Monday, 18 January 2021

MGANGA WA JADI ASAKWA KUSABABISHA KIFO CHA MTOTO WAKE AKIMSAFISHA NYOTA KAHAMA


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 18,2021

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linamsaka mtuhumiwa Dela Megejuwa Lwaho (44) kwa kusababisha kifo cha mtoto wake Juma Dela Megejuwa (12) na watu wengine wawili kuzirai baada ya kuwapa dawa ya miti shamba idhaniwayo kuwa na sumu ili wasafishiwe nyota zao. 

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Jumatatu Januari 18,2021 Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema tukio hilo limetokea Januari 16,2021 majira ya saa tisa na nusu alasiri katika kijiji cha Mwaningi kata ya Bulige wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga. 

“Juma Dela Megejuwa ambaye ni mtoto wa mganga wa jadi (mtuhumiwa) Dela Megejuwa Lwaho alifariki dunia baada ya kunywa dawa ya kienyeji inayodhaniwa kuwa na sumu akiwa na watu wawili nyumbani”,amesema. 

“Watu hao wawili waliokuwa nyumbani kwa mtuhumiwa ni Loya Nsalala Ngusa (66) jirani wa mtuhumiwa na Bahati Ludahila Ngusa (25) mkazi wa Shilima Kwimba Mwanza ambaye ni mgeni aliyefikia nyumbani hapo kwa mtuhumiwa ambao walikunywa dawa hiyo ya kienyeji na kuzirai papo hapo na kukimbizwa kituo cha afya Chela kwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri”,ameeleza Kamanda Magiligimba.
 
"Mganga huyo wa jadi alitwanga dawa kwenye kinu ambayo ilitakiwa waioge ili kuosha nyota zao badala yake akawaambia wainywe",ameongeza

Amesema mtuhumiwa (mganga wa jadi) alikimbia mara baada ya tukio hilo na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Halmashauri Mji Kahama kwa uchunguzi zaidi. 

Kamanda Magiligimba ametoa wito kwa waganga wa jadi kuwa na uhakika na matumizi ya dawa zao pamoja na matumizi mazuri ya vibali/leseni zao ili kuepuka kusababisha vifo na madhara kwa wateja wao na jeshi la polisi halitamuonea muhari mganga yeyote anayekwenda kinyume na maelekezo ya vibali/leseni zao.
Share:

AMUUA BABU YAKE BAADA YA KUONA ANATESEKA NA MARADHI MUDA MREFU


Picha haihusiani na habari hapa chini

Saidi Kihundwa (98), Mkazi wa Kijiji cha Mlangoni katika Kata ya Gararagua, Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, anadaiwa kuuawa kikatili na mjukuu wake, aliyeona babu yake anateseka na maradhi kwa muda mrefu.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Kamishna Msaidizi Leonard Makona, alithibitisha taarifa za kuuawa kwa mkazi huyo.

Tukio hilo lilitokea wiki iliyopita, majira ya jioni nyumbani kwa mzee huyo, mjukuu wake akidaiwa kumpiga na kitu kizito kichwani na kumsababishia umauti.

Soma zaidi: https://epaper.ippmedia.com

Share:

TARURA SINGIDA YAOKOA ZAIDI YA BILIONI 1.8 UJENZI WA DARAJA WILAYANI MANYONI

 

Watendaji wa  Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya Manyoni wakikagua daraja hilo.

Wananchi na vyombo vyao wakivuka mto Nkonjigwe kwa kutumia daraja hilo.
Wananchi wanaozunguka maeneo ya daraja Nkonjigwe wakifurahia kutokana na kujengewa daraja hilo.

Na Dotto Mwaibale, Singida.

SERIKALI ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Magufuli kupitia watendaji waaminifu wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) imeokoa zaidi ya bilioni 1.8 kwenye ujenzi ambao tayari umekamilika wa daraja la Mto Nkonjigwe Wilayani Manyoni mkoani hapa.

Kabla ya kuanza kwa ujenzi huo kati ya Juni na Septemba upembuzi yakinifu wa mradi huo kupitia wazabuni mbalimbali ulikadiriwa kufikia zaidi ya shilingi bilioni 2, kabla ya Tarura kufanya maamuzi magumu ya kutumia mfumo wa Force Account.

Kukamilika kwa ujenzi wa daraja hilo kunakwenda kufungua fursa za uhakika wa upatikanaji wa huduma za afya hususani kwa akina mama wajawazito sambamba na kuimarisha wigo wa kibiashara kwa wakazi wa kata takribani tano zinazotumia njia inayounganishwa na daraja hilo yenye urefu wa km 76.2.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wanaozunguka eneo hilo akiwemo Halima Abdallah mkazi wa Kijiji cha Chikuyu alisema wamefurahishwa na ujenzi wa daraja hilo ambalo litawasaidia akina mama wajawazito kuvuka na kwenda kujifungua kwenye Zahanati za Kilimatinde na Chikuyu kwani awali wengi walikatisha maisha yao kwa kushindwa kuvuka mto huo.

Halima alisema walikuwa wanatoa shilingi elfu 2 hadi elfu 3 kuvushwa kwenye Mto huo na watu wenye uzoefu wa kuogelea jambo ambalo halikuwa salama kwao kwani kuna wakati licha ya uzoefu wao hushindwa kuvuka na kupelekwa na maji pamoja na aliyekuwa anavushwa.

"Tulikuwa tukifika hapa tunavua nguo halafu ndio tunavushwa, tunatoa shilingi elfu 2 za mtu kuvushwa na shilingi elfu 3 za nguo.watu wamekufa wengi sana hapa hasa Wanawake wajawazito." alisema  Halima.

Thomas Minaloganawenda mkazi wa Kijiji cha Chinyika kilichopo Kata ya Sasajila alisema moja ya shughuli kubwa ya kiuchumi kwenye maeneo haya ni uchimbaji wa chumvi lakini kuna wakati ilikuwa ikiharibikia kwenye mto kutokana na kukosa daraja.

Alisema amefanya kazi ya kuwavusha watu kwenye mto huo kwa muda mrefu licha ya kujipatia ujira lakini ilikuwa inaumiza anapoona wengi wakipoteza maisha hakuwa anafanya kazi hiyo kwa raha ila ni katika kujaribu kuokoa maisha ya watu waliokuwa wanafika hapo na kuhitaji kuvuka kwenda kupata huduma.

Awali Mratibu wa TARURA Mkoa wa Singida Mhandisi Boniphace William alisema ujenzi wa daraja hilo umegharimu shilingi milioni 122,415,500 hadi kukamilika kwake ambapo limetumia mfumo wa raslimali za ndani 'Force Account' 

Aidha, William alisema daraja hilo linatoa fursa ya upatikanaji wa huduma mbalimbali kuzunguka Vijiji vya Chikuyu,Chibumagwa, Sasajila, Majiri na Sanza.

"Nawaomba wananchi wanaohudumiwa na daraja hili na miradi mingine sehemu mbalimbali kutambua miradi hiyo ni kwa ajili yao, hivyo ni wajibu wao kuitunza na sio suala la Tarura pekee, wakijenga tabia hiyo miradi mingi itadumu kwa muda mrefu." alisema William.

Kwa upande wake Meneja wa Tarura Wilaya ya Manyoni Mhandisi Yose Mushi alisema daraja hilo ambalo lina urefu wa mita 53 na mita 25 eneo la kupitisha maji, kadhalika lenye tuta mita 28 linatarajia kuchagiza kasi ya ustawi wa uchumi kwa wakazi wanaozunguka maeneo hayo. 

Share:

UBORA WA VIWANDA VYA NYAMA NCHINI WACHANGIA KASI YA USAFIRISHAJI NYAMA NJE YA NCHI

 


Kasi ya kusafirisha nyama kwenda nje ya nchi imeongezeka kutokana na kuwepo kwa ubora wa Viwanda vya nyama ikiwa ni uwekezaji mkubwa uliopo jambo linalosababisha kuwepo kwa nyama bora na salama kwa ajili ya matumizi ya binadamu na kukidhi soko la ndani na nje ya nchi.

Hayo yamesemwa na Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania Bwana Imani Sichalwe akiwa kwenye ziara ya kukagua mazingira ya usafirishaji wa nyama kutoka Tanzania kwenda nchi za nje aliyoifanya tarehe 16.01.2021 katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere Jijini Dar.

Uwepo wa viwanda hivi vya nyama vya kisasa hapa Nchini ndio vinafanya tuwe na ithibati ya kupeleka nyama nje ya nchi ambapo kiwanda Cha Tanchoice kilichopo Kijiji cha soga wilayani Kibaha Mkoani Pwani chenye uwezo wa kuchinja mbuzi 4500 kwa siku na ng’ombe 1000 kwa siku moja ambapo kwa Tarehe 16.01.2021 kimepeleka mbuzi 2000 waliochinjwa Sawa na kilo 20,000 au tani 20 kwenda Oman na Kuwait.

“Kwa Sasa kwa wiki kiwanda cha nyama cha Tanchoice kilichopo Kibaha Mkoani Pwani husafirishwa mbuzi waliochinjwa 6000 sawa na kilo 60,000 sawa na tani 60 kwenda Omani,Qatar na Kuwait na kwa wiki ijayo kiwanda kitaanza kupeleka nyama katika soko jipya la Hongkong. Kwa upande wa kiwanda Cha Nyama Cha Eliya Foods Overseas Limited kimeanza kupeleka nyama kwenda Oman Mbuzi 1874 sawa na tani 14.6” amesema Sichalwe.

Katika ziara hiyo ya kukagua mazingira ya usafirishaji wa nyama kwenda nje ya nchi Kaimu msajili Bodi ya Tanzania amesema ameridhika na namna shughuli nzima ya utaratibu unaofanywa kuanzia kushusha nyama kwenye gari,kuingiza kwenye vyumba maalumu vya kuhifadhia nakupooza pamoja na namna ya upakiaji wa nyama hizo kwenye ndege.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 18,2021
























Share:

Mlinzi TGOS A – (Nafasi 16) at Tume ya Utumishi wa Mahakama

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Msaidizi wa Kumbukumbu II TGS B – (Nafasi 2) at Tume ya Utumishi wa Mahakama

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Msaidizi wa Hesabu II TGS. B – (Nafasi 4) at Tume ya Utumishi wa Mahakama

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Afisa Hesabu II – TGS. D – (Nafasi 2) at Tume ya Utumishi wa Mahakama

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Msaidizi wa Ofisi TGOS. A (Nafasi 15) at Tume ya Utumishi wa Mahakama

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Katibu Mahsusi III TGS B – (Nafasi 4) at Tume ya Utumishi wa Mahakama

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The Constitution of the United Republic of Tanzania, 1977 vests the authority and responsibility to administer justice in the Judiciary of Tanzania. The Judiciary has its foundation on Article 107A (1) and 107B of the Constitution and states clearly about the Independence of the Judiciary in the United Republic of Tanzania. Now the strategic plan […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Operata wa Kompyuta II TGS C – (Nafasi 1) at Tume ya Utumishi wa Mahakama

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The Constitution of the United Republic of Tanzania, 1977 vests the authority and responsibility to administer justice in the Judiciary of Tanzania. The Judiciary has its foundation on Article 107A (1) and 107B of the Constitution and states clearly about the Independence of the Judiciary in the United Republic of Tanzania. Now the strategic plan […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Sunday, 17 January 2021

MWILI WA MSANII C PWAA WAZIKWA MAKABURI YA MWINYI MKUU MAGOMENI DAR ES SALAAM


Mazishi ya Msanii wa Bongo Fleva, Ilunga Khalifa maarufu C Pwaa yamefanyika jioni ya leo kwenye makaburi ya Mwinyi Mkuu Magomeni, Dar es salaam. Cpwaa amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Januari 17, 2021 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kaka mdogo wa msanii huyo ambaye alikuwa akimuuguza kipindi chote cha maradhi, Murad Omar Khamis amesema kaka yake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa homa ya mapafu (pnemounia) kwa wiki sasa lakini alizidiwa wiki hii na walimkimbiza hospitali ambapo alilazwa kabla ya umauti kumfika usiku wa kuamkia leo Januari 17.

"Alikuwa anaumwa wiki mbili zilizopita, na akaja kuishi hapa nyumbani kwa mama yake. Ila Jumatano alizidiwa ndiyo tukamkimbiza hospitali muhimbili, alilazwa ICU," aliongeza.
Msanii Cpwaa enzi za uhai wake
TAZAMA VIDEO HAPA
Share:

MTOTO AKIRI KUMCHINJA NA KUNYWA DAMU YA BINAMU YAKE



Kijana mmoja mwenye umri wa miaka 16 katika eneo la Embu nchini Kenya, anashikiliwa na Jeshi la Polisi nchini humo kwa tuhuma za kumuua binamu yake ambaye ni mtoto wa miaka minne, Brayden Mutwiri na kunywa damu yake kwa kile kinadhaniwa kuwa kitendo cha utoaji kafara kisha kuutupa mwili wa mtoto huyo mtoni.

Mwanafunzi huyo wa darasa la 8, juzi Jumatano aliwaongoza maofisa wa upelelezi nchini humo hadi katika Mto Thuci ambapo waliukuta mwili wa Mutwiri ukiwa ndani ya mto huo huku ukiwa umeharibika vibaya hata kushindwa kuutambua vizuri kwani umekaa ndani ya maji kwa wiki nzima.

Mutwiri alipotea mwishoni mwa mwezi Desemba, mwaka jana 2020, nyumbani kwao Kavengero, Mbeere Kaskazini.

 Mtuhumiwa huyo pamoja na wenzake walikamatwa Jumatatu na kushikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Siakago kwa mahojiano baada kupatikana kwa taarifa kuwa anahusika na tukio.

Imeelezwa kuwa, baada ya mahojiano, mtuhumiwa aliwaelekeza polisi kwenye mto ambapo mwili wa mtoto huyo waliutupa, baada ya kufika eneo la tukio, waliukuta mwili ukiwa umekwama katikati ya miamba miwili huku ukiwa umeharibika kutokana na kuvimba pamoja na majeraha uliyokuwa nayo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la tukio, mjomba wa watoto hao, Nephat Nyaga alisema mtuhumiwa alisimulia jinsi yeye na wenzake walivyomuua mtoto huyo, kunywa damu yake, kisha kutupa mwili wake mtoni.

Aliendelea kueleza kuwa, yeye pamoja na mwenzake walimshawishi mtoto huyo wakati akicheza nyumbani kwao, kisha wakaondoka naye na kumpeleka mtoni ambako walitekeleza unyama huo.

Chifu wa eneo hilo, Charles Njeru akizungumza na waandishi wa habari, alisema kwamba mtoto huyo alitoweka nyumbani kwao katika mazingira ya kutatanisha mwishoni mwa Desemba, mwaka jana na amekuwa akitafutwa na familia yake bila mafanikio.

Njeru aliongeza kuwa, familia ya marehemu itasubiri matokeo ya uchunguzi wa mwili huo ili kubaini chanzo cha kifo na kuthibitisha iwapo mwili huo ni wa mtoto Mutwiri. 

Aidha, alisema hicho kimekuwa kisa cha pili cha mtoto aliyepotea na kupatikana akiwa amekufa mtoni. Mtoto mwingine ambaye alikuwa wa kike alipotea na mwili wake ukakutwa mtoni miezi mitatu iliyopita.

Njeru aliwaonya wananchi kutojichukulia sheria mkononi, pia aliwaasa kutokuwa na chuki dhidi ya familia zao, watoto wao kwa kushambulia na kuwaua kwa vigezo vya kafara na kutafuta mali kishirikina, na badala yake kufuata taratibu za kisheria za kutatua mizozo na kutafuta mali. Wananchi wa Embu wamelaani vikali mauaji hayo na kutaka uchunguzi wa haraka ufanyike ili wauaji wachukuliwe hatua za kisheria.
Share:

RAIS MAGUFULI AMTUMBUA MKURUGENZI MKUU WA TUME YA MATUMIZI YA ARDHI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi, Dkt. Steven Justice Nindi kuanzia leo, Januari 17, 2020, na nafasi iyo itajazwa hapo baadaye.

Share:

JITIBU TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA FULL POWER.. UUME MDOGO ZAT 50 NDIYO SULUHISHO



Zati 50


Full Power



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume:

⇒Ngiri,


⇒Henia


⇒Kisukari


⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri


⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu


⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi


⇒Msongo wa mawazo 

⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.

ZAT 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa
⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

MSHAHARA WA CHIKWENDE SIMBA SC BALAA MTUPU


UNAWEZA kusema ni kufuru mara baada ya uongozi wa Simba kukubali kumpa staa mpya wa timu hiyo, Perfect Chikwende mshahara wa dola za Kimarekani 8,000 ambazo ni sawa na Sh 18,470,900 za Kitanzania.

Chanzo cha kumaminika kutoka ndani ya Simba, kilieleza kuwa ulitokea mvutano mkubwa kwenye mshahara huo ambao Simba walitaka kumpa dola 6,000 (Sh 13,853,200), lakini jamaa akaweka ngumu akitaka dola 8,000 huku akiwaambia kama wakishindwa atakwenda zake Azam ambao walikuwa tayari kutoa mpunga huo.

Kikizungumza na Spoti Xtra, chanzo hicho kilisema mshahara wa Chikwende ni mkubwa zaidi pengine kuliko wachezaji wengine.

“Chikwende atakuwa analipwa dola za Marekani 8,000, ambazo ni zaidi ya Sh milioni 18 za Kitanzania, Simba walikuwa wanataka wampe chini ya hapo, kwenye dola 6,000 au 5,000, lakini jamaa akagoma kabisa akidai kama wakishindwa kumpa anachotaka atakwenda zake Azam,” kilisema chanzo hicho.

Simba imesajili Chikwende kwa mkataba wa miaka miwili unaotajwa kufikia thamani ya dola 55,000 ambazo ni sawa na Sh 126,987,000 na inaelezwa kama Simba wangezubaa kidogo mwamba huyo alikuwa anatua ndani ya Azam FC.


STORI: MUSA MATEJA NA ISSA LIPONDA
CHANZO - Global Publishers

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger