Saturday, 18 July 2020

Aboubakar Juma Aboubakar Ajitosa kugombea Urais kupitia chama cha NCCR-MAGEUZI.

...
Ndugu Aboubakar Juma Aboubakar leo Julai 18,2020 ametia nia kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha NCCR-MAGEUZI.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa NCCR-Mageuzi, Evarist Komu amemtaka mgombea huyo kupeperusha bendera ya chama kwa kusimamia misingi ya chama hicho ambayo ni pamoja na kutetea utu, haki, udugu, usawa na upendo kwa mustakabali wa chama na Watanzania kwa ujumla.

Abubakar ameahidi kusimamia misingi ya chama chake na kuweka mazingira yatakayokuwa chachu ya kuleta maendeleo endelevu nchini.

Komu amesema hadi sasa wanachama 232 wamechukua fomu za kuomba kugombea ubunge na zaidi ya 3,000 wamechukua fomu za kuomba kugombea udiwani.


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger