Wednesday, 14 July 2021

MUFTI WA TANZANIA ASEMA SIKUKUU YA EID EL-ADH’HAA ITAKUWA 21 JULAI 2021

Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir ametangaza kuwa Sikukuu ya Eid El-Adh’haa itakuwa Julai 21, 2021, ambapo itakuwa siku ya mapumziko kitaifa.

Taarifa ya Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) imeeleza kuwa maadhimisho ya sikukuu hiyo kitaifa yatafanyika mkoa wa Dar es Salaam ambapo swala itafanyika katika Msikiti wa Mtoro na Baraza la Eid litafanyika hapo hapo.

Mufti ametumia nafasi hiyo kuwatakia Waislam na Watanzania wote sikukuu njema na amewaomba kusherehekea kwa usalama na amani huku wakiendelea kuchukua tahadhari dhidi ya UVIKO-19.


 


Share:

Finance Manager at THPS

Finance Manager     Anticipated USAID Tanzania Orphans and Vulnerable Children (OVC) Next Generation NOFO Number 72062121 RFA 00003 Tanzania Health Promotion Support (THPS) is an indigenous NGO established under non- governmental organization Act No 24 of 2002 in 2011. THPS works in partnership with the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children (MOHCDGEC), […]

This post Finance Manager at THPS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Monitoring, Evaluation, and Learning (MEL)Manager at THPS

Monitoring, Evaluation, and Learning (MEL) Manager   Anticipated USAID Tanzania Orphans and Vulnerable Children (OVC) Next Generation NOFO Number 72062121 RFA 00003 Tanzania Health Promotion Support (THPS) is an indigenous NGO established under non- governmental organization Act No 24 of 2002 in 2011. THPS works in partnership with the Ministry of Health, Community Development, Gender, […]

This post Monitoring, Evaluation, and Learning (MEL)Manager at THPS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Pwani Na Dar Es Salaam Zaongoza Uvamizi Wa Ardhi


Na. Hassan Mabuye, Pwani
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amesema mkoa wa Pwani na Dar es salaam kwa sasa ndio inaongoza kwa uvamizi wa ardhi za watu kwa kutumia nguvu kinyume na utaratibu.

Waziri Lukuvi ameyasema hayo jana wakati wa uzinduzi wa kampeni maalumu ya kusikiliza, kutatua na kutokomeza kabisa migogoro ya ardhi kwa mkoa wa Pwani katika mkutano uliyofanyika ofisi ya mkuu wa mkoa Pwani na kuhudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa.

“Hii mikoa miwili ya Pwani na Dar es salaam inaongoza kwa uvamizi wa ardhi na matumizi ya nguvu katika kujimilikisha ardhi za watu wanaomiliki kihalali. Watu wanatoka Dar es salaam wanakuja mkoa wa Pwani kuchukua ardhi za watu na kudai kumilikishwa” Amesema Waziri Lukuvi.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Pwani ni eneo muhimu sana kwa uwekezaji kwa hiyo haiwezekani kuwaachia watu kuvamia maeneo ya viwanda, mashamba, maeneo ya umma na maeneo ya wazi ambayo yapo kisheria.

Waziri Lukuvi amemtaka kila mkuu wa wilaya aitambue migogoro ya ardhi katika maeneo yake, awe na taarifa ya kina ya kila mgogoro na atengeneze daftari la migogoro ya ardhi kwa kushirikiana na wataalamu wa ardhi katika kuitatua na kama kuna afisa ardhi sio muadilifu aletwe kwake ili amchukulie hatua.

Katika hatua nyingine Waziri Lukuvi amesema Wakurugenzi ndio wenye mamlaka ya upangaji wa miji, kama wataruhusu utendaji mbovu wa sekta ya ardhi katika halmashauri zao, watawajibika kwa kuwa katika sheria ya ardhi wao ndio wasimamizi wakuu wa sekta ya ardhi.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge ambaye ndiye aliyezindua rasmi Kampeni ya kushughulikia Migogoro ya Sekta ya Ardhi Mkoani Pwani ameeleza kuwa watafanya ziara na Mhe. Waziri wa Ardhi katika Wilaya za Kibaha, Bagamoyo, Mafia, Mkuranga, Rufiji na Kibiti kuanzia Tarehe 14 Julai, 2021  hadi Tarehe 22 Julai 2021 kushughulikia na kutatua Migogoro ya Ardhi.

Kunenge, amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wote Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanatumia nafasi zao katika kutatua migogoro ya Ardhi katika maeneo wanayoyaongoza.

Kunenge pia amewataka Viongozi hao wa Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanaboresha Daftari la makazi na kuhakiki idadi ya mifungo iliyopo mkoani Pwani ili kuepukana na Migogoro ya Ardhi.

Katika hatua Nyingine Kunenge amesema kuwa hatosita kumchukulia hatua kali za kisheria kwa yeyote yule atakaefanya uvamizi wa aina yoyote katika mkoa wa Pwani.

“Sheria zipo wazi watu wanavamia lakini hawachakuliwi hatua, hivyo sasa tutachukua hatua  kali hatutaonea mtu ila tutatenda haki” alisema Kunenge.

Aidha, Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Pwani Bibi. Lucy Kabyamela amesema kwamba wakazi wengi wa mkoa wa Pwani wamekuwa na kasumba ya kuamini kwamba mtu kumiliki ardhi kubwa kisheria ni makosa, ndio maana wanavamia maeneo ya watu na kujigawia kwa nguvu.


Share:

Waziri Mkuu Majaliwa Akutana Na Waziri Mkuu Na Waziri Wa Mambo Ya Nje Wa Morocco


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Julai 12, 2021 kwa nyakati tofauti amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Africa wa Morocco Nasser Bourita na Waziri Mkuu wa Morocco Saad Dine El Otmani.

Katika Mzungumzo hayo Waziri Mkuu alizungumzia kuimarisha ushirikiano mzuri na wa kihistoria kati ya Tanzania na Morocco ulioasisiwa na kujengwa na wasasisi wa nchi hizi mbili Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mfalme Mohammed V.

Sponsored: Je, Unatafuta Kazi Serikalini? Bofya Hapa

Waziri Mkuu alisisitiza umuhimu wa nchi hizi kuendelea kushirikiana katika sekta mbalimbali ikiwemo Elimu, Kilimo, Utalii, Nishati na Uvuvi.

Katika mazungumzo hayo, Waziri Mkuu aliambatana na Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda, Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale wa Zanzibar Leila Muhamed Mussa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk.



Share:

Waziri Biteko Atoa Onyo Stamigold


 Na. Steven Nyamiti, Kagera
Waziri wa Madini Doto Biteko amemuagiza Meneja Mkuu wa Mgodi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Bodi na Menejimenti pamoja na wafanyakazi wote wa mgodi wa STAMIGOLD, kujitafakari kama utendaji wao una manufaa kwa Taifa.

Amesema hayo Julai 13, 2021 Biharamulo Mkoani Kagera katika ziara aliyoifanya ya kutembelea mgodi wa STAMIGOLD ambayo ni Kampuni tanzu ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) uliyopo katika wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera.


Akizungumza na menejimenti pamoja na wafanyakazi wa mgodi wa STAMIGOLD amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Madini inachukizwa sana na vitendo vya utoroshaji madini ya dhahabu vinavyofanywa na baadhi ya watumishi wasiowaaminifu.

“Mungu amewapa bahati ya kuwa kwenye mgodi huu nawasihi uleeni mgodi huu. Mkiulea na nyinyi utawalea. Shirika hili likifa wengi mtapoteza ajira na kukosa mishahara” ameeleza Waziri Biteko.

Waziri Biteko amemuagiza mwenyekiti wa bodi ya STAMICO kuhakikisha anachukua hatua za kiutumishi dhidi yao na wale waliopo mahakamani hatua za ndani zifuatwe za kazi ili wawajibishwe.

Naye, Meneja Mkuu wa mgodi wa STAMIGOLD Injinia Gilay Shamika akieleza taarifa ya Maendeleo ya mgodi huo hadi kufikia Mwezi Mei 2021 amesema wafanyakazi wote wa mgodini kwa sasa wanafanya kazi kwa kujituma kwa kila hali ili kuongeza uzalishaji na kuhakikisha hawarudi nyuma tena katika kuilinda rasilimali madini katika mgodi huo.

Aidha, Injinia Shamika ameipongeza STAMICO kwa kuendekea kufanikisha shughuli mbalimbali za Uwekezaji za mgodi wa STAMIGOLD.

Katika ziara hiyo, Waziri Biteko alitembela na kujionea miundombinu iliyopo katika mgodi wa STAMIGOLD ikiwemo mtambo wa uchenjuaji wa Dhahabu na Bwawa la kuhifadhia topesumu (TSF).Pia Waziri Biteko ametembelea Mgodi wa wachimbaji wadogo wa Dhahabu Matwiga ambapo amezungumza na wachimbaji wa eneo hilo kuhusu changamoto mbalimbali zinazowakabili na kuzitolea majibu.

Wengine walioshiriki ziara hiyo ni Mkuu wa wilaya ya Biharamulo Kimelembe Rwota, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Dkt. Venance Mwasse, Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Geita Lucas Mlekwa, Kaimu katibu mtendaji wa Tume ya Madini Ramadhani Lwamo, Kaimu kamishna wa madini Muhandisi Zephania Nsungi na wafanyakazi wa STAMIGOLD.



Share:

Manager: Trade Finance Sales at NBC

Manager: Trade Finance Sales    NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Job Summary Provide specialized products selling to ever growing corporate clients base by engaging the Corporate Bankers, focusing on growing […]

This post Manager: Trade Finance Sales at NBC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Renewable Explorer (Rex) – Senior Business Developer Renewables at Total

Renewable Explorer (Rex) – Senior Business Developer Renewables     Job Description Market analysis:   Analyze key factors for the development of renewable projects in the market: Electricity market (regulation, price structure) Electricity demand (segmentation, location, growth) Electricity production (mix, emissions, production centers) Grid (age, quality, development projects, interconnection, access) Renewable resources Land availability Keep yourself […]

This post Renewable Explorer (Rex) – Senior Business Developer Renewables at Total has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Finance Officer at Norwegian Refugee Council

Finance Officer     Job Description All NRC employees are expected to work in accordance with the organisation’s core values: dedication, innovation, inclusivity and accountability. These attitudes and believes shall guide our actions and relationships. ROLES AND RESPONSIBILITIES    Implement NRC’s systems and procedures at area level. Ensure adherence to NRC policies, handbooks, guidelines and donor […]

This post Finance Officer at Norwegian Refugee Council has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Finance Technical Assistant at Norwegian Refugee Council

Finance Technical Assistant     Job Description All NRC employees are expected to work in accordance with the organization’s core values: dedication, innovation, inclusivity and accountability. These attitudes and believes shall guide our actions and relationships.   ​​​​​Adhere to NRC policies, tools, handbooks and guidelines. Assist with the implementation of the support function portfolio according to […]

This post Finance Technical Assistant at Norwegian Refugee Council has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Principal Credit Appraisal Officer at TADB

Background of TABD   Tanzania Agricultural Development Bank Limited (TADB) is a government institution operating under the Ministry of Finance and Planning. Established in 2012 TADB is registered under the Companies Act, 2002 and licensed under the provisions of the Banking and Financial Institutions Act No 5 of 2006 and the Banking and Financial Institutions […]

This post Principal Credit Appraisal Officer at TADB has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JULAI 14,2021




























Share:

Tuesday, 13 July 2021

SERIKALI YAWATAKA WANANCHI KUZINGATIA MAELEKEZO YA KUJIKINGA NA CORONA


Na Mwandishi Wetu, Kigoma
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mwanaidi Ali Khamis amewataka wananchi kuzingatia maelekezo yanayotolewa na wataalam wa afya nchini kujikinga na ugonjwa wa homa ya mapafu inayoletwa na virusi vya wa Corona.  

Naibu Waziri Mwanaidi Ali Khamis ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake Mkoani Kigoma katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa huo pamoja na Makazi ya wa Wazee Kibirizi.

Ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan itahakikisha inawalinda wananchi wake dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa kuhakikisha elimu ya kujikinga inatolewa kwa kasi.

Sponsored: Nafasi Mpya za Kazi Serikalini, Taasisi Binafsi. Bofya Hapa


“Niseme tuchukue tahadhari zote tunawe mikono kwa maji tiririka, tuvae barakoa na tuepuke misongamano ili tuweze kuondokana na maambukizi ya ugonjwa huu ambao wimbi la tatu limeibuka” alisema Naibu Waziri Mwanaidi

Aidha, Naibu Waziri Mwanaidi amekagua Dirisha maalum kwa ajili ya utoaji wa huduma kwa wazee ambapo ameeleza kuvutiwa kwake na huduma zinazotolewa na kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kulivalia njuga suala la kuboresha huduma kwa kundi hilo muhimu kwa Taifa.

Amewaagiza watendaji katika sekta ya Afya kushirikiana na maafisa Ustawi wa Jamii katika ngazi zote kuhakikisha kwamba huduma za afya na huduma nyingine za kijamii zinaboreshwa ili Wazee waishi maisha bora na yenye staha.

Akisoma taarifa ya Hospitali ya Maweni, Mganga Mfawidhi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Dkt. Osimundi Dyegura amesema huduma za katika Hospitali hiyo zimeboreshwa ikiwa ni pamoja kuanzishwa kwa madirisha maalum kwa makundi maalum zikiwemo huduma kwa wazee.

Pamoja na mafanikio hayo Dkt Dyegura amesema miongoni mwa changamoto zinazoikabili Hospitali hiyo ni pamoja na uchakavu wa baadhi ya majengo na uhaba wa madaktari Bingwa kwa baadhi ya magonjwa.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Mwanaidi ametembelea Makazi ya Wazee Wasiojiweza Kibirizi Mkoani Kigoma ambapo amevutiwa na huduma zinazotolewa na maafisa kwa kushirikiana na uongozi wa Halmashauri ya Manispaa na Mkoa wa Kigoma.

Amesisitiza kuwa Serikali inawatambua na kuwathamini Wazee wote nchini hivyo wana kila sababu ya kutembea kifua mbele wakiwa na imani kwamba Serikali itaendelea kuboresha huduma kwa wazee kadiri inavyopata rasrimali.

Akizungumza kwa niaba ya Wazee, Katibu wao, Veronica Ramadhan amemshukuru Naibu Waziri kwa kuwatembelea na kuwapelekea Zawadi ya Mbuzi wawili kwa ajili ya kitoweo na kushukuru kwa huduma wanayoipata katika Makazi hayo.

Bibi Veronica ameshukuru kwa zawadi hiyo na kusema imewaongezea moyo wa Imani kwa serikali huku akituma salamu za shukrani kwa Rais Samia  Suluhu Hassan kwa kuwaelekeza wasaidizi wake kuyatembelea makundi maalum likiwemo kundi la Wazee.

Pia katika ziara yake Naibu Waziri Mwanaidi ametembelea Dawati la Polisi la Jinsia Wilayani Kigoma ambapo ameelezwa kuwa kiwango cha ukatili wa kijinsia Mkoani kiko juu na hatua mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa na kuvielekeza vyombo vinavyoshughulikia na kesi za vitendo vya ukatili kuhakikisha kesi hizo zinashughulikiwa kwa haraka na watuhumiwa pamoja na wahanga wa vitendo hivyo wanapata haki yao.



Share:

MRADI WA UJENZI WA KITUO CHA MAFUNZO YA KILIMO WA BARRICK KUNUFAISHA WAKULIMA KAHAMA


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2021 Luteni Josephine Mwambashi akikata utepe kuweka jiwe la msingi la kituo cha mafunzo ya kilimo cha Mwendakulima wilayani Kahama
Meneja anayesimamia mradi wa ujenzi wa kituo cha Mafunzo ya Kilimo kinachofadhiliwa na Barrick, Elibariki Jambau akisona risala kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru na viongozi wa mkoa wa Shinyanga
Baadhi ya wafanyakazi wa Barrick katika hafla hiyo
Wafanyakazi wa Barrick na wafanyakazi kutoka sekta mbalimbali za Serikali wakati wa hafla hiyo

***
Mradi wa ujenzi wa kituo cha mafunzo ya kilimo na ufugaji katika kata za Mwendakulima na Mondo unaofadhiliwa na kampuni ya madini ya Barrick,mgodi wa Buzwagi, umeanza kunufaisha wakulima na iwapo watatumia ujuzi wanaopata kituoni hapo watafanikiwa zaidi kwa kuongeza uzalishaji wa mazao na ufugaji wa kisasa.

Hadi sasa mradi huo ambao ulianzishwa mwaka 2018 umeishanufaisha wakulima zaidi ya 3,924 kutoka vijiji 9 katika eneo la Mondo na Mwendakulima katika wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Akiongea wakati wa hafla ya uwekaji wa kuweka jiwe la msingi wa kituo cha Mwendakulima jana uliofanywa na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi, Meneja wa mradi huo kutoka Barrick, Bw. Elibariki Jambau, alisema kuwa mradi huo unatekelezwa kwa kipindi cha miaka 5 kuanzia mwaka 2018 na utamalizika mwaka 2023.

Alisema lengo la mradi huo ni kuongeza tija kwa mazao ya kilimo na mifugo vilevile kituo kuwa ni kitovu cha upatikanaji maarifa ya kilimo na taarifa za masoko ya mazao kutoka kwa wataalamu mbalimbali wa Serikali.

Jambau alisema mpaka mradi huu kukamilika utagharimu kiasi cha shilingi milioni 529 na hadi sasa kazi ambazo zimekamilika katika mradi zimegharimu kiasi cha shilingi milioni 138,763,285,00.

"Mpaka sasa kazi zilizokamilika ni upandaji miti ya mbao, ubebeshaji wa miche ya matunda, ujenzi wa kitalu nyumba, ujenzi wa kisima cha maji, ununuzi wa Trekta, Mashine ya kupukuchua mahindi, mpunga, kununua mashine ya kupima unyevu, uzito, pamoja na kutoa mafunzo kupitia mashamba ya mfano kwa wakulima 1,801, sawa na asilimia 46.8 na wakulima waliolengwa.

Mafanikio ambayo yamepatikana hadi sasa alisema ni kuongezeka kwa mavuno ya wakulima kutoka magunia 15 hadi 28 ya mahindi kwa kila ekari na magunia 18 hadi 32 za mpunga, kuwaunganisha wakulima na wadau 17 wa pembejeo na zana za kilimo na masoko 14 ndani na nje ya Kahama, kusambaza miche 69,000 ya miti mbalimbali kwa wakulima pamoja na shule 14.Vilevile vyama 2 vya Ushirika wa mazao (AMCOS) pamoja na uanzishwaji wa vikundi 29 vya uzalishaji”, alisema Jambau.

Aliongeza kuwa shughuli nyingine inayotarajiwa kufanyika katika kituo hiki ni uboreshaji wa koosafu za mifugo kwa kutumia njia ya chupa katika uzalishaji (Uhamilishaji) ili kuboresha ng’ombe wa kienyeji na kupata ng’ombe chotara kwa ajili ya kuongeza tija ya uzalishaji wa maziwa na nyama.

Akiongea baada ya kuweka jiwe la msingi la kituo hicho, Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi,aliipongeza kampuni ya Barrick kwa kuanzisha mradi huo ambao utanufaisha wakulima wengi na kuwataka wakulima wausimamie uwe endelevu.

Ametoa wito kwa wakulima kuchangamkia fursa ya mafunzo yanayopatikana kituoni hapo ili waweze kupata maarifa yatakayowawezesha kuendesha kilimo cha kisasa na ufugaji wa kisasa ili wapate mavuno mengi.

Akiongea kwa niaba ya wakulima ,Tembo Mihango, mkulima kutoka kijiji cha Penzi kata ya Mondo ,alisema Barrick kwa kuanzisha mradi huu imetekeleza msemo wa “kama unataka kusaidia mtu usimpe samaki bali mfundishe kuvua” kwa kuwa wakulima kwa kupatiwa maarifa wanaweza kujitegemea kutokana na shughuli zao sambamba na kuboresha maisha yao.
Share:

Nafasi za Kazi: Watendaji wa Kijiji Daraja la tatu


Nafasi za Kazi: Watendaji wa Kijiji Daraja la tatu

Kwa nafasi nyingi za kazi kama hizi <<BOFYA HAPA>> 


 

Nafasi za Kazi: Watendaji wa Kijiji Daraja la tatu

Kwa nafasi nyingi za kazi kama hizi <<BOFYA HAPA>> 



Share:

WATUMISHI TISA WA AFYA WASIMAMISHWA KAZI UWANJA WA NDEGE DAR KWA KUTOKUFIKA KAZINI KUTOA HUDUMA YA VIPIMO VYA CORONA


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Watumishi tisa wamesimamishwa kazi katika Kitengo cha upimaji wa COVID - 19 kwa wasafiri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere (JNIA).

Agizo hilo limetolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Prof. Abel Makubi alipofanya ziara uwanjani hapo kukagua utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa juzi alipofika hapo akiwa ameambatana na Katibu mwenzake wa Wizara ya Uchukuzi.

Prof. Makubi amesema hakufurahishwa na kitendo cha utovu wa nidhamu, kilichofanywa na watumishi cha kutokufika kazini bila kutoa taarifa rasmi kwa uongozi hapo jana na leo.

"Jana watumishi wanane hawakufika na leo mmoja bila kutoa sababu ya msingi, jumla wanakuwa tisa," amebainisha.

Ameongeza "Imeonekana hapa hili zoezi la baadhi ya watumishi kutokuja kazini limekuwepo, sasa hii imenisikitisha sana kwa baadhi ya viongozi kushindwa kuchukua hatua zinazostahili na kulindana kwa kuficha uozo.

"Kwa hiyo hawa ambao hawakufika jana ambao jumla walikuwa wanane na kati yao wanne walikuwa wameajiriwa na Wizara ya Afya na wanne wameajiriwa na Manispaa ya Dar es Salaam, wapo chini ya RAS wa Dar es Salaam.

"Nimeagiza hawa walio chini ya Wizara ya Afya wasimame kufanya kazi ili tufanye uchunguzi na kuchukua hatua stahiki.

"Huu ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu ambapo mtumishi anaamua kuacha kuja kazini na kusababisha usumbufu kwa wenzake na abiria ambao wanakuja hapa kwa sababu yeye 'gap yake haijawa covered' na mtu yeyote," amesisitiza.

Prof. Makubi ameongeza "Lakini vile vile ambao wameajiriwa na Ofisi ya RAS nitashauri mamlaka husika nao wachukuliwe hatua hivyo hivyo ambazo zimechukuliwa kwa hawa wa Wizara.

Amesema Serikali haiwezi kuvumilia watumishi wasio na nidhamu na wanaodharau majukumu wanayopewa.

"Hizo ndizo hatua ambazo tumechukua, lakini pia tutahakikisha tutaleta wengine 'ku-replace' hao tisa waweze kuendelea ili tusije tukaathiri hizi shughuli za upimaji hapa 'airport'," amesema.

Ametoa onyo kwa watumishi wa afya nchini, wawe tayari kufanya kazi popote pale watakapopangiwa.

"Waende wakafanye kazi siyo kwamba ukipelekwa upande mmoja unaamua kususia kama hawa ambavyo waliamua ni kwa sababu walihamishwa kutoka kwenye vituo vyao vya awali wameletwa huku.

Amewataka watumishi wote wa afya kutanguliza uzalendo wa hali ya juu katika utendaji wa kazi zao na kwa kujituma.

"Hapa tunapofanya upimaji, ni upimaji unawakilisha sura ya Nchi yetu. Kwa hiyo mtu yeyote anayeletwa hapa maana yake ndiye anayetoa taswira ya nchi yetu kwa ujumla.

"Anavyohudumia wasafiri, customer care yake na yeye mwenyewe kujibidiisha wanapofika hapa. Niwaombe watumishi ni vizuri watangulize uzalendo katika kazi zao lakini pia kuwajibika kwa kile walichopangiwa kwa kujitoa ili kuepusha malalamiko kwa wananchi.

"Najua watumishi wengi wanaojituma ila kwa hawa wachache niwaombe wazingatie uzalendo, uwajibika na 'customer care' nzuri wanapohudumia wananchi," ameagiza.

Awali, Prof. Makubi amesema maelekezo waliyoyatoa na Katibu mwenzake wa Wizara ya Uchukuzi yametekelezwa ikiwamo la kuongeza watumishi katika eneo la upimaji.

"Nimefarijika kuna maboresho zaidi yamefanyika, hasa hasa kuongeza sehemu za kupima lakini pia maeneo ambayo abiria wanaweza kuwa wanapimwa.

"Nimeona wameongeza upande mmoja ambao abiria watakuwa wanaingia wakifuata mstari na pia kwa umbali wa mita moja moja kwa kuachana.

"Lakini pia upande wa kushoto na kwenyewe nimekuta kumeongezwa maeneo ambayo watakuwa wanaingia na kupimwa na kuna watumishi 20 tumeongeza kama tulivyokuwa tumeongea siku zile," amesema.

Amesema watumishi hao wameongezeka kulingana na ongezeko la abiria.

"Kwa sababu mwanzoni abiria walikuwa wachache sasa hivi wamekuwa wengi, kwa hiyo kama Wizara tumeweza kuhakikisha kwamba ile changamoto waliyokuwa nayo ya watumishi ili waweze kuendana na abiria imeweza kutekelezwa, wameshafika na wamefanyiwa 'orientation' ili waweze kufanya kazi na wenzao" amesema.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Prof. Abel Makubi akizungumza baada ya kutembelea uwanja wa ndege wa kimataifa wa JNIA
Share:

Head Of Human Resources & Administration

Background of TABD   Tanzania Agricultural Development Bank Limited (TADB) is a government institution operating under the Ministry of Finance and Planning. Established in 2012 TADB is registered under the Companies Act, 2002 and licensed under the provisions of the Banking and Financial Institutions Act No 5 of 2006 and the Banking and Financial Institutions […]

This post Head Of Human Resources & Administration has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger