Sunday, 22 November 2020

WAKULIMA PERAMIHO WAIPOKEA SHERIA YA TAIFA YA UMWAGILIAJI

  

Picha ni Bw. Daudi Mkoma Mtaalam kutoka katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Mkoani Ruvuma, akiongea katika mkutano na wakulima wa skimu ya Umwagiliaji ya Nakahuga iliyopo Peramiho wilayani Songea.

baadhi ya wakulima wa kilimo cha umwagiliaji katika kijiji cha Nakahuga wakifuatilia mkutano na wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.
Mkulima katika skimu ya kilimo cha uwagiliaji ya Nakahuga iliyopo Peramiho wilayani Songea Bw. Albert Mtani akiuliza swali wakati wa mkutano na wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.

Na Mwandishiwetu – Peramiho

Wakulima katika skimu ya kilimo cha umwagiliaji ya Nakahuga iliyopo Peramiho wilayani Songea mkoani Ruvuma wameipokea sheria ya Taifa ya kilimo cha umwagiliaji na kuonesha utayari wa kuchangia katika mfuko wa maendeleo yakilimo cha umwagiliaji kwa kukiri kuilewa sheria hiyo mara baada ya mafunzo waliyopata  toka kwa wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.

 Akizungumza wakati wa mkutano wa majumuisho uliofanyika katika kijiji cha Nakahuga,mmoja wa wakulima hao Bw. Albert Mtani  alisema kuwa kilimo cha umwagiliaji kwao ni mkombozi kwani ni kilimo cha uhakika.

 “Binafsi ninaishukuru serikali kwa kuleta mradi huu nani naamini inania njema ya kuendelea kuboresha miondombinu katika skimu hii na kwa kuwa tunapata faida nyingi zitokanazo na shughuli zetu zakilimo, hivyo sio ni tatizo kwenye uchangiaji katika mfuko kwani ninaamini kuwa mifereji itakapo haribika kwa namna yoyote ile serikali itaitengeneza kupitia mfuko huo,  na tutaendelea na shughuli zetu za kilimo bila wasiwasi.” Alisema.

Sambambana hilo kwa nyakati tofauti katika ushiriki wa mkutano huo, baadhiya wakulima walisikika wakisema kuwa Sheria ya Taifa ya Umwagiliaji sasa imekaa vizuri kwani kabla yakuwepo kwa sheria hiyo ushirikishwaji wa wakulima kuhusu shughuli za umwagiliaji ulikuwa ni mdogo na kulikuwa na usimamizi mbovu wa miundombinu yaumwagiliaji

Waliongeza kwa kusema kuwa sheria ya  Taifa ya umwagiliaji pia itaweza kusaidia kutatua migogoro midogo midogo iliyopo katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji.
Share:

SPRF INAVYOSHIRIKISHA WANAFUNZI KUTOKOMEZA UKATILI

 

Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Munkinya, Yoden Ngogo akiwakaribisha Maafisa wa Shirika lisilo la Kiserikali la Stars of Poverty Rescue Foundation (SPRF) la mkoani Singida mwishoni mwa wiki,  kuzungumza  na wanafunzi wa shule hiyo, kuhusiana na masuala yahusuyo athari za ukatili wa kijinsia.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Munkinya wakisikiliza mafunzo ya ukatili wa kijinsia yalikuwa yakiwasilishwa na watendaji wa SPRF (hawapo pichani)
Wanafunzi wa Munkinya Sekondari wakiwasilisha mpango kazi wa utekelezaji majukumu yao kuhusiana na vita iliyopo dhidi ya matukio ya ukatili wa kijinsia.

Mafunzo yakiendelea.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Siuyu wakifuatilia mafunzo hayo.

Kaimu Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Ikungi, Paul Mgelwa akifuatilia mafunzo hayo, kulia ni wanafunzi wa Shule ya Sekondari Siuyu.

Mratibu wa Mradi kutoka SPRF, Mwalimu Bernard Maira akizungumza na wanafunzi wa sekondari ya Siuyu (hawapo pichani)

wa Shule ya Sekondari Siuyu wakifuatilia mafunzo hayo.

Mratibu wa Mradi kutoka SPRF, Mwalimu Bernard Maira akizungumza na wanafunzi wa sekondari ya Siuyu wakati wa mafunzo hayo.

 


Na Godwin Myovela, Singida


MATUKIO ya unyanyasaji wa kijinsia kwa wasichana wenye umri mdogo, ikiwemo mimba na ndoa za utotoni, vitendo vya ukeketaji na ubakaji yameendelea kupungua katika wilaya ya Ikungi mkoani hapa- huku sababu kubwa ikitajwa kuwa ni matokeo ya ushirikishaji wa makundi rika katika kupambana na vita hiyo ndani ya jamii, imeelezwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la Kiserikali la Stars of Poverty Rescue Foundation (SPRF) nchini, Dkt Suleiman Muttani, aliyasema hayo jana muda mfupi baada ya shirika hilo kutembelea na kufanya mijadala ya pamoja kwa kushirikisha shule za sekondari Munkinya na Siuyu zilizopo wilaya ya Ikungi, mkoani hapa.

“Tumeunda ‘Clubs’ za wanafunzi mashuleni ambao pamoja na mambo mengine tunawapa fursa ya kuchagua viongozi, tunawajengea uwezo na kuwasimamia kutengeneza mpango kazi ambao unawasaidia katika kuwawezesha kufichua na kupeana elimu ya matukio ya kutokomeza ukatili, mimba na ndoa za utotoni wao kwa wao,” alisema Muttani. 

Afisa Ufuatiliaji na Tathmini wa shirika hilo, Mwedinuu Beleko, akiwasilisha mada kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wanafunzi wa shule hizo, aliitaka jamii kujitokeza haraka na kutoa taarifa yenye ushahidi pindi matukio ya ukatili yanapojitokeza ili kurahisisha mwenendo wa shauri.

“Nawaomba wanafunzi msiogope, wala msitishwe na mtu yeyote tukio lolote la ukatili linapojitokeza basi hakikisheni aliyefanyiwa ukatili huo anashiriki mara moja katika kutoa taarifa yenye ushahidi…na msipoteze huo ushahidi na vielelezo vyote ili kuharakisha mchakato wa kesi kuendelea kwa wakati,” alisema Beleko.

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii wilayani hapa, Paul Mgelwa aliwasihi wanafunzi kuwa makini na kutodanganyika ili kukabiliana na mimba zisizotarajiwa ambazo hufifisha ndoto na matarajio yao-na kusisitiza kuwa daima wanapaswa kuweka kipaumbele cha elimu kwanza kwa kuzingatia elimu ndio ukombozi wa maisha katika kupambana na umasikini.

Katibu wa Shirika hilo, Dkt Mwajuma Mikidadi alisema malengo ya SPRF, ambayo miradi yake ipo chini ya ufadhili wa Foundation for Civil Society (FCS), ni kukuza ushirikiano miongoni mwa wadau na jamii, taasisi za kitaifa na kimataifa katika kutokomeza umaskini wa kipato, sambamba na kuimarisha uwezo wa kitaasisi katika kukua na kutekeleza programu endelevu.

“SPRF na jamii ndio moto wetu kwa sasa, programu hii imesaidia kumfanya kila mwanafunzi wa kike kutambua haki zake, lakini madhara ya mila zilizopitwa na wakati na kandamizi, masuala ya ukeketaji na mimba na ndoa utotoni ndani ya jamii,” alisema Mikidadi.

Mratibu wa mradi huo, Mwalimu Bernard Maira, alisema hata hivyo shirika hilo limefanikiwa kuanzisha Kamati za MTAKUWWA kwenye vijiji 8 zinazopinga Ukatili wa Kijinsia dhidi ya Wanawake na Watoto huku wakihamasisha uanzishwaji wa vikundi mathalani Sauti ya Mwanamke na Sauti ya Mwanafunzi, ambavyo vimekuwa chachu ya mageuzi ya kifikra dhidi ya mila potofu na masuala ya ukatili ndani ya jamii zao.

Share:

MBUNGE MTATURU AWASHUKURU WANANCHI WA SINGIDA MASHARIKI,ATAJA VIPAUMBELE SABA ATAKAVYOANZA NAVYO

Gari la Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu akiwasili katika jimbo hilo kwa ajili ya kuwashukuru wananchi kwa ushindi waliompatia.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akipokelewa kwa shangwe na mafaruko ya wananchi wake na Chama cha Mapinduzi(CCM) kutoka Bungeni Dodoma,alipowasili jimboni kwake kutoa shukrani za ushindi wa CCM.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akifurahia na wananchi wake pamoja na Chama cha Mapinduzi(CCM) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akicheza ngoma baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwa na Mwenyekiti Wilaya ya Ikungi ,Mika Likapakapa wakipiga makofi kwa vikundi vya ngoma (havipo pichani) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akvishwa vitu vya kimila na Wazee baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwashukuru wananchi wake pamoja na Chama cha Mapinduzi(CCM) kwa kumpatia zawadi mara baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwa ameshikiria silaha za jadi baada ya kukabidhiwa na Wazee mara baada ya kuwasili jimboni huko akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Mzee Maarufu Ikungi Bw.Hussein Sungita akitoa neno kwa Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,(hayupo pichani) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Katibu wa Wilaya ya Ikungi Kangaeli Akyoo akizungumza na wananchi waliojitokeza kumpokea Mbunge wao wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu mara baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Mwenyekiti wa wilaya ya Ikungi Mika Likapakapa akiongea na umati wa wananchi wa wa Jimbo la Singida Mashariki, waliojitokeza kumpokea Mbunge wao Miraji Mtaturu baada ya kuwasili jimboni huko akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Mama wa Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu, Mariam Sepetu

Mama wa Miss Tanzania 2006/07 ,Wema Sepetu,Mariam Sepetu ,akielezea furaha aliyonayo baada ya Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu kuchaguliwa tena kuwa Mbunge na anaamini kuwa ataendelea kuwatumika wananchi mpaka aatakampochoka mwenyewe kuliongoza jimbo hilo.

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,akiwahutubia mamia ya wananchi wake pamoja na Chama cha Mapinduzi(CCM) baada ya kuwasili jimboni humo akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Sehemu ya wananchi wakifatilia hotuba ya Mbunge wao wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu wakati akiwashukuru na kuwapongeza kwa kumpa ridhaa ya kuwatumikia tena miaka mitano mengine mara baada ya kuwasili jimboni huko akitokea Bungeni Dodoma,kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushindi waliompatia kuliongoza jimbo hilo kwa miaka mitano tena.

Na.Alex Sonna,Ikungi Singida

Hivi ndivyo unaweza kusema kuwa ni Mafuriko ya wananchi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa Mbunge wao Mhe.Miraji Mtaturu walivyompokea kwa shangwe na furaha baada ya kuwasili katika Jimbo hilo la Singida Mashariki akitokea bungeni Dodoma kwa ajili ya kuwashukuru kwa kumuani tena miaka mitano tena kwa ushindi wa kishindo.

Akizungumza na baada ya kupokelewa na wananchi wake na Chama cha CCM Mhe.Mtaturu amewashukuru wananchi wa jimbo hilo kwa kuendelea kumuamini tena huku akisema kuwa atawatumikia wananchi bila kuwabagua kwa itikadi zao za kisiasa.

Aidha Mtaturu amewambia wananchi kuwa uchaguzi kwasasa umekwisha hivyo wananchi washirikiane kuhakikisha Wilaya ya Ikungi inapata mafanikio na yeye kama kiongozi wao atawatumikia wote bila ubaguzi.

“Tayari Mimi ni Mbunge wenu nipo tayari kushirikiana nanyi, lakini pia tujenge mahusiano, tuachane na itikadi zetu za kisiasa sasa tujenge uchumi wa Jimbo la Ikungi, tumechelewa sana,”amesisitiza

Hata hivyo Mhe.Mtaturu ametaja vipaumbele saba atakavyoanza navyo ikiwemo suala la elimu ambapo atasimamia kuhakikisha watoto wanapata elimu bora,Maji,Umeme,Afya pamoja na miradi iliyopo inatekelezwa na kuibua mingine.

Aidha Mhe.Mtaturu amewahamasisha akinababa kuunda vikundi vya wakulima ili waweze kupata mikopo itakayosaidia kuinua kilimo chao katika wilaya ya Ikungi na pia wataweza kupata mikopo wakiunda vikundi hivyo.

Share:

JITIBU TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA FULL POWER.. UUME MDOGO ZAT 50 NDIYO SULUHISHO




Zati 50


Full Power



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume:

⇒Ngiri,


⇒Henia


⇒Kisukari


⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri


⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu


⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi


⇒Msongo wa mawazo 

⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.

ZAT 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa
⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

KARIBU GVEN WEAR UPATE MUONEKANO WA PEKEE .....HUDUMA ZA KIPEKEE


Karibu Gven Wear.Tunapatikana karibu na NMB Bank Manonga Mjini Shinyanga, wasiliana nasi 0767926671
'Your look is our priority'

Share:

WANAFUNZI 1050 WAFUTIWA MATOKEO MTIHANI DARASA LA SABA


Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dkt. Charles Msonde.

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), limefuta matokeo ya mitihani ya Taifa ya darasa la 7 kwa shule 38, ambazo zimebainika kufanya udanganyifu kwenye mitihani hiyo iliyofanyika Oktoba 7 na 8, 2020, huku pia likiwafutia matokeo watahiniwa 1,059, baada ya kubainika wamefanya udanganyifu.

Taarifa hiyo imetolewa Novemba 21, 2020, na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dkt. Charles Msonde, ambapo amesema kuwa mbali na hao Baraza hilo pia, limezuia matokeo ya watahiniwa 110 ambao waliugua wakati wa kufanya mitihani hiyo na hivyo watalazimiika kurudia mtihani mwakani kwa mujibu wa sheria.

Shule zilizofutiwa matokeo ni pamoja na Mafiri, Kibogoji, Ng’wambe, Digalama, Dihinda kutoka Halmashauri ya Mvomero na shule za msingi za Nyawa A iliyopo Halmashauri ya Bariadi vijijini, Ngiloli, Nguyami, Ibuti, Ihenje, Bwawani, Mogohigwa, Chakwale na Msingisi zilizopo Halmashauri ya Gairo.

Shule zingine ni Sikonge Tabora ikiwemo shule ya msingi Chabutwa, Usagari, Uyui Tabora Siashimbwe iliyopo Moshi Kilimanjaro, Dominion Arusha, Matogoro ya Tandahimba Mtwara, Ng’arita Bariadi vijijini mkoani Simiyu, Olkitikiti Kiteto iliyopo Manyara na Nyamimina Buchosa Mwanza.

Aidha katika hatua nyingine Dkt. Msonde, amesema kuwa ufaulu wa wanafunzi wa darasa la saba, umeongezeka kwa wanafunzi kupata alama hadi 250 kwa masomo yote na hivyo kufikia asilimia 82.68

Kuhusu mitihani ya kidato cha nne inayotarajiwa kuanza wiki ijayo, Dkt Msonde amewahimiza walimu na wanafunzi kuacha kushiriki vitendo vyovote vya udanganyifu kwa kuwa wakibainika watafutiwa matokeo yao ya mitihani.
Share:

Saturday, 21 November 2020

WAAJIRI MKOANI ARUSHA WAMESISITIZIWA KUWEKA MIFUMO MADHUBUTI KUWALINDA WAFANYAKAZI


Mgeni rasmi kwenye hafla ya ufunguzi wa Mafunzo ya Vision Zero, Richard Kwitega Katibu tawala Mkoa wa Arusha (Katikati) akiwa na Mkurugezi wa Usalama na Afya Mhandisi Alex Ngata Pamoja na Mkurugenzi wa Mafunzo,Utafiti na Takwimu Ndugu Joshua Matiko
Mhandisi Alex Ngata akiongea kwenye mafunzo ya Vision zero Mkoani Arusha

Baadhi ya Wawakilishi waViwanda,wafanyabiashara,taasisi,kampuni za mkoa wa Arusha wakifuatilia kwa makini, mafunzo ya Vision zero Mkoani Arusha
Baadhi ya Wawakilishi wa Maeneo ya kazi mkoa wa Arusha wakifuatilia kwa makini, mafunzo ya Vision zero Mkoani Arusha 

*********************** 

Mwandishi wetu, Arusha 
Katibu tawala Mkoa wa Arusha Mhe. Richard Kwitega amewasisitiza waajiri mkoani Arusha kuweka mifumo madhubuti ilikuwalinda wafanyakazi dhidi ya magonjwa na ajali katika maeneo yao ya kazi. 

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, kwenye ufunguzi wa mafunzo maalumu ya Vision zero yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA) jijini Arusha, maalamu kwa wamiliki wa meoeo ya kazi mkoa wa Arusha, amesema uwepo wa mifumo mizuri maeneo ya kazi itasidia kuwakinga wafanyakazi dhidi ya magonjwa na ajali zinazotokea maeneo ya kazi. 

Ndugu Richard amesema wafanyakazi ni kipuri namba moja,kwa tassisi au kampuni yeyote katika ufanisi wakazi yeyote, amesema wafanyakazi wana mchango mkubwa sehemu ya kazi hivyo hawana budi kuhakikisha wanawalindwa dhidi ya magojwa na ajali zinazoweza kutokea sehemu za kazi, ilikuwawezesha kufikia malengo waliojiwekea. 

Aidha katibu tawala huyo amesisitiza waajiri kutoa ushirikiano kwa OSHA ilikuhakikisha suala hili linatekelezwa bila vikwazo, amesema wafanyakazi wanamchango mkubwa kwenye suala la usalama na afya mahali pa kazi kwani wao ndio watendaji wa kazi, endapo ushirikiano utakuwepo baina yao, itasaidia kupunguza ajali na magonjwa sehemu za kazi. 

“Suala hili ni la pande tatu yaani mwajiri,mwajiriwa, na serikali naendapo ushirikiano huo utadumishwa basi ajali na magonjwa yatapungua ama kwisha kabisa sehemu za kazi” aliongeza Katibu tawala huyo wa mkoa wa Arusha.

Amewataka wafanyakazi wajenge utamaduni wakujilinda wao wenyewe wakiwa kazini, kwani wao wanabeba jukumu kubwa la kujilinda dhidi ya magonjwa na ajali sehemu za kazi kutokana na majukumu yao ya kila siku.

Akiongea kwa niaba ya Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Mkurugenzi wa Usalama na Afya mhandisi Alex Ngata amesema, Kampeni ya Vision Zero ni kampeni ya kidunia, nchi mbalimbali dunia nizinatekeleza kampeni hii, na lengo kuu la Vision zero ni kupunguza ajali na magonjwa sehemu za kazi. 

Mhandisi Ngata amesema uwepo wa mfumo sehemu za kazi utawawezesha waajiri kujikagua wenyewe, na hivyo kuweza kuzuia magonjwa na ajali sehemu za kazi.

“Mfanyakazi ni msingi imara katika biashara na uzalishaji ambao OSHA unaungalia bila wao hawawezi kuzalisha na kufanyabiashara hivyo ni muhima kuzingatia usalama na afya zao wakiwa kazini ni vema kuwepo na mfumo maeneo yenu ya kazi ilimuweze kulinda nguvu kazi hiyo”.Alisema Mhandisi Ngata.

Kwa upande wao washiriki wa mafunzo hayo wamesema, Vision zero itawasaidia kwenda kuweka mifumo mizuri yakuwalinda wafanyakazi juu ya ajali na magonjwa sehemu za kazi, wamesema mafunzo hayo yamewajengea uelewa mpana juu ya masuala ya usalama na afya, vitu ambavyo walikuwa hawavifahamu.

“Kama mwajiri atatekeleza kama ambavyo vision zero inataka, Kuondoa magonjwa na ajali sehemu za kazi, nakama utafuata maelekezo, natumaini tutazalisha sana sehemu za kazi na hivyo kuongeza pato la taifa, na ukisema umeondoa ajali na magonjwa sehemu za kazi , hata wafanyakazi watakuwa na moyo wakufanya kazi zaidi na pia watakuwa nguvu za kufanyakazi zaidi, tutawashawishi waajiri wetu watekeleze kama ambavyo lengo kubwa la Vision zero linataka”alisema Bwana Emmanuel Mvamila Mwakilishi wa kiwanda cha TPC Moshi. 

Vision zero ni Kampeni ya Kidunia iiliyoanzishwa kwa lengo ya kupunguza ajali na magonjwa sehemu za kazi,kampeni hiyo inazitaka maeneo ya kazi kuweka mifumo ya kuwalinda wafanyakazi dhidi ya magonjwa na ajali sehemu za kazi, na kampeni hii inatekelezwa kwenye mataifa mbalimbali duniani.
Share:

Picha : TGNP YAKUTANA NA WADAU INAOFANYA NAO KAZI KUTETEA HAKI ZA WANAWAKE NA WASICHANA 'MRADI WA TAPO: SAUTI YA WANAWAKE NA UONGOZI'

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger