Friday, 31 March 2023

WOMEN FOR CHANGE WATOA MSAADA WA MASHINE ZA KUSAIDIA KUPUMUA WATOTO NJITI HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA SHINYANGA

Viongozi wa Kikundi cha Women For Change (kushoto) wakikabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) ambao mapafu hayajakomaa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mashine za kusaidia watoto kupumua zikiwa kwenye maboksi

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Kikundi cha Wanawake na Mabadiliko Manispaa ya Shinyanga (Women For Change - WFC), kinachojihusisha na Ununuzi wa Hisa ili kuinuana kiuchumi na chenye mfuko wa kusaidia jamii na watoto walioko kwenye mazingira magumu kimetoa msaada wa mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) ambao mapafu hayajakomaa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.


Women For Change wamekabidhi mashine ‘cPAP’ mbili zenye thamani ya shilingi Milioni 2.4 kwa Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. John Luzila leo Ijumaa Machi 31,2023.


Akizungumza wakati wa kukabidhi mashine hizo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga, Mwenyekiti Msaidizi wa Kikundi cha Women For Change, Lucy Mwita amesema mashine hizo zitasaidia kupumua kwa watoto waliozaliwa kabla ya muda ambao mapafu yao hayajakomaa.

Kikundi chetu cha Women For Change, kina wanachama20, tunajihusisha na Ununuzi wa Hisa ili kuinuana kiuchumi na tuna mfuko wa kusaidia jamii na watoto walioko kwenye mazingira magumu.

Tumekuwa tukisaidia katika sekta ya elimu kwa kuchangia madawati,kukarabati mabweni na shughuli mbalimbali, leo tumekuja kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali katika kuboresha sekta ya afya kwa kuchangia mashine hizi (cPAP) zenye thamani ya shilingi milioni 2.4 ili kuokoa maisha ya watoto wanaozaliwa kabla ya muda (njiti)”,amesema Lucy ambaye ni Mkurugenzi wa Shule za Little Treasures.


Kwa upande wake, Daktari Bingwa wa Watoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Tzeba amesema hospitali hiyo imekuwa ikipata watoto wengi wanaozaliwa kabla ya muda ‘Pre –mature’ hivyo mashine hizo zitasaidia sana kuokoa maisha ya watoto.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. John Luzila amekishukuru Kikundi cha wanawake ‘Women For Change’ kwa msaada huo kwani watoto wanaozaliwa kabla ya muda wanapata shida katika upumuaji hivyo wameokoa maisha ya watoto.






Mwenyekiti Msaidizi wa Kikundi cha Women For Change, Lucy Mwita akizungumza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga ambapo wamekabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti Msaidizi wa Kikundi cha Women For Change, Lucy Mwita akizungumza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga ambapo wamekabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mwanachama wa Kikundi cha Women For Change, MC Mama Sabuni akizungumza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga ambapo wamekabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa Kikundi cha Women For Change, Ansila Benedict maarufu Lulekia akizungumza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga ambapo wamekabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa Kikundi cha Women For Change,  Ansila Benedict akikabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga. Aliyevaa tai katikati ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. John Luzila.
Viongozi wa Kikundi cha Women For Change (kushoto) wakikabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga. Aliyevaa tai katikati ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. John Luzila.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. John Luzila akizungumza wakati Kikundi cha Women For Change kikikabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. John Luzila akizungumza wakati Kikundi cha Women For Change kikikabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Daktari Bingwa wa Watoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Tzeba akizungumza wakati Kikundi cha Women For Change kikikabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Wakikundi cha Women For Change wakipiga picha ya kumbukumbu katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga walipofika kukabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) 
Wakikundi cha Women For Change wakipiga picha ya kumbukumbu katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga walipofika kukabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) 
Wakikundi cha Women For Change wakipiga picha ya kumbukumbu katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga walipofika kukabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) 
Wakikundi cha Women For Change wakipiga picha ya kumbukumbu katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga walipofika kukabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) 
Wakikundi cha Women For Change wakicheza muziki katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga walipofika kukabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti) 
Wakikundi cha Women For Change wakicheza muziki katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga walipofika kukabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti)
Wakikundi cha Women For Change wakicheza muziki katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga walipofika kukabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti)
Wakikundi cha Women For Change wakicheza muziki katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga walipofika kukabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti)
Wakikundi cha Women For Change wakicheza muziki katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga walipofika kukabidhi mashine za kusaidia kupumua kwa watoto (njiti)
Watumishi katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Watumishi katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Watumishi katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Watumishi katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Watumishi katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Watumishi katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Watumishi katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Watumishi katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Watumishi katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
 Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yakiendelea katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga
Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yakiendelea katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga
Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yakiendelea katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:

WAZIRI NDALICHAKO AWAPA SOMO WAJASIRIAMALI MTWARA



***************

Na Mwandishi Wetu, Mtwara

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Prof.Joyce Ndalichako amewaasa wajasiriamali mkoani Mtwara kutumia Mwenge wa Uhuru kama chachu ya kukuza biashara na huduma.

Akifungua maonesho ya biashara, uwekezaji na fursa kwenye viwanja vya mashujaa park Mtwara Machi 30, 2023, Prof. Ndalichako, amesema kupitia Mwenge fursa mbalimbali ziibuliwe na kutengeneza ajira huku akiwapongeza walioona fursa na kuzitumia. Aidha, amelitaka Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) kuweka mkakati endelevu wa kuwasaidia wajasiriamali hao kupata masoko ya kudumu nchini na nje ya nchi.

“Wajasiriamali kumbukeni kuwa soko la Afrika Mashariki lipo wazi kwa nchi zote wanachama hivyo tuwe wabunifu ili kuweza kulitumia soko hilo na kuonesha ushindani wa bidhaa baina yetu na wenzetu,”amesema.
Share:

RC DODOMA APOKEA TUZO YA RAIS SAMIA NI KATIKA MASUALA YA MAENDELEO YA  ELIMU.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara,Hezbon Mwera ,akimkabidhi Tuzo ya Heshima Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe.Rosemary Senyamule iliyotolewa na Taasisi ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kutambua mchango wake Katika maendeleo ya sekta ya Elimu nchini wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya elimu Mkoani Dodoma.Kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw Ally Gugu.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara,Hezbon Mwera ,akimkabidhi Tuzo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe.Rosemary Senyamule kwa kumpongeza yeye pamoja na wasaidizi wake katika kuongeza ufaulu mkoani humo iliyotolewa na Taasisi ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya elimu Mkoani Dodoma.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara,Hezbon Mwera,akielezea tuzo zilizotolewa na taasisi hiyo kwa viongozi kwa kutambua mchango wa Elimu nchini wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya elimu Mkoani Dodoma.


MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Mh. Rosemary Senyamule,akiipongeza taasisi hiyo kwa kazi nzuri inazofanya katika sekta ya elimu kwenye mikoa mbalimbali nchini wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya elimu Mkoani Dodoma.


KATIBU Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw Ally Gugu,akizungumza wakati wa Mkutano wa wadau wa Sekta ya Elimu katika Mkoa wa Dodoma.




Mkurugenzi wa Taasisi ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara,Hezbon Mwera ,akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe.Rosemary Senyamule ,Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw Ally Gugu wakifatilia mada mbalimbali wakati wa Mkutano wa wadau wa sekta ya elimu Mkoani Dodoma.


SEHEMU ya washiriki wakifatilia mada mbalimbali wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya elimu Mkoani Dodoma.



Na.Alex Sonna-DODOMA

TAASISI ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara inayojishughulisha na masuala ya elimu imempa tuzo Rais Dr. Samia Suluhu Hassan kutokana na mchango wake katika maendeleo ya sekta ya elimu nchini.

Tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mh. Rosemary Senyamule na Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Hezbon Mwera Machi 30, 2023 katika mkutano wa wadau wa sekta ya elimu Mkoani Dodoma.

Akizungumza kwa niaba ya Prof. Mwera,Mkurugenzi wa Taasisi hiyo,Hezbon Mwera amesema kwa kutambua jitihada na mchango katika sekta ya elimu unaotolewa na Rais Samia wameamua kumpa tuzo hiyo ya heshima.

Amesema Taasisi hiyo inajishughulisha na mambo ya kijamii na wamepewa kibali na ofisi ya Tamisemi kufanya shughuli zao ndani ya Mikoa 10 ya Tanzania.

Amesema shughuli wanazozifanya ni pamoja na kuhamasisha vijana kujiunga na vyuo vya ufundi kwani kila mmoja anajua umuhimu wa vijana kupata mafunzo ya Elimu ya ufundi baada ya kumaliza darasa la saba na kidato cha nne wakati wakisubiri matokeo.

"Nipende kumpongeza Rais Samia kwa kuanzisha vyuo katika kila Wilaya.Taasisi yetu hii pia inashirikiana na Ofisi za Mikoa kutoa tuzo kwa wanafunzi wanaofanya vizuri katika mitihani ya kitaifa ya darasa la saba, kidato Cha nne na sita,"amesema

Mkurugenzi huyo wa Taasisi hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wakuu wa Vyuo vya Ufundi Kanda ya Ziwa, amesema wametoa tuzo katika Mikoa ya Mwanza,Kigoma,Simiyu,Shinyanga,Geita ,Mara.

Pia alimkabidhi tuzo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule kwa kumpongeza yeye pamoja na wasaidizi wake katika kuongeza ufaulu mkoani humo.

Tuzo za jumla zilizotolewa katika hafla hiyo zilidhaminiwa na taasisi ya ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara.

Kwa upande wake,Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mh. Rosemary Senyamule,ameipongeza taasisi hiyo kwa kazi nzuri inazofanya katika sekta ya elimu kwenye mikoa mbalimbali nchini.



RC Senyamule amesema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan amefanya jitihada kubwa kuhakikisha watoto wote wanaenda shuleni na matarajio ya Serikali ya awamu ya sita ni kuona elimu bora inatolewa pamoja na changamoto zote zinatatuliwa.

"Ili Mkoa uweze kusonga mbele kielimu ni lazima tuhakikishe watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanaandikishwa na wanahudhuria shule wakati wote,"amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Mkuu huyo wa Mkoa ameupongeza Mkoa huo kwa kushika nafasi ya 10 kitaifa kwa matokeo ya mwaka 2022.

"Niendelee kusisitiza yale tutakayokubaliana tukayatekeleze,niwaombe tuzidi kupambana kuhakikisha tunafanya vizuri,"amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Naye,Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw Ally Gugu,amesema wataliendeleza tukio hilo na litakuwa la kila mwaka.

Amesema ili ipatikane Dodoma yenye maendeleo lazima wawe wamoja katika kusimamia ubora wa elimu.

Amesema lengo la kikao hicho ni kuangalia namna bora ya kuongeza ubora wa elimu mkoani humo na kuongeza ufaulu wa Kitaifa.

Ameyataja malengo ya Mkoa ni kutoka katika asilimia 83.01 mwaka 2022 hadi 85 kwa mwaka 2023 katika mitihani ya kumaliza elimu ya msingi.

Amelitaja lengo la pili ni kutoka asilimia 91.27 mwaka 2022 Hadi 100 mwaka 2023 katika upimaji wa elimu kitaifa katika darasa la nne.
Share:

TCRA KUKAGUA VIFAA VYA MAWASILIANO NJE YA NCHI


Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) John Daffa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na vifaa vya mawasiliano kukaguliwa kabla ya kuingia nchini , Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya waagizaji wa vifaa vya Mawasiliano wakifatilia agizo kwenye mkutano , jijini Dar es Salaam.

******************

*Kazi ya Ukaguzi inafanywa na wakala waliongia mkataba

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuanzia Mei 23, mwaka huu vifaa vya mawasiliano ya kielektroniki vinavyoingizwa nchini vitatakiwa kukaguliwa kwenye nchi vinakoagizwa ili kuepusha kuingiza vifaa vilivyokwisha muda wa matumizi.

Aidha, imewataka watengenezaji na waingizaji wa vifaa hivyo, kulipa ada ya usimamizi wa taka za kielektroniki kwa kila kifaa kinachoingizwa kama gharama za usimamizi wa vifaa hivyo vinapofika mwisho wa matumizi.

Hatua hiyo ni katika kutekeleza maazimio ya mkutano wa tano wa Taasisi za Mawasiliano katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACO) kudhibiti ongezeko la taka za kielektroniki.

Akizungumza katika mkutano uliowakutanisha Wasambazaji wa vifaa vya kielektroniki Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, John Daffa alisema kuwa kanuni za ubora wa vifaa vya mawasiliano ya kielektroniki na usimamizi wa taka za kielektroniki za mwaka 2020 zinaelekeza kuhakikisha vifaa vyote vinavyoingia nchini havijafika mwisho wa matumizi.

Pia alisema kanuni hizo zinataka kuhakikisha kuwa vifaa vyote vilivyofika mwisho wa matumizi vinapelekwa kwa watoa huduma wenye leseni za kukusanya taka , kukarabati au kuendesha mitambo ya kuchakatwa vifaa vya mawasiliano pale vinapofika mwisho wa matumizi.

Daffa alisema TCRA ina jukumu la kusajili taarifa za vifaa vya mawasiliano ya kielektroniki ambavyo vimeingizwa au kutengenezwa nchini pamoja na kuweka makubaliano na watoa huduma waliopewa leseni kwa ajili ya kukusanya na kuendesha mitambo ya kuchakatwa taka za kielektroniki.

"Kuanzia Mei 23 mwaka huu maombi yote 6a kuingiza vifaa vya mawasiliano ya kielektroniki yatawasilishwa kwa njia ya mtandao kupitia https://ift.tt/ylc9EdX ili kuwezesha uwasilishaji wa taarifa zote za vifaa vinavyoingizwa," alisema Daffa.

Alieleza kuwa baada ya maombi yao kupokelewa, uchambuzi na tathmini kuhusiana na vifaa vitakavyoingizwa pamoja na ada ya usimamizi wa taka za kielektroniki itafanyika ili kuruhusu hatua za utekelezaji.

Alifafanua kuwa uingizaji wa vifaa vya mawasiliano nchini unahitaji leseni tofauti yaani Importation License na vifaa vyote vitakavyoingizwa nchini vinatakiwa kuhakikiwa ili kutathmini ulinganifu na mwingiliano wakati wa matumizi.

Hata hivyo, alisema kuwa mtumiaji wa vifaa vya mawasiliano ya kielektroniki hatahusika katika gharama hizo na kwamba hakutakuwa na ongezeko la gharama za ununuzi wa vifaa hivyo hapa nchini.

Pia alisema suala hilo ni jipya kuanza kutekelezwa nchini licha ya kuwepo kwa kampuni ambazo zilikuwa zinakusanya taka za kielektroniki bila kufuata utaratibu maalum.

Alisisitiza kuwa TCRA itashirikiana na Baraza la Hifadhi na Usimamizi wa mazingira (NEMC), katika usimamizi wa taka za kielektroniki.
Share:

TASAC MTWARA KUELEKEZA NGUVU ELIMU KWA JAMII



Na Mwandishi wetu, Mtwara 

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu)Joyce Ndalichako ametoa rai kwa wananchi wa Mtwara kuzichangamkia fursa za kibiashara zilizopo mkoani humo ili kukuza uchumi.

Ndalichako amesema hayo Mkoani Mtwara wakati akifungua maonesho ya biashara,Uwekezaji na fursa yanayofanyika katika viwanja vya mashujaa kuanzia Machi 19 hadi Machi 31,mwaka huu.

 Amesema kuwa Mkoa huo unakuwa kwa kasi kiuchumi hivyo ni vyema kila mwananchi akatambua kuwa hiyo ni fursa katika kukuza uchumi kibiashara.

"Maonesho haya ya Biashara, Uwekezaji na Fursa  ni maonesho ya Kwanza kufanyika Mkoani Mtwara yakiwa na lengo la kuwaleta pamoja wadau mbalimbali katika Sekta hiyo ili kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kujifunza biashara na uwekezaji wa kisasa pamoja na fursa zilizopo katika sekta hiyo na Mkoa wa Mtwara kwa ujumla,"amesema Ndalichako.

Aidha  Ndalichako alitumia fursa hiyo kuwakaribisha  wananchi katika uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru utakaowashwa   Aprili 1 mwaka huu katika kiwanja cha Nangwanda sijaona,Mkoani hapo.

Akizungumza  na Vyombo ya habari Kaimu Afisa Mfawidhi wa  TASAC Mkoa wa  Mtwara katika maonesho hayo Mha. Joseph Myaka amesema kuwa katika kutekeleza majukumu yao Shirika hilo limejikita katika kutoa elimu kwa wananchi kufahamu shirika hilo linavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria. 

Amesema kuwa licha ya majukumu makubwa waliyonayo pia TASAC imeshiriki maonesho hayo ili kuwapa elimu wananchi kuhusu  fursa za biashara zilizopo katika Sekta ya Usafiri kwa njia ya Maji  sambamba na elimu kuhusu Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa mazingira majini jukumu linalotekelezwa na Shirika hilo. 

“TASAC tunashiriki maonesho haya ya Biashara Uwekezaji na Fursa mkoani Mtwara ili kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yanayotekezwa Kisheria kama mdhibiti wa shughuli za usafiri kwa njia ya maji tunasimamia huduma zinazotolewa na Bandari, tunadhibiti na kusimamia ulinzi, usalama na utunzaji wa mazingira na kuratibu shughuli za uokoaji na utafutaji pale panapotokea dhoruba majini,

“Pia tunatoa elimu kwa wananchi wa Mtwara na wadau wa usafiri kwa njia ya maji katika jukumu letu la Udhibiti wa Safari kwa njia ya Maji na udhibiti Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa Mazingira majini, wanaweza kufanya shughuli zao kwa usalama na kupata maendeleo na kuongeza pato la Taifa,"ameeleza Myaka.

Aidha ameeleza kuwa kwa  mujibu wa Sheria, TASAC ina wajibu wa kusimamia kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhimiza usimizi na shughuli za uwakala wa meli wenye ufanisi, kuhimiza shughuli za bandari na huduma za meli zenye ufanisi, kuhakikisha kunakuwepo usalama na ulinzi wa shehena, kuhimiza na kutunza mazingira, usalama na ulinzi wa bahari, maziwa na mito.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger