Thursday, 11 July 2019

Senegal Na Nigeiria Zatinga Nusu Fainali Afcon 2019

Nigeria na Senegal zimefanikiwa kupenya na kuingia hatua ya nusu fainali ya michuano ya kandanda ya mataifa ya Afrika AFCON inayoendelea kutimua vumbi nchini Misri.

Ilianza Senegal kuitupa nje Benin kwa kuichapa 1-0 Uwanja wa Juni 30 mjini Cairo, bao pekee la kiungo wa Everton, Idrissa Gana Gueye dakika ya 69 akimalizia pasi ya mshambuliaji wa Liverpool, Sadio Mane.

Mane alitumbukiza mipira miwili nyavuni, lakini mara zote mabao yake yalikataliwa kwa Msaada wa Teknolojia ya Video (VAR) na Benin ikamaliza pungufu baada ya Olivier Verdon kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 82
 
Nigeria iliiadhibu Afrika ya Kusini bao 2 kwa 1 huku goli la ushindi likiwekwa wavuni kutoka mpira wa kona uliochongwa vizuri na William Ekong, dakika moja kabla ya mchezo kumalizika.

Samuel Chukwueze aliipatia Nigeria bao la kuongoza katika dakika 45 za kwanza za pambano lililopigwa katika uwanja wa kimataifa wa michezo wa mjini Cairo.

Kocha wa Nigeria Gernot Rohr alisema baada ya mchezo kwamba ilikuwa bahati walifanikiwa kupata bao la pili lililofanikisha ushindi na akaongeza kuwa amejawa furaha kutokana na mafanikio ya timu yake kwenye mchezo wa robo fainali.
 
Katika mchezo huo, Afrika Kusini ilisawazisha mnamo dakika ya 71 kwa goli maridhawa lililowekwa wavuni na mshambuliaji wake Bongani Zungu.

Goli hilo nusura likataliwe baada ya mshika kibendera kusema ulikuwa mpira wa kuvizia lakini hilo lilisawazishwa baadaye na teknolojia ya msaada wa vidio kwa waamuzi wa kandanda, maarufu kama VAR.

Goli la Zungu lilikuwa moja ya magoli matatu yaliyoamuliwa na teknolojia ya VAR katika siku ya kwanza ya kutumiwa teknolojia hiyo kwenye michuano ya AFCON.

Maamuzi yote matatu kuhusu magoli wakati wa mechi mbili za jana yalitoa ushindi.

Teknolojia ya msaada wa vidio kwa waamuzi wa kandanda, VAR, itaendelea kutumika katika michezo itakayopigwa leo na hadi mchezo wa mwisho wa fainali za AFCON.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi 11 July






















Share:

Wednesday, 10 July 2019

MALKIA WA AFRIKA YVONNE CHAKA CHAKA ATUA ZANZIBAR, KUFANYA ONESHO NA MAKONGAMANO ZIFF 2019

Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF, ambaye ni Waziri wa Habari, Utalii na mambo ya Kale, Mahmoud  Thabit  Kombo akiwa katika picha  ya pamoja na Mama Yvonne Chaka Chaka Mjini Unguja, Zanzibar.
***

Na Andrew Chale, Zanzibar, Tanzania

Malkia wa Muziki wa Afrika, Mama Yvonne Chaka Chaka tayari yupo visiwani hapa kwenye tamasha la 22 la Filamu la Kimataifa la Zanzibar (ZIFF)  ambapo atafanya shughuli mbalimbali ikiwemo makongamano na Wanawake pamoja na wadau wengine wakiwemo wasanii wa filamu na muziki.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Masoko wa ZIFF, Isihaka Mlawa amebainisha kuwa, Mama Yvonne ni miongoni mwa wageni maalum kwa mwaka huu ambapo pia atafanya shughuli za kijamii ikiwemo makongamano na warsha ya Wanawake, wasanii wa filamu na wale wa muziki shughuli zilizoandaliwa na ZIFF 2019.

“Mama Yvonne Chaka Chaka amefika jana Zanzibar na leo ataendelea na programu maalum ikiwemo kukutana na Wanafunzi wanaopata mafunzo ya filamu lakini pia atakutana na Wasanii wa muziki kutoka Chuo cha Muziki cha Dhow Country Music Academy.” Alieleza Isihaka.

Aidha, Isihaka Mlawa ameongeza kuwa, wanatarajia Mama Yvonne Chaka Chaka na mwanamuziki aliyeimba wimbo wa Zanzibar miaka 40 iliyopita, Sipho Mabuse kufanya tukio maalum la muziki kidogo kwenye shughuli za tamasha hilo linaloendelea visiwani hapa na kutarajiwa kufikia tamati Julai 14, mwaka huu.

Mama Yvonne Chaka Chaka na Sipho Mabuse wapo visiwani hapa kama wageni maalum waalikwa wa tamasha hilo kwa mwaka huu ambapo wamekuwa kioo na kielelezo kutokana na nyimbo zao mbalimbali zilizotamba Bara la Afrika pamoja na umaarufu wao katika jamii inayowazunguka.

Msanii Mama Yvonne Chaka Chaka (Jina la kuzaliwa Yvonne Machaka ambapo alizaliwa mnamo mwaka 1965 ni mwimbaji kutoka Afrika ya Kusini.

Kuitwa kwake Malkia wa Afrika ni kutokana na kuwa mstari wa mbele katika muziki maarufu wa Afrika Kusini kwa miaka 20.

Nyimbo kama "I'm burning Up", "I'm in Love with a DJ", "I Cry for Freedom", "Makoti", "Motherland" na "Umqombothi" ("Pombe ya Afrika") zimeweza kumuweka kwenye ramani ya Afrika na kuwa maarufu zaidi.

Msanii huyo alizaliwa Dobsonville huko Soweto na alikuja kuwa mototo wa kwanza wa Kiafrika kuonekana kwenye televisheni Afrika Kusini. Mwaka 1981 "Sugar Shack", kipindi cha wenye talanta, kilimjulisha kwa umma wa Afrika Kusini.

Katika harakati za muziki, Chaka Chaka alianza kuimba akiwa na miaka 19 mwaka 1985 wakati Phil Hollis wa Dephon Records alimgundua mjini Johannesburg- Muda mfupi baada ya albamu yake "I'm in Love With a DJ", kuuzwa nakala 35,000.

Pia katika nyimbo zake zilizowahi kushinda tuzo mbalimbali ni kama "Burning Up", "Sangoma", "Who's The Boss", "Motherland", "Be Proud to be African", "Thank You Mr DJ", "Back on my Feet ", " Rhythm of Life "," Who's got the Power "," Bombani (Tiko Rahini), "Power of Afrika", "Yvonne and Friends" na "Kwenzenjani".

Share:

TAMASHA LA ZIFF 2019 LATOA MAFUNZO KWA WATOTO MFANANO (DOWN SYDROME)

Na Andrew Chale, Zanzibar

TAMASHA la Kimataifa la Filamu Zanzibar (ZIFF) la 22 kwa mwaka huu leo limeendesha mafunzo kwa Watoto wenye tatizo la Down Syndrome ama Watoto mfanano kama wanavyojulikana visiwani Zanzibar.

Mafunzo hayo yanayotolewa na ZIFF kwa kushirikiana na taasisi ya kutoka Uholanzi ya Media Lab ambayo imekuwa ikitoa mafunzo kwa watoto mbalimbali visiwnai hapa kwa kutumia teknolojia kwa masuala ya sanaa ikiwemo utengenezaji wa vikatuni, Uigizaji, utangazaji, uandishi wa habari, kuchora na mambo mengine katika masuala ya Sanaa.

Kwa mujibu wa Mratibu wa Warsha za ZIFF 2019, Ahmed Harith amebainisha kuwa, mafunzo hayo ni ya mara ya kwanza kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati ambapo wanatarajia Watoto zaidi ya 1,000 kushiriki mafunzo hayo.

“Mafunzo haya yanatolewa kila siku kuanzia Julai 5 na yataisha mpaka mwisho wa tamasha. Ambapo kwa siku watoto zaidi ya 100 wanapata kushiriki.Watoto hao wanatoka shule mbalimbali za visiwani hapa na baadhi yao nje ya skuli” alisema Ahmed Harith.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Down syndrome Initiative Zanzibar, Bi. Ahlam Abdalla Azzam amelipongeza tamasha la ZIFF 2019 kwa kuwakumbuka watoto hao ambao wameweza kujifunza mambo mbalimbali kama watoto wengine licha ya uelewa wao kuwa mdogo.

“Tunaipongeza ZIFF kwa kuwajali watoto Mfanano wameweza kujifunza vitu vingi ikiwemo kuimba, kucheza na kufanya vitu vya ubunifu.Pia wameweza kujfunza namna ya kuchora michoro na na kutengeneza vikatuni kupitia program za kisasa za teknolojia ya Media Lab” alieleza Bi. Ahlam Abdalla Azzam.

Zanzibar inaelezwa kuwa na Watoto wengi wenye tatizo la Down Syndrome ambapo Serikali na wadau wamekuwa wakichukua hatua za kuwasaidia watoto hao. 









Share:

Waziri Mkuu Akutana Na Rais Wa Misri ...Wazungumzia Namna Ya Kuimairisha Ushirikiano Baina Ya Nchi Hizo Mbili

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Misri Abdel Fattah Al- Sisi, ambapo wametumia fursa hiyo kuzungumzia masuala mbalimbali ikiwemo namna ya kuimarisha ushirikiano baina ya nchi za Tanzania na Misri.

Mbali na kuzungumzia masuala hayo ya kuimarisha ushirikiano katika nyanja mbalimbali zikiwemo za kisiasa, kiuchumi na kijamii, pia Waziri Mkuu amemfikishia Rais wa Misri salamu kutoka kwa Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli.

Mazungumzo baina ya Waziri Mkuu na Rais wa Misri yamefanyika leo (Jumatano, Juni 10, 2019) Ikulu jiji Cairo, ikiwa ni katika siku ya tatu na ya mwisho ya ziara yake ya kikazi nchini Misri. Katika ziara hiyo ameambatana na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga.

Waziri Mkuu amemaliza ziara yake ya kikazi nchini Misri ambapo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Cairo ameagwa na Waziri wa Kilimo na Uhaulishaji wa Ardhi wa Misri, Dkt. Ezz Eldien Abo Setit.

Akiwa ziarani nchini Misri, Waziri Mkuu alikutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Misri, Dkt. Mostafa Madbouly katika siku yake ya kwanza ya ziara yake, ambapo aliwakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Misri waje kuwekeza nchini.

Pia, Waziri Mkuu alitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo nchini humo ambayo ni pamoja na mradi wa ujenzi wa makao makuu mapya ya nchi hiyo, mradi wa awamu ya pili ya upanuzi wa mfereji wa Suez Canal na kiwanda kikubwa cha ngozi.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Picha : MKUU WA JESHI LA POLISI 'IGP SIMON SIRRO' AKAGUA NYUMBA ZA KISASA ZA MAKAZI YA POLISI SHINYANGA

Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro ametembelea na kukagua nyumba 10 za kisasa za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la Kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga na kugharimu shilingi milioni 225.

Mkuu huyo wa jeshi la polisi amekagua nyumba hizo leo Jumanne,Julai 10,2019 na kueleza kuridhishwa jinsi zilivyojengwa kwa umaridadi na ubora wa hali ya juu. 

Nyumba hizo 10 ni sehemu ya nyumba 114 ambazo ujenzi wake umekamilika nchi nzima ikiwa ni sehemu ya nyumba 400 zinazojengwa maeneo mbalimbali nchini kwa ajili ya makazi ya askari polisi.

"Ujenzi huu umegharimu shilingi milioni 225,ni kweli nyumba hizi ni nzuri sana,nimpongeze sana Mhe. Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe.Zainab Telack na kamati yake ya ulinzi na usalama,kamati ya ujenzi na wadau wote walioshiriki kwa kazi hii nzuri"

"Sasa tunamsubiri Mhe. Rais,Dkt.John Pombe Magufuli muda siyo mrefu atazindua hizi nyumba 114 nchi nzima. Pesa zilizotolewa ni kwa ajili ya kujenga nyumba 400,lakini mpaka sasa zilizokamilika sasa ni 114",alisema IGP Sirro. 

Kwa upande wake,Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack alimshukuru Rais Magufuli kwa kutoa pesa kwa ajili ya ujenzi wa makazi ya askari polisi huku akimuomba IGP Sirro kutafuta pesa kwa ajili ya ukarabati wa baadhi ya nyumba za askari ambazo hali yake siyo nzuri.

ANGALIA PICHA
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro alipowasili mkoani Shinyanga kukagua nyumba 10 za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la Kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga leo Jumanne Julai 10,2019. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akizungumza wakati akikagua nyumba 10 za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la Kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga leo Jumanne Julai 10,2019.Kulia ni Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Richard Abwao,kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack.
Muonekano wa nyumba 10 za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Nyumba 10 za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la Kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Muonekano wa nyumba 10 za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack akimuonesha Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akikagua nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akikagua nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Awali Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akisamiliana na askari polisi alipowasili mkoani Shinyanga kukagua nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akisamiliana na askari polisi alipowasili mkoani Shinyanga kukagua nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akisamiliana na askari polisi alipowasili mkoani Shinyanga kukagua nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akisamiliana na askari polisi alipowasili mkoani Shinyanga kukagua nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akisamiliana na waendesha bodaboda katika eneo la nyumba za makazi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga na kuwakumbusha kuzingatia sheria za usalama barabarani na kuwasihi kuacha kubeba mishikaki,wavae kofia ngumu na wawe na leseni. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Share:

Serikali yaanzisha utalii wa fukwe ziwa Viktoria

Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamis Kigwangala amesema wameanzisha utalii wa fukwe katika ziwa Viktoria na kwamba tayari Mamlaka ya hifadhi za Taifa Tanzania (Tanapa) inajenga kivuko kitakachokuwa na uwezo wa kupakia magari manne hadi sita na abiria wasiopungua 100.

Kigwangala ameyasema hayo jana Jumanne Julai 9, wilayani Chato mkoani Geita katika hafla ya uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi – Chato yenye ukubwa wa kilometa za mraba 4,702 ambapo amesema kuwa kuna wanyama waliokuwepo katika hifadhi hiyo na baadae wakatoweka hivyo watafanya jitihada za kuwarudisha katika makazi yao ya asili.

“Katika mapori haya kulikuwa na Faru lakini walitoweka na tunajua aina ya Faru waliokuwepo hapa hivyo tutafanya jitihada za kuwarudisha katika makazi yao, pia tunatarajia kupokea faru 10 wenye asili ya Tanzania kutoka nchi za nje kuja kuongeza idadi ya faru katika nchi yetu,” amesema.

Aidha amesema kuwa walipopandisha hadhi mapori hayo uwindaji umekoma na matumizi yatabadilika na kwamba kiwango cha ulinzi na uhifadhi kitaongezeka kwa kiwango cha juu.

“Katika kipindi ambacho uvamizi ulikuwa umetamalaki wanyama wengi walitoweka lakini tangu tumepandisha hadhi mapori haya idadi imeanza kurudi,” amesema.


Share:

Aliyelazwa Mwaka Mmoja Mloganzila Apatiwa Mashine Ya Kupumua

Hospitali ya Taifa Muhimbili- Mloganzila, imempatia msaada wa mashine ya kusaidia kupumua (Oxygen Concentrator) Bw. Hamad Awadhi kutokana na matatizo yake ya afya ambayo yanamlazimu kutumia mashine ya oxygen muda wote ili aweze kupumua.
 
Akikabidhi msaada huo Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-MNH-Prof. Charles Majinge amesema hospitali imempatia msaada Bw. Awadhi kwa lengo la kuokoa maisha yake sanjari na kuimarisha afya yake lakini pia kumuwezesha kuendelea na shughuli zake za kawaida ili kutokua tegemezi kutokana na hali yake.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Prof. Lawrence Museru ameeleza kwamba mashine hiyo inathamani ya shilingi milioni tatu na nusu imenunuliwa na Hospitali ya Mloganzila ambapo wataalam wamempatia mafunzo Bw. Awadhi namna ya kuitumia na kuitunza ipasavyo.
 
Prof. Museru amemtaka Bwan. Awadhi kuitunza na kuitumia vema mashine hiyo kama ambavyo ameelekezwa na wataalam ili afya yake itakapoimarika iweze kusaidia watanzania wengine.
 
“Hospitali imekupatia msaada wa mashine hii ya kukusaidia kupumua- kwa lengo la kuhakikisha afya yako inaimarika zaidi hivyo tunaomba uitunze na utakapopona kabisa utairejesha hospitali ilituwasaidie wengine” amesema Prof. Museru.
 
Naye Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani MNH- Mloganzila Dkt. Patricia Munseri amesema, Bw. Awadhi kwa muda wote aliokuwepo hospitalini ameishi kwa kutegemea mashine ya oxygen ambayo inamsaidia kupumua ambapo kwa siku alikua akitumia gesi wastani wa lita 5,760.
 
Bw. Hamad Awadhi alifikishwa Hospitali ya Taifa Muhimbili- Mloganzila Julai 9 mwaka 2018 na kuruhusiwa Julai 9 mwaka 2019 baada ya afya yake kuimarika.


Share:

Wazungu Watatu Waliokamatwa na Madini ya Dhahabu Warudishwa Rumande

Watu watatu raia wa kigeni kutoka nchi za Ireland na Uingereza wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya kwa tuhuma za kupatikana na madini aina ya dhahabu yenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 98 kinyume na sheria na taratibu za nchi.

Akisoma Shtaka Mwendesha Mashitaka wakili Msomi wa Serikali Mwandamizi Jacqueline Nyantori, anasema washtakiwa hao kwa pamoja wametenda kosa hilo la uhujumu uchumi July 3, 2019 na kukamatwa katika uwanja wa Ndege  Songwe uliopo Mkoani Mbeya ambapo walikutwa na madini aina ya yenye uzito wa gram 1043.33 yenye thamani ya shilingi milioni 98.5 .

Wakili huyo amewataja washtakiwa hao kuwa ni Clive Rooney (62) raia wa Irish ambaye ni Meneja wa fedha, Ross Harris (34) na Robert Wheedon (59)ambao ni raia wa Uingereza ambapo wamekamatwa na madini hayo wakiyasafirisha kuelekea Jijini Dar es Salaam.

Mwendesha mashtaka wa Serikali amesema washtakiwa hao wamekamatwa na Madini kinyume cha Sheria ya Uhujumu uchumi namba 18 (1) na 4 kifungu cha (1a) na kifungu cha sheria ya madini namba 14 cha mwaka 2010, ikiwa ni pamoja na aya ya 27 ya jedwali la kwanza na kifungu namba 57 kifungu kidogo.

Aidha Kaimu Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya Venance Mulingi amesema Mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza shtaka hili ambapo washtakiwa wamerudishwa wamerudishwe rumande hadi July 22 mwaka huu.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger