Friday, 28 May 2021

Waziri Mhagama: Tatizo la ajira nchini, Tafiti mbili kwenye nguvu kazi na Rasilimali watu kufanyika mwaka huu.


Katika kuhakikisha malengo ya kutatua masuala ya ajira na kazi, yanafikiwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), imepanga mwaka huu kufanya tafiti mbili kubwa ambazo zitajikita kwenye kubaini nguvu kazi pamoja na rasilimali watu.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, wakati akifungua Kongamano la Wadau wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo  tarehe 27 Mei, 2021, Jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wanaendelea kushirikiana ambapo Wizara hiyo inapitia sera ya elimu na huku Ofisi hiyo ikifanya tafiti.

“Mwaka huu tumeamua kufanya tafiti mbili kubwa ambapo tafiti moja tunaendelea nayo ambayo ni hali ya nguvu kazi nchini. Utafiti huo utatausaidia kujua ni asilimia ngapi ya vijana wanaofundishwa ndani ya  nchi na  wanaweza kuajirika nchini  na kama hawajaajiriki ni kwa nini. Aidha Utafiti huo utatusaidia kuelewa sekta ipi yenye fursa nyingi kuliko sekta nyingine ya ajira hii itasaidia mafunzo ya ufundi yaendane na mahitaji yetu ya ajira” Amesisitiza Mhagama

Aidha, Mhe. Mhagama amefafanua kuwa serikali imeshakamilisha utaratibu wa kufanya utafiti wa Hali ya rasilimali watu nchini. Utafiti huo utasaidia kuelewa juu ya watanzania waliopo nchini na waliopo nje ya nchi kama wanaendana na mahitaji ya ajira kwa sasa.

Ameongeza kuwa, Ofisi ya Waziri Mkuu imekuwa ikisimamia vibali vya ajira kwa wageni, hivyo wataelewa sababu ambazo hupelekea wawekezaji kuhitaji kuwaleta watu wao wenye ujuzi ile hali wenye ujuzi wa viwango hivyo wapo hapa Tanzania, lakini pia itaeleweka maeneo gani ambayo nchi haina ujuzi na wangependa ujuzi huo upatikane hapa nchini.

Mhe. Mhagama amewataka wadau wa elimu ya Ufundi kuendelea kushirikiana na serikali katika kuhakikisha changamoto za ajira zinashughulikiwa ipasavyo nchini. Amesisitiza kuwa ili kuweza kuwa na uchumi wa kati endelevu hadi kufikia uchumi wa juu tunahitaji kuwa na mfumo rasmi wa kuwandaa vijana katika viwango vya juu vya maarifa, ujuzi, na stadi za kutenda.

Mhe. Mhagama amefafanua kuwa kwa sasa serikali inaendelea kutekeleza miradi ya kimkakati kwenye sekta ya nishati ya umeme, Reli ya kisasa, kwenye Sekta ya Afya na Elimu pamoja na Barabara na hivi karibuni utatekelzwa mradi wa Bomba la mafuta kutoka Tanzania hadi nchini Uganda. Ameeleza kuwa miradi hiyo ili iwe endelevu ipo haja ya kuwa na wataalamu wenye ujuzi wa kuendeleza uangalizi wa miradi hiyo.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la (NACTE), Prof. John Kondoro na Katibu Mtendaji (NACTE) Dkt. Adolf Rutayuga,wamefafanua kuwa  Kongamano hilo litalisaidia Baraza hilo kuwa na mipango ya kuunganisha nguvu ili kuwekeza kiasi cha kutosha katika Elimu ya Ufundi.

Aidha, wamefafanua kuwa wataweza kuwa na suluhisho kwenye masuala ya kupata maeneo ya kutosha ya mafunzo ya vitendo, Upatikanaji wa Takwimu sahihi za wataalamu kwenye sekta za ajira, Kuimarisha uhusiano kati ya Taasissi za Mafunzo na soko la ajira, na hatimaye Elimu na Mafunzo ya Ufundi itaweza kutoa mchango mkubwa katika Maendeleo ya sekta zote za kiuchumi hapa nchini.

Pia, Mkurugenzi Idara ya Wanachama, Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Zachy Mbenna ameiomba serikali kushirikiana na sekta Binafsi katika juhudi za kuendeleza kukuza ujuzi kwa kusimamia tozo inayotozwa ya kukuza ujuzi  kwa kuelekezwa kwenye kukuza ujuzi moja kwa moja  kwa kuishirikisha sekta Binafsi kwenye maoni ya matumizi yake.

Ameomba kiwepo chombo cha kitaifa kitakacho ratibu juhudi za kukuza ujuzi kwa kuwaunganisha wanaotoa mafunzo ya kukuza ujuzi. Aidha, ameomba kuwapa motisha waajiri wenye utaratibu wa kukuza ujuzi katika maeneo yao ya kazi kwa kupewa utambuzi wakati wa kulipa kodi, ameomba wadau hao wa sekta Binafsi wanaochangia masuala ya ujuzi kupewa mazingira ya kipaumbele wakati wa uwekezaji. Utekelzaji wa masuala hayo yatasaidia kuongeza idadi ya wadau wanaotekeleza masuala ya kukuza nchini.

Kauli Mbiu ya Kongamano hilo ilikuwa ni “Kuimarisha Ushirikiano wa Wadau katika Kukuza Ujuzi kwa Maendeleo ya Uchumi wa Viwanda” Wadau hao ni Serikali, Taasisi zinazotoa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, na Waajiri. Kongamano hilo limeandaliwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) kwa ushirikiano na Taasisi ya Sekta Binafsi.

MWISHO.


Share:

Jeshi la Polisi Shinyanga lakamata Dawa za Kulevya


 SALVATORY NTANDU
Masunga Nindwa (36)mkazi wa Lunzwe mkoani Geita na Peter Matiko mkazi wa nyakato mkoani Mwanza wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Shinyanga kwa tuhuma za kupatikana na dawa za kulevya aina ya bangi kilogramu 20 na mirungi kilogramu 25.

Akizungumza waandishi wa habari  Kamanda wa jeshi la polisi mkoani humo (ACP) Debora Magiligimba alisema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa katika matukio mawili tofauti baada ya kufanyika kwa msako mkali wa jeshi hilo ambao umefanikisha kukamatwa kwa dawa hizo.

Katika tukio la kwanza Masunga Nindwa alikamatwa na jeshi la polisi wilayani kahama mei 21 mwaka huu katika nyumba ya kulala wageni ya kalunde iliyopo katika mtaa wa nyasubi akiwa na debe mbili za bangi zenye uzito wa kilogramu 20 huku akijua wazi kuwa kufanya hivyo ni kosa la jinai.

Kamanda Magiligimba alisema kuwa katika tukio la pili mei 21 mwaka huu majira ya asubuhi katika kata ya Ibinzamata Peter Matiko alikamawa na jeshi hilo akiwa na mirungi kilogramu 25 iliyokuwa imewekwa kwenye mabegi aliyokuwa anaisafirisha kwenda mkoani Singida.

“Jeshi la polisi lilipata  taarifa za kiintelijensia kutoka kwa wasamaria wema na kuanza kuafuatilia na kisha kufanikiwa kuwakamata na dawa hizo za kulevya,mtuhumiwa wa mirugi alikiri kutumia na kuuza dawa hizo upelelezi ukikamilika tutawafiksha mahakamani,”alisema Magiligimba.

Sambamba na hilo Magiligimba alisema kuwa jeshi hilo pia linamshikilia Elida Zakaria (19)mkazi wa kagongwa kwa tuhuma za kukutwa na kete 111 za dawa za kulevya aina ya bangi zilizokuwa zimefungwa kwenye magazeti  nyumbani kwa Lucia Luhende ambaye ndiye mmiliki wa dawa hizo

“Tunatarajia kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote upelelezi ukikamilika na tunatoa rai kwa wananchi kuwafichua watu wanaouza na kusafirisha dawa za kulevya ambazo zimekuwa zileta athari kwenye jamii”,alisema Magiligimba.

Mwisho.


Share:

HEALTH LABORATORY ASSISTANT – 14 POST at Ministry Of Health (MOH)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST HEALTH LABORATORY ASSISTANT – 14 POST POST CATEGORY(S) HEALTHCARE AND PHARMACEUTICAL EMPLOYER Ministry Of Health (MOH) APPLICATION TIMELINE: 2021-05-27 2021-06-09 JOB SUMMARY NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To maintain cleanliness of the laboratory , glassware and equipment; ii. To perform Phlebotomy duties; iii. To keep records of received specimens, laboratory investigations and procedures under […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

LABORATORY TECHNOLOGIST II – 9 POST at Ministry Of Health (MOH)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST LABORATORY TECHNOLOGIST II – 9 POST POST CATEGORY(S) HEALTHCARE AND PHARMACEUTICAL EMPLOYER Ministry Of Health (MOH) APPLICATION TIMELINE: 2021-05-27 2021-06-09 JOB SUMMARY NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To rreceive, extract and record samples for laboratory examination; ii. To prepare laboratory equipment and chemical tests and examinations; iii. To inspect and store laboratory reagents, equipment […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Mwalimu akamatwa akijifanya Usalama wa Taifa ili atapeli


SALVATORY NTANDU
Jeshi la polisi mkoa wa shinyanga linawashikilia watuhumiwa watatu Dismond Zakaria mwalimu (33) Feisal Husein mtaalamu wa teknolojia ya mawasiliano (27) na Juma Almasi (35)mfanyabiashara kwa tuhuma ya kupatikana na nyaraka za serikali za kughushi kwa lengo la kufanya utapeli kwa wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari wilayani Kahama kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga (ACP) Debora Magiligimba amesema kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa mei 26 mwaka huu katika mtaa wa namanga wilayani humo katika msako maalumu wa kupambana na wahalifu.

Alisema kuwa baada ya kukamatwa walipatikana na nyaraka mbalimbali za serikali ikiwemo kitambulisho cha Idara ya usalama wa taifa,vitambulisho viwili vya jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) mhuri mmoja na barua mbalimbali zenye nembo ya jeshi la hilo.

“Watuhumiwa hawa hutumia magari mawili kufanya utapeli katika maeneo mbalimbali ya Tanzania yenye namba za usajili T 677 BMA Toyota Carina na T 110 DSX Toyota Rumion kwa kujiwasilisha kwa wafanyabiashara hususani watoa huduma za kifedha kuwa wao ni maafisa wa umma na wakifanikisha azima yao hutoroka,”alisema Magilimba.

Kamanda Magiligimba amesema kuwa watuhumiwa hao wanatumia vitambulisho vya Jeshi la wananchi viwili vyenye cheo cha Kanali na kimoja cha idara ya usalama wa taifa,pamoja na sare kwa lengo la kuwahadaa wananchi ili kujipatia fedha kwa njia isiyo halali huku wakijua wazi kuwa suala hilo ni kinyume cha sheria.

“Tumewakamata wakiwa na karatasi bandia zinazotumika kutapelia watoa huduma za za fedha,walikuwa wanatumia mbinu ya kuacha mabegi yao yenye karatasi hizo bandia katika ofisi hizo na kisha hurudi jioni na kuwaaminisha kuwa ni fedha halali,jambo ambalo halina ukweli wowote,”alisema Magiligimba.

Amefafanua kuwa mbinu nyingine inayotumiwa na watuhumiwa hao ni pamoja na kuwatongoza na kuwanywesha pombe wanawake na kuwaibia vitu vya thamani kama vile simu na fedha pamoja na kuwaahidi kuwapatia kazi kwa idara ya usalama wa taifa na jeshi la wananchi wa Tanzania.

“Bado tunaendelea kuwahoji na upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili na kuwaomba wananchi kuendelea kutoa taarifa pindi wanapowatilia shaka watu wanamna hiyo ambao hutumia vibaya nyaraka za serikali kujipatia kipato kwa njia isiyo halali,”amesema Magiligimba.

Mwisho


Share:

Waziri Mkuu Majaliwa awasimamisha kazi Mkaguzi Mkuu, Mkaguzi Msaidizi pamoja na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Fedha


 Waziri Mkuu, Mheshimwa Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi Mkaguzi Mkuu,  Mkaguzi  Msaidizi pamoja na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Fedha na Mipango ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha  za umma zinazowakabili.

Akizungumza katika Kikao Kazi na Waziri wa Fedha na Mipango, Kaibu Mkuu,Manaibu  Katibu Wakuu na Watendaji Waandamizi wa Wizara hiyo kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma Mei 27, 2021,  Mheshimiwa Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kamishna wa Polisi ACP Salum Rashid Hamdun kufanya uchunguzi kuhusu tuhuma hizo na ikithibitika kwamba tuhuma si za kweli wahusika watarejeshwa kazini.

Mheshimiwa Majaliwa alizitaja baadhi ya tuhuma hizo kuwa ni malipo yaliyofanyika  Machi 31, Mwaka huu  kupitia vocha 30 ya sh.milioni 251  yakielezwa kuwa ni malipo maalum bila kutaja kazi hiyo maalum ni kazi gani na nani aliifanya hiyo kazi.

Amesema  siku hiyo hiyo  ya Machi 31 pia zililipwa  sh. milioni 198.8 kwa madai kuwa ni posho ya honoraria.

Mheshimiwa Majaliwa  amesema Aprili 8 mwaka huu watumushi  27 wa  Wizara hiyo walilipwa sh. milioni 44.5 zikiwa ni posh ya kazi maakum ya wiki nne. Pia  Aprili 13 mwaka huu zililupwa sh. Milioni 155.2 kwa watumishi 68 ikiwa ni posho ya ya kazi maalum ya wiki tatu.

Aidha, Aprili 30 mwaka huu zililipwa sh. milioni 43.9 kwa ajili ya kuandaa  mpango wa kuhifadhi mazingira na siku hiyo hiyo zililipwa sh  miloni 14.4 kwa ajili ya siku ya wanawake. Fedha nyingine sh. Milioni 43 zililipwa siku hiyo na kufanya  jumla ya malipo yaliyolipwa siku hiyo kuwa shilingi mikioni101.8.

Amesema kuwa, mei 1 asubuhi mwaka huuzililipwa  sh. milioni 184.1 na mchana zililipwa sh  milioni 264 zikiwa ni malipo ya kazi maalum. "Sisi tulikuwa Mwanza tunasherehekea siku ya wafanyakazi duniani nyinyi hapa ndani mnalipana posho"

Aliongeza kuwa Mei 3 mwaka huu zililipwa sh. milioni146.5 kwa  watumishi 125 zikiwa ni malipo ya kuandaa Mpango Kazi wa Manunuzi kazi ambayo  ni sehemu ya majukumu yao ya jila siku.  Tarehe hiyohiyo zililipwa  sh. milioni 171.2 kwa ajili ya kuandaa nyaraka za Bunge.

Mheshiniwa Majaliwa  amesema sh. milioni155 zililipwa kwa baadhi ya watumishi zikiwa ni posho yakuandaa miongozo wakazi. " Yaani hii kazi ya ukaguzi ineliowa kwenye maeneo manne, huu ni utaratibu wa wa wapi? Mnazidi kutupunguzia imani,  na sijaongekea eneo la kuhamisha mafungu na utaratibu kuhamisha fedha  kisha mnakwenda kuzichukuwa huko mlikozihamishia."

Mheshimiwa Majaliwa amewataka watendaji wa Wizara hiyo kujenga uaminifu kwa wanaokusanya mapato kwa kufanya kazi kwa uaminifu na alitahadharisha kuwa watakaoendekea kuchen na pesa za umma hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Aidha, Waziri Mkuu aliwapongeza watendaji wengine wa wizara hiyo ambao wameendelea kufanya kazi kwa weledi “na nimesema hapa si wote wenzenu wachache wanatumia vibaya nafasi zao kutuchafua wizara ya fedha”

MWISHO.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,



Share:

HEALTH SECRETARY II at Ministry Of Health (MOH)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST HEALTH SECRETARY II – 1 POST POST CATEGORY(S) HEALTHCARE AND PHARMACEUTICAL EMPLOYER Ministry Of Health (MOH) APPLICATION TIMELINE: 2021-05-27 2021-06-09 JOB SUMMARY NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To provide advice on health management services at the NPHL; ii. To assist in supervising resources for management of health services; iii. To participate in preparation of […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

LABORATORY SCIENTIST GRADE II – 18 POST at Ministry Of Health (MOH)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST LABORATORY SCIENTIST GRADE II – 18 POST POST CATEGORY(S) HEALTHCARE AND PHARMACEUTICAL EMPLOYER Ministry Of Health (MOH) APPLICATION TIMELINE: 2021-05-27 2021-06-09 JOB SUMMARY NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To perform specialized laboratory tests; ii. To implement the quality management system; iii. To train junior members of staff on matters related to Laboratory tests; iv. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Veterinarian at FAO

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

FAO seeks gender, geographical and linguistic diversity in its staff and international consultants in order to best serve FAO Members in all regions. FAO is committed to achieving workforce diversity in terms of gender, nationality, background, and culture Qualified female applicants, qualified nationals of non-and under-represented member nations, and person with disabilities are encouraged to apply Everyone […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Animal Production Specialist at FAO

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

FAO seeks gender, geographical and linguistic diversity in its staff and international consultants in order to best serve FAO Members in all regions. FAO is committed to achieving workforce diversity in terms of gender, nationality, background, and culture Qualified female applicants, qualified nationals of non-and under-represented member nations, and person with disabilities are encouraged to apply Everyone […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

40 Job Opportunities At Tunduma Town Council

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Tunduma Town Council is a town in Songwe Region, Tanzania, on the border between Tanzania and Zambia It is also the junction for the tarmac road which runs via Sumbawanga through the remote far-western districts of Tanzania to Kasulu and Kibondo in the north-west. According to the 2012 census, it has a population of 97,562. Tunduma […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Mtendaji Wa Kijiji III At Newala Town Council

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Newala town council is the major town on the Makonde Plateau. Thanks to its perch at 780m altitude, it offers a pleasantly brisk climate, and views over the Ruvuma River valley and into Mozambique. There are numerous paths from the edge of town leading down to the river. Job Opportunities At Newala Town Council Newala […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Thursday, 27 May 2021

NACTE online Application for 2021/2022 is now open – Apply Now

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The National Council for Technical Education (NACTE)  Student’s Admission Verification System for Certificate and Diploma Applicants  and online application system is now open for the 2021/2022 Admission Cycle  The Nacte online application System allows you to apply for Admission into Certificate and Diploma programmes for academic year 2022/2022. Currently Available Application Categories:- Health and Allied Sciences […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Rais Samia akutana na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Sylvain Ore, Ikulu Jijini Dar es Salaam.



Share:

POLISI SHINYANGA WAKAMATA MATAPELI WANAOGHUSHI NYARAKA, KUTONGOZA NA KUIBIA WANAWAKE

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linawashikilia watuhumiwa watatu  Dismond Zacharia  (33) ambaye ni mwalimu, Feisal Hussein  (27) Mpemba, mtaalamu teknolojia ya mawasiliano, Juma Almas (35) Mfanyabiashara baada ya kuwakamata wakiwa na nyaraka mbalimbali za kughushi kwa lengo la kutapeli Wananchi. 

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Mjini Kahama, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema  watuhumiwa hao walikamatwa Mei 26, 2021 majira ya saa 07:00 asubuhi huko maeneo ya Namanga Manispaa ya Kahama.

Amesema watuhumiwa hao wamekamatwa kufuatia msako mkali unaoendelea kufanywa na Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga wa kupambana na uhalifu na wahalifu.

"Baada ya watu hao kukamatwa na kufanyiwa upekuzi walikutwa na vitambulisho viwili vya Jeshi la wananchi (JWTZ), kitambulisho cha Idara ya Usalama wa Taifa (TISS),  Mhuri mmoja wa Jeshi la Wananchi Tanzania pamoja na nyaraka mbalimbali za Jeshi hilo. Orodha ya nyaraka hizo ni barua za utambulisho kwenye mabenki, ripoti za Jeshi la Wananchi, fomu za kusafirishia mizigo ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)",amesema Kamanda Magiligimba. 

Kamanda Magiligimba amesema watuhumiwa hao wanatumia mbinu mbalimbali kufanya utapeli huo kama vile kufika kwa watoa  huduma za kifedha mikoa mbalimbali kwa kutumia magari (T.677 BMA Toyota  Carina namba  T.110 DSX Toyota RUMION) na kuulizia ofisi za viongozi wa Serikali na pindi wanapoonyeshwa hushusha begi linalosadikiwa kuwa na fedha na kuliacha kwa wakala aliyewekeza ili hali begi hilo likiwa na makaratasi yaliyokatwa mithili ya fedha na kuweka fedha juu na chini ya vibunda vya makaratasi hayo.

 "Na baada ya muda hurudi na kufungua begi na kutoa shukrani kuwa fedha wamezikuta salama na baada ya hapo huja tena baada siku moja na kuacha tena begi na kuelekea kwenye hizo ofisi tena na huomba kurushiwa fedha kuanzia Tshs.500,000/= na kwamba watazirudisha watakapokuja kuchukua begi na huzirejesha na kuchukua begi,  baada ya hapo huja tena na kuacha begi na kuomba kutumiwa fedha  kuanzia milioni moja 1,000,000/= na kuendelea na kuahidi kuzirejesha watakapoijia begi pindi wakirushiwa pesa hizo hutokomea na mtoa huduma anapofungua begi hukuta ni makaratasi na simu zao zinakuwa zimezimwa",ameeleza.

"Mbinu nyingine wanayotumia ni kutongoza wanawake na kuwanywesha Pombe kisha kuwaibia fedha na simu zao pamoja na vitu vya thamani",ameongeza.

Amesema watuhumiwa hao pia hujitambulisha kuwa wao ni maofisa wa Serikali kutoka Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na kuwaahidi kuwapatia ajira.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga anatoa wito kwa Wananchi kuwa makini na mtandao huo wa matapeli na yeyote mwenye taarifa za matapeli wa aina hiyo au aina yeyote ile anaombwa kuzifikisha haraka katika kituo cha Polisi kilicho karibu ili waweze kushughulikiwa haraka kabla hawajaleta madhara kwa jamii.

Pia anasisitiza Wananchi wachache wenye tabia kama hizo za utapeli kuacha mara moja na wafanye kazi halali ili wajipatie kipato halali kwa ustawi wa Mkoa wetu na Taifa kwa ujumla.


Share:

MHE.CHAMUHIRO ATEMBELEA BANDA LA BRELA KATIKA MAONESHO YA WADAU WA SEKTA YA UJENZI

 

Waziri wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Mhandisi Leonard Chamuhiro, akipatiwa maelezo na maafisa wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), alipotembelea banda hilo mapema leo, baada ya ufunguzi wa maonesho ya Wadau wa Sekta ya Ujenzi, yanayofanyika leo na kesho katika viwanja vya Diamond Jubilee, Dar es Salaam. Maafisa wa BRELA kutoka kushoto ni Afisa Usajili Bw. Englibert Barnabas, Msaidizi wa Usajili Bi. Yvonne Massele na Afisa Leseni Bi. Saada Kilabula.

Maafisa wa BRELA wakitoa elimu na huduma kwa watembeleaji wa Maonesho ya Wadau wa Sekta ya Ujenzi yanayofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

Afisa Leseni wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Saada Kilabula ( aliyesimama kushoto) akitoa maelekezo ya huduma zitolewazo na BRELA kwa Msanifu majengo Bw. E.Nnunduma, katika maonesho ya Wadau wa Sekta ya Ujenzi, yanayofanyika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, tarehe 27 -28 Mei, 2021.

Afisa Usajili kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bw. Englibert Barnabas (kulia), akitoa ufafanuzi wa huduma zitolewazo na BRELA kwa mteja kutoka Kampuni ya Agrovision Limited Bw. Arfaan Ahmed Alwani, alipotembelea banda la BRELA, katika maonesho ya wadau wa Sekta ya Ujenzi, yanayofanyika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

Share:

WATOA HUDUMA ZA AFYA, WADAU WATAKIWA KUZINGATIA USAHIHI WA VIPIMO

Meneja wa Kanda Nyanda za juu kusini Bw.Abel Mwakasonda akizungumza na washiriki wa semina ya Umuhimu wa Vipimo katika sekta ya afya iliyofanyika katika ukumbi wa Dk. Shein Jijini Mbeya. Mwakasonda alisema TBS kwa kushirikiana na taasisi zingine zenye dhamana ya kushughulika na vipimo zimejipanga kuhakikisha kila mtoa huduma katika sekta ya afya anapata uwezo wa kutoa huduma kwa kuzingatia vipimo sahihi.

 ****
Watoa huduma katika sekta ya afya na wadau wote kila mmoja kwa nafasi yake wametakiwa kuchukua hatua stahiki kwa pamoja kuhakikisha wanalinda afya za Watanzania kwa kuzingatia upimaji sahihi, kufuata miongozo na viwango vya kitaifa na kimataifa.

Wito huo umetolewa leo Mei 27 2021 na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya, Mwajabu Nyamkomora, katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa lengo la kutoa uelewa kwenye masuala ya Sayansi ya Vipimo hususani katika sekta ya afya kwa wadau. 

Semina hiyo ni sehemu ya mwendelezo wa maadhimisho ya Siku ya Vipimo Duniani yaliyofanyika Mei 20, mwaka huu kitaifa mkoani Dodoma, kauli mbiu ikiwa na ujumbe usemao; "Umuhimu wa Vipimo Katika Sekta ya Afya." 

Nyamkomora alisema vipimo ni huduma muhimu sana katika utoaji wa huduma za afya na uzalishaji wa dawa katika viwanda vyetu, kwani Taifa ambalo watu wake hawana afya, haliwezi kuzalisha.

Aliongeza pia ni muhimu watoa huduma za afya, madaktari, wauguzi na watu wa maabara, watoe huduma kwa kuzingatia viwango, miongozo ya Serikali, weledi, kujituma na kufanya kazi kwa bidii na kwa kukumbuka viapo vyao.

"Lakini pia tutambue kuwa uhai na ustawi wa taifa letu upo katika mikono yenu (watumishi wa afya) hivyo wafanye kazi kwa bidii," alisema Nyamkomora.

Mgeni huyo rasmi, Nyamkomora aliwataka watoa huduma katika sekta ya afya kujitathmini kama wanatoa huduma ya vipimo inayokidhi viwango. 

"Tujikague kwa kujiuliza maswali. Je, una elimu, ujuzi na maarifa ya kutosha kutumia vifaa unavyotumia katika upimaji, je, hali ya vifaa unavyovitumia inaruhusu kufanya vipimo? Je, tunafuata ushauri wa kitaalamu kuhusu matumizi, utunzaji, matengenzo ya muda na yale ya baada ya hitilafu kwa vifaa tunavyotumia?" Alihoji, Nyamkomora na kuongeza;

"Mtoa huduma anatakiwa kujiuliza kama kifaa chako kimehakikiwa kwa usahihi wake wa kutoa majibu sahihi?  Je, umefanya ugezi (Calibration) kwenye vifaa vyako? 

Unatumia cheti cha ugezi kutoka kwa aliyekupa huduma hiyo? je,aliyekupa huduma ya ugezi ana weledi wa kazi anayofanya na je mfumo wa kuhakiki majibu yanayotoka ni sahihi?"

Alisema ni muhimu kila mmoja kwa nafasi yake akachukua hatua stahiki ili wote kwa pamoja tuhakikishe wanalinda afya za Watanzania kwa kuzingatia upimaji sahihi, kufuata miongozo na viwango vya kitaifa na kimataifa.

Alisema ni matumaini yake kuwa baada ya semina hiyo kila mmoja kwa nafasi yake atachukua hatua stahiki ili wote kwa pamoja tuhakikishe tunalinda afya za Watanzania.

Kwa upande wa Meneja wa TBS Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Abel Mwakasonda, alisema vifaa vinavyotumika katika uchunguzi wa afya vina mchango mkubwa katika kuhakikisha ugonjwa ambao mtu anaugua.

Aliwataka wamiliki na waendeshaji wa hospitali, maabara za afya, viwanda vya kuzalisha dawa na taasisi zinazosimamia sekta ya afya kutambua kuwa huduma bora za afya zinawezekana tukizingatia ubora wa vipimo vyetu.

Alisema mtoa huduma katika sekta ya afya anapata uwezo wa kutoa huduma kwa kuzingatia vipimo sahihi.

"Vipimo sahihi ni huduma muhimu sana katika utoaji wa huduma bora za afya, nawashauri wamiliki wa viwanda, hospitali, vituo vya afya, maabara za uchunguzi na watoa huduma wote wa sekta ya afya mtumie vipimo sahihi kwa wakati sahihi na kupata huduma ya ugezi wa vifaa (mashine zinazotumika kupimia ama kutunzia sampuli zenu kutoka katika Taasisi zinazofanya vipimo kwa usahihi ili muweze kutoa huduma bora kwa Watanzania," alisema Mwakasonda na kuongeza;

"Vipimo sahihi ni kiwezeshi cha utoaji wa huduma bora na salama. IIi kuenzi siku ya Vipimo Duniani."

Kwa upande wa Mkuu wa maabara ya ugezi Bw. James Mahilla alisema TBS kupitia Maabara ya Vipimo (Metrolojia) ndiyo watunzaji wa Viwango vya Taifa vya Vipimo.
Mkuu wa Maabara ya Ugezi Bw.James Mahilla akizungumza na washiriki  wa semina ya umuhimu wa vipimo katika sekta ya afya iliyofanyika katika ukumbi wa Dk. Shein jijini Mbeya.
Mahilla alisema ili kuenzi siku ya vipimo duniani,TBS imeandaa semina kwa lengo la kutoa uelewa kwenye masuala ya sayansi ya Vipimo hususani katika sekta ya Afya

Kaimu Katibu tawala wa Mkoa wa Mbeya Bi. Mwajabu Nyamkomora akifungua semina ya umuhimu wa vipimo katika sekta ya afya iliyofanyika katika ukumbi wa Dr. Shein jijini Mbeya mapema leo.
Nyamkomora alitoa wito kwa watoa huduma za afya,madaktari,wauguzi na watu wa maabara  kulinda afya za Watanzania kwa kuzingatia upimaji sahihi, kufuata miongozo pamoja na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Baadhi ya washiriki wa semina ya Umuhimu wa Vipimo Katika Sekta ya Afya iliyofanyika mapema leo katika ukumbi wa Dr.Shein jijini Mbeya

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger