Monday, 6 September 2021

KABURI LAFUKULIWA, MWILI WATOLEWA KWENYE JENEZA NA WASIOJULIKANA MANYONI

...

Wananchi wakiwa kwenye kaburi hilo

Hali ya taharuki imetokea katika kitongoji cha Kipondoda wilayani Manyoni mkoani Singida, baada ya mwili wa marehemu Julia Amasi mwenye umri wa miaka 93 kuzikwa hapo jana na asubuhi ya leo kukuta kaburi likiwa limefukuliwa likiwa na jeneza pekee huku mwili ukiwa pembezoni mwa makaburi hayo.

Mara baada ya kukuta kaburi hilo likiwa hakuna mwili wa marehemu ndipo wakaanza kutafuta na kuukuta mwili ukiwa kando kidogo ya makaburi hayo.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Kipondoda Jackson Job amelaani tukio hilo kwa kuwa vitendo hivyo vya uchimbuaji makaburi baada ya kuzika vimezidi kukithiri katika mji wa Manyoni.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Manyoni Amina Mohammed ametoa wito kwa wananchi kuwafichua wale ambao hawatambuliki wakiwemo waganga wa kienyeji ambao ndiyo wanasadikika kuwa chanzo cha kutokea vitendo hivyo.

Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger