. It enables a reliable and secure ‘end-to-end’ protection to the whole system. Finally, Huawei’s intelligent network O&M solutions enable faults to be detected in one minute, diagnosed in three minutes, and rectified in five minutes.



Huawei Cloud, the world's fastest-growing major cloud service provider, can additionally support the hybrid multi-cloud service required by banks. Huawei’s digital energy solutions, meanwhile, can help to provide an uninterrupted and green power supply for the banking sector. This effectively addresses power deficit issues and supports ‘non-stop’ banking.


That kind of technological innovation will be important because, as Jason Cao, CEO of Huawei Global Digital Finance pointed out, financial services are becoming mobile and intelligent at a blistering pace.


“The financial industry should pay acute attention to users and their demands, embracing changes,” he said. “Huawei is dedicated to helping its African financial customers address challenges and accelerate changes across six fields: shifting from transaction to digital engagement, cloud-native and agile businesses, data democratization, secure and reliable infrastructure, hybrid multi-cloud and Lego-style modular services, and automated and predictable operation.”


“In this way, Huawei will facilitate financial digitalization and innovatively improve productivity in Africa. Revolving around stability, agility, and intelligence, Huawei aims to build ‘non-stop’ financial services, and achieve ‘non-stop’ development alongside ’non-stop’ innovation,” he added.


Beyond technology, Huawei issued a call for all parties in the industry to come together and build more robust ICT infrastructure, facilitate more measures and policies to encourage digital finance innovation, cultivate a sound innovative ecosystem, and train more digital talent for the industry.


Huawei is particularly active on the last two points. Huawei Cloud’s Spark programme, for example, has pledged to assist 1 000 SMEs over the next three years. And having already trained more than 80 000 digital talents in Africa, it has launched the ‘LEAP’ digital talent training programme in Sub-Saharan Africa region, aiming to train another 100 000 people in the next three years.


The Huawei Intelligent Finance Summit for Africa 2023 brought together more than 200 attendees, including key industry opinion leaders, as well as executives from major banks across Africa.
Share:

MBUNGE CHIKOTA ASHAURI IUNDWE TUME YA KUCHUNGUZA KUSHUKA KWA UZALISHAJI KOROSHO


Na Mwandishi Wetu, DODOMA

Mbunge wa Nanyamba (CCM), Abdallah Chikota, ameomba kuunda Tume huru ya kuchunguza kushuka kwa uzalishaji wa zao la korosho ndani ya miaka mitatu mfululizo licha ya jitihada za kupanua wigo wa kilimo cha zao hilo kwenye mikoa mbalimbali.

Akichangia jana mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake kwa mwaka 2023/24, Mbunge Chikota alisema pamoja na jitihada za serikali za kuratibu upatikanaji wa pembejeo kuna mdondoko wa zao hilo.



“Napongeza serikali ya awamu ya sita kwa kazi kubwa anayoifanya katika kuwekeza katika tasnia ya korosho, tumeona kwa miaka mitatu mfululizo, Serikali ikitoa pembejeo bure kwa wakulima wa korosho, tunaendelea kuishukuru Serikali.”

“Mwaka huu kuna mikataba yenye thamani ya Sh bilioni 340 ambayo imetolewa na nina matumaini pembejeo hizi zitafika kwa wakati na wakulima wa korosho watanufaika na pembejeo,”alisema Chikota.

Kadhalika, alisema pamoja na uwekezaji ulifanywa na serikali kwenye tasnia ya korosho bado kuna anguko la uzalishaji wa korosho nchini ambapo kwa kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2017/18, Tanzania ilifikisha uzalishaji wa tani 320,000.

“Lakini kwa masikitiko makubwa katika msimu uliopita uzalishaji umepungua hadi kufikia tani 160,000 pamoja na uwekezaji mkubwa uliofanywa, ukiuliza Bodi ya Korosho hawana majibu ya uhakika na hata taasisi ya utafiti ya TARI Naliendele hawana majibu ya kutoshereza ya anguko kubwa na uzalishaji wa korosho,”alisema.



Alisisiza “Haiwezekani mikoa ya uzalishaji wa korosho imeongezeka, serikali imefanya uwekezaji wa kutosha lakini uzalishaji unazidi kuwa mdogo.”

Chikota alisema malengo ya Bodi ya Korosho mwaka huu ilikuwa ni kufikisha tani laki nne na Ilani ya Chama cha Mapinduzi na kufikisha tani 700,000 ifikapo mwaka 2025.

“Kwa anguko hili kuna kazi kubwa inayopaswa kufanywa ili kufikia malengo nashauri serikali kuunda tume hii huru yenye wataalamu kutoka nje ili kupata mawazo mapya,”alisema.

Aliomba watumie wataalamu wa nje na SUA ili kuangalia mfumo wa uagiziaji na udhibiti wa pembejeo kwa kuangalia ubora wake.

“Tusiendelee kuwatumia wataalamu wale wale wa TARI na Bodi ya Korosho watatuletea majibu yela yale tuliyoyazoea. Tupate timu mpya, ikiwezekana tuchukue uzoefu kutoka huko,”alisema.

Pamoja na hayo, Chikota aliishauri Serikali kuimarisha miundombinu ya barabara na reli ili kufungua mikoa ya kusini.

Pia alishauri Serikali kutekeleza mradi wa maji kutoka Mto Ruvuma ili kuweza upatikanaji wa maji hatua ambayo itavutia wawekezaji.
Share:

WIZARA YA ARDHI KUWAFIKISHA MAHAKAMANI WADAIWA SUGU


Kamishna wa Ardhi msaidizi mkoa wa Dodoma Jabir Singano.
Mkuu wa Kitengo cha kodi wa Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Denis Masami akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu ukusanyaji wa madeni ya pango la ardhi.


Na Dotto Kwilasa,DODOMA.

SERIKALI kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imesema itawafikisha mahakamani watu wote wanaodaiwa malimbikizo ya kodi ya pango la ardhi pamoja na kukamata mali zao na kubatilisha hati zao mara baada ya kuisha kwa kipindi cha msamaha wa Rais Aprili 30, 2023.

Hayo yameelezwa leo Jijini Dodoma na Mkuu wa Kitengo cha kodi wa wizara hiyo Denis Masami,wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ukusanyaji wa madeni ya pango la ardhi katika kipindi ambacho serikali ilitoa msamaha kwa wadaiwa kulipa bila riba.

Denis amesema,"Mheshimiwa Rais alitoa msamaha kwa waliolimbikiza malipo ya kodi ya pango la ardhi katika kpindi cha kuanzi mwezi Julai hadi Desemba mwaka jana ambapo watu 6,000 walijitokeza kutumia fursa hiyo na kulipa bila riba.

Cha kushangaza watu wengi waliomba muda uongezwe na serikali kutoa msamaha kwa awamu ya pili ya kuanzia mwezi Machi hadi Aprili mwaka huu, ambapo hadi sasa ni watu 8,725 wamejitokeza kulipa bila riba”,amesema.

Amesema hadi sasa kiasi cha malimbikizo ya kodi ambacho kimeshalipwa ni Sh. bilioni 31.5 na kiasi cha riba ambacho kimesamehewa ni Sh. bilioni 21.3.

“Hivyo basi niwasihi wananchi kutumia fursa hii ya msamaha wa Rais wetu Samia Suluhu Hassan, kulipa malimbizo ya madeni yao kodi ya pango la ardhi bila riba kwani muda ukifika mwisho wote walishindwa kulipa tutawachukulia hatua ikiwemo kuwafikisha mahakamani na kushikilia mali zao na kubatilisha hati zao”,amesema.

Kwa upande wake Kamishna wa Ardhi msaidizi mkoa wa Dodoma Jabir Singano, amesema katika kipindi cha msamaha wa Rais watu zaidi ya 1,200 wamejitokeza kulipa madeni yao.

Amefafanua kuwa kwa mkoa wa Dodoma pekee watu zaidi ya 1,200 wamejitokeza kulipa na kiasi cha Sh. bilioni 1.2 kimeshalipwa hadi sasa na kwamba wanaendelea kuhimiza wote ambao bado wanadaiwa kulipa katika muda huu uliobaki.

Amesema katika jitihada za kuongeza makusanyo mkoa umeendelea kutatua kero zilizokuwepo ikiwemo kukwama kwa malipo ya miamala ya maombi ya wateja.

“Lakini pia kulikuwepo na shida ya upatikanaji wa namba za malipo (contral numbar) hili pia tumelifanyia kazi ambapo tumetoa namba za malipo zaidi ya 4,050 kwa wateja kupitia timu yetu tuliyoiunda kulifanyia kazi suala hili lililokuwa kikwazo kwa wananchi wetu”,amesema
Share:

Wednesday, 12 April 2023

CHIKOTA:NANYAMBA KUNA UPUNGUFU WA WATUMISHI WA AFYA 610




Na Mwandishi Wetu, DODOMA

SERIKALI imeombwa kupeleka watumishi wa kada za afya kwenye Halmashauri zinazokabiliwa na uhaba mkubwa ikiwamo Halmashauri ya Mji wa Nanyamba yenye upungufu wa watumishi wa kada hiyo 610.

Akiuliza maswali bungeni leo, Mbunge wa Nanyamba (CCM), Abdullah Chikota, amesema upungufu watumishi huo upo kwenye Kituo Cha Afya Majengo, Jinyecha, Kilomba na Hospitali ya Halmashauri hiyo.

"Serikali Ina mpango gani wa dharura wa kupunguza tatizo la watumishi Nanyamba. pia Wizara ya Afya imetoa mwongozo wa wanafunzi waliomaliza masomo kada za afya wajitolee kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, je serikali haioni ni wakati muafaka wa kutenga fedha kwasasa waanze kufanya kazi kwenye maeneo yenye upungufu mkubwa,"amesema.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Dk.Festo Dugange, amekiri kuwapo na upungufu huo na kwamba mpango wa serikali ni kuajiri na kupeleka kwenye maeneo yenye upungufu.

"Nikuhakikishie katika ajira zilizotangazwa Halmashauri zenye upungufu mkubwa zitapewa kipaumbele,"amesema.

Katika swali la msingi, Mbunge huyo alitaka kujua mkakati wa Serikali wa kupeleka watumishi na vifaa tiba katika Kituo cha Afya Majengo.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri huyo alisema katika miaka mwili ya mwaka 2020/21 na 2021/2022 Serikali iliajiri Watumishi wa Kada za Afya 10,328 na kati ya hao Halmashauri ya Mji Nanyamba ilipata Watumishi 51 wa kada mbalimbali za afya.

Dk. Dugange alisema Serikali inatambua changamoto ya uhaba wa wataalam wa afya katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Aidha, alisema Kituo cha Afya Majengo kilipangiwa watumishi nne ambao ni Mteknolojia Maabara, Tabibu Msaidizi na Wauguzi wawili.

Dk. Dugange alisema katika mwaka wa fedha 2022/23, Serikali imepeleka vifaa na vifaa tiba katika Halmashauri ya Nanyamba vyenye thamani ya shilingi milioni 300 kwa ajili ya vituo vya huduma za afya.

Share:

RAIS MSTAAFU WA MSUMBIJI CHISANO MGENI RASMI UTOAJI TUZO YA UANDISHI BUNIFU JIJINI DAR ES SALAAM



Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Joaqium Alberto Chissano amewasili nchini kushiriki hafla ya utoaji tuzo ya Kitaifa ya Mwl. Nyerere ya Uandishi Bunifu inayotarajiwa kufanyika Aprili 13, 2023 jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia ujio wa Kiongozi huyo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof. Adolf Mkenda amesema Rais Mstaafu Chissano anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika utoaji wa Tuzo hizo ambazo zinatolewa kwa mara ya kwanza nchini.

Prof. Mkenda ameongeza kuwa Kamati maalum ya Tuzo ilimpendekeza Rais Chissano kuwa mgeni rasmi kutokana na ukweli kwamba ni Rais wa kwanza kuhutubia kutumia lugha ya kiswahili katika Mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika.

"Tunayo furaha kuwa na Mgeni Rasmi Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Joaquim Alberto Chissano ambaye mbali na kuongea lugha ya kiswahili vizuri lakini pia ni Mkuu wa nchi wa kwanza kutumia lugha ya kiswahili katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika," amesema Prof. Mkenda

Ameongeza kuwa mshindi wa Tuzo hiyo mbali ya kupata zawadi ya fedha taslimu, vitabu vyake vitachapishwa na kusambazwa katika shule pamoja na maktaba kwa gharama za Serikali.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Kitaifa ya Mwl. Nyerere Prof. Penina Mlama amesema Kamati ilipokea miswada 283 ya riwaya na mashairi tuzo ambayo ilishindanishwa na kupata washindi watakaotangazwa Aprili 13, 2023.

Prof. Mlama ameongeza kuwa katika hafla hiyo waandishi nguli na maarufu watashiriki akiwemo Prof. Abdallatif Abdalla, Prof. Farouk Taban, Ida Hadjivayanis na Moyez Vassanji.

Aidha Mwenyekiti huyo amesema kumalizika kwa hafla ya utoaji tuzo za Mwaka 2023 ndio kuanza kwa maandalizi ya tuzo za Mwaka 2024 ambapo Miswada itaanza kupokelewa kuanzia Juni 1, 2023

Tuzo ya Taifa ya Mwl. Nyerere ya Uandishi Bunifu inatolewa kwa lengo la kuhamasisha uandishi Bunifu, usomaji vitabu, kutunza utamaduni ,kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili na kuimarisha Uchapishaji.
Share:

LHRC YAZINDUA RIPOTI YA HAKI ZA BINADAMU YA MWAKA 2022, YAIPONGEZA SERIKALI


*********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wameipongeza Serikali kwa kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari ikiwemo kwa kuvifungulia vyombo vinne vya habari vilivyokuwa vimefungiwa.

Pongezi hizo zimetolewa leo Aprili 12,2023 uzinduzi wa Ripoti ya Haki za Binadamu ya mwaka 2022 ambayo imefanyika kwa njia ya mtandao kwa kuwajumuisha waandishi wa habari mbalimbali.

Amesema licha ya Serikali kufanya vizuri kwenye suala hilo lakini bado kuna sheria mbalimbali ambazo zina vifungu vinavyominya uhuru wa vyombo vya habari, ikiwemo Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016.

"Tunafurahi pia kuondolewa kwa katazo la mikutano ya kisaisa ya hadhara hivi karibuni, ambalo lilikuwa linakiuka uhuru wa kujumuika na kukuanyika kwa muda mrefu, ikiwemo mwaka 2022.

Aidha amesema katika upande wa vitendo vya ukatili, tathmini walioifanya inaonyesha watoto walikuwa ni wahanga wakuu wa vitendo hivyo (47%), wakifuatiwa na wanawake (33%), na wazee (10%), watu wenye ulemavu (4%), na wengine, ikiwemo wanaume, (6%), hivyo kukiuka haki ya uhuru dhidi ya ukatili.

Amesema Matukio ya wananchi kujichukulia sheria mkononi yameendelea kuwa mwiba kwa haki ya kuishi, ambapo kwa mwaka huu LHRC imekusanya matukio 40, ambayo ni 18 zaidi ukilinganisha na mwaka 2021.

Hata hivyo amesema kuwa matukio ya mauaji yanayotokana na imani za kishirikina yamepungua, lakini bado ni changamoto, hasa kwa wanawake, ambao walikuwa ni 52% ya wahanga.

"Mashambulio na mauaji ya watu wenye ualbino pia yameibuka upya miaka ya hivi karibuni, na mwaka 2022 lilitokea tukio jingine la mauaji ya mtu mwenye ualbino mkoani Mwanza, ambaye alifariki baada ya kukatwa mkono. Mauaji ya mwenza yanayofanywa na mwenza pia yameendelea kuathiri haki ya kuishi yakisababishwa na wivu wa kimapenzi". Amesema

Amesema Haki ya usawa mbele ya sheria imeandelea kuwa mojawapo ya haki zinazokiukwa zaidi kwa sababu ya vikwazo mbalimbali vya upatikanaji haki na changamoto katika mfumo wa haki jinai.

"Mojawapo ya vikwazo vikubwa vya upatikanaji haki kwa mtazamo wa wanajamii ni rushwa (82%), ikifuatiwa na kesi kuchukua muda mrefu na uelewa mdogo kuhusu sheria (54%)". Amesema
Share:

PURA, EACOP WABADILISHANA UZOEFU USHIRIKI WA WATANZANIA

Meneja wa Ushiriki wa Wazawa wa Kampuni ya EACOP, Bw. Olivier Foulonneau (wa kwanza kushoto), Mkuu wa Masuala la Kujenga Uwezo, Bi. Martha Makoi (wa pili kushoto), Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wazawa na Uhusishwaji wa Wadau kutoka PURA, Bw. Ebeneza Mollel (wa pili kulia) na Bw. Hakeem Mwaruka kutoka PURA katika picha ya pamoja mara baada ya kikao.

****************

Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imekutana na kufanya mazungumzo na Kampuni ya Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) - upande wa Tanzania kwa lengo la kubadilishana uzoefu katika eneo la kuongeza ushiriki wa wazawa kupitia programu za kujenga uwezo. Mazungumzo hayo yalifanyika tarehe 11 Aprili 2023 katika Ofisi za EACOP Jijini Dar es Salaam. Miongoni kwa waliohudhuria kikao hicho ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wazawa na Uhusishwaji wa Wadau kutoka PURA, Bw. Ebeneza Mollel na Meneja wa Ushiriki wa Wazawa kutoka Kampuni ya EACOP, Bw. Olivier Foulonneau.

Akiongea katika kikao hicho, Bw. Ebeneza alieleza kuwa, miongoni mwa mikakati inayotumiwa na PURA kuongeza ushiriki wa watanzania katika shughuli za mkondo wa juu wa petroli ni kuwafikia na kuwashirikiana na wadau mbalimbali wa sekta hiyo. Kupitia mashirikiano hayo, PURA hupata mawazo ya wadau juu ya jinsi ya kuongeza ushiriki wa watanzania na kupata kusikia changamoto zinazowakabili wadau hao wakati wa utekelezaji wa matakwa ya kisheria ya ushiriki wa watanzania.

“PURA inaamini kuwa, suala la kuongeza ushiriki wa watanzania linahitaji juhudi shirikishi ili kufikia matokeo yanayotarajiwa. Kwa kuwa EACOP ni mmoja wa wadau wenye mchango mkubwa katika kuongeza ushiriki wa watanzania, PURA iliona ipo haja ya kukutana na kampuni hii kubadilishana uzoefu katika suala hili” aliongeza Bw. Ebeneza.

Kwa upande wake, Bw. Oliver alisema ni heshima kubwa kuwa na mazungumzo na PURA kama mmoja wa wadau kujadili suala la ushiriki wa watanzania ikiwemo jitihada zinazofanywa na Kampuni ya EACOP katika eneo hilo.

“Kampuni ya EACOP, mbali na kuhakikisha kuwa wakandarasi wakuu wa mradi wanazingatia matakwa ya ushiriki wa watanzania kama yalivyoainishwa katika Mkataba wa Nchi Hodhi na Kanuni za Ushiriki wa Watanzania za mwaka 2017; Kampuni imekuwa ikifanya programu mbalimbali za kuwajengea uwezo watanzania na watoa huduma wakitanzania” aliendelea bwana Olivier.

Akifafanua zaidi kuhusu mikakati inayotekelezwa EACOP Tanzania katika kuwajengea uwezo watanzania, Afisa anayehusika na masuala ya kujenga uwezo, Bi.Martha Makoi alisema kuwa kampuni hiyo inashirikiana na vyuo mbalimbali vya ufundi stadi kama vile Chuo cha Ufundi Arusha na Taasisi ya Teknolojia Kilimanjaro (KIITEC). Mashirikiano haya yatawezesha vyuo hivyo kuwa na uwezo wa kuzalisha wataalamu watakaohitajika katika Mradi wa EACOP (upande wa Tanzania).

Mradi wa EACOP unahusu ujenzi wa bomba la mafuta lenye urefu wa kilomita 1,443 litakalosafirisha mafuta ghafi kutoka maeneo ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania ambapo mafuta hayo yatauzwa katika masoko ya nje. Kwa upande wa Uganda, bomba litapitia wilaya 10 na kaunti 25 na litakuwa na jumla ya kilomita 296. Nchini Tanzania, bomba litakuwa na urefu wa kilomita 1,147 na litapita katika mikoa 8 na wilaya 25. Utekelezaji wa mradi huu utaleta na fursa nyingi zikiwemo ajira na ugavi wa bidhaa na huduma.
Share:

DART KUPANDA MITI 1,000 KWENYE MIUNDOMBINU YAKE DAR ES SALAAM

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba, Mwenyekiti wa Bodi DART Dkt. Florens Turuka,Mkurugenzi wa DART, Dkt. Edwin Mhede pamoja na viongozi wa NMB wakiwa katika uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba akipanda mche wa mti katika kando ya barabara ya mabasi yaendayo kasi wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023



Mwenyekiti wa Bodi DART Dkt. Florens Turuka akipanda mche wa mti katika kando ya barabara ya mabasi yaendayo kasi wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023
Mkurugenzi wa DART, Dkt. Edwin Mhede akipanda mche wa mti katika kando ya barabara ya mabasi yaendayo kasi wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba akizungumza wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023
Mwenyekiti wa Bodi DART Dkt. Florens Turuka akizungumza wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023.
Mkurugenzi wa DART, Dkt. Edwin Mhede akizungumza wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023

************


WAKALA wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), imepanga kupanda miti zaidi ya 1,000 kwenye kilomita 154 ambayo miundombinu ya mabasi yake inapita jijini hapa.


Hayo yalisemwa leo Aprili 12,2023 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa DART, Dkt. Edwin Mhede, wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti hiyo kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo.


Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Dar es Salaam wamiwemo wa benki ya NMB.


Dk. Mhede alisema kabla ya ujenzi wa miundombinu ya mwendokasi kulikuwa na uoto wa asili na miti ya aina mbalimbali hivyo DART inawajibika kuirejesha hali ilivyokuwa.


“Sisi tunapojenga barabara kwa kiasi kikubwa tunaharibu uoto wa asili na miti kwasababu kama kulikuwa na mti tunaukata na nyinyi mliokuwa Dar es Salaam wakati huo naamini mnakumbuka hali ilivyokuwa hapa Ubungo kabla ya ujenzi huu, ile hali haipo tena ndiyo sababu tunaona tunawajibika kuirejesha,” alisema Dk. Mhede


Alisema asilimia 45 ya wakazi wa Dar es Salaam wanatumia njia za kwenda kwa miguu (shoroba), ambazo kwa sasa hazina miti ambayo zamani iliwasaidia kupita kivulini hali ambayo alisema lazima irejelezwe.


“Nitoe wito kwa watumiaji wa hizi njia za kwenda kwa miguu waitunze hii miti kwasababu itakuwa msaada mkubwa kwao tumeanza kupanda miti leo lakini tutaendelea mpaka kufikia miti zaidi ya 1,000,” alisema


Naye Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba, alisema uzinduzi wa upandaji miti hiyo ni jambo kubwa na la kihistoria kwa wakazi wa Ubungo na jijini Dar es Salaam kwani itasaidia kwa kiwango kikubwa kurejeleza mazingira yaliyoharibiwa kutokana na shughuli mbalimbali za ujenzi.


“Mazingira ni uhai hivyo ukiyahifadhi mazingira na yenyewe yatakuhifadhi ukiyaharibu na yenyewe yatakuadhibu kwa hiyo natoa wito kwa wananchi wa Ubungo waunge mkono kampeni hii kwa kutunza miti itakayopandwa, kila mtu ambaye miti hii itapandwa mbele ya nyumba yake au eneo lake la biashara atawajibika kuitunza” alisema


Mkuu huyo wa Wilaya alisema alishatoa maelekezo kwa viongozi wa mitaa na kata kuitambua miti hiyo na kuitunza kwa hali na mali itakapopandwa na DART na wafanyabiashara ndogo ndogo wafanye biashara zao sehemu ambazo hazina miti.


“Wafanyabiashara ndogo ndogo lazima wajue umuhimu wa kutunza mazingira kwaajili yao na vizazi vijavyo na wakumbuke kwamba ukiyalinda mazingira na yenyewe yatakulinda kwa hiyo kila mmoja wetu awe mlinzi wa mazingira kwa kuhakikisha miti hii inastawi,” alisema


Aliwataka watanzania kuona fahari ya kupanda miti kwa kushiriki vyema kwenye kampeni ya upandaji miti kwa Mkoa mzima akisema kuwa hata yeye binafsi amekabidhiwa mti ambao ameupanda na kuuwekea alama kwaajili ya kuhakikisha anafuatilia ukuaji wake.


“Huu mti ambao nimeupanda leo nimeagiza wauwekee alama ili niwe naupitia mara kwa mara kuumwagilia na kuuwekea mbolea na mti huu utakapokuwa nitakuwa nimetoa mchango mkubwa kwa taifa katika kuhifadhi mazingira,” alisema


Alisema viongozi wa kitaifa, Rais Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais, Dk. Phillip Mpango na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wamekuwa mstari wa mbele kuhamasisha upandaji wa miti kwaajili ya kuhifadhi mazingira hivyo wananchi wanapaswa kuiga mfano huo na kupanda miti.




Share:

WANNE WATUPWA JELA MIAKA 20 KWA KUKUTWA NA PEMBE ZA NDOVU


Watu wanne wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 kwenda jela baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kukutwa na vipande tisa vya pembe za ndovu, kinyume cha sheria ya wanyama pori ya mwaka 2005 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016 wakiwa katika hatua za mauzo ya nyara hizo za serikali.

Hukumu hiyo imetolewa katika mahakama ya hakimu mkazi Mkoa wa Shinyanga na hakimu mkazi Yusuph Zahoro, baada ya kupitia ushahidi wa pande zote mbili na kuwatia hatiani washitakiwa wote wanne waliokuwa wanakabiliwa na Kesi ya uhujumu uchumi namba 1 ya mwaka 2022.

Washitakiwa hao walikutwa na vipande 9 vya pembe za ndovu vyenye thamani ya milioni 69.21 ambapo washitakiwa walikamatwa wakiwa katika hatua za kuuza nyara hizo kata ya Solwa wilaya ya Shinyanga.

Waliohukumiwa kifungo cha miaka 20 jela ni Emanuel Shija Basu, Shija Kaswahili, Revocatus Mtara na Daud Ndizu ambao walitenda kosa hilo July 13 , 2022 baada ya kukutwa na nyara za serikali kinyume cha sheria.

Chanzo - EATV
Share:

Tuesday, 11 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 12,2023





























Share:

MAKABIDHIANO YA BOTI MBILI ZA DORIA TRA NA KAMPUNI YA AMIKAN VENTURES

Boti za doria ambazo zimekabidhiwa na kuzinduliwa katika kituo cha forodha cha TRA leo Aprili 11,2023 Jijini Dar es Salaam 
Kamishna Mkuu wa TRA, Bw.Alphayo Kidata akizungumza katika hafla ya makabidhiano na uzinduzi wa boti za doria na kampuni ya Amikan Ventures katika kituo cha forodha cha TRA leo Jijini Dar es Salaam Jijini Dares Salaam
Kamishna wa Forodha na Ushuru wa TRA Bw. Said Athumani akizungumza 
katika hafla ya makabidhiano na uzinduzi wa boti za doria na kampuni ya Amikan Ventures katika kituo cha forodha cha TRA leo Jijini Dar es Salaam Jijini Dares Salaam


*****************


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MAMLAKA ya mapato Tanzania (TRA) wamefanya makabidhiano ya boti za doria na kampuni ya Amikan Ventures katika kituo cha forodha cha TRA Jijini Dares Salaam ambapo boti mbili zimekabidhiwa na kuzinduliwa kwaajili ya kuanza kazi.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Aprili 11,2023 Jijini Dar es Salaam katika hafla hiyo, Kamishna Mkuu wa TRA, Bw.Alphayo Kidata amesema boti hizo zitafanya kazi ya doria katika pwani ya Tanzania na maziwa kupambana na vitendo vya magendo ambavyo vinahatarisha mipango ya TRA katika kukusanya mapato ya nchi.

Amesema waingizaji wa bidhaa bandia na bidhaa za magendo wamekuwa wakitumia mwanya wa urefu wa mpaka wa pwani ya bahari ya hindi kwa kuingiza bidhaa bandia ikijumuisha dawa, vyakula, mavazi, viatu, vifaa vya elektroniki, na vinywaji vyenye pombe.

"Uingizaji wa bidhaa kama hizi zinaathiri vibaya uchumi wa nchi kupitia kukosa mapato, kukwamisha ukuaji wa viwanda vya ndani na biashara halali, na kuathiri afya na usalama wa watumiaji". Amesema Bw.Kidata.

Aidha amesema gharama za ununuzi ya boti hizo zilipitishwa wakati wa bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22 ambapo Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ilitenga bajeti ya Tsh 2.5 Billioni kwa ajili ya ununuzi wa boti mpya za doria. Hivyo basi boti hizo mbili ambazo wamekabidhi wameona wazipeleke zikafanye kazi za doria kwa mikoa ya Dar es salaam na Kigoma ambapo kuna matukio mengi ya magendo.

Kwa upande wake Kamishna wa Forodha na Ushuru wa TRA Bw. Said Athumani amesema boti hizo ambazo zimekabidhiwa ni sehemu ya bajeti ya Tsh. Billioni 2.5 iliyotengwa katika mwaka wa Fedha 2021/2022.

Amesema Mchakato wa Manunuzi katika bajeti hiyo umehusisha boti tatu za wazi na moia va kufungwa, ambapo Kampuni ya Amikan Ventures Limited ilishinda kandarasi ya kutengeneza boti tatu za wazi kwa thamani ya Tshs 1,589, 109,302.82 yaani kila boti thamani yake ni Tsh. 529,703, 100.94.

"Kamishna Mkuu, leo tutakuomba upokee na kuzindua boti 2 badala ya boti 3 kwani boti moja ilianguka wakati wa kushusha bandarini na kupata hitilafu kubwa. Mkandarasi ametakiwa kuleta boti nyingine mpya kwa gharama zake. Amepewa muda wa miezi 8 kuanzia mwezi wa Machi 2023 awe amekabidhi boti hiyo". Amesema Bw.Athumani.

Share:

PATA ODDS KUBWA UCL LEO



Jisajili Meridianbet leo upate mizunguko 50 ya bure kucheza moja ya mchezo uupendao ya kasino ya mtandaoni kuna Aviator, Poker, Titan Roulette na mingine mingi. Kujisajili bonyeza hapa https://a.meridianbet.co.tz/c/NpUbSL

 

 

Zilianza timu 32, zikafika 16, na hatimaye zimebaki 8 tu hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa, unatabiri timu zipi zitafuzu hatua ya Nusu fainali? Meridianbet inakuhakikishia unapata Odds kubwa na machaguo Zaidi ya 1000+ Tembelea www.meridianbet.co.tz kubashiri soka na kucheza kasino ya mtandaoni.

 

Odds kubwa za Jumanne ya Mabingwa

 

Ni vita vya mbinu kati ya Mwanamitindo na Bisho wa Kikatalunya Pep Guardiola akiliongoza jeshi lake la Man City, huku Luteni Jenerali Erling Haaland atasaidiana na Kapteni Kelvin De Bruyne kusaka ushindi dhidi ya Jeshi la Thomas Tuchel aliyekimbilia mafichoni Bayern Munich kwenye jiji la Munich nchini Ujerumani, huko kuna kijana mdogo tisho sana Kingsley Coman ni hatari wanapaswa kumchunga Zaidi. bashiri mubashara kupitia duka la ubashiri la Meridianbet.

 

Meridianbet wakali wa odds kubwa na kasino ya mtandaoni yenye michezo pendwa ya sloti kama Aviator, Poker na Roulette wameongeza machaguo Zaidi 1000+ kwenye mechi hizi za Ligi ya Mabingwa. Bonyeza hapa kuona machaguo Zaidi na mchanganuo wa odds kubwa bashiri mubashara.

 

Ni mechi ya kwanza ya robo fainali UCL Lisbon itachafuka kwa shangwe au giza litatanda kwa kipigo? ni Benfica vs Inter Milan miamba kutoka Jiji na Milan Italia. Odds za ushindi ni 2.25 vs 3.33 Meridianbet CHAGUA TUKUPE iwe odds kubwa watakupa, Kasino ya mtandaoni, kubashiri mubashara unaweza, michezo ya sloti kama Aviator, poker na Roulette yote unaipata kubwa Zaidi ukiona jamvi lako linataka kuchanika unaweza kucash out/Kuturbo.

 

Jumatano ya Mabingwa

 

Dimba la Giusepee Meazza litawaka moto ni vita ya wanaume 22, chini ya viongozi 2 ni Pioli Stefano na Spalletti Luciano. Ni AC Milan vs Napoli kila mmoja anataka kusonga mbele hatua ya nusu fainali utamu wa mechi hii imenogeshwa na odds kubwa za Meridianbet 2.74 vs 2.65 huku sare ina 3.14

 

Big Match Big day! katika dimba la Santiago Bernabeu ni Real Madrid vs Chelsea mara nyingi Chelsea huwa anafufukia kwenye timu kubwa lakini mabingwa hawa watetezi na mara nyingi Zaidi wa UCL linapokuja suala la Ligi ya Mabingwa huwa hawana jambo dogo, Mechi hii unaipa matokeo gani.  Kama sio mpenzi wa kubashiri soka, Chagua tukupe michezo ya kasino ya mtandaoni yenye sloti pendwa kama Aviator, Poker na Roulette. Bashiri na Meridianbet.

 

NB: Meridianbet imekuja na Jackpoti kubwa ya mechi 13 kwa dau dogo la kuanzia 1,000/=TZS mshindi atajinyakulia donge nono la Tsh 85,000,000/= PIGA *149*10#

 

#MERIDIANBET CHAGUA TUKUPE



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger