Tuesday, 26 January 2021

RAIS MAGUFULI KUWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA OPD HOSPITALI YA MJI KAHAMA, KUZINDUA MRADI WA MAJI


Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Telack akizungumza na waandishi wa habari wilayani Kahama
Na Salvatory Ntandu - Kahama
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Telack amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli anatarajia kuanza ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo, ambapo ataweka mawe ya msingi katika majengo mbalimbali pamoja na kuzindua mradi wa maji wa Kagongwa - Isaka.

Akizungumza leo Jumanne Januari 26, 2021 na Waandishi wa habari wilayani Kahama,Telack amesema kuwa Rais Magufuli ataweka jiwe la msingi la wagonjwa wa nje hospitali ya Kahama Mji ambalo limegharimu shilingi bilioni 3.9 fedha za mapato ya ndani kwa lengo la kupunguza msongamano kwa akina mama wanaokwenda kujifungua katika hospitali hiyo.

Alisema kuwa kwa siku katika hospitali ya Mji Kahama zaidi ya watoto wachanga 35 hadi 75 wanazaliwa hivyo kusababisha akina mama wajawazito kukosa sehemu salama ya kujifungulia kutokana na kupokea idadi kubwa ya wajawazito kwa siku.

“Kwa mwezi watoto wapya zaidi 1000 wanazaliwa katika hospitali hii,serikali imejenga jengo hili la ghorofa mmoja ambalo litakuwa maalumu kwaajili ya kinamama wajawazito na watoto,tumetumia shilingi milioni 204 kujenga kituo cha afya Maalumu cha Nyasubi ambacho ni mahususi pia kwa akinamama kujifungulia,”alisema Telack.

Telack amefafanua kuwa bado akina mama wajawazito wanakabiliwa na changamoto mbalimbali lakini kukamilika kwa jengo hilo litasaidia kupunguza msongamano wa akinamama wajawazito katika hospitali hiyo ambayo inapokea idadi kubwa ya wagonjwa kwa siku huku wengi wao wakiwa ni akinamama wajawazito.

Amefafanua kuwa pia Rais Dk Magufuli ataweka jiwe la msingi katika jengo la utawala la halmashauri ya Mji kahama na Viwanda vya mwekezaji Mzawa vya Kampuni ya KOM GROUP OF CAMPANIES vya kusindika mazao mbalimbali ambacho kinatarajiwa kutoa ajira mpya kwa wakazi zaidi ya 2000.

“Pia Rais Magufuli atazindua mradi mkubwa wa maji ya ziwa Viktoria wa Kagongwa –Isaka ambao umekamilika na wananchi wameanza kupata huduma,niwaombe wakazi wa mkoa huu kujitokeza kwa wingi kumsikiliza katika mitutano yake miwili anatakayowahutubia,”alisema Telack.
Share:

AKAMATWA UWANJA WA NDEGE AKISAFIRISHA VINYONGA 74



Mwanaume mwenye umri wa miaka 56 ambaye hakutambuliwa zaidi  amekamatwa na Mamlaka nchini Austria katika uwanja wa ndege wa Vienna akiwa anatorosha vinyonga 74 kutoka nchini Tanzania.

Kwa Mujibu  wa gazeti la The Telegraph la Uingereza jamaa huyo alikuwa amewaficha wanyama hao katika soksi na masanduku ya barafu alipokamatwa na maofisa forodha wa uwanja huo wa Vienna.

Naibu katibu mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii nchini Tanzania, Allan Kijazi amesema mwanaume huyo alisafiri kwenda Austria kutoka Tanzania kupitia Ethiopia na kwamba mujibu wa gazeti hilo vinyonga hao walikuwa wakipelekwa kwenye bustani ya wanyama ya Schoenbrunn na ilibainika kuwa watatu wamekufa.

Amesema wanyama wote walikuwa wanatoka katika milima ya Usambara Tanzania na walikuwa katika umri wa wiki moja hadi wakubwa ambao walitakiwa kuuzwa katika masoko ya ulanguzi.



Share:

WAZIRI NDAKI AAGIZA KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA 67 WA UTOROSHAJI WA MIFUGO NA MAZAO YAKE

 

Na.Alex Sonna,Dodoma

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki ameliagiza Jeshi la polisi nchini kikosi cha kuzuia wizi wa mifugo, kuwasaka na kuwamakata mara moja watuhumiwa 67 wa utoroshaji wa mifugo na mazao yake.

Agizo hilo amelitoa leo Januari 26,2021 jijini Dodoma wakati akiwasilishiwa ripoti ya uchunguzi, kuhusu utoroshaji wa mifugo mipakani ambapo ripoti hiyo imebaini utoroshaji wa mifugo na mazao yake kwenda nchi za jirani.

Amefafanua kuwa serikali haiwezi kuvumilia uwepo wa watu wenye nia ovu kwa kutorosha rasilimali za nchi pamoja na kutoa onyo kwa watu wengine ambao wanatorosha mazao ya mifugo na mazao yake pamoja na wale wenye nia ya kufanya hivyo.

“Watoroshaji wa mifugo na mazao yake waanze kukamatwa kuanzia leo, wakamatwe mara moja tuanze na hawa 67 ambao wanajulikana walipo. Amesema Waziri Ndaki wakati akimuagiza Kamishna Msaidizi wa Polisi Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Mifugo nchini Yusuph Sarungi.

Aidha, amewaonya wafanyabiashara ambao wanajihusisha na utoroshaji wa mifugo na mazao yake waanze kutafuta kazi nyingine ya kufanya kwa kuwa wizara haitavumilia mtu yeyote ambaye atajihusha na vitendo hivyo kwa kuwa vinaenda kinyume na sheria za nchi na kuikosesha serikali mapato.

Pia, kuhusu urasimu na utoaji wa vibali mbalimbali vya mifugo na mazao yake Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amewataka watumishi wa wizara waliopo kwenye minada ya upili na mipakani kuacha urasimu wa kuchelewesha kutoa vibali mbalimbali na kuagiza kupatiwa orordha ya watumishi hao na viongozi wao na muda waliohudumu katika ofisi hizo na kuwachukulia hatua za kinidhamu watakaobainika kwenda kinyume na utaratibu wa kazi.

"Nataka nipatiwe taarifa za watu hao kuanzia vyeo vyao, umri wao na muda waliohudumu kwenye minada husika ili tuweze kuboresha kwenye eneo kwa sababu utaratibu wa kufanya kazi kwa mazoea umeshapitwa na wakati." Amefafanua Mhe. Ndaki

Ili kuhakikisha mifugo na mazao ya mifugo hayatoroshwi kuelekea nchi za jirani, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amemuagiza Katibu wa wizara hiyo anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel kuchambua ripoti hiyo na kuainisha mapendekezo yaliyotolewa ili sekta ya mifugo iweze kuwa na mchango mkubwa zaidi katika pato la taifa.

Waziri Ndaki ametaka pia ushirikiano kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) katika kutatua changamoto zinazowakabili wafugaji ili mifugo isikae muda mrefu wakati wa kusafirishwa kwends sokoni.

Awali akisoma ripoti ya uchunguzi, kuhusu utoroshaji wa mifugo mipakani, Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi Julius Mjengi amesema kabla ya tarehe 7 Novemba, 2020, mifugo iliyokuwa inatoka kwenye minada ya awali ya Handeni na Kilindi kuelekea nchini Kenya kupitia mpaka wa Horohoro haikuwa inafuata taratibu za forodha kama shehena nyingine.

Ameongeza kuwa takwimu za daftari la mifugo katika mpaka wa Horohoro zinaonyesha idadi ya mifugo iliyopitishwa kuelekea nchini Kenya kwa kipindi cha miaka 17 kutoka mwaka 2003 hadi Novemba, 2020 ilikuwa ni ng’ombe 24,980 na Mbuzi na Kondoo 9,368 (sawa na wastani wa Ng’ombe 122 na Mbuzi/Kondoo 46 kwa mwezi).

Taarifa hiyo ilibainisha pia baada ya uchunguzi, ilionekana kuwa kati ya tarehe 7 Novemba, 2020 hadi tarehe 9 Desemba, 2020 (kipindi cha mwezi mmoja tu) jumla ya Ng’ombe 1,096 na Mbuzi na Kondoo 1,044 walipitishwa katika kituo cha Forodha kuelekea nchini Kenya, ambapo huo ni wastani wa idadi ya mifugo iliyopita mpakani ndani ya mwezi mmoja ukilinganisha na siku za nyuma.

Taarifa imebaini pia viashiria vya udanganyifu wa kurekodi idadi sahihi ya mifugo inayokaguliwa kwenda Kenya hususan katika mpaka wa Hororohoro – Tanga.

Share:

SKAUTI JIJINI MBEYA WAKARABATI MAENEO YALIYO ATHIRIWA NA MAFURIKO

Vijana wa Chama cha Skauti Mkoa wa Mbeya wakikarabati kivuko cha watembea kwa miguu  katika Mtaa wa Mayombo Kata ya Iwambi baada ya kuharibiwa na mafuriko.

Vijana wa Chama cha Skauti Mkoa wa Mbeya wakiwajibika.
Vijana wa Chama cha Skauti Mkoa wa Mbeya wakisafisha mitaro
Kazi ikiendelea.
Kazi ikiendelea.

Na Dotto Mwaibale

 KUTOKANA  na mvua zinazo endelea kunyesha Mkoa  wa Mbeya na kuharibu miundombinu ya barabara Chama cha Skauti mkoani humo kimeendelea kutoa huduma ya kukarabati miundombinu hiyo kwa wathirika wa mafuriko.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi Kamishna wa Skauti  Mkoa wa Mbeya, Sadock Ntole alisema  mvua iliyonyesha Januari 23 mwaka huu ilileta athari kubwa kSatika Kata ya Iwambi na kuharibu miundombinu mbalimbali.


Alisema kufuata hali hiyo walikaa na kuratibu namna ya kufika katika maeneo hayo kutoa msaada ambapo kikosi cha uokoaji cha skauti wapatao 16 walikwenda kutoa huduma ya kusafisha  mitaro na makaravati. 

 " Mafuriko hayo yalisababisha athari za kubomoa kuta za nyumba za wakazi wa tatu wa eneo hilo na kuharibu vivuko vya watembea kwa miguu na kuleta changamoto ya matumizi ya barabara kwa wakazi  na wanafunzi waishio mtaa wa Mayombo na mitaa jirani ambao wanasoma katika Shule ya Sekondari Sinai, Nsenga, Maziwa, Stella Farm na Shule ya mmMsingi ya Iwambi."  alisema Ntole. 

Mratibu wa Majanga, Uokoaji  na Hali hatarishi wa chama hicho mkoani humo, Lusajo Sanga alisema kazi hiyo ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na ushirikiano kutoka kwa viongozi wao.

Alisema kazi kubwa walioifanya ilikuwa ni kurekebisha miundombinu ya kupitisha maji ambayo ilijaa taka na kusababisha maji kutoka nje ya mkondo wake na kuingia kwenye makazi ya watu na kujenga  vivuko vya waenda kwa miguu. 

Alisema kazi hiyo walifanya kwa kushirikiana na viongozi wa Serikali ya Mtaa wa Mayombo akiwepo Mwenyekiti  Philipo Mbembati, Mjumbe wa mtaa huo, James Ngungula pamoja na wakazi wa eneo hilo.

Sanga aliwataja skauti walioshiriki kazi hiyo kuwa ni Kamishna wa Skauti Mkoa Mbeya, Sadock Ntole, Mratibu wa Habari na Mawasiliano Mkoa Mbeya Barnaba Moses, Waratibu wa Skauti Wilaya ya Mbeya, Baraka Martin, Emanuel Mwasikili na Stephano Mwangosi.

Aidha Sanga aliwataja kwa majina  skauti waliounda kikosi kilichoshiriki kufanya kazi hiyo kuwa ni Evaristo Sanga, Glory Augustino, Beckam Frank, Elika Mwakabana, Skauta Macklin Lamsi, Elisha, Ckelvi Ekela, Bambo Ekela na Ali.

Sanga alitumia fursa hiyo kusema kwamba Skauti mkoani humo wapo tayari kutoa huduma kwa jamii pamoja na elimu ya jinsi ya kuepukana na athari zitakazotokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali ya mkoa  huo.

Kamishna wa Skauti Mkoa wa Mbeya, Sadock  Ntole alitoa rai kwa wananchi na wakazi wa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya kuchukua tahadhari na kuhakikisha miundombinu ya mitaro na makaravati inayopitisha maji inakuwa Safi na salama wakati wote ili kuruhusu maji kupita kwa urahisi katika mkondo wake ambapo pia aliwasisitiza wanaozalisha taka wazipeleke kwenye maghuba  sahihi ya kuhifadhia ili kurahisisha ubebaji wa taka hizo na kuzipeleka kwenye dampo kuu.

Share:

Updates : PAKUA APP YA MALUNDE 1 BLOG IMEFANYIWA MABORESHWA 2021

Share:

JITIBU TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA FULL POWER.. UUME MDOGO ZAT 50 NDIYO SULUHISHO



Zati 50


Full Power



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume:

⇒Ngiri,


⇒Henia


⇒Kisukari


⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri


⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu


⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi


⇒Msongo wa mawazo 

⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.

ZAT 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa
⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

Regional Strategic Information (SI) Officer at FHI 360

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Regional Strategic Information (SI) Officer   FHI 360 is a nonprofit human development organization dedicated to improving lives in lasting ways by advancing integrated, locally driven solutions. Our staff include experts in Health, Education, Nutrition, Environment, Economic Development, Civil Society, Gender, Youth, Research and Technology; creating a unique mix of capabilities to address today’s interrelated […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Credit Officers at ABC Computers

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POSITION: Micro-CREDIT OFFICER (2POST)   INTERNSHIP Summary  The main purpose of this role is to assume full responsibility of the Micro-Credit Portfolio, leading a team of professionals in the area of credit management, ensuring compliance with the local regulations, risk management practices and impartingdeveloping skill sets of personnel in Micro-Credit Department. Essential Duties And Responsibilities    To […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

IT Officers at ABC Computers

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POSITION: IT OFFICER (2 POST)   Description  INTERNSHIP  Summary We are currently seeking a qualified, knowledgeable IT Professional to helpour company develop, use, and integrate IT systems.   Minimum Qualification:Bachelor degree in related field (note less than 3 yearsfrom the year of completion). Experience Level: Entry level   Duties and responsibilities    Administer network and data security, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Information Management Officer at UN Volunteer

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

information Management Officer     Eligibility criteriaMinimum age: 22 years old. Applicants must be nationals of or legal residents in the country of assignment. Description of taskThe UN Volunteer will work under the supervision of the UNDP Resident Representative and Deputy Resident Representative, in the key functions listed below. He will also work closely with the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Program Officer and Administrative Support at USAID

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

OVERVIEW: The Global Health Supply Chain Program Technical Assistance – Tanzania (GHSC-TA-TZ) project, supported by the United States Agency for International Development (USAID), provides expert technical assistance to Tanzania, to strengthen country supply chain systems across all health elements, e.g., malaria, family planning (FP), HIV/AIDS, tuberculosis (TB) and Reproductive, maternal, newborn and child health (MNCH). […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Data Entry Intern at THPS

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

ECHO Data Entry Intern   VOLUNTEERSHIP PROGRAM FOR ECHO DATA ENTRY INTERN Reports to ECHO PO / NHLS Project Coordinator Tanzania Health Promotion Supports (THPS) is an indigenous NGO established under non- governmental organization act No 24 of 2002 in 2011. THPS works in partnership with the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Lecturer – History at Mwalimu Nyerere Memorial Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST: LECTURER – HISTORY(RE-ADVERTISED) – 1 POST POST CATEGORY(S) SOCIOLOGY, POLITICAL SCIENCE, COMMUNITY AND SOCIAL DEVELOPMENT EMPLOYER The Mwalimu Nyerere Memorial Academy (MNMA) APPLICATION TIMELINE: 2021-01-22 2021-02-04 DUTIES AND RESPONSIBILITIES   To teach up to NTA level 8 for Master’s degree holders and NTALevel 9 for PhD holders; To guide and supervises students in building up their […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Assistant Lecturer Library And Information Management at Mwalimu Nyerere Memorial Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST: ASSISTANT LECTURER – LIBRARY AND INFORMATION MANAGEMENT SYSTEM(RE-ADVERTISED) – 1 POST POST CATEGORY(S) HR & ADMINISTRATION EMPLOYER The Mwalimu Nyerere Memorial Academy (MNMA) APPLICATION TIMELINE: 2020-01-22 2021-02-04 JOB SUMMARY Candidate should be a person of the highest integrity and professionalism who will work closely with MNMA team to achieve agreed objectives. DUTIES AND RESPONSIBILITIES   To […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Communication Manager at Dangote Group Tanzania

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Careers at Dangote Group The Dangote Group is one of Nigeria’s most diversified manufacturing conglomerates. The Group continues to grow its vision of becoming the leading provider of essential needs in Food and Shelter in Sub-Saharan Africa with sustained market leadership in Cement Manufacturing, Sugar Milling, Sugar Refining, Packaging Material Production and Salt Refining. Upcoming […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Head of Marketing at Dangote

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Head of Marketing (Cement Industry)   Description Key Duties and Responsibilities   Demonstrate ownership of and communicate the strategic direction and objectives of the Sales and Marketing department to all staff within the department. Oversee the articulation of the organisation’s sales and marketing strategies and ensure alignment with DCP’s corporate strategy, goals and objectives. Champion the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

ZAIDI YA BILIONI 8 KUTUMIKA MRADI WA KUONGEZA UZALISHAJI MAJI JIJI LA TANGA

MSIMAMIZI wa Mradi kutoka Tanga Uwasa Adella Mboya akisisitiza jambo wakati wa kutoa elimu kwa wananchi wa Kata ya Kiomoni Jijini Tanga kutambulisha mradi huo ambao utakuwa ni wa kuboresha hali upatikanaji wa maji safi katika Jiji hilo.


Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa wateja Rogers Machaku akizungumza wakati wa mkutano huo
Diwani wa Kata ya Kiomoni (CCM) Mohamed  Mfundo akieleza jambo wakati wa mkutano huo ambapo aliishukuru Tanga Uwasa kuwafikia wananchi wake na kuwapa elimu wa pili kushoto ni Afisa Uhusiano  Msaidizi wa Tanga Uwasa Anna Makange
AFISA Uhusiano Msaidizi wa Tanga Uwasa Anna Makange akitolea ufafanuzi baadhi ya maswali yaliyoulizwa kwenye mkutano huo
Afisa Mtendaji wa Kata ya Kiomoni Adam Harson Chinduka akizungumza jambo wakati wa mkutano huo kulia ni Diwani wa Kata ya Kiomoni (CCM) Mohamed Mfundo na kushoto ni Afisa Uhusiano Msaidizi wa Tanga Uwasa Anna Makange


ZAIDI ya Bilioni 8 zinatarajiwa kutumika katika mradi mkubwa kuongeza uzalishaji wa maji Jijini Tanga kutoka lita za ujazo 30 kwa siku  hadi  kufikia lita 45 kwa siku utakaosimamiwa na Mamlaka ya Maji Tanga (Tanga Uwasa) kupitia wataalamu wake.


Hayo yalibainishwa leo na Msimamizi wa Mradi kutoka Tanga Uwasa Adela Mboya wakati wataalamu wa mamlaka hiyo walipokuwa wakitoa elimu kwa wananchi wa Kata ya Kiomoni Jijini Tanga kutambulisha mradi huo ambao utakuwa ni wa kuboresha hali upatikanaji wa maji safi katika Jiji hilo.


Alisema kwamba mradi huo utakuwa ni wa miezi 12 na utakuwa na manufaa makubwa mawili katika mji wa Tanga la kwanza wananchi upatikanaji wa  maji ya uhakika ambayo hayakatikikatiki na maji yatapatikana maeneo yote masaa 24.


Alisema pia wakati wa utekelezaji mradi vijana watanufaika  kwa sababu watakwenda kuongeza machujio mawili kwenye mtambo wa kusafishia maji uliopo mowe Pande.


Aidha alisema hivyo kazi ya ujenzi kubwa itakayofanyika na kuna tenki la kuhifadhi maji lenye ujazo wa lita milioni 1 na watakwenda kujenga jengine lenye ujazo wa lita milioni 1 eneo la Pande .


Alisema kazi nyengine watalaza bomba kubwa lenye kipenyo cha milimita 600 kwa urefu wa kilomita 12.5 kutoka mowe mpaka Kange Jeshini na kwenye tenki  hilo bomba litakuwa na kazi ya kusafirisha maji wanayoyazalisha na watakiwa na mabomba mawili makubwa ya kupelekea maji Tanga.


“ Hivyo vijana watanufaika kwenye kazi za ujenzi kuchimba mitaro kwani kwenye mikataba ambayo wataingia na wakandarasi  kwamba kazi yoyote ambayo haihitaji wataalamu maalumu inatakiwa itoke sehemu ya mradi Kata ya Kiomoni”Alisema 


Aliongeza kwamba hivyo vijana wajitokeza kwa wingi kupata hizo  ajira za muda huku akiwaomba wananchi kuwa tayari kupokea mradi na kutoa ushirikiano wakati ukitelekezwa kwenye maeneo yao .


“Kutokana na hilo ndio maana tumepanga kufanya mradi wa  kuongeza miuondombinu ya kuzalisha maji kutoka mita za ujazo elfu 30 mpaka elfu 45 kwa siku na mradi huo utaanza mwezi Aprili mwaka huu”Alisema

Awali akizungumza katika mkutano huo,Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa wateja Rogers Machaku alisema wanaboresha kwa kiasi kikubwa mtambo wa Mowe hatua ambayo itasaidia kuongezeka kwa maji yanayozalishwa .


Alisema pamoja na kuboresha lakini wanachangamoto ya bomba linalotoka Mowe kwenda mjini eneo la Kange hilo bomba limezidiwa na uwezo hivyo wanataka kuweka mabomba yawe mawili ambao yote yatakuwa yakipeleka maji mjini.


Naye kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kiomoni (CCM) Mohamed  Mfundo aliishukuru Tanga Uwasa kwa kufika kwenye Kata hiyo huku akieleza Kata hiyo ndio eneo ambalo mamlaka hiyo imewekeza kwa kiasi kikubwa lakini ni jambo la aibu kwamba baadhi ya maeneo yao hakuna huduma ya maji lakini kwenye maeneo mengine Jijini humo kuna maji.


Alisema analizungumza hilo makusudi kwqa sababu mmefika eneo hilo mtaona namna ya kulifanyia kazi ili kuweza kuondosha changamoto kwenye maeneo ya Masaini,Mijihoroni,Misufini hayo maeneo kuna watu wanaishi na huduma ya maji ni ya kwanza.


“Bila maji hakuna chakula,hakuna mimea,uhai wa chochote hivyo naombeni hizi changamoto mzichukue muende kuzifanyia kazi hilo ni ombi langu kama kiongozi wa Kata  mlichukue muone ni namna nani mnaweza kuwapa huduma maeneo yenye changamoto hizo“Alisema Diwani huyo.

   

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger