Thursday, 22 July 2021

CHUO CHA CCOHAS KINATANGAZA NAFASI ZA MASOMO DIPLOMA YA UFAMASIA NA UTABIBU


Share:

Mpyaa : PAKUA APP YA MALUNDE 1 BLOGTUWE TUNAKUTUMIA HABARI BURE MOJA KWA MOJA KWENYE SIMU YAKO

Share:

YANGA WATUA KIGOMA KUKIPIGA NA SIMBA SC JUMAPILI


Wachezaji wa Yanga wakishuka kwenye Ndege baada ya kufika mkoani Kigoma

Kikosi cha Yanga SC kimefika salama mkoani Kigoma tayari kwa maandalizi ya mchezo wa fainali ya kombe la Azam Sports Federation Cup dhidi ya watani zao Simba SC mchezo utakaochezwa siku ya Jumapili Julai 25, 2021 katika dimba la Lake Tanganyika.

Timu hiyo ya wananchi iliondoka leo Asubuhi jijini Dar es salaam kwa usafiri wa ndege, na wamewatangulia watani zao Simba ambao bado wapo Dar es salaam. Huu utakuwa ni mchezo wa nne timu hizi zinakutana msimu huu kwenye mashindano yote, kwenye michezo miwili ya Ligi Kuu Tanzania bara msimu huu Yanga wameshinda mchezo mmoja na wametoka sare mchezo mmoja lakini pia Yanga waliifunga Simba kwenye fainali ya Mapinduzi Cup kule visiwani Zanzibar kwa mikwaju ya penati 4-3.

Na kueleka mchezo huu wa fainali tayari shirikisho la soka nchini TFF limetangaza waamuzi watakao chezesha mchezo huu, ambapo mwamuzi wa kati ni Ahmed Arajiga kutoka Manyara, mwambuzi msaidizi namba moja yani Line 1 ni Ferdnand Chacha kutoka Mwanza, msainizi namba mbili Line 2 ni Mohamed Mkono wa Tanga na mwamuzi wa akiba yani fourth official ni Elly Sassi wa Dar es salaam.

Chanzo -
Share:

POLISI WENYE MABOMU NA MBWA WAZUIA KONGAMANO LA CHADEMA


Mbwa na Polisi waliozuia kongamano la CHADEMA Mwanza

Kongamano la Chama cha Siasa cha CHADEMA la kudai Katiba mpya lililokuwa lifanyike leo Jijini Mwanza, limeshindwa kufanyika baada ya polisi waliobeba mabomu ya machozi, silaha za moto pamoja na magari yenye mbwa kutanda katika eneo la hoteli mahali ambapo kongamano hilo lingefanyika.

Hapo jana Julai 20, 2021, Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel, alipiga marufuku mikusanyiko isiyo ya lazima katika mkoa huo kwa ajili ya kuzuia maambukizi ya ugonjwa hatari wa Corona.

Via EATV

Share:

Accountant at Health for a Prosperous Nation

Accountant     About Us Health for a Prosperous Nation (H-PON) is a Local Nongovernmental organization with a vision of a healthy Tanzanian population. The H-PON works to contribute towards the Government efforts via its development agenda of having a healthy Tanzanian population which engages effectively in development efforts and hence reduce poverty and generating a […]

This post Accountant at Health for a Prosperous Nation has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Driver at SEGA Secondary School

Driver  Secondary Education for Girls Advancement (SEGA) is a non-profit organization with offices at Mkundi area, Morogoro Municipal, mandated to operate in Tanzania mainland with registration No OONG/ R2/0000232. With a particular focus on vulnerable girls, its mission is to educates and equips bright Tanzanian girls with academic, leadership, and business skills to unleash their […]

This post Driver at SEGA Secondary School has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Fundraising Officer at SEGA Secondary School

  Fundraising Officer   Secondary Education for Girls Advancement (SEGA) is a non-profit organization with offices at Mkundi area, Morogoro Municipal, mandated to operate in Tanzania mainland with registration No OONG/ R2/0000232. With a particular focus on vulnerable girls, its mission is to educates and equips bright Tanzanian girls with academic, leadership, and business skills to […]

This post Fundraising Officer at SEGA Secondary School has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JULAI 22,2021

































Share:

Wednesday, 21 July 2021

WAPENZI WAFARIKI WAKIPUNGUZA BARIDI CHUMBANI



Watu wawili wamefariki dunia baada ya kuingia na jiko la mkaa katika chumba cha kulala kwa ajili ya kupunguza baridi mkoani Njombe.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Hamisi Issah amewataja waliofariki dunia kuwa ni Benitho Mbatha (23) mpiga debe wa mjini Njombe na Jazila Said (27) mkazi wa Namtumbo mkoani Ruvuma.

“Baada ya kufariki hakuna mtu ambaye aligundua kama kuna watu wamefariki, tukio hili limetokea Julai 17,2021 majira ya saa tano nusu usiku huko mtaa wa National Housing kata ya Njombe mjini wakiwa wamelala kwenye chumba kimoja,”amesema Kamanda Issah.

Amesema sababu ya kifo chao inaonyesha wakati wakiwa hai waliweka moto wa mkaa kwa ajili ya kujihifadhi na baridi ambapo mtindo huo umekuwa ukitumika na watu wengi mkoani Njombe.

Mmiliki wa nyumba aliyokuwa akiishi marehemu Benitho Mbatha, Amani Samsoni amesema yeye alikuwa wa kwanza kushuhudia tukio hilo baada ya kwenda kumtembelea marehemu na kuwaona wote wawili wakiwa wamefariki

“Lakini bado mimi nilifuatilia kwa majirani wanasema yule mwanamke alikuwa anaelekea Madaba,alikosa nauli na huyu kijana kwa kuwa yupo pale kwenye magari akamwambia njoo upumzike kwanza na kesho nitakusaidia nauli ya kukufikisha kwenu kwa hiyo hiki kitu kinahuzunisha sana”,amesema Samson.

Nao majirani akiwemo Winfrida Msalilwa wamesema “Marehemu huwa anapenda sana kuja hapa na alikuja pia akachukua moto na akachukua chipsi mayai akasema nina mgeni wangu huko ndani lakini siku baada ya siku tukashangaa haonekani mpaka tulipoona wanakuja polisi".
Share:

JITIBU TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA FULL POWER.. UUME MDOGO ZAT 50 NDIYO SULUHISHO



Zati 50


Full Power



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume:

⇒Ngiri,


⇒Henia


⇒Kisukari


⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri


⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu


⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi


⇒Msongo wa mawazo 

⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.

ZAT 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa
⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

Naibu Waziri Mabula Aitaka Manispaa Mpanda Kuandaa Mpango Kazi Kutekeleza Mpango Kabambe


Na Munir Shemweta, KATAVI
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya makazi Dkt Angeline Mabula ametoa wito kwa halmashauri ya na Wadau wa maendeleo katika halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kuandaa mkakati na mpango kazi wa utekelezaji mpango kabambe.

Dkt Mabula alitoa wito huo tarehe 20 Julai 2021 wakati wa uzinduzi wa Mpango Kabambe wa Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi uliofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri mkoani humo.

Aidha, aliitaka halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kutafuta wabia na wawekezaji kwa ajili ya kuwekeza kwenye sekta mbalimbali zilizoainishwa kwenye Mpango Kabambe.

‘’Nitoe wito kwa taasisi zinazotoa huduma mbalimbali katika Manispaa ya Mpanda kuutumia Mpango Kabambe ulioandaliwa katika utekelezaji shughuli zao na miradi ya maendeleo’’ alisema Dkt Mabula

Aliitaka halmashauri ya Manispaa ya Mpanda katika mkoa wa Katavi kuendelea kuratibu utekelezaji Mpango Kabambe aliouzindua kwa kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ya Manispaa.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, Kifungu cha 4 (3) cha sheria ya mipango miji ya mwaka 2007 kinazitaka Mamlaka za upangaji yaani Mamlaka za miji midogo, Manispaa na Majiji kuandaa ripoti za utekelezaji wa Mipango Kabambe na kuiwasilisha kwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Makazi kila mwaka na kubainisha kuwa ripoti hiyo haiwezi kutayarishwa bila ya kuwa na mipango na mikakati mahsusi ya utekelezaji.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Michael Nzyungu kwa upande wake alisema, mkakati wa utekelezaji mpango kabambe wa Manispaa ya Mpanda 2018-2038 unatekelezwa kwa awamu tatu na kuainisha vyanzo vya mapato kwa ajili ya utekelezaji wake ni kutoka mapato ya ndani ya halmashauri.

Nzyungu alitaja vyanzo vingine kuwa ni kutoka serikali kuu, ubia na sekta binafsi, mifuko ya barabara pamoja na wafadhili mbalimbali. Wakati huo huo, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amezindua na kuukabidhi ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi. Ukumbi huo umejengwa na shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa gharama ya shilingi milioni 367.


Share:

Waziri Simbachawene Kuanza Ziara Mkoa Wa Kilimanjaro, Arusha Kesho, Kukagua Miradi, Utendaji Kazi Wa Taasisi Zake


 Na Felix Mwagara, MOHA-Dodoma.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi Mkoani Iringa, anatarajia kuanza ziara ya siku tano katika Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro ya kukagua miradi mbalimbali pamoja na utendaji kazi wa Taasisi zake katika Mikoa hiyo.

Waziri huyo anatarajia kuanza ziara hiyo Julai 22 hadi 27, 2021 ambapo ataambatana na Wakuu wa Taasisi wa Wizara yake katika Mikoa hiyo katika siku zote atakazofanya ziara.

Akizungumza na Mwandishi wa Habari hii, Waziri Simbachawene amesema, amemaliza salama ziara yake katika Mkoa wa Iringa, ambapo amezipongeza Taasisi zake ambazo ni Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji, Uhamiaji na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Mkoani humo kwa kuwa na umoja pamoja na kufanyakazi kwa weledi.  

“Lengo kuu la ziara yangu ni kuona utendaji kazi wa hizi Taasisi zangu na pia kufanya ukaguzi wa miradi mbalimbali katika Mikoa hiyo pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili na kuzitatua, na pia kuwasisitiza utendaji kazi wa haki kwa kuwajali na kuwasikiliza wananchi wanapopatwa na matatizo mbalimbali wakihitaji huduma kutoka kwenye Taasisi hizo,” alisema Simbachawene.

Aliongeza kuwa, anatarajia kuwasili Mkoani Kilimanjaro Julai 22, 2021 na katika Mkoa huo baada ya kufanya Kikao na Mkuu wa Mkoa huo, atakagua shughuli za kiutendaji katika Chuo cha Polisi Moshi (CCP), Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda Moshi (TRITA) na baadaye atazungumza na Wakuu wa Taasisi zote zilizopo ndani ya Wizara yake katika Mkoa huo.

Katika ziara ya Mkoa wa Arusha, Waziri huyo amefafanua kuwa, Julai 24, 2021 ataanza ziara Mkoani humo kwa kutembelea Makao Makuu ya Taasisi zake na kuangalia utendaji kazi wao pamoja na kukagua miradi iliyopo katika Mkoa huo.

“Ziara yangu ya Iringa, na pia hii ya Kilimanjaro na Arusha inanisaidia kujua mengi kuhusu hizi Taasisi zangu na pia kujua mafanikio yao pamoja na changamoto walizonazo, ambapo ndani ya Mkoa wa Arusha pia nitafika Mpaka wa Namanga kwa ajili ya kukagua Mpaka huo pamoja na shughuli za kiutendaji za Uhamiaji Mpakani hapo,” alisema Simbachawene.  

Waziri Simbachawene anatarajia kumaliza ziara yake Julai 27, 2021 na atarejea ofisini kwake jijini Dodoma kuendelea na shughuli za kiofisi.




Share:

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH ....Anatafsri Nyota, Pete za Bahati



Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH  ALHAJI SHARIFF SIMBA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo fanya mawasiliano kupitia wasaa Husika.
.
JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasiliana nae sasa atatue tatizo lako.
 ALHAJI SHARIFF SIMBA Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu . Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, .MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI
.
Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi,Kwa mawasiliano piga simu namba 
+255 689 060 821
+255 712 35 77 75
.
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE


Share:

Waziri Mkuu Atahadharisha kuhusu corona


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa rai kwa viongozi wa dini na waumini waendelee kuvumiliana, kustahamiliana na kushikamana katika kufanya ibada na kuienzi tunu ya amani.

“Tuendelee kufanya ibada, kuwaombea wenzetu waliotangulia mbele za haki, tuoneshane upendo na mshikamano hata baada ya kumalizika kwa masiku haya kumi bora ya Dhul Hijja.”

Waziri Mkuu ametoa rai hiyo leo (Jumatano, Julai 21, 2021) katika Baraza la Eid El Adha lililofanyika katika Msikiti wa Mtoro, Ilala jijini Dar es Salaam.

Amesema kila Mtanzania anapaswa kutambua kwamba anao mchango mkubwa katika kutunza na kuimarisha amani ya nchi, hivyo amewasihi wananchi wote waendelee kuitunza tunu hiyo.

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwakumbusha na kuwasisitiza wananchi wote waendelee kuchukua hatua za kujikinga na ugonjwa wa UVICO-19.

“Tuendeleze tabia ya kunawa mikono mara kwa mara na maji safi yanayotiririka na sabuni na tukikosa maji tutumie vitakasa mikono. Tuvae barakoa zilizothibitishwa na mamlaka zetu.”

Waziri Mkuu amesema ni vema kwa sasa wananchi wakajiepusha na mikusanyiko isiyokuwa ya lazima na wazingatie kukaa umbali wa mita moja au zaidi kutoka mtu mmoja hadi mwingine.

Amesema wananchi wanatakiwa wafanye mazoezi ya mara kwa mara kulingana na afya zao pamoja na mazingira yanayowazunguka, pia amewasihi wazingatie lishe bora.

“Kwa wale wenye umri mkubwa na wenye uzito uliopitiliza na wenye magonjwa sugu kama moyo, pumu, kisukari na figo wanapaswa kuchukua hatua madhubuti zaidi kujikinga na ugonjwa huu.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu amewasisitiza wananchi wawahi katika vituo vya kutolea huduma za afya mara waonapo dalili za mafua makali, maumivu ya koo, kichwa kuuma, kupumua kwa shida, kukosa hamu ya kula na kupoteza uwezo wa kunusa harufu mbalimbali.”

Akizungumzia kuhusu chanjo ya Ugonjwa huo, Waziri Mkuu amesema chanjo hiyo ipo tayari nchini mwananchi yoyote anayetaka kuchanjwa akachanje kwa ajili ya kupata kinga dhidi ya ugonjwa huo.

Kwa upande wake, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Aboubakar Zubeir Bin Ally amewataka watanzania kuendelea kuimarisha maadili mema yatakayoisaidia nchi yetu “Pia tumuombe Mwenyezi Mungu ili tuondokane na majanga yanayoikabili nchi yetu na ulimwengu mzima”  

Naye, Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA), Sheikh Nuhu Jabir Mruma amesema baraza hilo linatoa wito kwa waislamu na Watanzania kwa ujumla waendelee kuienzi na kuilinda amani wanaposherehekea sikukuu ya Eid Al-Adh’haa.

“Tunafanya hivi kwa kutambua kwamba amani ndio msingi wa maisha bora na yenye furaha kwa mwanadamu. Mwenyezi Mungu anatuelekeza juu ya faida ya amani katika kitabu chake kitukufu cha Qur’an sura ya 16 aya ya 112 na nanukuu “Na Mwenyezi Mungu amepiga mfano wa mji uliokuwa na amani na utulivu, riziki yake ikiufikia kwa nafasi kutoka kila mahali.”

Akizungumzia wimbi la tatu la ugonjwa wa UVIKO-19, Sheikh Mruma ametumia fursa hiyo kuipongeza Serikali hususan Wizara ya Afya kwa namna inavyochukua hatua za kukabiliana na kudhibiti janga hilo.

Amesema hatua hizo zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali zimepunguza kwa kiasi kikubwa kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa huo nchini.”Tunawashukuru Watanzania kwa namna wanavyopokea, kutii na kuyafanyia kazi maelekezo ya viongozi katika kujikinga na kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo.

Pia kiongozi huyo amesema baraza hilo linaendelea kuwahimiza Waislamu na wananchi kwa ujumla waendelee kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kukuza uchumi. “Tunaamini kwa kufanya hivyo ndiyo tutakuwa tumeunga mkono kwa dhati juhudi za Serikali yetu katika kufikia malengo yake ambayo ni huduma bora kwa jamii yote.”

 (Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

BARRICK YAPELEKA KICHEKO,TABASAMU KWA WAJASIRIAMALI KUTOKA VIJIJI 14 KUZUNGUKA MGODI WA BULYANHULU


Mmoja wa wajasiriamali wanaowezesha na Barrick,Mamuu Makere akionesha ufugaji bora wa kuku katika maonyesho ya biashara mkoani Shinyanga
Baadhi ya wajasiriamali wanaowezeshwa na Barrick wakionyesha bidhaa zao katika Maonesho ya 45 ya kimataifa ya biashara jijini Dar es Salaam
Baadhi ya wajasiriamali wanaowezeshwa na Barrick wakionyesha bidhaa zao katika Maonesho ya 45 ya kimataifa ya biashara jijini Dar es Salaam
Baadhi ya wajasiriamali wanaowezeshwa na Barrick wakionyesha bidhaa zao katika maonyesho ya biashara Shinyanga yaliyofanyika karibuni
**

Ukosefu wa ajira kwa miaka mingi imekuwa moja ya changamoto kubwa katika maeneo mbalimbali nchini mijini na vijijini.Tatizo hili linaathiri maisha ya wananchi na uchumi wa nchi kwa ujumla.

Hata hivyo, Serikali inajitahidi kutatua tatizo hilo katika maeneo mbalimbali, kwa kushirikiana na wahisani na wadau mbalimbali mfano kampuni ya madini ya Barrick.

Wakazi wa maeneo ya vijiji mbalimbali kuzunguka mgodi wa Bulyanhulu wanasifia juhudi hizo. Kwa mfano, Clementina Felix, ni mama wa watoto wawili, mkazi wa Kijiji cha Bugarama mkoani Shinyanga anasema kwa miaka mingi yeye na wanawake wenzake wamekuwa na changamoto ya kujikwamua kiuchumi na kuishi maisha duni na tegemezi.

Lakini, anasema hivi sasa yeye na wenzake wameanza kuondokana na changamoto ya maisha duni baada ya kujiingiza katika shughuli za ujasiriamali, kilimo cha kisasa na ufugaji. Anaeleza kuwa kampuni ya madini ya Barrick, inawawezesha kufanikisha ndoto zao za kujikwamua kimaisha kwa kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali na kufadhili shughuli zao mbalimbali.

“Tulikuwa tunateseka kwa kutojua nini cha kufanya ili kujikwamua kiuchumi kwa kuendesha shughuli za kilimo na ufugaji bila ujuzi na kuishia kutopata mafanikio. Tunaishukuru Barrick kwa kuja na programu inayolenga kutuwezesha kiuchumi wakazi zaidi ya 200 wa vijiji vinavyozunguka mgodi wake”, anasema Clementina huku akitabasamu.

Berita Nyawanga, yeye ni mkazi wa kata ya Mwinguru , ambako pia Barrick inaendesha programu za kuwakwamua na sasa wananchi wanafaidi. Berita anaomba kampuni kuendelea kuwezesha wajasiriamali katika maeneo yake yote ya migodi nchini hususani Wanawake na vijana ambao wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ajira.

Meneja Mahusiano ya jamii wa Barrick katika mgodi wa Bulyanhulu ,Anthony Sebastian, anafafanua uwezeshaji wajasiriamali katika maeneo yanayozunguka mgodi ni utekelezaji wa Sera ya Barrick chini ya Mpango wa Kusaidia Jamii (CSR) kuzunguka maeneo yake ya kazi. Anasisitiza kuwa wamepania kuboresha maisha ya wananchi kwa kuwapatia elimu ya ujasiriamali, kilimo cha kisasa na ufugaji.

“Kampuni inatambua kuwa ujasiriamali, ufugaji na kilimo ni maeneo ambayo yanaweza kutoa ajira kwa wananchi wengi sambamba na kuwawezesha kujikwamua kuchumi na ndo maana imeanzisha programu ya kuwezesha waanchi kutoka kata mbalimbali zinazozunguka mgodi”, alisema.

Antony anasema ili kuhakikisha shughuli zao zinakuwa endelevu kampuni Imekuwa inafadhili mafunzo ya ujasiriamali kila wiki ambapo wanavijiji hukusanyika pamoja na kupatiwa mafunzo mbalimbali ya kuendesha shughuli zao kwa ufasaha ambayo yanayolewa na wataalamu mbalimbali.Kwa wale wafugaji pia hupatiwa pia mbolea na mbegu bora.

Aliongeza kusema kuwa mbali na kuwapatia mafunzo pia kampuni Imekuwa ikiwafadhili wajasiriamali hao kuhudhuria maonyesho mbalimbali kama Sabasaba na mengineyo ili kuonyesha bidhaa zao ,kutafuta masoko zaidi na kujifunza mbinu za biashara kutoka kwa wafanyabiashara wenzao, pia alisema kuwa wajasiriamali hao wamekuwa wakiuza bidhaa zao kwa wafanyakazi wa mgodini.

Kampuni ya Barrick pia inazo progamu madhubuti za kusaidia shughuli za elimu, afya na mazingira kwa jamii kwa lengo la kuinua maisha ya wananchi.

Antony, ametaja baadhi ya miradi ya kijamii iliyotekelezwa na kampuni ya Barrick Bulyanhulu kuwa ni ujenzi wa vyumba madarasa katika sekondari ya Bulyanhulu, ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Kakola,Ujenzi wa bweni la wasichana sekondari ya Bugarama, kuwezesha kituo cha Afya cha Bugarama kununua mashine ya X-ray na kutengeneza chumba cha kuhifadhi maiti.Katika kufanikisha miradi hiyo alisema kampuni imechangia zaidi ya shilingi bilioni 1.

Alishukuru kwa ushirikiano ambao kampuni Imekuwa akipiga kutoka kwa watendaji wa Serikali wa ngazi mbalimbali na kuahidi kuwa itaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kupunguza changamoto za kijamii ili kuwezesha maisha ya wananchi kuwa bora.
Share:

Matapeli 5 Wa Ardhi Bagamoyo watiwa Mbaroni

Na. Hassan Mabuye, Pwani
WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi aamuru kutiwa mbaroni matapeli watano maarufu wa kuuza na kunyanganya ardhi za watu Wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani.

Waziri Lukuvi alitoa maagizo hayo jana wakati akiwa katika mkutano wa kusikiliza kero za migogoro ya ardhi ya wakazi wa mkoa wa Pwani na kuzitolea ufumbuzi eneo la Mapinga Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani.

Katika mkutano huo ambao wakazi wa eneo hilo walijitokeza na kutoa ushuhuda wa kutapeliwa maeneo yao kwa muda mrefu Waziri Lukuvi aliagiza kukamatwa kwa watu watano waliothibitika kutapeli viwanja na mashamba ya watu wengi akiwemo Katibu Muenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Mapinga Wilaya ya Bagamoyo kufanyiwa mahojiano kwa tuhuma za kuhusika na utapeli wa kuuza maeneo na kusababisha migogoro katika kata hiyo.

Watuhumiwa hao ni Omari Shabani ambaye ni Katibu Muenezi wa kata ya Mapinga, Ramadhani Rashidi aliyekuwa katibu wa kitongoji cha Kiembeni, Marwa Muhoni, William Urio na Mwanahamis Habibu.

Mhe. Lukuvi alitoa amri kwa Kamanda wa Polisi wa wilaya ya Bagamoyo ya kuwaweka chini ya ulinzi watuhumiwa hao watano baada ya kutajwa na wananchi walioshiriki kwenye mkutano huo wakidaiwa kuhusika kuuza viwanja na mashamba kiholela na kusababisha migogoro ya ardhi ya kila mara.

“matapeli wengi wa ardhi hapa mkoa wa Pwani hasa Bagamoyo ni viongozi, viongozi wa mitaa na kata wanafanya utapeli, viongozi hata wa chama nimekuta kule viongozi wa mashina wanasaini nyaraka za mauziano ya ardhi. Kiongozi wa shina wa chama anahusikaje kuweka saini hati ya mauzino ya ardhi” alihoji Waziri Lukuvi.

Lukuvi alimuagiza mkuu wa Polisi wilaya ya Bagamoyo kufanya mahojiano ya kina na watuhumiwa hao na wakibainika hatua za kisheria zichukuliwe kukomesha migogoro ya ardhi.

Pamoja na wananchi kuwataja watuhumiwa hao pia Diwani wa kata ya Mapinga Chandika Dismas pamoja na baadhi ya viongozi walikiri kiongozi huyo wa Chama kuwa na jopo lake ambalo linashiriki kuuza maeneo na kuchochea migogoro katika eneo hilo.

Lukuvi ameitaja wilaya ya Bagamoyo hasa eneo la Mapinga kuongoza kwa migogoro ya ardhi ambayo imechangiwa na viongozi wa ngazi za chini wakiwemo viongozi wa mashina ya chama.

Lukuvi alisema migogoro hiyo imekua kero na kuwafanya wananchi kukosa amani na kushindwa kufanya shughuli za maendeleo.

“tayari ninayo majina ya watu 54 wanaodaiwa kuwa vinara wa kuuza ardhi katika Wilaya ya Bagamoyo wakiwemo Viongozi wa mitaa” Alisema Mhe. Likuvi.

Alionya baadhi ya viongozi wa chama cha Mapinduzi ( CCM) wanaojihusisha kuuza ardhi kwa kutumia mihuri ya Chama kuacha mara moja na hatua zitachukuliwa kwa atakayehusika.

Katika hatua nyingine, Waziri Lukuvi aliwataka wakazi wa Bagamoyo kuacha kuvamia maeneo ya Serikali ambayo hayajaendelezwa likiwemo la Lazaba linalomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Alisema Viongozi wa Serikali wanatakiwa kulinda maeneo hayo pamoja na Lazaba yanayomilikiwa na Serikali kwani ipo mpango ya uwekezaji hivyo yeyote atakayevamia asitarajie kulipwa fidia.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge aliahidi kufanyia kazi malekezo ya Waziri kukomesha uvamizi wa Mkoa huo.

Kunenge alisema migogoro mingi katika Wilaya hiyo inadaiwa kuchangiwa na watendaji na Viongozi wa kisiasa.

Kaimu Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bagamoyo Abubakari Mlawa alikiri kupata taarifa za tuhuma za Viongozi hao na kusema "Kama chama tuhuma zilitufikia na taratibu za kufuatilia tuhuma hizo zinaendelea"

Alisema wanatarajia kukaa vikao na kujadili tuhuma za Viongozi hao na kwamba atakayebainika atavuliwa nafasi ya uongozi kwani Kata hiyo imekua kinara wa migogoro ya ardhi.

Mlawa ameongeza kuwa hatua hizo si kwa Viongozi wa chama tu hata Viongozi wa Serikali waliopata dhamana za uongozi wao kupitia chama Cha Mapinduzi ambao wametuhumiwa nao watachukuliwa hatua kali.


Share:

Health Programming and Training Specialist at Peace Corps

Health Programming and Training Specialist     About the United States Peace Corps: The Peace Corps is an independent United States federal agency that has been working in Tanzania since 1961. Peace Corps Volunteers work with governments, schools, and communities in the areas of education, health, HIV/AIDS, information technology, agriculture, and the environment. About the Programming […]

This post Health Programming and Training Specialist at Peace Corps has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger