Saturday, 18 September 2021

AMUUA MKE, WATOTO WAKE WAWILI KWA MCHI WA KUTWANGIA

...

Jeshi la Polisi mkoani Tabora linamshikilia mwanaume mmoja kwa tuhuma za mauaji ya mkewe na watoto wawili wanaodaiwa kuuawa kwa kupigwa kichwani na mchi wa kutwangia kisha miili yao kutelekezwa ndani ya nyumba waliokuwa wakiishi huko katika Kijiji cha Mkolye Wilayani Sikonge mkoani Tabora.

Kamanda wa Polisi mkoa waTabora, ACP Safia Jongo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo majira ya saa moja usiku ikiwa ni mfululizo wa mauaji ya raia wasiokuwa na hatia ambayo yameendelea kutokea wiki hii huko mkoani Tabora.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger