• Home
  • About
  • Support
  • Contact
  • Advertise

MASWAYETU BLOG

  • Home
  • Business
    • Internet
    • Market
    • Stock
  • Downloads
    • Dvd
    • Games
    • Software
      • Office
  • Parent Category
    • Child Category 1
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • Featured
  • Health
    • Childcare
    • Doctors
  • Uncategorized
Menu
  • Home
  • Business
    • Internet
    • Market
    • Stock
  • Downloads
    • Dvd
    • Games
    • Software
      • Office
  • Parent Category
    • Child Category 1
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • Featured
  • Health
    • Childcare
    • Doctors
  • Uncategorized

Friday, 8 July 2022

MISA TANZANIA YAKUTANA NA WAHARIRI…JESSE KWAYU ATAKA KELELE MAREKEBISHO SHERIA KANDAMIZI

 Unknown     13:51:00     NEWS     No comments   

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Brain Incorperated Ltd, Jesse Kwayu akitoa mada kuhusu sheria mbalimbali za vyombo vya habari kwenye semina kwa Wahariri wa Habari iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Brain Incorperated Ltd, Jesse Kwayu amewataka waandishi wa habari nchini Tanzania kuungana na kuendelea kusukuma  mabadiliko ya vifungu mbalimbali vya sheria zinazosimami taaluma ya uandishi wa habari,ambavyo vinaminya utendaji na ukuaji wa vyombo vya habari.

Aidha, amewataka kuzisoma mara kwa mara sheria hizo,kutoa maoni yao kwenye mchakato wa mabadiliko uliopo sasa,kwani kwa kufanya hivyo ni kuonyesha kujali na kwa kiasi gani jambo linawagusa.


Kwayu ametoa rai hiyo leo Ijumaa Julai 8,2022 Jijini Dar es salaam wakati wa Semina kwa Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu sheria mbalimbali za habari za vyombo vya habari nchini Tanzania, yaliyoandaliwa na Taasisi ya vyombo vya Habari Kusini mwa Jangwa la Sahara (Media Institute of Southern Africa,Tawi la Tanzania (MISA Tanzania) kwa Kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari Wananchi nchini (TAMWA) kupitia Mradi wa International Media Support - IMS.


Semina hiyo ililenga kuwajengea uwezo Wahariri wa Habari kutambua na kuchambua sheria hizo pamoja na kutoa maoni yao.


Kwa mujibu wa Kwayu, baadhi ya vifungu vya Sheria ya Huduma za Habari , Sheria ya Takwimu na Sheria ya Udhibiti wa Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOCA), zinaminya uhuru wa kujieleza, upatikanaji wa taarifa na ukuaji wa vyombo vya habari nchini na kwamba zinahitaji kufanyiwa marekebisho ili kuwa rafiki kwa maendeleo ya nchi.


 "Ukishakuwa na sheria mbaya huwezi jua saa ngapi itakukamata. Tusilale tusome, tupige kelele kuhusu sheria zinazotukandamiza, hizi sheria bado hazijarekebishwa,tupo kwenye mchakato ambao ni lazima tushiriki kwa kuwa inakuhusu,"amesema.


"Sheria hizi zina mamlaka makubwa sana, mfano Sheria ya EPOCA ni kubwa, inatugusa katika maisha yetu ya kila siku, kelele za kufanyia marekebisho sheria hii ziendelee kila siku. Tuna wajibu wa kupaza sauti kujitetea wenyewe juu ya sheria hizo ili pale inapowezekana ziweze kufanyiwa marekebisho ili zisiwe mwiba kwa wanahabari na vyombo vya habari", ameongeza Kwayu.


Katika hatua nyingine Kwayu amewasisitiza waandishi wa habari kuwa mstari wa mbele kutetea haki zao na kutetea za wananchi katika jamii, kwa kuwa wengi wamezikosa kwa kutozitambua jambo ambalo siyo sahihi.


“Waandishi wa habari ni watetezi wa haki za binadamu. Jambo linaloumiza mtu wewe mwandishi wa habari lazima likukere . Kama mwandishi wa habari hukereketwi na jambo la jamii achana na kazi ya uandishi wa habari kafanye kazi nyingine,ni lazima mjisimamie na kuwa tayari kusaidia mtu au jamii inapoumizwa”,amesema Kwayu ambaye alikuwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Nipashe.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa TAMWA, Dkt. Rose Reuben  amewataka waandishi wa habari kuona umuhimu wa kuzingatia utekelezaji wa masuala ya jinsia kwa kuzingatia masuala ya usawa wa kijinsia wanapoandika habari zao.

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Brain Incorperated Ltd, Jesse Kwayu akitoa mada kuhusu Haki na Uhuru wa Kujieleza kwenye semina kwa Wahariri wa Habari iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA leo Ijumaa Julai 8,2022 jijini Dar es salaam. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Brain Incorperated Ltd, Jesse Kwayu akitoa mada kuhusu sheria mbalimbali za vyombo vya habari kwenye semina kwa Wahariri wa Habari iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA leo Ijumaa Julai 8,2022 jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Brain Incorperated Ltd, Jesse Kwayu akitoa mada kuhusu sheria mbalimbali za vyombo vya habari kwenye semina kwa Wahariri wa Habari iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA leo Ijumaa Julai 8,2022 jijini Dar es salaam.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA
Mkurugenzi wa TAMWA, Dkt. Rose Reuben akitoa mada kuhusu masuala ya kijinsia kwenye semina kwa Wahariri wa Habari iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA
Mkurugenzi wa TAMWA, Dkt. Rose Reuben akitoa mada kuhusu masuala ya kijinsia kwenye semina kwa Wahariri wa Habari iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA
Mshauir wa Vyombo vya Habari/ Mkufunzi, Rose Haji Mwalimu akizungumza kwenye semina kwa Wahariri wa Habari iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.
Wahariri wa Habari  wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa MISA Tanzania kwa kushirikiana na TAMWA.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:
Read More →

KUFUNGULIWA KWA DIRISHA LA UDAHILI KWA WAOMBAJI WA SHAHADA YA KWANZA KATIKA TAASISI ZA ELIMU YA JUU KWA MWAKA WA MASOMO 2022/2023

 Unknown     13:51:00     NEWS     No comments   



Share:
Read More →

DIWANI AFARIKI GHAFLA MSIKITINI

 Unknown     11:51:00     NEWS     No comments   


CHAMA cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Ilala kimepata pigo kufuatia Diwani wake wa Kata ya Mahohe Mohamed Ngonde, kufariki leo alfajiri.


Akizungumza kwa njia ya simu Katibu wa Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Busoro Pazi, alisema Marehemu Mohamed Ngonde alifariki akiwa katika Ibada ya alfajiri leo Julai 8, 2022 akiwa ibadani msikitini.


Katibu wa Madiwani Busoro Pazi amesema taratibu za mazishi bado kila wakati atakuwa anatoa taarifa baada kukaa na familia ya marehemu.


"Kwa Sasa tunafanya taratibu za kwenda kuifadhi mwili wa marehemu katika hospitali ya Rufaa Mkoa Amana "amesema Busoro.


Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Wilaya ya Ilala Said Sidde amesema taarifa za Kifo cha MH, Diwani wake Mohamed Ngonde alifariki na taarifa alitoa Mwenyekiti wa CCM kata Majohe ambapo amesema Marehemu Mohamed Ngonde alifariki ghafla.


Mwenezi CCM Wilaya ya Ilala Alhaj Said Sidde amesema kila wakati taarifa kamili zitatolewa kuhusiana na msiba huo mzito kwa Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na wana CCM kwa ujumla.


Alhaj Said Sidde,pia ongeza kuwa alimwelezea Mh Ngonde kuwa kada mahiri aliyekitumikia chama cha Mapinduzi kwa muda mrefu na kushikilia nyadhifa mbalimbali ikiwemo Mwenyekiti serikali ya mtaa Kichangani ,Majohe
Share:
Read More →

MWALIMU BENKI YAENDELEA KUTOA MIKOPO SABASABA

 Unknown     10:51:00     NEWS     No comments   
Mkuu wa Kitengo Cha Ukuzaji Biashara na Masoko wa Benki ya Mwalimu (MCB), Bi.Leticia Ndongole akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea jijini Dar es Salaam.  Baadhi ya wananchi wakipata huduma kwenye banda la Mwalimu Benki mara baada ya kutembelea banda hilo katika Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea jijini Dar es Salaam Watumishi wa Mwalimu Benki wakipata picha ya pamoja katika banda lao kwenye Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea jijini Dar es Salaam

****************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WANANCHI wameendelea kutembelea banda la Mwalimu Benki katika Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea jijini Dar es Salaam ambapo mpaka sasa wameshawahudumia watanzania 50 waliotembelea banda hilo.

Akizungumza katika maonesho hayo leo Julai 7,2022 Mkuu wa Kitengo Cha Ukuzaji Biashara na Masoko wa Benki ya Mwalimu (MCB), Bi.Leticia Ndongole amesema wanatarajia idadi ya wakopaji na wateja wapya itaongezeka kwa kuwa huduma zinatolewa kwa watu wote.

“Tunaposema huduma tunatoa kwa watu wote maana yake ni walimu, wafanyabiashara, wanafunzi wa vyuo, wakulima, wafugaji, wasafirishaji, vijana na wazee... hatuachi mtu. Tunafungua akaunti za aina mbalimbali kwa hapa tumefungua akaunti 35 hivyo tunawakaribisha wote kuja kupata huduma zetu bora kwenye sekta ya benki". Amesema Bi.Leticia.

Aidha Bi.Leticia amesema wanatoa huduma kwenye mikoa yote hapa nchini kwenye matawi na kidijitali kupitia mawakala wa Mwalimu Benki, Mwalimu Mobile na Mwalimu Visa Card pia wateja wao hupata huduma zote za bima na mikopo ya vifaa mbalimbali vya ujenzi.

Pamoja na hayo amewakaribisha wananchi kwa ujumla kutembelea banda lao kwaajili ya kupata huduma za kibenki hasa mikopo ambayo itawasaidia kujiinua kiuchumi binafsi na taifa kwa ujumla.
Share:
Read More →

MCHENGERWA ATEMA CHECHE KWENYE USIKU WA MASTAA WA SOKA

 Unknown     09:51:00     NEWS     No comments   

********

Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amevitaka vilabu vya michezo kufanya uwekezaji ikiwa ni pamoja na kujenga miundombinu ili kuinua michezo.

Mhe. Mchengerwa ametoa kauli leo Julai 7, 2022 kwenye usiku wa utoaji wa Tuzo za Mashindano ya NBC ya Shirikisho la soka nchini 2022.

Ameambatana na Katibu Mkuu, Dkt. Hassan Abbasi na Naibu Katibu Mkuu Saidi Yakubu na watendaji wa sekta ya michezo.

Katika tukio hili lililovuta hisia za wanamichezo ndani na nje ya nchi tuzo 43 katika maeneo mbalimbali zinatolewa huku tukio hilo likirushwa mubashara na kituo cha televisheni cha Azam na mitandao mbalimbali ya kijamii kutokea jijini Dar es Salaam.

Mhe amesisitiza kuwa wakati umefika wa Vilabu vya Tanzania kumiliki viwanja vyao kama vilabu vingine duniani ambapo ameliagiza Baraza la Michezo la Taifa(BMT) na Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) kuratibu kikao baina yake na viongozi wa vilabu mapema juma lijalo ili kujadili utekelezaji wa suala hilo.

"Ninaagiza BMT na TFF wiki ijayo ratibuni kikao na viongozi wa vilabu tulimalize suala hili." Amesisitiza Mhe Mchengerwa

Aidha, amewataka viongozi wa vilabu kuzingatia maadili na kuachana na vitendo vya ukiukaji wa maadali ambapo amefafanua kwamba vilabu haviwezi kupiga hatua katika michezo endapo havitazingatia suala hilo.

" Wenzetu wanafanikiwa sana kwenye michezo kwa kuwa wanazingatia maadili" ameongeza, Mhe. Mchengerwa

Amelitaka BMT kuchukua hatua kali kwa yoyote atakaye bainika kuvunja maadili.

Pia amesema Serikali inatarajia kujenga viwanja vya michezo ya ndani na sanaa eneo la Kawe ambapo amesisitiza baada ya kukamilika utoaji wa tuzo kwa mwaka ujao utafanyika katika kumbi hizo za kisasa.

Ameongeza kuwa dhamira ya Serikali kwa sasa ni kuifanya michezo kuwa uchumi.

Amesema kwa Serikali imeshatenga fedha kwa ajili ya kukarabati viwanja sita nchini ambapo amefafanua kuwa lengo ni kuandaa mashindano ya soka ya AFCON.

Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hassan kwa maono yake makubwa ya kuendeleza michezo nchini.
Share:
Read More →

Thursday, 7 July 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULAI 8,2022

 Unknown     23:51:00     NEWS     No comments   













Share:
Read More →

News Alert : TAZAMA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA KATI AWAMU YA PILI

 Unknown     09:51:00     NEWS     No comments   

 


KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Prof.Riziki Shemdoe anawatangazia wananchi wote kuwa orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano awamu ya pili kwa mwaka 2022 imetoka.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Bi.Nteghenjwa Hosseah ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI). Bonyeza mkoa wako hapo chini kulingana na hitaji lako;

OFISI YA RAIS - TAMISEMI

UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2022


BOFYA HAPA CHINI KUONA ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPANGWA KWENDA SHULE MOJA


CHAGUA MKOA ULIKOSOMA

ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA
GEITA IRINGA KAGERA
KATAVI KIGOMA KILIMANJARO
LINDI MANYARA MARA
MBEYA MOROGORO MTWARA
MWANZA NJOMBE PWANI
RUKWA RUVUMA SHINYANGA
SIMIYU SINGIDA SONGWE
TABORA TANGA
Share:
Read More →

Wednesday, 6 July 2022

IMANI POTOFU MAFUTA YA KENGE KUCHANGANYWA KWENYE PAMBA KUONGEZA UZITO

 Unknown     13:51:00     NEWS     No comments   

Wakulima wakiuza pamba yao kwenye kituo cha ununuzi Amcos
Pamba safi ikiwa kwenye kituo cha pamba ununuzi kwaajili ya kununuliwa
Mwandishi wa Makala haya Daniel Limbe akishuhudia ubora wa pamba inayo nunuliwa kwenye Amcos ya Chato
Mwonekano wa zao la pamba likiwa bado shambani

**

Na Daniel Limbe,Chato

KENGE ni mnyama anayefanana na mamba mdogo kwa umbile, na hupenda kuishi nchi kavu pamoja na kwenye madimbwi ya maji, huku mafuta yake yakitajwa kuwa matibabu ya masikio.

Nikutokana na wataalamu wa tiba asilia kuamini kuwa mafuta ya kenge yanatibu ugonjwa wa sikio linalouma au kutokwa usaha.

Mbali na kuwa ni tiba ya ugonjwa wa sikio,Baadhi ya wakulima wa zao la pamba wilayani ya Chato mkoa wa Geita, wanasema kuwa mafuta ya Kenge ni muhimu katika kuongeza uzito wa zao hilo na hivyo kuwaongezea kipato zaidi.

IMANI POTOFU

Inaelezwa kuwa kuchanganya mafuta ya Kenge kwenye zao la pamba ni imani potofu na ni kichocheo cha kuporomoka kwa bei na thamani yake ndani na nje ya nchi.

Uchunguzi umebaini uwepo wa mchezo mchafu unaofanywa na baadhi ya wakulima wa pamba kwa kuichanganya na mafuta ya Kenge wakiamini kuwa huongeza uzito wakati wa kuuza zao hilo.

Baadhi ya wakulima wanaamini kuwa wakitumia mafuta ya kenge (Uru)kunyunyizia pamba safi iliyokwisha vunwa shambani kabla ya kufikishwa kwenye masoko ili kuuzwa huongeza uzito kwenye zao hilo kwa lengo la kujipatia fedha nyingi.

Mwandishi wa makala haya amefanikiwa kuzungumza na familia ya Nyangeta Masatu, ambaye ni mkulima wa pamba kwa zaidi ya miaka 34 bila shaka anakiri kuwepo kwa tabia hiyo kwa baadhi ya wakulima wa pamba.

Anasema sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kuamini kuwa mafuta hayo huongeza uzito wa pamba, hivyo kumsaidia mkulima kupata kilo nyingi anapouza pamba yake.

Anataja namna ambavyo mafuta hayo hutumika na kusema kuwa hupakwa kwenye pindo za shuka (nguo) inayotumika kuuzia pamba kabla ya zao hilo kupandishwa kwenye mzani wa kupimia.

Masatu anasema kuwa njia nyingine ni kupaka mafuta ya kenge kwenye jiwe dogo ambalo huwekwa ndani ya kifungashio kilichobeba pamba hiyo.

Ernest Philipo, mkazi wa Nyarubungo anasema uharifu wa kutumia mafuta ya kenge aliushuhudia mwaka 1976 baada ya rafiki yake kutumia wakati wa msimu wa mauzo ya pamba.

Anasema pamoja na kuwa yeye hakuwahi kutumia mafuta hayo ila anatambua kuwa baadhi ya wakulima wa zao hilo hutumia mafuta hayo kujiongezea kipato hasa wakulima waliopo maeneo ya ukanda wa ziwa viktoria.

Zacharia Kapandekado, mkazi wa kijiji cha Katemwa Muganza, anakiri baadhi ya wakulima kutumia mafuta ya kenge pamoja na maji kuongeza uzito wa pamba.

Anasema vitendo hivyo hufanyika kwa kificho kwa kuwa wanatambua wazi kuwa kufanya hivyo ni kosa kisheria, huku akidai wanafanya uharifu huo hutokana na kuwa na pamba kidogo ikilinganishwa na wenye pamba nyingi.

 MWENYEKITI CCU AELEZA THAMANI YA PAMBA 

Mwenyekiti wa Chama kikuu cha ushirika Chato (CCU) Greon Chandika, anasema kuwa zao la pamba lina manufaa makubwa kwa jamii iwapo usimamizi wake utaimalishwa kuanzia ngazi ya familia, kitongoji, kijiji, kata, wilaya, mkoa na taifa kwa ujumla.

Anasema kuwa usimamizi huo unapaswa kuenenda sambamba na miongozo na maelekezo ya serikali katika kuhakikisha elimu zaidi inaongezwa kwa wakulima,kupitia taasisi zake pamoja na wadau wengine wa maendeleo.

Chandika anasema pamba ina faida rukuki iwapo itatunzwa na kuvunwa vizuri kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo hicho kwa kuwa inapovunwa na kuuzwa mkulima huanza kunufaika moja kwa moja kwa kujipatia fedha.

Mbali na mkulima, makampuni nayo huchakata na kutengeneza nyuzi (robota) ambazo huuzwa kwenye soko la dunia na nyingine hubaki nchini kama mali ghafi ya viwanda vya kutengeneza nguo.

Anadai kuwa mbegu ya pamba hukamuliwa mafuta ya kupikia ambayo hupendwa sana na wananchi wengi kutokana na ubora wake huku makapi ya mbegu hizo yakitengenezwa chakula cha mifugo (mashudu) pia hukamuliwa na kutengenezwa sabuni za kufulia na kuoshea vyombo.

Kadhalika magugu ya zao la pamba nayo yakitumika kama kuni za kupikia chakula hasa maeneo ya vijijini, hivyo kusababisha zao hilo kupata umaarufu na kupewa jina la dhahabu nyeupe.

 KAULI YA MKAGUZI UBORA WA PAMBA 

Ofisa Mkaguzi Ubora wa Pamba kutoka Bodi ya Pamba(TCB) wilayani Chato mkoani Geita,na Biharamulo mkoani Kagera, Samweli Mdidi, anathibitisha kuwepo kwa uharifu huo kutoka kwa baadhi ya wakulima wenye kuamini kufanikiwa kwa kutumia mafuta hayo.

Licha ya baadhi ya wakulima kuamini hivyo, anasema imani hiyo haina ukweli wowote zaidi ya kusababisha kuozesha pamba.

"Ni kweli kuna hayo malalamiko kutoka kwa baadhi ya wadau wetu wa pamba...tunaendelea kukagua na kutoa elimu kwa wakulima kuachana na imani hizo potofu kwa kuwa hakuna ukweli wowote wa kilo kuongezeka iwapo mkulima atatumia mafuta ya kenge badala yake ni kuozesha pamba"anasema Mdidi.

Anasema kuwa madhara mengine yanayoweza kutokea kutokana na uchafuzi huo ni kushuka kwa bei ya pamba kutokana na wanunuzi kupata hasara kwa kununua pamba isiyokuwa na ubora pamoja na kushuka thamani ya robota zetu kwenye soko la dunia.

 OFISA WANYAMA PORI 

Kwa upande wake, Daktari mwandamizi kitengo cha wanyama pori nchini, Dk.Emmanel Macha, anasema kitaalamu hakuna uhusiano wowote kati ya mafuta ya kenge na suala la kuongezeka uzito ndani ya pamba.

"Kwanza itambulike kuwa ili kupata mafuta hayo lazima kenge auawe...mbali na kuwa ni imani potofu zisizo kuwa na ukweli wowote lakini kuna wasiwasi kubwa ya kuwaangamiza wanyama hao wasio na madhara yoyote kwa jamii"anasema Dk. Macha.

"Suala hilo halihitaji hata elimu kubwa...kama wanapakashia mafuta hayo kwenye jiwe halafu uzito umaongezeka kwenye pamba basi watambue kinachokuwa kimeongeza ni jiwe  wala siyo mafuta hayo"anasema.

Aidha anawataka wakulima kuachana na imani hizo badala yake walime pamba kwa kuzingatia majira ya msimu wa kilimo, kuzingatia kanuni bora pamoja na kusikiliza na kuzingatia kwa kina ushauri unaotolewa na wataalamu wa kilimo hatua itakayo wasaidia kupata tija.

MKURUGENZI TCB

Kwa mujibu wa Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Pamba nchini, Marco Mtunga, anasema kuwa umaskini wa wakulima wa pamba hausababishwi na ukosefu wa nguvu kazi bali nikutokana na tija ndogo inayotokana na kutokuzingatia kanuni za kilimo bora.

"Wanatumia nguvu nyingi bila maarifa hivyo kuwafanya mara nyingi kulalamikia bei ndogo hali inayosababisha kuuza hata pamba chafu.

"Bila kutatua tatizo la tija ndogo, hata bei ikipanda maradufu, bado umaskini hautaondoka...uzalishaji wa kilo 300 kwa ekari ni mdogo sana"anasema Mtunga.

"Wakulima wengi wa pamba wamekuwa wakishindwa kuwapa ushirikiano wakaguzi wanapobaini kuwepo kwa pamba chafu katika vituo vya kuuzia pamba kwa kuhofia kutouza pamba yao...pasipo kujua kuwa pamba chafu ndiyo chanzo kikuu kinachofanya bei ya pamba kuporomoka kwenye soko la dunia"anasema.

Mtunga anawataka wakulima kutoa ushirikiano kwa wadau wa pamba na serikali ili kuwa na uzalishaji wa pamba wenye tija lakini pia wakulima wajiunge kwenye ushirika ili kuleta mabadiliko chanya badala ya kuendelea kuwa walalamikaji.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo kwenye tovuti ya TCB, Zao la Pamba hulimwa katika mikoa 17 ya Tanzania bara,na kwamba hutengenezwa nyuzi (robota) na kuuzwa kwenye soko la dunia, ambapo serikali hujipatia fedha za kigeni na kuchangia uchumi wa taifa.

Inaelezwa kuwa mkoa wa Singida, Simiyu, Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita, Tabora na Kigoma inazalisha aslimia 90 ya pamba mbegu yote inayolimwa nchini.

Huku aslimia 10 ya pamba mbegu ikilimwa na mikoa ya Kagera,Dodoma, Katavi, Iringa, Kilimanjaro, Morogoro, Tanga, Manyara na Pwani.

Miongoni mwa mikakati ya serikali ni kukuza uzalishaji wa pamba kutoka wastani wa tani 300,000 hadi kufikia tani 1,000,000 ifikapo mwaka 2025.

Hatua hiyo inakuja huku baadhi ya mataifa mengi duniani ikiwemo nchi ya Misri huzalisha kilo 2,000 kwa ekari tofauti na Tanzania ambapo inazalisha kilo 300.

Tovuti hiyo inaonyesha kuwa tangu  uzalishaji wa pamba uanze hapa nchini mwanzoni mwa karne ya 20, uzalishaji wa juu kabisa ulifikiwa msimu wa 2005/2006 ambapo jumla ya tani 376,000 sawa na robota 700,000 zilizalishwa.

 WAZIRI WA KILIMO 

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, anasema ili kuinua kilimo cha pamba nchini,serikali imeamua kuwaondolea wakulima makato ya fedha ya  dawa na mbegu walizokopeshwa wakati wa kilimo.

"Pesa hizo wakulima walitakiwa kurejesha wakati huu wa msimu wa 2022/23 wa ununuzi wa zao la pamba ambao umeshaanza nchi nzima"anasema Bashe.

Bashe anawataka wakulima wa pamba kutokubali kuibiwa na wanunuzi, na kwamba bei watakayoikuta kwenye vituo vya kununulia pamba haitakiwi mkulima kukatwa hata senti kwa madai serikali imetoa ruzuku kwa zao hilo.

Anasema Chato ni moja kati ya wilaya zilizokuwa zinalima pamba kwa wingi lakini zao hilo liliporomoka kutokana na sababu mbalimbali hali iliyosababisha kiwanda cha kuchakata pamba cha Chato Co-operative Union (CCU)kufa.

 PAMBA YOTE KUNUNULIWA 

Mwenyekiti wa Chama cha wakulima wa Pamba nchini (TCA) Boaz Ogolla, anasema kwa msimu wa 2022/23 TCA imejipanga kununua pamba yote itakayozalishwa na wakulima kwa njia ya ushindani kwa kuzingatia mwenendo wa soko la kimataifa la ununuzi wa pamba.

Inaelezwa kuwa mkakati wa serikali kufufua zao la pamba, kuanzia msimu wa mwaka jana 2021/22 na mwaka huu 2022/23 umewezesha serikali kuwapatia wakulima pembejeo ikiwemo mbegu na dawa bure ili kuongeza tija.

 NINI KIFANYIKE

Jamii iendelee kuelimishwa kuzingatia kanuni bora 11 za kilimo cha pamba kupitia maofisa ugani vijijini,ikiwa ni pamoja na kuwasaidia kupata pembejeo mapema kabla ya msimu wa kilimo kuanza.

Maofisa ugani kwa kushirikiana na ofisa maendeleo ya jamii vijijini wasaidie kuelimisha wakulima kujiepusha na imani potofu za kutumia mafuta ya kenge kuongeza uzito wa pamba.

Bodi ya pamba waendelee kukagua ubora wa pamba kabla na baada ya kununuliwa hatua itakayosaidia kusafirisha pamba nyuzi zenye ubora unaotakiwa kwenye soko la dunia.

Wananchi wahamasishwe kuendelea kulima pamba, kutokana na kuwa ni zao la biashara lenye manufaa rukuki kwa manufaa ya kaya na serikali.

Serikali iweke ruzuku kwenye zao la pamba hasa kipindi bei inapo shuka kwenye soko la dunia, hali itakayo wavutia wakulima wengi kuendelea na kilimo hicho.
Share:
Read More →
← Newer Posts Older Posts → Home
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

  • MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
    Kama kawaida yetu MASWAYETU BLOG katika nusanusa yetu tumefanikiwa kunasa hii ambayo ilikuwa ikisubiriwa na watu wengi,ni kuhusu ...
  • UPDATED:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA SELECTION YA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
    Habari yako, Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa m...
  • NECTA:HAYA HAPA MATOKEO DARASA LA SABA 2017
    NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2017 EXAMINATION RESULTS ANGALIA MATOKEO YAKO KWA KUBONYEZA MKOA WAKO HAPO CHINI, ...
  • MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI 10,027 WALIOKOSEA KUJAZA FORM ZA MIKOPO BODI YA MIKOPO 2016/2017
      KUONA MAJINA HAYO   << BONYEZA HAPA--PDF >>
  • BREAKING NEWS:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO MWAKA WA MASOMO 2016/2017
      Bodi ya mikopo ya elimu ya juu wametangaza majina ZAIDI YA 20000 ya wanafunzi waliopata mkopo 2016/2017. Kama utahitaji kuangaliziwa j...
  • MPYA:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA SECOND ROUND VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
    Habari yako, Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa ma...
  • MPYA:HAYA HAPA MAJINA (KATIKA PDF) WANAFUNZI SPECIAL DIPLOMA WALIOPANGIWA KURUDI UDOM &VYUO VINGINE 2016
    >>> CLICK HERE FOR LIST OF SELECTED STUDENT - UDOM (53.28 kB)<<<  CLICK HERE FOR LIST OF SELECTED STUDENTS - TEACHER ...
  • ANGALIA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWAPAMOJA NA APPLICATIONS FOR ADMISSION INTO NON DEGREE (DIPLOMA AND CERTIFICATE) PROGRAMMES FOR ACADEMIC YEAR 2016/2017-NACTE
                      Nacte wametoa majina ya wanafunzi waliofanikiwa kuchaguliwa  katika vyuo mbalimbali  afya,ualimu ,kil...
  • MPYA:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA SECOND ROUND VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
    Habari yako, Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa ma...

Unordered List

Pages

Blog Archive

  • ▼  2026 (70)
    • ▼  January (70)
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 30, 2026
      • SERIKALI YATOA MIKOPO KIASI CHA SHILINGI MILION...
      • KIJANA APITIA MATESO MAZITO LAKINI AKAJA KUWA MTU ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 28,2026
      • TWIGA, TANGA CEMENT WAPEWA SAA 48 KUJISALIMISHA
      • WAASISI CCM RUVUMA WATOA WITO WA KUZINGATIA KATIBA...
      • CCM MIAKA 49: WAZAZI WAONGOZA MAPAMBANO YA UTUNZAJ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 27,2026
      • WAKULIMA TABORA WALALAMIKIA UPUNGUFU WA TAARIFA ZA...
      • RAIS SAMIA AMEIMARISHA UCHUMI GEITA KUPITIA UJENZI...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 25,2026
      • MV NEW MWANZA: MKOMBOZI WA UCHUMI NA BIASHARA KAND...
      • BILIONI 67 ZIMETUMIKA KUJENGA BARABARA NA MASOKO M...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 24, 2026
      • TUTACHUKUA HATUA KALI KWA WATAKAOTUMIA TAARIFA BIN...
      • MASLAHI YA TAIFA KWANZA: MAPINDUZI YA KIFIKRA NA K...
      • ILALA TUNAJIVUNIA RAIS SAMIA, AMETULETEA MAENDELEO...
      • WANANCHI WA UKONGA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUDUM...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 22,2026
      • Tanzia : MUASISI NA MWENYEKITI WA KWANZA WA CHADEM...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 21, 2026
      • KANISA LA MLIMA WA MOTO LAZINDUA MAOMBEZI YA KUIOM...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 20,2026
      • HUWEZI KUISHIWA PAWA UKIPANDA MLIMA LOLMALASIN
      • SIMBA WA TERANGA WANG’ARA MOROCCO, WANYAKUA UBINGW...
      • WANA SANTA RC BUNJU WAPIGWA MSASA MATUMIZI SAHIHI ...
      • SAUTI ZA WANANCHI: AMANI NDIO MSINGI WA MAENDELEO ...
      • WAZIRI AWESO ATAKA KAZI ZIFANYIKE USIKU NA MCHANA ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 18,2026
      • MCHINJITA AONYA SIASA ZA MIHEMKO, APINGA MIITO YA ...
      • VIJANA 5,746 WACHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UA...
      • WATUMISHI WAPYA TASAC WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 17,2026
      • HAPA KUNA MKAKATI PEKEE UNAOWEZA KUIFANYA BIASHARA...
      • WANANCHI MSATA WAFAIDIKA NA ZOEZI LA MEDANI LA EX...
      • KWA NINI UNAPOTEZA KAZI KILA MARA? USILAUMU UZEMBE...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 15, 2026
      • INAMAANISHA NINI WAKATI HUWEZI KUSHIKILIA KAZI KWA...
      • YANGA BINGWA MAPINDUZI CUP
      • MTOTO WANGU ALICHELEWA KUTEMBEA NA KUONGEA HATUA M...
      • WANAOSEMA 'SAMIA MUST GO' AKITOKA UNAMUWEKA NANI P...
      • MWANAMKE HUYU ANASIMULIA JINSI MGANGA WA JADI ALIV...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 13,2026
      • Tanzania: IPTL's Patience Pays Off in $168m Disput...
      • BILIONI 6.7 KUBORESHA AFYA YA MAMA NA MTOTO KAHAMA
      • PROF. MKENDA AIPONGEZA LALJI FOUNDATION KUUNGA MKO...
      • MAKAMU WA PILI WA RAIS KUZINDUA MASHINDANO MAKUBWA...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 9,2026
      • SERIKALI IMEFANIKISHA AJIRA 1400 NJE YA NCHI: SANGU
      • KILA MTU NILIYEMWAMINI ALIISHIA KUNISALITI, HADI N...
      • HAPPY BIRTHDAY MALUNDE!
      • VETA MOSHI YATAJWA MFANO WA MAFANIKIO YA ELIMU YA ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 8, 2026
      • KILA MTU NILIYEMWAMINI ALIISHIA KUNISALITI, HADI N...
      • SERIKALI YASEMA BARRICK NI MFANO WA KUIGWA KWA KUW...
      • START NEW YEAR 2026 WITH GOOD NEWS DOING BUSINESS ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 7,2026
      • RAIS MSTAAFU WA DKT. KIKWETE, AZINDUA JENGO LA AFI...
      • RAIS MSTAAFU WA DKT. KIKWETE, AZINDUA JENGO LA AFI...
      • CHADEMA WAJIFUNZE KUTOKA KITABU CHA HESABU: KUKIRI...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 5,2026
      • SH MILIONI 500 ZA RAIS SAMIA KWA TAIFA STARS NI UW...
      • TAHADHARI: ‘UTANDAWAZI NI CHUI’, TUJILINDE NA UTEK...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 4,2025
      • SHAMRASHAMRA ZA MWAKA MPYA 2026: AMANI YA TANZANIA...
      • CHIKAMBO AKAGUA MIUNDOMBINU KOROFI MASONYA TARURA ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 3,2026
      • WANANCHI KIJIJI CHA LAJA WILAYANI KARATU WAISHUKUR...
      • WAKAZI WA JIJI LA DODOMA WAKISHEREHEKEA MWAKA MPYA...
      • DC NKINDA ACHUKUA HATUA ZA HARAKA KUTATUA KERO YA ...
  • ►  2025 (993)
    • ►  December (73)
    • ►  November (67)
    • ►  October (72)
    • ►  September (92)
    • ►  August (82)
    • ►  July (84)
    • ►  June (76)
    • ►  May (92)
    • ►  April (86)
    • ►  March (91)
    • ►  February (83)
    • ►  January (95)
  • ►  2024 (1017)
    • ►  December (89)
    • ►  November (89)
    • ►  October (73)
    • ►  September (94)
    • ►  August (86)
    • ►  July (85)
    • ►  June (86)
    • ►  May (94)
    • ►  April (92)
    • ►  March (101)
    • ►  February (30)
    • ►  January (98)
  • ►  2023 (1772)
    • ►  December (99)
    • ►  November (101)
    • ►  October (130)
    • ►  September (102)
    • ►  August (150)
    • ►  July (162)
    • ►  June (165)
    • ►  May (178)
    • ►  April (172)
    • ►  March (188)
    • ►  February (162)
    • ►  January (163)
  • ►  2022 (1846)
    • ►  December (173)
    • ►  November (161)
    • ►  October (190)
    • ►  September (188)
    • ►  August (185)
    • ►  July (146)
    • ►  June (116)
    • ►  May (130)
    • ►  April (126)
    • ►  March (120)
    • ►  February (136)
    • ►  January (175)
  • ►  2021 (7035)
    • ►  December (284)
    • ►  November (598)
    • ►  October (641)
    • ►  September (638)
    • ►  August (619)
    • ►  July (616)
    • ►  June (617)
    • ►  May (637)
    • ►  April (581)
    • ►  March (621)
    • ►  February (539)
    • ►  January (644)
  • ►  2020 (7392)
    • ►  December (597)
    • ►  November (589)
    • ►  October (586)
    • ►  September (618)
    • ►  August (680)
    • ►  July (625)
    • ►  June (614)
    • ►  May (591)
    • ►  April (606)
    • ►  March (632)
    • ►  February (624)
    • ►  January (630)
  • ►  2019 (7895)
    • ►  December (611)
    • ►  November (643)
    • ►  October (673)
    • ►  September (664)
    • ►  August (679)
    • ►  July (677)
    • ►  June (619)
    • ►  May (725)
    • ►  April (622)
    • ►  March (477)
    • ►  February (604)
    • ►  January (901)
  • ►  2018 (409)
    • ►  December (388)
    • ►  August (1)
    • ►  July (1)
    • ►  June (2)
    • ►  May (2)
    • ►  April (7)
    • ►  March (2)
    • ►  February (1)
    • ►  January (5)
  • ►  2017 (450)
    • ►  December (1)
    • ►  November (1)
    • ►  October (119)
    • ►  September (7)
    • ►  August (2)
    • ►  July (10)
    • ►  June (23)
    • ►  May (28)
    • ►  April (39)
    • ►  March (16)
    • ►  February (77)
    • ►  January (127)
  • ►  2016 (2803)
    • ►  December (246)
    • ►  November (198)
    • ►  October (274)
    • ►  September (286)
    • ►  August (251)
    • ►  July (233)
    • ►  June (260)
    • ►  May (309)
    • ►  April (210)
    • ►  March (233)
    • ►  February (264)
    • ►  January (39)
  • ►  2015 (1416)
    • ►  December (24)
    • ►  November (102)
    • ►  October (186)
    • ►  September (89)
    • ►  August (80)
    • ►  July (229)
    • ►  June (197)
    • ►  May (61)
    • ►  April (266)
    • ►  March (105)
    • ►  February (50)
    • ►  January (27)
  • ►  2014 (1347)
    • ►  December (21)
    • ►  November (33)
    • ►  October (51)
    • ►  September (43)
    • ►  August (40)
    • ►  July (202)
    • ►  June (287)
    • ►  May (328)
    • ►  April (159)
    • ►  March (61)
    • ►  February (118)
    • ►  January (4)

Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger