Monday, 18 January 2021
MGANGA WA JADI ASAKWA KUSABABISHA KIFO CHA MTOTO WAKE AKIMSAFISHA NYOTA KAHAMA
AMUUA BABU YAKE BAADA YA KUONA ANATESEKA NA MARADHI MUDA MREFU

Soma zaidi: https://epaper.ippmedia.com
TARURA SINGIDA YAOKOA ZAIDI YA BILIONI 1.8 UJENZI WA DARAJA WILAYANI MANYONI
Watendaji wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya Manyoni wakikagua daraja hilo.
Wananchi na vyombo vyao wakivuka mto Nkonjigwe kwa kutumia daraja hilo.Wananchi wanaozunguka maeneo ya daraja Nkonjigwe wakifurahia kutokana na kujengewa daraja hilo.
Na Dotto Mwaibale, Singida.
SERIKALI ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Magufuli kupitia watendaji waaminifu wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) imeokoa zaidi ya bilioni 1.8 kwenye ujenzi ambao tayari umekamilika wa daraja la Mto Nkonjigwe Wilayani Manyoni mkoani hapa.
Kabla ya kuanza kwa ujenzi huo kati ya Juni na Septemba upembuzi yakinifu wa mradi huo kupitia wazabuni mbalimbali ulikadiriwa kufikia zaidi ya shilingi bilioni 2, kabla ya Tarura kufanya maamuzi magumu ya kutumia mfumo wa Force Account.
Kukamilika kwa ujenzi wa daraja hilo kunakwenda kufungua fursa za uhakika wa upatikanaji wa huduma za afya hususani kwa akina mama wajawazito sambamba na kuimarisha wigo wa kibiashara kwa wakazi wa kata takribani tano zinazotumia njia inayounganishwa na daraja hilo yenye urefu wa km 76.2.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wanaozunguka eneo hilo akiwemo Halima Abdallah mkazi wa Kijiji cha Chikuyu alisema wamefurahishwa na ujenzi wa daraja hilo ambalo litawasaidia akina mama wajawazito kuvuka na kwenda kujifungua kwenye Zahanati za Kilimatinde na Chikuyu kwani awali wengi walikatisha maisha yao kwa kushindwa kuvuka mto huo.
Halima alisema walikuwa wanatoa shilingi elfu 2 hadi elfu 3 kuvushwa kwenye Mto huo na watu wenye uzoefu wa kuogelea jambo ambalo halikuwa salama kwao kwani kuna wakati licha ya uzoefu wao hushindwa kuvuka na kupelekwa na maji pamoja na aliyekuwa anavushwa.
"Tulikuwa tukifika hapa tunavua nguo halafu ndio tunavushwa, tunatoa shilingi elfu 2 za mtu kuvushwa na shilingi elfu 3 za nguo.watu wamekufa wengi sana hapa hasa Wanawake wajawazito." alisema Halima.
Thomas Minaloganawenda mkazi wa Kijiji cha Chinyika kilichopo Kata ya Sasajila alisema moja ya shughuli kubwa ya kiuchumi kwenye maeneo haya ni uchimbaji wa chumvi lakini kuna wakati ilikuwa ikiharibikia kwenye mto kutokana na kukosa daraja.
Alisema amefanya kazi ya kuwavusha watu kwenye mto huo kwa muda mrefu licha ya kujipatia ujira lakini ilikuwa inaumiza anapoona wengi wakipoteza maisha hakuwa anafanya kazi hiyo kwa raha ila ni katika kujaribu kuokoa maisha ya watu waliokuwa wanafika hapo na kuhitaji kuvuka kwenda kupata huduma.
Awali Mratibu wa TARURA Mkoa wa Singida Mhandisi Boniphace William alisema ujenzi wa daraja hilo umegharimu shilingi milioni 122,415,500 hadi kukamilika kwake ambapo limetumia mfumo wa raslimali za ndani 'Force Account'
Aidha, William alisema daraja hilo linatoa fursa ya upatikanaji wa huduma mbalimbali kuzunguka Vijiji vya Chikuyu,Chibumagwa, Sasajila, Majiri na Sanza.
"Nawaomba wananchi wanaohudumiwa na daraja hili na miradi mingine sehemu mbalimbali kutambua miradi hiyo ni kwa ajili yao, hivyo ni wajibu wao kuitunza na sio suala la Tarura pekee, wakijenga tabia hiyo miradi mingi itadumu kwa muda mrefu." alisema William.
Kwa upande wake Meneja wa Tarura Wilaya ya Manyoni Mhandisi Yose Mushi alisema daraja hilo ambalo lina urefu wa mita 53 na mita 25 eneo la kupitisha maji, kadhalika lenye tuta mita 28 linatarajia kuchagiza kasi ya ustawi wa uchumi kwa wakazi wanaozunguka maeneo hayo.
UBORA WA VIWANDA VYA NYAMA NCHINI WACHANGIA KASI YA USAFIRISHAJI NYAMA NJE YA NCHI

Kasi ya kusafirisha nyama kwenda nje ya nchi imeongezeka kutokana na kuwepo kwa ubora wa Viwanda vya nyama ikiwa ni uwekezaji mkubwa uliopo jambo linalosababisha kuwepo kwa nyama bora na salama kwa ajili ya matumizi ya binadamu na kukidhi soko la ndani na nje ya nchi.
Hayo yamesemwa na Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania Bwana Imani Sichalwe akiwa kwenye ziara ya kukagua mazingira ya usafirishaji wa nyama kutoka Tanzania kwenda nchi za nje aliyoifanya tarehe 16.01.2021 katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere Jijini Dar.
Uwepo wa viwanda hivi vya nyama vya kisasa hapa Nchini ndio vinafanya tuwe na ithibati ya kupeleka nyama nje ya nchi ambapo kiwanda Cha Tanchoice kilichopo Kijiji cha soga wilayani Kibaha Mkoani Pwani chenye uwezo wa kuchinja mbuzi 4500 kwa siku na ng’ombe 1000 kwa siku moja ambapo kwa Tarehe 16.01.2021 kimepeleka mbuzi 2000 waliochinjwa Sawa na kilo 20,000 au tani 20 kwenda Oman na Kuwait.
“Kwa Sasa kwa wiki kiwanda cha nyama cha Tanchoice kilichopo Kibaha Mkoani Pwani husafirishwa mbuzi waliochinjwa 6000 sawa na kilo 60,000 sawa na tani 60 kwenda Omani,Qatar na Kuwait na kwa wiki ijayo kiwanda kitaanza kupeleka nyama katika soko jipya la Hongkong. Kwa upande wa kiwanda Cha Nyama Cha Eliya Foods Overseas Limited kimeanza kupeleka nyama kwenda Oman Mbuzi 1874 sawa na tani 14.6” amesema Sichalwe.
Katika ziara hiyo ya kukagua mazingira ya usafirishaji wa nyama kwenda nje ya nchi Kaimu msajili Bodi ya Tanzania amesema ameridhika na namna shughuli nzima ya utaratibu unaofanywa kuanzia kushusha nyama kwenye gari,kuingiza kwenye vyumba maalumu vya kuhifadhia nakupooza pamoja na namna ya upakiaji wa nyama hizo kwenye ndege.
Mlinzi TGOS A – (Nafasi 16) at Tume ya Utumishi wa Mahakama
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Msaidizi wa Kumbukumbu II TGS B – (Nafasi 2) at Tume ya Utumishi wa Mahakama
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Msaidizi wa Hesabu II TGS. B – (Nafasi 4) at Tume ya Utumishi wa Mahakama
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Afisa Hesabu II – TGS. D – (Nafasi 2) at Tume ya Utumishi wa Mahakama
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Msaidizi wa Ofisi TGOS. A (Nafasi 15) at Tume ya Utumishi wa Mahakama
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Katibu Mahsusi III TGS B – (Nafasi 4) at Tume ya Utumishi wa Mahakama
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
The Constitution of the United Republic of Tanzania, 1977 vests the authority and responsibility to administer justice in the Judiciary of Tanzania. The Judiciary has its foundation on Article 107A (1) and 107B of the Constitution and states clearly about the Independence of the Judiciary in the United Republic of Tanzania. Now the strategic plan […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Operata wa Kompyuta II TGS C – (Nafasi 1) at Tume ya Utumishi wa Mahakama
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
The Constitution of the United Republic of Tanzania, 1977 vests the authority and responsibility to administer justice in the Judiciary of Tanzania. The Judiciary has its foundation on Article 107A (1) and 107B of the Constitution and states clearly about the Independence of the Judiciary in the United Republic of Tanzania. Now the strategic plan […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Sunday, 17 January 2021
MWILI WA MSANII C PWAA WAZIKWA MAKABURI YA MWINYI MKUU MAGOMENI DAR ES SALAAM


MTOTO AKIRI KUMCHINJA NA KUNYWA DAMU YA BINAMU YAKE

RAIS MAGUFULI AMTUMBUA MKURUGENZI MKUU WA TUME YA MATUMIZI YA ARDHI
JITIBU TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA FULL POWER.. UUME MDOGO ZAT 50 NDIYO SULUHISHO
MSHAHARA WA CHIKWENDE SIMBA SC BALAA MTUPU



















