Friday, 15 October 2021

ALIYEUA WATOTO 10 NA KUWAFYONZA DAMU AUAWA KWA KUPIGWA NA WANAKIJIJI

...

Masten Wanjala, Muuaji aliyekiri kuuwa watoto zaidi ya 10

Watu wenye hasira kali wamemuua muuaji aliyekiri kuwaua watoto zaidi ya 10 nchini Kenya, Masten Wanjala, ambaye alitoroka kwenye kituo cha polisi cha Jogoo Jijini Nairobi siku ya Jumatano. Wanjala ameuawa leo Oktoba 15, 2021, alfajiri majira ya saa 12:45.

Polisi wanasema Masten Wanjala, alifuatwa na wanakijiji katika mji wa Bungoma na kupigwa hadi kufa

Wanjala alikamatwa kwa mara ya kwanza mwezi Julai 2021, ambapo alikiri kutumia kemikali inayofanana na unga kwa wathiriwa kwa kuwalazimisha wainywe ama kuwapulizia usoni kabla ya kuwaua kwa kuwanyonga au kuwafyonza damu.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger