Monday, 20 July 2020

Mchujo Mkali Wa Kura za Maoni Kwa Wagombea CCM Waanza Leo

...
Mchakato wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa kupata wagombea katika nafasi mbalimbali unaanza leo ambapo mikutano ya ngazi ya wilaya/majimbo itapiga kura za mapendekezo kati ya leo na kesho.

Upigaji wa kura unaoanza leo unahusisha kura za maoni za kuwapata wagombea katika nafasi za ubunge, uwakilishi, udiwani (Tanzania Bara) na usheha kwenye wadi visiwani Zanzibar.

Baada ya mikutano hiyo, Julai 30 kutakuwa na vikao vya kamati za siasa za majimbo kuwajadili wagombea na kutoa mapendekezo kwenye kamati za siasa za wilaya.

Vikao vya uteuzi kwa wagombea ubunge vitafanywa na Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM kwa Tanzania Bara na ujumbe wa Baraza la Wawakilishi ni Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Zanzibar.


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger