Thursday, 13 October 2022

SUNGUSUNGU WASIMIKA VIONGOZI WAPYA, DC MBONEKO AWATAKA KUKOMESHA VIBAKA MITAANI



Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akizungumza kwenye kikao cha usimikaji viongozi wapya wa Jeshi la Jadi (Sungusungu) Tarafa ya Shinyanga mjini.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

JESHI la Jadi (Sungusungu) Tarafa ya Shinyanga mjini limewasimika viongozi wapya wa Jeshi hilo, huku Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akiwataka kukomesha vibaka mitaani.


Usimikaji wa viongozi hao wapya Sita wa Jeshi la Jadi (Sungusungu) Tarafa ya Shinyanga mjini umefanyika leo Oktoba 13, 2022 katika bwalo la Jeshi la Polisi Manispaa ya Shinyanga.

Mboneko akizungumza wakati wa kufungua kikao hicho, amelitaka Jeshi hilo la Jadi kuimarisha masuala ya ulinzi na usalama katika mitaa yote, ikiwamo na kudhibiti wimbi la vibaka Mitaani ambao wamekuwa wakipora vitu mbalimbali zikiwamo Simu na Pochi za akina mama.

“Naagiza Jeshi hili la Jadi Sungusungu liwepo kwenye kila Kata Manispaa ya Shinyanga, ili kuimarisha masuala ya ulinzi na usalama, sababu Polisi hawatoshi kufanya kazi peke yao, tunataka uhalifu uishe mitaani kusiwepo na vibaka wala watu kukatwa mapanga hovyo kama ilivyotokea huko Kolandoto,”amesema Mboneko.

Katika hatua nyingine, amelitaka Jeshi hilo la Jadi kusimamia kikamilifu miradi ya maendeleo ambayo inatekelezwa kwenye maeneo yao, ili kusiwepo wizi wa aina yoyote ile wa vifaa, pamoja na kuacha kuwapa adhabu viongozi wa Serikali bali wao wana mamlaka ambazo zinawashughulikia.

Pia amewataka Sungusungu kuzuia ndoa za utotoni kwa wanafunzi ambao wamehitimu elimu ya darasa la saba ili matokeo yakitoka wote wakutwe wapo na salama na kuendelea na masomo yao kidato cha kwanza.

Naye Afisa Taarafa wa Shinyanga Mjini Charles Maugila, amesema sasa hivi vibaka wamezidi mitaani, na kuliomba Jeshi hilo la Jadi Sungusungu liwashughulikie.

Kwa upande wake Mwenyekiti Mpya wa Jeshi la Jadi Sungusungu Tarafa ya Shinyanga Mjini Paulo Madale, ameahidi Jeshi hilo litafanya kazi zake kwa weledi kukomesha uhalifu mitaani, pamoja na fedha ambazo watakuwa wakitoza faini zitakuwa zikipelekwa kwenye miradi ya maendeleo.

Viongozi wapya wa Jeshi la Jadi Sungusungu Tarafa ya Shinyanga mjini ambao wamesimikwa ni Paul Madale ambaye ni Mwenyekiti, Makamu wake Juma Mipawa, Katibu Mkuu ni Ngaja Ngasa, Msaidizi wake Lucas Shija, Kamanda Mkuu ni Thomas Mwita, Msaidizi wake Rashidi Ngoeji.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akizungumza kwenye kikao cha usimikaji viongozi wapya wa Jeshi la Jadi (Sungusungu) Tarafa ya Shinyanga mjini.

Afisa Tarafa wa Shinyanga mjini Charles Maugila akizungumza kwenye kikao cha usimikaji viongozi wapya wa Jeshi la Jadi (Sungusungu) Tarafa ya Shinyanga mjini.

Makamu Mwenyekiti wa Jeshi la Jadi Sungusungu Manispaa ya Shinyanga Idd Pyalimu, akizungumza kwenye kikao cha usimikaji viongozi wapya wa Jeshi la Jadi (Sungusungu) Tarafa ya Shinyanga mjini.
 
 Kamanda Mkuu wa Jeshi la Jadi Sungusungu Manispaa ya Shinyanga John Kadama, akizungumza kwenye usimikaji huo wa viongozi wapya wa Sungusungu Tarafa ya Shinyanga mjini.

Mwenyekiti mpya wa Jeshi la Jadi (Sungusungu) Tarafa ya Shinyanga mjini Paul Madale akizungumza mara baada ya kumaliza kusimikwa.

Viongozi wapya wa Jeshi la Jadi (Sungusungu) Tarafa ya Shinyanga mjini wakisimikwa rasmi kulitumikia Jeshi hilo.

Viongozi wa Jeshi la Jadi (Sungusungu) kutoka Kata Mbalimbali Tarafa ya Shinyanga mjini wakiwa kwenye kikao cha usimikwaji viongozi wapya wa Jeshi hilo tarafa ya Shinyanga mjini.

Zoezi la usimikaji viongozi wapya wa Jeshi la Jadi Sungusungu Tarafa ya Shinyanga mjini likiendelea.

Zoezi la usimikaji viongozi wapya wa Jeshi la Jadi Sungusungu Tarafa ya Shinyanga mjini likiendelea.

Zoezi la usimikaji viongozi wapya wa Jeshi la Jadi Sungusungu Tarafa ya Shinyanga mjini likiendelea.

Zoezi la usimikaji viongozi wapya wa Jeshi la Jadi Sungusungu Tarafa ya Shinyanga mjini likiendelea.

Zoezi la usimikaji viongozi wapya wa Jeshi la Jadi Sungusungu Tarafa ya Shinyanga mjini likiendelea.
Zoezi la usimikaji viongozi wapya wa Jeshi la Jadi Sungusungu Tarafa ya Shinyanga mjini likiendelea.

Viongozi wapya wa Jeshi la Jadi Sungusungu Tarafa ya Shinyanga mjini wakisimikwa rasmi kulitumikia Jeshi hilo.
 
 
 
 
 


Share:

Tanzia : MBUNGE MUSSA HASSAN MUSSA AFARIKI DUNIA


Mbunge wa Jimbo la Aman (CCM), Mussa Hassan Mussa amefariki dunia leo Alhamisi Oktoba 13, 2022 nyumbani kwake visiwani Zanzibar.

Kupitia taarifa ya kifo hicho iliyotolewa leo Alhamisi Oktoba 13, 2022 na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa, Ofisi ya Spika wa Bunge imeeleza kuwa Spika Dk Tulia Ackson amesema kuwa ofisi ya bunge kwa kushirikiana na familia inaratibu mipango ya mazishi.


“ Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mhe. Mussa Hassan Mussa, natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa, waheshimiwa wabunge na wananchi wa Jimbo la Amani. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu”

Share:

KINANA ATAJA MAMBO MANNE YALIYOKUWA YAKISIMAMIWA NA MWALIMU NYERERE ILI KULETA MAENDELEO


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa ,Abdulrahman Kinana (wa tatu kulia) akiwa na viongozi Waandamizi wa Taaisis na Shule ya Mwalimu Nyerere pamoja na Wageni waalikwa wakifuatilia mijadala iliyokuwa ikitolewa ukumbini humo mara baada ya ufunguzi wa mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere,Oktoba 12,2022 Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani.PICHA ZOTE NA MICHUZI JR- KIBAHA PWANI.

Na Mwandishi Wetu,Kibaha

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Tanzania Bara Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana ametaja mambo manne ambayo Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alikuwa akiyasimamia enzi ya uhai wake kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania.


Kinana ameyataja mambo hayo leo Oktoba 12, 2022 wilayani Kibaha mkoani Pwani wakati wa mdahalo kuelekea kumbukizi ya miaka 23 ya hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.


Akifungua Mdahalo huo Uliofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere, Uliokutanisha vyama rafiki vya ukombozi Kusini mwa Afrika, Viongozi mbalimbali pamoja na Wanazuoni, Kinana amesema falsafa ya Mwalimu Nyerere ilijengwa na misingi imara kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania na Bara la Afrika kwa Ujumla.


" Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere alikuwa na maono ya kujua Uelekeo wa Taifa na Wapi Watanzania wanatakiwa kuelekea na hiyo ilitokana na Msimamo wake na kutotetereka," amesema Kinana.


Kuhusu suala la Uadilifu, Kinana amesema Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere alikuwa na misingi ya uadilifu na kwa kujali aliokuwa akiwaongoza ambapo alipenda Uongozi Shirikishi.


"Pia Mwalimu Nyerere alikuwa na Ushawishi mzuri kwenye Chama na Serikali na hiyo ilisababishwa na uwezo wake mkubwa wa Kujenga hoja kwa ajili ya maslahi ya aliokuwa akiwaongoza," amesisitiza Kinana.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Paul Kimiti ameomba watanzania kuyaendeleza yale yote mema yaliyofanywa na mwalimu ili kulijenga taifa katika misingi imara ya upendo mshikamano na umoja zaidi.


Wakati huo huo Mkuu wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Profesa Maselino Chijoliga amewakaribisha viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali kwenda kusoma kozi fupi za uongozi zilizopo katika chuo hicho ili ziwajengee uwezo wa kuongoza vyema kwa maadili ya uzalendo.


Katika hatua nyingine Taasisi ya Mwalimu Nyerere imemkabidhi Komredi Kinana Katiba na Hati ya Usajili wa Taasisi hiyo pamoja Vipeperushi vinayoelezea Historia ya Mwalimu Nyerere kwa Ujumla.


Oktoba 14 mwaka huu itakuwa ni kumbukizi ya miaka 23 ya hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere tangu alipoaga Dunia. Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa ,Abdulrahman Kinana akizungumza jana Oktoba 12,2022 wakati akifungua mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Paulo Kimiti akimkabidhi Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa ,Abdulrahman Kinana Katiba na Hati ya Usajili wa Taasisi hiyo pamoja na Vipeperushi vinayoelezea Historia ya Mwalimu Nyerere kwa Ujumla mara baada ya kufungua mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere,Oktoba 12,2022 Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani. 


Wageni waalikwa wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini hummo katika mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere,Okotoba 12,2022 Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani. PICHA ZOTE NA MICHUZI JR- KIBAHA PWANI. Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa ,Abdulrahman Kinana wa tatu kulia akiwa ameambatana na Viongozi Waandamizi wa Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere na Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere sambamba na Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Pwani (kulia) Mhe.Abbubakar Kunenge akielekea ukumbini kwa ajli ya kufungua mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere jana Oktoba 12,2022 Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani. Muonekano wa Jukwaa kuu Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa ,Abdulrahman Kinana akiwasili kwenye jukwaa kuu jana Oktoba 12,2022 kwa ajili ya kufungua mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani.PICHA ZOTE NA MICHUZI JR- KIBAHA PWANI. Baadhi ya Wakuu wa Wilaya mkoa wa Pwani wakishiriki ufunguzi wa Mdahalo huo






Mkuu wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Prof Marcelina Chijoriga akiwakaribisha viongozi wa Jukwaa na Kuu na Wageni waalikwa mbalimbali waliofika kuhudhuria ufunguzi wa mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani. Wachokoza Mada wa Mdahalo huo,pichani kulia ni aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CCM Ndg Wilson Mukama,Mkurugenzi Mkuu wa TBC Dkt Ayub Rioba,Mkuu wa Utawala wa CCM OND-Lumumba Christopher Ngubiagai pamoja na Aliyewahi kushika Nyadhifa mbalimbali za Uwaziri nchini Mhe.Fatma Said Ally Mchuno


Mdahalo ukiendelea ukumbini


Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Paulo akitoa utambulisho na neno la kumkaribisha rasmi Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa ,Komredi Abdulrahman Kinana kwa ajili ya ufunguzi wa mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere,Oktoba 12,2022 Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani. Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa ,Abdulrahman Kinana akizungumza jana Oktoba 12,2022 akisisitiza jambo wakati akifungua mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani.




Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi Wilson Mukama akieleza mada iliyohusu Mchango wa Mwalimu Nyerere katika Uongozi wa Chama wakati wa mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani.


Picha mbalimbali juu zikiomuonesha Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa ,Abdulrahman Kinana akisalimiana na Viongozi Waandamizi wa Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere na Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere mara baada ya kuwasili jana Oktoba 12,2022 kwa ajili ya


kufungua mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani.


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa ,Abdulrahman Kinana alipokelewa pia na Gwaride la heshima kuoka kwa Vijana wa CCM mara baada ya kupokewa na Viongozi Waandamizi wa Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere na Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere kwa ajli ya kufungua mdahalo wa kumbukizi ya miaka 23 ya Mwalimu Julius Nyerere,ulioandaliwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere kwa kushirikiana na shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani.PICHA ZOTE NA MICHUZI JR- KIBAHA PWANI.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger