Monday, 23 November 2020
VSO YATOA VIFAA KWA WAHITIMU VETA WAKAJIAJIRI WENYEWE
MEYA SINGIDA AJIVUNIA KUIACHA MANISPAA IKIWA NA HATI SAFI
Na Godwin Myovela, Singida
MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Singida aliyemaliza muda wake, ambaye ni Diwani wa Kata ya Mtamaa mkoani hapa, Gwae Chima Mbua, amesema mpaka sasa anajivunia kuiacha manispaa hiyo ikiwa inashikilia cheti cha hati safi kutokana na usimamizi madhubuti uliojengwa katika misingi ya nidhamu, hususan kwenye eneo la makusanyo na matumizi ya fedha za umma.
Akizungumza na vyombo vya habari mkoani hapa leo, vilivyomtaka aeleze kwanini anastahili tena kupewa dhamana ya nafasi ya umeya na si diwani mwingine, alijibu kila mgombea hupimwa kwa uwajibikaji wake na sio kimitazamo wala mihemko.
Alisema mpaka alipokabidhi ofisi hiyo hivi karibuni, aliacha manispaa hiyo ikiwa kwenye makusanyo ya takribani asilimia 83, sambamba na kufanikiwa kuwaunganisha madiwani na watumishi katika kuendelea kuijenga Singida kwa kasi na muktadha unaoendana na maono ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli.
“Nawashukuru madiwani na serikali walinipa ushirikiano mkubwa sana, lakini nidhamu, uadilifu na kasi tuliyokwenda nayo vilichochea kasi ya maendeleo yetu hadi kuzivutia hata halmashauri nyingine zipatazo 19 kutoka maeneo tofauti nchini kuja kujifunza- hasa kupitia umahiri wa mradi wa stendi ya misuna,” alisema Mbua.
Alisema mpango uliopo kama atapata ridhaa ya kuchaguliwa tena, ni kuchagiza kwa kuharakisha mchakato wa maboresho ya soko la vitunguu kwa kuhakikisha linawekewa miundombinu ya kisasa ikiwemo zege na lami kwenye barabara zinazolizunguka ili kuondoa kero ya tope na mazingira yasiyo rafiki hasa wakati wa mvua.
Alisema tayari manispaa hiyo imefanikiwa kufungua akaunti maalumu ya mikopo ya akina-mama, hivyo jukumu lililo mbele yake kama atapata ridhaa ni kuimarisha fursa hiyo kwa ustawi wa maisha ya wanawake wa singida, lakini shabaha kubwa ni kuhakikisha makusanyo yanapanda kwa zaidi ya asilimia 83.
Mbua alisisitiza kama atachaguliwa tena ataendelea kuhamasisha nidhamu ya matumizi ya fedha kama alivyofanikiwa kwa miradi mbalimbali iliyotangulia, ikiwemo ule wa fedha zilizotolewa na serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali.
“Tunakwenda vizuri na kwa kasi ya aina yake, natamani kuiona singida ikiwa jiji…kwa sasa kuna maeneo fulani tayari yameshaanza kuitwa Ubungo, naitamani singida isiyo na rushwa, singida ya maendeleo ya kweli,” alisema Diwani huyo wa Mtamaa na kuongeza:
“Bado kuna mambo mengi ya kuweka sawa mathalani pale stendi bado tunahitaji kufunga CCTV Camera, lakini tunahitaji kukamilisha mchakato wa kutenga maeneo ya viwanda, kupima viwanja zaidi, kujenga machinjio ya kisasa, kuboresha mifumo ya ukusanyaji taka, pamoja na kuboresha soko letu la vitunguu.”
Mipango mingine iliyopo kama atapata ridhaa ni kuhakikisha anasukuma kwa kasi ujenzi wa soko la kisasa litakalojengwa eneo la Mandewa nje kidogo ya manispaa hiyo, sambamba na kuboresha ‘High Schools’ za Mungu Maji na Mandewa, juhudi ambazo anashukuru kwamba zinaungwa mkono na serikali.
“Nina nia njema ya kuwatendea haki watu wa manispaa ya Singida kwa nafasi ya Meya, suala kubwa ni kuleta maendeleo na faraja,..lakini pia kuunga mkono kwa vitendo kasi ya mheshimiwa Rais katika kuifanya manispaa yetu kuendelea kuwa njema tena njema sana,” alisema Gwae Mbua.
MRADI WA MAJARIBIO WA KILIMO CHA MTAMA WA TBL PLC , FTMA, WFP WANUFAISHA WAKULIMA 1,300 NCHINI
Graduate Management Trainee Program at Diamond Trust Bank (DTB) Tanzania
EXCITING CAREER OPPORTUNITIES IN DIAMOND TRUST BANK TANZANIA DTB Graduate Management Trainee Program 2020 Overview Program Descriptions Diamond Trust Bank has today grown into a leading commercial bank offering a wide spectrum of banking services. With 28 operational branches in Tanzania, Diamond Trust Bank Tanzania is now looking for capable individuals who have the […]
The post Graduate Management Trainee Program at Diamond Trust Bank (DTB) Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.
Human Resource and Administration Manager at Wildlife Conservation Society (WCS)
Human Resource and Administration Manager Wildlife Conservation Society Job Summary Under the general supervision of the Country Director, the incumbent shall facilitate the achievement of organizational objectives by providing organizational development services, sourcing, developing, managing and retaining quality human resources for the operations of WCS-Tanzania. Job Description/Requirements Reports to: Country Director, Tanzania Location: Mbeya, Tanzania […]
The post Human Resource and Administration Manager at Wildlife Conservation Society (WCS) appeared first on Udahiliportal.com.
General Manager at Golden Tulip Hotels, Suites & Resorts
General Manager Company Name Golden Tulip Hotels, Suites & Resorts Company Location Dar es Salaam, Tanzania Job Description: The ideal candidate will have experience leading a team and managing the daily operation of the business. They will be responsible for maintaining the standard of work from employees as well as onboarding and hiring new […]
The post General Manager at Golden Tulip Hotels, Suites & Resorts appeared first on Udahiliportal.com.
Asset at Orica, Operator
Operator – Asset Orica Bubada, Geita, Tanzania Orica is the world’s largest provider of commercial explosives and innovative blasting systems to the mining, quarrying, oil and gas and construction markets, a leading supplier of sodium cyanide for gold extraction, and a specialist provider of ground support services in mining and tunnelling. Orica has a diverse […]
The post Asset at Orica, Operator appeared first on Udahiliportal.com.
Call for Tender at AFYA Micro Finance Company Limited (AMiF)
AFYA Micro Finance Company Limited (AMiF) TENDER – LOAN MANAGEMENT SOFTWARE Job Summary AFYA Micro Finance Company Limited (AMiF) is a specialized Microfinance Institution that provides affordable to the private health care providers in Tanzania. AMiF targets the lower end market in the health sector, in particular, Accredited Drug Dispensing Outlets (ADDOs), Pharmacies, dispensaries, small clinics, […]
The post Call for Tender at AFYA Micro Finance Company Limited (AMiF) appeared first on Udahiliportal.com.
Rise Programs Coordinator at Grumeti Fund Trust
RISE PROGRAMS COORDINATOR Description DEPARTMENT: RESEARCH AND INNOVATION FOR THE SERENGETI ECOSYSTEM (RISE) DUTY STATION: GRUMETI, MARA REGION, TANZANIA REPORTING: LINE HEAD SCIENTIST – RISE DUTIES AND RESPONSIBILITIES: Support on-going research programs via field data collection, updating records, and data maintenance. Summarize and analyze data regularly, providing project oversight and contributing to routine reports. Develop […]
The post Rise Programs Coordinator at Grumeti Fund Trust appeared first on Udahiliportal.com.
GIS And Data Analysis Specialits at Grumeti Fund Trust
GIS AND DATA ANALYSIS SPECIALIST Details Description The Grumeti Fund Trust’s Research & Monitoring department is looking for a highly qualified and motivated candidate to be recruited for the position of GIS and Data Analysis Specialist. This is a management role within the department and the specialist will be expected to also fulfill the […]
The post GIS And Data Analysis Specialits at Grumeti Fund Trust appeared first on Udahiliportal.com.
ARTISAN II 4 POSTS Transfer Vacancies/ at Mbeya University
Mbeya University of Science and Technology (MUST) is a result of the transformation of the Mbeya Institute of Science and Technology (MIST) through the Universities Act No.7 (2005) and Charter of Mbeya University of Science and Technology, 2013 with the aim of becoming the leading centre of excellence for knowledge, skills and applied education in […]
The post ARTISAN II 4 POSTS Transfer Vacancies/ at Mbeya University appeared first on Udahiliportal.com.
MEDICAL ATTENDANT II Transfer Vacancies at Mbeya University
Mbeya University of Science and Technology (MUST) is a result of the transformation of the Mbeya Institute of Science and Technology (MIST) through the Universities Act No.7 (2005) and Charter of Mbeya University of Science and Technology, 2013 with the aim of becoming the leading centre of excellence for knowledge, skills and applied education in […]
The post MEDICAL ATTENDANT II Transfer Vacancies at Mbeya University appeared first on Udahiliportal.com.
Sunday, 22 November 2020
WAKULIMA PERAMIHO WAIPOKEA SHERIA YA TAIFA YA UMWAGILIAJI
Picha ni Bw. Daudi Mkoma Mtaalam kutoka katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Mkoani Ruvuma, akiongea katika mkutano na wakulima wa skimu ya Umwagiliaji ya Nakahuga iliyopo Peramiho wilayani Songea.
baadhi ya wakulima wa kilimo cha umwagiliaji katika kijiji cha Nakahuga wakifuatilia mkutano na wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.Mkulima katika skimu ya kilimo cha uwagiliaji ya Nakahuga iliyopo Peramiho wilayani Songea Bw. Albert Mtani akiuliza swali wakati wa mkutano na wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.
Na Mwandishiwetu – Peramiho
Wakulima katika skimu ya kilimo cha umwagiliaji ya Nakahuga iliyopo Peramiho wilayani Songea mkoani Ruvuma wameipokea sheria ya Taifa ya kilimo cha umwagiliaji na kuonesha utayari wa kuchangia katika mfuko wa maendeleo yakilimo cha umwagiliaji kwa kukiri kuilewa sheria hiyo mara baada ya mafunzo waliyopata toka kwa wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.
Akizungumza wakati wa mkutano wa majumuisho uliofanyika katika kijiji cha Nakahuga,mmoja wa wakulima hao Bw. Albert Mtani alisema kuwa kilimo cha umwagiliaji kwao ni mkombozi kwani ni kilimo cha uhakika.
“Binafsi ninaishukuru serikali kwa kuleta mradi huu nani naamini inania njema ya kuendelea kuboresha miondombinu katika skimu hii na kwa kuwa tunapata faida nyingi zitokanazo na shughuli zetu zakilimo, hivyo sio ni tatizo kwenye uchangiaji katika mfuko kwani ninaamini kuwa mifereji itakapo haribika kwa namna yoyote ile serikali itaitengeneza kupitia mfuko huo, na tutaendelea na shughuli zetu za kilimo bila wasiwasi.” Alisema.
Sambambana hilo kwa nyakati tofauti katika ushiriki wa mkutano huo, baadhiya wakulima walisikika wakisema kuwa Sheria ya Taifa ya Umwagiliaji sasa imekaa vizuri kwani kabla yakuwepo kwa sheria hiyo ushirikishwaji wa wakulima kuhusu shughuli za umwagiliaji ulikuwa ni mdogo na kulikuwa na usimamizi mbovu wa miundombinu yaumwagiliaji
Waliongeza kwa kusema kuwa sheria ya Taifa ya umwagiliaji pia itaweza kusaidia kutatua migogoro midogo midogo iliyopo katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji.
SPRF INAVYOSHIRIKISHA WANAFUNZI KUTOKOMEZA UKATILI
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Siuyu wakifuatilia mafunzo hayo.
Kaimu Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Ikungi, Paul Mgelwa akifuatilia mafunzo hayo, kulia ni wanafunzi wa Shule ya Sekondari Siuyu.
Mratibu wa Mradi kutoka SPRF, Mwalimu Bernard Maira akizungumza na wanafunzi wa sekondari ya Siuyu (hawapo pichani)
Mratibu wa Mradi kutoka SPRF, Mwalimu Bernard Maira akizungumza na wanafunzi wa sekondari ya Siuyu wakati wa mafunzo hayo.
Na Godwin Myovela, Singida
MATUKIO ya unyanyasaji wa kijinsia kwa wasichana wenye umri mdogo, ikiwemo mimba na ndoa za utotoni, vitendo vya ukeketaji na ubakaji yameendelea kupungua katika wilaya ya Ikungi mkoani hapa- huku sababu kubwa ikitajwa kuwa ni matokeo ya ushirikishaji wa makundi rika katika kupambana na vita hiyo ndani ya jamii, imeelezwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la Kiserikali la Stars of Poverty Rescue Foundation (SPRF) nchini, Dkt Suleiman Muttani, aliyasema hayo jana muda mfupi baada ya shirika hilo kutembelea na kufanya mijadala ya pamoja kwa kushirikisha shule za sekondari Munkinya na Siuyu zilizopo wilaya ya Ikungi, mkoani hapa.
“Tumeunda ‘Clubs’ za wanafunzi mashuleni ambao pamoja na mambo mengine tunawapa fursa ya kuchagua viongozi, tunawajengea uwezo na kuwasimamia kutengeneza mpango kazi ambao unawasaidia katika kuwawezesha kufichua na kupeana elimu ya matukio ya kutokomeza ukatili, mimba na ndoa za utotoni wao kwa wao,” alisema Muttani.
Afisa Ufuatiliaji na Tathmini wa shirika hilo, Mwedinuu Beleko, akiwasilisha mada kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wanafunzi wa shule hizo, aliitaka jamii kujitokeza haraka na kutoa taarifa yenye ushahidi pindi matukio ya ukatili yanapojitokeza ili kurahisisha mwenendo wa shauri.
“Nawaomba wanafunzi msiogope, wala msitishwe na mtu yeyote tukio lolote la ukatili linapojitokeza basi hakikisheni aliyefanyiwa ukatili huo anashiriki mara moja katika kutoa taarifa yenye ushahidi…na msipoteze huo ushahidi na vielelezo vyote ili kuharakisha mchakato wa kesi kuendelea kwa wakati,” alisema Beleko.
Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii wilayani hapa, Paul Mgelwa aliwasihi wanafunzi kuwa makini na kutodanganyika ili kukabiliana na mimba zisizotarajiwa ambazo hufifisha ndoto na matarajio yao-na kusisitiza kuwa daima wanapaswa kuweka kipaumbele cha elimu kwanza kwa kuzingatia elimu ndio ukombozi wa maisha katika kupambana na umasikini.
Katibu wa Shirika hilo, Dkt Mwajuma Mikidadi alisema malengo ya SPRF, ambayo miradi yake ipo chini ya ufadhili wa Foundation for Civil Society (FCS), ni kukuza ushirikiano miongoni mwa wadau na jamii, taasisi za kitaifa na kimataifa katika kutokomeza umaskini wa kipato, sambamba na kuimarisha uwezo wa kitaasisi katika kukua na kutekeleza programu endelevu.
“SPRF na jamii ndio moto wetu kwa sasa, programu hii imesaidia kumfanya kila mwanafunzi wa kike kutambua haki zake, lakini madhara ya mila zilizopitwa na wakati na kandamizi, masuala ya ukeketaji na mimba na ndoa utotoni ndani ya jamii,” alisema Mikidadi.
Mratibu wa mradi huo, Mwalimu Bernard Maira, alisema hata hivyo shirika hilo limefanikiwa kuanzisha Kamati za MTAKUWWA kwenye vijiji 8 zinazopinga Ukatili wa Kijinsia dhidi ya Wanawake na Watoto huku wakihamasisha uanzishwaji wa vikundi mathalani Sauti ya Mwanamke na Sauti ya Mwanafunzi, ambavyo vimekuwa chachu ya mageuzi ya kifikra dhidi ya mila potofu na masuala ya ukatili ndani ya jamii zao.
MBUNGE MTATURU AWASHUKURU WANANCHI WA SINGIDA MASHARIKI,ATAJA VIPAUMBELE SABA ATAKAVYOANZA NAVYO

Gari la Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu akiwasili katika jimbo hilo kwa ajili ya kuwashukuru wananchi kwa ushindi waliompatia.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akipokelewa kwa shangwe na mafaruko ya wananchi wake na Chama cha Mapinduzi(CCM) kutoka Bungeni Dodoma,alipowasili jimboni kwake kutoa shukrani za ushindi wa CCM.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akifurahia na wananchi wake pamoja na Chama cha Mapinduzi(CCM) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.


MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akicheza ngoma baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwa na Mwenyekiti Wilaya ya Ikungi ,Mika Likapakapa wakipiga makofi kwa vikundi vya ngoma (havipo pichani) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akvishwa vitu vya kimila na Wazee baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwashukuru wananchi wake pamoja na Chama cha Mapinduzi(CCM) kwa kumpatia zawadi mara baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwa ameshikiria silaha za jadi baada ya kukabidhiwa na Wazee mara baada ya kuwasili jimboni huko akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Mzee Maarufu Ikungi Bw.Hussein Sungita akitoa neno kwa Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,(hayupo pichani) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Katibu wa Wilaya ya Ikungi Kangaeli Akyoo akizungumza na wananchi waliojitokeza kumpokea Mbunge wao wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu mara baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Mwenyekiti wa wilaya ya Ikungi Mika Likapakapa akiongea na umati wa wananchi wa wa Jimbo la Singida Mashariki, waliojitokeza kumpokea Mbunge wao Miraji Mtaturu baada ya kuwasili jimboni huko akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Mama wa Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu, Mariam Sepetu
Mama wa Miss Tanzania 2006/07 ,Wema Sepetu,Mariam Sepetu ,akielezea furaha aliyonayo baada ya Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu kuchaguliwa tena kuwa Mbunge na anaamini kuwa ataendelea kuwatumika wananchi mpaka aatakampochoka mwenyewe kuliongoza jimbo hilo.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwahutubia mamia ya wananchi wake pamoja na Chama cha Mapinduzi(CCM) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Sehemu ya wananchi wakifatilia hotuba ya Mbunge wao wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu wakati akiwashukuru na kuwapongeza kwa kumpa ridhaa ya kuwatumikia tena miaka mitano mengine mara baada ya kuwasili jimboni huko akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.
Na.Alex Sonna,Ikungi Singida
Hivi ndivyo unaweza kusema kuwa ni Mafuriko ya wananchi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa Mbunge wao Mhe.Miraji Mtaturu walivyompokea kwa shangwe na furaha baada ya kuwasili katika Jimbo hilo la Singida Mashariki akitokea bungeni Dodoma kwa ajili ya kuwashukuru kwa kumuani tena miaka mitano tena kwa ushindi wa kishindo.
Akizungumza na baada ya kupokelewa na wananchi wake na Chama cha CCM Mhe.Mtaturu amewashukuru wananchi wa jimbo hilo kwa kuendelea kumuamini tena huku akisema kuwa atawatumikia wananchi bila kuwabagua kwa itikadi zao za kisiasa.
Aidha Mtaturu amewambia wananchi kuwa uchaguzi kwasasa umekwisha hivyo wananchi washirikiane kuhakikisha Wilaya ya Ikungi inapata mafanikio na yeye kama kiongozi wao atawatumikia wote bila ubaguzi.
“Tayari Mimi ni Mbunge wenu nipo tayari kushirikiana nanyi, lakini pia tujenge mahusiano, tuachane na itikadi zetu za kisiasa sasa tujenge uchumi wa Jimbo la Ikungi, tumechelewa sana,”amesisitiza
Hata hivyo Mhe.Mtaturu ametaja vipaumbele saba atakavyoanza navyo ikiwemo suala la elimu ambapo atasimamia kuhakikisha watoto wanapata elimu bora,Maji,Umeme,Afya pamoja na miradi iliyopo inatekelezwa na kuibua mingine.
Aidha Mhe.Mtaturu amewahamasisha akinababa kuunda vikundi vya wakulima ili waweze kupata mikopo itakayosaidia kuinua kilimo chao katika wilaya ya Ikungi na pia wataweza kupata mikopo wakiunda vikundi hivyo.










