Saturday, 2 February 2019

TIMU YA NJOMBE MJI YASHINDWA KUTAMBA MBELE YA NAMUNGO FC UWANJA WA NYUMBANI

Na.Amiri kilagalila Timu za NJOMBE MJI FC na NAMUNGO FC zimegawana pointi moja, baada ya kumaliza dakika tisini za mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara uliofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba mjini Njombe mkoani mkoani humo, matokeo ambayo yamewafanya mashabiki wa soka wa Njombe mji kutoa lawama za wazi kwa waamuzi wanaochezesha michuano hiyo. Penati iliyochezwa dakika tatu kabla mpira haujamalizika...
Share:

RAIS MAGUFULI AMJULIA HALI CHARLES KITWANGA ALIYELAZWA HOSPITALI MUHIMBILI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amemjulia Mbunge wa Jimbo la Misungwi, Charles Kitwanga aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam. January 31 mwaka huu alisafirishwa kutoka Dodoma kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi....
Share:

MCHIMBAJI WA MADINI AFARIKI KWA KUFUKIWA KIFUSI

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Joachimu Kibinda, (48), mchimbaji wa madini na mkazi wa Songambele, wilayani Simanjiro, amefariki dunia baada ya kuangukiwa na kifusi cha udongo akiwa anachimba madini.  Kamanda wa Polisi mkoani Manyara, Augustino Senga, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo...
Share:

ABIRIA WANUSURIKA KIFO KATIKA AJALI YA BASI BIHARAMULO

Biharamulo, Na mwandishi wetu Abiria waliokuwa wakisafiri kutoka Bukoba kuelekea mikoani wamenusurika kifo huku Watu wanane wakijeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao baada ya kupata ajali wakiwa katika basi la Frester linalofanya safari zake Bukoba kwenda Dar es Salaam kisha kuacha njia na kupinduka katika kata ya Katahoka wilayani Biharamulo mkoani kagera. Gari hilo limetambulika kwa namba za...
Share:

NABII MTATA ANAYEPAA ANGANI AKAMATWA

Nabii mwenye utata raia wa Afrika Kusini Shepherd Bushiri wa kanisa la Enlightened Christian Gathering Church (ECG) ametiwa nguvuni.  Bushiri alikamatwa Ijumaa, Februari 1, jijini Rustenberg, Afrika Kusinia na kulingana na taarifa kutoka kanisa lake nabii huyo na mke wake wanatuhumiwa kwa ulanguzi...
Share:

DIWANI WA CHADEMA AWEKWA NDANI KWA AMRI YA RC KISA DHARAU KAKUNJA NNE KWENYE KIKAO

 Diwani wa Susuni (Chadema), Abiud Solomon amesimulia jinsi alivyoondolewa kwenye kikao na mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima na kuwekwa ndani kwa saa saba kisha kuachiwa akielezwa kuwa ana dharau kwa kuwa alikunja nne kikaoni. Akizungumza na Mwananchi leo Jumamosi Februari 2, 2019 amesema Malima...
Share:

MTOTO MWINGINE AUAWA NJOMBE

Mtoto wa miaka 10, ambaye ni mwanafunzi wa darasa la pili, amekutwa ameuawa kikatili na mwili wake kutelekezwa kichakani eneo la Lupembe, wilayani Njombe.  Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Renata Mzinga, amesema kuwa maiti hiyo iliokotwa karibu na nyumbani kwao na mtoto huyo, baada ya majirani...
Share:

ALIYEONDOLEWA JELA KWA MSAMAHA WA RAIS AKAMATWA NA SARE ZA JWTZ

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linamshikilia aliyekuwa mfungwa katika Gereza la Segerea na kuachiwa kwa msamaha wa Rais mwaka jana, Emmanuel Magoti (18), kwa tuhuma za kukutwa na sare za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ). Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini...
Share:

WANNE WAUAWA TENA NJOMBE

Na Amiri kilagalila Mtoto mwingine anayekadiliwa kuwa na umri kati ya miaka 7-10 aliyefahamika kwa jina la RECHAEL MALEKELA mkazi wa kijiji cha Matebwe wilayani Njombe amekutwa ameuawa kwa kuchomwa na vitu vyenye ncha kali mita chache kutoka nyumbani kwao. Akithibitisha tukio hilo mkuu wa wilaya ya Njombe RUTH MSAFIRI alisema kuwa ni kweli mtoto huyo amekutwa amefariki na walizipata taarifa hizo...
Share:

BABA MZAZI AWAPACHIKA MIMBA MABINTI ZAKE WAWILI

 Baba wa mabinti wawili mjini Eldoret nchini Kenya anasakwa na maafisa wa polisi baada ya kuwabaka na kuwapachika mimba watoto hao kwa wakati tofauti. Baba huyo anasemekana kuanza kuwabaka wanawe mwaka wa 2014 mama yao alipoaga dunia.  Mshukiwa alikuwa amerejea nyumbani kutoka gerezani...
Share:

MWALIMU MKUU ATUPWA JELA KWA WIZI WA FEDHA ZA SHULE

Mwalimu Mkuu shule ya sekondari Mikwambe, Paulo Lorry, amehukumiwa kifungo cha miaka sita na kutakiwa kulipa Sh milioni 16 katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke alizoiba kutoka akaunti ya shule. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Taasisiya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa wa...
Share:

LUGOLA AWATAKA VIJANA KUTUNZA WAZEE WAO..HAKUNA ATAKAYESALIMIKA MAUAJI YA WAZEE

Waziri Mambo ya Ndani Kangi Lugola ametoa wito kwa vijana wote nchini kuachana na tabia ya mauaji ya vikongwe na Wazee Nchini na kutoa onyo kwamba hakuna muuaji hata mmoja atakaye salimika na kukwepa mkono wa sheria. Amesema hayo jana jijini Dodoma katika hotuba yake ya ufunguzi wa kikao kazi kilichowakutanisha...
Share:

TPDC YAIMARISHA SEKTA YA ELIMU MKOANI MTWARA

Bi. Marie Msellemu, Meneja Mawasiliano wa TPDC akimkabidhi hundi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mh. Bw. Gelasius Byakanwa kiasi cha Tsh,. 13, 258,042 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa Mkoani Mtwara. Meneja Mawasiliano wa TPDC Bi. Marie Msellemu akikabidhi hundi kwa mratibu wa tasisi ya TAKUWA Bi. Hadija...
Share:

WASANII WA FILAMU NCHINI WATAKIWA KUZINGATIA WELEDI NA UFANISI KWENYE KAZI ZAO

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Monica Kinala akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya filamu wa mkoa wa Tanga Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Joyce Fissoo akizungumza katika mafunzo hayo Katibu Mkuu wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Mathew...
Share:

KAGAME ATEULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI - EAC

Rais wa Rwanda, Paul Kagame ameteuliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Rais Kagame amechukuwa nafasi ya Rais wa Uganda, Yoweri Museveni aliyemaliza muda wake. Akizungumza Ijumaa Februari Mosi, 2019 jioni baada ya kutangazwa kwake katika mkutano wa wakuu wa nchi...
Share:

Friday, 1 February 2019

Video Mpya : CHIEF MAKER - BHOKE...NGOMA KALI UTATA WA BINTI WA KIKURYA

Msanii Chief Maker anakualika kutazama video yake mpya kuhusu Binti wa Kikurya inaitwa Bhoke..Bonge moja la ngoma mtu wangu..Itazame hapa chini...
Share:

WAWILI WAFARIKI,WATANO HOI BAADA YA KUBUGIA DAWA ZA MITI SHAMBA

Watu wawili wamefariki dunia huku wengine watano wakilazwa hospitalini baada kunywa dawa za miti shamba mtaani Karen jijini Nairobi nchini Kenya.  Watu hao saba wanasemekana kunywa dawa hizo walipokuwa wakifanya kazi ya ujenzi wa jengo eneo la Kazuri kule Marula Alhamisi Januari 31,2019.  Waathiriwa...
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger