Monday, 23 November 2020

VSO YATOA VIFAA KWA WAHITIMU VETA WAKAJIAJIRI WENYEWE

 

Na Marco Maduhu, Shinyanga
Shirika la Voluntary Services Overseas (VSO), limetoa vifaa kwa wahitimu wa fani mbalimbali kutoka chuo cha ufundi stadi VETA mkoani Shinyanga, ambao walikuwa wakiwafadhili kupata mafunzo chuoni hapo, kwa ajili ya kwenda kujiajiri wenyewe na siyo kutegemea kuajiriwa.

Zoezi la kukabidhi vifaa hivyo lilifanyika kwenye chuo hicho cha ufundi stadi VETA, ambapo wahitimu hao walikuwa wamesomea fani za mapishi, Saluni, Mapambo, Mabomba, Aluminium, umeme, na ufundi pikipiki. 

Mratibu wa mradi wa kuwezesha vijana kiuchumi kutoka Shirika hilo la VSO Josam Katanga, ambao wanajishughulisha na masuala ya kijamii Kanda ya Ziwa, alisema kuwa wamefadhili mafunzo ya ufundi Stadi kwa vijana 200 kutoka mkoani Shinyanga ili kuwapatia ujuzi na kuendesha maisha yao. 

"Shirika letu baada ya kufadhili vijana hawa mafunzo ya ufundi na kuhitimu, tukaona ni vyema kuwaunga kwenye vikundi vya ujasiriamali na kuvisajili, na kuwapatia vifaa ambavyo wataanza navyo kujiajiri wenyewe kulingana na fani zao," alisema Katanga. 

“Vifaa ambavyo tumetoa ni vya Mapishi, Saluni, ushonaji zikiwamo cherehani, ufundi umeme, Aluminium, Mapambo, Mabomba, na pikipiki, ambavyo vijana hawa vitawasaidia kuanzisha shughuli zao na kujipatia kipato, kuliko kurudi nyumbani kukaa kusubiri ajira na hatimaye kupoteza ujuzi wao,”aliongeza. 

Naye Afisa Vijana kutoka halmashauri ya manispaa ya Shinyanga Charles Ruchagula, aliwataka vijana hao licha ya kusajili vikundi vyao, wasisite kwenda kuomba mkopo halmashauri fedha za asilimia 10, ambazo nne kwa vijana zitakazowasaidia kupanua mitaji yao. 

Kwa upande wake Msajili wa wanafunzi Chuo cha Ufundi stadi VETA mkoani Shinyanga Rashid Ntahigiye, aliwataka vijana hao wanapoingia kwenye Soko la kujiajiri wenyewe, wakawe wabunifu kwenye utengenezaji wa bidhaa zao, ili wafanikiwe kupata wateja wengi na kuinuka kiuchumi. 

Nao baadhi ya wahitimu hao akiwamo Magreth Zabron aliyesomea fani ya saluni, walishukuru Shirika hilo kuwafadhili mafunzo hayo pamoja na kuwapatia vifaa vya kuanza kazi, na kuahidi kwenda kujituma kuchapa kazi kwa ajili ya mustakabali wa maisha yao, na hawato waangusha. 

TAZAMA PICHA HAPA CHINI 
Mratibu wa mradi wa kuwezesha vijana kiuchumi kutoka Shirika hilo la VSO Josam Katanga, akikabidhi vifaa kwa wahitimu wa fani ya ushonaji kwa ajili ya kwenda kujiajiri wenyewe.
Mratibu wa mradi wa kuwezesha vijana kiuchumi kutoka Shirika hilo la VSO Josam Katanga, akikabidhi vifaa kwa wahitimu wa fani ya Aluminium, ili kwenda kujiajiri wenyewe.
Mratibu wa mradi wa kuwezesha vijana kiuchumi kutoka Shirika hilo la VSO Josam Katanga, akikabidhi vifaa kwa wahitimu wa fani ya mapambo na salooni ili kwenda kujiajiri wenyewe.
Zoezi la kubidhi vifaa likiendelea.
Zoezi la kubidhi vifaa likiendelea , kwa wahitimu wa fani ya mapishi.
Watendaji wa shirika la VSO, wakiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Serikali manispaa ya Shinyanga na chuo cha ufundi stad VETA Mkoani Shinyanga, wakwati wa hafla ya kukabidhi vifaa kwa wahimitu wa fani mbalimbali chuoni hapo. waliofadhiliwa masomo yao na VSO.
Picha ya pamoja wahitimu wa VETA, watendaji wa Shirika la VSO, watumishi wa Serikali na VETA.
Mratibu wa mradi wa kuwezesha vijana kiuchumi kutoka Shirika hilo la VSO Josam Katanga, akizungumza kwenye hafla hiyo ya kukabidhi vifaa kwa wahitimu wa mafunzo VETA.
Msajili wa wanafunzi chuo cha ufundi stadi VETA mkoani Shinyanga Rashidi Ntahigiye, akizungumza kwenye hafla hiyo ya kukabidhi vifaa kwa wahitimu chuoni hapo waliofadhiliwa mafunzo yao na Shirika la VSO.
Afisa vijana kutoka halmashauri ya manispaa ya Shinyanga Charles Ruchagula, akizungumza kwenye hafla hiyo ya kukabidhiwa vifaa wahitimu VETA.
Afisa mtendaji wa Kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga Joshua Masengwa, akizungumza kwenye hafla hiyo.
Afisa maendeleo Kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga Wema Mashaka, akizungumza kwenye hafla hiyo ya kukabidhiwa vifaa wahitimu wa VETA.
Wahitimu wa fani mbalimbali kutoka chuo cha ufundi stadi VETA Mkoani Shinyanga waliofadhiliwa masomo yao na Shirika la VSO, wakiwa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kwenda kujiajiri.
Wahitimu wa fani mbalimbali kutoka chuo cha ufundi stad VETA Mkoani Shinyanga waliofadhiliwa masomo yao na Shirika la VSO, wakiwa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kwenda kujiajiri.
Wahitimu wa fani mbalimbali kutoka chuo cha ufundi stadi VETA Mkoani Shinyanga waliofadhiliwa masomo yao na Shirika la VSO, wakiwa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kwenda kujiajiri.
Wahitimu wa fani mbalimbali kutoka chuo cha ufundi stad VETA Mkoani Shinyanga waliofadhiliwa masomo yao na Shirika la VSO, wakiwa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kwenda kujiajiri.
Wahitimu wa fani mbalimbali kutoka chuo cha ufundi stad VETA Mkoani Shinyanga waliofadhiliwa masomo yao na Shirika la VSO, wakiwa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kwenda kujiajiri.
Wahitimu wa fani mbalimbali kutoka chuo cha ufundi stadi VETA Mkoani Shinyanga waliofadhiliwa masomo yao na Shirika la VSO, wakiwa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kwenda kujiajiri.
Wahitimu wa fani mbalimbali kutoka chuo cha ufundi stadi VETA Mkoani Shinyanga waliofadhiliwa masomo yao na Shirika la VSO, wakiwa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kwenda kujiajiri.

Na Marco Maduhu- Shinyanga.

Share:

MEYA SINGIDA AJIVUNIA KUIACHA MANISPAA IKIWA NA HATI SAFI


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida aliyemaliza muda wake, ambaye ni Diwani wa Kata ya Mtamaa mkoani hapa, Gwae Chima Mbua (katikati), akiongoza moja ya vikao vya baraza la madiwani.

Na Godwin Myovela, Singida

MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Singida aliyemaliza muda wake, ambaye ni Diwani wa Kata ya Mtamaa mkoani hapa, Gwae Chima Mbua, amesema mpaka sasa anajivunia kuiacha manispaa hiyo ikiwa inashikilia cheti cha hati safi kutokana na usimamizi madhubuti uliojengwa katika misingi ya nidhamu, hususan kwenye eneo la makusanyo na matumizi ya fedha za umma.

Akizungumza na vyombo vya habari mkoani hapa leo, vilivyomtaka aeleze kwanini anastahili tena kupewa dhamana ya nafasi ya umeya na si diwani mwingine, alijibu kila mgombea hupimwa kwa uwajibikaji wake na sio kimitazamo wala mihemko.

Alisema mpaka alipokabidhi ofisi hiyo hivi karibuni, aliacha manispaa hiyo ikiwa kwenye makusanyo ya takribani asilimia 83, sambamba na kufanikiwa kuwaunganisha madiwani na watumishi katika kuendelea kuijenga Singida kwa kasi na muktadha unaoendana na maono ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli.

“Nawashukuru madiwani na serikali walinipa ushirikiano mkubwa sana, lakini nidhamu, uadilifu na kasi tuliyokwenda nayo vilichochea kasi ya maendeleo yetu hadi kuzivutia hata halmashauri nyingine zipatazo 19 kutoka maeneo tofauti nchini kuja kujifunza- hasa kupitia umahiri wa mradi wa stendi ya misuna,” alisema Mbua.

Alisema mpango uliopo kama atapata ridhaa ya kuchaguliwa tena, ni kuchagiza kwa kuharakisha mchakato wa maboresho ya soko la vitunguu kwa kuhakikisha linawekewa miundombinu ya kisasa ikiwemo zege na lami kwenye barabara zinazolizunguka ili kuondoa kero ya tope na mazingira yasiyo rafiki hasa wakati wa mvua.

Alisema tayari manispaa hiyo imefanikiwa kufungua akaunti maalumu ya mikopo ya akina-mama, hivyo jukumu lililo mbele yake kama atapata ridhaa ni kuimarisha fursa hiyo kwa ustawi wa maisha ya wanawake wa singida, lakini shabaha kubwa ni kuhakikisha makusanyo yanapanda kwa zaidi ya asilimia 83.

Mbua alisisitiza kama atachaguliwa tena ataendelea kuhamasisha nidhamu ya matumizi ya fedha kama alivyofanikiwa kwa miradi mbalimbali iliyotangulia, ikiwemo ule wa fedha zilizotolewa na serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali.

“Tunakwenda vizuri na kwa kasi ya aina yake, natamani kuiona singida ikiwa jiji…kwa sasa kuna maeneo fulani tayari yameshaanza kuitwa Ubungo, naitamani singida isiyo na rushwa, singida ya maendeleo ya kweli,” alisema Diwani huyo wa Mtamaa na kuongeza:

“Bado kuna mambo mengi ya kuweka sawa mathalani pale stendi bado tunahitaji kufunga CCTV Camera, lakini tunahitaji kukamilisha mchakato wa kutenga maeneo ya viwanda, kupima viwanja zaidi, kujenga machinjio ya kisasa, kuboresha mifumo ya ukusanyaji taka, pamoja na kuboresha soko letu la vitunguu.”

Mipango mingine iliyopo kama atapata ridhaa ni kuhakikisha anasukuma kwa kasi ujenzi wa soko la kisasa litakalojengwa eneo la Mandewa nje kidogo ya manispaa hiyo, sambamba na kuboresha ‘High Schools’ za Mungu Maji na Mandewa, juhudi ambazo anashukuru kwamba zinaungwa mkono na serikali.

“Nina nia njema ya kuwatendea haki watu wa manispaa ya Singida kwa nafasi ya Meya, suala kubwa ni kuleta maendeleo na faraja,..lakini pia kuunga mkono kwa vitendo kasi ya mheshimiwa Rais katika kuifanya manispaa yetu kuendelea kuwa njema tena njema sana,” alisema Gwae Mbua.

Share:

MRADI WA MAJARIBIO WA KILIMO CHA MTAMA WA TBL PLC , FTMA, WFP WANUFAISHA WAKULIMA 1,300 NCHINI


Mmoja wa wakulima wa zao la Mtama katika eneo la Kibaigwa wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma,Sebastian Msola (Kulia) akitoa maelezo kwa ujumbe kutoka TBL , WFP na FtMA walipofika kumtembelea shambani kwake mwishoni mwa wiki wakati wa tathmini ya mradi wa pamoja wa kuwezesha wakulima wa zao hilo katika mikoa ya Dodoma na Manyara.
Baadhi ya wakulima wa mtama wanawake katika mkutano wa tathmini
****
Bi Hilda Madeje, mkulima wa mtama katika kijiji cha Sagala B kilichopo wilayani Kongwa mkoani Dodoma.sasa ana soko la uhakika la kuuzia magunia 30 ya mtama ambayo ni ongezeko la 70% kulinganisha na miaka ya nyuma.Hali hii imemuwezesha kupata fedha za kutosha kujenga nyumba ya kuishi familia yake na kulipia ada ya shule kwa watoto wake 4.

Bi Madeje ni mmoja wa washiriki wa mradi wa majaribio wa kilimo cha mtama wa kampuni ya bia ya TBL Plc, taasisi ya Farm to Market Alliance(FtMA) na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), ambao ulilenga kuwawezesha wakulima wa mtama mbinu za kisasa za kulima zao hilo kwa kuwapatia mbegu bora za mtama na kuongeza mavuno sambamba na kuwahakikishia soko la uhakika la mavuno yao.

Mradi huu wa ushirikiano ulianza mwezi Januari 2020 ambapo kampuni ya TBL Plc ilikubali kununua mtama unaozalishwa na wakulima mkoani Dodoma, TBL Plc, FtMa na WFP iliwasaidia wakulima hao kupata mbegu ya mtama; bima ya mazao; itifaki za usimamizi wa zao la mtama; huduma za ugani za kilimo; pamoja na ujumuishaji bora na soko la uhakika ili waweze kuongeza mavuno yao.

Akizungumza wakati wa tathmini ya msimu uliopita iliyofanyika mkoani Dodoma wiki iliyopita, Meneja Kilimo wa TBL Plc, Joel Msechu, alisema kuwa TBL Plc ililipa wakulima wadogo jumla ya Tzs 1.75 bilioni kwa ajili ya kununua tani 3,000 za mtama uliozalishwa katika wilaya za Mpwapwa, Kongwa, Kondoa, Bahi na Chamwino mkoani Dodoma, ambapo kila kilo ya mtama ilinunuliwa kwa shilingi 550. "Mradi umekuwa na matokeo mazuri na umewezesha kuboresha maisha ya wakulima wa mtama" aliongeza.

Kwa mujibu wa Msechu kampuni kwa sasa inanunua asilimia 74% ya malighafi zake nchini na imedhamiria kuongeza kiwango cha ununuzi wa malighafi nchini katika miaka ijayo.TBL Plc imejipanga kuhakikisha inashirikiana na wakulima wa mtama wapatao 6,000 katika msimu wa 2020-2021 ili kukidhi kupata mahitaji yake ya tani 10,000 za mtama kwa ajili za kuzalisha chapa zake za Eagle na Bingwa.

Akiongea katika mkutano huo wa tathmini,Mwakilishi wa WFP, Lusajo Bukuku alisema kabla ya kuanzishwa kwa mradi huo wakulima walikuwa wanazalisha magunia 3 hadi 4 ya mtama kwa ekari.Kutokana na kupatiwa mbinu bora za kilimo na usimamizi mzuri mavuno yao kwa sasa yameongezeka kufikia karibu magunia kati ya 10 hadi 11 kwa ekari.

Naye Mwakilishi wa Farm Africa ,William Mwakyami,alisema kupitia mradi huu,taasisi yao imesaidia kuwezesha wakulima wapatao 846 ambao wamenufaika kwa kujiongezea kipato kutokana na kuzalisha zaidi kulinganisha na kipindi cha nyuma kabla ya mradi na wameweza kuwa na soko la uhakika la mavuno yao.

Kaimu Afisa Kilimo wa Wilaya ya Kongwa, Bi Amina Msangi, amesema kabla ya kuanzishwa kwa mradi huu wakulima walikuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa soko la uhakika la mavuno yao. Alitoa wito kwa wakulima kuchangamkia fursa hii ya soko la uhakika iliyopatikana ili iwasaidie kujikwamua kimaisha.

Mpango wa TBL Plc wa kununua malighafi nchini ni moja ya mchango wa kampuni ambao unaenda sambamba kufanikisha jitihada za Serikali katika kukuza uchumi wa Tanzania.

Mwaka 2018, ABInBev ilijitoa kuwapatia ujuzi, kuwaunganisha na kuwawezesha kifedha wakulima mpaka kufikia mwaka 2025. Kutokana na mkakati huo,TBL Plc imefanya uwekezaji wenye lengo la kuwainua wakulima wadogo nchini Tanzania kwa kuwaanzishia huduma mbalimbali-Kilimo Uza. 

Kutumiwa meseji za simu kuwapatia taarifa mbalimbali kama hali ya hewa, taarifa za masoko, ushauri wa kitaalamu. huduma ya mkopo wa pembejeo, mafunzo kuhusiana na masuala ya fedha na ununuzi wa pembejeo bora na matumizi yake, matokeo ya utafiti wa mbegu bora za mtama unaofaa kuzalishwa nchini, mbinu za kilimo cha kisasa sambamba na kuwasaidia katika kipindi chote cha msimu wa kilimo ili waweze kusimama na kufanya vizuri zaidi.










Share:

Graduate Management Trainee Program at Diamond Trust Bank (DTB) Tanzania

EXCITING CAREER OPPORTUNITIES IN DIAMOND TRUST BANK TANZANIA DTB Graduate Management Trainee Program 2020   Overview Program Descriptions Diamond Trust Bank has today grown into a leading commercial bank offering a wide spectrum of banking services. With 28 operational branches in Tanzania, Diamond Trust Bank Tanzania is now looking for capable individuals who have the […]

The post Graduate Management Trainee Program at Diamond Trust Bank (DTB) Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Human Resource and Administration Manager at Wildlife Conservation Society (WCS)

Human Resource and Administration Manager  Wildlife Conservation Society Job Summary Under the general supervision of the Country Director, the incumbent shall facilitate the achievement of organizational objectives by providing organizational development services, sourcing, developing, managing and retaining quality human resources for the operations of WCS-Tanzania. Job Description/Requirements Reports to: Country Director, Tanzania Location: Mbeya, Tanzania […]

The post Human Resource and Administration Manager at Wildlife Conservation Society (WCS) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

General Manager at Golden Tulip Hotels, Suites & Resorts

General Manager   Company Name Golden Tulip Hotels, Suites & Resorts Company Location Dar es Salaam, Tanzania Job Description: The ideal candidate will have experience leading a team and managing the daily operation of the business. They will be responsible for maintaining the standard of work from employees as well as onboarding and hiring new […]

The post General Manager at Golden Tulip Hotels, Suites & Resorts appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Asset at Orica, Operator

Operator – Asset Orica Bubada, Geita, Tanzania Orica is the world’s largest provider of commercial explosives and innovative blasting systems to the mining, quarrying, oil and gas and construction markets, a leading supplier of sodium cyanide for gold extraction, and a specialist provider of ground support services in mining and tunnelling. Orica has a diverse […]

The post Asset at Orica, Operator appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Call for Tender at AFYA Micro Finance Company Limited (AMiF)

AFYA Micro Finance Company Limited (AMiF) TENDER – LOAN MANAGEMENT SOFTWARE Job Summary AFYA Micro Finance Company Limited (AMiF) is a specialized Microfinance Institution that provides affordable to the private health care providers in Tanzania. AMiF targets the lower end market in the health sector, in particular, Accredited Drug Dispensing Outlets (ADDOs), Pharmacies, dispensaries, small clinics, […]

The post Call for Tender at AFYA Micro Finance Company Limited (AMiF) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Rise Programs Coordinator at Grumeti Fund Trust

RISE PROGRAMS COORDINATOR   Description DEPARTMENT: RESEARCH AND INNOVATION FOR THE SERENGETI ECOSYSTEM (RISE) DUTY STATION: GRUMETI, MARA REGION, TANZANIA REPORTING: LINE HEAD SCIENTIST – RISE DUTIES AND RESPONSIBILITIES:   Support on-going research programs via field data collection, updating records, and data maintenance. Summarize and analyze data regularly, providing project oversight and contributing to routine reports. Develop […]

The post Rise Programs Coordinator at Grumeti Fund Trust appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

GIS And Data Analysis Specialits at Grumeti Fund Trust

GIS AND DATA ANALYSIS SPECIALIST    Details Description The Grumeti Fund Trust’s Research & Monitoring department is looking for a highly qualified and motivated candidate to be recruited for the position of GIS and Data Analysis Specialist. This is a management role within the department and the specialist will be expected to also fulfill the […]

The post GIS And Data Analysis Specialits at Grumeti Fund Trust appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

ARTISAN II 4 POSTS Transfer Vacancies/ at Mbeya University

Mbeya University of Science and Technology (MUST) is a result of the transformation of the Mbeya Institute of Science and Technology (MIST) through the Universities Act No.7 (2005) and Charter of Mbeya University of Science and Technology, 2013 with the aim of becoming the leading centre of excellence for knowledge, skills and applied education in […]

The post ARTISAN II 4 POSTS Transfer Vacancies/ at Mbeya University appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MEDICAL ATTENDANT II Transfer Vacancies at Mbeya University

Mbeya University of Science and Technology (MUST) is a result of the transformation of the Mbeya Institute of Science and Technology (MIST) through the Universities Act No.7 (2005) and Charter of Mbeya University of Science and Technology, 2013 with the aim of becoming the leading centre of excellence for knowledge, skills and applied education in […]

The post MEDICAL ATTENDANT II Transfer Vacancies at Mbeya University appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Sunday, 22 November 2020

WAKULIMA PERAMIHO WAIPOKEA SHERIA YA TAIFA YA UMWAGILIAJI

  

Picha ni Bw. Daudi Mkoma Mtaalam kutoka katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Mkoani Ruvuma, akiongea katika mkutano na wakulima wa skimu ya Umwagiliaji ya Nakahuga iliyopo Peramiho wilayani Songea.

baadhi ya wakulima wa kilimo cha umwagiliaji katika kijiji cha Nakahuga wakifuatilia mkutano na wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.
Mkulima katika skimu ya kilimo cha uwagiliaji ya Nakahuga iliyopo Peramiho wilayani Songea Bw. Albert Mtani akiuliza swali wakati wa mkutano na wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.

Na Mwandishiwetu – Peramiho

Wakulima katika skimu ya kilimo cha umwagiliaji ya Nakahuga iliyopo Peramiho wilayani Songea mkoani Ruvuma wameipokea sheria ya Taifa ya kilimo cha umwagiliaji na kuonesha utayari wa kuchangia katika mfuko wa maendeleo yakilimo cha umwagiliaji kwa kukiri kuilewa sheria hiyo mara baada ya mafunzo waliyopata  toka kwa wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.

 Akizungumza wakati wa mkutano wa majumuisho uliofanyika katika kijiji cha Nakahuga,mmoja wa wakulima hao Bw. Albert Mtani  alisema kuwa kilimo cha umwagiliaji kwao ni mkombozi kwani ni kilimo cha uhakika.

 “Binafsi ninaishukuru serikali kwa kuleta mradi huu nani naamini inania njema ya kuendelea kuboresha miondombinu katika skimu hii na kwa kuwa tunapata faida nyingi zitokanazo na shughuli zetu zakilimo, hivyo sio ni tatizo kwenye uchangiaji katika mfuko kwani ninaamini kuwa mifereji itakapo haribika kwa namna yoyote ile serikali itaitengeneza kupitia mfuko huo,  na tutaendelea na shughuli zetu za kilimo bila wasiwasi.” Alisema.

Sambambana hilo kwa nyakati tofauti katika ushiriki wa mkutano huo, baadhiya wakulima walisikika wakisema kuwa Sheria ya Taifa ya Umwagiliaji sasa imekaa vizuri kwani kabla yakuwepo kwa sheria hiyo ushirikishwaji wa wakulima kuhusu shughuli za umwagiliaji ulikuwa ni mdogo na kulikuwa na usimamizi mbovu wa miundombinu yaumwagiliaji

Waliongeza kwa kusema kuwa sheria ya  Taifa ya umwagiliaji pia itaweza kusaidia kutatua migogoro midogo midogo iliyopo katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji.
Share:

SPRF INAVYOSHIRIKISHA WANAFUNZI KUTOKOMEZA UKATILI

 

Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Munkinya, Yoden Ngogo akiwakaribisha Maafisa wa Shirika lisilo la Kiserikali la Stars of Poverty Rescue Foundation (SPRF) la mkoani Singida mwishoni mwa wiki,  kuzungumza  na wanafunzi wa shule hiyo, kuhusiana na masuala yahusuyo athari za ukatili wa kijinsia.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Munkinya wakisikiliza mafunzo ya ukatili wa kijinsia yalikuwa yakiwasilishwa na watendaji wa SPRF (hawapo pichani)
Wanafunzi wa Munkinya Sekondari wakiwasilisha mpango kazi wa utekelezaji majukumu yao kuhusiana na vita iliyopo dhidi ya matukio ya ukatili wa kijinsia.

Mafunzo yakiendelea.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Siuyu wakifuatilia mafunzo hayo.

Kaimu Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Ikungi, Paul Mgelwa akifuatilia mafunzo hayo, kulia ni wanafunzi wa Shule ya Sekondari Siuyu.

Mratibu wa Mradi kutoka SPRF, Mwalimu Bernard Maira akizungumza na wanafunzi wa sekondari ya Siuyu (hawapo pichani)

wa Shule ya Sekondari Siuyu wakifuatilia mafunzo hayo.

Mratibu wa Mradi kutoka SPRF, Mwalimu Bernard Maira akizungumza na wanafunzi wa sekondari ya Siuyu wakati wa mafunzo hayo.

 


Na Godwin Myovela, Singida


MATUKIO ya unyanyasaji wa kijinsia kwa wasichana wenye umri mdogo, ikiwemo mimba na ndoa za utotoni, vitendo vya ukeketaji na ubakaji yameendelea kupungua katika wilaya ya Ikungi mkoani hapa- huku sababu kubwa ikitajwa kuwa ni matokeo ya ushirikishaji wa makundi rika katika kupambana na vita hiyo ndani ya jamii, imeelezwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la Kiserikali la Stars of Poverty Rescue Foundation (SPRF) nchini, Dkt Suleiman Muttani, aliyasema hayo jana muda mfupi baada ya shirika hilo kutembelea na kufanya mijadala ya pamoja kwa kushirikisha shule za sekondari Munkinya na Siuyu zilizopo wilaya ya Ikungi, mkoani hapa.

“Tumeunda ‘Clubs’ za wanafunzi mashuleni ambao pamoja na mambo mengine tunawapa fursa ya kuchagua viongozi, tunawajengea uwezo na kuwasimamia kutengeneza mpango kazi ambao unawasaidia katika kuwawezesha kufichua na kupeana elimu ya matukio ya kutokomeza ukatili, mimba na ndoa za utotoni wao kwa wao,” alisema Muttani. 

Afisa Ufuatiliaji na Tathmini wa shirika hilo, Mwedinuu Beleko, akiwasilisha mada kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wanafunzi wa shule hizo, aliitaka jamii kujitokeza haraka na kutoa taarifa yenye ushahidi pindi matukio ya ukatili yanapojitokeza ili kurahisisha mwenendo wa shauri.

“Nawaomba wanafunzi msiogope, wala msitishwe na mtu yeyote tukio lolote la ukatili linapojitokeza basi hakikisheni aliyefanyiwa ukatili huo anashiriki mara moja katika kutoa taarifa yenye ushahidi…na msipoteze huo ushahidi na vielelezo vyote ili kuharakisha mchakato wa kesi kuendelea kwa wakati,” alisema Beleko.

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii wilayani hapa, Paul Mgelwa aliwasihi wanafunzi kuwa makini na kutodanganyika ili kukabiliana na mimba zisizotarajiwa ambazo hufifisha ndoto na matarajio yao-na kusisitiza kuwa daima wanapaswa kuweka kipaumbele cha elimu kwanza kwa kuzingatia elimu ndio ukombozi wa maisha katika kupambana na umasikini.

Katibu wa Shirika hilo, Dkt Mwajuma Mikidadi alisema malengo ya SPRF, ambayo miradi yake ipo chini ya ufadhili wa Foundation for Civil Society (FCS), ni kukuza ushirikiano miongoni mwa wadau na jamii, taasisi za kitaifa na kimataifa katika kutokomeza umaskini wa kipato, sambamba na kuimarisha uwezo wa kitaasisi katika kukua na kutekeleza programu endelevu.

“SPRF na jamii ndio moto wetu kwa sasa, programu hii imesaidia kumfanya kila mwanafunzi wa kike kutambua haki zake, lakini madhara ya mila zilizopitwa na wakati na kandamizi, masuala ya ukeketaji na mimba na ndoa utotoni ndani ya jamii,” alisema Mikidadi.

Mratibu wa mradi huo, Mwalimu Bernard Maira, alisema hata hivyo shirika hilo limefanikiwa kuanzisha Kamati za MTAKUWWA kwenye vijiji 8 zinazopinga Ukatili wa Kijinsia dhidi ya Wanawake na Watoto huku wakihamasisha uanzishwaji wa vikundi mathalani Sauti ya Mwanamke na Sauti ya Mwanafunzi, ambavyo vimekuwa chachu ya mageuzi ya kifikra dhidi ya mila potofu na masuala ya ukatili ndani ya jamii zao.

Share:

MBUNGE MTATURU AWASHUKURU WANANCHI WA SINGIDA MASHARIKI,ATAJA VIPAUMBELE SABA ATAKAVYOANZA NAVYO

Gari la Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu akiwasili katika jimbo hilo kwa ajili ya kuwashukuru wananchi kwa ushindi waliompatia.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akipokelewa kwa shangwe na mafaruko ya wananchi wake na Chama cha Mapinduzi(CCM) kutoka Bungeni Dodoma,alipowasili jimboni kwake kutoa shukrani za ushindi wa CCM.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akifurahia na wananchi wake pamoja na Chama cha Mapinduzi(CCM) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akicheza ngoma baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwa na Mwenyekiti Wilaya ya Ikungi ,Mika Likapakapa wakipiga makofi kwa vikundi vya ngoma (havipo pichani) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akvishwa vitu vya kimila na Wazee baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwashukuru wananchi wake pamoja na Chama cha Mapinduzi(CCM) kwa kumpatia zawadi mara baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwa ameshikiria silaha za jadi baada ya kukabidhiwa na Wazee mara baada ya kuwasili jimboni huko akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Mzee Maarufu Ikungi Bw.Hussein Sungita akitoa neno kwa Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,(hayupo pichani) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Katibu wa Wilaya ya Ikungi Kangaeli Akyoo akizungumza na wananchi waliojitokeza kumpokea Mbunge wao wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu mara baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Mwenyekiti wa wilaya ya Ikungi Mika Likapakapa akiongea na umati wa wananchi wa wa Jimbo la Singida Mashariki, waliojitokeza kumpokea Mbunge wao Miraji Mtaturu baada ya kuwasili jimboni huko akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Mama wa Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu, Mariam Sepetu

Mama wa Miss Tanzania 2006/07 ,Wema Sepetu,Mariam Sepetu ,akielezea furaha aliyonayo baada ya Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu kuchaguliwa tena kuwa Mbunge na anaamini kuwa ataendelea kuwatumika wananchi mpaka aatakampochoka mwenyewe kuliongoza jimbo hilo.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwahutubia mamia ya wananchi wake pamoja na Chama cha Mapinduzi(CCM) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Sehemu ya wananchi wakifatilia hotuba ya Mbunge wao wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu wakati akiwashukuru na kuwapongeza kwa kumpa ridhaa ya kuwatumikia tena miaka mitano mengine mara baada ya kuwasili jimboni huko akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Na.Alex Sonna,Ikungi Singida

Hivi ndivyo unaweza kusema kuwa ni Mafuriko ya wananchi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa Mbunge wao Mhe.Miraji Mtaturu walivyompokea kwa shangwe na furaha baada ya kuwasili katika Jimbo hilo la Singida Mashariki akitokea bungeni Dodoma kwa ajili ya kuwashukuru kwa kumuani tena miaka mitano tena kwa ushindi wa kishindo.

Akizungumza na baada ya kupokelewa na wananchi wake na Chama cha CCM Mhe.Mtaturu amewashukuru wananchi wa jimbo hilo kwa kuendelea kumuamini tena huku akisema kuwa atawatumikia wananchi bila kuwabagua kwa itikadi zao za kisiasa.

Aidha Mtaturu amewambia wananchi kuwa uchaguzi kwasasa umekwisha hivyo wananchi washirikiane kuhakikisha Wilaya ya Ikungi inapata mafanikio na yeye kama kiongozi wao atawatumikia wote bila ubaguzi.

“Tayari Mimi ni Mbunge wenu nipo tayari kushirikiana nanyi, lakini pia tujenge mahusiano, tuachane na itikadi zetu za kisiasa sasa tujenge uchumi wa Jimbo la Ikungi, tumechelewa sana,”amesisitiza

Hata hivyo Mhe.Mtaturu ametaja vipaumbele saba atakavyoanza navyo ikiwemo suala la elimu ambapo atasimamia kuhakikisha watoto wanapata elimu bora,Maji,Umeme,Afya pamoja na miradi iliyopo inatekelezwa na kuibua mingine.

Aidha Mhe.Mtaturu amewahamasisha akinababa kuunda vikundi vya wakulima ili waweze kupata mikopo itakayosaidia kuinua kilimo chao katika wilaya ya Ikungi na pia wataweza kupata mikopo wakiunda vikundi hivyo.

Share:

JITIBU TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA FULL POWER.. UUME MDOGO ZAT 50 NDIYO SULUHISHO




Zati 50


Full Power



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume:

⇒Ngiri,


⇒Henia


⇒Kisukari


⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri


⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu


⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi


⇒Msongo wa mawazo 

⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.

ZAT 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa
⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger