Wednesday, 27 January 2021

RAIS MAGUFULI ATOA MSIMAMO CHANJO YA CORONA...."SITEGEMEI KUTANGAZA KUJIFUNGIA NDANI"


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Butengo Chato mkoani Geita kabla ya kuzindua Shamba kubwa la Miti lenye jumla ya ekari elfu 69 mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.
**
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amewatahadhalisha kuhusu chanjo ya COVID 19 inayoendelea katika mataifa mbalimbali na kuwasisitiza kusimama imara huku akisisitiza kuwa hategemei hata siku moja kuwatangazia wananchi wajifungie ndani kwa sababu ya Ugonjwa wa Corona.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jumatano January 27,2021 wakati azindua shamba la miti la Silayo mkoani Geita.

"Mtatishwa sana ndugu zangu Watanzania lakini simameni imara, najua wapo baadhi ya watanzania hata wameondoka ndani ya nchi na kukimbilia maeneo mengine na kwenda kuchanjwa na walikochanjwa huko wamekuja huku wametuletea corona ambayo ni ya ajabu ajabu simameni imara.”

“Chanjo hazifai kama Wazungu wangekuwa na uwezo wa kuleta chanjo, hata chanjo ya Ukimwi ingekuwa imeshaletwa, chanjo ya kifua kikuu ingekuwa kifua ingeshaondoka, hata chanjo ya malaria ingekuwa ishapatikana hata chanjo ya kansa ingekuwa imeshapatikana, lazima watanzania tuwe waangalifu kwa mambo ya kuletewa letewa,” amesema Rais Magufuli.

“Sisi Watanzania hatujajifungia ndani na hatutegemei kujifungia ndani, na wala sitegemei kutangaza hata siku moja kwamba tunajifungia ndani kwa sababu Mungu wetu yupo hai na ataendelea kutulinda Watanzania. Tutaendelea kuchukua tahadhali nyingine za kiafya ikiwa pamoja na kujifukizia, unajifukizia huku unamuomba Mungu unasali..., sali huku unapiga zoezi la kulima mahindi, viazi ili ule vizuri ushibe. Corona ashindwe kuingia katika mwili wako,” ameongeza Rais Magufuli.
Share:

TAKUKURU SINGIDA YAOKOA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 270

 

Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Singida, Adili Elinipenda (katikati) akitoa taarifa ya utekelezaji kwa kipindi cha miezi mitatu Oktoba hadi Disemba 2020.

 Na Dotto Mwaibale, Singida

TAASISI ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Singida imeokoa zaidi ya shilingi 270.7 kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo mikopo umiza.

Akitoa taarifa ya utekelezaji kwa kipindi cha miezi mitatu Oktoba hadi Disemba 2020 Mkuu wa Taasisi hiyo Mkoani hapa Adili Elinipenda alisema Takukuru imeokoa shilingi milioni 270,079,600 ndani ya kipindi hicho kutoka maeneo mbalimbali.

Elinipenda alisema shilingi milioni 154,416,000 pekee zimeokolewa kutoka mikopo umiza, shilingi milioni 28,000,000 ziliokolewa kutokana na fidia ya maeneo ya wananchi yaliyotwaliwa kufanya shughuli za uchimbaji madini Wilayani Mkalama,wakati kiasi kingine kikiokolewa kutoka maeneo mengine ikiwemo mahakama ya Manyoni.

"Fedha hizi tulizikabidhi kwa wahusika baada ya kuokolewa ambapo fedha tulizoziokoa kutoka mikopo umiza, Mkuu wa Mkoa Dk Nchimbi aliwakabidhi wananchi hao wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani Manispaa ya Singida." alisema Elinipenda.

Alisema katika kuhakikisha Vitendo vya Rushwa vinaisha Takukuru kwa kushirikiana na wadau wengine imeendelea kutoa Elimu kwa jamii kwa kushirikisha makundi mbalimbali ikiwemo Vijana wa shule za msingi, Sekondari na Vyuo.

Aidha Elinipenda alisema Taasisi hiyo imeanzisha utaratibu wa Takukuru inayotembea (MOBILE PCCB) ambapo itatenga siku moja ndani ya mwezi ili kuwatembelea wananchi kwenye maeneo yao lengo la kufanya hivyo ni kusikiliza na kutatua kero zao.

Hata hivyo Taasisi hiyo inazidi kutoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Singida kujiepusha na Vitendo vya Rushwa huku ikiwataka kushiriki kikamilifu katika kutoa taarifa za Vitendo hivyo pamoja na kutoa ushirikiano kwenye uchunguzi na kutoa ushahidi mahakamani

Share:

WATOTO WAFARIKI KWA KUANGUKIWA UKUTA MVUA IKINYESHA GEITA

Eneo la ukuta wa nyumba walio kuwemo watoto tisa wa familia moja ambao wawili kati yao walipoteza maisha baada ya kuangukiwa na ukuta wa nyumba yao.

***
Watoto wawili wa familia moja wamefariki dunia baada ya kuangukiwa na ukuta wa nyumba chanzo kikitajwa kuwa ni mvua inayoambatana na upepo iliyonyesha wilayani Geita juzi Jumapili Januari 24, 2021.

Waliofariki ni Asheri Malima(4) na Laurencia Malima (2) waliokuwa wakiishi kijiji cha Kasesa kata ya Kaseme.

Baba wa watoto hao, Malima Kengere amesema aliwaacha wanae tisa nyumbani na kwenda kuuza mahindi ya kuchoma lakini mmoja wa watoto wake alimfuata na kumueleza kuwa nyumba yao imeanguka. Amesema wakati ukuta ukianguka watoto hao walikuwa wenyewe nyumbani.

“Walipoona ukuta unaanguka walikimbia lakini hawa wawili walikuwa wadogo hawakuweza, walifukiwa na kifusi,” amesema akibainisha kuwa siku hiyo mvua ilinyesha kuanzia saa nane mchana hadi saa 10 jioni.

Kamanda wa polisi mkoani Geita, Hendry Mwaibabe amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wazazi kuwa waangalifu hasa nyakati za mvua ili kuepuka majanga yanayoweza kuzuilika.

CHANZO- MWANANCHI

Share:

DC AGEUKA MBOGO WAFANYAKAZI MGODI WA DHAHABU MAHIGA - MWAKITOLYO KUNYANYASWA NA WAWEKEZAJI

 

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akizungumza na wafanyakazi wa Mgodi wa madini ya Dhahabu (ZEMD) uliopo Mahinga- Mwakitolyo wilayani humo, unaomilikiwa na Raia wa China, wakati akisikiliza na kutatua kero zao.

Na Marco Maduhu, Shinyanga. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, amefanya ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wafanyakazi katika mgodi wa madini ya Dhahabu (ZEMD) uliopo Mahiga Kata ya Mwakitolyo wilayani humo, ambao unamilikiwa na Raia wa China.

Ziara hiyo imefanyika Januari 26,2021 ambapo mkuu huyo wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, aliambatana na kamati ya ulinzi na usalama wilaya, wataalamu wa madini, Afisa kazi, wakala wa usalama na afya mahala pa kazi OSHA pamoja na Afisa kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC). 

Akizungumza mara baada ya kusikiliza malalamiko ya wafanyakazi wa mgodi huo, Mboneko amesikitishwa na manyanyaso ambayo wanafanyiwa na waajiri wao, likiwemo suala la kutothaminiwa uhai wao, kutumikishwa muda mrefu bila ya kupewa chakula, mikataba mibovu, kutopewa vifaa kinga, pamoja na kufukuzwa hovyo bila ya utaratibu hasa pale wanapoumia. 

Aidha akitoa maagizo kwa uongozi wa mgodi huo, amewataka wabadili mienendo yao na kuacha kunyanyasa wafanyakazi wao, bali wafuate sheria za nchi, ajira, masuala ya usalama na afya kazini, utunzaji wa mazingira, pamoja na kuacha kuwapiga na kuwatolea lugha za matusi. 

"Serikali tunahitaji sana wawekezaji, lakini mfuate sheria za nchi na taratibu zote zilizowekwa, na siyo kunyanyasa wafanyakazi ambao ni Watanzania, na leo nimekuja ili kuwekana sawa,kwa sababu kama hakuna amani kwenye mgodi huu, basi haina haja ya nyie wawekezaji kuwepo hapa," amesema Mboneko. 

"Nafahamu Tanzania na nchi ya China sisi ni marafiki, lakini nyie mnachokifanya hapa kwa wafanyakazi wenu si sahihi kabisa. Fanyeni kazi katika mazingira rafiki, ili na hawa watumishi wenu licha ya kupata ajira nao wafurahie kazi yao na siyo kuwanyanyasa," ameongeza. 

Pia ametoa mwezi mmoja kwa uongozi wa mgodi huo, mapungufu yote ambayo yamejitokeza wayafanyie kazi, pamoja na Wakala wa usalama na afya kazini OSHA, na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), watembelee kumaliza changamoto zote mgodini hapo, ili kuhakikisha usalama wa wafanyakazi una kuwapo. 

Katika hatua nyingine aliutaka mgodi huo kuajiri mtu ambaye atakuwa akisikiliza kero za wafanyakazi, meneja rasilimali watu (HR), na kisha kuziwasilisha kwa viongozi wa mgodi na kutafutiwa ufumbuzi, kuliko hivi sasa wanaisha bila ya kuwapo kwa mtumishi huyo wa kuwasemea shida zao. 

Nao baadhi ya wafanyakazi wa mgodi huo, awali wakiwasilisha kero zao kwa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, wamesema kwenye mgodi huo hawana mikataba ya ajira ambayo ni halali, na wamekuwa wakisainishwa bila ya kuusoma na wala hawajui kiwango cha mshahara. 

Aidha wamesema wamekuwa wakikatwa makato ya NSSF, pamoja na Kodi inayofahamika Magufuli, bila ya kupewa risiti, na wala kutokuwa na namba ya makato ya NSSF, huku wakikatwa kiwango cha fedha kisichokuwa na kiwango sahihi. 

Pia walilalamikia suala la usalama kazini ,ambapo wanafanya kazi bila ya kupewa vifaa kinga, pamoja na kulazimishwa kufanya kazi kwenye maeneo ambayo yana moshi wa sumu (blasting), na wakigoma kufanya kazi hadi moshi huishe hutishiwa kufukuzwa kazi ama kufukuzwa kabisa. 

Mmoja wa wafanyakazi hao Yohana Daudi, amesema Wachina wamekuwa wakilipua miamba(blasting) kipindi wao wapo chini ya shimo, ambapo moshi wa sumu huwa unawazidi, na kusababisha baadhi yao kuzimia, na wanapotoka nje hufokewa na kulazimishwa warudi tena shimoni. 

"Juzi tu kidogo watu tufe kwa kosa hewa, mara baada ya Wachina kulipua miamba( blasting) ambapo Moshi wenye sumu ulituzidi na wenzangu wawili waliishiwa nguvu na kuzimia, ikabidi niwapandishe kwenye vibelenge kinyume na utaratibu ndipo tukatoka nje, lakini ukiwazuia wasifanye hivyo sisi tunapokuwa chini hawaelewi," amesema Daudi. 

Naye Teddy Malima ,ambaye ni mtaalamu wa kutengeneza Baruti, alilalamikia suala la kutopewa vifaa kinga ,zikiwamo groves, pamoja na Masks, huku pia wakiwa wanapewa kazi zingine ambazo siyo taaluma zao. 

Kwa upande wake Kaimu meneja wakala wa usalama na afya mahali pa kazi (OSHA) Kanda ya ziwa Mhandisi Mjawa Shenduli, amesema awali walishatoa maelekezo kwenye mgodi huo juu ya kufuata sheria za usalama na afya, lakini bado hawazingatii, na kubainisha hatua inayofuata ni kuwapiga faini. 

Aidha Meneja msaidizi wa mgodi huo wa (ZEMD) Zhao Chao, amesema watarekebisha makosa yote ambayo wamepewa maelekezo na Serikali, ili kuhakikisha changamoto zote zinatatuliwa, na wafanyakazi wao kufanya kazi kwa Uhuru na kupata stahiki zao kwa mujibu wa sheria, ikiwamo na mikataba halali inayoonyesha kiwango cha mishahara yao.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akizungumza na wafanyakazi wa Mgodi wa madini ya Dhahabu (ZEMD) uliopo Mahinga- Mwakitolyo wilayani humo, wakati akisikiliza na kutatua kero zao.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akiendelea kutoa maelekezo ya Serikali, wakati akitatua kero za wafanyakazi kwenye Mgodi wa dhahabu (ZEMD)uliopo Mahiga Kata ya Mwakitolyo wilayani humo, ambao unamilikiwa na Raia wa China.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akiendelea kusisitiza jambo kwenye kikao hicho.
Afisa kazi mkoani Shinyanga Revocatus Mabula, akitoa maelezo namna ya kuajiri wafanyakazi na kupata stahiki zao.
Kaimu meneja wakala wa usalama na afya mahali pa kazi (OSHA) Kanda ya ziwa Mhandisi Mjawa Shenduli, akielezea jinsi maelekezo ya usalama na afya ambayo walishayatoa awali kwenye mgodi huo.
Mhandisi Mchenjuaji kutoka Ofisi ya madini mkoani Shinyanga Camilius Seneda, akizungumza kwenye kikao hicho cha utatuzi wa kero za wafanyakazi wa mgodi wa ZEMD.
Afisa kutoka ofisi ya uhamiaji mkoani Shinyanga Godson Mwanawima, akizungumza kwenye kikao hicho cha utatuzi wa kero za wafanyakazi katika Mgodi wa ZEMD.
Awali katibu tawala wilaya ya Shinyanga Boniphace Chambi, akifungua kikao hicho cha utatuzi wa kero za wafanyakazi katika mgodi wa ZEMD.
Mfanyakazi wa Mgodi wa ZEMD Philibert Elisha akitoa kero kwenye kikao hicho.
Mfanyakazi wa Mgodi wa ZEMD Juma Gambaliko, akitoa kero kwenye kikao hicho.
Mfanyakazi wa Mgodi wa ZEMD Yohana Daudi, akitoa kero kwenye kikao hicho.
Mfanyakazi wa Mgodi wa ZEMD Teddy Malima akitoa kero kwenye kikao hicho.
Meneja msaidizi wa mgodi huo wa (ZEMD) Zhao Chao, akitoa majibu ya utekelezaji wa maagizo ya Serikali kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko.
Watumishi wa Mgodi wa ZEMD wakiwa kwenye kikao cha usikilizwaji wa kero zao na kutafutiwa ufumbuzi.
Watumishi wa Mgodi wa ZEMD wakiwa kwenye kikao cha usikilizwaji wa kero zao na kutafutiwa ufumbuzi.

Watumishi wa Mgodi wa ZEMD wakiwa kwenye kikao cha usikilizwaji wa kero zao na kutafutiwa ufumbuzi.
Kikao cha usikilizwaji wa kero na utatuzi kikiendelea.
Kikao cha usikilizwaji wa kero na utatuzi kikiendelea.
Kikao cha usikilizwaji wa kero na utatuzi kikiendelea.
Kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Shinyanga ikiwa kwenye kikao hicho.
Awali mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akiwasili kwenye Mgodi wa ZEMD kwa ajili ya kusikiliza kero za wafanyakazi wa Mgodi huo na kuzitafutia ufumbuzi. akimpokea na Meneja Msaidizi wa mgodi huo Zhao Chao.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, mara baada ya kumaliza kusikiliza kero za wafanyakazi wa Mgodi wa ZEMD na kuzitafutia ufumbuzi, alikwenda pia kuangalia ujenzi wa kituo cha Polisi Mwakitolyo.

Na Marco Maduhu- Shinyanga.

Share:

WAITARA AMTAKA DED TARIME KULIPA DENI LA MIL.185 LINALODAIWA NA MSD NA KUSABABISHA KUTOPATIWA DAWA


Mbunge wa jimbo la Tarime vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akizungumza na wagonjwa waliofika katika kituo cha afya Nyangoto wakati wa ziara yake ya kutembelea kituo kubaini changamoto. Picha na Dinna Maningo.
Mbunge wa jimbo la Tarime vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara akizungumza na wagonjwa waliofika katika kituo cha afya Nyangoto wakati wa ziara yake ya kutembelea kituo kubaini changamoto. Picha na Dinna Maningo.
Veronica Tontora mwenyekiti wa kitongoji cha Lamboni akionyesha eneo ambao limetelekezwa kwa zaidi ya mwaka mmoja ambalo lilikuwa linatumika wagonjwa na wanaojifungua kufua nguo zao lakini halitumiki kwa madai limeziba.
Katibu wa Chama cha Mapinduzi(CCM) wilaya ya Tarime mkoani Mara Hamis Mkaruka akitizama eneo hilo.

Na Dinna Maningo,Tarime.
Hali ya upatikanaji wa dawa kwenye zahanati na vituo vya afya katika halmashauri ya wilaya ya Tarime imekuwa gumzo kila kona jambo ambalo limekuwa kero kwa wananchi wanapokwenda kupata huduma ya afya baadhi ushindwa kumudu gharama za dawa kwenye maduka binafsi ya dawa kutokana na kuwa na gharama kubwa.

Kufuatia uhaba huo wa dawa mbunge wa jimbo la Tarime vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Muungano na Mazingira Mwita Waitara amemtaka mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Tarime Apoo Tindwa kuhakikisha halmashauri inalipa deni la shilingi mil.185 inayodaiwa na Bohari ya dawa (MSD) ili kunusuru afya za wananchi wanaopata huduma za afya katika zahanati na vituo vya Serikali.

Waitara aliyasema hayo wakati alipokitembelea kituo cha afya Nyangoto- ili kujionea huduma zinazotolewa baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi wake kuhusu kituo hicho kukabiliwa na changamoto zikiwemo za ukosefu wadawa,gharama za kitandani, gharama za mgonjwa afikishwapo kituoni hapo, wanaojifungua kwenda na nguo kufua nyumbani,gharama za vipimo,ukosefu wa gari la wagonjwa.

Wakieleza kero zilizopo, Diwani wa viti maalumu Ferister Julius alisema kuwa kituo hicho hakina dawa na baadhi ya vifaa tiba na kila anaopofatilia kujua sababu ya kutokuwepo kwa dawa uelezwa kuwa hakuna dawa kwakuwa kituo hicho kina deni la dawa.

"Hali ya huduma kwenye kituo ni mbaya kila kitu ni chakununua ,nilileta mgonjwa hata karatasi za kuandikia hakuna nikaambiwa nikanunue daftari,ukileta mgonjwa unalipia sh.5,000/= , kitanda 5,000/= kila kipimo unalipia sh.2,000/= bado unaambiwa ununue dawa,bado mabomba ya sindano,gloves hii ni kero wagonjwa wanapata tabu nilipofuatilia kwa DMO nikaambiwa kuwa kituo kina deni la dawa ndiyo maana hakuna dawa japo sikufahamu ni deni la shilingi ngapi",alisema.

Diwani wa viti maalumu Elizabeth Marembera alisema kuwa ukosefu wa dawa umesababisha wananchi kugoma kujiunga na mfuko wa afya ya jamii ICHF na na mfuko wa bila ya afya NHIF kwakuwa hata walio na bima ujigharamikia dawa kwa fedha zao hali ambayo imesababisha wananchi kutoshawishika kujiunga.

Diwani wa kata ya Kemambo Rashid Bogomba aliongeza, "Kuna hospitali zingine ukienda huna bima wanakushangaa lakini ukiwa na bima wanakujali kama mfalme shida ya hapa wao wanajali watu wanaotoa fedha kuliko watu wenye bima".

Diwani wa kata ya Matongo Godfrey Kegoye alisema kuwa huduma ya afya ni hafifu ambapo wodi ya wanawake ina upungufu wa vitanda na kusababisha wagonjwa wawili kuchangia kitanda kimoja na wakiwa wengi wengine ulala chini hali inayosababisha watu kukikimbia kituo hicho cha serikali nakwenda kupata huduma kwenye zahanati na vituo binafsi.

Licha ya kuwepo kwa gari lililoandikwa kituo cha afya Nyangoto lakini limekuwa halikai muda wote kituoni, mgonjwa akipewa rufaa ndugu hulazimika kutumia usafiri wa gari za kukodi na wasio na fedha hupoteza maisha.

Wambura Machugu Mwenyekiti wa kitongoji cha Kebamonche na mjumbe wa kamati ya afya na mazingira kijiji cha Mjini Kati alisema kuwa kukosekana kwa gari la wagonjwa baadhi ya wagonjwa wanaopata rufaa kwenda hospitali ya wilaya,mkoa na Bugando hufariki kwa kuwa wengine wanashindwa kumudu gharama za usafiri.

“Juzi kuna mgonjwa alilazwa hapa kituoni alikaa siku mbili hali yake ilikuwa mbaya ikatakiwa asafirishwe kwenda mkoani lakini hapakuwa na gari hali ikawa mbaya akafia hapa kituoni,na hapa sasa hivi hakuna damu ukiishiwa damu unaambiwa uende hospitali ya wilaya au mkoani, hii inaumiza kituo kikubwa kama hiki kina gari lakini gari linakwenda kufanya kazi kwingine nawakati lililetwa kwa matumizi ya kituo hiki", alisema.

Mjumbe wa serikali ya kijiji cha Mjini Kati ambaye pia ni Mwenyekiti wa umoja wa wanawake Tanzania (UWT) kata ya Matongo Pendo Mnata alisema kuwa baadhi ya watoa huduma wakiwemo wauguzi wamekuwa na kauli mbaya kwa wagonjwa wakiwafoka na wakati mwingine kupuuza shida zao,aliwataka kuzingatia maadili ya kazi zao na kuwa na lugha rafiki kwa wagonjwa.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Lamboni Veronica Tontora alisema"akina mama wakijifungua unaambiwa uondoke na nguo ukafulie nyumbani kuna mmoja alinieleza kuwa alipojifungua aliambiwa aondoke na kondo na nguo akafulie kwake,hakuna sehemu ya kufua nguo unapokuwa umejifungua hata wagonjwa wengine wanateseka tunaomba huduma ziboreshwe".

Mwenyekiti wa kamati ya Afya kituo cha afya Nyangoto,Isaack Zabroni alisema eneo lililotengwa kwa ajili ya kufua nguo za wanojifungua na wagonjwa lina mwaka mmoja halitumiki hivyo watu ulazimika kufua katika bafu zilizopo kituo cha afya pindi wanapooga na kwamba hakuna akina mama wanaokwenda kufua nguo nyumbani kwa kuwa hufua kwenye bafu wakati wanapooga.

"Ni mwaka mmoja sinki halitumiki lilitengenezwa chini ya kiwango na kampuni ya Kemambo iliyokuwa na zabuni ya kufanya usafi kwenye kituo cha afya wakaweka tundu dogo likaziba ili lizibuiwe mpaka lichimbwe shimo ambao watu wakifua maji yanatiririka kwenda ndani ya shimo tofauti na hapo hata likizibuliwa litachukua muda mfupi na kuziba",alisema.

Akizungumzia ukosefu wa dawa aliongeza "MSD iliingia mkataba na serikali sasa inadaiwa fedha za dawa haijalipa na hata dawa zikija zile zenye umuhimu haziletwi hii inasababisha baadhi ya wauguzi kuja na dawa zao kwaaji ya kuwauzia wagonjwa kama kuwarahisishia wagonjwa wakiona nesi kamwambia kuwa hakuna dawa alafu anamwambia atoe pesa na kumuuzia anaona kama anauziwa dawa za serikali".

“Kuna baadhi ya wauguzi walikuwa wanakuja kituoni wakiwa na mabegi yenye dawa hii ilitupa wasiwasi kujua je kweli ni dawa zao binafsi au wanachukua za kituoni ilitubidi tuzuie hilo zoezi tukakataa hakuna nesi kumwelekeza mgonjwa duka la kununua dawa au muuguzi yeyote kuuza dawa na wengine walihamishwa”,alisema Zabroni.

Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya Nyangoto Dk. Josephat Kirambo alisema kuwa kituo hicho kimeanzishwa mwaka 1987,kwa mujibu wa sensa ya 2012 kituo kina hudumia wakazi 30,110 kutoka kata mbili ya Matongo na Kemambo zenye jumla ya vijiji nane.

Kirambo alisema kuwa mbali na huduma kwa vijiji hivyo inahudumia vijiji jirani vinne ambavyo ni Nyakunguru,Nyarwana,Nkerege,Weigita kata ya Kibasuka,kwa kata ya Nyarukoba ni Msege,Genkuru,Komarera,Nyabirongo na wilaya ya jirani ya Serengeti katika kijiji cha Nyiboko,Borega,Nyamitita,na Nyansurura kutoka wilayani Serengeti.

Mganga huyo alisema kuwa kituo hicho kina watoa huduma ya afya 38 ,kina changamoto ya upungufu wa dawa kituoni,upungufu wa watumishi, ukosefu wa duka la dawa la kituo na ICHF kuwa chini kwa kuwa na kaya 31 kwa kipindi cha miezi 6.

Akizungumzia juu ya wanaojifungua kuondoka na nguo kwenda kufua nyumbani alisema "Ile sehemu ya kufulia nguo maji machafu yaliziba watu walikuwa wanaweka nepi na vitambaa wanashindilia mle ndani ya tundu la kwenye sinki,tulielekeza namna ya kufanya usafi wakati tunaandaa sehemu nyingine na wakati mwingine nilikuwa nasimamia mimi mwenyewe lakini hawakuelewa.

“Tulielekeza kama unafua nguo za uzazi zenye damu nyingi kusanya zile damu pamoja ziwekwe kwenye shimo la pracenta lakini haikuwezekana,siamini kama mtu aliambiwa akafulie nyumbani kama yupo aliyewaambia kwakweli alifanya makosa tunaomba mtusamehe halitajirudia tena na sina taarifa ya mtu kuambiwa aondoke na kondo hakuna aliyenilalamikia”,alisema Mganga mfawidhi.

Akizungumzia suala la wagonjwa kutozwa sh.5,000/= ya kitanda,2,000/= za vipimo, 5,000/= kwa wagonjwa alisema :"Ni kweli wanachangia 5,000/= ya usajili wa mgonjwa,vipimo elfu 2,000 kila kipimo na 5,000/= ya kitanda huu ni utaratibu mpya tulioelekezwa baada ya kuwepo kwa upungufu wa dawa tulipewa maagizo na halmashauri na sisi ni kusimamia na malipo yote yanapitia kwenye mfumo”.

Alisema kuwa kituo hicho hakipati dawa kwa kuwa kilikuwa kinadaiwa deni milioni 82 na kituo kupitia mapato ya ndani kimelipa deni sh.mil.27 na kubaki na deni la mil.55 hali ambayo imesababisha kutokuwa na mahusiano mazuri na wagonjwa pale wanapokosa huduma ya dawa.

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Tarime Apoo Tindwa alisema kuwa upungufu wa dawa ni kwenye zahanati na vituo vyote vya afya ambapo halmashauri inadaiwa deni la dawa na MSD sh.mil.185 na wanajitahidi kuhakikisha deni linalipwa.

“Zahanati ya Kerende itapandishwa hadhi na kuwa kituo cha afya,zahanati ya Itandora inaelekea kukamilika na Genkuru ili kupunguza wimbi la wagonjwa kituo cha afya Nyangoto,tunachangamoto ya gari la wagonjwa kwenye vituo tuna gari moja la kituo cha Nyangoto linalolazimika kutoa huduma na kwenye vituo vingine”,alisema Tindwa.

Mbunge Waitara alimtaka mkurugenzi kuhakikisha yanafanyika mabadiliko makubwa ya usimamizi wa huduma ya afya kikiwemo kituo cha Nyangoto ili kuondoa malalamiko mengi ya wananchi ambao wengi wao wanaopata huduma kwenye vituo vya serikali ni watu wenye uwezo wa chini wa kipato.

Waitara alisema kuwa wananchi wasipopata huduma vizuri uisema vibaya serikali na chama jambo ambalo halimpendezi nakwamba kazi yake ni kuhakikisha anatatua kero za wananchi ili zinatafutiwa ufumbuzi.

Share:

RC NCHIMBI AAGIZA TAKUKURU KUWASAKA MAWAKILI NA MAHAKIMU UMIZA MITAANI “BUSH LAWYERS”

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 27,2021






























Share:

RAIS MAGUFULI KUZINDUA SHAMBA LA MITI LEO CHATO

Rais Dkt. John Magufuli Jumatano Januari 27, 2021 anatarajiwa kuzindua shamba la miti Chato lenye ukubwa na hekta elfu 69.

Shamba hilo la pili kwa ukubwa katika mashamba yanayomilikiwa na Serikali lipo wilayani Chato, mkoani Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel amewaambia waandishi wa habari mkoani humo kuwa Rais Magufuli atazindua shamba hilo mapema kesho.

Akielezea manufaaa ya shamba hilo, Mhandisi Gabriel amesema ni matunda ya jitihada za Serikali ya awamu ya tano ya kuhifadhi na kuinua uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali za misitu.

“Mradi huu mkubwa wa upandaji miti ambao Serikali imewekeza katika shamba hili unatarajiwa kutoa mchango mkubwa katika sekta mbalimbali hapa nchini,” amesema Mhandisi Gabriel.

Shughuli ya upandaji miti katika shamba hilo jipya la Chato ilianza mwaka 2018 na pia ni miongoni mwa mashamba 23 yanayosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).
Share:

Tuesday, 26 January 2021

Graphic Design Intern at Abel & Fernandes

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Graphic Design Intern   Abel & Fernandes Communications Dar es Salaam, Tanzania Abel & Fernandes is an integrated marketing agency specialising in a strategic hybrid of traditional PR, SEO, Social media and media-rich content. Based in Dar es Salaam, Tanzania Abel & Fernandes has over 20 years of collective experience working with some of the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Assistant Nursing Officer at Muhimbili Orthopaedic Institute

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Assistant Nursing Officer     TEMPORARY EMPLOYMENT OPPORTUNITIES BACKGROUND Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous institute established through an Act of parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing service in the fields of Orthopedics, Traumatology and Neurosurgery. Also to offer training and research on how to provide best services to Tanzanians. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Laboratory Technologist II at Muhimbili Orthopaedic Institute

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Laboratory Technologist II     TEMPORARY EMPLOYMENT OPPORTUNITIES BACKGROUND Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous institute established through an Act of parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing service in the fields of Orthopedics, Traumatology and Neurosurgery. Also to offer training and research on how to provide best services to Tanzanians. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Legal Officer II at Muhimbili Orthopaedic Institute

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Legal Officer II    TEMPORARY EMPLOYMENT OPPORTUNITIES BACKGROUND Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous institute established through an Act of parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing service in the fields of Orthopedics, Traumatology and Neurosurgery. Also to offer training and research on how to provide best services to Tanzanians. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger