Saturday, 17 July 2021

Mfumo Wa Kielektroniki Kutumika Kujaza Fomu Za Uhiari Wa Kupata Huduma Za Chanjo Dhidi Ya Corona.


 Na WAMJW – DOM.
Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi amesema kuwa Serikali imejiapanga kuwa na mifumo miwili ya kujaza fomu ya uhiari wa kupata huduma ya Chanjo ya Corona ikiwemo kupitia njia ya Kielektroniki na njia ya karatasi.

 Dkt. Subi amesema hilo wakati akiongea katika Taarifa ya Habari iliyorushwa na TBC (ARIDHIO) ikiwa ni mwendelezo wa kutoa elimu kwa wananchi juu ya mlipuko wa tatu wa ugonjwa wa Corona na umuhimu wa Chanjo ili kupambana dhidi ya ugonjwa huo.

 “Utaratibu ambao Serikali imeweza kuuweka ni kwamba, tutakuwa na mifumo ya aina mbili moja itakuwa ni mifumo ya kielektroniki ambapo mtu anaweza akatoa uhiari wake kwa kujaza mwenyewe kwamba anahitaji kwenda katika kituo Fulani kupata chanjo za ugonjwa wa COVID-19” Dkt. Subi.

 Aliendelea kusema kuwa, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  imekuwa ikiendelea kutoa Elimu kwa Wananchi juu ya huduma mbali mbali za tiba ana kinga, hivyo kusisitiza kuwa baada ya utoaji wa Elimu, mwananchi anakuwa na uhiari wa kupata huduma au kutopata.

 “Sisi kama Wizara ya afya tumekuwa tukiwapatia Wananchi elimu ya kutosha juu ya huduma fulani, sasa ukishampatia elimu ya kutosha , mwananchi anakuwa na uhiari wa kupata huduma au kutoipata, sawa sawa na mgonjwa anapoenda kufanyiwa huduma za upasuaji, tumekuwa tukimpatia huduma ya fomu ya uhiari” Dkt. Subi

 Aidha, Dkt. Subi amesema kuwa, hiari inaweza kuwa kwa njia ya mdomo au kwa njia ya maandishi, hivyo  katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona Serikali ikaona ni vizuri kwa Watanzania kuendelea kutoa hiari yao katika kupata huduma hizi za Chanjo ya Corona.

 Mbali na hayo Dkt. Subi aliwatoa hofu wananchi kwa kusema kuwa, Chanjo za ugonjwa wa Corona ni bora, salama, zina ufanisi wa kutosha na zimeorodheshwa na Shirika la Afya Duniani kwaajili ya matumizi ya dharura ili kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Corona.

 “Chanjo hizi ni salama na zina ufanisi wa kutosha lakini pia ni bora, tunaposema Chanjo hizi zimeweza kuorodheshwa na Shirika la Afya Duniani kwaajili ya matumizi ya dharura hususan katika kipindi hiki ambacho Dunia imekubwa na wimbi kubwa la ugonjwa wa COVID – 19” alisema Dkt. Subi

 Alisisitiza kuwa, Serikali imedhamiria kwa dhati kuutokomeza ugonjwa wa Corona, na ndio maana inatumia afua zote za kupambana dhidi ya maambukizi ikiwemo uvaaji sahihi wa Barakoa, kunawa mikono kwa sabuni na maji safi tiririka, kuepuka misongamano isiyo ya lazima, kutumia vipukusi, kufanya mazoezi na matumizi ya Chanjo ya ugonjwa wa Corona.

 Hata hivyo, Dkt. Subi amewatoa hofu Watanzania na kuwataka waendelee kuiamini Serikali na kufuata maelekezo yote kutoka kwa Wataalamu wa Afya katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu wa Corona, huku akisisitiza kuwa Sayansi haiwezi kupindishwa na maneno ya mitandao ya kijamii.


Share:

Naibu Waziri Mabula Aagiza Mashauri Ya Ardhi Kuisha Ndani Ya Miaka Miwili


Na Munir Shemweta, MBARALI

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maenseleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewaagiza Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya kuhakikisha mashauri yanasikilizwa na kuisha katika kipindi kisichozidi miaka miwili tangu shauri kufunguliwa.

Dkt Mabula alitoa agizo hilo  tarehe 16 Julai 2021 wilayani Mbarali mkoani Mbeya wakati akizindua Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya ya Mbarali mkoani humo.

Naibu Waziri wa Ardhi aliwaagiza pia wenyeviti na watumishi katika Mabaraza ya Ardhi kuhakikisha wanatumia uzoefu wao kuelimisha wananchi kuhusu taratibu muhimu zinazopaswa kuzingatiwa katika uendeshaji wa mashauri yatokanayo na migogoro ya ardhi kuwarahisishia wanaofuatilia haki zao.

“Ninawaagiza Wenyeviti na watumishi katika mabaraza kuhakikisha mnatumia uzoefu wenu kuwaelimisha wananchi taratibu muhimu katika uendeshaji mashauri kuwarahisishia wanapofuatilia mashauri yao” alisema Dkt Mabula.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, Serikali kwa kuzingatia umuhimu wa vyombo vya kushughulikia migogoro itokanayo na matumizi ya ardhi inalo jukumu la kuvipatia vitendea kazi vyombo hivyo ili viweze kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

Alisema, wizara yake itaendelea kuyapatia vitendea kazi Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya wilaya ili kuhakikisha Mabaraza hayo yanatoa huduma ya kutatua migogoro ya ardhi kwa urahisi.

Alitoa rai kwa halmashauri zote nchini kuhuisha Mabaraza ya Kata na Vijiji kwa yale yaliyomaliza muda wake na kutoa elimu kwa wajumbe wake ili kufahamu majukumu yao.

“Halmashauri nyingi hazitengi bajeti kwa ajili ya kuwawezesha wajumbe kupata vitendea kazi kama vile shajala na usafiri jambo linalofanya mabaraza ya kata na vijiji kujiamulia kuweka tozo kwa wananchi bila kuzingatia malengo ya uanzishwaji wa Mabaraza” alisema Dkt Mabula

Aliwataka wajumbe walioteuliwa kufanya kazi kwenye Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya kufanya kazi kwa weledi na kuepuka vishawishi vya rushwa ili kujenga imani kwa wananchi.

Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya wilaya Stela Tulo aliupongeza uongozi wa wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya kwa juhudi zake zilizowezesha uanzishwaji baraza hilo.

Aliwataka wananchi wa Mbarali kulitumia vizuri baraza hilo la Ardhi na kuongeza kuwa, Wizara ya Ardhi imejipanga kuhakikisha inaanzisha mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya wilaya katika wilaya nyingine ili kuweza kutatua migogoro ya ardhi iliyoshindikana kwa njia ya mazungumzo.

Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya ya Mbarali linafanya mkoa wa Mbeya kuwa na jumla ya Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya matatu. Mabaraza mengine ni yale ya wilaya za Tukuyu pamoja na Kyela.

Aidha, Naibu Waziri Mabula mbali na uzinduzi wa Baraza la Ardhi aligawa hati za ardhi 144 kwa wamiliki wa ardhi katika wilaya ya Mbarali waliorasimishiwa makazi yao na kuwaeleza kuwa hati walizokabidhiwa zitawahakikishia usalama wa miliki zao pamoja na kuzitumia katika shughuli za maendeleo.



Share:

Nchi Za Rwanda na Tanzania Kuendelea Kujengeana Uwezo Sekta Ya Tehama


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk. Faustine Ndugulile amesema nchi za Tanzania na Rwanda zitaendelea kushirikiana na kujengeana uwezo kwenye sekta ya Tehama ili kuhakikisha zinawasaidia wananchi wa pande zote kunufaika kupitia eneo hilo.

Waziri Dk. Ndugulile ameyasema hayo, alipozungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam akiwa na Waziri wa Tehama na Ubunifu wa nchi ya Rwamda, Bi. Paula Ingabire ambaye amefanya ziara ya siku mbili nchini Tanzania.

Dk. Ndugulile amesema ziara ya Bi. Ingabire inajumuisha kufanya majadiliano na kubadilishana uzoefu katika sekta ya mawasiliano kwa pande zote mbili. Aliongeza kuwa Tanzania na Rwanda ni nchi ambazo zimekuwa na ushirikiano kwa muda mrefu kupitia Shirika la Mawasiliano la Tanzania na lile la Rwanda na mahusiano ya kibiashara.

“TTCL ni moja ya wadau anayepeleka mawasiliano katika nchi ya Rwanda na amekuwa akitoa mawasiliano hayo kwa zaidi ya miaka 10 sasa, hivyo nimemkaribisha Waziri kwanza aje kuona sehemu ambayo mawasiliano yake ya nchi ya Rwanda yanapita na pili kuja kubadilishana uzoefu kwa pande zote mbili.

“..Nchini kwetu hii ni Wizara Mpya (Tehama) na kwa Rwanda kuna hatua ambazo wamepiga katika maendeleo ya Tehama, lakini pia kuja kuangalia fursa zinazopatikana Tanzania na sisi kuangalia fursa hizo kwa nchi ya Rwanda,” alisema Waziri Dk. Ndugulile.

Alisema katika ziara hiyo Waziri wa Rwanda na Tanzania watafanya majadiliano kuangalia maeneo ambayo wanaweza kubadilishana uzoefu kwa lengo la kuboresha zaidi mahusiano ya pande zote. Sisi kama Wizara ya Teknolojia na Mawasiliano tumefarijika sana kwa ujio wa Mh. Waziri wa Tehama na Ubunifu wa nchi ya Rwamda, Bi. Ingabire ili sasa kuangalia yale ambayo tumekuwa tukiwasiliana kwa maandishi tuweze kuonana ana kwa ana na hata kujionea uwezo tulionao.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba akizungumza katika ziara hiyo, alisema ziara ya kiongozi huyo licha ya kudumisha mahusiano baina ya nchi hizo inaendelea pia kukuza mahusiano ya kibiashara kwani TTCL inatoa huduma za internet nchini Rwanda.

Alisema katika ukanda wa Afrika Mashariki nchi ya Rwanda ni miongoni mwa mataifa yaliopiga hatua kubwa kwenye teknolojia (ICT), hivyo ujio wa ziara hiyo ni fursa tosha kwa Tanzania. Alisema katika majadiliano wamekubaliana kuendelea kufanya biashara na nchi hiyo pamoja na maboresho zaidi ya kiushirikiano.

Aidha alibainisha kuwa wamekubaliana kuendelea kubadilishana teknolojia, mafunzo ya kujengeana uwezo, na TTCL inahakikisha inatumia fursa hiyo vizuri ili kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha mawasiliano katika ukanda wa Afrika Mashariki na Ukanda wa nchi za SADC kutimiza malengo ya Serikali.

Naye Waziri wa Tehama na Ubunifu wa nchi ya Rwamda, Bi. Paula Ingabire akizungumza alisema Rwanda na Tanzania zimekuwa na mahusiano ya kubadilishana teknolojia za kidijitali kwa muda mrefu takribani zaidi ya miaka 10 hivyo ziara hiyo imekuja kuangalia namna ya kuboresha zaidi mahusiano hayo.

Alisema Rwanda licha ya kuwa na mahusiano kibiashara kupitia TTCL imekuwa na utaratibu wa mashirikiano kati ya taasisi za serikali zinazosimamia mawasiliano yaani TCRA kwa Tanzania na RURA kwa Rwanda hivyo ziara yake itaboresha zaidi mahusiano na ushirikiano huo.

Waziri Bi. Paula Ingabire katika ziara hiyo aliongozana na viongozi wakuu wa taasisi zinazo ratibu na kusimamia mawasiliano nchini Rwanda na kutembelea na kufanya majadiliano ya kimkakati na taasisi za TTCL, Kituo cha taifa cha kuhifadhi Data (Data Center) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).


Share:

Chief Finance and Administration Officer at Swiss Tropical and Public Health Institute (SWISS-TPH)

Overview The Swiss Tropical and Public Health Institute (Swiss TPH) is a world-leading institute in global health with a particular focus on low- and middle-income countries. Associated with the University of Basel, Swiss TPH combines research, services, and education and training at the local, national and international level. About 850 people from more than 80 […]

This post Chief Finance and Administration Officer at Swiss Tropical and Public Health Institute (SWISS-TPH) has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Consultant at Tanzania Interfaith Partnership

Consultant  Final Evaluation Consultant (Open to local applicants) The Tanzania Interfaith Partnership (TIP) has been working in Tanzania since 2010 on issues of health and Children’s Rights. TIP is currently implementing a Faith and Community Initiative (FCI) Project on HIV/AIDS and Justice for Children in Mwanza region. The project is funded by PEPFAR/CDC through Ariel […]

This post Consultant at Tanzania Interfaith Partnership has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

AMUUA MPENZI WAKE KWA KUMFUNGIA NDANI KISHA KUCHOMA MOTO NYUMBA DAR


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ACP Muliro Jumanne,

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, linamshikilia Grace Mushi (25) kwa tuhuma za kumuua aliyekuwa mpenzi wake Khamis Abdallah (25), mkazi wa Mbezi Makabe baada ya kumfungia ndani ya nyumba na kuimwagia mafuta ya petroli na kisha kuichoma moto nyumba hiyo.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo Muliro Jumanne, na kusema kuwa tukio hilo limetokea Julai 16, 2021, majira ya saa 8:30 usiku na uchunguzi umebaini kwamba wapenzi hao walikuwa na mgogoro mkubwa wa mapenzi.

"Baada ya tukio hilo mtuhumiwa alijaribu kutoroka lakini kwa kushirikiana na wananchi alikamatwa na uchunguzi wa awali umeonesha kwamba ulikuwepo mgogoro mkubwa wa kimpenzi kabla ya kufanyika kwa tukio hili la mauaji ya kikatili," ameeleza Kamanda Muliro.

CHANZO - EATV
Share:

KIGOGO WA JESHI LA POLISI NIGERIA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI


Meja Jenerali Hassan Ahmed

Watu wasiojulikana nchini Nigeria wamempiga risasi na kumuua mmoja wa vigogo wa jeshi la nchi hiyo, Meja Jenerali Hassan Ahmed.

Meja Jenerali Ahmed aliuawa usiku wa Alhamisi nje kidogo ya Abuja wakati gari lake liliposhambuliwa kwa risasi, akitokea jijini Lokoja kwenda Abuja, akiwa na familia yake.

Dereva aliyekuwa anaendesha alijeruhiwa na mwanamke mmoja aliyekuwepo kwenye gari hiyo anayetajwa kuwa dada wa meja huyo, Safina Ahmed alitekwa.

Jeshi la nchi hiyo limeyaelezea mauaji hayo ni ‘tukio la kusikitisha’, huku kuuawa kwake kukiongeza hofu ya usalama nchini humo.

Meja Jenerali Ahmed hivi karibuni aliteuliwa na mkuu wa majeshi ya nchi hiyo kuwa Mkurugenzi wa jeshi makao makuu. Haijajulikana mara moja kina nani hasa walio nyuma ya shambulio hilo na lina lengo gani hasa.

Kwa muda sasa nchi hiyo imekuwa ikikumbwa na matukio ya kiusalama ambapo makundi mbali mbali yenye silaha yamekuwa yakiendesha mauaji na utekaji wakilengwa raia na wanajeshi. Kutokana na vitendo hivyo Mamlaka nchini humo zimekuwa zikitupiwa lawama kwa kushindwa kudhibiti hali hiyo.

Chanzo - BBC Swahili
Share:

POLISI ALIYEUA WANAUME WAWILI ADAIWA KUJIUA KWA KUJIPIGA RISASI



Afisa mmoja wa polisi ambaye amekuwa mafichoni baada ya kuwaua watu wawili amepatikana ameaga dunia.

Mwili wa Caroline Kagongo ambaye amekuwa akisakwa baada ya kuwaua watu wawili,umepatikana nyumbani kwa wazazi wake kaunti ya Elgeyo Marakwet eneo la Rift Valley.

Kulingana na polisi afisa huyo alimpiga risasi mwenzake John Ogweno Jumatatu tarehe 5 Julai na kisha kutorokea eneo la Juja viungani mwa mji wa Nairobi alipomuua mwanaume mwingine aliyetambuliwa kama Peter Ndwiga kwa kumpiga risasi katika chumba cha malazi hotelini.

Vyombo vya habari nchini Kenya vinamnukuu Kamishna wa Kanda ya Rift Valley George Natembeya kuthibitisha kisa hicho.

Ripoti hizo zinasema Kagongo alijiua kwa kujipiga risasi kutumia bastola ambayo alikuwa amejihami nayo na anayoshukiwa kuitumia kutekeleza mauaji ya hapo awali.

Mwili wake ulipatikana bafuni ambako alijiua mwendo wa saa moja unusu asubuhi.

Kagongo amekuwa akisakwa na polisi kwa wiki mbili .

Alikuwa amejihami

Polisi wamekuwa na wakati mgumu kujua aliko kwa sababu aliiacha simu yake katika eneo la kwanza alikotekeleza mauaji .

Mkurugenzi wa idara Jinai George Kinoti alitoa wito kwa umma kuwasaidia kumkamata polisi huyo ambaye alimtaja kuwa "Sugu, aliyejihami na hatari".

Kangogo amehudumu katika vituo mbalimbali vya polisi, pamoja na kitengo cha polisi wa Reli, kabla ya kupelekwa Nakuru, ambapo amekuwa akifanya kazi kwa karibu miaka mitatu.

."Tunaonya wananchi , haswa wanaume, kuchukua tahadhari dhidi ya afisa huyo mwovu ambaye anawashawishi wanaume katika mtego wake kabla ya kuwaua kikatili," alisema.

CHANZO - BBC
Share:

Finance and Administrative Officer at TRAFFIC WWF

Finance and Administrative Officer a    Background: TRAFFIC, the wildlife trade specialists, in alliance with WWF (World Wide Fund for Nature) is seeking a detailed-oriented Finance and Administrative Officer to work in TRAFFIC’S office in Arusha. TRAFFIC, the wildlife trade monitoring network, works to ensure that trade in wild animals and plants is not a […]

This post Finance and Administrative Officer at TRAFFIC WWF has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Head, Transactional & Liabilities Products at Standard Bank

Head, Transactional & Liabilities Products     New role from Future Ready Transformation Job Purpose To design, advise and build fit-for-purpose product solutions for Liabilities and Transactional, in alignment with PBB AR Product and country strategies, whilst trading off client solutioning with risk appetite and financial growth. Key Responsibilities/Accountabilities Jobholder is accountable for the development and […]

This post Head, Transactional & Liabilities Products at Standard Bank has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Quality Control Officer at KaziniKwetu

Quality Control Officer     Kazinikwetu Limited on behalf of a client is looking for a Quality Control Officer for a paints manufacturing company to be based in Dar-es salaam Tanzania Key Duties and Responsibilities   Build strategic SHEQ understanding Drive quality improvement in Manufacturing Maintain safety, health and environment standards Comply with quality systems, standards […]

This post Quality Control Officer at KaziniKwetu has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Application Administrator at Access Microfinance Bank

Application Administrator    EXCITING CAREER OPPORTUNITY (1 Post) Access Microfinance Bank Tanzania (AMBT) is a Microfinance bank with a special focus on small and medium enterprises. With very strong international shareholders such as AccessHolding, International Finance Corporation, KFW, African Development Bank and MicroVest. AMBT’s vision is to be committed to the development of financial systems […]

This post Application Administrator at Access Microfinance Bank has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo July 17



Share:

Risk & Compliance Manager at Airtel

Risk & Compliance Manager     About us Airtel Tanzania PLC is one of the leading providers of telecommunications and mobile money services with operations across Tanzania. Headquartered in Dar es Salaam, Airtel Tanzania ranks amongst the top 3 mobile services providers in Tanzania in terms of subscribers. Airtel Tanzania offers an integrated suite of telecommunications […]

This post Risk & Compliance Manager at Airtel has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Counter Trafficking INTERNSHIP Opportunity at IOM

Movement Operations Units in various IOM Country Offices, coordinated under the Division of Resettlement and Movement Management (RMM) in the Department of Operations and Emergencies (DOE) at IOM’s Geneva Headquarters (HQ), are responsible for all aspects of travel for migrants and refugees under IOM’s auspices, in accordance with the various framework agreements with resettlement and […]

This post Counter Trafficking INTERNSHIP Opportunity at IOM has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Friday, 16 July 2021

RC SENGATI AKUTANA NA WADAU KUPANGA MIKAKATI YA KUZUIA MAJANGA YA MOTO SHULENI....POLISI, ZIMAMOTO WATOBOA SIRI

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemoni Sengati akizungumza wakati akifungua kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemoni Sengati ameongoza kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto yanayotokea katika taasisi na shule mbalimbali.

Kikao hicho kimefanyika leo Ijumaa Julai 16,2021 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kukutanisha wadau mbalimbali wakiwemo Maafisa wa Jeshi la Polisi, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, Maafisa Elimu, Skauti,Waandishi wa Habari n.k ambao kwa pamoja wamekubaliana kushiriki kikamilifu katika kuzuia vyanzo vinavyosababisha kutokea kwa majanga ya moto.

Mkuu huyo wa mkoa amesema ni jukumu la kila mtu katika jamii kushiriki kuzuia vyanzo vinavyosababisha majanga ya moto kwani yanakinzana na suala la amani.

"Tumekutana hapa kwa ajili ya kujadili na kupanga mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwani tumekuwa tukisikia majanga ya moto katika mikoa mingine hivyo ni vyema tupange mikakati ya kuzuia majanga ili kuwa salama na kuwa na amani kwani majanga yanapotokea yanarudisha nyuma maendeleo",amesema Dkt. Sengati.

“Njia mojawapo ya kudhibiti majanga ya moto kwenye shule zetu hasa hizi za bweni ni kuwa na ulinzi shirikishi, kila shule iwe na Walimu walezi (Matron au Patron),kufanya ukaguzi wa mara kwa amara kwa wanafunzi ili kubaini kama wana vitu vinavyohatarisha usalama pamoja na kusuluhisha Migogoro ya ndani na nje ya shule”,amesema Dkt. Sengati.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP George Kyando ameitaja mikakati inayopendekezwa na Jeshi la polisi ili kuzuia majanga ya moto katika taasisi na shule kuwa ni pamoja kila shule na taasisi iwe na walinzi makini , wale waliopitia mafunzo ya ulinzi.

Pendekezo jingine ni pamoja na shule za bweni ziwe na ulinzi shirikishi, kila shule iwe na Matron au Patroni ili kuhakikisha wanafuatilia wanafunzi wanaokuwa mabwenini na kwamba ni vizuri shule iwe na fensi/uzio, geti ili kila anayeingia pale ajulikane, ahojiwe, anaingia kufanya nini.

Kamanda Kyando pia ameshauri pia viwepo vifaa vya awali vya kuzimia moto, mfano mchanga, Fire extinguisher na pia watu wapate mafunzo ya kutumia hivyo vifaa.

“Mienendo ya wanafunzi ifuatiliwe, Itikadi za wanafunzi zifuatiliwe mfano kujiingiza katika siasa au itikadi kali ili kuepuka vishawishi. Wanafunzi wakaguliwe mara kwa mara ili kubaini kama wana pasi za umeme,heater,viberiti, taa za kandili. Wasiwe na vitu visivyofaa kuwa navyo shuleni”,ameongeza Kamanda Kyando.

Kamanda Kyando amesema pia ni lazima migogoro ya ndani na nje ya shule itatuliwe mapema sanjari na utoaji elimu ya namna ya kujikinga na majanga ya moto itolewe kwa wanafunzi.

“Majengo mengi ya shule zetu na miundo mbinu yake imechakaa,hivyo ni vizuri maeneo ya shule yakaguliwe na Tanesco, nyaya ziangaliwe. Milango ya shule iwe ya kufungulia nje/kusukuma kwa nje, na madirisha yasiwekewe nondo”,ameeleza.

Kwa Upande wake Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Shinyanga, Inspekta Edward Lukuba amesema jeshi hilo lina wajibu wa kuzima moto na kutoa elimu ya namna ya kuzuia majanga ya moto akisema wanaendelea kutoa elimu katika shule na taasisi mbalimbali.

“Zipo sababu mbalimbali ambazo zimekuwa zikichangia kutokea kwa majanga ya moto, zipo hujuma lakini mifumo ya umeme inakuwa imechakaa, hitilafu ya umeme,migogoro shuleni,mifumo mibovu ya umeme ‘Wiring’ na mfumo mbovu wa majengo”,amesema Inspekta Lukuba.

“Ili kudhibiti majanga ya moto yanayotokana na sababu za kibinadamu ni Lazima tuboreshe hii mifumo ya umeme, tuwatumie mafundi kutoka TANESCO na ni vyema tuweke sera za usalama shuleni, Wakurugenzi wa halmashauri waajiri fire manager, wafanye risk assessment,tuwe na vifaa vya kuzimia moto na kuifanyia service,tuwe na Smoke detector, gas detector na fire water reserve”,ameongeza Inspekta Lukuba.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemoni Sengati akizungumza wakati akifungu kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga kilichofanyika leo Ijumaa Julai 16,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemoni Sengati akizungumza kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemoni Sengati akiteta jambo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zuwena Omary kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto.
Kamanda wa Jeshi la Polisi  Mkoa wa Shinyanga ACP George Kyando akizungumza kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Shinyanga Inspekta Edward Lukuba akizungumza kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Kahama, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu, Mhe. Joseph Modest Mkude akizungumza kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Wadau wakiwa kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Wadau wakiwa kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Wadau wakiwa kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Wadau wakiwa kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Wadau wakiwa kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Wadau wakiwa kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.
Wadau wakiwa kwenye kikao cha wadau kujadili mikakati ya namna ya kudhibiti majanga ya moto kwenye taasisi na shule mkoani Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog



Share:

RAIS SAMIA AWASILI NCHINI BURUNDI KUANZA ZIARA YA KITAIFA YA SIKU MBILI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa Melchion Ndadaye Jijini Bujumbura Burudi kwa ajili ya kuanza ziara ya kitaifa ya siku mbili leo Julai 16,2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Makamu wa Rais wa Burundi Mkuu wa Burundi Mhe. Prosper Bazombanza alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa Melchion Ndadaye Jijini Bujumbura Burudi kwa ajili ya kuanza ziara ya kitaifa ya siku mbili leo Julai 16,2021.(Picha na Ikulu)

Mapokezi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa Melchion Ndadaye Jijini Bujumbura Burudi kwa ajili ya kuanza ziara ya kitaifa ya siku mbili leo Julai 16,2021.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger