Sunday, 17 January 2021

BODI YA MAZIWA YAIWEKA KIKAANGONI KAMPUNI YA MAZIWA YA COWBELL


Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa Ndugu, Noely Byamungu amesema wamekamata kiasi cha Tani 4 za maziwa ya unga aina ya Miksimiksi ambayo yameiingia nchini bila vibali kwenye ghala la kiwanda cha kufungasha Maziwa ya unga aina ya Cowbell kilichopo cha Uruwira– Chang’ombe, wilaya ya Temeke kinachomilikiwa na Kampuni ya Hawaii products Supplies Limited.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Ndugu Byamungu amesema walibaini ukiukwaji mkubwa wa Sheria, Kanuni na Taratibu zinazosimamia Tasnia ya Maziwa unaofanywa na Kampuni ya Hawaii Products Supplies Limited ambayo iliingiza maziwa hayo nchini bila kupata kibali cha uingizaji wa maziwa ili kukwepa tozo.

Vilevile Ndugu Byamungu amesema katika ukaguzi huo walibaini kilo 3661.2 zimeongezewa muda wa kuisha matumizi kutoka tarehe 24.10.2021 kwakipiga chapa mpya ya tarehe ya mwisho wa matumizi ya bidhaa hizo hadi tarehe 24.8.2022 kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa afya za walaji.

Pia, jumla ya kilo 2592 zitokanazo na ujazo wa makopo yenye ujazo wa gramu 400 kilamoja yamefungashwa upya na kutengeneza boksi (carton) 1440 zenye pakiti ndogondogo 400 kwa kila carton zimepigwa chapa ya tarehe ya mwisho wa matumizi hadi 24.8.2022.

Kutokana na utaratibu huo unaofanywa na kampuni ya Hawaii products Supplies Limited, Bodi ya Maziwa ilisimamisha shughuli zote katika kiwanda hicho baada ya kuona udanganyifu na uvunjaji wa Sheria kwa makusudi.

“ Vitendo hivi havikubaliki, havivumiliki wala kuruhusiwa kwa mujibu wa sheria, hivyo sheria itachukua mkondo wake kwa wahusika” Alisema

Mmiliki wa kampuni ya Hawaii products Supplies Limited Bw. Ahmed Suleiman pamoja Meneja uzalishaji wa Kiwanda Bw. Ahmed Amanzi waliwekwa chini ya ulinzi na uangalizi wa polisi katika kituo cha polisi cha Chang’ombe kwa ajili ya mahojiano na kukamilisha taratibu za kisheria.

Share:

SUNGUSUNGU, MUUGUZI MBARONI KWA WIZI WA DAWA ZAHANATI NA KUZIUZA NYUMBANI..ZIMO ZILIZO 'EXPIRE'


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba
**
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linamshilikilia sungusungu wa kijiji cha Nyamalogo Fedson Matekele na William Desdez (27) muuguzi wa zahanati ya Nyamalogo kwa kosa la wizi wa dawa za binadamu katika zahanati hiyo iliyopo katika kata ya Nyamalogo wilaya ya Shinyanga na kuziuza nyumbani. 

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba tukio hilo limetokea Januari 12,2021 majira ya saa tisa kamili alasiri katika kijiji cha Nyamalogo, kata ya Nyamalogo, tarafa ya Nindo, halmashauri ya wilaya ya Shinyanga. 

Kamanda Magiligimba amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa dawa hizo zabinadamu ziliibiwa zahanati ya Nyamalogo na kwamba baadhi ya dawa hizo zimekwisha muda wake wa matumizi 'Zime - expire' lakini zimekuwa zikiuzwa na mtuhumiwa Fedson Matekele. 

Akifafanua zaidi kuhusu tukio, Kamanda Magiligimba amesema siku ya tukio uongozi wa kijiji cha Mwang'osha ulipokea taarifa kwamba kuna dawa za binadamu mali ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinauzwa nyumbani kwa mtuhumiwa Fedson Matekele ambaye ni sungusungu wa kijiji cha Nyamalogo. 

“Kufuatia tukio hilo jeshi la polisi mkoani Shinyanga kwa kushirikiana na Kaimu Afisa Mtendaji wa kijiji cha mwang'osha tulifanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao wawili pamoja dawa hizo mbalimbali za binadamu ambazo ni Depoprovera -Zivals ,Mrdt-23-strip,Ors-2 satchets, Female condoms o3pcs, Benexylpenillis injection 2 vial , Furasemicle injection 4 amps, Butter sd , Bioline 4 bottle ,baadhi ya dawa hizo zimekwisha muda wake wa matumizi lakini zimekuwa zikiuzwa na mtuhumiwa Fedson”,ameeleza Kamanda Magiligimba. 

“Watuhumiwa watafikishwa mahakamani baada ya kukamilisha uchunguzi.Natoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Shinyanga waendelee kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa kutoa taarifa za uharifu na wahalifu”,ameongeza.
Share:

Procurement and Supplies Officer at Uhuru Hospitals Group

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Procurement and Supplies Officer     Uhuru Hospitals Group Is a private Group of Hospitals established back In 2014 October In Mwanza Region. Since its establishment It has continued to observe a tremendous growth it being contributed upon by the quality of services which creates an Increasing demand. As of current the Uhuru Hospitals Group Is […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Assistant Accountant at Uhuru Hospitals Group

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Assistant Accountant    Uhuru Hospitals Group Is a private Group of Hospitals established back In 2014 October In Mwanza Region. Since its establishment It has continued to observe a tremendous growth it being contributed upon by the quality of services which creates an Increasing demand. As of current the Uhuru Hospitals Group Is aiming at […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Transportation Support at UNDP

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Transportation Support    BACKGROUND Under the guidance and supervision of the Administrative Assistant-Transport, the Driver provides reliable safe driving services to UNDP staff and other high-ranking UN officials and visitors ensuring highest standards of discretion and integrity, sense of responsibility, excellent knowledge of protocol and security issues. The Driver also demonstrates a client-oriented approach, courtesy, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Marketing & Business Analyst Officers at Job Junction

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Marketing & Business Analyst Officers   Details Business / Employer name JOB JUNCTION TANZANIA Job Level Mid level Work Type Full Time Minimum Qualification :Diploma/Bachelor Years of Experience 1 years Location: Dar Es Salaam The responsibilities will include: a. Business Development   Perform competitive analysis and identify gaps and opportunities in the marketplace for new products […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

M&E Advisor at IMA World Health

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job title: M&E Advisor, NTD (Secondment to TZ NTD Control Program – NTDCP)   Reports to: NTDCP Program Manager and Act|East Team Leader Employment Type: Full-Time /Fixed-Term Open to Expatriates and TCNs: No Location: NTDCP office in Dodoma, Tanzania (with up to 30% of in-country travel) About IMA: IMA World Health (IMA) is a member […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Leader, Living with Big Cats Initiative at WWF

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Leader, Living with Big Cats Initiative    About the job Want to make a positive difference to the future of people and our one shared home, the Earth? Working at WWF could be your opportunity of a lifetime. All around the world, people are waking up to the deepening crisis of nature loss. A growing […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Human Resource Manager at KKKT

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Human resource manager / Afisa Utumishi at KKKT January, 2021. The Evangelical Lutheran Church in Tanzania (ELCT) is the federation of Lutheran churches in Tanzania and one of the largest Lutheran denominations in the world, with more than 6 million members. The church is led by a presiding bishop and twenty-five diocesan bishops, representing 26 […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MEL Advisor at Crown Agents

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

MEL Advisor     1. Introduction Accelerating the Su­stainable Control and Elimination of NTDs (ASCEND) is a £200 million invest­ment from the UK government’s Department for International Development (DFID), to advance the impact and su­stainability of national programmes tackling neglected tropical diseases (NTDs). To be implemented between September 2019 to March 2022, ASCEND comprises of two […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Requestor/Material Planner at Serengeti Breweries Limited

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Requestor/Material Planner    About Us From Arthur Guinness to Johnnie Walker, our business was founded on people of great character, and in 250 years, nothing’s changed. We’re the world’s leading premium alcohol company. Our brands are industry icons. And our success is thanks to the strength of our people, in every role. It’s why we […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Manager; Energy Power & Utilities Sector at NMB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Senior Manager; Energy Power & Utilities Sector     Job Purpose To lead the Energy, Power & Utilities sector, providing leadership and support to relationship managers within the sector to drive growth across Corporate Banking businesses and providing strategic solutions for the clients.   Main Responsibilities   Manage Relationship Managers to ensure that work standards, quality […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

BUTONDO AFANYA ZIARA KUKAGUA UJENZI WA MADARASA NA MABARA KISHAPU...AMWAGA MAMILIONI YA FEDHA

Mbunge wa Jimbo  la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo mwenye nguo za bluu akishiriki ujenzi wa madarasa
**
Mbunge wa Jimbo  la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo amewapongeza wananchi kwa nguvu kazi na michango ya fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na maabara wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga.

Mhe. Butondo ametoa pongezi hizo alipokuwa kwenye  ziara yake ya siku mbili Jimboni humo ambapo alizindua kamati ya mfuko wa Jimbo na kutambulisha kikao cha kwanza kupitia mwenyekiti wa mfuko huo.

 Kikao hicho kiliazimia kutoa fedha kwa ajili ya kufunga mkono miradi ya maendeleo iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi hasa maabara na madarasa kwa lengo la kutekeleza agizo la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa la kuongeza Madarasa ili ifikapo Februari 2021 wanafunzi wapate mazingira mazuri ya kujisomea.

Katika ziara yake alitembelea tarafa ya Kishapu, Negezi na Mondo ambapo jumla ya miradi ya maendeleo 15 wilayani Kishapu imenufaika na mfuko huo wa Jimbo huku jumla ya kiasi cha fedha Tsh. Milioni 42, 612,000/= kilitolewa na Mhe. Butondo kupitia mfuko wa Jimbo. 

Fedha hizo zitaenda kukamilisha ujenzi wa madarasa na maabara ambayo yameanzishwa kwa nguvu za wananchi ikiwa ni kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano elimu bure.

Aidha, Mhe. Butondo ameunga mkono mradi wa Ujenzi wa Ofisi ya Makao Makuu ya Polisi Wilaya ya Kishapu iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi.

 Kadhalika, Mhe. Butondo amepongeza na kuwashukuru a wananchi wa Jimbo la Kishapu kwa kuwachagua kwa kushindo Rais, Wabunge na madiwani katika uchaguzi Mkuu uliopita na kuahidi kuwatumikia kwa nguvu zote. 

"Wananchi wa Jimbo la Kishapu mlinichagua kwa kuwa mna imani na Mimi, naomba tushirikiane ili kwa pamoja tuweze kujiletea maendeleo katika Jimbo letu, namba tushikane mkono hasa katika mradi mkakati huu wa ujenzi wa vyumba vya madarasa ili watoto wetu wapate elimu kwenye mazingira rafiki", alisema Butondo.

Aidha, Mbunge huyo amewaasa viongozi wa ngazi zote kuanzia kata, vijiji na vitongoji kusoma taarifa za mapato na matumizi kwa wananchi kupitia vikao na mikutano ya hadhara kwani kufanya hivyo kutawajengea uaminifu na wananchi wao.

Katika ziara hiyo alisisitiza pia suala la usimamizi wa thamani ya fedha kutokana na utekelezaji wa miradi na kuwataka wataalamu ngazi ya Halmashauri kusimamia ujenzi uwe katika kiwango kinachotakiwa ili miradi hii iweze kudumu muda mrefu.
Mbunge wa Jimbo  la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo mwenye nguo za bluu akishiriki ujenzi wa madarasa

Share:

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU UUZAJI NA ULAJI WA NYAMA YA NGURUWE 'KITIMOTO' KAHAMA


Na Salvatory Ntandu - Kahama
Kufuatia kutokea kwa mlipuko wa ugonjwa wa homa ya nguruwe wilayani Kahama mkoani Shinyanga Serikali imelazimika kupiga marufuku, uuzaji, usafirishaji na ulaji wa nyama ya nguruwe kwa muda usiojulikana baada ya kuripotiwa ugonjwa huo kusambaa kwa kasi na kusababisha vifo vya wanyama hao zaidi ya 800.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha wakati akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na hatua zilizochukuliwa na serikali baada ya kujitokeza kwa ugonjwa huo na namna walivyojipanga kuudhibiti ili usiendee kuleta madhara kwa wafugaji.

Alisema kuwa wamelazimika kuchukua hatua hiyo ili kudhibiti kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa huo ambao unaua wanayama aina ya nguruwe kwa kasi na watakaobainika kukiuka agizo hilo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

“Kwa sasa Kahama biashara ya wanyama aina ya nguruwe imepigwa marufuku, lengo letu ni kudhibiti ugonjwa huu,wataalamu wetu wanaendelea kufanya utafiti ili kuhakikisha wanaudhibiti mapema ili kuzuia madhara yasijitokeze zaidi,”alisema Macha.

Sambamba na hilo Macha aliwataka walaji wa nyama ya nguruwe kuacha kula nyama hiyo hadi watakapotangaziwa na serikali na badala yake watumie vitoweo vya wanyama wengine kama vile ng’ombe,mbuzi,kondoo na kuku ambapo ugonjwa huu hujawaathiri.

Kwa upande wake mkuu wa Idara ya Mifugo wa Halmashauri ya Mji Kahama Dk. Damin Kilyenyi alikiri kuwepo kwa ugonjwa wa homa ya nguruwe na kusema kuwa unasababishwa na mwingiliano wa nguruwe pori na wanaofungwa nyumbani na kwa Kahama uliwahi kujitokeza mwaka 2017 na kuwataka wafanyabiashara kuwa na subira wakati suala hilo likitafutiwa ufumbuzi wa kina.

“Ugonjwa huu unawaathiri wanyama aina ya nguruwe tu, na hauna madhara kwa binadamu na wanyama wengine dalili zake ni mnyama kuacha kula,kutokwa damu damu masikioni na kwenye macho na huishi kwa siku tatu ndio anapoteza maisha,”alisema Kilyenyi.

Aliongeza kuwa mpaka sasa ugonjwa huo hauna chanjo wala dawa na mnyama akipata lazima afe na kuwataka wafugaji kuchukua tahadhari ikiwa ni pamoja na kuwatenga wanyama ambao wameonekana na dalili za ugonjwa huo ili kudhibi usienee kwa wengine.

Evans John Kishiwa ni mfugaji wa nguruwe katika mtaa wa Mhongolo alisema kuwa mpaka sasa nguruwe 17 katika banda lake wamekufa kutokana na ugonjwa huo na kuiomba serikali kulitafutia ufumbuzi wa kina ili mifugo yao isiendelee kuangamia.

“Nguruwe akipata ugonjwa huu anaanza kutetemeka,hali chakula, anatokwa damu masikioni na kwenye macho,anaanza kubadilika rangi na baada ya hapo hufa ghafla,nimepata hasara ya zaidi ya shilingi milioni 2",alieleza.

Wilaya ya Kahama inatajwa kuwa na wafugaji wengi wa wanyama hao huku idadi ya nguruwe ikitajwa kufikia 2000 .

Share:

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA GEOFFREY MWAMBE ATAKA WAHITIMU CBE WAJIENDELEZE KIELIMU


Waziri wa Viwanda na Biashara Geoffrey Mwambe akizungumza kwenye mahafali ya 13 ya Chuo Cha Biashara (CBE) Kampasi ya Mwanza Januari 16 2021

Na Hellen Mtereko Mwanza

Waziri wa Viwanda na Biashara Geoffrey Mwambe amewataka wahitimu wa Chuo Cha Biashara (CBE) kuhakikisha wanajiendeleza kielimu katika ngazi tofauti na kuwa wabunifu ili kuacha dhana ya kuajiriwa.

Hayo aliyasema jana Januari 16 2021 wakati akizungumza kwenye  mahafali ya 13 ya chuo hicho kampasi ya Mwanza. 

Mwambe alisema wahitimu wenye Diploma wajiendeleze ili wafike ngazi ya Stashahada ili kuweza kuwa na nchi yenye wasomi watakaokuja kusaidia taifa.

Aliwataka wahitimu kutumia utalamu wao walioupata  kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii .

 Aliomba mashirika binafsi na ya Serikali yalete  wafanyakazi wao  ili waweze kupata Elimu katika chuo hicho. 

Aidha alisema Serikali itaboresha miundombinu ya Elimu katika vyuo vya CBE nchini kutokana na ongezeko la Wanafunzi wenye uhitaji wa kujiendeleza na sera ya Elimu bure inayoendelea kuinua wasomi wengi.

Aliiomba CBE kuhakikisha inafungua kampasi katika maeneo ya nyanda za Kaskazini na Kusini(Ruvuma/Lindi na Mtwara). 

Pia alikiagiza Chuo hicho kuhakikisha kinakuja na mkakati  wa Kukuza Ujasiriamali ili kupata wafanya biashara wenye Elimu na ujuzi kutoka chuoni hapo.

Mkuu wa Chuo cha CBE,Kampasi ya Mwanza Profesa Emmanuel Mjema alisema jumla ya wahitimu 447 wamehitimu katika ngazi tofauti. 

Mjema alisema chuo chao kipo katika mkakati wa kuweza kuanzisha kozi mpya ya Stashahada ya masoko na Utalii ili kwendana na kasi iliyopo.

Alisema Chuo chao kipo kwenye mkakati wa kuanzisha chuo  katika mkoa wa Iringa na Zanzibar kutokana na maombi mengi anayopokea kutoka kwa wananchi wenye kufahamu umuhimu wa Elimu.

Aliipongeza Serikali kwa kuwezesha kuongeza bajeti ya mikopo kwa Elimu ya juu ambapo na Chuo chao kimenufaika pia  ameipongeza Serikali kwa kuwalipia fedha za kununua eneo la chuo hicho katika eneo la Kangae mkoani Mwanza
Share:

Tanzia : MSANII WA BONGO FLEVA CPWAA AFARIKI DUNIA

Msanii Cpwaa enzi za uhai wake
Msanii wa Bongo Fleva Ilunga Khalifa maarufu 'C Pwaa'amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumapili Januari 17,2021 akiendelea na matibabu katika hospitali ya taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam.
CPWAA ambaye aliwahi kuunda kundi la Park Lane akiwa na msanii mwenzake Suma Lee kabla ya kundi hilo kuvunjika mwanzoni mwa miaka ya 2000.
Tutawaletea taarifa zaidi hivi punde
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 17,2021

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger